DISCUSSION/MJADALA

JE! UNAMUELEWAJE YESU NI MUNGU, MWANA WA MUNGU AU MTUME?
Toa maoni yako kuhusu unavyomuelewa Yesu.

HOW DO YOU UNDERSTAND ABOUT JESUS, IS HE GOD, A SON OF GOD, OR AN APOSTLE?
pleas write down what you know about this questions.

32 Responses to DISCUSSION/MJADALA

  1. D. Kibona says:

    Yeye ni kristu mwana wa mungu alie hai

    Like

    • mosespk says:

      ubarikiwe sana, lakini pia kuna swali hapa. tito 2:13 Yesu ni Mungu mkuu na Mwokozi wetu, Je Ikiwa yeye ni Mungu itakuwaje tena awe mwana wa Mungu? Je, tuna Mungu wawili? naomba tusaidiane ndugu zangu.

      Like

      • gologolo says:

        Yesu yeye ni yote katika yote, useme Mungu sawa, Mwana sawa, mtume sawa!

        Like

      • amini tu says:

        sasa hii ya gologolo ni mpya kwa hiyo Yesu alijizaa yeye, akajutuma ulimwenguni yeye, hujasoma aliposema, kama baba alivyonituma ulimwenguni nami natuma nyinyi! alisema silisemi la kwangu bali la yeye aliyenipeleka!

        Like

      • David Mgongolwa says:

        Mimi sidhani kusema Yesu alijizaa mwenyewe ni sasa, kwasababu ni kumchukulia Mungu kama mwanadamu ni hivi emu jiulize Mungu anasema wote walio mpokea aliwapa uwezo kuwa wana, manaake sisi sote ni wana wa Mungu je alituzaa lini? hapo Mungu anamaanisha watoto wake kiroho kumwamini Yesu ni kuzaliwa mara ya pili!

        kuhusiana na Yesu biblia inasema wazi kuwa Yesu ni Mungu, mwana wa Mungu na ni aliyetumwa na Mungu Yohana 1:1 biblia inasema “hapo mwanzo kulikuwa na neno naye neno alikuwa kwa Mungu, naye neno alikuwa Mungu…..” inaendelea kusema naye neno akavaa mwili aka kaa kwetu nasi tukaona utukufu wake, kama wa mwana pekee atokaye kwa Baba” utukufu ni udhihilisho Yesu aliijifunua katika mwili MUNGU(Neno) akavaa mwili akakaa kwetu alivyofika akajifunua kama mwana wa Mungu, Mungu anakawaida za kujifunua kwa majina tofauti tofauti duniani mfano Niko ambaye Niko alijifunua kwa Musa, Yehova na ndiyo maana biblia inasema mahali kuwa ” kwa Jina hilo hakujifunua mwanzo” Mungu ni Mungu wa Nyakati na majira! na kwwa kujifunua huko hakumaanishi kuwa nafasi yake mbinguni haipo na ndo maana Yesu akawa anasema kuna Baba aliyenituma ndio maana ya tafsiri ya neno EMMANUEL(Mungu pamoja nasi) barikiwa

        Like

      • dotto says:

        Bwana David Mgongolwa huu utata hautaisha Yohana 20.17 inatosha mbona, yesu alipoenda kujaribiwa na iblisi alijiita mwanadamu yaan mtu haishi kwa mkate tu. Mungu kamuita Yesu ni mwana wa Adamu yohana 5.25-27, kwan hujui kwamba Yesu katumwa na mungu ktk Yohana 17.3? mbona mabo yapo wazi weweee unaangaika nn? yohana 1.1 ni falsafa tu kama ni kweli mbona inapingana na aya kadhaa mfano nilizo taja hapo?

        Like

  2. Kashmir bashir says:

    ninachojua mimi ni kuwa yesu ni mwana wa mungu kwakupitia yeye tutamwona mungu ,na kwakupigwa kwake sisi sote tumepona.

    Like

    • mosespk says:

      kama yesu ni mwana wa Mungu, Je unaichukulia vipi Tito 2:13 iliyosema yesu ni Mungu mkuu na Mwokozi wetu, pia Isaya 9:6 Naye ataitwa Mungu mwenye nguvu. haya maandiko unayajuaje, unaweza kutueleza kwa upana zaidi. asante sana kashmir hapa tunataka watu wamjue Yesu vizuri ili wasiwe wanababaishwa na watu waitwao katika Biblia wataabishaji.

      Like

  3. fabian hosea says:

    Mh hii mada mziki waake mnene bwana,

    Like

  4. Kashmir bashir says:

    kila mtu aaminiye kwamba yesu ni kristo amezaliwa na mungu.na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa,ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye.

    Like

  5. Yvone Squire says:

    I simply want to mention I am just new to blogs and truly liked your web-site. Likely I’m want to bookmark your blog . You actually have really good articles and reviews. Thanks for sharing your webpage.

    Like

  6. Noemi Salvey says:

    The U-Detroit loss and losing to Illinois in their first game in the Big Ten tournament doomed Michigan, I would have hated to be near Borseth when that selection show finished. It sucks that we got swept by them this year but at the end of the day, we are dancing and they are going to the NIT.

    Like

  7. And even now you apparently act as an internationalist No Tarrifs again constitutuional [READ IT] and you beliee in allowing foreign parasites in when we cannot take care of our own, and allow the congress and senate to take foreign bribes.

    Like

  8. I just want to say I’m very new to blogs and certainly enjoyed you’re web blog. Most likely I’m want to bookmark your blog post . You really have terrific writings. With thanks for revealing your web-site.

    Like

  9. Magnificent goods from you, man. I’ve understand your stuff previous to and you’re just extremely fantastic. I really like what you’ve acquired here, really like what you are stating and the way in which you say it. You make it enjoyable and you still take care of to keep it wise. I can’t wait to read far more from you. This is actually a great site.

    Like

  10. logon says:

    So many positive comments here you’ve got. Your site seems to be quite busy.

    Like

  11. I have 5 brilliant Halloween costume ideas this year, but nowhere to go. Save me from having to get all dressed up just to strut through Safeway. This event would be perfect!

    Like

  12. Please explain to us further these posts so we can examine it.

    Like

  13. I keep listening to the news bulletin talk about receiving boundless online grant applications so I have been looking around for the most excellent site to get one. Could you tell me please, where could i get some?

    Like

  14. I believe that avoiding refined foods may be the first step to be able to lose weight. They will often taste excellent, but packaged foods contain very little vitamins and minerals, making you eat more simply to have enough electricity to get with the day. When you are constantly eating these foods, transitioning to whole grain products and other complex carbohydrates will assist you to have more electricity while ingesting less. Interesting blog post.

    Like

  15. Mpoki mwaki wa baba Groly says:

    Wengine wassema nabii,wengine mtume,wengine mwana wa Yoseph,wengine eliya mtishibi,Je na nyie mwasemaje?Petro wewe ni Yesu mwana wa Mungu aliye hai,oooooh Petro si wewe wala kwa ufahamu wakoila Mungu wa mbinguni amekufunulia haya,.

    Like

  16. frylnrind says:

    All trace holidays to March 8!!!

    Like

  17. Amani iwe kwako Moses,Naona rafiki yangu umeshikiIia sana andiko Ia tito 2:13..msemaji ni pauI…kumsemea Yesu km ifatavyo..
    Tito 2:13 “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu

    Je ni kweIi Yesu ni Mungu mkuu?hapana kwa ushahid huu wa maneno yake Yesu….
    Yohana 14:27..Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.

    Yesu anasema kwa maana Baba(Mungu) ni mkuu kuIiko yeye..kwahyo Yesu hawezi kuwa Mungu kwasababu anaye Mungu(baba) wake.

    Kuhusu “Mwana wa Mungu”
    Katika zama za wayahudi neno Mwana wa mungu maana yake ni mcha Mungu au mtu wa Mungu au mtumishi wa Mungu…kwasababu si Yesu tu pekee aIiyeitwa Mwana wa Mungu wapo wengi tu km ifwatavyo:

    2 Samweli 7:13-14, Mungu anamwita Nabii Suleimani Mwanawe, “Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele. Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu…”

    Malaika wanachukuliwa kuwa ni “wana wa Mungu” katika kitabu cha Ayubu 1:6, “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao”.

    Na km hamtokubaIiana na maneno yangu kuhusu mwana wa Mungu..naomba muIifkirie na andiko hiIi….

    Zaburi 89:26-27: “Yeye ataniita, Wewe baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu. Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.”

    Mungu ananukuliwa akimwambia Mtume Daudi, katika Zaburi 2:7, “Nitaihubiri amri, BWANA aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.”

    Mungu hawezi kuwa na mwana…kwa maana hyo ya kumpa umungu mwana kwasababu yeye ni mwana wa mungu..kwa fikra hzo basi manabii wte nao wana sifa za Mungu au ni Mungu..km daudi…suIeiman(soIomon), Ayubu na maIaika.

    Ahsante.

    Like

  18. TUKITAKA KUJUA KAMA YESU NI MWANA-WA-MUNGU AU MWANA-WA-ADAMU(kama mimi na wewe) LAZIMA TUMUULIZE YEYE MWENYEWE WALA SI PAULO KUMSEMEA.
    1.YESU NI MWANA WA ADAMU
    Mathayo 11:19 ” Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa……”
    Mathayo 12:40 “….hivi ndivyo mwana wa Adamu atakavyokuwa kwa siku tatu……”
    Mathayo 8:20 “…..lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake”
    Mathayo 9:6 “…lakini mpate kujua ya kwamba Mwana Wa Adamu anayo amri duniani….”
    JAMANI HAYO NI MANENO YAKE MWENYEWA ANAJIITA MWANA WA ADAMU.2

    2.NINI MAANA YA MWANA WA MUNGU?
    Mungu hazai bali Anaumba kwa hiyo hana mwana wa kumzaa.
    Mwana wa lina maanisha “mtukufu wa Mungu” wala si kama wakiristu wanavyodai kuwa Yesu ni Mwana pekee wa Mungu.
    kutoka 4:22`”Bwana Mungu asema Israeli(Yakobo) ni Mwanangu, mzaliwa wa kwanza Wangu”
    Yeremia 31:9 “Bwana asema, na ……Efraem ni mzaliwa wa kwanza wangu…”
    yohana 20:17 “…..enenda ukawaambie ndugu zangu, napaa kwenda kwa Baba, kwa kuwa Baba yangu ndiyo Baba yenu na Mungu Wangu ndiye Mungu wenu” kwa hiyo hta wewe ni mwana wa Mungu kwa Mujibu wa Bwana Yesu.

    Like

  19. M. J. N. Siyi says:

    Masaudi, hivi Alla ni Mungu? Unaweza kubainisha sifa za Alla kuwa ni Mungu? Hebu ondoa mtanziko wa mawazo huu maana mimi najua Alla siyo Mungu….. Nitafurahi kusikia kutoka kwako.
    siyimnn@yahoo.com kunipata kirahisi zaidi

    Like

    • umm suleym says:

      Ndugu, M.J.N Siyi,
      Nakushukuru sana kwa kutaka kwako kujua kwamba Allah ndiye Mungu; Kwa ujumla neno Allah ni la Kiarabu likiwa na maana Ya Mungu, kwani angalia hata biblia za kiarabu zimelitumia. Lakini naamini swali lako ulitaka kujua kuwa je Mungu wa waislam ni Mungu wa kweli?
      Kwanza kabisa ili kujua Allah wa waislam kama ndiye Mungu wa kweli ni lazima kwanza
      tuzijue ni zipi sifa za Mungu wa kweli alafu kwa kutumia ushahidi wa Quran tuone kama je
      Allaha wa waislam anazo?
      zifuatazo ni sifa anazotakiwa kuwa nazo Mungu wa kweli.
      1.Mungu mmoja,2.Mungu hakuzaa wala hakuzaliwa,3.Mungu hafi/ana uhai wa milele,4.kaumba mbingu na aridhi, 5.Mungu haonekani 6.kaumba kifo ila hafi.

      1.MUNGU MMOJA NA HAKUZAA WALA HAKUZALIWA
      quran sura 112:AL-IKHLAS
      “1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu(Allah) ni wa pekee.
      2. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
      3. Hakuzaa wala hakuzaliwa.
      4. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.”
      Hapo nimenakili sura nzima Allah mwenyewe anavyojitambulisha.

      2.ALLAH ANA UHAI WA MILELE WALA HAFI
      quran sura 2:255;AL BAQRA
      “Mwenyezi Mungu(Allah) – hapana mungu ila Yeye Aliye hai milele, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni
      na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake?
      Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika
      vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni
      na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na
      ndiye Mkuu.”

      3.ALLAH KAUMBA MAUTI NA KAUMBA MBINGU NA ARDHI
      quran sura 67;AL MULK
      “1. AMETUKUKA (Allah)ambaye mkononi mwake umo Ufalme wote; na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.
      2. Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni ni nani miongoni mwenu mwenye
      vitendo vizuri zaidi. Na Yeye ni Mwenye nguvu na Mwenye msamaha.
      3. Aliye umba mbingu saba kwa matabaka. Huoni tafauti yoyote katika uumbaji wa
      Mwingi wa Rehema. Hebu rudisha nadhari! Unaona kosa lolote?”

      4.ALLAH KAUMBA KILA KITU
      Quran sura 23:AL MUUMINUN
      “12. Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
      13. Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
      14. Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la
      nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama.
      Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa
      waumbaji.
      15. Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
      16. Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.”
      Ndugu wakiristu sifa za Allah ni nyingi mno hapa nimezieleza chache tu, ila kadiri mtakavyouliza nitaweza kujibu inshaallah!

      Like

  20. Yesu ni mwana wa Mungu naye ni Mungu yeye ni yote katika Yote! Tena ni jia iendayo uzimani!

    Like

  21. Dickson J.I says:

    Wapendwa na watumishi wa BWANA WETU YESU KRISTO, naomba kusaidiwa kuhusu utatu mtakatifu
    -imeandikwa “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani.Mara alipopanda kutoka majini,akaona mbingu zinapasuka,na ROHO,kama hua, akishuka juu yake; na sauti ikatoka mbinguni, We ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”
    INAKUWAJE KAMA NI MMOJA KUONEKANA NA KUSIKIKA KWA PAMOJA?

    Like

    • Dickson Kamugisha says:

      Mpendwa Dickson J.I

      SIRI YA UTATU MTAKATIFU NI FUMBO LA MUNGU(1 TIMOTHEO 3:15)

      Hakuna anayeweza kufumbua hili fumbo zaidi ya Roho Mtakatifu.
      1wakorintho 2:10 “…..Maana Roho huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu”
      UTATU MTAKATIFU ni fumbo la utendaji kazi wa Mungu.Yohana 1:1,14
      inamfunua Yesu kama Mungu lakini pia kama Neno.Kwahiyo Mungu amefunuliwa
      kama Neno na pia kama Yesu.NENO ni Yesu na Yesu ni Mungu.

      ISAYA 9:6 inamfunua Yesu kama Mungu mwenye nguvu,Baba wa milele,mfalme wa amani
      na mshauri wa ajabu.

      TITO 2:13 inamfunua Yesu kama Mungu mkuu na mwokozi wetu.

      Kwa mistari hii michache tunaweza kuona wazi kwamba Yesu ambaye ni Mungu mkuu tena
      mwenye nguvu anajifunua kama Neno.

      Aliposema nitamtuma Roho Mtakatifu ambaye ni msaidizi hilo pia ni fumbo!
      Kwasababu Roho Mtakatifu anaitwa ROHO WA MUNGU na pia anaitwa ROHO WA KRISTO.Kwahiyo ni Roho ya Yesu ambaye ni Mungu.

      HITIMISHO
      Yesu ni yote katika yote.Ni hekima ya neno la Mungu.Ni Roho Mtakatifu.
      Baba,Mwana na Roho Mtakatifu ni umoja!Yaani ni Mungu aliye hai
      ambaye anaitwa Yesu.1 YOHANA 5:8 inasema “MAANA WAKO WATATU WASHUHUDIAO MBINGUNI, BABA, NENO, na ROHO MTAKATIFU NA WATATU
      HAWA NI UMOJA.Ni umoja wa hekima ya utendaji kazi wa Mungu ambaye ni Yesu.
      Yesu anataka tujue jinsi ya kutofautisha katika kulitumia jina la BABA, jina la MWANA,
      na jina la ROHO MTAKATIFU.Matumizi ni tofauti lakini mamlaka ni ile ile ya Yesu.
      Bila ya Upako(mafuta) wa Roho Mtakatifu unaotufunulia habari za mambo yote,
      UTATU MTAKATIFU utabaki kama fumbo lisilo fumbuliwa(1 YOHANA :20,27)

      Huu ni mtaji wa wewe kuendelea kumshika Roho Mtakatifu ili akufundishe na kukufunuli
      zaidi jinsi hekima ya UTATU MTAKATIFU inavyotenda kazi.Soma kwa kutafakari YOHANA 17 yote.

      UBARIKIWE SANA MTUMISHI.

      Like

  22. Taysir says:

    Kwanza niwaulize nyinyi Wakristo,kama Yesu ni Mungu kwa hiyo waizrael waliishi na Mungu?
    Kama Yesu ni mwana wa Mungu kwa hiyo Maria ni mke wa Mungu?
    Chanzo cha Yesu kuja Duniani ni imani sawa kwa wote waislam na wakristo,alikuja na miujiza roho mtakatifu kwa Maria kumpatia mtoto ambaye ni huyo Yesu.
    Sisi waislam tunamjua Yesu na tunamuamini Yesu,Tatizo lenu nyinyi wakristo hamumuamini Muhammad.
    Yesu ni mtume wa Mungu na wala sio Mungu na wala sio mwana wa Mungu.
    Qur-an inamzungumzia Yesu hivi…
    (61:6 Na Isa bin Mariamu(Yesu) alipo sema: Enyi Wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, ninaye thibitisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na mwenye kubashiria kuja Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad! Lakini alipo waletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhaahiri! ).
    Sasa wewe uliekuwa humuamini Muhammad acha tu useme Yesu ni Mungu kwa sababu Muhammad humuamini eti kisa ni Muarabu,na dini ya Kiislam ni Imani ya waarabu?..weweeee….Hakika siku ya mwisho utamjua Mungu wa kweli.
    Mungu ni Yule aliyeiumba Ardhi na mbingu na vilivyomo ndani yake kwa muda wa siku 6.)Nyinyi wakristo muna Waungu wengi.Sisi waislamu tuna Mungu mmoja tu,na Mitume 25 ambayo wa Kwanza ni Adam…….wa 24 ni Issa(Yesu) na wa mwisho(wa 25) ni Muhammad.

    Like

  23. StephanSmall says:

    I have checked your site and i have found some duplicate content, that’s why you don’t rank high in google, but there is a tool that
    can help you to create 100% unique content, search for; Boorfe’s tips unlimited content

    Like

Leave a comment