ISLAMIC vs. CHRISTIANITY

Welcom on this page, here we will be discussing bout Islamic and Christianity, please let learn what is the real way to God between these two way.
=========================================================

Karibuni katika ukurasa huu, tutakuwa tukizungumza kuhusu uislamu na ukristo ni ipi njia sahihi ya kwenda kwa Mungu, Tafadhali njoni tujifunze.

485 Responses to ISLAMIC vs. CHRISTIANITY

  1. Rev.Forcus Rutaba says:

    Ninafurahi kusikia habari hii, ila nikuombe unapofundisha jambo hili jitaidi kuzama zaidi maana shetani amewateka wakristo wengi kwa kuwalaghai kwa kutumia mali, ambazo zimeonekana kuchanganya wengi. Kuna msemo wa vijana siku hizi wanautumia wakisema ” Ni heri kuishi maisha mafupi yenye raha kuliko maisha marefu yenye taabu”! Sijui wewe ndugu huko unakoishi mambo yakoje, maana taabu tuliyo nayo sasa ni suala la mali. Ninaomba kujua hayo makanisa mnayo saidia kuyaanzisha ni utaratibu upi unatumika? Lakini pia kulingana na maelezo niliyoyaeleza hapo juu tunaitaji kuhubiri injili ya kweli ili watu wa Mungu wapone. Asanteni kwa kunipa nafasi ya kutoa maoni yangu

    Bwana awabarikie huduma hii!!
    Rev. Forcus Rutaba.

    Like

    • FRANCIS VII says:

      Ndugu Rev. Forcus Rutaba- Jibu hili hapa
      (01).”shetani amewateka wakiristo wengi” hyo ni kweli kabisa ndg yangu wakiristo rafiki yao shetani.
      NI SAWA NA MAFUNDISHO YA QURAN TUKUFU
      QURAN 58:
      “19. Shetani amewatawala na akawasahaulisha kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Hao ndio kundi la Shetani. Kweli hakika kundi la Shetani ndilo lenye kukhasirika.
      20. Hakika wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hao ndio miongoni mwa madhalili wa mwisho.”

      (02). ” Ni heri kuishi maisha mafupi yenye raha kuliko maisha marefu yenye taabu” wakiristu wengi wanaitumia kauli hii ya kukata tamaa na maisha ni kama Allah Anavyobainisha ndani Ya Quran.
      ALLAH ANASEMA KATIKA QURAN TUKUFU
      QURAN 29:23
      “Na walio zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu (yaani wakiristu) na kukutana naye, hao ndio wenye kukata tamaa na rehema yangu, na hao ndio wenye kupata adhabu chungu.”

      (03) “Ninaomba kujua hayo makanisa mnayo saidia kuyaanzisha ni utaratibu upi unatumika?”
      JIBU LAKE: Utaratibu unaotumika ni wa shetani aliyelaaniwa. KIVIPI SASA? FUATANA NAMI.
      Mark 8:33 ” Yesu akamwambia Petro ” Petro nenda nyuma yangu shetani (wewe)
      u-kikwazo kwangu kwa maana huyawazi ya Mungu bali Ya wanadamu”
      Mathayo 16:16 Yesu akamwambia petro ” wewe u-mwamba na juu ya mwamba huu
      nitalijenga KANISA” YAANI KANISA JUU YA MWAMBA (SHETANI PETRO)
      Mathayo 13:38 Yesu akamwambia Petro”Amin! Amin! kabla ya jogoo kuwika asubuhi
      utanikana mara tatu” HUYU ALIYEMKANA YESU KANISA LASTAHILI KUJENGWA JUU YAKE?
      MAKANISA NI YA SHETANI NDO MAANA YAPO KIBIASHARA ZAIDI! WACHUNGAJI WANAISHI MAISHA YA KIFAHARI NA WAUMINI WANA MAISHA YA UMASIKINI KUPINDUKIA. JE HAYO NI MAFUNDISHO YA BWANA YESU? AU MAFUNDISHO YA KUBUNI KUTOKA KWA WATU WAOVU KAMA AKINA PAULO NA PETRO.?

      Like

      • kelvin hussein says:

        QURAN 1:-2 IMEANDIKWA NANUKUU QURAN IMETEREMSHWAKWA AJILI YA WATU WASIOONYWA NA BABA ZAONA WEWE PIA UMO

        Like

      • KELVIN says:

        UWE NA AKILI KIDOGO PETRO ATAKUWAJE SHETANI YESU ALIKUWA ANAMFUKUZA SHETANI ASIMKARIBIE PETRO NDIO MAANA TUNAPOKEMEA MAPEPO TUNAMWULIZA YULE MTU MWENYE MAPEPO WEWE NI NANI? ILI TUWEZE KUJUA KAMA YUPO KATIKA HALI YA KAWAIDA AU AMEPOTEZA UFAHAM, NA WEWE NAONA UMEPOTEZA UFAHAM UMEPAGAWA NA MAJINI NAKUKEMEA NENDA NYUMA YANGU SHETANI KATIKA JINA LA YESU WE UNAFIKIRI YESU HANA AKILI? ATAMPAJE SHETANI AONGOZE KANISA NYINYI MASHETANI NDIO NDUGU ZENU MNASALI NAYO

        Like

      • KELVIN says:

        HUATAKIWI KUOMBA MASOHABA WALA WATAKATIFU WOWOTE WALOKWISHA KUFA WALA WALIO HAI AYUBU 5:-2

        Like

      • Luckey Sangah says:

        Francis unayo ongea ni kwa akili yako lakini roho wa ukweli aakisha ingia ndani yako aki kinywa yako itabaki wazi na uchunge jehanamu yakungoja
        LUCKEY-KENYA

        Like

      • leonce says:

        umesha laaniwa kwa kuhubiri Injili nyingine! Hujui hata sasa kwamba mawazo ya Petro yalikuwa kama ya waisilamu hadi leo kwamba hawata kuua wala kukusulubu?! Hivyo rudini nyuma hamuwazi ya Mungu Bali MNA mawazo ya shetan!¿

        Like

      • ALANUS RESPICIUS says:

        USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA. NENDA UENDAKO, FIKIRI UWEZAVYO NA SHAWISHI UWEZAVYO, KANISA LA KWELI NI WEWE MWENYEWE, YESU MWENYEWE ALISEMA, ‘MTU AKIDHANI ANAYO DINI WAKATI HAJALI WAJANE NA YATIMA, DINI YA MTU HUYO IMEKUFA’ YESU HAKUFUNDISHA WALA KUSEMA TUSALI DINI GANI, ALIHITAJI TUWE NA MOYO WA KUTUBU, HIVYO JAMAA YANGU, UKITUMIA MDA WAKO KUNYOSHEA KIDOLE WATU WENGINE UKIWAHUKUMU KWA DINI ZAO UTAKUWA UNAKOSEA NA UTAKUWA UNAISAHAU NAFSI YAKO. KUHUKUMU SIYO KAZI YAKO, FANYA YAKO HUKUMU MUACHIE MUNGU MAANA UWE MWISLAMU AU MKIRISTO HAISAIDII KITU CHOCHOTE, FANYA NA TENDA KADRI IMANI YAKO INAVYOKUONGOZA. MUNGU ANAFUNDISHA UNYENYEKEVU NYIE WAISLAM MNAFUNDISHA NINI? UTAJIRI NI HAPA DUNIANI NA USIDHANI WEWE UNA CHAKUMPA MUNGU MAANA HATA WEWE MWENYEWE NI WAKE. INAONEKANA MUNAONGEA UBINADAMU, YESU HAKUMANISHA PETRO NI SHETANI ILA ALIONA KUWA SHETANI ANAANZA KUMSHAWISHI. UISLAMU WENYEWE UMEANZA MIAKA MIASTA NA ISHIRINI BAADA YA YESU KUTOKA DUNIANI.

        Like

      • Rom says:

        Hakika huyajui maandiko, nikurejeshe tu katika kitabu chako Surah Al Hijr 39 utapata majibu

        Like

      • Aida mwakalinga says:

        Shetani alijaribu kumtumia petro kudhoofiasha lile Yesu alilokuja kufanya yaan kufa kwaajili yetu ndipo Yesu akamkemea shetani aliye kuwa ndani ya petro,
        Lakini anaposema juu ya mwamba huu, ni yeye mwenyewe yesu, juu yake litajengwa kanisa, kupitia petro kwani ata ukiangalia maana ya petro ni jiwe sio mwamba

        Like

      • Raban says:

        Hutakuja kuelewa biblia kwa staili yako.
        Biblia imeandikwa kwa context, lakini quran imeandikwa bila context, kwahiyo kabla hujachukua andiko kama lilivyo tafuta context ya Yesu kuzungumza hivyo nini context behind that!
        Biblia inasema andiko lauwa ila roho ndiyo itiayo uzima, hata shetani anatumia maandiko hayohayo kuwadanganya watu wa Mungu kama vile alivyomdanganya Adam na Eva, kwahiyo wewe usimuige Shetani kutumia maandiko bila kujua context behind.

        Like

  2. Bwana Yesu apewe sifa Mtumishi, kwa kweli namshukuru Mungu maana ananisaidia sana na pia anawasaidia watu wengi kupitia kwangu, hii Injili ya pesa mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kwanza kuipigia kelele katika mtandao wa Strictly Gospel. nilikuwa nikikemea sana wahubiri na waimbaji waliotumia Neno la Mungu kama sehemu ya Biashara. Hata hivyo waimbaji na waandaji wa matamasha ya waimbaji walinipinga vikali wakidai kwamba kuimba ni kazi kama kazi zingine, basi waliponiambia hivyo nikakaa kimya maana nilitambua ya kwamba hawa hawana nia ya kufanya kazi ya Mungu bali ni Biashara katika kazi ya Mungu.
    Kuhusu makanisa tunayoanzisha tunayaanzisha katika msingi wa pentecoste, hivyo tunaamini kwamba Mungu anaweza kufanya miujiza, tunaamini kunakiyama, tunaamini Jehanamu ipo na mbigu ipo. hivyo hatuna tofauti na makanisa mengine ya Mungu. Kuhusu Mali sisi tunaamini Mungu anaweza kukubariki kuwa na mali, lakini sio lazima kila mwenye kuamini atakuwa na mali. asilimia kubwa waaminio hawana mali na ndio maana sisi waaminio tunadhiki kila iitwayo leo. Bwana akubariki mtumishi.

    Ev.Moses Mayila
    New Hope Ministry Tanzania

    Like

  3. Daniel Mwankemwa says:

    HIVI UNAJUA KUWA MAJINI (MASHETANI )NI NDUGU ZA WAISLAMU? (JINNIE (EVIL SPIRITS) HAVE SPIRITUAL RELATION WITH MUSLIMS)

    UTANGULIZI:
    Majini ni viumbe visivyoonekana kwa macho ya kawaida ya wanadamu. Hii ni kwa sababu viumbe hivi viko katika asili ya roho ya kutokuonekana. Majini huitwa pia Ibilisi, Shetani, Pepo mchafu au Joka la zamani.

    ASILI YAO:
    Majini yalikuwa ni malaika kabla ya kuungana na yule Muasi Mkuu wa Mungu, yaani Lucifer aliyemuasi Mungu mbinguni na kutaka ukubwa wa kufanana na Mungu, na ndipo akatupwa huku duniani yeye pamoja na malaika zake, na huku wakiwa wamenyang’anywa utukufu waliokuwa nao hapo awali. Vita hiyo iliongozwa na Malaika Mkuu wa Mungu wa Mbinguni yaani Jehova kumtupa chini huyo malaika muasi pamoja na malaika zake. Viumbe hivyo vilivyotupwa ndivyo leo vinavyoitwa MAJINI au MASHETANI au PEPO WACHAFU au IBILISI au JOKA LA ZAMANI.

    Uf. 12:7-12 “ Kulikuwa na vita mbinguni, Mikael na Malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake, nao hawakushinda, wala mahala pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa yule mkubwa nyoka wa zamani aitwaye Ibilisi na shetani audanganyaye ulimwengu wote, akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema sasa kumekuwa wokovu, na nguvu na ufalme wa Mungu wetu kwa maana ametupwa chini mshtaki wa ndugu zetu yeye awashtakiye mbele za Mungu wetu. Mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo na kwa neon la ushuhuda wao ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. Kwa hiyo shangilieni enyi mbingu, nanyi mkaao humo. OLE WA NCHI NA BAHARI! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”

    Hivyo kwa mistari au aya hizo unaanza kupata taswira ya kile tunachijifunza kuliusiana na majini.

    Ki- Biblia Malaika ni viumbe walio katika hali ya roho ila wanaweza kuonekana kwa umbile la mwanadamu Mw. 18:1-18, Lk 1:26-28, Kut 3:1-6

    Katika Ebr 1:13-14 “ Yuko Malaika aliyemwambia wakati wowote uketi mkono wangu wa kuume hata nitakapowaweka adui zako chini ya nyayo zako? Je, hao si ROHO watumikao wakitumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
    Biblia inazidi kubainisha namna ya kuumbwa kwao
    Mw. 2:1 “ Basi mbingu na nchi zikamalizika na JESHI LAKE LOTE”

    Ni katika jeshi hilo ambapo tunawapata hawa viumbe vya kiroho.

    Na katika Kol 1:1:16 “ kwa kuwa katika yeye vitu viliumbwa vilivyoko mbinguni na vilivyo juu ya nchi. Vinavyoonekana na visivyoonekana……”

    Jeshi hilo ni huru linaweza kujiamulia lolote na ndiyo maana 1/3 ya hao roho yaani malaika waliasi na kufanya machukizo mbele za Mungu na wakafukuzwa (Uf 12:7-12) na wengine wamefungwa.

    Katika Yuda 6 “ Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu amewaweka katika vifungu vya milele chini ya fiza kwa hukumu ya siku ile kuu”

    Tunasoma pia katika 2 Petro 2:4
    “ Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni akawatia katika vifungu vya giza walindwe hata ije hukumu”

    kwa hiyo Majini ndiyo mashetani na mashetani ndiyo majini.Katika kitabu Lawi 17:7

    “Wala hawatatoa tena sadaka zao kwa wale MAJINI ambao huwafuata ili wafanye uasherati nao, sheria hii itakuwa sheria ya milele kwao kizazi baada ya kizazi”.

    Kwa sababu majini hayo tangu yalipotupwa toka mbinguni wana wa Israel hawakuwa na ufahamu wa kutosha kuyahusu baadhi yao walijikuta wakiyatolea sadaka huku wakiamini kuwa wamemtolea Mungu sadaka. Na kumbuka kuwa mara nyingi wana wa Israel walipotoa sadaka zao nyingi zilikuwa za wanyama na hivyo kutakiwa kuchinja na kutoa damu ambayo ni sehemu kubwa ya chakula cha majini.

    Katika Zaburi 106:34-40.

    “ Hawakuwaharibu wtu wa nchi kama BWANA alivyowaambia, bali walijichanganya na mataifa wakajifunza matendo yao, wakazitumikia sanamu zao nazo zikawa mtego kwao naam walitoa wana wao na binti zao kuwa dhabihu kwa MASHETANI wakamwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana wao na binti zao walio watoa dhabihu kwa sanamu za Kaanani. Nchi ikatiwa unajisi kwa damu.

    Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao, wakafanya uasharati kwa matendo yao. Hasira ya Bwana ikawa juu ya watu wake akauchukua urithi wake.

    Hivyo kutokana na kutokuonekana kwao hayo majini yaliwahujumu wana wa Israel hata yakawasababishia wamwasi Mungu kwa kuyatolea sadaka kinyume cha Mungu wa mbinguni aliyehai.

    Katika Kumb. 32:17-20.
    “ walitoa sadaka kwa Pepo si Mungu, kwa miungu wasioijua, kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu ambayo baba zetu hawakuiogopa,
    Humkumbuki muumba aliyekuzaa Mungu aliyekuzaa humkumbuki. Bwana akaona akawachukia kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake. Akasema nitawaficha uso wangu nitaona mwisho wao utakuwaje maana ni kizazi cha ukaidi mwingi watoto wasio Imani ndani yao.

    Pia katika Math 12:43-45

    “ Pepo Mchafu amtokapo mtu hupitia mahali pasipo maji akitafuta mahali pa kupumzikia asipate. Halafu husema nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka hata akifa aiona tupu imefagiwa na kupambwa, mara huenda akachukua pamoja naye pepo mengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo, na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza.

    Katika Biblia tunaona kipindi Yesu alipotwaa mwili na kuja duniani, hao majini, au mashetani au Ibilisi au Mapepo wachafu yalimfahamu na yalianza kulalamika mbele zake.

    Math 8:28-31 “ Naye alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo (Majini) walikutana naye, wanatoka makaburuni wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama wakapiga kelele wakisema tuna nini nawe mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya muhula wetu………………. (MK 5:1-9).

    Majini hayo yanafahamu kuwa Yesu ndiye atakayewahukumu ila yalichoshangaa ni kwamba mbona amewahi kabla ya kipindi chenyewe cha yeye Yesu kuyahukumu kwenda Jehanamu ya Moto?

    Yesu alikuja duniani ili kumwokoa mwanadamu kutokana na mateso ya hayo majini au mashetani kwa sabahu katika Uf. 12:12 Malaika Mikael alipokuwa anawafukuza hao malaika waasi yaani hao majini au mashetani alisema OLE WA NCHI NA BAHARI ndiyo maana Yesu ilibidi aje duniani kupambana na huyo shetani, Joka, Ibilisi kwa niaba yetu maana sisi tusingeweza na wale, majini walisema kumuambia Yesu ukitutoa tuache tukawaingie nguruwe na ngurume wale wapatao 2000 waliona bora kufa baharini kuliko kuishi na viumbe hivi majini au mashetani miilini mwao na hivyo kutimiza ujumbe wa malaika Mikaeli “ Ole wa nchi na bahari”. Baharini ni sehemu mojawapo ambapo majini huishi.

    Unabii wa kuangushwa mji mkubwa uliojisifu sana (Babeli) ulipotolewa, ilitabiriwa kuwa, hayatakuwa tena makazi, bali patabaki yatafanya makazi huko.

    Isaya 13:12. lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani na nyumba zao zitajaa bundi, mbuni watakaa huko, na majini atacheza huko.

    Ndipo tunaposoma katika Yoh 12:31, Yesu anasema “ sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo, sasa Mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”.

    Na katika 1 Yoh 3:8
    “ atendaye dhambi ni wa Ibilisi kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi mwana wa Mungu alidhihirishwa ili azivunje kazi za Ibilisi.

    Kama tulivyosoma toka sura na aya mbalimbali ndani ya Biblia kuwa majini hayo yanasubiri adhabu Biblia inatueleza atakaye yahukumu.

    Math 25:31, 41 “ Hapo atakapokuja mwana wa Adamu pamoja malaika watakatifu pamoja naye…………… Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto ondokeni kwangu mliyolaaniwa mwende katika moto wa milele aliyowekewa tayari Ibilisi na malaika zake”.

    Hivyo kwa mujibu wa Biblia Majini yaani mashetani ni Adui yetu na ndiyo maana alipokuja Mohammad yalianza kukanusha kuwa Mungu hana mwana ili kuwavuruga waislamu wasiijue kweli (Soma Quran 112:1-4, Al- Kahf, 18:3) ya kumwamini mwana wa Mungu Yesu.

    Kwa bahati mbaya sana mambo yahusuyo majini katika imani ya Kiislamu ni tofauti sana na vile tulivyosoma katika Biblia. Ingawa Quran na Hadithi za Muhammed, Mtume wa Waislamu, Vinatutaka sisi wakristo tumwamini allah S.W. mungu anayeabudiwa na Waislamu Misitikini.

    Katika Suratul Waqia 51:56.

    “ Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu” katika Quran Suratul Al- Ankabut (Buibui), 29:46-47) “ Wala msibishane na watu waliopewa kitabu (kabla yenu) ila kwa yale (majadiliano) yaliyo mazuri isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao na semeni tunaamini yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwenu na Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja nasi ni wenye kunyenyekea kwake”.

    Waliopewa kitabu kwa mujibu wa Quran ni Wayahudi na Wakristo. Je, hoja kuwa Mungu wetu na Mungu wao wanayemwabudu kuwa ni mmoja je ni sahihi?. Tuchunguze kuhusiana na mafundisho ya Allah S.W. wa misikitini kuhusu majini ndipo tutajua ni mmoja au la!.

    Muislam yeyote ili imani yake ikamilike ni lazima aamini yanayoonekana na yasiyoonekana katika Suratul Al- Baqarah (Ng’ombe Jike la Njano), 2:1-3.

    “ Alif Lam Mym. Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake ni uongozi kwa wamchao mwenyezi Mungu ambao huyaamini yasiyoonekana (maadaam) yamesemwa na mwenyezi Mungu na Mtume wake) husimamisha sala na hutoa katika yale tuliyowapa.

    Quran peke yake ukiichunguza utaona kuwa majini yamechukuliwa kama ni viumbe tofauti na mashetani, wanasema hivyo kwa sababu katika uislamu majini yamepewa hadhi kubwa sana na ya kipekee. Hadhi hiyo ni kwa sababu majini waliamini Quaran.

    Tusomapo katika Quran Suratul al- Ahqaf, (Kichuguu cha mchanga) 46:29

    “ Na (wakumbushe) tulipokuletea kundi la majini (kuja kwako) kusikiliza Quran. Basi walipoihudhuria walisema (kuambiana):- “ Nyamazeni (msikilizeni maneno ya Mwenyezi Mungu)” Na ilipokwisha (Somwa) walirudi kwa jamaa zao wakiwaonya”.

    Na ndani ya Quran kuna sura nzima inayoitwa sura ya majini (Mashetani) hiyo ni sura ya 72. katika sura hiyo inasema 72:1-3, 14. “ Sema: imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini liliisikia (Qurani) likasema hakika tumesikia Qurani ya ajabu inaongoza katika uongofu. Kwa hivyo tumeiamini wala hatutamshirikisha yoyote tena na Mola wetu na kwa hakika utukufu wa Mola wetu umetukuka kabisa. Hakujifanyia mke wala mwana……………………. Nasi wamo miongoni mwetu na wamo miongoni mwetu waliokengeuka waliosilimu hao ndiyo waliotafuta uwongofu.

    Kwa hiyo aya hizi zinaonyesha kuwa Quran ilipokuja ndipo majini waliposilimu. Kumbuka kuwa Quran imeanza mwaka 610 B.K kipindi ambacho Biblia tayari ili kuwepo kwa karibu karne 6.

    Akifafanua asili ya majini Mwanazuoni mkubwa wa kiislamu aitwaye Abdalllah Saleh Farsy aliye kuwa Kadhi Mkuu Zanzibar, kisha akawa Kadhi Mkuu Kenya katika kitabu alichoandika kiitwacho “ Maisha ya Nabii Mohammad” ule Uk. 31 anasema “ Katika safari yake ya kurejea Taif ndipo walipomjia majini wakasilimu kama inavyoonesha haya katika Suratul Jinn. Majini ni viumbe vyepesi vinavyokaa angani. havina viwiliwili kwa hiyo haviwezi kuonekana na wanadamu ila vinapojibadili kwa umbo lenye kiwiliwili. Na vina uwezo huo wa kujibadili kwa sura ya kuweza kuonekana. WAO NA MASHETANI WANA ASILI MOJA. Kwa hiyo asili ya majini ni shetani.

    Suala linalohusu malaika linawasumbua sana waislam hata hawana uhakika wake.

    Tumesoma ndani ya Biblia kuwa kuna kundi la malaika waliokosa ambao ndiyo wanaoitwa majini lakini tusomapo Quran inatoa maelezo tofauti.

    Quran suratul As- Sajdah, (kusujudu) , 32:13 “ Na tungelitaka tungempa kila mtu uwongofu wake (kwa lazima kama tulivyowapa malaika lakini binadamu amepewa huria ya kufanya alitakalo- lililo jema na baya).

    Katika ulimwengu wa Kiislamu Malaika wote ni8 wema na wanamwabudu mungu.

    Hapa ndiyo tatizo linapoanzia. Quran iliyokuja baadaye inasema malaika wote ni wema wakati biblia kitalu kilichoitangulia Quran kinasema kuna malaika walioasi na wakafukuzwa katika utukufu wa Mungu.

    Katika Quran Suratul, al- Kahf, (Pango) 18:50 “ Na (Kumbukeni) tulipowaambia Malaika, Msujudieni Adamu. Basi wakamsujudia isipokuwa Ibilisi yeye alikuwa miongoni mwa majini na akavunja amri ya mola wake……..”

    Katika aya hiyo tunaona ibilisi akilaumiwa kwa kutomsujudia Adamu ingawa amri ya kusujudu walipewa malaika kumbe kwa mujibu wa Quran Ibilisi alikuwa miongoni mwao hao malaika yaani na yeye akiwa malaika.

    Kwa sababu Quran haina habari kuhusu malaika walioasi yaani majini ndiyo maana wanapata tabu kuhusu jambo hilo. Na ndiyo maana pamoja na kujua kuwa hayo majini ni mashetani, Muilsamu amehiari kushirikiana nayo kwa kuswali nayo msikitini. Na hata mwislamu huyu anapomaliza kusali husalimia kulia na kushoto akiwasalimia watu malaika na majini (mashetani) waliokuja kushiriki naye katika Ibada yake, soma katika (Irshadul Muslimiin, Sheikh Said Musa, Uk. 38).

    Katika Tafsiri ya Quran ya Iman Jalalaini Uk. 6:151 anasema kuhusu majini “ Hao ni watoto wa Ibilisi”

    Hii ndiyo sababu hata wanawake wa Kiislamu wakiwa katika kipindi cha hedhi hawaendi msikitini kwa sababu kuna majini na chakula cha majini ni damu. Tafakari kwa hiyo sifa ya hayo majini au mashetani kwa ujumla ni kuwa “ hujaribu kwa bidii sana kuwa karibu na waamini wale wanaosali, kufunga na kusoma Qurani “ (Asili ya majini, Dk. Ahmed H. Sakr Uk. 28) ndiyo maana baadhi ya waislam wao binafsi wasingependa kuwa waislamu lakini majini huwashurutisha kwenda kuswali.

    Kwa sababu wao waislamu hawajui kupambanua kati ya majini ambayo ni roho chafu na wale malaika watakatifu wa Mungu Jehova, ndiyo maana hata akiwa katika sala yake hana uhakika kwa sababu huyo jinni (shetani) amemteka na anamfanyia atakavyo na yeye ni mtumwa wa huyo jinni (shetani)

    Katika kitabu kiitwacho Mkweli Mwaminifu cha Sheikh Said Moosa Mohamed Al- Kindy wa Muscut Oman, juzuu 1-2 Uk 42 Hadithi Na. 74.

    “ Anamwijia mmoja wenu shetani (Jini) katika sala basi anapuliza (anampuliza) katika matako yake, basi (yule mtu) inamuijia fikra ya kuwa umemtoka upepo (kafusa) naye haukumtoka, basi akiona namna hiyo asiondoke (kwenye sala}) mpaka asikie sauti ( ya kutoka upepo) au anuse harufu ( ya huo upepo uliyomtoka, ndio aondoke).

    Huyo shetani, au jinni anayekuwa karibu sana na huyu mwamini wa kiislamu hamchezei tu mwislamu katika matako yake kama tulivyosoma hapo juu bali pia anapofanya tendo la ndoa .

    Katika kitabu kiitwacho Asili ya Majini, cha Sheikh Dr Ahmad H. Sakr Uk. 116 anasema “ Hadithi ya Mtume inathibitisha jambo hili kuwa majini (mashetani) na watu wanaweza kuoana aliposema kwamba iwapo mtu ataingia katika uhusiano wa kindoa na mkewe anatakiwa ataje jina la Mwenyezi Mungu ajilinde kwa Mwenyezi Mungu dhidi ya shetani aliyefukuzwa mbali na rehema. Vinginevyo shetani hujiviringisha katika dhakari (sehemu ya siri za mwanaume) ya mtu huyo na atashirikiana naye katika tendo hilo. Tafakari yetu kuwa hiyo jinni anayeshiriki naye tendo la ndoa pamoja naye kwa mkewe ametumwa na huyo huyo Mungu wao. Hiyo ni kesi ya ngedere kumpelekea nyani! Utashindwa tu!

    • Huhakikisha haweki wazi utambulisho wake vinginevyo watu wanaweza kumkwepa au hata kukimbia. Jina lake linawatisha watu wengi. Hivyo ni vyema asijitambulishe kama ni shetani , jini.
    • Huwapotosha watu kutoka kwa Mwenyezi Mungu ili waende naye Jehanamu, badala ya kwenda peke yake. (Kumbuka hukumu ya Yesu kwa Ibilisi na Malaika zake (Math 25:41)
    • Huwakatisha watu tamaa kwa sababu hana cha kuwapa ila matumaini ya uongo (Mf Q. 52:20)
    • Huhakikisha kwamba watu wanamheshimu kumfuata shetani maana yake ni kuwa mtu wa namna hiyo amejisalimisha (Kumbuka waislamu wanapowasalimia majini kulia na kushoto katika sala (Irshadul Muslimin Uk 38).
    • Huhakikisha kuwa hadhihirishi jina lake kama shetani lakini kama rafiki aliyejificha anayewatakiwa mema.
    • Huanzisha vurugu vinginevyo maisha yake huwa ya taabu. Huwa anafurahia kuona watu wakipigan wao kwa wao.

    Katika kipengele hiki tunaposoma katika Quran, Suratul – Al- Maidah, (Meza) 5:14.

    “ Na kwa wale waliosema sisi ni Wakristo tulichukua ahadi kwao, lakini wakaacha sehemu (kubwa) ya yale waliyokumbushwa kwa hivyo tukaweka baina yao (wenyewe kwa wenyewe) uadui na bughudha mpaka siku ya kiama na mwenyezi Mungu atawaambia waliyokuwa wakiyafanya”

    allah S.W. ndiye anayewaletea uadui na bughudha wakristo. Yeye atakuwa nani?
    Tafakari.

    • Hufundisha uchawi watu wanapaswa watoe kiapo cha utii kwake kabla ya kufundisha uchawi wa aina yoyote. Elimu ya uchawi ni kuwadhuru watu wengine hasa hasa waume na wake.

    Katika sehemu hii tumwangalie huyo shetani au jinni anayeruhusu na kufundisha uchawi.

    Katika Suratul, al- Bagarah, (ng’ombe jike), 2:102 “ Wakafuata yale waliyoyafuata mashetani wakadai kuwa yalikuwa katika ufalme wa nabii suleimani na Suleiman hakukufuru bali mashetani ndiyo waliokufuru, wakiwa fundisha watu uchawi waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani. Na uchawi uliteremshwa kwa malaika wawili Haruta na Maaruta katika mji wa Babeli wala malaika hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie hakika sisi ni mtihani wa kutazamwa kutii kwenu basi usikufuru wakajifunza kwao ambayo waliweza kumfarakisha mtu na mkewe na mengineyo wala hawakuwa wenye kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu……………………

    Katika aya hiyo inaeleza kuwa uchawi ni kazi ya Allah na ndiye anaye idhinisha. Yeye atakuwa nani? Na pia kuna waganga wa kienyeji wa kiislamu ambao hutumia Quran katika uganga wao. Hiyo Quran na majini na uchawi, ulioletwa na Allah S.W. vina uhusiano gani? Tafakari

    “ Juhudi kubwa anayoifanya shetani (Jini) ni kuleta mfarakano baina ya waume na wake. Kwa kufanya hivyo huhakikisha kuwa wanachukiana wao kwa wao. Kwa ajili hiyo huishia, katika talaka. Kwa hiyo matatizo yanajengwa katika familia hiyo. Utengano au talaka inapotokea, watoto hawawezi kulelewa kisawasawa na mzazi mmoja. Watakosa uimara katika utu wao, shetani (jinni) anapata urahisi kuingia ndani ya mioyo na akili za watoto. Atawaongoza kuelekea mahali pasipofaa na hapo anawafanya wawe wahalifu katika jamii (Asili ya majini, sheikh Dr. Ahmad H. Sakr Uk 39)

    Kwa mujibu wa Quran na vitabu vya kiislam huyo anayeamuru talka ni allah. S.W. Mungu wanayemuabudu waislamu.

    Katika suratul, Ahzab(Makundi), 33:49.
    “ enyi mulioamini mtakapowaona wanawake wenye kuamini, kisha mkawapa talaka kabla ya kuwagusa hamna eda juu yao mtakayohesabu. Wapeni cha kuwauliza na muachane muachano mzuri”

    Katika Suratul al- Baqarah, (Ng’ombe) 2:230.
    “ Na kama amempa talaka ya tatu basi mwanamke huyo si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine, na mwanamume huyo mwingine akimwacha basi hapo hapana dhambi kwao mume yule wa kwanza na mwanamke huyo kurejeana wakiona watasimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu.”

    Kama shetani (jinni) huleta faraka ili talaka zitokee, basi Allah S.W. yeye ameamrisha talaka kwa wafuasi wake bila kujali athari za watoto zitakazotokea. Tafakari yeye ni nani?

    Kumuabudu shetani (Jini)

    Katika Suratul Sabaa, 34:40-41
    “ Na kumbuka siku atakayowakusanya wote, kisha atawaambia malaika, “ Je hawa walikuwa wakikuabuduni?” waseme umeepukana na kila upungufu! Wewe ndiwe kipenzi chetu si hao bali walikuwa wakiwaabudu MAJINI; wengi wao waliwaamini hao majini”

    “ Shetani anapoamuru watu wamfuate pia anawaamuru wafanye madhambi na wakose maadili. Huwataka waseme uongo kuhusu Mwenyezi Mungu kutokana na kutokujua kwao. Wanaweza kusema kuwa sisi wanaadamu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu. Mungu alijifanyisha na kuwa umbile la kibinadamu. Mungu amezaa, na mwanaye niwa pekee. Zaidi ya hayo mwanaye si mtoto tu bali ni Mungu pia. Huyo mwana ni Bwana Yesu. Asiyeamini hivyo huchukulika kuwa ni kafiri au muasi hivyo ameangamia na atakwenda jehanamu” (Asili ya Majini, Sheikh Dr. Ahmad H. Sakr Uk 54)

    Hapa ndipo sura halisi ya huyu shetani yaani jinni inapojitokeza. Yesu alipokuwa duniani kabla Muhammad hajazaliwa, wala Uislamu haujaanzishwa na Mohamed wala Quran haijaandikwa na wale waarabu wanne Seyidna Abubakar, Omar, Othuman na Ally, Majini yaani mashetani yalipomuona Yesu yalimwita “ Mwana wa Mungu tuna nini nawe? Je, umekuja kututesa kabla ya muhula wetu? (Math 8:28-31) Mwaka 610 B.K majini hayo hayo yakaanza kuwadanganya waislamu kuwa Mwenyezi Mungu hana mwana (Quran 72:1-3) Na bila kuitafakari. Nao wao wanaamini tu kuwa Quran ni maneno ya Mungu bila kupambanua huyo ni Mungu yupi!!.

    Katika Suratul An- Nisaa (Wanawake) 4:120

    “ Shetani hawaahidi ila uwongo…………..”

    Hii ndiyo sababu Mohammad mtume wa waislamu katika kitabu “ Wakeze Mtume Wakubwa na Wanawe kilichoandikwa na Sheikh Abdallah Saleh Farsy Uk. 12, Mohammad anasema:-

    “ Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na mashetani na kuni haribu akili yangu na kunizuga………………”

    aliyasema maneno hayo baada yakubanwa na shetani (jinni) kule pangoni alikokuwa na baada ya hapo akaanza kujiita mtume. Hoja yetu ni mtume wa nani?

    Katika Kitabu cha Ibn Ishaq 132-133
    “ Kama huyu shetani (jinni) ambaye amekupagaa wewe ni yule ambaye huwezi kumtoa, tutamtafuta mganga na tutatumia vyote tulivyonavyo kukutibu kwa kuwa mara kwa mara shetani (jinni) humpagaa mtu. Lakini anaweza kuondolewa. Mtume alikuwa akisikiliza kwa makini”

    Kisha baadaye na yeye Mohammad katika Sahihi Muslim Juzuu 4 Hadithi na. 2814 kasema
    “ Wala hakuna yeyote katika nyinyi isipokuwa amepewa nguvu zinazotokana na majini. Wakasema (maswahaba) hata wewe mtume wa allah? Akasema hata mimi isipokuwa allah hunirahisishia juu yake hunyenyekea wala hayaniamrishi ila yaliyo mazuri”

    Kwa hiyo majini ni ndugu za waislam Q. 46:29- ufafanuzi wake. Katika kitabu Asili ya Majini cha Sheikh Dr. Ahmad H. Sakr Uk 80 anasema “ Imepokewa na Khalid Ibn Walid kuwa kuna wakati alipatwa na ukosefu wa usingizi basi mtume (S.A.W) akamwambia “ Nikufundishe maneno ambayo ukiyasema utapata usingizi? Sema Ewe mola! Wewe ni mola wa mbingu saba na kile kilichofunikwa nazo. Nawewe ni mola wa ardhi na kilichomo humo. Nawe ni mola wa mashetani (majini) na maovu yao. Nakuomba uwe mlinzi wangu dhidi ya viumbe vyako vyote………..”

    Hadithi hii inaonesha jinsi allah S.W. alivyo na uhusiano wa karibu na mashetani. Je, yeye ni nani?. Pia katika Q: 21:82, 34:12, 38:37 zinaeleza Allah alivyomtishia majini suleiman na yeye akiwa mlinzi wao hata kuwaadhibu wasiofanya vizuri.

    Katika Quran 19:83 “ Je, huoni ya kuwa tumewatuma mashetani juu ya makafiri wanaowachochea kufanya mabaya?”

    Katika Sahihi Muslim vol. IV H. 2667, Sahihi Al Bukhari Vol Vii H. 6243, Sunan Abuw Daud Vol II H. 2152.

    “ Hakika Allah amemkadiria kila mtu kipimo chake cha zinaa, ambavyo haikosi kutimia kwake”

    Tumeona kuwa majini au mashetani au pepo mchafu au Ibilisi walikuwa malaika walioasi walipotupwa chini huku duniani walitaka kurudi huko mbinguni lakini walishindwa.

    Katika Q 72:8-10 (majini) majini yanasema

    “ Nasi tulizigusa mbingu (tulikwenda mbinguni) tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na nyota (zing’arazo) na hakika tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza lakini anayetaka kusikiliza sasa atakuta kimondo (kijinga cha moto) kinamvizia. Nasi hatujui kama wanatakiwa shari wale wanaokaa katika ardhi au mola wao anawatakia (heri).

    Moja kati ya majina ya Allah ni AL-MUQADIM yaani, wa zamani (majina 99 ya Allah) majini yanajieleza kuwa hayajui Mungu wao ana watakia mazuri au mabaya wale wakaao duniani.

    Mungu wa mbinguni anasema katika Biblia kitabu kilichokuweko kabla ya Quran.

    Yer. 29:11 “ Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi asema BWANA ni mawazo ya mani wala si ya mabaya kuwapa nyinyi tumaini siku zenu za mwisho.

    Majini (mashetani) yanajua tu kuwa Yesu atayahukumu na hayajui lolote kuhusu mpango wa Mungu kumwokoa mwanadamu toka kwa shetani (majini)

    Mtume Paul katika 2 Kor 11:14 “ Wala si ajabu shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa Nuru…………..” Pia katika 1 Tim 4:1 “ Basi roho anena wazi wazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine (waislamu) watajitenga na imani wakisikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani (majini)” Tafakari Kuu: Allah katuma mashetani (majini) wako katika dini yake ya uislamu, yeye mwenyewe pamoja na wafuasi wake walikuwa wakifanyia kazi Suleiman wa ndani ya Quran na yeye allah S.W. akiwa msimamizi (Foreman) wao, mwisho wao wote pamoja na allah S.W. mwenyewe ni katika Jehanamu ya moto.

    Yeye Allah atakuwa nani??? Tafakari wewe ndugu yangu Mkristo shika sana ulichonacho asije mtu akakunyang’anya!!!.

    Na wewe rafiki yangu mwislamu okoa roho yako. Nenda kanisani ukajisalimishe upate nusura ya Mwenyezi Mungu!!.

    Tuandikie:

    Huduma ya Uinjilisti ya Biblia ni Jibu Tanzania
    S.L.P. 45290 Dar es Salaam,Tanzania
    Simu: +255 755-680101
    E- mail: tcc@yahoo.com
    d_mwankemwa@yahoo.co.uk

    Like

    • hivi mtume ndie mtu bora

      Like

      • jenifa shuma says:

        TAFAKARI KWANZA MBONA SHETANI KWENYE KITABU CHA AYUBU ALIHUDHURIA MBELE ZA MUNGU, SASA KIPI KISHANGAZACHO

        Like

      • KELVIN HUSSEIN says:

        JENIFA MASHETANI KWENDA AU KUHUDHURIA MBELE ZA MUNGU NI KAWAIDA NDIO MAANA YESU ALIKUWA ANATOA MAPEPO NA YESU NI MUNGU KAMA NA WEWEUNAYO MUOMBE MLOKOLE AYATOE KWA SABABU YESU ANAISHI NDANI YA WATU TULIOOKOKA MARKO 16:16-20, WAKORINTHO WA KWANZA 15:20-28, WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8

        Like

      • KELVIN says:

        JE MTUME NDIYO MTU BORA? SOMA BIBLIA TAKATIFU MATHAYO SURA YA 20 MSTARI WA 25 MPAKA 28

        Like

      • KELVIN says:

        PIA DHAMBI YA USHOGA INATAFUNA TAIFA LA TANZANIA KWA SIRI NA KWA WAZI JE ADHABU GANI BIBLIA TAKATIFU INAITAJA IWAPO MTU ATAPATIKANA NA MAKOSA YA KUTENDA JAMBO HILO KWA MAKUSUDI NA SI KWA KWA KUBAKWA? MAMBO YA WALAWI20:13.PIA CHUNGA SANA WANA ALAMA ZAO WANAPENDA KUVAA MAKOBASI YANI KANDAMBILI ZA NGOZI,NA PIA UKIKAA KULIA KWA MWANAUME MWENZAKO WANAKUITA SHOGA ,YANI KIFUPI WANAPENDA KUKAA KUSHOTO KWA WANAUME WENZAO HII NI ROHO YA ADUI

        Like

      • KELVIN says:

        JE NI HALALI KULA CHAKULA KWENYE MISIBA WAKORINTO WA KWANZA 10:27 NA 28, JE KUWATEGEMEA WATU WALIOKUFA KAMA MASOHABA NI SAHIHI? AYUBU:2:1-2.,mhubiri, 9:5 na 10

        Like

    • Kibona emanuel toka chuo kikuu cha Mkwawa-Iringa says:

      MUNGU AKUBARIKI SANA MTUMISHI WA JEHOVA DANIEL MWANKEMWA KWA AJILI YA KAZI HII YA INJILI KWA WAISLAMU WOTE NA WAKRISTOI WASIOAMINI
      kwa kweli napata faraja kubwa sana ninapoona Injili ya Yesu inasonga mbele hata kwa njia ya mtandao

      Like

    • Mwl Kibona Emanuel says:

      Mtumishi ubarikiwe sana kwa masomo hayo, maana ni muhimu kwa watu wote hasa waislam wanatakiwa wamjue Bwana Yesu kuwa ndiye mwokozi, tena hakuna mwingine kando yake

      Like

    • Rashid says:

      Samahani kaka yangu nakuomba unapoongea toa na ushahidi kwenye vitabu viwili Quraan au bibilia sina zaidi ni hivo tu inahitaji uwe msomi sio ujiongelee tu

      Like

    • Amiri says:

      Umesoma vibaya hadi umechanganyikiwa hujui hata unazungumza nini, ni muhimu upate ushauri nasaha

      Like

    • Pilly says:

      Daniel Mwankemwa, sishangazwi na maneno yako, Imani yako, Itikadi yako, kwani toka mwanzo makafiri walikanusha mitume wa Mungu aliye hai, walikanusha wahyi/ujumbe walokuja nao, kipindi cha Nuh, Musa, Yesu kote huko walikuwepo makafiri (WASIOAMINI) na walikuwamo wasomi waliotumia elimu yao kukanusha tena wakitumia na mifano, hivyo mimi kama MUISLAMU sishangazwi na maneno yako, pia wewe si RAFIKI wa MUISLAMU bali wewe ni ADUI wa MUISLAMU, Nusra ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako uweze kutambua HAKI.

      Like

    • Rama says:

      Wewe Jamaa akili yako ni ndogo sana,uliandika ayah za Quran hapo na kutoa tafasiri zako mwenyewe;Labda nikuulize swali,Mwenyezi Mungu aliumba viumbe vinahitwa Bakiteria;Je uliwahi kuviona kwa macho yako?Kuna vitu vinahitwa Virusi mbalimbali;Je uliwahi kuviona kwa macho yako?Mwenyezi Mungu alikupa akili ww,Je uliwahi kuiona kwa macho yako?Kwahiyo Mwenyezi Mungu aliumba vitu vingi sana na Viumbe vingi sana vyenye kuonekana na visivyo onekana na visivyoonekana ndiyo majini na mizimu na husichanganye mambo majini wa kiasi utaratibu wa Mungu ndiyo wanahitwa Masheitani na Binadamu akisariti sheria za Mungu ndiyo anahiwa Sheitani.

      Like

  4. Daniel Mwankemwa says:

    MOHAMMAD S.A.W MTUME WA WAISLMU, HAJAWAHI, SIYO , NA WALA HATAKUWA MTUME NA NABII WA KWELI

    Nimesoma kwenye blog ya jamii forums na kuona Waislamu wakiwashawishi watu wengine wamuamini Mohammad kuwa naye ni miongoni mwa manabii na mitume wa Mungu aliye hai, jambo ambalo si kweli.Fuatilia…..

    WAJUE MANABII WA UONGO
    Na Mwalimu Daniel Mwankemwa

    UTANGULIZI:
    Suala linalohusu kuwajua manabii wa uongo , limekuwa linaleta shida sana kwa watu wengi, kwa sababu manabii hao wa uongo wanapokuja kwa watu kuleta ujumbe wao hudai “ tumetumwa na Mwenyezi Mungu kuleta ujumbe wake na hivyo kuwataka wanadamu kuupokea, kuuamini na kuufuata”. Inapotokea nabii amekuja kwa mtindo huo na akakutana na watu wasiojua kuwapambanua manabii na mitume kwa misingi ya Neno la Mungu, ndipo ukengeufu hutokea, na makundi ya aina mbalimbali ya imani za uongo hujitokeza.

    Kwa hapa kwetu Tanzania,unaposoma katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Ibara ya 19 (i-iii) utakutana ma maelezo kuwa ,mfuasi wa dini yoyote anao uhuru wa kubadili dini yake ya awali na kujiunga na dini nyingine anayoona yeye kwake inamfaa. Lakini pamoja na uhuru huo si kila dini (njia) inafaa zingine zinaishia kwenye mauti ya milele.
    Mith 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”. (Angalia pia Mith 16:25).

    Miongoni mwa wanadamu wanaoitwa nabii na mtume, ni mtu aitwaye Muhammad s.a.w ibn Abdullah,ibn Abdu Mutallib, ambaye ni mtume na nabii katika dini ya Kiislamu.

    Pengine wewe msomaji wa somo hili unaweza kushangaa ni kwa vipi sisi ambao si Waislamu bali Wakristo tuanze kuhoji habari za Muhammad s.a.w mtume wa Waislamu?. Jibu lake ni kwamba kitabu cha Qur’an kinachotumiwa na Waislamu kimetutaja sisi Wakristo mara 62 kikitutaka kuupokea ,kuuamini na hatimaye kuufuata ujumbe wa Muhammad s.a.w kwa madai ya kuwa yeye ni nabii na mtume wa mwisho hata kwetu Wakristo, aliyetumwa na Mungu.

    Tunasoma hayo ndani ya Qur’an katika Suratul, Baqarah, (ng’ombe jike wa manjano), 2: 62 “Katika walioamini (Mitume ya zamani huko ) na Wayahudi na Wakristo na Wasabai, yoyote miongoni mwao atakayemwamini Mwenyezi Mungu (Sasa kama anavyosema Nabii Mohammed ) na akaamini siku ya mwisho na akafanya vitendo vizuri basi watapata thawabu zao kwa Mola wao, wala haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika”.

    Kwetu sisi kama Wakristo japo katika aya hii tumetajwa , kuna swali ambalo tunajiuliza kuhusu unabii na utume wa Muhammad nalo ni hili “ HIVI MWENYEZI MUNGU ALISAHAU NINI KATIKA KAZI YAKE YOTE KAMILIFU YA KUMKOMBOA MWANADAMU KUTOKA KATIKA DHAMBI MPAKA AMLETE MUHAMMAD S.A.W?”.

    Nabii ni mtu gani? Nabii ni mtu aliyeteuliwa rasmi kwa vigezo vya Kiungu ili kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu, kwa maneno mengine nabii ni msemaji wa siri za Mungu.
    Nabii: Ni mtu ambaye ni msemaji wa Mungu (a mouthpiece of God) .Husimama kati ya Mungu na binadamu, mwenye jukumu la kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu. Nabii anapokuwa msemaji wa Mungu, huvuviwa na Roho wa Mungu, bila ujumbe wake kuwa na makosa. Nabii hujizuia kabisa utashi wake, nafsi yake,,na mawazo yake, anapokuwa anatoa ujumbe wa Kinabii toka kwa Mungu. Wakati mwingine Mungu mwenyewe hutia maneno yake vinywani mwao (Kum 18:18, Yer 1:9). Nabii ni mtumishi wa Mungu (Zekaria 1:6) na mjumbe wa Mungu 2 Nyak 36:15). Unabii wao umegawanyika katika makundi matatu: Unabii unaoelezea hatima ya Waisrael, Nabii zinazohusiana na ujio wa Masihi, na nabii zinazoelezea mambo yajayo (Eschatological prophets). Kwa hiyo Sheria na Manabii inahusiana na Torati (Pentateuch) yaani Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati. Na manabii ni vile vingine vyote visivyo kuwa Torati.
    Kitabu cha nabii Amos 3:7 “Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake”Neno nabii asili yake ni katika lugha ya Kiebrani na maana yake mwonaji. 1Sam 9:9 “ Hapo zamani katika Israel, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa mwonaji”.
    Katika mstari huo hapo juu unatuonesha kuwa manabii wa kweli wa Mungu ni lazima chanzo cha ufunuo au ujumbe wao kiwe Mwenyezi Mungu mwenyewe (Roho Mtakatifu), au ndoto kutoka kwake, au maono kutoka kwake (Hes 12:6), au kupitia malaika watakatifu (Dan 8:15-21) . kinyume na hapo ni nabii wa uongo .

    Tahadhari ya Bwana Yesu: Bwana Yesu alipokuwa hapa duniani alituonya kuhusu kuwatambua manabii na mitume wa uongo kabla Muhammad hajazaliwa (amezaliwa 570 B.K), wala kabla Uislamu haujaanzishwa na Muhammad mwaka 610 B.K, wala kabla ya kuwepo kitabu kinachoitwa Qur’an. Tunayasoma maonyo hayo ya Bwana Yesu katika

    Mathayo 7:15-16 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali, mtawatambua kwa matunda yao”.

    Mathayo 24:11-13 “Na manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi na kwasababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho, ndiye atakayeokoka”.

    Mitume wa Bwana Yesu walisisitiza sana wakikazia kuhusu onyo la Yesu juu ya kuwajua manabii na mitume wa uongo .
    1Yohana 4:1-3,15 “Wapenzi msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, ya kwamba zimetokana na Mungu kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja na sasa imekwisha kuwako duniani. 15 “ Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake naye ndani ya Mungu”

    Vigezo hivi tulivyopewa na Biblia Takatifu kuwajua manabii na mitume wa uongo ni muhimu sana tukavichunguza katika maisha ya wale wanaoitwa nabii au mtume .

    Nabii wa kweli hupata ufunuo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu:- 2Petro 1:20-21.” Mkijua neno hili kwanza,ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu;bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu,wakiongozwa na Roho Mtakatifu”.

    1 Petro1:10-11 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta tafuta na kuchunguza chunguza ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi. Wakatafuta ni wakati upi na wakati wa namna gani ulioonywa NA ROHO WA KRISTO ALIYEKUWA NDANI YAO ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaokuwako baada ya hayo…..” (maneno ya msisitizo kwa herufi kubwa ni ya mwandishi)

    Ufunuo 19:10 “Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndiyo roho ya unabii”

    Hivyo manabii walisema ndani yao wakiongozwa na Roho wa Kristo mwenyewe, kabla hajaja ulimwenguni katika mwili. Je Muhammad s.a.w ni miongoni mwao hata tuuamini ujumbe wake?

    Muhammad hakujua kusoma wala kuandika
    Qur’an 7:157
    Ambao wanamfuata mtume nabii aliye ummy (asiyejua kusoma wala kuandika) na juu ya hivi atafundisha mafundisho hayo ya ajabu ya uislamu……….

    Na ushahidi mwingine unapatikana katika kitabu cha Maisha ya nabii Muhammad uk 8 kilichoandikwa na Sheikh Abdallah Saleh Al-Farsy, tunasoma kama ifuatavyo katika kipengele cha kujifunza kwake;-

    Habari ya kusoma haijakuwako katika nchi ya hijazi, hivyo mtume aliondokea kama Makureshi wengine bila ya kujua kusoma wala kusoma kilichoandikwa. Elimu yao ilikuwa kujifundisha mambo yanayohusu maisha yao ya kibedui, kama vita, kutunga mashairi ya kujisifu ushujaa wao na kutunga hotuba zinazoweza kuharakisha watu wapigane bila ya kufikiri.

    Hivyo basi Muhammad katika maisha yake hakujua kusoma wala kuandika na ndivyo alivyoishi katika maisha yake yote.

    Je Yesu alijua kusoma na kuandika? Luka 4:16-17. HOJA ya Waislamu wanasema katika Yoh 7:14 Yesu akiwa Yerusalemu watu wakashangaa kuwa amepataje elimu ambaye hakusoma? Ukweli ni kwamba Yerusalemu siko alikokulia Yesu. Yeye Yesu amekulia Nazareti ambako wanamfahamu kuwa anajua kusoma na ndiyo sababu alipewa chuo cha nabii Isaya ili akisome.

    JINSI MUHAMMAD (S.A.W) ALIVYOPATA UTUME NA WAHYI (UFUNUO) WAKE

    Ufunuo aliokuja nao Muhammad s.a.w , mtume wa Waislamu, ni tofauti sana na mitume wote walioishi kabla yake wanaotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Tofauti yake ni kwamba manabii na mitume wote waliotajwa ndani ya Biblia Takatifu, wameandika watu mbalimbali wapatao 40 kwa miaka mingi sana inayokaribia 1500, lakini ufunuo wao ni wa aina moja (it has comformity). Ule unabii wa Agano la Kale umetimizwa katika Agano Jipya. Hii ni kwa sababu chanzo cha ufunuo huo ni kimoja, Roho Mtakatifu.

    Lakini kwa upande wa Muhammad s.a.w , mtume wa Waislamu yeye chanzo cha ufunuo na hatimaye utume wake ni masuala yenye utata sana ambao hata wafuasi wa dini hiyo na wao hawajui kwa hakika ukweli ni upi.

    Hebu tuangalie kwa ufupi utata huo.

    Muhammad s.a.w alipotimiza umri wa miaka 38 alihama toka nyumbani kwake, akahamia katika mapango yaliyokuwa hapo karibu na mji wa Makka. Alipofikisha umri wa miaka 40 siku moja alitokewa na kiumbe ambacho Waislamu leo wanakiita Malaika Jibril.

    Wahyi (ufunuo) uliokuja kwa Muhammad alisikia makengele,uso kuwa mwekundu,jasho kumtoka. Katika Bukhar, Hadithi na 2, Juzuu na 1,Al-Lu’lu Kitabu cha 3.Uk. Na.874 Hadithi na 1505 “Hadithi ya Aisha r.a mama wa waumini amesema, kuwa Al Harith ibn Hisham r.a alimuuliza mtume wa Allah s.a.w ‘ Ewe mtume wa Allah hivi wahyi (ufunuo) hukujia vipi?’ mtume wa Allah s.a.w akajibu, “ Wakati mwingine hunijia kama mlio wa kengele, na aina hiyo ndiyo ngumu zaidi kwangu, inaondolewa hali hiyo kwangu wakati tayari nimeshapata wahyi. Na nyakati nyengine malaika anakuja kwangu akiwa katika mfano wa mtu, kwa hiyo ananieleza na ninayazingatia aliyoyasema.” Aisha r.a alisema , Na hakika nilimwona unamshukia wahyi siku ya baridi kali na ilipomuondoka hali hiyo, paji lake la uso lilichuruzika jasho.”

    Qurani 53:2 – 6 Suratul Najm (Nyota) “Kwamba mtu wenu huyu Nabii Muhamad (hakupotea kwa ujinga) na wala hakukosa (Na hali ya kuwa anajua). Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake). Hayakuwa haya (anayosema) ila ni wahyi (ufunuo) uliofunuliwa (kwake). Amemfundisha (malaika) mwenye nguvu sana. Mwenye uweza na yeye (huyu Jibril) akalingana sawa sawa.

    Huyu malaika Jibril ndiye Waislamu wanasema alimtokea Muhammad kule pangoni na kwamba yeye huyo malaika Jibril ndiye Roho Mtakatifu. Tunaposoma ufafanuzi wa aya ya 2:87 ya Suratul Baqarah, uliyomo ndani ya Qur’an unasema “Kwa Waislamu Roho Mtakatifu ni Malaika Jibril si yule wanaodai Wakristo kuwa ni mmoja wa asili ya utatu (Trinity)”.

    Jambo ninalopenda ulijue ni kwamba Waislamu wote hawakubahatika kupewa elimu ya Roho. Hii ni kuanzia mtume na nabii wao Muhammad . Tunasoma hayo katika Qur’an 3:7 “Yeye ndiye aliyekuteremshia kitabu (hiki Qur’an) ndani yake zimo aya Muhkam (nyepesi kufahamika) ambazo ndizo msingi (asili) wa kitabu (hiki) na ziko nyingine Mutashabihat (zinababaisha kama habari za akhera,za peponi na motoni na mengine ambayo yamekhusika na Roho).Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazo babaisha kwa kutaka kuwaharibu watu na kutaka kujua hakika yake vipi; na hakuna ajuaye hakika yake vipi ila Mwenyezi Mungu. Na wale waliozama katika ilimu husema:”Tumeziamini,zote zimetoka kwa Mola wetu.”Na hawakumbuki isipokuwa wenye akili.”

    Qur’an 17:85 Suratul Ban Israil (Wana wa Israeli). “Na wanakuuliza habari ya roho.Sema roho ni jambo lililohusika na Mola wangu (Mwenyezi Mungu),Nanyi hamkupewa katika ilimu (ujuzi) ila kidogo kabisa.(Nayo ni ilimu ya vitu visivyokhusika na roho”).

    Hivyo katika Uislamu elimu ya Roho hawana kwa mujibu wa Qur’an. Hii ndiyo sababu mara nyingi wao hushughulikia sana mambo ya nje (externalistics) zaidi kuliko ya Rohoni k.m kutawadha na kupandisha maji puani wakiamini wamemtoa Shetani aliyekuwa ndani ya pua. Katika kitabu kiitwacho Al-Lu’lu’ wal-Marjan, Juzuu 1. Hadithi na 183 uk. 96 inasomeka hivi “Amesimulia Abu Huraira (r.a), Mtume (s.a.w) alisema, “Mmoja wenu anapoamka kutoka usingizini, basi atawadhe na apandishe maji puani na apenge mara tatu, kwa sababu Shetani alilala ndani ya tundu za pua yake”. (Bukhari, Hadithi, Na.516 Juzuu 4)

    Baada ya kufahamu jinsi Waislamu wasivyokuwa na elimu ya Roho, ndipo tunapoanza kuhoji huyo malaika anayeitwa Jibril ni nani ? Je ni malaika wa Mungu wa Kweli YEHOVA?.

    Biblia Takatifu inaeleza juu ya malaika walioasi mbinguni kisha wakafukuzwa na kutupwa huku chini. 1Petro 2:4 “Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachia “malaika waliokosa” bali aliwatupa shimoni akawatia katika vifungo vya giza walindwe hata ije siku ya hukumu”.

    Kwa mafundisho haya ya Biblia yanatuonesha kuwa kuna kundi moja la malaika liliasi na likafukuzwa na hadi sasa kundi hilo linasubiri hukumu. Kundi hilo leo linaitwa Shetani,Majini au Mapepo wachafu.

    Lakini tusomapo kitabu cha Qur’an , kitabu kilichokuja baadaye sana karne ya 7 (610 B.K) ,baada ya kitabu cha Biblia, ndani yake tunapata taarifa tofauti kuhusu malaika.

    Qurani 32:13 Suratul As – Sajdah (Kusujudu) “Na tungalitaka tungempa kila mtu uwongofu wake (kwa lazima kama tulivyowapa malaika…”

    Ufafanuzi wa aya ya 13 ulio ndani ya Qurani unasomeka hivi:.
    “Angetaka Mwenyezi Mungu angemuumba binadamu kama malaika hawezi kufanya mabaya, maumbile yake ni kufanya mema tu; kwa hiyo halipwi kwa mema yake hayo kwani hayaonei taabu katika kuyafanya. Lakini binadamu ameumbwa kwa uweza wa yote mawili sawasawa na raha yake zaidi ni kufanya mabaya”

    Aya hii na ufafanuzi wake, vinaeleza kuwa malaika wote wa Mungu wa Muhammad ni wema hakuna aliyekosa, na kuwa miongoni mwa malaika hao mmojawao ndiye aliyemtokea Muhammad na kumpa utume na ufunuo wa Qur’an. Sasa hebu tuchunguze kule pangoni alikokuweko Muhammad ili kupata utume alitokewa na kiumbe gani?. Tutaongozwa na vitabu vya dini ya Kiislamu.

    Katika kitabu kiitwacho: Maisha Ya Nabii Muhammad s.a.w uk 16-17 kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy, tunasoma kama ifuatavyo;-

    Hata siku moja- katika mwezi wa Ramadhani mwezi 17, Jumatatu katika mwaka wa 40 ½ wa umri wake- mtume alimwona mtu kamsimamia mbele yake bila ya kumwona wapi katokea, akamwambia; “soma”. Mtume akamjibu; “Mimi sijui kusoma kwani sijapata kujifundisha kusoma.” Akaja akamkamata akambana, akamwambia tena; “soma,” Mtume akamjibu jawabu yake ileile. Hata mara ya tau akamwambia; “soma- Iqraa Bismi Rabbik.” Akamsomea sura hiyo ya 96 mpaka kati yake. Kisha mtume akaisoma kama alivyosomewa. Hii ndiyo sura ya kwanza kushuka katika Qur’an, ingawa haijawekwa mwanzo.

    Mara, yule mtu (Malaika) akaondoka machoni mwake- asimwone kenda wapi. Na mtume naye akarejea kwake-khofu imemshika. Alipofika nyumbani, Bibi Kadhija alidhani ana homa, akamfunika maguo gubigubi na akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka. Hata homa ilipomwachia alimweleza Bibi Kadhija yote yaliyomtokea; na Bibi Kadhija akamtuliza moyo wake, akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia. Mara bibi huyu akaondoka akenda kwa jamaa yake – Bwana Waraqa bin Naufal- akampa habari yote iliyompata mumewe. Naye akamwamrisha amwite. Na mtume akenda akamweleza habari yake yote. Bwana Waraqa akamwambia; “ Huyo ndiye Jibril aliyemshukia Nabii Musa na Nabii Isa. Basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu, nami natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako; Inshaallah nitakuwa mkono wako wa kulia” Wakarejea kwao na khofu yote imemtoka”.

    Alipokuwa pangoni alichezewa na Shetani: Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya

    “Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.

    Katika tukio hili lililompata Muhammad akiwa pangoni , ndipo Waislamu wote ulimwenguni wanapolieleza kuwa hapo ndipo Muhammad s.a.w alipoletewa wahyi (ufunuo) na kupewa unabii na utume. Lakini unapotafakari juu ya ujumbe huo utaona kuwa hata yeye mwenyewe hajui nini kilichokuwa kimemtokea kule pangoni. Ndiyo maana tunasoma kuwa alipofika nyumbani kwake mkewe Bi. Khadija alimfunika nguo mumewe akidhani ana homa. Muhammad alimweleza mkewe kilichomtokea kuwa ni “Shetani” hakumsema malaika yeyote kama Waislamu wanavyotaka kutuaminisha leo. Kwa sababu kama angekuwa ni malaika kama tunavyosoma ndani ya Biblia ,asingesita kujitambulisha kwa Muhammad kuwa yeye ni nani. Hii ni hoja ya kwanza.

    Hoja ya pili tunaona kuna mtu anaitwa Waraqah ibn Naufal, binamu yake na mke wa Muhammad s.a.w Bi Khadija. Yeye Waraqah anamwambia Muhammad huyo aliyekutokea ni malaika Jibril. Basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu !!!!! Je alikuweko pangoni wakati Muhammad s.a.w akitokewa na kiumbe asichokijua?.

    Hoja ya tatu tunaona hata huyo mkewe Muhammad anamwambia mumewe utume huo !!!!!!! Je na yeye alikuweko pangoni? Kama hakuweko ni nani aliyemwambia kuwa yule ni malaika Jibril ikiwa Muhammad mwenyewe aliyetokewa alisema nimetokewa na Shetani? Tafakari

    Katika kitabu kiitwacho Tafsir Al-Kashif, cha Muhammad Jawad Mughniyyah, uk74 paragrafu ya 7 inasomeka“ Hakuna njia ya kumjua Iblis, Shetani na Jini, isipokuwa kwa njia ya wahyi (ufunuo) tu”

    Qurani Suratul Sad 38:69 Muhammad amenukuliwa akisema “Sikuwa na ilimu ya viumbe watukufu(Malaika)…

    Kwa sababu ya Muhammad s.a.w kutowajua malaika kwake yeye anasema unapomwona punda akilia basi kamwona Shetani. Katika Kitabu kiitwacho Mkweli Mwaminifu, Juzuu 3-4 Hadith 789 uk 38 “ Punda akilia kamwona Shatani”

    Jambo hilo ni tofauti na jinsi Biblia Takatifu inavyoeleza kuhusu punda. Mungu anaweza kumtumia hata punda kuongea na wanadamu ili kuwajulisha ujumbe wake. Katika kitabu cha Hesabu 22:22-31 tunasoma habari ya Balaamu jinsi Mungu alivyomtumia punda kumwambia Balaamu asiendelee na safari yake , baada ya punda huyo kumwona malaika wa Bwana akiwa ameshika upanga na amesimama mbele yao akiwa amezuia njia aliyotakiwa kupita. Punda alimwambia Balaamu ule msitari wa 30-31 “ Yule punda akamwambia Balaamu, Je mimi si punda wako, nawe umenipanda maisha yako yote hata leo? Nimezoea kukutenda hayo? Akasema La!. Ndipo Bwana akafunua macho ya Balaamu, akamwona malaika wa BWANA amesimama njiani, ana upanga mkononi mwake, umekwisha kufutwa; naye akainama kichwa, akaanguka kifudufudi”

    Inaonekana kwa tukio hili lililomtokea Balaamu, Mungu alimfunua macho yake akamwona malaika. Lakini kwa Muhammad yeye anachokiona ni Shetani tu. Na ndiyo maana anasema punda akilia amemwona Shetani

    Kwa hiyo kama ufunuo wa Muhammad unaanza na Shetani kama vitabu sahihi vya dini ya Kiislamu vinavyoeleza, kwa mujibu wa ufafanuzi wa kitabu hicho cha Tafsir Al Kashif, inaonesha kwamba ufunuo, unabii na hata utume wa Muhammad una walakini mkubwa ukilinganisha na ujumbe wa manabii na mitume waliotajwa ndani ya Biblia Takatifu.

    Katika Biblia shetani ametajwa kuwa anaweza kujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
    2 Wakorintho 11:13-15 “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu, maana shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakajigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.

    Muhammad akiwa Medina aliulizwa na Wayahudi ikiwa ufunuo wake umetoka kwa Mungu wa Kweli kwa kumtaka atoe sifa za manabii. Akijibu swali hilo alisema:
    Mkweli Mwaminifu Juzuu 3-4 Uk.63.Hadithi Na. 880. “Kasema Mtume (s.a.w):- (Mambo) mane ya sheria za mitume (Kuwa na) na haya,na kujipaka mafuta mazuri,na kuowa (wake),na kupiga mswaki.

    Hizi si sifa za Ki-Mungu kwa nabii na mtume bali ni za kibinadamu tu.

    Manabii na watu mbalimbali katika Biblia hawakuona haya. Soma Isaya 50:7 “ Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimeukaza uso wangu kama gumegume, nami najua ya kuwa sitaona haya”. Zaburi 34:5 “ Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya” Zab 119:46 “ Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu” Warumi 1:16 “ Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye kwa Myahudi kwanza , na kwa Myunani pia” 1Petro 4:16 “ Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

    Zaidi ya hayo tunaona Muhammad alirogwa. Kurogwa ni hali ya mtu kuathirika na nguvu za giza yaani uchawi.. Je nabii au mtume wa Mwenyezi Mungu wa Kweli anaweza kurogwa?

    Katika Qur’an Suratul Ban-Israel, 17:47 “ Tunajua sana, sababu wanayosikiliza, na wanaponong’ona, wanaposema hao madhalimu. Nyinyi hamfuati isipokuwa mtu aliyerogwa”
    Pia katika Suratul Falaq, 113:1-5 “ Ninajikinga kwa mola wa ulimwengu wote na shari ya Alivyoviumba, na shari ya giza la usiku liingiapo, na shari ya wale wanaopulizia (vivia) mafundoni (wakavunja) mashikamano yaliyo baina ya watu yaani shari ya mafatani, Na shari ya hasidi anapohusudu”

    Tunasoma tukio hilo katika ufafanuzi wake uliyomo ndani ya Qur’an chapa ya nane uk.977 unaofafanua Sura ya 113-114 “Athari ya uchawi juu ya mtume (s.a.w). Swali la pili lijitokezalo kuhusu sura mbili hizi ni kwamba kwa mujibu wa hadithi uchawi ulifanywa dhidi ya mtume (s.a.w) naye akawa mgonjwa, na ili kuiondoa athari hiyo ya uchawi Jibril (a.s) alikuja na kumpa maelekezo Mtume (s.a.w) ya kusoma sura mbili hizi. Watafiti wengi zamani na wa sasa wamelifanyia upinzani jambo hilo, kwamba ikiwa hadithi zitakubaliwa, basi mfumo wote wa sharia utakuwa ni wa kutiliwa shaka, kwa sababu kama mtume (s.a.w) aliweza kuathirika kwa uchawi, na kwa mujibu wa hadithi hizi kweli uchawi huo ulionesha athari yake, basi hatuwezi kukaidi au kukana hadi kiwango gani maadui waliweza kumfanya Mtume (s.a.w) aseme na atende mambo kwa nguvu ya uchawi, na katika mafundisho yake mambo mangapi yatoka kwa Allah na mangapi yatokana na athari ya uchawi juu yake. Si hiyo tu, bali pia wasema kuwa baada ya kuyatambua hayo kuwa ni kweli katu haitawezekana hata kule kukaidi kuwa (s.a.w) alishawishiwa kudai utume kwa mauzauza ya kinjozi kuwa alimjia malaika. Pia wanasema hadithi hizi zapingana na Qur’an, na kama ilivyo katika Qur’an kuwa tuhuma hiyo batili kwa makafiri ilivyotajwa kuwa mtume s.a.w amerogwa naye ameathirika na uchawi: wanaposema hao madhalimu, ‘Ninyi hamumfuati isipokuwa mtu aliyerogwa’.” (17:47), lakini hadithi hizi zinathibitisha madai ya makafiri kuwa kwa kweli aliathirika na kuongozwa na uchawi……Kadri historia inavyohusika,ukweli kuwa kiasi fulani cha athari ya uchawi juu ya Mtume (s.a.w) ni hakika iliyothibiti; na kama kwa ustadi wa ubishi inawezekana kuthibitisha kuwa kweli.Limesimuliwa jambo hilo na Bukhari, Muslim, Nasai, Ibn Majah, Ahmad, ‘Abdur Razzaq, Humaid, Baihaqi, Tabarani, Ibn Sa’d, Ibn Marduyah, Ibn Abi Shaibah, Hakim, Abd bin Humaid na Muhadithina wengine toka kwa Bi. ‘Aisha (r.a), Zaid bin Arqam, Ibn ‘Abbas kupitia silsila nyingi mno kiasi kwamba jambo lenyewe limefikia hali ya ufululizo kamili, isipokuwa kila Hadithi, yenyewe ni ripoti kamili.

    Hii ni uthibitisho mwingine mzito unaoonesha kuwa utume wa Muhammad una utata. Ikiwa na wao Waislamu kwa mujibu wa hadithi hizi hawajui ni mambo mangapi Muhammad aliyoyasema yanatoka kwa Allah na mangapi aliyasema akiwa ameshinikizwa na wachawi , Je ufunuo na utume wake utakuwa umetoka kwa Mungu wa Kweli? Tafakari !!1
    Ndani ya Biblia Takatifu hakuma kurogwa kwa mtu wa Mungu. Hesabu 23:23 “ Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israel. Sasa habari za Yakobo na Israel zitasemwa , Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!”

    Kwa mujibu wa kitabu cha Biblia Takatifu, manabii na mitume wa kweli wa Bwana Mungu wanatoka katika taifa la Israel.
    Kitabu cha Ezekiel 13:9 “ Na mkono wangu utakuwa juu ya manabii wanaoona ubatili, na kutabiri uongo;hawatakuwa katika mashauri ya watu wangu, wala hawataandikwa katika maandiko ya nyumba ya Israel, wala hawataingia katika nchi ya Israel; Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU” .

    Pia kwa mujibu wa kitabu cha Qur’an manabii na mitume ni lazima watoke kwa Yakobo ambaye ni mtoto wa Is-haqa ambaye naye ni mtoto wa Ibrahim. Qur’an Suratul Al-Ankabuut, (Buibui), 29:27 “ Na tulimpa (kumzaa nabii) Is-haqa na (kumjukuu nabii) Yakubu na tukauweka katika kizazi chake unabii na (kupata) kitabu, na tukampa ujira wake katika dunia; naye katika akhera kwa yakini atakuwa miongoni mwa watu wema”.

    Aya hii, inaendelea kusisitiza kuwa ni kupitia kizazi cha Yakobo ndiko uliko unabii na kupata kitabu. Kwa bahati mbaya Muhammad ibn Abdullah, hatoki katika kizazi hicho wala kwa Ishmael kama wanavyodai Waislamu . Kwa sababu Ishmael ni Mwebrania kama baba yake mzee Ibrahim alivyo Mwebrania (Mwanzo 14:13) na Muhammad ni mwarabu kutoka kabila la Maqureysh. Kwa kutambua hilo ndipo tunamwoma Muhammad akiwaonya watu wengine wajiepushe na watu wa kabila lake.

    Sahih Al-Bukhari Vol.1.Hadithi Na. 801 na Al-Lu’lu Kitabu cha 3. Uk.1089.Hadithi Na.1846 inasomeka“Hadithi ya Abu Huraira (r.a) amesema ,“Mtume wa Allah (s.a.w) amesema,Kabila hili la Makuraish litawateketeza watu.’ Wakauliza, ‘Unatushauri nini?’ Akasema, Nashauri watu wajitenge nalo.”

    Kumzamisha nzi kwenye kinywaji
    Bukhar vol. 4 Hadith 537 “ Narrated Abu Huraira: The Prophet said: If a house fly falls in the drink of any one of you, he should dip it (in the drink) for one of its wings has a disease and the other has the cure for the disease”

    Tafsiri: Ilisimuliwa na Abu Huraira: Nabii alisema kama nzi akiangukia ndani ya kinywaji cha mmoja wenu, anapaswa kumzamisha kabisa (ndani ya kinywaji) kwa kuwa bawa lake moja lina ugonjwa na bawa lake jingine lina dawa

    Mitume wa Yesu ndani ya Biblia Takatifu walikwisha kutuonya kuhusu uchafu huo. Katika 2 Kor 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”

    Miongoni mwa mafundisho ya Muhammad ni kwamba kuna mambo kumi yanayokamilisha Uislamu nayo tunayasoma katika kitabu kiitwacho Mkweli Mwaminifu , Kilichoandikwa na Sheikh Said Moosa Al-Kindy wa Muscut, Juzuu 3-4 Uk 63.Hadithi Na.880 “ Kasema Mtume (s.a.w) (Mambo) kumi ya Uislamu (yanayokamilisha Uislamu):Kukata masharubu,na kuziweka ndevu,nakuziweka ndevu (kutozinyoa) ndevu,na kupiga mswaki,kusafisha ndani ya pua kwa maji,na kukata kucha,kuosha mikono baina ya vidole,na kung’oa (au kunyoa) nywele za kwapani,na kunyoa nywele za mbeleni (mavuzi),na upungufu wa maji. La kumi,kasema sahaba aliepokea hadithi hii kuwa nimesahau,lakini kasema bila shaka la kumi ni “kutahiriwa.”

    Kwa mujibu wa Biblia manabii na mitume wanathibitishwa kwa njia ya miujiza.
    Kutoka 14:21” Musa akanyosha mkono wake juu ya bahari,BWANA akaifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wa nguvu utokao mashariki,usiku kucha,akaifanya bahari kuwa nchi kavu”.

    Matendo 19:11-12 “Mungu alifanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida . Hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka”. Tazama pia Matendo 16:16-18, 20:7-12 na Matendo 13:6-12.

    Qur’an nayo inathibitisha kuwa manabii na mitume ni lazima wafanye miujiza.

    Qurani 40:78 Suratul Al-Muumini [Waumini] inasomeka “Na kwa yakini tumewatuma mitume kabla yako wengime katika wao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia na haikuwa kwa mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu”

    Muhammad hakupewa kufanya muujiza wowote ili kuthibitisha madai ya unabii na utume wake.
    Qur’an 29:50 Suratul Al-Ankabuut (Buibui). “Na walisema “Mbona hakuteremshiwa miujiza kutoka kwa Mola wake? Sema miujiza iko kwa Mwenyezi Mungu tu (akitaka atakuteremshieni na kama hataki basi),nami hakika ni mwonyaji mbainishaji (dhahiri tu).” (Taz. Qur,an 6:35-37 13:7,)

    Katika Qur’an iko aya ambayo tunapaswa tuitafakari wote kwa pamoja.Katika Surat An-Nisaa, (wanawake), 4:79 “Wema uliokufikia unatoka kwa Mwenyezi Mungu na ubaya uliokufikia unatoka nafsini mwako, mwenyewe umefanya mambo hata yakakufika hayo. Nasi tumekupeleka kwa watu kuwa mtume na Mwenyezi Mungu ni shahidi wa kutosha (hapaitajiwi shahidi mwingine)”

    Aya hii inaonesha kuwa Muhammad mtume wa Waislamu, alipelekwa kwa watu kuwa mtume, huku Mwenyezi Mungu akiwa shahidi tu. Siku zote shahidi si mtendaji bali ni mwonaji tu wa tendo lililotendeka.Hoja yetu tungependa kuwajua hao watu waliompeleka Muhammad kwa watu ni akina nani?. Kwa sababu tumeona kule nyuma baada ya Muhammad kutoka pangoni, mkewe Bi. Khadija anamwambia Muhammad kuwa “utume huo!!!!!!! Na Bwana Waraqah ibn Naufal akimwambia Muhammad kuwa “ basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu” kabla ya Qur’an .Je hao si wale “Nasi tumekupeleka” wanaotajwa kwenye aya hiyo hapo juu? Tafakari!! .

    Waislamu hudai kuwa Muhammad ametumwa na Mwenyezi Mungu wao, ambaye ni Mfalme wa Wafalme . Lakini tusomapo Biblia Takatifu katika kitabu cha Ufunuo 17:14 “ Hawa watafanya vita na Mwanakondoo, na Mwanakondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme; na hao walio pamoja naye ndiyo walioitwa na wateule, na waaminifu”

    Katika Ufunuo 19:11-16 “ Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa Neno la Mungu. Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA “

    Yesu Kristo ndiye Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana.Lakini tunaposoma Hadithi sahihi za Kiislamu zinaeleza kuwa adui mkubwa wa Allah (s.w) Mungu wanayemwabudu Waislamu, ni yule anayeitwa Mfalme wa Wafalme.
    Sahih Al- Bukhari, Vol.8.Hadithi Na.225, Al-Lu’lu Wal-marjan,Juzuu ya 3,Hadithi Na.1385 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) amesema,Mtume wa Allah (s.a.w) amesema,”Majina yaliyo dhalili mno na mabaya mbele za Allah ni mtu kujiita,Malikil-Amlaak (Mfalme wa Wafalme).”

    Hivyo, ufunuo aliopokea Muhammad, ambao anatutaka na sisi Wakristo tuuamini haujatoka kwa Mungu tunayemwamini sisi Wakristo, yaani, Yesu Kristo.Bali kama alivyonukuliwa katika vitabu vya Kiislamu, unatokana na kuchezewa na Shetani, na kwa sababu hiyo kwetu anakuwa nabii na mtume wa uongo’

    Biblia Takatifu imetuonya kuwachunguza mitume na manabii. Katika kitabu cha Ufunuo 2:1-2 “ Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao siyo ukawaona kuwa waongo”
    Kwa mujibu wa aya hizi Muhammad s.a.w hastahili kuitwa nabii na mtume wa Mungu wa Kweli, bali anaangukia katika kundi la manabii na mitume wa uongo. Hatufai.
    .
    Wasiliana nasi kwa maswali, maoni au kutaka ushauri:
    +255 755 680101,Email: www. Findtruefaith.blogspot.com , d_mwankemwa@yahoo.co.uk

    Like

    • unknownnnnnn says:

      if u have reverted,why do u still wear da islamic attire and wen u open a session in da church y do u open wid suratul FATIHAH………and y is ur name still adam haji……c u change it……………u suuuuuuuuck….nenda kajifunze QURAN translation vipoa……nkt

      Like

      • Esther Ndosi says:

        Napenda kukushauri Mungu si wa matusi hata siku moja. Mmekuwa na comments za matusi humu ndani sijui kwa nini? Hampendi kuambiwa ukweli mna baki kutukana tu. Na pia napenda kukwambia ukristo si mavazi, wala jina, wala lugha, wala mwili ni roho au moyo wako ndiyo maana ukifa vyote unaviacha hapa duniani roho tu ndio inaenda kwa Mungu hivyo(majina,lungha,mwili nk) tumepewa tuvitumie tukiwa hapa duniani. Na pia Yesu alipotukanwa hakurudisha matukano (1 Petro 2:23) na sisi tukiwa wafuasi wake hatutarudisha matukano zaidi sana tutawasamehe na kuwaombea.

        Like

      • Rama says:

        Hakuna anaye kushawishi bali unaunibiriwa maneno ya Mungu ukiona ukweli basi unakuwa Muislamu lakini husidanye watu kwamba wanakushawishi ww.Kwani Ukristo ni dini kutoka kwa Mwenyezi Mungu?;Lete ayah ya Biblia hapa .
        2.Lete aya inayosema Yesu dini yake alikuwa Mkristo
        3.Lete aya inayowaonesha Mitume waliomtangulia Yesu kama Musa,Ibrahimu,Daudi,Isaya,yona,Sulaimani,Ibrahimu wakiingia kanisani na kusali misa ili tuamini Ukristo ni dini ya kweli kutoka kwa Mungu.
        4.Wapi aya Yesu aliisoma Biblia?
        5.Wapi aya Biblia ni kitabu Kutoka kwa Mwenyezi Mungu?

        Like

    • Abdulatif msangi says:

      We jamaa kumbe chenga kweli

      Like

    • EV Keneth says:

      Mungu akubark mtumishi, Yesu ni Mungu hata kama hawaamin yoh1:1-12; Na uislamu ni iman ya kishetani

      Like

  5. Rev. Adam Haji Mohammed says:

    Like

  6. Elisha says:

    JE! YESU NI MUNGU AU SIO MUNGU,
    Angalia video hizi za hoja za waislam na wakristo ulifanyika katika chuo kikuu cha Dar es salaam University.

    Waislamu

    Like

  7. MOSES says:

    habari.nimeisoma habari hii kwa makini sana.
    Ila nikutake jambo ili mbele ya Mwenyezi Mungu siku ya mwisho (kama unayo imani ya siku Hii) UWE SHAHIDI KUWA ULIJUZWA JAMBO HILII ILA UKAWA NI MWENYE KUUPUUZA.kama umegusa pahala kutaka kujua basi ntachukua fursa hii kukupa yaliyo thibiti ili uyapitie kwa makini bila ya kuweka dini zetu mbele ili ukishajua,kwako litabaki suala moja,ima kukataa au kukubali juu ya hoja ulizo ziwakilisha.baada ya kumaliza ivo nami ntakupa hoja zilizowaz dhidi ya ukiristo wa mtume paulo kabla.Na utambue kwa nn quran inatambua vitabu vifuatavo INJILI(MT.YESU ),TORATI(MT. MUSSA),ZABURI (MT. DAUDI)
    Ili iwe faida kwa kondoo wa bwana unaonaje tukaitisha kongamano dhidi ya hoja hizi ili ibainike kuwa waislam wako njia mbaya ili wao wawe mashaidi kwa wenzao na kama laa basi itabainika ukiristo wa leo unamajibu gani kuhuusu dini yao(ukiristo).
    kama utakua tayari nifahaamishe tounane ili tuandae kongamano hili,suala la gharama wewe hutahusika……
    KONDOO KAZI YAO NI KUJUA HAKI IKO WAPI WAIFATE. HALAZIMISHWI MTU KUFATA DINI AITAKAYO.ILA NI VEMA PIA AKAJUA NI IPI DINI SAHIHI MBELE YA BWANA ILI AKUBALIWE MATENDO YAKE SIKU YA MWISHO.,TUWE WA WAZI KATIKA HOJA NA ISIWE VINGINEVO.
    TUSAIDIANE KUOKOA KONDOO WANAOPOTEZWA
    contact..
    0783 605961

    Like

    • paul says:

      watu wengi wanachanganya hawajui vita kati ya shetani na Yesu ilianza mbinguni unaweza soma ufunuo wa Yohana utaelewa zaidi. ni yote yanayotokea sasa ni kwa ajili Ya Yesu au shetani shetani yeye anampinga Yesu na uislamu ni mradi wa shetani kwani hata ukifuata amri zote usimuamini yesu ni bure kwa kuwa amri zilikuwapo tokea zamani na Yesu alikuja ili kutookoa kama amri zingeweza kutuokoa basi Yesu alikufa bure, wsaislamu wengi wanadhani dini itawaokoa na huu ni upotoshaji wa muhammad kwani kurani ilitungwa na ina visa vingi vya uongo na vya kubuni.
      Yesu ni njia ya kweli na uzima.
      Praise the lord.

      Like

    • Moses Nimefurahi kusikia hivyo naomba tufanye hilo kongamano. Mungu akubariki sana.

      Like

      • KELVIN says:

        WATU WA NEW HOPE MINISTRIES MSIWACHELEWESHE HAWA WAISLAM ANDIKENI KWENYE HII BLOGG AYA INAYOSEMA KUWA QURANI NI UCHAWI

        Like

      • Pilly says:

        New Hope Ministry, kutukana, ugomvi, visasi ni mambo ambayo hayaruhusiwi mbele ya Mwenyezi Mungu tangu kuumbwa kwa Adamu hadi sasa, vilevile UISLAMU haiko hivyo mnavyobuni, na hivyo vitabu mnavyochukua tafsiri sivyo QURAN ilivyo wala Vitabu vya Hadithi vilivyo, narudia tena WASOMI NDIO WANAOPOTOSHA UKWELI WA MUNGU, pia katika majadiliano haya si waislamu pekee wanaotukana hata wakristo wametukana tena wamepinduka mipaka, kumtukana Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ndivyo dini yenu inavyofundisha? naelewa hadi wewe kuandika mjadala hapo juu umesoma na UNAELEWA UKWELI UKO WAPI lakini IBILISI yuko kazini kupoteza wanaadamu.

        Like

  8. Assallamu Aleykum nadhani hamjambo nyinyi makafiri yote yamenikera ila kumkashifu ALLAH(SW) NA MTUME WAKE MUHAMMAD(SAW) LIMENIKERA ZAIDI NYINYI NI WAPUMBAVU NA MOTO WA KUNGOJEENI WASHENZI MAKAFIRI MUNGU WETU NI WA KWELI NA MTUME WETU PIA NI WA KWELI TENA NA KUOMBENI MUTUBU NA MUSALIMISHE NAFSI ZENU KWA HAKIKA MUMEPOTEA AHSANTENI.

    Like

    • Esther Ndosi says:

      Ndio utukane. Ni mungu gani huyo unamtetea kwa njia ya matusi kama si shetani.

      Like

      • Kweli Ester na ndio maana mimi sikumjibu. niliyemwona anabusara ni yule aliyenitaka tufanye kongamano halafu tujadili ni nani aliye sahihi.hata mimi nimekubaliana naye yule ndugu, nilimpigia simu akasema yuko songea atanijulisha akishakuwa tayari. ubarikiwe ester.

        Like

      • ally esry says:

        Lakumdinukum wal ya diin..,nyinyi mna dini yenu na mimi nina dini yangu.Wewe ester ndosi kwanza huna stara ya mwanamke ndo hata hujistiri baina ya wanaume ndio maana hata maradhi hayaishi unaongea kati ya wanaume bila stara hakika wewe ni dhalimu

        Like

      • islam4m4u says:

        esther plz n plz ……..nitaftie penye kumenukuliwa kuwa ukristo ni dini ya kweli katika bibilia

        Like

      • Yohana Mzuri says:

        Nawashangaa Waislamu waliopekua Biblia nzima kutafuta palipoandikwa “UKRISTO ni dini ya kweli”.
        HAWATAMBUI KUWA:
        -UKRISTO ni IMANI na sio DINI;
        “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16 soma hadi aya ya18.

        Like

    • wewe uliyelaaniwa na unayeleta lugha chafu na uliye na pepo kama umekelwa nyamaza co lazima ujibu hapa tunajadiliana ili kuipata dini iliyo ya kweli na sio kutupiana matusi km tunaujua ukweli tukausema unalalamika nn ? je nyinyi mnatusema sisi mbona sisi hatutukani kiasi hicho ? ujue mimi niliyekutumia comment hi ni mlemavu wa masikio ninayeshawishiwa sana na waislam ila msimamo wangu ni mkubwa kwa maana naamin yesu ndio masihi ht kama umeniona bp iman yangu palepalee

      Like

      • Pilly says:

        Alistidia Salvatory, anayetoa laana ni Mungu pekee, je wewe IMANI yako inakufundisha kutoa laana? je nyinyi hamtukani? nikujuze jambo moja katika IMANI YANGU YA KIISLAMU hairuhusiwi kumshawishi ASIEAMINI kuamini, pia yawapasa wote wasioamini kutumia elimu yao vizuri kupambanua haki na batili.

        Like

    • kelvin hussein says:

      UNATAKA TUWE NA CHAPA YA SHETANI SIJDA SOMA UFUNU 13:16 OKOKA WAKORINTHO WA PILI 6:1-2, LUKA19:27

      Like

    • KELVIN says:

      JE NI NANI NI MAKAFIRI KAMA SIYO MASHEHE? SOMA BIBLIA NEHAMIA 5:1-19

      Like

    • KELVIN says:

      UNATAKA TUWE NA ALAMA YA SHETANI KAMA WAISLAM WENZAKO HUJUI SIJDA NI CHAPA YA SHETANI SOMA BIBLIA UFUNUO SURA YA 13 MSTARI WA 16, KUOKOKA NI SASA WAKORINTHO WA PILI SURA YA 6 MSTARI WA 1 NA WA 2

      Like

    • KELVIN says:

      SOMA YOHANA 10:7 MTUME MOHHAMED NI MWIZI NA MNYANG`ANYI PIA SOMA MATENDO YA MITUME 4:10-12

      Like

    • alex burigura says:

      Ninamashwali naminingetaka muelekezo naufafanuzi bora:
      1.Niukweli muhammed alisemayakwamba tusimfuate kwakuwa nayeye hajuwiaendapo ?Q 46 9
      2.Je! Mwanamke akiwakatika mzunguuko wakewadamu anakuwanajisi nahawezikusali,kuingiya mskitini,w”ahaanausihano wowote naMungu?naikiwanikweli akifakwahaliiyo anaenda mbinguni?
      3.Nikweli kwamba Allah anamajina 99,ningitaji munitafsiriye nakunifafanuliya jinalake la 94
      4.niukweli maji kabisa inauwezo wakumuondoleya mwanadamu dhambi ? Naitaji msahada kwanza kwa hayo asanteni. Unijibu kwa account yangu ya facebook, jina MIRALDI ROGER

      Like

  9. Je mtume mohamed ni mtume wa kweli?

    Like

    • Mtume Muhammad (S.A.W) ni Mtume/Nabii wa MwenyeziMungu, na Yesu pia ni Mtume/Nabii wa M/Mungu wala hakuna sehemu yoyote katika biblia Yesu alikosema hivi “Mimi ni Mungu au Mniabudu” bali alisema hivi
      john 17:3 “Uzima wa milele ndio huu wakujue wewe Mungu “pekee” wa kweli na Yesu kristu uliyemtuma”

      mat 14:1 “msihuzunike mnamwamini Mungu niamini na mimi”

      john 7:28 “mimi mnanijua na huko nitokakako mnakujua kwa yule wa pekee aliyenituma msiyemjua nyinyi”

      Mathayo 15:24 “…akajibu akasema sikutumwa bali kwa kondoo waliopotea….israel.”
      john 14:24 “Bali baba aliyenipeleka”

      john 5:30 ” mimi sifanyi neno mwenyewe, na hukumu ninayohukumu si yangu bali nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu ni kweli kwani yashuhudia kuwa baba alinituma”
      SASA HAWA JAMAA UUNGU WA YESU WALIUTOA WAPI WAKWAMBIE. WAKIRISTU
      WANA DHAMBI KUBWA YA KUMTUNGIA YESU UONGO MANENO AMBAYO HAKUSEMA.
      I WELCOME EVERY KIND OF CHALLENGE IF ANY P’SE!!!!MSIOGOPE

      Like

      • sebard says:

        Kwa hiyo bwana Abdalah unakubali kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu?Mana aya zote hapo juu zinadhihirisha kuwa Yesu NI mwana wa Mungu ila ninyi Makafiri mnapinga hilo na kumkana wakati mna silimu,mnadhambi tubuni naye atawasamehe.

        Like

      • dotto says:

        Msitumie mwana wa mungu kumuita yesu Mungu hata mimi na wewe n wana wa Mungu vile vile yaan Mungu wa Yesu ndo mungu wetu teena baba yake Yesu ndo baba yetu John 20.17. SAWA BWANA Sebard?

        Like

      • KELVIN says:

        WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:20, WAFILIPI 2:4-12, WAKOLOSAI 1: 15-20, MUNGU WAKO WATATU WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8 MWANZO 18 SURA YOTE. FUATILIA COMMENTS ZANGU OKOKA WKORINTHO WA PILI 6:1-2

        Like

      • KELVIN says:

        YESU NI MUNGU WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:20, MUNGU WAKO WATATU, SOMA WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8 WISLAM WOTE MNATAKIWA KUWA WAKRISTO YOHANA 10:1-30, WAISLAM WOTE PAMOJA NA MTUME MOHAMMED MNAMILIKIWA NA YESU KRISTO YOHANA 10:1-30 KUOKOKA NI SASA WAKORINTHO WA PILI SURA YA 6:1-2, LUKA 19:27

        Like

    • kevin says:

      Nooooooooooo!!!!!

      Like

      • KELVIN says:

        MIMI NATETEA UKRISTO WA KIPENTEKOSTE NENO LOLOTE LITAKALOONGEZWA KATIKA BLOGG HII KWA KUTUMIA JINA LANGU KAMA SI LAKUTETEA UKRISTO WA KIPENTEKOSTE ULAANIWE KAMA UNA SWALI NIULIZE

        Like

    • emmanuel says:

      muhamad siyo mtume,hana sifa yoyote ya nabii na kuran haina vigezo vya kuwa kitabu cha Mungu.

      Like

      • dotto says:

        Ni udhaifu wako tu wa elimu nenda kwanza ukasome ndo uje hapa, thibitisha madai yako hatupo kwenye maonyesho hapa

        Like

  10. lipyanda says:

    kundi moja la majini waliomini qur’an ni sawa kabisa na wanadamu walioamini qur’an yaani waislam;
    kundi moja la majini hawajamini qur’an ni sawa kabisa na wanadamu wasioamini qur’an ni akina nani hao?
    ikumbukwe kwamba, muovu akitubu usamehewa, na yesu analijua hilo! Tatizo wapi? Mnakwama wapi?
    Mungu ndie muumba wa kila kitu.
    Mmekwama wapi? Mboma roho mtakatifu alimwongoza yesu aende akjaribiwe na shetani? Hili nalo kwanini hulizungumzi? Ndugu yako jini, shetani, kahaba, mzizi, mlevi, nk. akiacha tabia yake hiyo chafu na kumrejelea muumba, anakuwa mzuri na mungu umsamehe madhambi yake yote.
    NA KUHUSU SWALA LA MANABII WA UONGO aliotabiri yesu kuweza kujitokeza mtume Paulo linamgusa moja kwa moja. Ndugu hebu jaribu kusoma vizuri sana matendo ya mitume mwanzo mwisho utaligundua hili nalosema mimi.
    Mafundisho ya mtume huyu yametofautiana kabisa na mafundisho ya yesu wa nazareti. Ni kweli kabisa kwamba huyu mtu kadanganya wengi sana kwa kutumia picha ya yesu.
    Mathayo 5:17-19 ni msingi wa mafundisho ya yesu, lakini Paulo kauteketeza msingi huu. Je! huyu atakua mtu wa mungu kweli? Yaani jamaa anapingana na maagizo ya mungu ambayo yesu mwenyewe ambaye yeye anamhubiri hakutengua. Huyu jamaa kadanganya wengi sana, na waliodanganyika hawasikii wala hawashikiki pamoja na ushahidi kujionyesha waziwazi kwamba huyu mtu ni mdanganyifu.
    Jamani msisome maneno ya mungu kwa jazba, tafuteni ukweli. Maagano ya mungu yapo mawili ISAKA NA ISMAILI.
    ISAKA kwa ajili ya kizazi chake tu;
    ISMAILI TAIFA KUU!
    wasalam

    Like

    • Lipyanda ndugu yangu katika mwili, kinachokushangaza wewe Yesu kujaribiwa na Shetani ni kitu gani? kuwa wazi usaidiwe. Swala la majini ni kitu kingine, majini wote ni malaika walioasi kwa lugha ya biblia ni mapepo, hata qruan inajua hilo, qruan 72:14 hakika zamani tulikuwa tukikaa huko, lakini tulifukuzwa huko na sasa tukijaribu kwenda tunapigwa na vimondo” maneno haya waliyasema majini, na biblia katika ufunuo inasema Shetani alifukuzwa na theluthi ya malaika waliokuwa wakimuunga mkono. sasa shida yako iko wapi, nyinyi mnadanganywa na hao majini, na kwa sababu baba yenu shetani ni baba wa uongo nanyi mwakubaliana na huo uongo wa baba yenu. Biblia inasema 2petro 3:15 “Mambo aliyoyaandika mtumishi wa Mungu paulo, kwa watu wasio na elimu ni vigumu kuyatambua, na kwa watu wasio na akili huyapotoa kama wayapotoavyo na maandiko mengine” Najua kinachokuchanganya wewe ni suala la kutahiriwa pale paulo aliposema kutahiriwa si kitu! lakini ngonja nikuulize, Henoko mtu wa tano kutaka kwa adamu alionekana kuwa mkamilifu kuliko watu wote duniani, na Mungu alimtwaa mtu huyo, je! wapi henoko katahiriwa? inshu ya kutahiriwa ilifanyika kwa Ibrahimu na uzao wake tu basi. kama unabisha wapi adamu katahiriwa? wewe ndo umelengwa na kile kitabu cha Petro ya kwamba huna akili hivyo huwezi kuyaelewa mambo aliyoyaandika mtumishi wa Mungu Paulo. hatugombani ila tunaeleweshana.

      Ev.Moses Mayila

      Like

      • THOMASO says:

        Ndugu!
        1.Hata mm pia kinanishangaza inakuwaje Bwana Mungu (Yesu Kristo) ambaye ni Bwana na Mwokozi wa maisha yetu ajaribiwe na kiumbe alichokiumba tena akakilaani na akakiita sheitani na siku ya mwisho atakiangamiza katika jahanam kimburuze mpaka nyikani na kimuulize maswali ya kipuuzi(sily questions) yaani kimjaribu? Kweli shetani huyu ilikuwaje akawa na mamlaka juu ya Mungu wake? tena sio kidogo bali kwa masiku 40! sasa tutaaminije labda baada ya hapo alianza kusema maneno yaliyotoka kwenye mamlaka za giza!!

        TUANGALIE MUNGU ANASEMAJE KTK MANENO MATAKATIFU SASA!
        Yakobo 1:13 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, ninajaribiewa na Mungu; maana Mungu hawezi KUJARIBIWA na maovu (Ibilisi), wala mwenyewe hamjaribu mtu”

        2.Mtumishi wa Mungu umedanganya uliposema kutahiriwa kwa Ibrahim nanukuu “inshu ya kutahiriwa ilifanyika kwa Ibrahimu na uzao wake tu basi.” hiyo siyo kweli emb tusome biblia inasemaje.
        MWANZO 17:9 “Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako.Hili ndilo agano langu utakalolishika kati ya mimi na wewe na uzao
        wako, Kila mwana mume wa kwenu atatahiriwa.Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi MTOTO WA SIKU NANE ATATAHIRIWA
        KWENU, KILA MWANAUME KATIKA VIZAZI VYENU, MZALIWA NYUMBANI, NA MNUNULIWA KWA FEDHA, KILA MGENI ASIYEKUWA WA UZAO WAKO. MZALIWA
        NYUMBANI KWAKO NA MNUNULIWA KWA FEDHA YAKOO LAZIMA ATATAHIRIWA AN AGANO LANGU KATIKA MWILI WENU LITAKUWA LA MILELE. NA MWANAMUME MWENY GOVI ASIYETAHIRWA NYAMA YA GOVI LAKE, MTU YULE ATATENGWA NA WATU WAKE; AMELIVUNJA AGANO LANGU”
        je kama umeshindwa kufanya uadilifu katika biblia ambacho ni kitabu cha Bwana na Mwokozi wa maisha yetu Yesu Kristo je? uchambuzi wa Quran tukufu ya waislam utaifanyia uadilifu??
        NASUBIRI MAJIBU YA MTUMISHI WA BWANA!!

        Like

    • sebard says:

      Acha porojo ndugu eleza kwa ushahid uongo wa paulo ili ueleweke vinginevyo hizo ni propaganda tu na upotoshaji wa ukristo kubali kuwa ummemwasi Mungu kwa kuto mkiri kristo kuwa ni Bwana na Mokozi wa ulimwengu.

      Like

      • bothlegs says:

        wacheni ukafiri wenu huo,huo uungu yesu kaupata wapi.Mungu wa kweli ni yule aliyeumba mbingu na ardhi na kila kilichomo.Yesu hawezi kuumba hata inzi.

        Like

  11. Ezekiel says:

    Je yesu si ndio njia sahihi ya kwenda mbinguni?

    Like

    • lipyanda says:

      Manabii na mitume wote wa mungu ni njia sahihi ya kwenda mbinguni, kwa kuyashika na kutekeleza barabara mafundisho yao waliyofuniliwa na mungu kwa wanadamu.
      MUSSA aliteremshiwa taurati hili iwe fundisho kwa watu wake kumuelekea mungu;
      DAUDI na zaburi kwa watu wa wakati wake;
      YESU na injili kwa watu wa wakati wake;
      MUHAMMAD na qur’an kwa watu wa zama hizi. Vitabu hivi vyote vina ujumbe wa mungu kwa wanadamu.
      Kwa maana hiyo, zote hizi ni njia za kwenda mbinguni.
      Kwa maana nyingine ni kwamba, binadamu yeyote anapaswa kuyamini, kuyashika, na kutekeleza yale yote aliyoyasikia kwa manabii au mitume hili aweze kwenda mbinguni.
      Ukiacha kuyashika yale yaliyo maagizo ya mungu wewe umepotea njia. Mfano: mungu kasema tahiriwa alafu wewe unapinga na unasema kutahiriwa si chochote, moja kwa moja wewe unapingana na mungu.
      wasalaam

      Like

      • Lipyanda ndugu yangu unaposema Muhamad aliteremshiwa qruan kwa watu wa kizazi hiki mimi nakubaliana na wewe kwa njia moja. Muhamad kweli alipewa qruan lakini haikutoka kwa Mungu bali kwa Mashetani! angalia kitabu cha mkweli mwanifu ukurasa 26 au 29 hivi, kinaeleza jinsi muhamad alivyopokea utume. yeye mwenyewe kwa kinywa chake alisema “Najihofia nfasi yangu maana nimechezewa na mashetani” kauli hii aliisema baada ya kukabwa na mashetani huko kwenye majabali, yanamlazimisha kusoma hali ya kuwa muhamad wa watu hajuwi kusoma! muhamad anajibu mimi sijuwi kusoma, mashetani yanazidi kumlazimisha asome. na kwa waislamu wao hudai kwamba yule alikuwa malaika jibrir lakini hakuwa malaika wa Mungu bali alikuwa wa shetani, ndio maana Muhamad akasema anajihofia nfsi yake maana amechezewa na mashetani. halafu mkewe (Khadija) akamwambia usiseme hivyo wewe huwezi kuchezewa na shetani maana unasifa nyingi unafanya hivi unafanya vile, mimi naona umeshapata utume! tangu siku hiyo muhamad akaanza kujiita mtume hata kufa kwake.
        tuiangalia katika hali ya kawaida Mungu hawezi kumkaba mtu kama alivyokabwa muhamad halafu Mungu aondoke asijitambulishe kwake! angalia 4:4 Yeremia utaona jinsi Mungu anavyochagua mitume na manabii.

        Like

    • Ezekiel, Yesu peke yake ndiye njia sahihi matendo ya mitume 4:12 “Maana hapana jina jingine chini ya mbingu na nchi tulilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

      Like

      • chidy rakim says:

        hayo maandiko unayotoa ni ya paulo sio ya yesu wala mungu huo paulo aliepotosha watu

        Like

      • dotto says:

        Acha uongo Yesu mwenyewe alishasema hajaja kutengua torati bali kutimiliza kwani anajua wazi kwamba hata mitume iliyo kuwepo ilikua sahihi sawa New Hope Ministry? fanya uadilifu usidanganye watu bana

        Like

  12. lipyanda says:

    Unajua wewe ni mvivu wa kuyaelewa maandiko. Mungu uchagua manabii atakavyo. Yeremia 4:4 haitambui manabii wanavyochaguliwa ‘”4 Jitahirini kwa Bwana, mkaziondoe govi za mioyo yenu, enyi watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu; ghadhabu yangu isije ikatoka kama moto, ikawaka hata mtu asiweze kuizima, kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.'” Hapo kuna namna ya uchaguzi hapo?
    Ndugu yangu kaa ukijua ya kwamba Muhammad kabla ya kupewa utume alikua kama ulivyo wewe. Binadamu yyte mshangao lazima linapokuja swala ambalo hakutegemea kukumbana nalo, hisia nyingi zinaweza kumjia kwa muda mfupi.
    Sasa usiangalie upande mmoja na wa pili pia lazima tuangalie. Kwa mujibu wa maandiko Yesu kalaaniwa, hastahili kuwa njia ya kwenda mbinguni ushahidi upo. Yeremia 22:24-30 “” 24 Kama niishivyo mimi, asema Bwana, hata Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, angekuwa pete yenye muhuri katika mkono wangu wa kuume, ningekung’oa wewe hapo;
    25 nami nitakutia katika mikono ya watu wale wakutafutao roho yako, na katika mikono yao unaowaogopa, naam, katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya Wakaldayo.
    26 Nami nitakutupa nje, wewe na mama yako aliyekuzaa, mwende nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko.
    27 Lakini nchi ile ambayo wanatamani kuirudia, hawatairudia kamwe.
    28 Je! Mtu huyu, Konia, ni chombo kilichodharauliwa, na kuvunjika? Ni chombo kisichopendeza? Mbona wametupwa, yeye na wazao wake, na kutupwa katika nchi wasiyoijua?
    29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
    30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda””. Sema na hapo sasa, kauli ya mungu ndio hiyo ishatoka. Keshalaaniwa konia au yekonia au joachim pamoja na uzao wake ambapo katika uzao huo yesu yupo!
    La mwisho kabisa nataka nikwambie hivi: kuhusu swala la kumkukataa Muhammad kuwa mtume wako, haina maana na wengine wasimkubali, coz kwa uzoefu wangu hata jesus alikataliwa kwao.

    Like

  13. lipyanda says:

    Jamani, waliokuwepo kabla ya yesu wameokolewa kwa jina gani? Acheni kuzishabikia kauli za kibinadamu.
    Matendo ya mitume 4:12 ni maneno ya Petro! Petro huyu ni yule mwenye mawazo ya kibinadamu, hayawazi ya mungu.
    Wapi kwenye biblia mungu anasema hivyo au yesu mwenyewe?

    Like

  14. lipyanda says:

    sura ya majini hii hapa:

    KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

    1. Sema: Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini lilisikiliza, na likasema: Hakika sisi tumeisikia Qur’ani ya ajabu! ***

    2. Inaongoza kwenye uwongofu, kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu Mlezi. ***

    3. Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu Mlezi umetukuka kabisa; hana mke wala mwana. ***

    4. Na kwa hakika wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema uwongo ulio pindukia mipaka juu ya Mwenyezi Mungu. ***

    5. Nasi tulidhani kuwa watu na majini hawamzulii uwongo Mwenyezi Mungu. ***

    6. Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi. ***

    7. Na kwa hakika wao walidhani, kama mlivyo dhani nyinyi, ya kuwa Mwenyezi Mungu hatamleta Mtume. ***

    8. Nasi tulizigusa mbingu, na tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na vimondo. ***

    9. Na hakika tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza; lakini sasa anaye taka kusikiliza atakuta kimondo kinamvizia! ***

    10. Nasi hatujui kama wanatakiwa shari wale wanao kaa kwenye ardhi au Mola wao Mlezi anawatakia uwongofu. ***

    11. Na hakika katika sisi wamo walio wema, na wengine wetu ni kinyume na hivyo. Tumekuwa njia mbali mbali. ***

    12. Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani, wala hatuwezi kumponyoka kwa kukimbia. ***

    13. Nasi tulipo usikia uwongofu tuliuamini. Basi mwenye kumuamini Mola wake Mlezi basi haogopi kupunjwa wala kudhulumiwa. ***

    14. Na hakika wamo katika sisi Waislamu, na wamo kati yetu wanao acha haki. Basi walio silimu, hao ndio walio tafuta uwongofu. ***

    15. Na ama wanao acha haki, hao watakuwa kuni za Jahannamu. ***
    Ndugu Moises, kuna majini walioamini quran wakasilimu na kuna majini wasioamini, wao hawajasilimu. Maana yake ni hivi, wale wote waliosilimu wameacha kumwasi mungu na wale wote wasiosilimu wanaendeleza ushetani na ni ndugu na wakristo kwa ushahidi ufuatao:
    Walawi 16:7-10 7 Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweka mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania.
    8 Na Haruni atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya Bwana; na kura ya pili kwa ajili ya Azazeli.
    9 Na Haruni atamleta yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Bwana, na kumtoa awe sadaka ya dhambi.
    10 Bali yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atawekwa hai mbele za Bwana ili kumfanyia upatanisho, ili kumpeleka jangwani kwa ajili ya Azazeli.
    Azazeli ni shetani.
    Wamuzi 9:23-24
    23 Kisha Mungu akapeleka roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu; nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa udanganyifu;
    24 ili kwamba huo udhalimu waliotendewa hao wana sabini wa Yerubaali uje, tena kwamba damu yao iandikwe juu ya Abimeleki ndugu yao, aliyewaua, na juu ya watu wa Shekemu, waliomtia nguvu mikono yake ili awaue hao nduguze.
    Hapa tunaona Roho mbaya (shetani) anatoka kwa mungu.
    1 Samwel 16:14 14 Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.
    Kwa mara nyingine tunaona roho mbaya (shetani) akitoka kwa mungu wenu.
    1 Timoteo 1:20 20 Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
    Maneno hayo ni ya Paulo, yani shetani ni mshirika wake katika kuhubiri neno la mungu.
    1 Petro 3:19 19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;
    Huyu hapa ni yesu sasa, aliekwenda kuwahubiria roho zilizofungwa na mungu, yaani mashetani.
    Ayubu 1:6-11
    6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
    7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
    8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
    9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
    10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
    11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.
    Hapa shetani na mungu wanaongea kama mtu na rafiki yake, hana wasiwasi wowote!!!!
    Asili ya shetani ni kupinga neno la mungu.
    Sasa, ebu tuangalie Paulo mtume kapinga wapi? na kama kapinga si atakua shetani kwa mujibu wa maandiko? Henoko na Adam waliishi kabla ya sheria ndugu yangu, kwa maana hiyo hatuwezi kuwahesabia.
    Yesu alisema hivi katka math 5:17-19 17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
    18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie.
    19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.
    Katika hilo sasa Paulo anasemaje kwenye waefeso 2:15
    15 Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani..
    Hapa mimi nakumbuka pale aliposema yesu kwamba watatokea manabii wa uongo na watadanganya wengi, maana watu wanaacha kufuata mafundisho ya yesu mwenyewe wanakuja kuyapokea mafundisho ya mtu ambaye hajawahi kuwa mwanafunzi wa yesu hata kwa chembe moja.
    Yesu anasema nini matayo 7:21-23 21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
    22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
    23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
    Hapa yesu anasema matendo lazima katika imani.
    Paulo anasemaje kwa hilo?
    War. 3:28 28 Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria. Tofauti kabisa na yesu. Je mpaka hapo huyu jamaa atakuwa mtu wa mungu kweli?
    Mat. 7:15-20 15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
    16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
    17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
    18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
    19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
    20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.
    Nabii wa uongo anajulikana kwa matunda yake, yesu kasema. Ndugu yangu Paulo kwa hili linamgusa kwa % zote. Neno la mungu halipingwi

    Like

  15. Meshack says:

    Majini ni Mashetani (malaika walioasi mbinguni)no Justification, kushirikiana nayo kwa namna yoyote ni kuenda kinyume Mungu.

    Like

  16. lipyanda says:

    Mr. Meshack
    Mi nadhani wewe una ufinyu wa kuelewa mambo, na hoja zinazohusiana na mungu unazifanyia masihara. Unaposema no justification maana yake nini? Kama jambo ulielewi uliza ujibiwe.
    Sasa ebu nikufundishe:
    Mungu kaumba malaika na binadamu, hili tumwabudu. Katika sisi sote (malaika na binadamu) mwenye kumuasi mungu anaitwa shetani, mfano: jamii ya freemassons kwa wanadamu na majini kwa malaika. Ushetani ni tabia ya kumpinga mungu.
    Freemasson (shetani), akiacha ufreemasson wake na kuyapokea yaliyo ya mungu anakua nani?
    Vivyo hivyo kwa majini!!! Unakwama wapi ndugu yangu Meshack?
    Haya mambo ya majini, malaika wachieni waislamu wenye elimu nae. Qur,an ni maneno ya mungu tofauti na biblia ambayo ni maneno ya wandishi. Na siku zote wandishi wana tabia ya kupotoa ukweli na kujifurahisha wao, yeremia 8:8.
    Qur’an kaongea mungu mjuzi na muumba wa kila kitu.
    Halafu ushirika wa waislamu na mashetani haupo na hautakuwepo milele. Hila tu endapo ataacha tabia yake chafu tutashirikiananae. Sisi waislam kabla ya kutenda jambo lolote lile, tunaanza kwa kumlaani shetani.
    Kwenu nyinyi Meshack swala hilo halipo kwa sababu ya: 1 Timoteo 1:20 ” Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”. Maneno haya ya ushirika na shetani ni ya Mtume wako Paulo. Mpaka hapo hatujajua mangapi mmepokea kutoka kwa shetani na mangapi kutoka kwa Paulo.
    Galatia 2:7 “‘
    ”7 bali, kinyume cha hayo, walipoona ya kuwa nimekabidhiwa injili ya wasiotahiriwa, kama vile Petro ya waliotahiriwa; ”
    Kwa ushahidi wake paulo injili zipo mbili.
    Petro alikabidhiwa moja kwa moja na yesu (enendeni ulimwenguni kote mkayubiri injili kwa kila kiumbe). Sasa tuangalie je Paulo kweli alikabidhiwa na yesu? Maandiko yafuatayo yatatupa picha kamili:
    Mat. 24:4-5 ”4 Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye.
    5 Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.”’ Yesu anawaonya wanafunzi wake kwa namna hiyo.
    Mat. 24:23-26 ”23 Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.
    24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
    25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.
    26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki.”
    Meshack kwa mujibu ya maonyo ya yesu kwa wanafunzi wake, kupitia aya hizo hapo, YESU ALIENTOKEA PAULO WAKATI ANAENDA DAMESKY NI WA KWELI?
    Paulo sio mtume wa kweli kwa sababu injili yake inapingana na ya yesu:
    1- yesu anasema, sheria na manabii havitenguki mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka;
    lakini paulo anasema vimetenguliwa;
    2- yesu anasema, kwa baba yangu ambae ni baba yenu; kwa mungu wangu ambae ni mungu wenu;
    lakini paulo anasema yesu ni mungu mwenyewe;
    3- yesu analaani pombe;
    lakini paulo anabariki.
    YESU NA PAULO TUMKUBALI NANI? MBONA NYIE WAKRISTO MNAIFUATA INJILI FEKI YA SHETANI ANAEPINGANA NA MUNGU? MKIULIZWA HOO PAULO KASOMA SANA, KASOMESHWA NA NANI? NA HUYO ALIENSOMESHA PAULO ATAKUWA NANI SASA?
    ELIMU YA MUNGU INA MUNGU MWENYEWE SIO BINADAM.

    Like

    • meshack says:

      “MBONA NYIE WAKRISTO MNAIFUATA INJILI FEKI YA SHETANI ANAEPINGANA NA MUNGU?”

      Naomba uniambie injili liyosahihi iko wapi na hii ambayo sisi wakristo tunaitumia ina mapungufu sehemu gani??

      Like

  17. Meshack says:

    Vizuri sana Mr. Lipyanda naona saa hizi umeanza kuelewa baada ya kukataa muda mrefu. Kumbe kuna malaika waasi kwa mujibu wa biblia (ambao ni mashetani/majini) na hata kwa mujibu wako ulivyosema hapo juu “Mungu kaumba malaika na binadamu, hili tumwabudu. Katika sisi sote (MALAIKA na binadamu) mwenye kumuasi mungu anaitwa SHETANI” Na malaika walifanya uasi, na baadhi ya malaika wale waliomuasi Mungu leo tunawaita mashetani/majini
    katika
    Ufunuo. 12:7-12 “ Kulikuwa na vita mbinguni, Mikael na Malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake, nao hawakushinda, wala mahala pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa yule mkubwa nyoka wa zamani aitwaye Ibilisi na shetani audanganyaye ulimwengu wote, akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema sasa kumekuwa wokovu, na nguvu na ufalme wa Mungu wetu kwa maana ametupwa chini mshtaki wa ndugu zetu yeye awashtakiye mbele za Mungu wetu. Mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo na kwa neon la ushuhuda wao ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. Kwa hiyo shangilieni enyi mbingu, nanyi mkaao humo. OLE WA NCHI NA BAHARI! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”

    lakini hakuna malaika waasi kwa mujibu wa Quran, (kwa mujibu wa Quran Malaika wote ni wema)

    Quran suratul As- Sajdah, (kusujudu) , 32:13 “ Na tungelitaka tungempa kila mtu uwongofu wake (kwa lazima kama tulivyowapa malaika lakini binadamu amepewa huria ya kufanya alitakalo- lililo jema na baya).

    Lakini bado haohao malaika ambao Quran inadai wote ni wema, miongoni mwao (Haruta na Maaruta) ndio walioshusha uchawi duniani na Mungu wenu ALLAH akiwa ni mwenye kuidhinisha utendaji wa huo uchawi kwa binadamu.

    Katika Suratul, al- Bagarah, (ng’ombe jike), 2:102 “ Wakafuata yale waliyoyafuata mashetani wakadai kuwa yalikuwa katika ufalme wa nabii suleimani na Suleiman hakukufuru bali mashetani ndiyo waliokufuru, wakiwa fundisha watu uchawi waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani. Na uchawi uliteremshwa kwa malaika wawili Haruta na Maaruta katika mji wa Babeli wala malaika hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie hakika sisi ni mtihani wa kutazamwa kutii kwenu basi usikufuru wakajifunza kwao ambayo waliweza kumfarakisha mtu na mkewe na mengineyo wala hawakuwa wenye kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu(ALLAH).

    “NO JUSTIFICATION”
    Malaika Waliomuasi Mungu(YEHOVA) ni mashetani/majini yanasubiri moto wa Jehanamu tu.
    Amua sasa! Mfuate Yesu kristo wa nazareth aliye hai, achana na Muhammad.

    Like

  18. lipyanda says:

    Meshack!
    Mimi ni mfuasi mzuri sana wa Yesu Mnazareth kuliko wewe. Yaani wewe hujijui kama si mfuasi wa yesu. Wewe unamfuata Paulo ambae anatumia picha ya yesu hili kuwadanganya wengi. Mwenyewe yesu aliwatahadharisha waisraeli ambae alitumwa kwao, kujitokeza manabii wa uongo kama ilivyo kwa huyu. Paulo katika mahubiri yake alikuwa anashirikiana na shetani, 1timoteo 1:20 “” Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.”” Kwa ushahidi huo unatosha kabisa kubainisha ya kwamba, ukristo ni ushetani.
    Sehemu nyingine ni Roho ya mungu wenu ilishirikiana na ibilisi(shetani) hili wamjaribu yesu. mathayo 4:1-10 “” Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
    2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
    3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
    4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
    5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,
    6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
    7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
    8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
    9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
    10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.””
    Meshack! Hiyo ni mipango ya mungu wenu na shetani ya kutaka kumjaribu yesu.
    Nasikitika kwamba haya yote huyaoni, badala yake we unan’gan’gania majini tu kwa sababu ya kusikia qur’an na wakasilim? Mbona yesu alienda kuwahubiria roho mbaya zilizofungwa. Alikuwa na maana gani kufanya hivyo? 1 Petro 3:19
    ” ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; ” Mbona huyasemi haya mr. Meshack kwanini?
    Meshack! mungu kaumba mabaya na mazuri kwa ajili ya kuwachalenji binadamu na majini. Sasa, ukisikia neno malaika wa mungu ni viumbe waliyo kati ya mwanadam na mungu katika kuwasiliana au kwa jambo lengine lolote linalomhusu mungu. Malaika wa mungu ni viumbe safi mbele ya mungu. Kila laika mungu amempangia kazi yake ya kuifanya kama vile, uchawi, gharika, heri, kifo, wahai kwa manabii, nk…Waamuzi 9:23 ”Kisha Mungu akapeleka roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu; nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa udanganyifu; ” Mungu kapeleka roho mbaya(shetani), kachukuwa wapi?
    1sam. 16:14-15 ”
    14 Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.
    15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua. ” hapo vipi?
    Baada ya kujifunza ya kwamba wakristo ndio washirika na shetani, kwa maana nyingine kuwa ni mashetani, tujifunze sasa katika ufunuo 12:7-12. Meshack! Mi naona wewe si mtanzania, maana kiswahili hukijui, yaani kwa akili zako wewe lile joka la zamani lililozungumziwa hapo ni jini? Joka la zamani ni hili hapa: mw 3-1”1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
    2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
    3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
    4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,
    5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. ”Sasa baada ya haya mungu akamwambiaje huyu nyoka? mwz 3:14-15 ”14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;
    15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino. ” Haya sasa Meshack! joka katupwa chini kutoka kule bustanini kama alivyoahidi mungu katika mistari hiyo. We si unawaona majoka mengi mengi tu hapa chini wakitambaa? Ni nini kinakusumbuwa ndugu yangu?
    Katika kumalizia soma mistari ifuatayo: Ayubu 1:6-12 ”6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
    7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
    8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
    9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
    10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
    11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.
    12 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana. ” Ndugu yangu tumeona hapa shetani yupo kila kona, mpaka mbinguni kwa mungu yupo, tumeona mungu alivyomtumia shetani katika kufanikisha azma yake.
    Meshack mambo ya mungu usiyachukulie kama kiigizo, enendana na maagizo ya mungu ambayo yapo kwenye vitabu vya mungu.
    MAJINI yameumbwa na moto;
    MALAIKA wameumbwa na nuro;
    BINADAM kaumbwa kwa udongo;
    Shetani muasi kajitokeza katika kundi la majini. Hapa lazima uelewe, sio majini wote walioasi, ni mmoja wao nae akabilisi majini wenzake na wanadamu hili wazifuate njia zake. Wengine wakanfuata na wengine hawakunfuata.
    UKUBALI NA USIKUBALI, HAPA DUNIANI KUNA MAMLAKA MBILI. MOJA YA SHETANI NA MOJA YA MUNGU MWENYEZI.
    YA SHETANI KAZI YAKE NI KUPOTEZA WATU WASIMJUWE MUNGU WA KWELI
    WAPO WATU HAO HATA LEO HII WASIOMJUWA MUNGU WA KWELI.
    MAASI YANAONGEZEKA KILA KUKICHA; WAUME KUOANA WENYEWE KWA WENYEWE.
    WANAWAKE KUTEMBEA NUSU UCHI, KUYAACHA YALIYO MAAGIZO YA MUNGU NA KUYAFUATA YA KIBINADAM.

    NAKUOMBA UYAZINGATIE UKIBAINI UKWELI USISITE KUUFUATA. NJOO KWANGU HILI UNFUATE VIZURI YESU.

    Like

    • Gwebuuza! says:

      nimekuelewa mwalimu!
      yaani bwana wa wakiristu anamwambiea shetani(rafiki yake) ambaye ni ibilisi/jini/pepo kuwa amkufurishe Nabii Ayubu Kwa kumtia majaribu, duh!! siamini amri kama hii itoke kwa Mungu. ndo maana wenzetu wanapagawa sana na mapepo makanisani kwa sababu mungu wao ana ushirika na mashetani/mapepo ama majini. nakushukuru mwl nilikuwa sijui siri hiyo.

      Like

      • Sasa nyinyi waislamu mnshangazwa, kuona Mungu anamruhusu shetani amjaribu Ayubu lakini hamjuwi kama qruani inasema “Tumetuma mashetani juu ya makafiri ili wawaongoze kutenda mabaya” pia qruan hiyo hiyo inasema “Uchawi hauwezi kumdhuru mtu ila kwa idhini ya mwenyezi Mungu” na ndio maana hata mtume wenu Mohamad alilogwa akaugua sana! sasa aya hizi hamziangalii! je huyu mungu mnamweka kundi gani sasa?

        hebu leteni hoja zenye nguvu tujadili sio hizi za kitoto. pale dar es salaam tulikuwa tunajadili hoja zenye nguvu na akina mazinge na akina kabunga!

        Like

      • Gwebuuza! says:

        JIBU KWA MCHUNGAJI WA NEW HOPE MINISTRY
        Nakunukuu “Sasa nyinyi waislamu mnshangazwa, kuona Mungu anamruhusu shetani amjaribu Ayubu”

        AHAA KUMBE MUNGU “ANAMRUHUSU SHETANI” KUMJARIBU “NABII AYUBU”….
        JE HUONI KWAMBA UMEJIJIBU????
        VIVO HIVO MUNGU “ALIMRUHUSU(HAKUMTUMA) SHETANI KUMJARIBU MTUME (S.A.W) KWA KUMROGA.” Na ndo sababu Allah (SW) akashusha sura hii

        QURAN SURA 114.
        KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
        1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,
        2. Mfalme wa wanaadamu,
        3. Mungu wa wanaadamu,
        4. Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,
        5. Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,
        6.(na shari) inayotokana na majini na wanaadamu.

        2.KUMBE PIA UNATAMBUA KUWA SHETANI(MCHAWI) HAFANYI KAZI MPAKA MUNGU AMRUHUSU KAMA ALIVYORUHUSU KWA AYUBU.
        Ngoja nikufundishe sasa: Sisi waislam tunaamini kwamba Mungu ndo anao uwezo wa kutukinga na kila shari, ila asipotaka kukukinga basi hiyo shari haina budi ikupate.
        Shetani hawezi kumshinda Mungu bali Mungu anamwacha tu.

        3.SHETANI ALIMJARIBU MUNGU WA WAKIRISTU
        Shetani alipata wapi mamlaka ya kumjaribu mungu wenu kwa masiku 40??
        ina maana shetani ana nguvu kuliko mungu wenu?? au ni rafiki yake!!

        4. MUNGU ANASHINDWA KUJISAIDIA MSALABANI MPAKA ANAMWITA ALLAH!!
        Mungu wa wakiristu alipowambwa msalabani alimwita ALLAH(S.W) hii inaonesha jinsi gani anavyotambua uwezo wake…
        MATHAYO “ALLAH! ALLAH! LAMA SABAKHTAN YAANI MUNGU WANGU MUNGU WANGU MBONA UMENIACHA…”
        KARIBU KATIKA UISLAM! INSHAALLAH.

        Like

    • al-akhi shekijangwa says:

      Allah s.w.t akuongeze elimu yenye kukufaa dunia na akhera.
      Allah ni mjuzi wa yote

      Like

  19. Machibya J says:

    Ndugu zangu nachanganyikiwa kidogo hapa naomba verification, Yesu alipokua anahubiri alisema ….Mimi ni njia ya kweli na uzima Mtu haji kwa baba ila kupitia kwangu……(Not Cited) Nimesikia Malumbano youtube Presenter Mmoja anasema Muhamad S.A.W alisema kwamba …….hajui atakalotendewa yeye wala watakalotendewa wafuasi wake siku ya mwisho…….(Not Cited). Maneno haya ni kweli? na yana maana gani? Please ufafanuzi ndugu zangu and Mungu Muumba Mbingu na vitu vyote vinavoonekana na visivoonekana awabariki

    Like

    • dotto says:

      Kuhusu Yesu kuwa njia wa kweli ni sawa sababu yeye n mtume ndo aliyetumwa na Mungu kwa wanadamu ili kutujuza habari za mungu yaan yeye n mtume Yohana 17.3 na Kuhusu Mtume Muhammad (saw) yeye n mtume tu ila mwenyezi Mungu ana jua zaidi na ndo mfalme ktk siku ya hukumu

      Like

  20. lipyanda says:

    Mr. Machibya J
    Mwanzo 17:19 ” Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake.”
    KWA MUJIBU WA AYA HIYO, MUNGU ATAFANYA AGANO LAKE KWA ISAKA KWA AJILI YA UZAO WAKE TU.
    NA UZAO WA ISAKA NI PAMOJA NA YESU NA MANABII WENGINE WOTE WALIOTOKEA KWA IMANI YA KIYAHUDI.
    Yohana 14: 6 ” Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”
    HAPA, YOYOTE YULE AMBAE SIO MUISRAELI HAIMHUSU NJIA HII.

    Yohana 17:3-4 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
    4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.

    Yohana 17:6-9 6 Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
    7 Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako.
    8 Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
    9 Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
    KAULI YA YESU INASEMA HAUOMBEI ULIMWENGU, BALI WALE ALIOPEWA.

    Matendo 13:23 Katika uzao wake mtu huyo Mungu amewaletea Israeli Mwokozi, yaani, Yesu, kama alivyoahidi;

    Matendo 5:31 Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

    Matayo 15:24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

    Mr. unajichanganya unapomn’gan’gania Yesu kama mwokozi wako.
    Sasa basi, NI NANI MWOKOZI WAKO?

    Mwanzo 16:10 Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.
    11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako.
    12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
    HAPA TUNAONA AHADI YA MUNGU JUU YA MTOTO WA IBRAHIM ATAKAEZALIWA NA HAJIRI.

    MKONO WAKE UTAKUWA JUU YA WATU WOTE, NA MKONO WA WATU WOTE UTAKUWA JUU YAKE NAYE ATAKAA MBELE YA NDUGU ZAKE WOTE. MR. ZINGATIA SANA AYA HII, YAANI AGANO LA WATU WOTE LINATOKA KWA ISHMAELI KWA MUJIBU WA ANDIKO. MAAGANO MENGINE NI CHA MTOTO KWA SABABU ISHMAELI ANALISI BARAKA ZA BABA MZEE IBRAHIM.
    Mwanzo 17: 20 Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu.

    Waefeso 1:12 Nasi katika huyo tupate kuwa sifa ya utukufu wake, sisi tuliotangulia kumwekea Kristo tumaini letu.
    13 Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.
    14 Ndiye aliye ARABUNI ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake.

    Wagalatia 4:21 Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je! Hamwisikii sheria?
    22 Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana.
    23 Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa ahadi.
    24 Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri.
    25 Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko ARABUNI, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto.

    Matayo 21:
    42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?
    43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
    44 Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki.

    Marko 1:14 Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu,
    15 akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili.
    UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA, TUNAONA JINSI GANI BAADHI YA MATAIFA YAKITUMIA KITABU CHA AL QURAN KAMA KATIBA YAO. HUU NDIO UFALME WA MUNGU ALIOSEMA YESU UMEKARIBIA.

    Matayo 10:6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
    7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

    Matayo 23:36 Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
    37 Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
    38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
    39 Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
    HAPA TUNAONA MUNGU ANALITENGA TAIFA LA ISRAELI. LAKINI PIA KUNA KAULI YA AMEBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA. SWALI JIULIZE, NANI KAJA BAADA YA YESU?

    Yohana 14:2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
    3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
    MAANA YA AYA HII NI KWAMBA, NJIA YA KWENDA MBINGUNI HAIPO KWA YESU PEKEE, IPO PIA KWA MANABII WENGINE WA KABLA YAKE NA BAADA YAKE. NJIA INAMAANISHA, KUMWAMINI MUNGU, NA KUFUATA MAAGIZO YAKE AMBAYO MUNGU UWATUMIA MANABII.

    Matayo 24:36 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.
    HAPA NAJIBU HOJA YAKO JUU YA NABII MUHAMMAD(SAW), KUMBE HATA YESU HAJUI.

    Like

    • abdulkarim says:

      Habari wa pendwa.
      Kunajambo moja hawa makafiri. Wanashindwa kuelewa. Wanasema majini na waislam eti ni ndugu wao hawajioni. Marko 3:11 “na pepo wachafu, kila walipomwona(yesu),walianguka mbele yake,wakilia wakisema, wewe ndiwe mwana wa mungu.leo hii asilimia 95% ya wakristo wanaungana na mashetani katika kukufuru na kudai kuwa mungu yesu ni mtoto wake kumbe wao ndio mabest zao.

      Like

  21. khalifat says:

    asslm alkm: nakupenda sn lipyana na abdu kwa ajili ya Allah
    Makafiri wanauliza: Muhammad (S.A.W) hakusoma je Yesu alisoma mpaka level gani? Chekechea,msingi, secondary au chuo? Mimi nnavyojua manabii hawasomi shule ila Allah huwapa elimu yake.

    MAJINI MAKANISANI AU MSIKITINI?
    Mathayo 16:23 Yesu anamwabia Simon “Simon-Petro nenda nyuma yangu shetani (jini/pepo) wewe maana huyawazi ya Mungu bali ya wanadamu” PETRO ALIKUWA NA MAJINI/MAPEPO
    Mathayo(): Yesu anamwambia “wewe ni mwaba na juu ya mwamba huu nitalijenga KANISA(sio msikiti)”
    KANISA LIMEJENGWA JUU YA MWAMBA WA MAPEPO.
    Mathayo 13:36-38 Yesu anamwambia ” amin! amin! kabla ya jimbi kuwika utanikana mara tatu ” KWA KUWA UNA MAPEPO WACHAFU.
    Mathayo 26:36-46 Yesu akamwmbia “Petro je!hamkuweza kukesha nami hata siku moja” ALIKATAA KUKESHA AKIOMBA NA BWANA YESU KWA SABABU ALIKUWA NA MAPEPO/MASHETWAN/MAJINI
    Ajabu huyu mtu mwenye mapepo ndo aliyejenga kanisa la kwanza kabisa lililoko Vatican linaitwa St. PETER na WAKRISTO kote duniani wanamwita mtakatifu ajabu zaidi alimkana YESU Lakini hainyoshi sehemu yoyote kama Yesu alimsamehe, Hii ndo maana unakuta makanisani kuna mapepo na majini sana kwa sababu YESU alijenga kanisa kwa Mwamba wa MAJINI NA MAPEPO YAANI PETRO.
    MSIKITINI Huwezi kukuta MAPEPO HATA SIKU MOJA.

    Like

  22. byaru says:

    JE YESU(KATIKA BIBLE) AU MUHAMMAD(KATIKA QURAN) NANI ALILETA AMANI DUNIANI?
    Mathayo 10:34-35 “msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani la, sikuja kuleta amani, bali upanga. Kwa maana nalikuja kumfitinisha mtu na babaye, na binti na mamaye na mkew na mkwe mtu” LINGANISHA NA QURAN
    Quran 46:15 “Na tumemuusia mwanaadamu awatendee wema wazazi wake wawili. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu. Na kuchukua mimba kwake hata kumwachisha ziwa ni miezi thalathini. Hata anapo fika utu uzima wake, na akafikilia miaka arubaini, husema: Mola wangu Mlezi! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nitende mema unayo yapenda. Na unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na mimi ni miongoni mwa Waislamu.” MSIKIE TENA BWANA YESU KTK BIBLE

    Luka 14:26 “kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake na wanawe na ndugu zake waume na wa kike, naam na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu” HAYA SOMA QURAN TENA SASA
    Quran 4:36 “Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili na jamaa na mayatima na masikini na jirani wa karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wanao jifakhiri,” SIKIA TENA BWANA YESU KRISTO ANASEMAJE

    Luke 22:36 ” Je mwaadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia la sivyo bali mafarakano” HEMB TUISIKIE QURAN INATWAMBIAJE
    Quran 4:114 “Hakuna kheri katika mengi ya wanayo shauriana kwa siri, isipo kuwa kwa yule anaye amrisha kutoa sadaka, au kutenda mema, au kupatanisha baina ya watu. Na mwenye kufanya hayo kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi tutakuja mpa ujira mkubwa.”
    MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA MIMI SINA NYONGEZA.AKILI NI NYWELE….!!!!!

    Like

    • kelvin hussein says:

      KUOKOKANI SASA NI KWELI YESU HAKUJAKULETA AMANI KUOKOKA NI SASA NA NI LAZIMA WAKORINTHO WA PILI 6:1-2 NA LUKA 19:27 KAMA HUTAKI KULOKOKOKA UFE

      Like

  23. Melikizedek says:

    JE BWANA YESU NI MWANA PEKEE WA MUNGU?
    BIBLE SAYS “SO God Loved the World that he gave his only begotten son….”
    BIBLIA INASEMA ” Mungu aliupenda sana ulimwengu hadi akamtoa MWANAWE WA PEKEE…”
    Wakiristo kote Duniani wanajua kwamba Yesu ni mwana PEKEE wa Mungu je ukweli ni upi?
    exodus4:22 ” Israel is my son even my FIRST BORN” yaani
    kutoka 4:22 ” Bwana (Mungu) asema hivi, Israeli(Yakobo) ni mwnangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu”
    Zaburi 89:26-27 Bwana Mungu asema hivi ” Daudi ni mwana wa Mungu, yeye pia na mwana wa kwanza”
    Yeremia 31:9 Bwana Mungu asema hive “…..Efraim ni mzaliwa wa kwanza wangu”
    JE YESU YEYE ANASEMAJE?
    Mathayo 5:9 “heri wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu”
    Yohana 20:17 “Usinishike maana sijapaa kwenda kwa baba enennda kwa ndugu zangu ukawaambie ninapaa kwenda kwa Baba kwa maana BABA YANGU NDIYE BABA YENU na Mungu wangu ndiye Mungu wenu”
    NDUGU ZANGU TUMEONA KUWA HILI NENO “MWANA WA PEKEE WA MUNGU” SI LA MUNGU WALA YESU NIMENUKUU MANENO YA MUNGU NA YESU HAPO JUU. JE QURAN INASEMAJE?

    QURAN 10:68 “Wamesema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu, Aliye takasika! Yeye ni Mkwasi, Mwenye Kujitosheleza. Vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi ni vyake peke yake. Nyinyi hamna uthibitisho wowote wa haya! Mnamzulia Mwenyezi Mungu msiyo yajua?” TUPE TENA
    QURAN112:
    1.Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa MMOJA.
    2.Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
    3.HAKUZAA WALA HAKUZALIWA.
    4.Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
    UKISIKIA KENGELE YA HAKI-ELIMU “TAFAKARI”

    Like

  24. JE YESU NI MUNGU?
    Wapendwa katika Bwana. Tumsifu Kristu!
    Ili tujibu swali hilo ni lazima tujiulize Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ana sifa gani na tuone je hizo sifa Bwana Yesu Kristu Mwokozi wa Maisha yetu anazo.
    1.Bwana Mungu hajaribiwi
    Yakobo 1:13 ” Mtu ajaribiwapo asiseme ninajaribiwa na Mungu ; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu(Ibilisi), wala mwenyewe hamjaribu mtu” MH KWA HIYO!!!!
    Mathayo 4:1-5 ” Kisha Bwana Yesu Alipandishwa na Ibilisi nyikani ili ajaribiwe na Ibilisi”

    2.Bwana Mungu hafi na hatakufa
    Mathayo 27:50″Naye Yesu akisha kupaza sauti akaitoa roho yake”

    3.Mungu anauwa na kufufua hauwawi
    Ezekieli 28:8-9 “watakushusha hata shimoni; nawe utakufa kifo chao waliouawa kati ya bahri.je, utazidi kusema mbele yake huyo akuuaye, Mimi ni Mungu? Lakini u mwanadamu, wala si Mungu, mkononi mwake aktiaye jeraha.” YESU ALIULIWA
    MATENDO 5:30 “Mungu wa Baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimuuwa mkimtundika katika mti”

    4.MUNGU HASINZII WALA HALALI
    zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi yeye aliye mlinzi wa Israel”
    Quran 2:255 “Mwenyezi Mungu – hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala”TUMUANGALIE BWANA WETU YESU SASA
    marko 4:37-38 “…naye mwenyewe alikuwako juu ya shetir amelala tukamwabia mwalimu; si kitu kwako ya kuwa tunaangamia (nawe umelala!) na
    mathayo 8:23-25 “…..naye(YESU) alikuwa amelala usingizi”

    5. MUNGU HACHOKI
    ISAYA 40:28 “Bwana Mungu wa milele yeye yu aumba miisho ya dunia, hasinzii wala hachoki, akili zake hazichunguziki” JE SIFA HII BWANA NA MWOKOZI WETU YESU KRISTU ANAYO?
    YOHANA 4:6 “N a hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, Basi Yesu kwa sababu (alikuwa) amechoka kwa safari akaketi vivi hivi kisimani.Nayo yapata saa sita”

    “NDUGU ZANGU KATIKA BWANA SIFA ZA MUNGU NI NYINGI MNO AMBAZO BWANA WETU YESU KRISTU HAKUWAHI KUWA NAZO.MTU MMOJA ATAJITETEA KUSEMA ALISHUKA KATIKA MWILI ILI AZIFUNGE NGUVU ZA GIZA KUZIMU NA MWANADAMU APATE KUOKOKA NDO MAANA HIZO SIFA HAKUZIONESHA”
    SWALI JE ALISHINDWA KUZIFUNGA NGUVU ZA GIZA AKIWA HUKO MBINGUNI?
    LAKINI JE KAMA LENGO NI HILO BASI PIA HAKUFANIKIWA(ALISHINDWA)MANAAKE KILA MTU NI SHAHIDI JINSI SHETANI ANAVYOZIDI KUIKAMATA DUNIA!!!
    JE MUNGU NI MWENYE KUSHINDWA??? LA HASHA!!!

    Like

    • Samwel B. Murro says:

      Thanks God now I’m inn. Hapo ni upekee wa maana kuwa tofauti na si upekee wa peke yake LA! Hats yeye Yesu mwenyewe alisema mkinikiri na nnipokea wore mtafanyika wana.

      Like

  25. Rashidi kassaku says:

    Njia sahihi ni uslamu ushahid Q,6,126=sababu islamu sio jina la mtu,sasa kama mkristo anayo aya iliyondiwa ukristo din walete,,,,

    Like

    • IDRISSA NIMBONA says:

      Ndugu zangu wa kristu hamujaskiya paka ivi?uwislam ndo dini ya haki,Nakuingiya pepo nilazima uwe mwislam qur’an 3-17,Yesu musimusemeye uongo hakuanzisha ukristo,uri anzishwa nawapagani wawili Paulo na Barnaba mwaka wa 50nyuma ya Yesu Antiokia soma,matendo yamitum 11.26

      Like

      • alfa says:

        si nyie mnaosema mmegundua injil ya barnaba inayomtabil mtume asiyejua anakwenda wapi wala atawapeleka wapi.leo amekuwa mpagani tena?au technic yenu imeshindwa?mungu hapiganiwi,jitahidin kudanganya kwa stail zote,pindueni maandiko kwa stail zote,lakini roho zenu zinawashuhudia myatendayo,matunda ya muhamad ndo hayo,magomvi,ghadhabu,chuki,magaid,vurugu kila kona,uongo hata ktk maandiko,hata sura zinaonyesha mlichojaza moyoni,bt i wish walioandikiwa upanga wataangamia tu,wakuokoka wataokolewa,nakutakia aman ya kristo.

        Like

      • kelvin hussein says:

        KITABU PEKEE BIBBLIA TAKATIFU KINACHOELEZA MATUKIO YA MAISHA YA BINADAM KWA USAHIHI SOMA HABARI ZA ISRAEL KUSHAMBULIA GAZA KATIKA BIBLIA SOMA AMOSI 1:7 ZEFANIA 9:5 YEREMIA 47 YOTE KUOKOKA NI LAZIMA WAKORINTHO WA PILI 6:1 NA 2,LUKA 19:27

        Like

    • kelvin hussein says:

      SWALA SIO UKRISTO NI DINI AU LA SWALA HAPA NI MAFUNDISHO YAPI NI YA KWELI, JE KUTAWADHA KABLA YA KUSALI KWA WAISLAM NI SAWA? SOMA BIBLIA MARKO 7:1-9, SIJDA NI CHAPA YA SHETANI UFUNUO 13:9. WISLAM WOTE MNAMILIKIWA NA YESU KRISTO WARUMI 14 :7-9, YESU ANATAWALA SASA WAKORINTHO WA KWANZA 15:20-28, MUNGU ANAZAA TORATI 32:18, WAISLAMWOTE MNATAKIWA KUOKOKA, YOHANA 10: 1-30 WAKORINTHO WA PILI 6:1-2, LUKA 19:27,NDOA ZA MITAALA (WAKE WANNE) NI DALII YA KIAMA ISAYA 4:1, YESU ANASUJUDIWA, MATHAYO 28:9.MUNGU ANA MTOTO, MITHALI 30:4, ZABURI 2:7, MUNGU WAKO WATATU WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8, YESU ANAABUDIWA LUKA 24:50-52, YESU ALIKUFA NA KUFUFUKA NA MWILI WAKE HAUKUIBIWA, MATHAYO 28 SURA YOTE YESU NI MUNGU WAFILIPI SURA YA 2 MSTARI WA 2-12 WARAKA WA KWANZA WA YOHANA SURA YA 5 MSTARI WA 20 NITALETA ZAWADI WAKTI MWINGINE KILA MWISLAM ASOME HAPA.MWISLAM MMOJA ASEME ZAMU YANGU INAKUJA

      Like

  26. Abdul Majid says:

    YESU SI MUNGU, HATAKUWA NA HAJAWAHI KUDAI KUWA YEYE NI MUNGU!! anayebisha ajibu hoja za MCHUNGA KONDOO hapo juu!!! nimependa sana alivyowakilisha.

    Like

    • kelvin hussein says:

      JE MUNGU WAKO WATATU? MWANZO 1:26, MWANZO 18 YOTE, WARAKAWA KWANZA WA YOHANA 5:8, JE MUNGU ANZAZAA? KUMBUKUMBU LA TORATI 32:18 ZABURI:2:7 WAEBRANIA 1:1-4 SOMA NYINGIE HAPO JUU

      Like

  27. mhina says:

    Nafikiri huyo ndugu unaemuunga mkono ni mchunga kondoo wa chekechea..hivyo basi nitakusaidia kwa kukupa maelezo yangu machache tu…wewe na waislamu wengine watakaotaka kujifunza nitakachoandika hapa….Ndugu waislamu wote na watu wengineo…Mungu sio ,MTU’…Mungu ni ‘ROHO’…Yaani yeye HAONEKANI WALA HANA UMBO LA KIBINAADAMU KAMA SISI.Soma(yohana 4:24)…Naomba niparudie hapa maana ndipo penye kuwachanganya watu wengi hata baadhi ya wakristo wenyewe hawaelewi elimu hii ya kiroho ya mungu.Nimesema kuwa Mungu sio ‘MTU’ Yaani HANA MWILI WALA HAONEKANI….HIVYO Biblia inapomtaja Mungu katika yesu kristo haiongelei mambo ya mwili tena bali inaongelea mambo ya rohoni kwa kuwa tumekwishajifunza kuwa ‘MUNGU SIO MTU NA WALA HANA MWILI WA KIBINAADAMU KAMA SISI.,.Sasa basi unapoendelea kulaumu kuwa mbona yesu kama ni mungu alikula,alioga,sijui alilia nk..fahamu ya kuwa umekwishaachwa na njia ya kumjua mungu wako wa kweli aliekuumba siku nyingi sana ndugu yangu!!.Muwe makini sana ndugu zangu maana biblia inasema,mambo ya mwili ni ya mwilini na mambo ya roho ni ya rohoni na wala mambo ya rohoni mwili HAUYAWEZI.Tunapoongelea mungu tunaongelea mungu roho akaae ndani yetu…Mungu alimwambia nabii musa’NITAKUFANYA UWE KAMA MUNGU MBELE YA FARAO.Soma(kutoka 7:1-2)….na kweli biblia inatuonyesha kuwa nabii musa alijiliwa na mungu kwa uwezo wa roho mbele ya farao na kufanya mambo ya ajabu mno yasiyokuwa ya kibinaadamu hata aliweza kuitia giza nchi yote ya misri…upande mwingine tunaona akizuia hata bahari isitembee ili awavushe wana wa israel kutoka utumwani.Sasa tujiulize kama mungu alimjilia nabii musa akawa na uwezo wa kiungu na kuwa kama mungu,je,si zaidi mwana wake aliemtuma kuja kutukomboa wanadamu? Cha ajabu cha kumsingizia mtume paulo mwanasheria wa mungu ni nini wakati biblia yote kwa ujumla iko wazi kabisa ikiufunua ukweli wake?…hata bwana yesu mwenyewe aliwashangaa mayahudi wa kipindi kile kwa kuwaambia kwenye torati yenu manabii waliitwa miungu je,sembuse mwana atokae kwa baba kusema yeye ni mwana wa mungu mnashangaa nini? Soma(yohana 10:34-39)…ndivyo ilivyo yesu ni mungu kweli katika roho na mwanaadamu kweli katika mwili yaani mungu yuko ndani yake kwa roho na yeye yuko ndani ya mungu kwa mwili ndiyo maana anaitwa neno la mungu yaani NENO LILIFANYIKA MWILI.Soma(yohana 1:14)…ndugu zangu waislamu ni kwamba katika ulimwengu wa roho sisi sote ni watoto wa mungu na mungu wetu alituumba kwa mfano wake yaanh roho zetu..sasa hata jambo hili mkilitazama kimwili simtasema nakufuru nyinyi?…njooni kwa bwana yesu njia ya kweli maana mhamadi alijua torati tu..tena kidocho sana ndio maana sheria yake haifanani na ile ya musa ya kweli…na kuhusu njia ya kweli ndiyo kabisaaaa!!..hakuijua,hakuiona wala kuisikia vizuri masikini mungu amrehemu.sasa kwanini nyie mliebahatika kuiona kweli kutoka kwa wakristo mnatukebehi namna hiyo mnapoambiwa ukweli?…haya sio mambo sijui ya kafu,chadema ccm haya ni mambo ya mungu yanayohusu roho za watu kuweni makini sana!!…njooni kwa yesu mbarikiwe.

    Like

    • ndugu Mhina:
      Kwanza nakushukuru kwa kuwa umeonesha maendeleo makubwa katika kumtambua Mungu tofauti na wakiristo wengine (blind followers)…kidogo tu utakuwa muislam Inshaallah! Umetambua kuwa
      1. Mungu HAONEKANI.(Kama waislam tunavyoamini)

      2.MUNGU SIO MTU NA WALA HANA MWILI WA KIBINAADAMU KAMA SISI. (kama waislam tunavyoamini)

      4.Lakini zaidi umetumia mfano mzuri Mungu anamwambia Musa katika kutoka 7:1-2 “NITAKUFANYA UWE KAMA MUNGU…”
      ulitaka kumaanisha kuwa manabii wote wana roho wa Mungu ndani yake kwa hiyo ni miungu kimwili si kiroho kwa sbb roho(Mungu) haionekani.ukiwa unataka kumaanisha kwamba na Yesu ni mungu kwa sbb “roho wa Mungu yu ndani yake”. Kama hivyo ndo ilivyo mbona sijawahi kusikia mkisema Musa ni mungu, Yakobo ni mungu, Yohana ni mungu, Isaka ni mungu?? ili hali na wao walikuwa wana roho wa Mungu ndani yao???

      5.Lakini kama kuwa “ndani ya Mungu kiroho” ndo sbb uitwe mungu kwa hiyo na wanafunzi wa Yesu ni miungu kwa sababu aliwaambia hivi:-
      YOHANA 14:20 “Siku ile nanyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu…” kwa hiyo Mungu yu ndani ya Yesu kiroho kwa hiyo Yesu ni Mungu, na wanafunzi wako ndani ya Yesu kwa hiyo nao ni miungu.!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

      6.Msikie Bwana YESU tena MARKO 10:17 “Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamuuliza Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? Yesu akamwambia kwa nini KUNIITA MWEMA ? hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu” hii inaonesha Yesu kama binadamu alikuwa anafanya makosa kama watu wengine..kwa hiyo anajua kuwa “he is not perfect as a human being”. lakini angekuwa Mungu asingekana kwa sbb ” God is all perfect” yaani ni mwema.

      7. Paulo hatumtambui kwa sbb
      2WAKORINTHO 11:18 “Nilinenalo silineni agizo la Bwana, bali kama kwa upumbavu, katika ujasiri huu wa kujisifu..” Haneni agizo la BWANA.
      2WAKORINTHO 11:21 “Nanena kipuuzi mimi nami ninao ujasiri”,
      2WAKORINTHO 11:23 “Nanena kiwazimu mimi ni zaidi katika taabu kuzidi”
      kwa nini sasa ananena kipuuzi na kiwazimu na haneni agizo la Bwana??? sababu anaitaja mwenyewe;
      2WAKORINTHO 12:7 “Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa MWIBA KATIKA MWILI, SHETANI ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi, kwa ajili ya kitu hicho nalisihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke” Sasa haioneshi kama kilimtoka au la!!! kwa hiyo yeye alikuwa haneni agizo la Bwana ila Shetani.
      Allah akuoneshe ukweli Inshaallah!

      Like

  28. mhina says:

    Nakushukuru ndugu Abdallah kwa hoja na changamoto hizo ulizonipatia….Kama nilivyokwisha sema ya kwamba manabii wote wa mungu wameongozwa na roho wa mungu akiwa ndani yao.Wanakuwa na Mungu mwenyewe kwa uwezo wa kujiliwa na Mungu kiroho na wala sio kimwili kama ndugu Abdallah unavyojaribu kubadilisha nilichomaanisha.Yote hayo mungu anayafanya kupitia manabii ili kutujulisha na kutuonyesha mapenzi yake jinsi alivyo mkuu na mwenye nguvu.Mfalme daudi alithibitisha jambo hili pale aliposema’ROHO YA BWANA ILINENA NDANI YANGU NA NENO LAKE LIKAWA ULIMINI MWANGU.Soma(2 Samweli 23:2).Hata mtume petro alisema’manabii hawakunena kwa mapenzi yao bali walinena yaliyotoka kwa mungu wakiongozwa na Roho…hivyo Mungu anajilia roho za watakatifu na kufanya mapenzi yake kwa ajili ya watu wake,hivyo inakuwa sio nabii anayefanya yale bali ni Mungu mwenyewe akaaye ndani yao.Soma(2 Petro 1:21).Wakristo tunaposema Yesu ni Mungu haimaanishi Mwenyezi mungu ni Yule bwana yesu unaemuona kwa mwili bali ni Mungu kwa uwezo wa roho akaaye ndani yake.Tomaso Mwanafunzi wa bwana yesu wakatifulani alipoamini aliliona jambo hili linalokosa elimu ya kibinaadamu na kuhitaji majaliwa ya maono ya kiroho pale alipomwita bwana yesu’BWANA WANGU NA MUNGU WANGU’.Soma(yohana 20:28).Bwana yesu mwenyewe mara nyingi sana katika injili yake analithibitisha jambo hili,kwa mfano pale alipomwambia mwanafunzi wake Filipo’MIMI NI NDANI YA BABA NA BABA YU NDANI YANGU,HAYA MANENO NIWAAMBIAYO MIMI SIYASEMI KWA SHAURI LANGU LAKINI NI BABA AKAAYE NDANI YANGU HUZIFANYA KAZI ZAKE.Soma(Yohana 14:10-11).Hoja nyingine uliyotoa ndugu Abdallah unalazimisha kwa kusema,manabii hao ni miungu kwa mwili kwa sababu eti roho kwakuwa haionekani kwa macho yetu…nasema hapana sio kweli kuwa ni miungu kwa mwili kwa sababu sisi wakristo biblia haitufundishi mambo ya mungu kwa mwili na macho ya kumuona kama mwanadamu bali ni kwa roho na imani kupitia yesu kristo ndio maana nilikutahadhalisha huko juu ya kwamba mambo ya rohoni kamwe mwili hauyawezi.Mimi nakushauri vyema kwamba ungepiga hatua sasa kutoka elimu ya quruani ukaokoa nafsi yako kwa kumkubali bwana yesu.Biblia iwazi kabisa yasema:MUNGU NI ROHO KWA HIYO WAMWABUDUO WA KWELI WANAMUABUDU KATIKA ROHO NA KWELI…Sio wamwabuduo wa kweli wanamwabudu katika mwili na kweli kama nyinyi waisilamu ya kwamba usipo tawaza mara saba masikioni huingii msikitini!!.Soma(yohana 4:24).Huku kanisani kwetu waislamu wengi sana wanabatizwa mpaka nashangaa!!…lakini nafahamu kuwa hiyo ni kazi ya mungu mwenyewe kusema na watu wake…hivyo ndugu yangu Abdallah nawewe usichelewe.Swali lako jingine ndugu Abdallah umeuliza kwanini manabii wote wa nyuma wasiitwe miungu kama anavyoitwa bwana yesu?…mimi nakushangaa ndugu Abdallah, kwani si nilikwisha kuonyesha ile (kutoka 7:1-2) ikionyesha mungu mwenyewe akimwambia nabii musa kwamba atakuwa kama mungu mbele ya farao tatizo liko wapi? Pia sinilikwisha kuonyesha huko juu maneno ya bwana yesu akionyesha manabii wa zamani waliitwa miungu kwenye (yohana 10:35-36) Sasa tatizo liko wapi kwa sisi wakristo wa wakati huu tukilitukuza jina la mungu katika yesu kristo?…maana biblia inatufundisha ya kwamba yeye ndiye njia yetu ya haki katika kustahili mbele za YEHOVA MUNGU WETU….Huku tukiendelea kuamini ya kwamba mungu yuleyule wa ibrahimu,isaka na yakobo alienena nao kwa njia mbalimbali Mwisho wa siku hizi anasema na sisi kupitia yesu kristo aliyemweka kuwa mrithi wa manabii wote.Hebu soma(ebrania 1:1-3)…umeona kuwa biblia haisemi mwisho wa unabii wake mungu amesema na sisi kupitia muhamadi bali inasema kupitia yesu kristo…sasa sijui muhamadi alitumwa na mungu yupi asiyekuwepo katika historia yeyote ya manabii!!.Hata hivyo uwezi kamwe kumfananisha na kumlinganisha bwana yesu na manabii wote wengine waliopita kwa kuwa yeye ni nabii aliyeshuka kutoka mbinguni akija duniani kwa njia ya bikira ili kuufunua utukufu wa mungu kwa njia ya’NENO’…Biblia inasema hivi kumhusu Bwana yesu ‘NAWE MTOTO UTAITWA NABII WAKE ALIYE JUU.Soma(luka 1:76).Kwa heshima hiyo ya Bwana yesu aliyokujanayo kutoka mbinguni ilimpa heshima ya kipekee ambayo mungu mwenyewe aliamua kujifunua mbele zake pasipo mipaka wala kipimo.Soma(yohana 3:34)(mathayo 3:16).Sababu hizi za kipekee za Bwana yesu pia ndizo zilizompa heshima zaidi na kupewa jina la kipekee kabisa ‘MUNGU MKUU BWANA NA MWOKOZI WETU.Soma(isaya 9:6)linganisha na (yohana 5:43).Biblia kumhusu bwana yesu yaendelea kutuambia hivi: KWA KUWA UWEZA WAKE WA UUNGU UMETUKIRIMIA VITU VYOTE VIPASAVYO UZIMA NA UTAUWA KWA KUMJUA YEYE ALIYETUITA KWA UTUKUFU WAKE NA WEMA WAKE MWENYEWE TENA KWA HAYO AMETUKIRIMIA AHADI KUBWA MNO ZA THAMANI ILI KWAMBA KWA HIZO MPATE KUWA WASHIRIKI WA TABIA YA UUNGU MKIOKOLEWA NA UHARIBIFU ULIOMO DUNIANI KWA SABABU YA TAMAA!!!……Inanivutia mno.Soma(2petro1:3-4).Ndugu Abdallah ukaniuliza kuwa kama wanafunzi wa bwana yesu nao ni miungu…kwani ni lipi la ajabu lisilowezekana mbele za mungu?…mungu mwenyewe ndiye anayewawezesha kwa uwezo wake ili wafanye mapenzi yake kwa nyakati anazozichagua kuwajilia kiroho yeye mwenyewe…hii sio sifa au cheo kama unavyofikiri wewe bali hizi ni kazi za utumishi ambazo hata wewe hivi leo mungu anaweza kukupatia ndugu Abdullah.Mungu akituahidi kwamba tutang’ara kama Jua basi tunamuamini ni kweli,soma(mathayo 13:43)…akisema tutakuwa watakatifu kama yeye na kufanana nae basi tunamuamini,Soma(1petro 1:16)…akisema tutaitwa watoto wake kule mbinguni tunamuamini,Soma(1yohana3:1-3).Hakuna linaloweza kuzuia makusudi ya muumba wetu….kumhusu bwana yesu kuwa hakuwa mkamilifu hayo ni mawazo yako unayoyapenda mwenyewe ili ujenge hoja za uongo kwa kuwa kwa mujibu wa biblia yote bwana yesu alikuwa mtakatifu na mkamilifu kwa asilimia mia moja…yeye hakutenda dhambi wala kupigana vita kama mtume mhamad.Soma(yohana 8:46)(luka 1:35)(1Petro2:22)nk…ndugu Abdallah ile (marko10:17) Uliyojengea hoja yako ya uongo kwa kuinukuu kimstari ukiisoma injili yote ya marko utagundua ni nini bwana yesu alichokuwa anataka kuwafundisha wanafunzi wake,lilikuwa ni somo la utiifu na unyenyekevu pasipo kujikweza akiwafundisha wasipende kuhoji habari za wema bali watekeleze huo wema na mungu ndiye baba wa wema.Soma(mathayo 19:17)….paulo pia unamnukuu vibaya utakavyo wewe kama wafanyavyo waislamu wenzako wengi ili kupindisha ile kweli ya mungu…kwa hili nitakupa kazi ya kufanya ili upate majibu wewe mwenyewe.Umenukuu (2wakorintho 11:23)ungesoma pia (2wakorintho11:30) ili uelewe vyema mafumbo ya kiimani ya watu wa mungu kama paulo wasivyopenda kujisifu ovyo ovyo bali hujishusha kwa unyenyekevu ili injili iwafikie wengi…akionyesha jinsi uweza wa bwana yesu unavyotimilika katika udhaifu wa mtu.Soma(2wakorintho12:9-10)…unashangaa nini wakati hata ayubu mtumishi wa mungu yalimtokea mambo kama haya…soma kwa makini(Ayubu 2:7-11)….kwa ufupi naona hoja zako zote huku chini ni za kitoto hebu nikupe nafasi uniandikie hoja nyingine za maana ili nikusaidie na kama huna…je,unaniruhusu mimi nikuulize maswali manne tu kuhusu dini yako ya uisilamu ambapo ukishindwa kuyajibu utayapeleka msikitini kwa mashekhe wako ili wakusaidie kama wataweza….niruhusu nikuulize kama uko tayari kama haupo tena kwenye blog hii basi kwaheri na mungu akusaidie utoke gizani huko.

    Like

    • 1.NAWE MTOTO UTAITWA NABII WAKE ALIYE JUU(Mungu).Soma(luka 1:76)” hili ndo jibu sahihi ndg Mhina.Pili soma (yohana 17:3 ) anadai ametumwa, Mungu hatumwi.

      2.Maskini wakiristu wanababaika hawamjui Mungu, mpaka analazimika kukubali kuwa hata manabii walikuwa miungu ili muradi tu Yesu naye awe mungu subhanallah!!! yaani ww ndo mkiristu wa kwanza kusikia ukiamini hivyo…

      3.MUNGU MKUU BWANA NA MWOKOZI WETU.Soma(isaya 9:6)linganisha na (yohana5:43) LAKINi Yesu anakataa kuitwa “MUNGU MKUU”.(Soma Yohana 14:28)”…. Maana BABA ni MKUU kuliko mimi” Sasa sijui tumsikilize Paulo au Yesu!?

      4.Paulo haneni agizo la Bwana(2WAKORINTHO 11:18),pili ananena kipuuzi(2WAK 11:21) na kiwazimu(2WAK 11:23) kama anavyojitambulisha yeye mwenyewe,kwa hiyo sisi waislam hatumkubali lakini Yesu tunampenda sana na alikuwa nabii wa Mungu na si Mungu.

      5.Weka topic yoyote kuhusu Uislam nitakusaidia ndugu yangu, Allah anaweza kuleta nusra ukamtambua kuwa yeye ni mmoja tu, inshaallah.

      6.Nimeweka topic mpya hapo chini jinsi biblia inavyowadhalilisha manabii.

      Like

  29. BIBLIA INAVYO WATUKANA MANABII WA MUNGU.
    1.1 NABII NUHU KATIKA BIBLIA
    Nuhu anaripotiwa kuwa alilewa hadi akawa uchi mbele ya watoto
    wake walio wakubwa (Mwanzo 9:23-24): “Shemu na Yafethi
    wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda
    kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao
    zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. Nuhu
    akaelevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo
    alivyomtendea.”

    1.2 NABII NUHU KATIKA QURAN
    SURA 3:AL- IMRAN.
    33. Hakika Mwenyezi Mungu alimteuwa Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote.
    34. Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua
    SURA 6: AL-AN-A’AM
    84. Na tukamtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaakub(Yakobo). Kila mmoja wao tulimwongoa. Na Nuhu tulimwongoa kabla

    2.1 NABII SULEIMAN KATIKA BIBLIA
    Suleimani ameshutumiwa kuwa ana abudu miungu ya uwongo yaani wanadai ati amekufuru.
    (1 Wafalme 11:9-10) “Basi BWANA
    akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye
    amemwacha BWANA, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili,
    akamwamuru katika habari ya jambo hilo hilo asifuate miungu
    mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru BWANA.”
    2.2 NABII SULEIMAN KATIKA QURAN
    SURA 2: AL-BAQRA
    102. Na (wapotofu)wakafuata yale waliyo zua mashet’ani kuuzulia ufalme wa Suleiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet’ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi.

    3.1 NABII HAARUN KATIKA BIBLIA
    Haruna, mtume aliyeongozana na Musa, nduguye, katika kazi yake kwa
    Firauni(Faraoh), anatuhumiwa kuwa aliwaundia wana wa Israeli ndama wa
    dhahabu ili wamwabudu (Kutoka 32:4): “Akaipokea mikononi mwao
    akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa
    kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli
    iliyokutoa katika nchi ya Misri.”

    3.2 NABII HAARUN KATIKA QURAN
    SURA 21: AL-ANBIYAAI
    48. Na kwa yakini tuliwapa Musa na Haaruni kipambanuzi, na mwangaza, na
    makumbusho kwa wachamngu,
    49. Ambao wanamkhofu Mola wao Mlezi faraghani, na wanaiogopa Saa ya Kiyama

    4.1 NABII LUTU KATIKA BIBLIA
    Unaweza kusoma juu ya Lutu anakabiliwa na tuhuma za kujamiiana na mabinti zake wawili (Mwanzo 19:36): “Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao”

    4.2 NABII LUTU KATIKA QURAN
    74. Na Lutu tukampa hukumu na elimu na tukamwokoa na ule mji ulio kuwa
    ukifanya maovu. Hakika hao walikuwa watu wabaya, wachafu.
    75. Na tukamuingiza katika rehema yetu. Hakika yeye ni miongoni mwa watenda mema

    5.1 NABII DAUDI KATIKA BIBLIA
    Nabii Daudi ametuhumiwa kuzini na mke wa mtu(fornication) (2 samweli 11:4-5):
    “Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; {mke wa Uriiah} naye
    akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke
    amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani
    kwake. Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na
    kumwambia Daudi, akasema, Ni mja mzito”

    5.2.1 NABII DAUDI KATIKA QURAN.
    SURA 34: SABAA
    10. Na tulimpa Daudi fadhila kutoka kwetu, (tukasema): Enyi milima! Karirini kumtakasa Mwenyezi Mungu pamoja naye! Na ndege pia. Na tukamlainishia chuma.

    5.2.2 SURA 38. SURAT S’AAD
    30. Na Daudi tukamtunukia Suleiman. (Kwa hakika) Alikuwa mja mwema.

    6.1 KUMTUKANA DAUDI NI KUMTUKANA YESU
    SWALI LANGU: Vipi Yesu anaingia katika kizazi cha Daudi(Mathayo 1:1)
    wakati Daudi ameelezwa kuwa ni mtu mzinifu?ina maana Yesu ni mwana haram??????( Allah aepushie mbali jambo hilo!) Je, hili halipingani na kile kilichotajwa katika Kumbukumbu la Torati 23:2 “Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa
    BWANA; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa BWANA.”

    7.1 LAKINI WAKIRISTO WAKAONA HAITOSHI
    Wakamtukana mpaka Ibrahimu kwamba alizini na Hajir ndo akapatikana Ismael. Lakini hapo hapo wanadai kuwa Ibrahim ndo baba yao wa imani, sasa sijui imani yao inaongozwa na mtu mzinifu jamaaani!!!? hawa watu hawana hata aibu, adhabu ya Allah inawangoja.

    7.2. QURAN SURA 2: AL-BAQRA
    130. Na nani atajitenga na mila ya Ibrahim isipo kuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini Sisi tulimteuwa yeye katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema.

    SURA 60. SURAT AL-MUMTAH’INAH
    4. Hakika nyinyi mna mfano mzuri kwenu kwa Ibrahim na wale walio kuwa pamoja naye,…

    QURAN SURA 2: AL-BAQRA
    135. Na wakasema: Kuweni Mayahudi au Wakristo ndio mtaongoka.Sema: Bali tunashika mila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa katika washirikina

    JE UKIRISTU NA UISLAM NI IPI IMANI YA KWELI????
    HATA MTOTO MDOGO HAPO ATAKUPA JIBU SAHIHI.EWE NDUGU MKIRISTU TAFAKARI!!!

    Like

    • jmc says:

      swala la wokovu ni gharama na sioni kama itakuwa rahisi kwa mwanadamu kuokolewa kama si mungu mwenyewe kuhusika. dhambi ya kwanza ilipo ingia edeni kulikuwa na visingizio vingi sana ambavyo havingeliweza kusahihisha kosa lao bali aibu iliwajaa uchi wao haukuzibika kwa mavazi ya majani walio jitengenezea mpaka mungu alipoonyesha upendo wake kutoa uhai wa mnyama ili kuwatenenezea mavazi ya kuziba uchi wao. leo hii kila mtu anatakikana kuungana na yohana mbatizaji tazama mwana kondoo wa mungu aondoaye dhambi za ulimwengu (yohana 1:29)

      Like

  30. Samir says:

    wanamtukana hadi Yesu Wanayedai kumpenda
    MOJA:Em! angalia hiyo picha waliyoiweka hapo juu huyo mungu wao Yesu alivyoachama kwa maumivu, kweli huku ni kumpenda au kumdhihaki. Eti hiyo ni siku aliyokuwa akilaaniwa msalabani (wagalatia 3:13)” kwa maana kila aangikwaye mtiini amelaaniwa” yaani analaaniwa kwa ajili ya midhambi yako na wenzako wewe Mhina..em acheni kashfa bwana!
    MBILI: Yesu aliomba aepushiwe asisulubiwe MATHAYO 26:39 “alienda mbele kidogo, akaanguka kifudfudi akaoba akisema, Baba yangu ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke walakini si kama nitakavyo mimi bali kama utakavyo wewe”
    TATU:lakini Yesu anasema “Ombeni nanyi mtapewa…..je ni mzazi gani ambaye mtoto wake ametaka andazi akampa jiwe…au amuombe samaki akampa nyoka..?.”
    ajabu kubwa sana yeye aliomba aepushiwe kusulubiwa hakukubaliwa maombi yake..sasa itakuwaje kwenu kama Bwana wenu aliomba dua haikukubalika?
    NNE: imeandikwa Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe inakuwaje mungu wenu asulubiwe NA watu aliowaumba ndo nyie mpate uwokovu??
    Nilikuwa mkiristu lakini nilijiuliza maswali ambayo hayakupata majibu ndipo mwaka 2010 nikaona hakuna haja…sisemi hivyo ili niwashawishi hapana atakayejua ukweli atafuata yy mwenyewe.

    Like

  31. mhina says:

    Tatizo lako ndugu Abdallah wewe unayatazama mambo haya kwa mwili tu….wakati kuyaona kiroho umetiwa giza kabisa na Baba wa ulimwengu huu ambaye amekupofusha macho ili usione wala kuelewa usije ukaokoka.Kama utamuangalia bwana yesu kimwili tu…basi nikweli kabisa kuwa ametumwa na mungu na mungu ni mkuu kuliko yeye kama ulivyonukuu kwenye(yoh 14:28)….lakini kama tukiitafakari vyema injili ya bwana yesu na kuyaelewa maneno yake vizuri basi hakika tutamuona mungu mwenyewe ambaye ni roho akaaye ndani yake..lakini si kumuona kwa macho na akili za kibinaadamu bali kwa roho na imani anayotupa mungu mwenyewe kupitia roho mtakatifu.Kwenye quruan elimu ya kiroho hakuna kama mlivyoonyeshwa huko juu ndiyomaana kwenu elimu hii ni upuuzi.Biblia inasema: KWA SABABU NENO LA MSALABA KWAO WANAOPOTEA NI UPUUZI BALI KWETU SISI TUNAOOKOLEWA NI NGUVU YA MUNGU.Soma(1Wakorintho 1:18)….Mimi binafsi nawapenda sana ndugu zangu waislamu kwa kuwa nafahamu sisi sote ni ndugu kwa asili yetu…kwahiyo tuendeleeni kubadilishana mawazo kwa upendo na amani…na kama niliwakwaza huko juu naomba mnisamehe.Lakini bado nimegundua kuwa mchango wangu huko juu wa mambo ya rohoni haujawatosheleza…najiuliza hivi: Nilipomnukuu bwana yesu akisema mwenyewe: SIFANYI LOLOTE KWA SHAURI LANGU BALI NI BABA AKAAYE NDANI YANGU HUZIFANYA KAZI ZAKE….Sijui bwana Abdallah na waisilamu wengine mlielewaje hapo bwana yesu alichomaanisha!!….Labda nitoke kidogo kwenye biblia halafu niwafuate kwenye elimu zenu hizi za dunia labda mtanielewa vyema…..Nilifundisha kuwa Mungu ni Roho lakini….Shetani nae ni Roho ila tofauti ni kwamba Shetani ni roho iliyomuasi mungu yaani yeye ni roho ovu kinyume na mungu lakini pia yeye haonekani lakini tunaamini yupo akiendesha wafuasi wake…Baadhi ya watu wenye matatizo wakienda kwa waganga wa kienyeji au mashekhe wa visomo vya kiislamu utasikia wakifundishwa elimu hii…wanaambiwa wanamashetani kwa njia za roho na wanaoongea sio wao ila ni mashetani yanayokaa ndani yao huwaendesha…..ijapokuwa mteja wao labda anaitwa Asha lakini utawasikia huyu ni shetani anaeongea wala sio Asha….shetani ndiye anayemuongoza kuongea na kutenda yote hayo!!….Sasa kwa maelezo hayo mimi huwa najiuliza: HIVI MBONA ELIMU YA SHETANI YA ROHONI NDUGU WAISLAMU WANAIELEWA VYEMA LAKINI ILE YA ROHONI YA MUNGU KUJIFUNUA KIROHO KWA NJIA YA MANABII WANAKUWA HAWAIELEWI?…Je,huyo siye shetani anaepingana na mungu kiroho ili kuwapoteza waislamu huku akiyafumba yale ya mungu msiyajue?….mimi sijui mtatafakari wenyewe!!….ndugu Abdallah ulinishanga nilichokuwa nakielezea huko juu ukasema mimi ni mkristo wa kwanza kuonesha imani ile ya kiungu kwa manabii na bwana yesu mwenyewe lakini yote yale ni elimu ya biblia ndiyomaana nikaambatanisha na mistari yake….Tatizo ni wewe kukosa misingi ya imani…kesho nitakutupia maswali yangu unijibu na kuhusu hoja mpya ulizotoa huko juu zimenishangaza na kunichekesha kwelikweli!!…Hivi kumbe kwa mujibu wa kitabu chenu kipenzi Quran ni kwamba manabii wote wakina ibrahimu,daudi sijui lutu nk…hawakutenda dhambi hatakidogo yani walikuwa kamilifu kama malaika!!…hivi kumbe kwa mujibu wa quran ni kwamba manabii wote walikuwa kama malaika tena safi kabisa.,..Sasa kama ni hivyo mbona msiwafuate hao na kuwaamini badalayake mnamkumbatia nabii mwingine atokae kwenye taifa jingine alie MPIGANAJI VITA NA MUUAJI..ANAEWAFUNDISHA NYIE KUWEKA VISASI NA NDUGU ZENU WAKRISTO MPAKA KIAMA?…..PIA MBONA ALIKIRI YEYE MWENYEWE KUWA HAJUI ATAKALOTENDEWA SIKU YA MWISHO YEYE NA NYIE WAFUASI WAKE?….NA KUHUSU WALE NDUGU ZENU MAJINI MNAOSEMA WALISILIMU NA KUSAMEHEWA NA MUNGU…MBONA MAELEZO YAO BADO YANAONYESHA BADO NI ADUI WA MUNGU KAMA BIBLIA INAVYOTUONYESHA PALE YANAPOSEMA”NASI TULIZIGUSA MBINGU NA TUKAZIONA ZIMEJAA WALINZI WENYE NGUVU NA VIMONDO NA HAKIKA TULIKUWA TUKIKAA HUMO KATIKA BAADHI YA MAKAO ILI KUSIKILIZA LAKINI SASA ANAYETAKA KUSIKILIZA ANAKUTA KIMONDO KIKIMVIZIA!!….Du!! Wanajielezea kwasasa hawana nafasi tena huko mbinguni kupata mambo mema na ujumbe mzuri wa huko na tena wakijaribu hata kusikiliza wanatolewa mbio na malaika wema wa mungu wetu ndiyo maana wakamalizia kwa kusema: NASI HATUJUI KAMA WANATAKIWA SHARI WALE WANAOKAA KWENYE ARDHI AU MOLA WAO MLEZI ANAWATAKIA UONGOFU!!!!…..Hapohapo huku duniani tunaambiwa ni ndugu wa waisilamu tena kuna dada huku kwetu yalimtisha abadili dini awe muislamu sivyo YATAMUUA nae kwa uoga dada yangu akakubali…sasa mimi nashangaa malaika gani hawa wa mungu wanatisha kuuwa kwa sababu ya dini?….halafu mnatuambia ni wa mungu na siyo shetani?…mwenyemacho ya kweli kabisa kabisa hataambiwa atazame…..Ndugu yangu Abdalah naomba mchango wangu huu usikuuzi bali tuendelee tu kupeana changamoto lakini nitafurahi kama ukinijibu hoja hii ya majini halafu na mimi kesho nitakujibu hoja zako zote nisizozijibu na zaidi nitakupa yaletmaswali yangu manne. Ubarikiwe.

    Like

    • ibrahim hassan says:

      Mr.Mhina kabla ya yote nakupa angalizo.
      Mithali 30:5 Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.
      6 Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.
      Andiko hili lina maana sana kama tutazingatia yafuatayo:
      1 Nukuu zote za maneno ya mungu yawe na ushahidi kamilifu kama kweli yanatoka kwa mungu;
      2 Nyaraka za paulo ili ziaminike zimenukuliwa sehemu gani au kashushiwa na mungu kipindi gani.
      Nasema hivi kwa sababu nina wasiwasi sana na maneno ya kijitungia kuweza kuingizwa kwenye hiyo biblia. Maana ukisoma dibaji inaeleza uwazi kabisa kwamba yalibadilishwa na majina zaidi ya 3500 na binadamu.
      Na sehemu nyingine ni hii hapa:
      Yeremia 23:14 Katika manabii wa Yerusalemu nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo, hutia nguvu mikono ya watendao maovu, hata ikawa hapana mtu arejeaye na kuuacha uovu wake; wote pia wamekuwa kama Sodoma kwangu, na wenyeji wake kama Gomora.
      15 Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote.
      16 Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; hunena maono ya mioyo yao wenyewe; hayakutoka katika kinywa cha Bwana.
      Andiko hili, nina wasiwasi na akina Paulo kujitafutia umaarufu. Hutia nguvu mikono ya watendao zambi, yaani mtu anaambiwa akiwa na imani ataokoka bila kuzingatia matendo ambayo ni agizo la bwana mungu. Mimi nashangaa kitu kimoja kwa wakristo, andiko la sheria kutoka kwa mungu limeonekana ,sasa iweje na lile la kuvunja sheria pia lisitoke kwa mungu badala yake linatoka kwa mdomo wa wanadamu,sasa tumuamini nani kati ya paulo na mungu?
      Mr. Mhina nimekupa haya kwa sababu wewe unapenda sana kunukuu nyaraka za paulo kuliko hata za yesu mwenyewe.
      Sura ya majini isome vizuri, usisome kwa jazba, hapo kuna vipindi viwili vinaongeleka, kabla ya kusilimu na wakati wa kusilimu.
      Swala la Muhammad kuuwa hata yesu alibariki luka 19:27 wale adui zangu, wasiotaka niwatawale waleteni muwauwe mbele yangu.
      Kwa hiyo muhammad kaja na ufalme wa mbinguni ambao yesu alikuja kuhubiri akiwambia watu ya kwamba umekaribia.
      Taifa jingine yesu kasema ya kwamba ufalme wa mungu kwenu umehama, wamepewa taifa jingine.

      Like

    • Ndugu Mhina,
      nashkuru kwa maswali yako kuhusu uislam, maswali yako ni kuhusu;
      1. Majini
      2.Mtume gani muuaji na mlipiza kisasi?

      MAJINI NI NINI KWA USHAHIDI WA QURAN TUKUFU?
      Majini ni viumbe walioumbwa kwa moto hivyo hawaonekani.Wameumbwa kabla ya kuumbwa Baba yetu Adam.
      1.QURAN Sura 15:26-2726. “Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti,
      unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.. Na majini tuliwaumba kabla kwa ulimi wa moto.”

      Baadae majini walimuasi M/Mungu(walikataa kutii amri ya Allah) kama inavyoeleza chini.Yeye hakuwa malaika kwa sababu malaika hawamuasi M/Mungu hata kdogo.

      2.QURAN sura 18:50 “Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Walimsjudia isipo kuwa Iblisi.Yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi. Je!
      Mnamshika yeye na dhuriya(jamaa) zake kuwa marafiki badala Yangu, hali wao ni adui
      zenu? Ni ovu mno badala hii kwa wenye kudhulumu”

      hiyo haya hapo juu inaonesha kuwa Allah anachukia mtu kufanya urafiki na majini badala ya kufanya urafiki na Allah.kwa hiyo muislam au mkiristu anayefanya hivyo ni machukizo makubwa mno mbele ya Allah.

      3.QURAN sura 4:51 “Na ambao hutoa mali yao kwa kuonyesha watu, wala hawamuamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho; na yule ambaye Shet’ani amekuwa ndiye rafiki yake, basi ana rafiki mbaya mno.”
      Allah (s.w) Anasisitiza ubaya wa kuwafanya mashetani marafiiki badala yake.

      SASA TUONE MASHETANI NI MARAFIKI WA WATU GANI?
      QURAN SURA 7:27. “Eny wanaadamu! Asije Shet’ani kukufitinini kama alivyo watoa wazazi wenu(Adam na Hawa)Peponi, akawavua nguo zao kuwaonyesha tupu zao. Hakika yeye na kabila yake wanakuoneni, na nyinyi hamuwaoni. Hakika Sisi tumewafanya Mashet’ani kuwa ni marafiki wa wasio amini”
      kwa hiyo Allah anatuambia usipomuamini bila shaka unawaamiini mashetani yaani Majini.

      MAJINI KUSILIMU.
      Kusilimu maana yake ni kujisalimisha au kusalim amri au kutii amri.
      Majini walijisalimisha(walisilimu) kwa Bwana Yesu kabla ya kuja Nabii Muhammad (S.A.W)

      Math 8:28-31 “ Naye alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo (Majini) walikutana naye, wanatoka makaburuni wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama wakapiga kelele wakisema tuna nini nawe mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya muhula wetu………………. (MK 5:1-9).
      Hiyo inaonenekana walitambua kuwa huyo ni mtu mtakatifu kwa hiyo wakamtii na kumuogopa.

      pia majini haohao waliwatii(walisilimu) wanafunzi wa Yesu miaka 500 kabla ya Kuja Nabii Muhammad (S.A.W)
      Luka 10:17 ” Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18 .Akawaambia nilimuona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme.”

      HALI YA MAJINI BAADA YA KUJA NABII MUHAMMAD.
      kundi moja la Majini waliposikia Mtume Muhammad akisoma Quran tukufu, walijua kuwa si maneno ya kawaida bali yametoka kwa Allah hivyo wakatii (wakasilimu).

      QURAN SURA 46: ” 29. Na wakati tulipo waleta kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur’ani. Basi walipo ihudhuria walisema: Sikilizeni! Na ilipo kwisha somwa, walirudi kwa kaumu yao kwenda kuwaonya.
      30. Wakasema: Enyi kaumu yetu! Sisi tumesikia Kitabu kilicho teremshwa baada ya
      Musa, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinacho ongoza kwenye Haki na
      kwenye Njia Iliyo Nyooka.
      31. Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mwenye kuitia kwa Mwenyezi Mungu, na muaminini,
      Mwenyezi Mungu atakusameheni, na atakukingeni na adhabu chungu.”

      Hili ni kundi moja tu lililo amini, lakini wengine waliendelea na uasi. majini waliotii walitoa ushuhuda wao kama ifuatavyo.

      QURAN SURA 72:6.” Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi.”

      wakaendelea
      QURAN SURA 72: 12. ” Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani, wala hatuwezi kumponyoka kwa kukimbia.
      13. Nasi tulipo usikia uwongofu tuliuamini. Basi mwenye kumuamini Mola wake
      Mlezi basi haogopi kupunjwa wala kudhulumiwa.”

      Hawa ndo majini walioshindwa kumponyoka nabii Muhammad(S.A.W) kama vile walivyoshindwa kumponyoka nabii Yesu (A.S) na wanafunzi wake pia kama tulivyoona kwenye Biblia. kama utakuwa na swali uliza kabla sijajibu swali lako la pili la kuhusu vita na kisasi.
      Allah akujaalie inshaallah uone ukweli!!

      Like

    • nakunukuu “hivi kumbe kwa mujibu wa quran ni kwamba manabii wote walikuwa kama malaika tena safi kabisa.,..Sasa kama ni hivyo mbona msiwafuate hao na kuwaamini badalayake mnamkumbatia nabii mwingine atokae kwenye taifa jingine…”

      1.Ndugu Mhina: katika uislamu kuna nguzo tano za uislam na nguzo sita za imani ya uislam ,kuwaamini mitume wote ni nguzo ya nne ya imani ya uislam.

      2.Pia waislam tunawafuata manabii wote kama Quran inavyosema. SURA 3: IMRAN
      “84. Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo
      teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo
      pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina
      yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake.”

      3.huyo dada anayesumbuliwa na majini anatakiwa ajichunguze na abadili tabia kama ana tabia ya kuacha kichwa wazi,kutoswali, kuzini, kuvaa vimini(nusu uchi), kusema upuuzi aache mara moja maana mambo hayo huwakaribisha mno majini. na mtu anayejikinga na mambo hayo na akaswali swala tano majini humuogopa na hayawezi kumsogelea.pia aende kwa mashekhe watiifu/waaminifu wamsomee dua inshaallah Allah atayaondoa na kumuacha huru, asithubutu kwenda kwa waganga wa kienyeji maana hao ni marafiki wa majini.
      Allah amuondolee adha akiwa yeye ni muumini wa kiislam inshaallah!

      Like

  32. mhina says:

    Bw.Samir….Hivi wewe katika imani unapata imani kwa kutazama picha fulani au neno la mungu linavyofundisha?….mbona unanishangaza sana!!.Pia umenukuu (galatia 3:13)…ukijifanya ulikuwa mkristo lakini kwa sababu ya kumuonea huruma bwana yesu jinsi wakristo tunavyotangaza mateso yake ukaona uhame!!!…Unachekeshakwelikweli wewe na pia unasikitisha kwa kukosa maarifa kama bwana yesu alivyosema kuwa watu wake wanapotea kwa kukosa maarifa.Njia yote katika biblia ni njia ya mungu mwenyewe na ni HAKI NA KWELI.Usijifanye unahuruma zaidi ya huruma wa mungu mwenyewe.Biblia inasema:KWA SABABU KARAMA ZA MUNGU HAZINA MAJUTO WALA MWITO WAKE.Soma(rumi11:29).Mungu alifanya vile ili wewe asikuhukumu siku ya mwisho kama utafuata injili ya bwana yesu vizuri.Biblia inasema:YEYE ASIYEJUA DHAMBI ALIMFANYA KUWA DHAMBI KWA AJILI YETU ILI SISI TUPATE KUWA HAKI YA MUNGU KATIKA YEYE.Soma(2Wakorintho5:21).Tatizo ni kwamba kazi ya sheria ni KUSOMA DHAMBI NA KUHUKUMU NA KAMWE SIO KUMUOKOA MWANADAMU.Hebu mtazame bwana yesu anavyowaambia wale waliokuwa wakifuata sheria”MSIDHANI KWAMBA MIMI NITAWASHITAKI KWA MUNGU….YUKO ANAYEWASHITAKI,NDIYE MUSA MNAYEMTUMAINI NYINYI KWA MAANA KAMA MNGALIMUAMINI MUSA MNGENIAMINI MIMI KWA SABABU YEYE ALIANDIKA HABARI ZANGU LAKINI MSIPOYAAMINI MANENO YAKE MTAYAAMINI WAPI MANENO YANGU?….Huyu pia ndiye mhamadi na wafuasi wake…hakuiamini torati ya musa akaandika kitabu chake cha quran na kuwachota watu wengi wasiojua maandiko….sasa kama mhamad alichakachua torati ya musa nyinyi wafuasi mnaomuamini mtawezaje kumuamini bwana yesu?…Torati ilikuja kwa mkono wa musa bali neema na kweli zimekuja kupitia bwana yesu.Soma(yoh3:14,15).Tangu zamani hakukua na kitu kinachoitwa quran hatakidogo!!.Kujidai unafuata sheria ambayo pia chakusikitisha sio ile ya asili ya mungu mwenyewe ni kupenda hukumu ya mungu kwa hiari yako kabisa kabisa ndugu zangu.soma(warumi 3:19).Hakuna hata mtu mmoja anayeweza kusimama mbele ya mungu kwa kujidai eti alichagua njia ya kufuata sheria badala ya njia ya wakristo ya kujinyenyekeza mbele za mungu kwa utiifu na kumuamini mungu kuwa ndiye mwenye kutuokoa kwa uwezo wake tu.Pia ulisema mbona bwana yesu aliomba asisulubiwe lakini wapi..,.fahamu kuwa hata kabla ya hapo tayari bwana yesu alikwisha tabiri na kujua kuwa lazima atasulubiwa kwa ajili ya wanadamu ila yeye aliktwa anaonyesha kuwa mapenzi na makusudi ya mungu ni lazima yatimie si kwa matakwa yake bali matakwa ya mungu mwenyewe aliyekusudia kutuokoa kwa damu ya thamani…yaani kwa kupigwa kwake yeye mmoja wengi tumepona kwa kuwa kama kweli nyinyi mnabaki kwenye sheria takatifu za mungu za kweli sasa mbona hatuwaoni mkiadhibiana kwa sababu ya haki ya sheria ya mungu iliyotakatifu?MMEPOTEZWA HAKIKA KWA KUWA HAMJUI ASILI YA SHERIA ZA MUNGU NA MAHITAJI YAKE…..Kilamtu atabeba mzigowake mwenyewe ni kweli kabisa tatizo ni nini?…kama huitii injili ya bwana yesu aliyofundisha kwanini usibebe huo mzigo wako?….unanukuu kamstari kammoja badala ya kuisoma injili yote ili upate wokovu!!….RUDI KWA BWANA YESU KAKA UNAANGAMIA.

    Like

  33. Samir says:

    Mchungaji nakunukuu
    1.”:KWA SABABU KARAMA ZA MUNGU HAZINA MAJUTO WALA MWITO WAKE.Soma(rumi11:29).Mungu alifanya vile ili wewe asikuhukumu siku ya mwisho kama utafuata injili ya bwana yesu vizuri”

    Lakini Mbona Bwana Yesu mwenyewe alijuta msalabani??? tena alijuta majuto makubwa mno na kutoa lawama kwa Mungu wake?
    Mathayo 27:45 “Eloi(Allah)! Eloi(Allah)! lama sabakhtan yaani Mungu wangu! Mungu wangu! mbona umeniacha!” Eloi(kiebrania)=Allah(kiarabu) analaumu kuwa ameachwa kwa nini alaumu wakati alijua itamtokea hivyo.

    2.”YEYE ASIYEJUA DHAMBI ALIMFANYA KUWA DHAMBI KWA AJILI YETU ILI SISI TUPATE KUWA HAKI YA MUNGU KATIKA YEYE.Soma(2Wakorintho5:21)”
    Sub-hanallah!! ametakasika MwenyeziMungu!! kwa kweli ni kosa kubwa katika uislamu kusema kwamba Mungu amfanya asiye dhambi kuwa na dhambi kwa hakika hii ni kazi ya Shetani na sio kazi ya Mungu.

    3.”MSIDHANI KWAMBA MIMI NITAWASHITAKI KWA MUNGU….YUKO ANAYEWASHITAKI,NDIYE MUSA MNAYEMTUMAINI NYINYI KWA MAANA KAMA MNGALIMUAMINI MUSA MNGENIAMINI MIMI KWA SABABU YEYE ALIANDIKA HABARI ZANGU LAKINI MSIPOYAAMINI MANENO YAKE MTAYAAMINI WAPI MANENO YANGU?”

    hapo mlikuwa mnaambiwa wakiristu ambao mna ipinga taurati ya Musa kwa maneno ya Paulo
    “Kristo ametukomboa kwenye laana ya torati” yaani mnadai torati ya Musa ina laana kwa hiyo Yesu anadai kwa maneno yenu hayo Musa atawashitaki kwa Mungu..Yesu aliendelea kukemea wanaoipinga torati na kudai kuwa atawatoa katika laana ya torati.

    MATHAYO 5:17 “Msidhani nalikuja kutengua torati wala manabii la! bali nimekuja kutimiza, kwa maana nawaambia , mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie….”

    4.Ni wapi Quran imeipinga torati kama ulivyodai? toa ushahidi nitakusaidia.

    5.Sheria zote za torati (sio kumbumbukumbu la torati) zimo ndani ya Quran tukufu hatuzifanyi kwa sababu tupo chini ya serikali za kipagani (hazina dini). lakini kwa walio na serikali za kiislam kama Pakistan, Saudi Arabia, Iran,Indonesia. hizo nchi zinaongozwa na sheria za Quran ambazo ni mrithi wa zile za torati ya Musa kwa hiyo wanahukumiwa kwa sheria za Quran zilizotoka kwa Allah.

    6. Unasema “RUDI KWA BWANA YESU KAKA UNAANGAMIA.”
    Allah anasema:
    QURAN SURA IMRAN;102. “Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha; wala msife ila nanyi ni Waislamu.”

    Na kwa taarifa yako waislam tunampenda sana Yesu kuliko wakiristu wanaosema kalaaniwa kwa ajili ya dhambi zao. kwa waislam ni kufuru kudai Yesu kalaaniwa kwa ajili ya watu na hayo ndo mapenzi halisi aliyo nayo Mungu wa Waislam kwa Bwana Yesu.
    QURAN SURA 3: IMRAN
    “45. Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu
    anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa
    Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa
    (kwa Mwenyezi Mungu)”

    hiyo haya inasema Yesu ana heshima duniani na akhera wala hakuwa mwenye kulaaniwa kwa ajili ya wakosefu.
    7. kwa nini unapokuwa mkiristu unalazimika kuamini yesu kalaaniwa kwa ajili ya dhambi zako, hiyo inaonesha kuwa mkiristu ni laana kwa hiyo laana zinakombolewa kwa kuamini kulaaniwa kwa Yesu kutundikwa msalabani (Mathayo 15:3).
    Anayependa awe muislam asiyependa si juu yangu, hakika mimi nimefikisha.

    Like

    • KELVIN says:

      NITAKUJIBU SWALI MOJA KWA UFUPI, SABABU YA MUDA KWA NINI YESU ALIJUTA MSALABANI?. ALIVUA NGUVU ZA KIUNGU AKABAKI KUWA MWANADAMU WA KAWAIDA NA NDIO MAANA ALISIKIA MAUMIVU KAMA WENGINE WAFILIPI 2:1-12. USISAHAU SIJDA NI CHAPA YA SHETANI UFUNUO WA YOHANA 13:16 OKOKA KUOKOKA NI SASA WAKORINTHO WA PILI 6:1-2 MARKO 16:16-20. FUATILIA COMMENTS ZANGU TOKA JUU MPAKA CHINI ZIKO NYINGI ZITAKUSAIDIA

      Like

  34. chidy rakim says:

    YESU NI MUISLAMU NA DINI YA HAKI NI UISLAMU
    **************************************
    Kuoa Wake Wengi Katika Uislamu. Hata Katika Biblia Kumetajwa Kuoa Wake Wengi

    “Akichukua mke mwingine, basi asifanya upungufu wowote katika mlo wa zamani, mavazi au sheria za ndoa”. (Biblia, Kutoka 21:10)

    “Kama mtu ana wake wawili, mmoja anayempenda na mwingine ambaye hamuoni …” (Biblia, Kumbukumbu la Torati 21:15)

    “Yeye alikuwa na wake wawili …” (Biblia, Samuel 01:02)

    “Kwa hiyo, Daudi alifika huko pamoja na wake zake wawili …” (Biblia ya Samuel 02:02)

    “Lakini wakati wa usiku aliamka na kuchukua wake wake wawili na watu wake wawili wahuduma na wanawe kumi na mmoja….” (Biblia, Mwanzo 32:22

    Ni Haramu Kwa Waislamu Kunywa Pombe. Biblia Inatueleza Wazi Yafutayo

    “Uasherati na pombe lazima uondoshe akilini” (Hosea 4:11 Biblia)

    Je, wamesahau kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msidanganyike! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti. wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang’anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu. (Biblia Kwanza Wakorintho 6:9-10)

    Waislamu Hawali Nguruwe, Damu, Au Wanyama Wafu. Biblia Pia Inakataza Hilo

    “Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi. Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga yao”(Biblia Walawi 11:7-8)

    Baadaye katika aya ya 21 ya sura hiyo tunasoma yafuatayo: “usile kitu kilichokufa chenyewe.

    “… Na wale wenye kula nguruwe na uchafu mwingine, ndiyo, pia panya, watapotea wote, asema Bwana”. (Isaya 66:17 Biblia)

    “Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.”(Biblia Matendo 15:20)

    “Ni lazima tu subiri si kwa kula damu. Kwa sababu damu ni roho na roho usile na nyama. Unapaswa kumwaga kwenye ardhi kama maji “. (Kumbukumbu 12:23-24 Biblia)

    “Na kama mtu wa nyumba ya Israeli, au mmoja wa wageni ambao wanaishi kati yao, akinywa damu yoyote, nami nitaweka uso wangu dhidi yake ambae anakunywa damu na kumkatilia kwake mbali na watu wake” (Mambo ya Walawi 17:10 Biblia)

    “Na hakuna damu yoyote mtayokunywa, ama kwa ndege au mifugo, bila kujali wapi mlipo. Kila mtu anaekunywa damu yoyote, huyo atakatiliwa mbali na watu wake “. (Walawi 7:26-27 Biblia)

    Waislamu Wanachukua Wudhuu (Kutawadha) Kabla Ya Kuswali. Biblia Inasema Yafuatayo

    “Na Musa na Haruni na wanawe baadaye akanawa mikono na miguu kwa maji kutoka humo. Mara nyingi walipokuwa wakenda ndani ya hema ya kukutania, au kuja mbele ya madhabahu, Walikuwa wakijiosha, kama Bwana alivyomwagiza Musa. (Kutoka 40:31-32 Biblia)

    “Wale ambao hujitolea na kujisafisha kwa maombi katika bustani, wakiongozwa na mtu ambaye anasimama pale katikati …” (Isaya 66:17 Biblia)

    UISLAMU NDIO DINI YA HAKI NA UKIRISTU SIO DINI YA HAKI MAANA ILIBUNIWA NA WATU MAALUMU NA LAIIT KAMA HUJABUNIWA NAULIZA SWALI JE WAKIRISTU WANAFATA MAFUNDISHO HAYA,WALAH WABILAH NA HAKUNA ANAEFATA.ALLAH AWAONGOE WOTE WAJE KATIKA UISLAAMU

    Like

  35. mhina says:

    (1) Ndugu Ibrahimu:Hongera sana kwa changamoto ulizonipa,Mimi nitaanza na wewe mpaka nitamfikia wa mwisho.Wewe umenukuu(yeremia 23:14) na kumtupia lawama paulo mtume wa mungu ambaye cha kusikitisha kamwe nyakati zile alikuwa hajazaliwa ukidai kuwa ni baadhi ya manabii walioipotosha biblia….lakini ukweli ni kwamba zile zilikuwa ni nyakati za zamani sana ambapo ni kweli kabisa kulitokea manabii wa uongo wa ‘BAALI ‘ambao idadi yao ilikua 400,lakini kamwe hawahusiani na manabii wa kweli wa Mungu walioandika biblia takatifu,soma(1Wafalme18:17-30-31).Manabii hawa Waliovuma hata Yerusalemu na kutabiri mambo ya uongo kamwe hawajapata nafasi kuandika biblia neno takatifu la mungu wetu.Sasa basi,kwasababu wewe lengo lako ni kuchafua neno la mungu lionekane ni la uongo,hebu tuangalie maneno ya mungu yanavyosema halafu sisi wote tutatafakari kuwa tumuamini mungu au wewe muisilamu.Mungu anasema’NA MKONO WANGU UTAKUWA JUU YA MANABII WANAOONA UBATILI NA KUTABILI UONGO HAWATAKUWA KATIKA MASHAURI YA WATU WANGU.Soma(ezekiel,13:9).Umeona hapo ndugu ibra..ni kwamba mungu wetu sisi wakristo ndiye anaelilinda neno lake yeye mwenyewe kwa kuteua na kutunza manabii wake wachache kama wakina isaya,yeremia na wote wanaoonekana katika biblia Kwa ajili ya mataifa yote duniani tusije tukalikosa neno lake la kweli akatuangamiza kama sodoma na gomora.Soma(Isaya 1:9)(warumi 9:27-29).Sisi wakristo imani,upole na unyenyekevu ndiyo msingi wa dini yetu na pia ndiyo tabia na asili ya Yehova mungu wetu.Katika biblia yeye anaendelea kutuhakikishia hivi:MIMI SITALIHALIFU AGANO LANGU,SITALIBADILI NENO LILILOTOKA KINYWANI MWANGU,NENO MOJA NIMELIAPA KWA UTAKATIFU WANGU,HAKIKA SITAMWAMBIA DAUDI UONGO,WAZAO WAKE WATADUMU MILELE,NA KITI CHAKE KITAKUA KAMA JUA MBELE ZANGU,KITATHIBITIKA MILELE KAMA MWEZI.SHAHIDI ALIYE MBINGUNI MWAMINIFU.Soma(Zaburi 89:33-37)…Looh!!!..Ndugu unaesoma mahalihapa nakuthibitishia kutoka moyoni mwangu kuwa mimi naugua mno mno na kutokwa na machozi ninapoendelea kuyatafakari hayo maneno mazito mno aliyotuwekea mungu wetu kuwa silaha kali ya kutulinda na mchezo mchafu wa ibilisi anaoendelea kuufanya ili kupotosha wateule wa mungu!!.Ndugu ibra hapo utakua umeona kuwa sisi wakristo uhakika na ushahidi wa neno la biblia tunaloliamini umetoka kwa mungu mwenyewe na wala si ushahidi au maneno ya mtu fulani tena mmoja tu au viumbe fulani kama majini nk.hapana si hivyo ndugu!!.Biblia imeandikwa na manabii wengi kwa nyakati mbalimbali.Ndio maana pia mkitoa sababu eti sijui paulo kafanya hili na lile..tunawapuuza na kuhisi mmechanganyikiwa!!.Hoja yako nyingine ndugu ibra ni kwamba uliwatetea ndugu zenu majini waliomo kwenye quran yenu ukisema kuwa wao ni wema kwa sababu walisamehewa na mungu…lakini ukichunguza quruan yako utagundua kuwa wao majini ndiyo waliotangaza kujinyenyekeza kwa mungu na kusamehewa…hayakuwa maneno ya mungu mwenyewe ila wao walijisamehe wenyewe kupitia kitabu hicho cha mhamad alichopewa kule mapangoni kwa njia ya kutiwa kabari na kuminywa na mashetani kama alivyoripoti yeye mwenyewe kabla ya kubadilishwa maneno yake na mkewe…na pia lazima tutambue kuwa mwanamke pia alihusika kumpotosha Adamu mbele za mungu kwa kubadili maneno ya kweli.Hivyo alama ya upotevu kibiblia yatoka kwa mwanamke kubadili ukweli yaani hawa…na pia alama ya wokovu yatoka kwa mwanamke huyohuyo yaani Mariamu kumzaa bwana yesu.Pia ukatoa hoja nyingine kwangu kuwa unashangaa kwanini andiko la sheria litoke kwa mungu alafu andiko la kuvunja sheria litoke kwa wanadamu?….jibu ni kwamba sio kweli kwa kuwa hakuna andiko la mwanadamu la kuvunja sheria za mungu katika biblia yetu takatifu!!…umeona wapi?…labda kwenye quruan.Ila lipo andiko la sheria ambalo linapatikana kwenye agano la kale na pia lipo andiko la KUTIMIZA SHERIA(sio kuvunja sheria)lililopo katika agano jipya yaani INJILI…Na yote haya yameletwa na Mungu sio mwanadamu.Tatizo wewe unamuelewa mtume paulo vibaya alafu unataka kusema yeye ndiye aliyeleta utimilifu wa sheria…hapana sio yeye bali ni mungu mwenyewe,kasome(yeremia 31:31-34).Na mtume paulo anaposema mwisho wa sheria hamaanishi tuishi bila ya kufuata sheria za mungu bali anamaanisha kuzifuata kwa roho kama mungu mwenyewe alivyotuagiza kwenye ile yeremia 31:31.thibitisha hili kwa kumsoma paulo kwenye(warumi 8:4).katika quruani ndiko tunaona kukosekana kwa nuru ya neno la kweli la mungu pale inapowafundisha waisilamu kufuata mambo ya sheria za mungu kwa mwili jambo ambalo kila muislamu unaekutana nae anakwambia hatuwezi kabisa kufuata kwa asilimia mia kama Allah anavyotaka ukimuuliza kwanini anakujibu kwa sababu tupo nchi ya wapagani!!!…loh!..poleni sana ndugu zangu kwa sababu ukikiri hivyo wewe mwenyewe inamaana mungu wako ameshindwa na wewe umeshindwa lakini usikate tamaa okoa nafsi yako kwa kuja kwa bwana yesu nae atakupokea…utakua umeshindwa kweli kabisa pale utakapoendelea kumkataa bwana yesu mpaka mauti yako.Naomba ninukuu majibu ya waisilamu wengi wanavyonijibu swala hili pale ninapowauliza…wao hujibu:TUPO KWENYE SERIKALI YA KIPAGANI KWA HIYO HATUWEZI KUFUATA SHERIA ZA ALLAH…Looh!! Masikini waisilamu!!…mambo yako wazi kabisa…sasa kwanini mnamkataa bwana yesu? Nakuuliza wewe ndugu ibra na waislamu wenzako?? Maana hapo jibu lenu lilitakiwa kuwa hivi:TUPO KWENYE DINI YA KIPAGANI KWA HIYO HATUWEZI KUFUATA SHERIA ZA NCH…Ndio maana kutwa ni kuchoma makanisa!!.Sasa sijui ni mungu gani huyo muumba mbingu na nchi ya kwamba wewe ufe alafu kule mbinguni ukampe sababu ya kutotii sheria zake zote kuwa ni hiyo mnayotoa halafu eti yeye asiwaadhibu!!..loh loh!!…naugua roho kuwaona ndugu wakipotea waziwazi… halafu bado unataka kushindana na biblia neno la kweli la mungu pasipo kujua kua ile ndiyo nuru ya dunia!!.SIHUBIRI DINI HAPA…MIMI MHINA NAHUBIRI UKWELI AMBAO HATA WEWE MUISILAMU HUKO ULIKO UNAJIHISI KUTAABIKA LAKINI SIKU ZOTE NDIVYO ILIVYO UKWELI UNAUMA SI NDIVYO TUNAVYOSEMA MITAANI?..Basi ndugu ibra na wenzako mfuateni bwana yesu anayejielezea njia zake vyema kwenye biblia na isiwe yule isa yesu wa quruani wala mhamad maana mkiendelea hivyo hakika mwisho wake ni MAUTI…Haiwezekani hata kidogo eti uongo upewe nguvu halafu uonekane kama nao ni ukweli au ufanane na ukweli..HAYO NI MAKUFURU MBELE ZA MUNGU NYINYI WAISILAMU MKIJI IMANISHA NYINYI WENYEWE NA KUWATEKA VIPOFU WASIOJUA MAANDIKO KWA UFASAHA WA ANGALAU WA KUWATOSHA NA KUWALINDA….Pia ndugu ibra ulinipa hoja yako ya kusema kuwa iweje sisi wakristo tufundishwe kwamba mtu akiwa na imani ataokoka bila ya kutenda matendo mema?…sasa hapo najiuliza kuwa sijui ni mkristo gani au kanisa gani ulipopata elimu hiyo?..hilo ni tatizo lako la kutoisoma biblia vizuri na kuielewa…matendo mema kwa mkristo ni sehemu ya kutii injili ya bwana yesu na neno lote la mungu katika biblia…ndio maana wakristo hatuchomi miskiti wala kulipa ovu kwa ovu kama injili ya bwana yesu kupitia mtume paulo inavyotufundisha…tatizo ni wewe mwenyewe kutoielewa biblia.Sasa kama nyie quruani inawafundisha vijana wake matendo mema kuliko wakristo mbona hali ni tofauti kabisa jinsi vijana hawa wanavyoonekana ukilinganisha na wale wa kikristo?MIMI SIJUI LABDA JAMBO HILI ULITAFAKARI MWENYEWE…Hoja yako nyingine ukasema eti bwana yesu alibariki kufa kwenye(luka19:27) lakini ukiisoma injili yote ya luka utagundua kuwa hamaanishi uuaji wa kuchinja kama alivyokuwa akifanya mhamad maana hebu tujiulize hivi:MBONA WALE WANAFUNZI WAKE HAWAKUMLETEA KWELI BWANA YESU HAO MAADUIA AKAWAUWA KWELI KIMWILI KAMA VILE TUNAVYOONYESHWA KATIKA QURUAN MHAMAD AKIWAPIGA KWELI MAJAMBIA NA MAPANGA MAADUI ZAKE PALE ANAPOAMURU WALETWE?..PIA JE,TUKIZITAZAMA TABIA ZA BWANA YESU KWA UJUMLA WAKE KATIKA BIBLIA ANAWEZA KUFANYA MAMBO KAMA HAYO?…MBONA KATIKA INJILI ZAKE ZOTE HUSISITIZA UPENDO’KUSAMEHEANA NA HATA MWISHOWE YEYE MWENYEWE KUULIWA BILA YA SABABU?…Sasa ndugu ibra na waisilamu wenzako yatafakarini hayo ambayo ni baadhi tu ya sifa za bwana yesu halafu mtatambua kua hamkumuelewa alichomaanisha kwa kuwa mambo yake mengine yalikuwa ni mafumbo ya rohoni ambayo kwa kawaida mtu anayetazama mambo ya mwili tuuu…kama nyie anakuwa na sifa tatu,kwanza awezi kuamini,pili awezi kuelewa na tatu hapokei…yeye huona giza kwa hiyo pia hutafuta giza tu..sio mwanga na matumaini.cha kusikitisha ndugu ibra ni kwamba hata kuruani yako haikufundishi na kuku maanisha hivyo…humsifu sana sana yule isa yesu katika kitabu chenu ambae nyinyi mnamuamini kuwa ndiye Bwana yesu..sasa mbona wapingana na hata kitabu chako tena?.Ndugu ibra ukamalizia hoja zako kwa kusema:Ufalme wa mungu wakapewa Taifa jingine ukitaka kutuimanisha ni Taifa la kiarabu ambapo ulijua kuwa ikiwa hivyo basi nyinyi waislamu mtahusika…hakika hicho ni kichekesho maana hata ndugu wengi zaidi wa kiislamu huaminishwa hivyo…lakini ukweli ni kwamba hilo ni Taifa teule takatifu la mungu la watu wa milki kuu ya huko mbinguni wakiongozwa na bwana yesu mwenyewe akiwa jiwe au msingi uliokataliwa na waislamu lakini wakristo tukampokea na kuwa mawe madogomadogo yanayojenga Taifa hilo la mungu huko mbinguni….Sasa ndugu yangu kama unayobiblia kathibitishe haya kwa kusoma(isaya28:16-18)linganisha na(1Petro2:5-10)(waefeso 2:19-22).Naamini ukimaliza kuyasoma masomo hayo uongo wako utakuwa umekutoka.Nimemaliza kukujibu hoja zako lakini nakuomba uyatafakari yote kwa kina..na pia nakuomba uendelee kutazama wenzako wote nitakaowajibu kwani naamini utapata mengi zaidi ya kujifunza.UBARIKIWE.

    Like

  36. mhina says:

    (2)Ndugu Abdallah nawewe kwa mujibu wa maelezo yako uliyotoa huko juu ni kwamba majini ni viumbe aliowaumba Allah mungu wenu,wenye uwezo wa kumuasi mungu wenu huyohuyo Allah..maana ulikiri wewe mwenyee kwa kusema:MALAIKA WEMA KAMWE HAWAWEZI KUMUASI MUNGU…Kwa hiyo Allah kaumba majini ambayo kwa asili yao tangu mbinguni ni waasi wa Allah tofauti na wale malaika wema wasioweza kumuasi Allah…halafu huku duniani tunaambiwa na waislamu kuwa hao majini walioumbwa kwa asili kuwa waasi wa Allah ni ndugu zao!!!..hainiingii akilini hata kidogo…ndio maana pia kwa mujibu wa aya za quruani majini hayo yametengewa aya zao na kuonekana wakijibariki na kujisamehe thambi wao wenyewe wakishindwa kabisa kuelewa huko mbinguni kukoje na wanasema tukijaribu kwenda twapigwa na vimondo na hatujui mungu anawatakia shari au la wanadamu wa duniani,ajabu kweli….eti malaika wanaotakiwa kulinda enzi ya mungu huko mbinguni wanasema maneno hayo.Kwa vyovyote vile majini kama kweli wangekuwa ni malaika wema wa mungu iliwabidi huku duniani katika vitabu vyetu vya dini wasingeweza kuendelea kuonyesha udhaifu wao kwa kuwa iliwabidi wawe tayari safi kwa ajili ya kukaa salama na wanadamu ili kutupa mambo mema ya huko.Hebu ndugu Abdallah tafakari kweli mambo hayo yanaingia akilini?…alafu bado eti tunaambiwa walipokea msamaha wao kupitia kitabu kilichopokelewa kwa siri mapangoni huku mpokeaji huyo akitiwa kabari na kuminywa na pia kukiri yeye mwenyewe kuwa ni mashetani yaliyomchezea!!.Sasa wewe ndugu Abdallah naamini kuwa unaakili timamu za kutafakari mambo bila hata kutumia elimu kubwa lakini hebu tusaidiane kutafakari jambo hili:MALAIKA GANI HAO WA MUNGU WANAOMTOKEA NABII WA MUNGU ALAFU ETI WANAMLAZIMISHA KULIPOKEA NENO HILO WALILOLILETA KUTOKA KWA MUNGU NA KUMUACHA HOI NABII YULE AKIJAA HOMA TELE TELE?…HIVI HUYU MUNGU HAKUJUA ASILI DHAIFU YA MWANADAMU ALIE MUUMBA MWENYEWE NA KUMPA UWEZO WA KUYAPOKEA HAYO?….Kwa mujibu wa biblia yetu takatifu ni kwamba pepo wote hao ni mashetani na kamwe mungu hajawasamehe.ndugu Abdallah katika hoja zako huko juu ulijaribu kusema kuwa walijisalimisha mpaka kwa bwana yesu lakini kwa taarifa yako kujisalimisha kule ni kwa uoga na wasiwasi wao na wala sio kwamba walijisalimisha ili watufae kwa maisha yetu.Biblia yenyewe inawaita PEPO WACHAFU..Soma(marko 5:13)…Wakimhoji bwana yesu:JE,UMEKUJA KUTUTESA KABLA YA MUHULA WETU?….Alafu ndugu Abdallah wewe kwenye hoja zako huko juu unadai ni ndugu zenu na ndio maana walijisalimisha kwa bwana yesu!!!…hivi ndugu wewe ni muislamu kweli unaeyajua maandiko yako au unapigapiga kelele tu,kwenye mitandao?maana hoja zenu mnaonekana kama hamuelewi mambo vizuri lakini nawashauri mngetuletea mashehe labda wao watakua na hoja kali na za maana.Nimalizie kujibu hoja zako ulizonipa kwa kusisitiza tena kuwa ndugu Abdallah na waislamu wenzako njooni kwa bwana yesu njia ya kweli…msiendelee kuabudu na mashetani waliojitia uelevu wa hali ya juu kabisa ili kuwapotezeni nyinyi kwa kuwa biblia yetu takatifu inalithibitisha jambo hili kwa kusema hivi:NA MALAIKA WASIOLINDA ENZI YAO WENYEWE,LAKINI WAKAYAACHA MAKAO YAO YALIYOWAHUSU,AMEWAWEKA KATIKA VIFUNGO VYA MILELE CHINI YA GIZA KWA HUKUMU YA SIKU ILE KUU.Soma(yuda 1:6)…Hapo inaonyesha wazi kuwa walivyoadhibiwa kulekule mbinguni hakukuwa na msamaha wa mungu tena dhidi yao ndio maana maandiko yanaviita kuwa ni VIFUNGO VYA MILELE…Maana hebu tujiulize kwa akili zetu za kibinadamu kuwa kama kweli kungekuwa na waliosamehewa huku duniani sisi kama wanadamu tungewezaje kuwatafautisha maana nilitoa hoja huko juu kuwa dada mmoja alilazimishwa na majini kuwa eti ni lazima awe muisilamu na kama hataki WATAMUUA!!….Sasa jini huyu anaeupenda uisilamu na kutishia hata kuua sijui alikuwa wa Allah na dini yake au sijui ni wale majini wasiosamehewa? Na kama ni jini mwema wa Mungu wenu mwema Allah..mbona ni muuaji?…NDUGU ABDALLAH NA WAISLAMU WENZAKO NJOONI KWA BWANA YESU TUJADILIANE MAMBO YA KWELI YA MUNGU KWA KUWA BADO HAMJACHELEWA.Mwisho ubarikiwe na kuiona njia ya kweli lakini nakushauri usome na hoja za wenzako uone nilivyowajibu kwani naamini utapata cha kujifunza na kujihoji wewe mwenyewe…ijapokuwa mimi sio mwalimu wa biblia wala mchungaji…mimi ni mkristo wa kawaida tu.

    Like

    • Takbir!! Allah Akbar! Allah Akbar!
      (Ndugu Mhina)Namshukuru sana Allah kwa kunijalia kukufahamisha uliyokuwa huyajui kuhusu uislam. nitajibu hoja zako kwa kunukuu uliposhindwa kunielewa.Inshaallah!

      1.Unasema “halafu huku duniani tunaambiwa na waislamu kuwa hao majini walioumbwa kwa asili kuwa waasi wa Allah ni ndugu zao!!!”
      nilikupa haya inayokataza kufanya urafiki na majini nashangaa bado unaendelea kuniambia “tunaambiwa”, “tunaambiwa”, “tunaambiwa majini ni ndugu zao” mwambie huyo anayekwambia akupe haya ya Quran inayosema hivyo.

      2.unasema “majini hayo yametengewa aya zao na kuonekana wakijibariki na kujisamehe thambi wao wenyewe”
      hakuna haya inayoonesha majini wakijibariki au wakijisamehe dhambi zao hata moja! bali kuna haya inayoonesha majini wakinyenyekea baada ya kuisikia Quran ikisomwa na wakakiri kuwa ni maneno yasiyo ya kawaida bali yana maonyo makali dhidi ya watenda dhambi. soma QURAN SURA 47:29-32.(ipo kwenye hoja zangu hapo juu).

      3.unasema “hatujui mungu anawatakia shari au la wanadamu wa duniani,ajabu kweli….eti malaika wanaotakiwa kulinda enzi ya mungu huko mbinguni wanasema maneno hayo” hakuna sehemu nilikosema majini ni malaika, nilinukuu haya inayosema majini ni miongoni mwa ibilisi, hivi we haya yote unayatoa wapi? ningekuwa na uwezo ningemuuliza mwalimu wako wa primary ulikuwa unakuwa wa ngapi darasani maana nimenukuu haya ziko wazi kabisa au hukuzisoma vizuri ndg? naomba urudie usome vizuri kabla hujajibu.

      4.unasema “lakini kwa taarifa yako kujisalimisha kule ni kwa uoga na wasiwasi wao na wala sio kwamba walijisalimisha ili watufae kwa maisha yetu”. kwani ni haya gani ya Quran inayoruhusu waislam kuwatumia majini kwa manufaa yetu?????mbona unapenda sana kuniambia “unasikia” , “unasikia”. nanukuu tena haya ya quran majini wakitoa ushuhuda

      QURAN72:6.” Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa
      wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidishia upotovu.”

      5. unasema “Alafu ndugu Abdallah wewe kwenye hoja zako huko juu unadai ni ndugu zenu na ndio maana walijisalimisha kwa bwana yesu!!!”
      Wallahi! sijasema hivyo! sasa hili sijui umelitoa wapi..

      6.unasema “msiendelee kuabudu na mashetani waliojitia uelevu wa hali ya juu kabisa ili kuwapotezeni anyinyi”
      Ndugu Mhina,usiseme kwa sababu tu unasema, ni sehemu gani katika quran inayosema sisi tunaabudu pamoja na mashetani???? sikia Allah anasemaje hapa chini.

      QURAN SURA 35:6. “Hakika Shet’ani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui. Kwani yeye analiita kundi lake liwe katika watu wa Motoni.”

      Ukinukuu kutoka kwenye Quran itakuwa bora zaidi kuliko kuniambia unasikia,au unaambiwa. kwa sababu hao unaowasikia mimi siwajui wengine ni maadui wa uislam.mimi naitambua Quran tukuf kuwa ndo mwongozo wa maisha yangu.

      Allah akiamua atakuongoa na kukuleta kwenye nuru inshaallah, mimi ni mwonyaji tu.

      Like

      • kelvin hussein says:

        allah siyo jina la MUNGU KUTOKA SURAYA 6, WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:20 MUNGU WAKO WATATUWARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8. OKOKA KUOKOKANI SASA WAKORINTHO WA PILI SURA YA 6 MSTARI WA 1 NA WA 2

        Like

  37. mhina says:

    (3)Ndugu Samir: Mimi ninamengi ya kusema na wewe kuliko wenzako huko juu kwa kuwa wewe unajifanya ulikuwa mkristo halafu eti ukabadili dini kwa kuhisi eti umepotea kumbe hata hujui kwanini yesu alilia msalabani!!…sasa wewe ulikuwa mkristo gani?….nyie ndio wakristo mnaomtaabisha bwana yesu maana badala ya kumpa maji akate kiu mnampa siki inayozidisha kiu na maumivu!!….Sasa naomba unipe sikio lako ili nikujibu hoja zako zote lakini usiogope maana mimi SIO MCHUNGAJI WALA MWALIMU kama ulivyoniita huko juu bali mimi ni mkristo wa kawaida lakini mimi najitahidi kumpa bwana yesu maji ili akate kiu sio kama wewe uliempa siki…Sasa naomba nianze kujibu hoja yako ya kwanza kwa kukunukuu,uliniuliza:MBONA BWANA YESU ALIJUTA PALE MSALABANI???…..Kwanza nianze kwa kukurekebisha ndugu kuwa bwana yesu hakujuta pale msalabani bali ALILIA……Bwana yesu alilia pale msalabani si kwa lengo la kujuta au kulalamika bali kwa lengo la KUONYESHA MATESO NA MATUMAINI YA MUADILIFU.Bwana yesu alituonyesha kwamba hata siku za mateso yetu tuendelee kumsifu na kumtukuza mungu mbele za watu wote.Kwa hiyo ndugu Samir,yale maneno na kile kilio cha bwana yesu kamwe sio kilio cha maneno ya mtu aliekata tamaa na kujuta bali kwetu sisi wakristo ni maneno na kilio cha sala ya mtu mwenye haki na mwenye kutupa matumaini makubwa mno katika mateso yetu tunayopitia hapa duniani.Bwana wetu yesu kristo pale msalabani alitufundisha kuwa katika mateso yetu tunayopitia hapa duniani,tusikate tamaa bali tumtumikie na kumtegemea mungu wetu pekee.Watu wengi kwa kawaida kwenye matatizo yao huenda kwa waganga wa kienyeji kwani wanadhani mungu amewaacha!!.lakini kilio na maneno ya bwana yesu yanatufundisha kuwa wakati wa matatizo ndiyo haswa wakati wa muafaka wa kusali zaidi na kumlilia mungu wetu pekee.Daudi mtumishi wa mungu,maelf ya miaka hata kabla ya kuzaliwa kwa bwana yesu… Yeye alitokewa na roho wa mungu na kutabiri visa vyote vitakavyokuja kumpata bwana yesu kwenye(zaburi 22:1-30)…haswa ule mstari wa kwanza,tunaona mfalme Daudi akiwa amejiliwa na roho wa Mungu anasema:MUNGU WANGU,MUNGU WANGU MBONA UMENIACHA?MBONA U MBALI NA WOKOVU WANGU,NA MANENO YA KUUGUA KWANGU?….Sasa kama ndugu Samir na waisilamu wenzako mngekuwa kweli hamumpingi bwana yesu basi mngeanza na daudi mtumishi na nabii wa mungu kutuhoji kuwa mbona alilalamika vile na wakati yeye ni nabii wa mungu?…lakini kama nilivyoelezea huko juu kuwa kila kilichoandikwa kwenye biblia yetu ni nuru lakini kwa wanaopotea ni giza kwao…maana waliwekwa na viburi vyao ili yawapate hayo lakini kila atakaejaribu kuliamini na kuliheshimu neno la mungu ATAOKOLEWA NA MUNGU WETU HAKIKA…Na huu pia ni baadhi tu ya ushahidi wa wazi kua ni kweli bwana yesu alisulubiwa kwa kua tunaiona nuru ya injili na wokovu wa mungu ukianzia mbali kabisa na mungu wetu ametuwekea hazina hizo za ushahidi ili sisi wateule wake tusidanganywe hata kidogo maana tukigeuka nyuma na tukikengeuka kwa kufuata elimu zilizokuja baadae za mataifa hakika tutakuwa kama mke wa lutu aliegeuka nyuma akawa jiwe la chumvi!!.Maana pale msalabani bwana yesu alisema:NAONA KIU…Lakini kiu hii sio kiu ya kinywaji bali ni kiu ya bwana yesu kuona mimi na wewe ndugu Samir tunaungama na kutubu dhambi zetu na kumtumaini yeye na kamwe sio mhamad…maana mhamad alishakufa na kukiri yeye mwenyewe kuwa hanamsaada tena kwako.Lakini kwa upande wa bwna yesu tunaona kuwa bwana yesu ni TOBA.Toba ni nini?…Toba ni tendo la mtu kutafuta rehema au huruma ya mungu.Ndio maana siku zote bwana yesu katika injili alikuwa anasisitiza hivi:CHAKULA CHANGU NDICHO HIKI NIYAFANYE MAPENZI YA BABA ALIYENIPELEKA!!!……Hoja yako nyingine ndugu Samir uliuliza hivi ni kwanini unapokuwa mkristo unalazimika kuamini kuwa yesu kalaaniwa kwa ajili ya dhambi zako? Ukasisitiza kwa kusema’ hiyo ni kazi ya shetani na ni kosa kubwa kwa muisilamu kuamini hivyo…..Sasa kama ni kweli kama ulivyosema kuwa:HILO NI KOSA KUBWA KWA MUISILAMU,Lazima ujiulize mwenyewe kile Allah alichowaficha kutambua hapo lakini mimi kwa kukusaidia naona Allah amewaficha nyie kutambua HAKI NA UTAKATIFU WA KWELI WA MUNGU WA KWELI UNAVYOPASWA KUA.,..Sasa tuangalie kuhani mkuu wa zamani katika torati ya mungu ambaye ni nabii musa jinsi alivyofanya ili tuone kuwa kati ya Muhamad na quran yake na bwana yesu,kati ya hawa ni nani aliepindisha sheria za mungu na kukosa njia muafaka ya kuwapa waumini wake?…..Tunaanza kwa kumuangalia muhamad anavyowafundisha waumini wake jinsi wanavyoweza kusamehewa dhambi zao zote kiholela bila ya kufuata utaratibu wa mungu utafikiri wanasamehewa na mwalimu wakiwa darasani…kwa kisingizio eti mungu wao Allah katakasika!!.lakini kwetu sisi wakristo tunapomtazama nabii musa katika torati,tunamuona mungu anamfundisha kuwa,UHAI WA MTU UPO KATIKA DAMU…Tena anamwambia kuwa nimewapa ili mfanye UPATANISHO KWA AJILI YA NAFSI ZA WATU KWANI NI HIYO DAMU IFANYAYO UPATANISHO KWA SABABU YA NAFSI.(walawi17:11).Tumeona hapo kuwa kumbe tukimkosea mungu lazima katika ibada zetu tutoe kafara ya kuchinja na hii kumbe ni kanuni ya kisheria ya utakatifu wa mungu.pia ndugu Samir soma zaidi(kutoka 24:5-8)(waebrania 9:22).Lakini tunafahamu kuwa damu za wanyama ilikuwa ni kielelezo tu,kwa kuwa mdhambi anayestahili adhabu hiyo haswa ni mwanadamu mwenyewe anaemkosea mungu…lakini pia tunajua kuwa chimbuko la dhambi ni baba yetu Adamu.Mungu wetu kwa kutupenda hakutaka kushughulika na mtu mmojammoja pia hakutaka tena wanyama waendelee kuuwawa kamasadaka bali yeye kwa kumuonyesha ishara baba yetu ibrahimu kwa kumwambia amchinje mwanae(mwanzo 22:1-3)….akaamua aliadhibu chimbuko la dhambi maramoja kwa kumtoa kuhani mkuu kabisa ambaye ni bwana yesu kwa kuwa sheria yake takatifu inasema hivi:PANAMADHARA MTATOZA UHAI KWA UHAI.Soma(kutoka 21:23)…Mungu alimtoa bwana yesu kwa sababu yeye pekee ndiye aliyekuwa mkamilifu wa kulipia uhai mkamilifu alioupoteza baba yetu adamu.Ndiyo maana ukija kwenye injili biblia inasema:KAMA WATU WOTE WANAKUFA KWA DHAMBI KATIKA ADAMU KADHALIKA NA KATIKA YESU KRISTO WATU WOTE WANAOKOLEWA.Soma(warumi 5:19)(1wakorintho15:22)…pia soma zaidi utabiri wa nabii isaya tangu zamani,kwenye(isaya 53:4-12).Biblia kamwe haitufundishi kuwa bwana yesu ndiye alie laaniwa kama waislamu wanavyotangaza bali inasema mungu kwa kuheshimu sheria zake takatifu na pia kwa kutupenda sisi akamtoa bwana yesu ili atutengenezee toba na sisi tuuone huruma wake na kusamehewa kwa njia moja tu,ya kumuamini katika kazi yake hiyo…ndiyo maana bwana yesu katika injili anatangaza kuwa MIMI NDIMI NJIA NA KWELI NA UZIMA MTU HAJI KWA BABA ILA KWA NJIA YA MIMI..kwa kuwa sisi ndiyo tuliolaaniwa kwa sababu ya madhambi yetu na yeye ni huruma wetu mbele za mungu kama nabii musa alivyowatoa wanyama kwa niaba ya watenda dhambi lakini pia tunaonakuwa wanyama wale hawakuwa na hatia tena walikuwa safi na wakamilifu kabisa….Sasa basi kwa maelezo hayo machache na ya harakaharaka tunamuona jinsi muhamadi alivyokwenda kinyume kabisa kabisa na torati ya musa pia na njia sahihi ya mungu ndugu…amewaacha kwenye mataa waumini wake hata hawaelewi mambo wanayoyafuata yanamanufaa gani kwa mungu wao!….huku masikini wakionyesha juhudi ya kumpenda Allah na mtume wake pasipokujitambua kua hicho walichovaa ni KITANZI CHA MAUTI…njooni kwa bwana yesu ndugu…..Namalizia hoja yako ya mwisho uliyoiandika mwenyewe ndugu Samir inayonisikitisha mno!!!….ulikiri wewe mwenyewe huko juu kuwa waisilamu hamuwezi kufuata sheria za Allah kikamilifu kwa sababu mko katika nchi ya kipagani…sasa na mimi nikuulize maswali.je,kwa hali hiyo unakubali sasa kwamba dini ya kiislamu ni ya kipagani isiyokuwa na njia sahihi ya kuweza kufuatwa na jamii ya watu?…na kama ni hivyo mbona mnawakazania watu wawe waisilamu wakati nyie wenyewe mnaona kuwa mbele hakuna njia?…mnafikiri mungu aliyemtakatifu anaweza kusikiliza sababu zenu hizo za kibinaadamu kwamba utamjibu kule mbinguni kuwa hukufuata sheria zake kwa sababu ulikuwa kwenye nchi ya kipagani?,..hivi kwa hali hiyo tu,ya kushindwa kwako huko, hujui kuwa mnaishi chini ya laana ya mungu?.maana sheria za mungu ziko wazi kabisa zinasema hata ukijikwaa kwa kukosea sheria moja tu…basi wewe ni mkosaji wa zote!!!…tena hata usijisumbue kwa kuwa hata hao sijui saudi arabia,iraki,iran wanaojifanya wanazitekeleza ni uongo mtupu wa kujiongezea mathambi tu,kwa kuwa njia ya mungu ni kupitia bwana yesu pekee.Mwisho ubarikiwe na huyu mgeni hapo juu alietoa hoja zake za kitoto namuweka kiporo kwanza ila mimi nawashauri msikubali kamwe kufa chini ya imani ya Allah kwa kuwa hayo ni mauti ya wazi kabisa ya nyinyi waislamu kujitakia.UBARIKIWE NDUGU SAMIR.

    Like

    • Samir says:

      umekazania nikujibu usijali kila hoja yako ina majibu.
      1. Unasema Bwana Yesu hakujuta msalabani! inaelekea hujui nini maana ya kujuta.Ndugu Mhina mimi na wewe tunaamini kuwa Yesu alikuwa hasemi uwongo hata kidogo!! kwa hiyo kitendo cha mtu ambaye hajawahi kusema uwongo lazima kila neno analosema liwe la kweli!!! kama ndo hivo Yesu alipokuwa msalabani alidai Mungu wake amemuacha yaani amemtupa!!!.Kwa hiyo mimi na wewe lazima tukubali kuwa ni kweli Mungu wake alimuacha kwa sababu Yesu hawezi kudangnya!!!. Hivi na wewe ukiwa katika matatizo utasema Mungu amekuacha!!! Hivi ndivo mungu wenu anawakimbia mkiwa na matatizo!!?

      Mungu wa waislam hatuachi hata kidogo katika matatizo
      QURAN SURA2:153.” Enyi mlio amini! Takeni msaada kwa subira na Sala. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanao subiri.”
      Mwenyezimungu anatuahidi kuwa pamoja nasi endapo tutaswali na kusubiri hatatuacha kama alivyo muacha Bwana Yesu msalabani.huyo ndo Mungu wa kweli.

      2. katika uislamu ni kosa kusema Yesu yaani mungu wenu kaangikwa na kutundikwa mtini kwa maana
      (galatia 3:13)imeandikwa amelaaniwa kila aangikwaye mtini
      (kumbukumbu la torati 21:23) aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu.

      Laana ni neno lililo tokana na neno la kiarabu yaani la’aana maana yake ni “kuwa mbali na Mungu” kwa hiyo Allah anatuambia Yesu ni miongoni mwa watu waliokaribu nae kwa hiyo hili swala la kutundikwa msalabani hasa halimpasi.

      QURAN SURA 45.” Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu
      anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa
      Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa
      (kwa Mwenyezi Mungu).”

      3.Ndugu mhina una hamu ya kutaka kujua anayeipinga torati; mpingaji torati mkubwa ni Paulo mtume wenu nyie msiotahiriwa/wenye magovi(galatia 2:7) wakati yeye katahiriwa((wafilipi 3:5)

      MATHAYO 5:17 “Msidhani nalikuja kutengua torati wala manabii la! bali nimekuja kutimiza, kwa maana nawaambia , mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie basi mtu yoyte atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni;.”
      Hapo juu unasema sheria za Mungu ni takatifu,sasa tumsikei paulo mtume wa wenye magovi(wasiotahiriwa) anasema kwake sheria za Mungu katika torati ni laana soma(WAGALATIA 2:16-21, 3:10-13, na WARUMI 7:1-25) anasema hizo sheria za torati ni laana. kwa hiyo mtume wenu paulo ataitwa mdogo katika ufalme wa mbinguni kwa maana amewafundisha watu ndivyo sivo kwa kusema kiristu amewakomboa kwenye laana ya torati kwa kufa msalabani.wewe unasema sheria takatifu Paulo anasema sheria hizo ni laana.Dhdhdhdddhhhhhh!!!mnapingana wenyewe thatha!!

      4.Ndugu Mhina, kinachoniuma zaidi ni kwamba hata biblia yako mwenyewe lakini unajaribu kuikwepa na kufundisha uongo. Umekopi msitari huu “PANA MADHARA MTATOZA UHAI KWA UHAI.Soma(kutoka 21:23)” kisha ukadai kuwa Inamlenga Yesu kwamba atatoa uhai wake mwenyewe kwa ajili ya dhambi zenu!!! siyo kweli kabisa hiyo haiuhusiani na Yesu kabisa. hiyo haya ni kwa ajili ya kulipiza kisasi na inasema hivi;
      KUTOKA 21:23 “LAKINI KWAMBA PANA MADHARA ZAIDI, NDIPO UTATOZA UHAI KWA UHAI, JICHO KWA JICHO, JINO KWAJINO,MKONO KWA MKONO, MGUU KWA MGUU,KUTEKETEZA KWA KUTEKETEZA, JERAHA KWA JERAHA, CHUBUKUKO KWA AJILI YA CHUBUKO” UHAI KWA UHAI maaana yake ni kwamba aliyeuwa na auwawe.Sasa Yesu alimuua nani hadi akauwawa msalabani????

      Ahaahaaahaaahaahaaaahhaaa!!!!!!!!aibu yako ndugu yangu!
      Lengo ulitaka kuonesha ni jinsi gani Mtume Muhammad (S.A.W) alivyoenda tofauti na torati lakini kumbe wewe ndo hukuilewa torati, sasa tusome quran hapa chini tuone jinsi Mtume Muhammad (S.A.W) anaenda sawa na mafundisho ya torati.

      SURA ALMAIDA 5:45.” Na humo tuliwaandikia ya kwamba roho kwa roho, na jicho kwa jicho, na pua kwa pua, na sikio kwa sikio, na jino kwa jino, na kwa majaraha kisasi. Lakini atakaye samehe basi itakuwa ni kafara kwake. Na wasio hukumu kwa yale aliyo
      yateremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhaalimu.”

      5.”MIMI NDIMI NJIA NA KWELI NA UZIMA MTU HAJI KWA BABA ILA KWA NJIA YA MIMI.”
      Enhe! hii kauli huwa inanifurahisha sana! kwamba hakuna atakayeenda mbinguni mpaka aamini Yesu kafa msalabani…, Kwa hiyo maskini akina Ezekieli, Elisha,Yeremia na wote watakatifu wenu waliokuwepo kabla Yesu hajaja duniani wataangamia mno kwenye shimo la Jehannam maana hawakushuhudia kusulubiwa kwa Yesu na hawayajui mafundisho yake kwa hiyo njia ya kwenda kwa Baba hawaijui pia kwa sababu yeye ndo njia pekee.duh pole yao!! si makosa yao ni ya mungu wao wa biblia aliyewaumba kabla ya kuiweka njia ya kuelekea kwake, hivyo wakaishia kupotea tu.

      6.Mwisho ndugu Mhina sheria za kiislam kweli ni pana sana na zimegawanyika.
      i. SHERIA KUU NI(1.kushuhudia kuwa Mungu ni mmoja na Mtume Muhammad ni Mjumbe wake,2.kuswali, 3.kufunga,4.kutoa zaka, 5.kutoa sadaka) hizi ni lazima kwa kila muislam popote awapo kuzitekeleza kama hana dharula.
      ii.SHERIA ZA MAZINGIRA-hizi ni sheria ambazo mtekelezaji lazima mpaka mazingira yamruhusu kuzifanya, kama mazingira hayamruhusu si lawama na Si dhambi kwake lakini anatakiwa kuendelea kutafuta mazingira mazuri ya kuzitekeleza.Na mara nyingi hizi si sheria za kutekelezwa na mtu mmoja mmoja kama tulivyoona kwenye sheria kuu laa! bali hizi ni sheria zinazotekelezwa na dola au serikali ya Kiislam tu. kwa mfano mwizi kukatwa mkono au aliyeuwawa naye kuuwawa hapa lazima muwe na dola ya kiislam na ndo inawajibika kuzilinda na kuzitekeleza sheria hizi. kwa mfano Saudia,Pakistani,Indonesia,Iran hawa wanazitekeleza ipasavyo kwa sababu ni dola za kiislamu.
      HAYA NAOMBA UJIBU HIYO MADA NLIYOKUWEKEA I!NDUGU YANGU USIOGOPE.

      Like

  38. Samir says:

    MASKINI WAKIRISTU HAWAYAJUI HAYA KUWA YAPO KWENYE BIBLIA
    1.ASKOFU ANATAKIWA AWEJE?

    1TIMOTHEO 3:2 “Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja…”
    1TIMOTHEO 3:5 “Yaani mtu asiyejua kusimamia nyumba yake mwenyewe atalitunzajje kanisa la mungu?” Maaskofu huku hawaoi..Ndo maana kesi za mapadre na maaskofu za kubaka na kufanya ushoga zinaongezeka hasa kanisa katoliki na Anglicans hasa huko ulaya.

    2.NI VIPI JINSI YA KUNENA KWA LUGHA?
    1WAKORINTHO 14:26-32 “Basi ndugu imekuwaje mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi ana fundisho ana ufunuo ana LUGHA , ana tafsiri. Mambo hayo yote na yatendeke kwa kusudi la KUJENGA. kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu na mmoja atafsiri, lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa aseme na nafsi yake tena na mungu wake”

    je ni kweli hivi ndo mnavyonena makanisani mwenu?? kwamba mnanena kwa zamu, mmoja anafasiri na wengine wananyamaza? kama hamna mfasiri mnakuwa kimya??

    3.AMRI JUU YA WANAWAKE
    1WAKORINTHO 14:34 “Wanawake na wanyamaze katika kanisa maana hawana ruhusa kunenabali watii, kama vile inenavyo torati nayo, na wakitaka kujifunza neno llote, na wawaulize waume zao wenyewe nymbani mwao maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa au je Neno la Mungu lilitoka kwenu?” Mmesikia nyie mashosti waimba kwaya?

    1TIMOTHEO 2:11-12Mwanamke ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha wala kumtawala mwanamume, bali awe katka utulivu.” Mmesikia mama Rwakatare na wenzako!!? mimi nimejitolea kuwafundisha biblia bila malipo.

    4.HAKUNA MKIRISTU MWENYE IMANI HATA CHEMBE.
    LUKA 17:7 “Kama mngekua na imani kiasi cha chembe ya haridali mngeuambia mkuyu huu, ng’oka, kapandwe baharini nao ungewatii” Hii hata Papa Francis II hawezi kufanya.

    MATHAYO 17:20 “Mkiwa na imani ya punje ya haridali, matuambia mlima huu ondoka hapo nenda kule nao utaondoka wala halitakuwepo neno lisilowezekana kwenu” Kakobe, mz. wa upako,mwingira vipi hamna imani hata chembe ya haridali kweli au Yesu anawasingizia!

    YOHANA 14:12-13 Yesu anasema mtaweza kufanya hata zaidi yake.
    tuone je ni kweli? katika MATHAYO 9:24 Yesu anafufua maiti. lakini maskini maelfu kwa maelfu wakiristu wanakufa kila siku, hadi viongozi wao wanakufa! Padre Mushi kauliwa,mchungaji Kachila Sengerma kauliwa wakiristu walisikitika sana lakini sikusikia hata mchungaji mmoja au padre aliyejiktokeza kufufua wapendwa wao. Duh aibu yao!!Bwana Yesu watu wako imani hata chambe hawana.

    5.YESU KATIKA BIBLIA SIYO MFALME WA AMANI NI MFALME WA MAFARAKANO NA UPANGA
    MATHAYO 10:34-35 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani. la sikuja kuleta amani bali upanga”
    LUKA 14:26 ” Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake na mama yake na mke wake na wanawe na ndugu ze, na mke na mkwewe naam na hta nafsi yake mwenyewe hawezi kwea mwanafunzi wangu” kazi kwenu msio wachukia wazazi wenu Yesu hawatambui.

    LUKA 12:51 ” JE mwadahni kwamba nimekuja kuleta amani duniani? nawaambia la sivyo bali mafarakano” Kazi kwenu msiopenda mafarakano

    6.MAKATAZO YA KUPAYUKA KATIKA SALA
    MATHAYO 6:7-9 “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi, Basi msifanane na hoa.Baba yenu anajua mnayo hitaji kabla hamjayaomba”

    kupayuka maana yake ni kupaza sauti kwa nguvu, hii haitakiwi katika ibada lakini ndo imekuwa kawaida kwa makanisa ya “Born again au walokole” kupayuka kwenye ibada wakidhani ndo Mungu wao atawasika.Hivi wanaisoma biblia gani hawa???
    Mr.Mhina nina sababu nyingi mno za kuuacha ukiristu na hivi karibuni nitatunga kitabu Inshaallah.
    Allah awape mwanga wakiristu wote muingie katika uislam.

    Like

    • kelvin hussein says:

      NDOA ZA MITAALA WAKE WANNE NI DALILI ZA KIAMA ISAYA 4:1

      Like

      • Benn says:

        Kwa asilimia kubwa,Quran inapinga maandiko ya biblia na ndo maana tunasema Mungu anayeaminiwa na kuabudiwa na waislamu na yule wa wakristo si mmoja,ni Mungu wawili tofauti kabisa,kumbuka munhgu simkigeugeu mara aseme mke mmoja mara wengi,

        Like

  39. mhina says:

    Ndugu Samir na waislamu wenzako…nawaombeni tushindanishe mambo ya kitabu cha biblia, dhidi ya kitabu cha quruan ,ili tuone kipi ni kitabu cha kweli kutoka kwa mungu wa kweli,Maana kamwe mungu wa kweli hawezi kutuletea vitabu viwili tofauti vya muongozo wake vinavyopingana!!.Pia tumpambanishe muhamad wa Allah na Bwana yesu wa Yehova ili pia tuone ni Nabii yupi kati ya hawa,atakuwa kweli ametumwa na mungu kwa ajili ya wanadamu wote.Kwa hali hiyo,mijadala yetu yote itakuwa ni yamaana,ya haki na yenyekutupa majibu kujua haswa ukweli uko wapi….Maana kamwe hatuwezi kuacha njia sahihi za mungu eti kwa sababu sijui Askofu kafanya hili,Padre kabaka,Shekhe afuga majini,imamu kashiriki kuchoma makanisa kamwe hatutafikia muafaka kamili wa mambo haya ili kujua ukweli ulipo….hakuna haja ya kutafuta ukweli wa mungu kupitia tabia za wanadamu maana sikuzote wanadamu hawakosi kasoro zao,lakini njia za mungu kamwe hazipaswi kuwa na kasoro.Kwa kuwa ingekupasa pia kujiuliza hivi kabla ya kulaumu kanisa na viongozi wake:Kama uislamu ndio unamuongozo sahihi kwa asilimia zote,mbona nao wamegawanyaka katika mathehebu tofauti?…tena kutwa mitaani tunawaona wakichapana waziwazi kugombania miskiti jambo ambalo ni la aibu na kusikitisha mno kwa viongozi wowote wale,wanaodai kuwa ni mashahidi wa haki wa mungu.Lakini mimi sikuyaandika yote hayo,kwa kuwa ninatambua kuwa mwanadamu hawezi kuwa mkamilifu hata kidogo.Mimi na.ona umeshindwa kujibu hoja zangu huko juu…hebu nijibuni kwanza huko juu kama mimi ninavyofanya hakuna kuendelea tena mpaka mtetee dini yenu ya uislamu kwa hoja zote nilizotoa huko juu!!.kama mmeshindwa tufungeni mjadala….huwezi kukimbilia hoja nyingine wakati huko juu kuna hoja zangu tele mnazotakiwa mzijibu.HIYO NI DALILI YA KUSHINDWA!!….hoja zako mpya hizo zinajibika lakini kama nilivyosema kuwa teteeni kwanza dini yenu huko juu ili kwa wale watakaotaka kuwa waislamu,muwe mmewasaidia!.

    Like

  40. mhina says:

    ndugu Abdallh kwanza nakuomba upunguze jazba.pili kuhusu elimu yangu…ungeanza kwanza kuitafuta ya yule mhasisi wa dini yenu ili ujue alisoma kama mimi elimu ya awali au yeye alikua sifuri kabisa???…tatu,wewe ndio muislamu wa kwanza kukusikia unakataa kuwa majini sio ndugu zenu,baada ya wewe mwenyewe kugundua kuwa nimekunasa na point muhimu!!…kwa kuwa tunaambiwa kuwa waisilamu wote ni ndugu,sasa kama ni hivyo,MAJINI PIA SI MNASEMA NI WAISILAMU WALIOJISALIMISHA KWA ALLAH KUPITIA KITABU CHENU CHA QURAN HUKU NAO WAKIIAMINI NA KUITEGEMEA ELIMU HIYO ILI NAO WAENDE MBINGUNI KAMA NYIE….KWANINI NAO SASA MNAKATAA KUWA SIO NDUGU ZENU WAKATI MNASEMA WAISLAMU WOTE NI NDUGU? WAMEKOSANINI HAWA NAWAKATI WAO PIA NI WAISLAMU?….Mimi nafikiri ndugu Abdallah kabla ya kunilaumu ungekitafakari kitabu chako unachokiamini wewe mwenyewe kwanza…kwakuwa kamwe hapo hapakwepeki,maana hata kama ukikataa utaona kuwa majini/mashetani yanaitukuza na kuiamini quran,sasa hebu tafakari….iweje mashetani yaamini njia moja na wanadamu, wakati sikuzote tunajua kua njia ya mashetani ni JEHANAM?….HIVI NDUGU ABDALLAH,SHETANI ANAWEZA KUWA NA NJIA MOJA NA IMANI MOJA NA MWANADAMU?….Nakuomba kama umekosa hoja za kujitetea vizuri anza kuwasaidia wenzako kujibu hoja zangu zote.NILIKWISHASEMA KUWA SITAENDELEA MPAKA NISOME MAJIBU YA HOJA ZOTE NILIZOZITOA HUKO JUU.

    Like

    • QURAN SURA 72:majini wanasema
      “11. Na hakika katika sisi wamo walio wema, na wengine wetu ni kinyume na hivyo.
      Tumekuwa njia mbali mbali.
      12. Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani, wala hatuwezi
      kumponyoka kwa kukimbia.”

      hivo ndivo wanavojitambulisha majini wapo wema ambao hawana mahusiano na mwanadamu na wapo majini waovu ambao humuingia mwanadamu na wengine hutumiwa na waganga wa kienyji na wachungaji wa kikiristu wanaokwenda Nigeria kuwasaka hao majini hivyo wanakuja nao; na hao ni majini wakiristu

      QURAN 72:6. Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha Upotovu”
      majini wema hawana uhusiano na binadamu, majini ni waovu hata kama wakikuamrisha kusali.

      wapo majini wakiristu hao ni ndugu zenu wanaosema mungu ana mwana;
      Math 8:28-31 “ Naye alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo (Majini) walikutana naye, wanatoka makaburuni wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama wakapiga kelele wakisema tuna nini nawe mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya muhula wetu”
      hawa ndio majini ndugu za wakiristu wanaowaingia na ndo maana makanisani sa hizi ni jambo la kawaida kukuta kanisa lote lina mapepo. ni kawaida kuona wanawake wa kikiristu wakianguka makanisani wakiwa na mapepo wachafu. hii ni kwa sababu wote wanaamini mungu ana mwana kwa hiyo inakuwa rahisi kuwaingia kama ndugu zao.

      Like

  41. mhina says:

    ndugu abdala kwanza punguza jazba.halafu kuhusu elimu yangu ungeanza kwanza kuchunguza ile ya muasisi wenu kama alisoma hata elimu ya awali kama yangu au??.kwa ufupi ni kwamba sijaona kosa langu lolote la msingi…tena wewe ndio muislamu wa kwanza kukusikia ukipinga kuwa majini sio ndugu zenu!!.Majini tunaambiwa ni waisilamu kwa kuwa walijisalimisha na kuiamini quran.Napia tunajua kuwa waislamu wote ni ndugu…sasa majini nao si ni waisilamu mbona unakataa kuwa sio ndugu zenu!!.Wewe umeona wapi mashetani yanakua na njia moja ya kwenda mbinguni na wanadamu?…kama sio njia ya kuzimu hiyo,unafikiri itakua njia gani tena!!…kamwe,imani ya mwanadamu na njia zake za kumuokoa haziwezi kuwa sawa na zile za shetani!!…kama umekosa cha kujitetea ni kheri uwasaidie wenzako kujibu hoja zangu zote badala ya kuleta hoja mpya.

    Like

  42. mhina says:

    Nawashukuru sana ndugu Abdallah na waislamu wenzako kwa kuwa naamini kuwa sasa angalau,naamini injili ya bwana yesu imewafikia ndio maana mnakosa sera za maana na uwezo wa kujibu hoja zangu zote huko juu.Mimi nawapenda sana ndugu zangu na kama niliwakwaza huko juu naomba mnisamehe sana lakini pia nawaomba myatafakari yote mliyoyashuhudia huko juu kwenye hoja zangu kwa kuwa mimi naamini ni mungu mwenyewe kwa kuwapenda nyie,akawaleta kwenye blog hii ili mjihoji upya katika njia zenu.KWA MAANA SASA NAONA MNAZIDI KUCHANGANYIKIWA NA KUANZA KUYAGAWANYA MASHETANI/MAJINI KAMA KARANGA ILIMRADI MKWEPE HOJA….Kwanza kabisa huko juu ya hoja zako ndugu Abdallh ulisema kuwa kulikuwa na makundi mawili yaliyoumbwa na Allah,yaani Malaika wema wasioweza kumuasi muhu hata kidogo! na Majini/mashetani ambayo ni kundi la viumbe waliomuasi mungu wenu Allah na kufukuzwa toka mbinguni.Sasa ndugu Abdallah unapaswa kujiuliza kuwa,inakuwaje mashetani hawa waliomuasi mungu alie mtakatifu mno!!..eti halafu mungu huyohuyo tena kwa urahisi tu,hukuduniani ajekuwatangazia msamaha wa kirahisi tu…kupitia kitabu cha quran ambacho chenyewe upatikanaji wake ni wa kimashetani shetani kutoka mapangoni!!….hivi tujiulize kuwa,huyo mungu atakuwa mungu alie mtakatifu na wakweli? Kama ni hivyo,mbona sasa maneno yake ya kuwaadhibu majini hao aliyoyatoa kule mbinguni yanamrudia yeye mwenyewe kwa kubadilisha msimamo wake? Je,ndivyo mtakatifu Allah anavyowafundisha utakatifu wake hivyo?….kumbe ndio maana hata nyie mnasamehewa dhambi zenu kiholela kama Allah mwenyewe anavyowafundisha bila hata kufuata kanuni za kisheria za utakatifu wa kweli!!!.Kama Allah ni kweli yuko na tabia hiyo ya kubadilisha maneno yake bila ya mpangilio maalumu wa kufuata kanuni zake za kisheria,basi kamwe yeye sie mtakatifu kwa kuwa tabia hizo ni zetu sisi wanadamu kwa kuwa sisi sio wakamilifu.Ndio maana ukisoma majibu niliyomuandikia ndugu Samir,nilionyesha kitu alichokifanya bwana yesu kinachounganisha sheria za mungu kupitia nabii musa mpaka neema na huruma wa mungu ulivyotufikia…vyenginevyo ni kwamba, kama mungu wetu angetupitishia msamaha wa kiholela kwa jambo alilolikataza tangu mwanzo,basi nae,kamwe asingekuwa mtakatifu, bali angefanana na mungu wenu Allah!!.ndugu waislamu hivyo ndivyo kanuni za anaejiita mtakatifu zinavyotakiwa kuwa…sio sisi wanadamu ndiyo tumshinde mungu kwa kufanya dhambi halafu eti yeye alie mkamilifu anatusamehe kiholela tu,HAPANA!!…Lazima neno lake yeye ndio lishinde.Biblia takatifu inatufundisha jambo hili kwa kusema:ILI MUNGU AONEKANE HAKI NA KWELI NENOLAKE LIKASHINDE KWA WATU WOTE WAOVU WAINGIAPO HUKUMUNI.Soma(warumi3:3-4)(zaburi 51:4)….na wala sio kwamba eti sisi tufanye dhambi na kumshinda yeye alie mkamilifu kwa yeye kutusamehe kiolela,tabia hiyo kamwe sio ya mungu alie mtakatifu kweli…na hali hii,ndiomaana wakristo tunasema kuwa kamwe sheria haziwezi kutuokoa maana zinasimamia utakatifu wa mungu tu,pia ndio maana majini wenyewe walipomuona bwana yesu walimuuliza:JE,UMEKUJA KUTUHUKUMU KABLA YA MUHULA WETU?…maana walishajua kuwa kamwe hakuna njia ya kupona na kupata msamaha tena, mbele za mungu…huku wakijua wazi kuwa bwana yesu ametumwa kuokoa kwa njia ya neema na huruma wanadamu tu,waliodanganywa lakini kamwe sio eti amsamehe shetani ambaye alisha hukumiwa na maneno ya mungu alie mtakatifu mno!!.Kwa hali hii pia ndipo tunapopata sababu ya bwana yesu kusema kuwa, kamwe hakuna jina wala njia nyingine inayomfaa mwanadamu zaidi ya yeye.Kwa hiyo ndugu zangu waislamu,kamwe mtu asiwadanganye kuwa eti mashetani/majini yamegawanyika!!…malaika wema wa mungu hawagawanyiki na wote huenda njia moja na pia majini/mashetani hayagawanyiki kwa kuwa yote huelekea njia moja…na pia jambo la mwisho ni kwamba,MUNGU WA KWELI HASAMEI DHAMBI ZA VIUMBE WAKE KIHOLELA KWA KUWA YEYE NI MUNGU ALIEMTAKATIFU…TABIA YA MANENO YAKE NA HUKUMU ZAKE HAVIBADILIKI KIHOLELA NAMNA HIYO…Hayo majini ni serikali ya shetani aliyoianzisha huku duniani ili ili kudanganya wanadamu ndio maana waliposikia kuruani wakaipenda na kuiamini huku wakijisalimisha kwa kuwa hakukua na njia nyingine kwao ya kuwapa matumaini yoyote.NJOONI KWA BWANA YESU NDUGU ZANGU.

    Like

    • Nakushukuru ndugu Mhina,
      1.Sijakuelewa unaposema Mungu anasamehe dhambi kiholela au kirahisi!! kusamehe na kuadhibu ni kazi ya Allah, sisi hatuna mamlaka ya kusema kuna anao wasamehe kiholela kwa hakika kusema hivyo ni kufuru kubwa mno kwani unampangia Allah amsamehe nani na amuadhibu nani?

      QURAN SURA 3:129.” Na ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Yeye humsamehe(amtakaye) na humuadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Msamehevu Mwenye kurehemu.”

      2.Lakini pia unasema Mungu wenu hatawasamehe mashetani lakini cha ajabu Mungu wenu huyo anaonekana kushirikiana na mashetani hao kwenda kumkufurisha Ayubu, sasa hatawasamehe vipi wakati yeye ndo muajiri wao anawatuma wanaenda???

      KITABU CHA AYUBU2:6-7 “Bwana akamwambia Shetani tazama yeye(Ayubu) yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake basi shetani akatoka mbele za uso wa Bwana akampiga Ayubu na Majipu mabaya tangu uwayo wa mguu hadi utosi wa kichwa”
      Hivi huyu ndo Mungu wenu wa huruma???

      3.Lakini mungu wenu huyo mchawi hakuishia hapo akaona amtumie Paulo mashetani
      2WAKORINTHO12:7 “Na makusudi nisipate kujisifu kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, MJUMBE WA SHETANI ili anipige nisije nikajivuna kupita kiasi”
      Alimuomba Bwana kimtoke mara tatu!! naye akamjibu “neema yangu yakutosha” duh yaani kuwa na mjumbe wa shetani mwilini mwa Paulo hiyo ndo neema ya mungu wenu?

      4.Sasa nini kilimtokea Paulo baada ya kupigwa “neema ya mungu wenu” mwilini mwake?
      2WAKORINTHO11:21 “..nanena kiwazimu nami ninao ujasiri”
      akapata wazimu kutokana na wale mapepo(neema ya mungu wenu) akaanza kunena kiwazimu akaanza kujitangazia utume kwa watu wa mataifa wasiotahiriwa lakini.

      MOJA WAPO YA ALAMA YA UWAZIMU WA PAULO
      Paulo ni Mrumi, lakini mapepo walipomuingia akapata wazimu akasahau kabila lake akaanza kuropoka
      2WAKORINTHO11:22 “wao ni waebrania? na mimi pia.wao ni waisraeli? na mimi pia, wao ni uzao wa ibrahimu? na mimi pia.” eti yeye ni muisraeli….toka lini akawa muisraeli kama si mapepo aliyotumiwa na mungu wenu hayo yanafanya kazi ndani yake.

      Like

  43. mhina says:

    Ndugu Samir, kwanza nikupongeze kwa kufuata utaratibu kwa kunijibu zile hoja nilizokupa.Ijapokuwa majibu yako sikulizika nayo kwa kiasi nilichotaka….basi naomba na mimi kwanza nifuate utaratibu wa kukujibu hoja zako zote mpya ulizonipa ili twende sambamba halafu mwisho ndiko nitakuhoji yale ambayo niliyoyaona kuwa hukuyajibu vyema…Hoja yako ya kwanza uliyohoji ni neno kujuta, ukilikazania kuwa maana yake sio kulia.Hebu twende kwa ukweli na kwa haki,hivi unaweza kunionyesha kuwa ni wapi kwenye biblia penye maandiko yanayosema kuwa bwana yesu alijuta pale msalabani na sio kuwa alilia kama nilivysema mimi?ONESHA MAANDIKO HAYO!!….Lakini hata kama ukitaka hivyo kuwa alijuta,bado naamini kuwa maelezo yangu yalitosha kabisa kujibu hoja yako kuwa kwanini yote yale yalitokea.Hilo ndilo lililokuwa dhumuni la swali lako naamini.Halafu maelezo yako mengi uliyoyaendeleza pale,hayakuwa ya msingi kabisa kwangu kwa kuwa mimi sikukuhoji mambo yale uliyokuwa ukiyaelezea huko juu..sijui mungu wenu hawaachi au anawaacha maana haiwezekani kamwe kuchanganya tabia za Allah na tabia za Yehova mungu wetu.Hoja nyingine ukasema kuwa,ANAEPINGANA NA TORATI NI PAULO MTUME WETU SISI TUSIOTAHIRIWA WAKATI YEYE AMETAHIRIWA:Jibu ni kwamba wakristo tumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani ambayo hiyo,haikutokana kamwe na nafsi zetu bali ni kipawa cha mungu mwenyewe.Wokovu aliotupatia mungu sio wokovu wa matendo yoyote ya mwili ambayo tunaweza kujisifu bali ni kwa tohara ya rohoni aliyotujalia yeye mwenyewe kupitia bwana yesu ambaye ndiyo amani yetu.Biblia inatuambia:MMEKUWA KARIBU YA MUNGU KWA DAMU YAKE YESU KRISTO….Yaani tumestahilishwa tusiostahili,na hii ndiyo pia maana ya NEEMA.Mungu anasema:MIMI NAYAUMBA MATUNDA YA MIDOMO,AMANI,AMANI,KWAKE YEYE ALIYE MBALI NA KWAKE YEYE ALIYE KARIBU,ASEMA BWANA,NAMI NITAMPONYA.Soma(Isaya 57:19)…Hoja yako nyingine ulinihoji kuwa,KWANINI SHERIA ZA MUNGU MIMI NINAZIITA TAKATIFU WAKATI MTUME WETU PAUL ANAZIITA ZA LAANA?…Ndugu Samir,hoja yako hiyo,inanikumbusha maneno yamtume petro aliyesema kuwa,mambo ya hekima aliyopewa mtume paulo na mungu ili kutuhubiria,watu wasio na elimu,wasio imara,HUYAPOTOSHA KAMA VILE WAYAPOTOSHAPO MAANDIKO MENGINE KWA UVUNJIFU WAO WENYEWE.Soma(2petro3:15-18)…Mtume paulo kamwe hamaanishi kama ndugu yangu Samir unavyotakaiwe,bali anamaanisha laana ya mtu anayoweza kuipata mtu kutoka kwenye sheria za mungu…yaani kama vile kusema:SHERIA ZA MUNGU NI LAANA KWETU TUKIZIASI….Laana inayozungumziwa hapo,ni ile adhabu kali inayoamuru sheria itoe.Lakini mimi kama mkristo nabaki nikijiuliza hivi:hivi ndugu yangu Samir anaufinyu wa akili mpaka aniletee hoja ya kitoto kama hii?!!….kama ni kweli ndugu Samir kwamba unatafuta ukweli, na kamwe sio mashindano yasiyo na tija,kwanini basi pia usimnukuu mtume paulo pale aliposema:BASI TORATI NI TAKATIFU,NA ILE AMRI NI TAKATIFU,NA YA HAKI NA NJEMA.Soma(warumi 7:12)…Halafu unadai kuwa hakuiita sheria ya mungu kuwa takatifu kama nilivyoiita mimi,sasa ulikuwa wataka umdanganye nani huko uliko ili uonekane wewe ni mkweli zaidi ya manabii wa mungu??!!..Hoja yako nyingine unasema hivi:PANAMADHARA MTATOZA UHAI KWA UHAI HAIMUHUSU BWANA YESU…UKAHOJI’ KWANI BWANA YESU KAMUUA NANI MPAKA NAE AUWAWE:Ndugu Samir nilinukuu(kutoka 21:23)….Sio kwa lengo la kubeba yale maelezo na kusema kwamba pale bwana yesu alikuwa anaongelewa yeye..LA HASHA!!…Bali nilikuwa nanukuu kanuni ya kisheria iliyoweza kutumiwa na mungu wetu katika kumtoa bwana yesu kuwa fidia ya haki mbele zake.Maana kama nisingenukuu kanuni ya kisheria iliyohalalisha jambo lile,basi ndugu yangu Samir,ungenihoji mambo mengi zaidi ya hili.Pengine ungehoji…kwanini mpaka afe ili kulipia fidia ya mungu?…na mimi ningekujibu kuwa kwa sababu kanuni ya kisheria ya mungu wetu alie mtakatifu ndivyo ilivyohitaji ili kufanya usawazo wa haki ya mungu.Na pia kama ulisoma zaidi mpaka chini basi ni vizuri maana umeona kanuni nyingi zaidi za kisheria ambazo cha ajabu waisilamu hawazifuati halafu wanasema eti ni zakimazingira!!!looh…kumbe kwa mujibu wa kuruani baadhi ya sheria za mungu ni ZAMAZINGIRA MAANA MAZINGIRA YAKIKATAA ALLAH ANAAMBIWA SUBIRI KIDOGO MPAKA YAKAE SAWA!!…HALAFU ETI TUNAAMBIWA NI MUNGU ALIYEMTAKATIFU HUYU.!!…Wanavyuoni huko uarabuni hakika mmelaaniwa nyinyi kwa kuibadili quran na kuwapoteza wateule wa mungu!!.Kuruani yenyewe sio neno la mungu maana,ilishabadili sheria za mungu wa kweli na kuzifanya kama za nchi fulani au kama za mwanadamu,alafu tena wanavyuoni wanazidi kutia ufundi wao kila kukicha…masikini waisilamu!!!.Allah kaleta sheria za kufuatwa zilizotakatifu kwa mujibu wa maelezo yake..halafu hapohapo anageuka na kusema kuwa,WASIOHUKUMU NI MADHALIMU!!…na atakae samehe ni KAFARA KWAKE!!!!!…kwa hali hiyo isiyoeleweka ni muislamu gani hapa duniani anaeweza kupona??…yaani haki na hukumu vimewekwa mikononi mwa watu ili waamue wenyewe na si mikononi mwa mungu wao..Mwisho wa hoja zako ni hii:UMEHOJI KUWA VIPI KUHUSU WAKINA EZEKIEL,ELIA,YEREMIA NA WATU WOTE WA ZAMANI KABLA YA BWANA YESU KUJA…WALIOKOKAJE NA JE,WATAENDA MOTONI?…Swali hili ni rahisi mno kujibu na kama ungekuwa makini kwenye hoja niliyokujibu huko juu kuhusu sadaka za wanyama na damu zilizotolewa katika torati ya musa ili kufanya upatanisho baina ya watu na mungu kwa wakati ule kwa ajili ya nafsi zao basi usingeniuliza tena swali hili.Soma(walawi 17:11).Kwa hiyo jibu ni rahisi tu,kwamba HAWAENDI MOTONI KWA SABABU KWA WAKATI WAO ULE,MUNGU ALIWAPA NJIA INAYOUNGANA SAWA NA NJIA YA BWANA YESU ILI SIKU YA MWISHO DUNIA YOTE IWE IMEFUATA KANUNI ZA MUNGU KWA NYAKATI ZAKE HUKU DAMU IKIWA NDIO MSINGI WA WATEULE WOTE WA MUNGU WAKIUNGANISHWA NA DAMU MOJA YA THAMANI YA BWANA YESU KATIKA KUFANYWA HAKI WOTE KWA PAMOJA….Lakini labda utahoji,kuwa….vipi kabla kabisa ya hata musa nae kuanza kazi hiyo,yaani watu wa mwanzo kabisa?….jibu:Kwanza tunawaona watoto wa Baba yetu adamu kule mwanzo kabisa wa biblia.Katika kumtolea mungu sadaka zao,biblia inatuonyesha kuwa,mungu aliikubali sadaka ya kuchinja ya wanyama aliyoleta Habil na hatimaye kumhesabia jambo hilo kuwa HAKI.Soma(mwanzo 4:4) na pia kwa uthibitisho zaidi tunasoma katika kitabu cha(waebrani,11:4) inayosema:KWA IMANI HABILI ALIMTOLEA MUNGU DHABIHU ILIYOBORA KULIKO KAINI,KWA HIYO ALISHUHUDIWA KUWA KUWA ANA HAKI,MUNGU AKAZISHUHUDIA SADAKA ZAKE NA KWA HIYO IJAPOKUWA AMEKUFA,ANGALI AKINENA…umeona sasa ndugu Samir,ni kwamba,biblia inasema’KWA SADAKA ILE YA WANYAMA IJAPOKUWA AMEKUFA ANGALI AKINENA!!…Hivyo kanuni ya kisheria ya mungu kutoa sadaka za wanyama ilianza tangu mwanzo,lakini tunaona kwa upande wa ndugu yake kain alibadili maagizo,akaamua amtolee Mungu mazao ya shambani,Mungu akamkatalia na kumwambia hukufanya sawa.soma(mwnzo4:3-7).Tunaona kuwa kizazi kilichofuata ni cha Nuhu,ambacho kilikuwa kikaidi kufuata kanuni na utaratibu wa mungu kama sasa hivi ndugu zetu waislamu wanavyomkataa bwana yesu na njia zake.Mungu wetu pasipo huruma wowote akaamua kuwaangamiza waovu wote.Soma(mwanzo 6:5-7).(mwanzo7:21-23).Tunaendelea kuona wajumbe wa mungu waliofuata,yaani wakina Ibrahimu ambao mungu aliwapa ishara zote za njia zake,nae Ibrahimu akaitwa rasmi kuwa baba wa imani..akamtangaza mungu na kumtumikia pamoja na nyumba yake,mtaa wake mpaka nchi yake yote.Baada ya hapo tunampata mwanae isaka aliyewazaa esau na yakobo…waliendelea vyema naye yakobo mwana wa isaka aliwazaa watoto 12 ambazo ni kabila za israel chimbuko la nabii musa aliyezaliwa utumani misri ambaye kwa mkono wake pale mlima sinai,ndiko alikokabidhiwa torati na mungu…naweza kuendelea hata ukitaka nikuelezee biblia yote,lakini kwa maelezo haya machache ndugu Samir,mimi naamini nimejibu hoja zako zote….NJOO KWA BWANA YESU.

    Like

    • Samir says:

      Umesema”Mtume paulo kamwe hamaanishi kama ndugu yangu Samir unavyotakaiwe,bali anamaanisha laana ya mtu anayoweza kuipata mtu kutoka kwenye sheria za mungu…yaani kama vile kusema:SHERIA ZA MUNGU NI LAANA KWETU TUKIZIASI”

      Kwa hiyo unamaanisha yoyote anayeziasi sheria za torati laana itamshukia, na ukasema
      hivyo ndivyo mtume wenu paulo alivyomaanisha!!si ndiyo eeeh!!?
      OK sasa nataka nione kama je ni kweli hizo sheria za torati mnazitekeleza au mpo chini
      ya laana.

      1.MAMBO YA WALAWI 15:16-18 “..naye nguruwe kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.Msile nayma yao,
      wala msiiguse mizoga yao hao ni najisi kwenu”

      je ni kweli hii sheria ya torati mnaitekeleza??? kama hamuitekelezi hii sheria ya torati
      moja kwa moja mtakuwa chini ya laana.

      2.MWANZO 17:10-14 “Mume wa kwenu atatahiriwa, mtatahiriwa nyama ya magovi yenu na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na nyinyi. mtoto wa siku nane atatahirwa kwenu; kila mwanamume katka vizazi vyenu mzaliwa nymbani na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni, asiyekuwa wa uzao asiyekuwa wa uzao wako, mzaliwa nymbani mwako na mnulnuliwa kwa fedha yako,lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu kuwa agano la milele. Na mwanaume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu”

      Hapa tunaona kila mzaliwa uzao wa Ibrahim(akiwemo Yesu na Musa), na wasio wa uzao wa ibrahimu(akiwemo mimi na wewe) Mungu anasema agano lake hili litakuwa la milele yaani mpaka mwisho wa dunia na asiyetahiriwa anapaswa kutengwa yaani yu najisi!

      Lakini ajabu kabisa Paulo anasema yeye injili yake ni kwa ajili ya watu wasiotahiriwa
      WAGALATIA 2:7 “bali kinyume cha hayo walipoona nimekabidhiwa injili ya wasiotahiriwa..”

      Sasa hapa lazima tujiulize Mungu anasema kila aliye wa uzao wa ibrahim na wasio wa uzao wake watahiriwe! Je hii injili ya Paulo kwa watu ambao Mungu wa kweli kasema watengwe yeye kapewa na nani injili hiyo kama si injili ya shetani anayeshindana na Mungu?
      Je huyu Paulo si katoka katika sheria za Mungu? je huku si kuzikataa sheria za Mungu?
      WAGALATIA 5:2 “Tazama mimi Paulo nawaambia mkitahiriwa Kristu hatawafaidia kitu neno”
      Mungu anasema ni agano la milele Paulo anasema si la milele na wala si kitu! Je hatuoni kuwa hii injili ya paulo ilitoka kwa shetani kwa sababu inapingana na sheria za Mungu wa kweli?
      Kazi kwako ewe mkiristo ndo hao manabii wa uongo aliowatabiri Yesu.

      Like

  44. mhina says:

    Ndugu.Samir:Wakristo,tumekombolewa kutoka kwenye HIZO LAANA ZA TORATI ULIZOZITAJA, ambapo katika yesu kristo,TUNA UKOMBOZI WA MSAMAHA WA DHAMBI.Bwana yesu alituambia:MIMI NIMEKUJA ILI WAWE NA UZIMA!!!.Soma(yohana 10:10).Bwana yesu alizaliwa chini ya sheria na akiwa muebrania kimwili,ilimlazimu aishi na kushika sheria zote za mungu kupitia torati ya Nabii Musa,ili kuyatimiza yale yote yaliyohitajika,akatuleta kwenye njia na neema ya Mungu’HAKI ITAKWENDA MBELE ZAKE NAYO ITAZIFANYA HATUA ZAKE KUWA NJIA.Soma(Zaburi 85:13).Kamwe wewe muislamu usijifananishe njia zako wewe na njia za mkristo!!.Hizo lawama ulizotoa zinakuhusu wewe….wewe ndugu Samir ndiyo unaehitajika KUKATWA GOVI LAKO kwa sababu mpo chini ya shinikizo la kufuata sheria za mungu kwa mwili,kwa kuwa mmekataa njia za mungu za wokovu alizotuletea bwana yesu…lakini mimi mkristo,tayari kupitia imani yangu kwa kazi aliyoifanya bwana yesu, Mungu ananipa haki ya kuhesabika kuwa nimetimiza sheria zake zote na maagizo yake yote.Kilichobaki kwa mkristo ni iman kwa bwana yesu na kufuata sheria za Mungu kwa roho ili tuwe waadilifu na wenye haki,tupokee wokovu wetu mbele za mungu’HAKIKA MTU MWOVU HATAKOSA ADHABU BALI WAZAO WA WENYE HAKI WATAOKOKA!!.Soma(mithali 11:21)….Hakika bwana yesu ndiye HAKI YETU.Ubarikiwe.

    Like

  45. Halima Juma says:

    jamani sory, ni mara yangu ya kwanza kuchangia ingawa huwa naifatilia blog hii.
    ,unajua mimi huwa nashangaa sana hawa wakiristu huwa wanashindwa kuelewa wanachokisimamia hasa pale wanapodai uwokovu unapatikana kwa damu ya Yesu kumwagwa msalabani;
    1.hivi kwa nini Yuda Iskariote aliitwa msaliti wakati wakiristu wote wanajua fika kuwa bila Yuda uwokovu wao usingepatikana?
    2. mimi ninavyojua usaliti ni kazi ya shetani na biblia inasema shetani alimuingia Yuda hivyo Yuda “akamsaliti” Yesu hivi ina maana hii kazi ya shetani ni njema na inastahili kupongezwa na kila mkiristu kwa sababu imepelekea kupatikana uwokovu wao.
    3. lakini pia huwa najiuliza ni kwa nini Yuda asiitwe mheshimiwa na wakiristu badala ya kumuita msaliti huku wakiendelea kufaidi matunda ya kazi yake?
    4.pia huwa najiuliza inakuwaje shetani aliyelaaniwa anakuwa chanzo cha uokovu wa wakiristu.
    5. Pia huwa sielewi kwa nini wakiristu wanauheshimu msalaba lakini wanambeza Yuda aliye chanzo cha Yesu kutundikwa msalabani!
    6. Huwa nafikiri kama Yuda ataendelea kuitwa msaliti na wakiristu basi waelewe pia msalaba ni lshara ya laana na usaliti na si ishara ya upendo kama wanavyodhani.

    SIJUI WENZANGU MNASEMAJE JUU YA HILO.

    Like

    • alfa says:

      alfa don killa baibe!we humpend huyo kiongoz wak,hujamuenz ipasavyo,niambie ulipokuwa na miaka sita uliolewa na ulipokuwa na miaka nane ukajua raha za dunia ndo ntaamini,nyie endeleen kufanya uasherat na miungu ya ulimwengu kama mji wa tito,kutwa kucha mnatoa sadaka za kuchinja mara udi kwa ajil ya miungu yenu(mapepo/majini)na ndiyo ulinz wenu,polen najua hamna hoja mpaka mnadokoa kanusu mstar lakn wapi,nawapenda sana na napenda nnavyowaonaga mkitapatapa kutafuta uhalali masikini,kwa musa hampo kwa yesu hampo wala roho c muhmad,poreeeeniii!!!hyo dini ya watu waliokataliwa,ishmail pundamwitu hatorith kamwe,hakuna ondoleo la dhamb pasip damu,mudy yupo hapo,au ye amewafundisha ushirikina tu manak!!!,anyway halma ucmaind ma sista we ar all tanzanian,cheka nijue hujamaind ukwel,kama huna yesu we utakuwa mshirikina na ndo mnaongoza wenyewe mnadai kawaida,eti majin wazur,mtafukizia uvumb wenu na kuyatolea sadaka za damu na fedha zenu sana tu hao ndio miungu wenu.

      Like

    • alfa says:

      nimefurah sana mpendwa,kwani ubaya uko wapi ndugu yangu mpendwa ktk bwana!mi nataka nione kama kweli unamuenz,nimezaliwa nigeria,bt unanielewa na ndo maana umenijibu,halafu mnaniachaga hoi kweli mitaani,ooo yesu alivaa kanzu tho yesu ni muislam,mbna hawasemi mafarisayo na masadukayo ni waislam kwamb nao wana kanzu,mi napata raha sana kuwaona watu wanaotapatapa kujitafutia uhalal!hollah it`z me don killa hapa,alfa the don,ngoja n2lie nsije nkawamwaga machoz,ingekuwa poa nimsalimie mdogo wangu huyo,mpe hi mwambie kaka ake anamsalimia one day atakuwa mtumish wa yesu huyo.blinblan!!!.sina chuk nimejaa upendo na furaha,mr yohana ujumbe umefka baabu!kaoe kabint ka six yearz ka kwel unamuenz kiongoz wak mnayehaha kumtafutia uhalali,halaf ktk nyumb ya bwana kuna design tofaut za wa2,dat y nipo alfa don killa na mliowazoea.sry ka nimekukwaza,ukwel bwana unaumiza sana ikiwa utapeleka bila ganzi.baiiii mpendwa ktk bwana!!!

      Like

  46. mhina says:

    ndugu samir+Abdallah na waislamu wote…nawashukuruni kwa hoja zenu zote…ndimewaandama vya kutosha mpaka naona mmeishiwa na hoja!!…mimi naishia hapa ili tuwape wengine nafasi ya kuchangia mawazo yao.Katafakarini sana yote huko juu alafu mfanye maamuzi ya busara kuokoa roho zenu…hoja mnazotoa sasa naona ni hoja za watu walioishiwa hoja nzito na zamaana.MBARIKIWE SANA SANA WOOOOTE.AKSANTENI.

    Like

    • ok! ahsante sn.
      nime-enjoy sana kupitia blog yenu, nimeondoa kasoro na mafundisho ya uongo mnayofundishwa na watauwa wa kikiristu huko makanisani kuhusu uislam.siku zote nimekuwa nikiitamani nafasi hii.
      al-hamdulillah, tnx to Allah!
      tchaoooo!!!

      Like

  47. Kim says:

    Uislam ndio dini ya kweli. inaruhusu kujiuwa na kuua kwa jina la Allah, ukifa kwa jina la Allah lazima uende peponi. ukristo ni dini ya uongo ndo mana tunawalipua ninyi na makanisa yenu, hatuwapendi.

    Like

    • Halima Juma says:

      Kim anavyosema sio kweli jamani kwa sababu mimi nimeipitia biblia sijaona palipoandikwa neno “UKIRISTO NI DINI” labda yeye ameliona jamani aniambie liko wapi
      sehem gani agano la kale au jipya?

      lakini nilipopitia Quran nikaona imeandika hivi SURA AL-MAIDA:3″ Leo hii nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini yenu”

      Like

  48. SAMUEL LAMILE says:

    GOD BLESS U

    Like

  49. ibrahim hassan says:

    Mr. Mhina, hii hoja ya majini, mimi sikuelewi inapokuchanganya, kwa sababu KUNDI MOJA LA MAJINI WALIPOSIKIA QURANI WALIAMINI ikiwa na maana kwamba kuna kundi jingine la majini ambalo bado halijaamini. Na katika sisi wanadamu, KUNA KUNDI MOJA LIMEAMINI QURANI, NA KUNA LINGINE BADO HALIJAAMINI. Sasa hoja yangu ni kwamba, kama wanadamu na majini walioamini qurani ni ndugu basi wale wanadamu na majini wasioamini qurani ni ndugu pia.
    Na hili la pili, ninao ushahidi uliokamilika:
    1Timotheo 1:20 ” Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.” Hivi ni kweli kwamba shetani anaweza kutumiwa katika kumfanya mtu anjue mungu? Jamani, shetani kazi yake ni kuntoa mtu katika njia iliyonyooka ya mungu.
    Udugu wa mashetani na wakristo bado unajionesha dhahiri kabisa kwenye biblia pale mungu wao alipopatana na ibilisi (hatujui kwa ujira gani walikubaliana) ili wanjaribu yesu. MATH 4:1

    ”1 Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. ” HAPA INANESHA KWAMBA MUNGU NA IBILISI WALIKUWA NA NIA MOJA YA KUNJARIBU YESU.

    1SAMWELI 16:14” Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.” Hapa tunaona shetani akitoka kwa mungu.

    Ayubu 1:6-” Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
    7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
    8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
    9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
    10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
    11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.”
    Hapa tunaona ukamilifu wa mungu wa biblia juu ya udugu wake na shetani.

    Petro1 3:19” ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;” Aya hii YESU ALIWAENDEA ROHO WALIOKAA KIFUNGONI, YAANI, MASHETANI, KUWAHUBIRI.

    Kwa mujibu wa kitabu chenu cha biblia, Yesu ni laana.
    Yeremia 22:24 Kama niishivyo mimi, asema Bwana, hata Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, angekuwa pete yenye muhuri katika mkono wangu wa kuume, ningekung’oa wewe hapo;
    25 nami nitakutia katika mikono ya watu wale wakutafutao roho yako, na katika mikono yao unaowaogopa, naam, katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya Wakaldayo.
    26 Nami nitakutupa nje, wewe na mama yako aliyekuzaa, mwende nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko.
    27 Lakini nchi ile ambayo wanatamani kuirudia, hawatairudia kamwe.
    28 Je! Mtu huyu, Konia, ni chombo kilichodharauliwa, na kuvunjika? Ni chombo kisichopendeza? Mbona wametupwa, yeye na wazao wake, na kutupwa katika nchi wasiyoijua?
    29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
    30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda. SASA HUYU KONIA AU YEKONIA NI NANI? BILA LA SHAKA NI MTIRIRIKO MZIMA WA UKOO WA YESU KRISTO KWA USHAHIDI WA MATH 1:11.
    Halafu na kitu kingine mungu wa biblia ni malaya, eeh! mungu wa namna hiyo ni bomu. Haya sio maneno yangu :
    Isaya 23-17 Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, Bwana ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia.
    MUNGU HUYU SIJUI WA KIUME AU WA KIKE NI BALAA!

    Like

  50. Beka j4 says:

    BIBLIA HAINA MAADILI.
    2timotheo 3:16 “kila andiko lenye pumzi ya mungu lafaa kwa mafundisho,na kwa kuwaonya watu makosa yao,na kwa kuwaongoza,na kwa kuwaadabisha katika haki ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”
    KWA MUJIBU WA AYA HIYO HAPO JUU SASA TUANGALIE HIZI AYA ZIFUATAZO:
    waamuzi 16:1 “Samson akaenda Gaza akaona huko mwanamke kahaba, akingia kwake”
    waamuzi 19:25 “lakini hao watu hawakukubali kumsikia; basi mtu huyo akamshika suria wake, na kumleta nje kwao; nao wakamjua, na kumtenda uovu usiku kucha hata asubuhi kisha kulipoanza kupambazuka wakamwacha aende zake.”
    2samweli 16:22 “Basi wakamtandikia Absalomu, Hema juu ya nyumba darini; naye Absalom akingia kwa masuria ya babaye(akabaka) machoni pa Israeli wote.”
    1samweli 18:27 “basi Daudi akainuka akaenda yeye na watu wake, akaua katika wafilisti watu mia mbili; na Daudi akazileta govi zao, wakampa mfalme hesabu kamili awe mkwewe mfalme”
    Ezekieli 4:11-12 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza”
    Mithali 31:6 “Mpe kileo yeye aliyekaribu na kupotea; kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini. Anywe akausahau umasikini wake; asiikumbuke tena taabu yake.”
    Ezekieli 4:15 “Ndipo Bwana akaniambia Taazama nimekupa mashonde(mavi) ya ng’ombe badala ya mashonde(mavi) ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo” Mashonde maana yake ni mavi au kinyesi.”
    Je kwa mujibu wa 2timotheo 3:16 naomba uniambie unapata mafundisho gani, au unapata mwongozo upi, au unapata onyo gani, au unajifunza adabu gani wewe MKIRISTU?
    inakuwaje mungu anaandika kitu ambacho ndani yake hakupatikani onyo wala funzo lolote kwa wa wasomaji?
    je mtu akiwa na shida apewe pombe ili asahau shida zake.Je haya ndo maadili ya Bwana mungu wa biblia?

    Like

  51. Amani Rashid says:

    ZIJUE KASORO NDANI YA BIBLIA
    1,je Yuda alikufaje?(a)(MATHAYO 27:5) “Alijinyonga”(b ).(MATENDO 1:18) “Alianguka kwa kasi akapasua matumbo”

    2.Yesu alipokuwa anapita Forodhani alimwona nani ameketi? (a)Lawi wa Alfayo (MARKO 2:14; LUKA 5:27) (b)Matayo (MATAYO 9:9)

    3.Tofauti na Yesu je kuna mwingine aliyepaa kwenda mbinguni? (a) (YOHANA3:13) Hapana(b) (2 WAFALME 2:11)Ndiyo Eliya alipaa kwa upepo wa kisulisuli.

    4.Je Yesu akijushuhudia mwenyewe ushahidi wake ni kweli? (a)(YOHANA 5:31)Si kweli. (b) (YOHANA 8:14)Ni kweli.

    5.Je Yuda alimbusu Yesu ili wamsulubishe? (a) (MATAYO 26:48-50)Ndiyo. (b)(YOHANA 18:3-12)Hapana hakumsogelea kabisa.

    6.Je Yesu alijichukulia msalaba wake mwenyewe mpaka Golgotha? (a) (YOHANA 19:17)Ndiyo. (b) (MATAYO 27:31-32)Hapana

    7.Je nani alimwambia Daudi akawahesabu Israeli?(a)(2 SAMWELI 24:1)Bwana (b) (1 M/NYAKATI 21:1)Shetani

    8..Wana wa Hashumu ni wangapi? (a) (EZRA 2:19)mia mbili ishirini na watatu. (b) (NEHEMIA7:22)Miatatu ishirini na wanane

    9.Ni lipi jina la mama yake mfalme Abiya(a) (2 M/NYAKATI 13:2)Maaka binti Urieli wa Gibea. (b) (2 M/NYAKATI 11:20)Maaka binti Absalomu.Lakini Absalomu alikuwa na binti mmoja tu naye ni Tamari(2 SAMWELI 14:27).

    10.je Simoni Petro alipataje kujua kuwa Yesu ndiye Kristu? (a) (MATAYO 16:17) Alifunuliwa na Baba kutoka mbinguni. (b) (YOHANA 1:40-41)Aliambiwa na ndugu yake Andrea

    Je Mungu anaweza kuwa msahaulifu kiasi hiki? hapana hii inaonesha hawa waandishi wa Biblia hawakutumwa na Mungu sbb angewatuma basi wasingetofautiana.Naomba mtafakari sana jamani.Ndugu wakiristu, kitabu pekee kisichokuwa na shaka ndani yake ni QURAN TUKUFU.
    Tafuteni ukweli mkiwa na mawazo huru Allah atawajaalia mtaupata inshaallah!

    Like

  52. umm suleym says:

    BUSARA IKO WAPI NDANI YA BIBLIA?
    HII NI STORI NDANI YA BIBLIA INAWAHUSU WANAWAKE WAWILI OHOLA NA HOLIBA.
    Ezekieli 23:5″ Na Ohola alifanya mambo ya kikahaba alipenda mno wapenzi wake, Waashuri jirani zake”

    Ezekieli 23:7 “Akawagawia mambo yake ya kikahaba watu wateule wa Ashuru, wote pia; akajitia unajisi kwa vinyago vyote vya kila mmoja wa hao aliowapenda, wala hakuyaacha mambo yake ya kikahaba,tangu siku za Misri, kwa maana wakati wa ujana wake walilala naye,WAKAYABANA MATITI YA UBIKIRA WAKE, wakamwaga uzinzi wao juu yake.”

    Ezekieli 23:10 “Na hawa wakaufunua uchi wake, wakatwaa wanawe na binti zake wakamwua yeye kwa upanga;”

    SASA SOMA UONE YALIYOMPATA MWANAMKE OHOLIBA UMBU LAKE OHOLA
    Ezekieli 23:17 “Na watu wa Babeli wakamwendea katika kitanda cha mapenzi, wakamtia unajisi kwa uzinzi wao”

    Ezekieli 23:18 “Basi alifunua uziznzi wake na KUFUNUA UCHI wake ndipo roho yangu ikafarakana naye kama ilivyofarakana na umbu lake.”

    Ezekieli 23:20 “Akawapendelea wapenzi wao, ambao nyama ya mwili wao ni kama nyama ya mwili wa punda, nacho kiwatokacho ni kama kiwatokacho farasi , ndivyo ulivyokumbuka uasherati wa ujana wako ulipobanwa matiti yako na Wamisri,kwa maziwa ya ujana wako.”

    Ezekieli 23:41-42 ” ukaketi ju ya kitanda cha enzi na (ukaweka)meza imeandikwa TAYARI mbele yake, ambayo juu yake uliweka uvumba wangu na mafuta yangu na sauti za wingi wa watu wenye hali raha zilikuwa pamoja naye; na pamoja na watu wasio na adabu, waliletwa walevi toka jangwani; wakatia vikuku mikononi na taji nzuri juu ya vichwa vyao.”

    SASA SIKIA MAAGIZO YA MUNGU WA BIBLIA JUU YA MWANAMKE MKONGWE(OHOLIBA) ALIYEKUWA MZINIFU KATIKA UJANA WAKE.
    Ezekieli 23:43″Ndipo (mimi mungu)nikasema, Huyo aliye mkongwe atafanya uzinzi!sasa hao watazini naye, naam, na yeye!.”

    Ezekieli 23:44 “Wakamwingilia kama watu wamwingiliavyo kahaba; ndivyo walivyowaingilia Ohola na Oholiba wanawake wale waasherati.”

    ………………………………………………………………………………………………………………………………
    Jamani ndugu wakiristu hiyo ni biblia yenu wenyewe, ndiyo biblia ya mungu mwenye neema na huruma; Je,Hayo ndiyo maneno ambayo mungu wenu anayatumia wakati anapotaka kuonesha jinsi gani hapendi uzinifu?Hapana hayo kwa kweli siamini kama ni maneno ya Mungu wa kweli, Mungu mwingi wa busara, naamini kabisa ni maneno ya waandishi wa biblia ambao wanajaribu kumchafua Mungu kwa kuandika mambo kwa matamanio ya nafsi yao wala Mungu hakuwatuma.Ki ukweli ni maneno ambayo baba hawezi kuyasoma mbele ya binti yake aliyebalehe, au mama akayasoma mbele ya wanawe waliobalehe. Sisi waislamu hatuamini kama Mungu ndiye aliwatuma hao waandishi wa Biblia, bali walijituma kwa nafsi zao wenyewe.Tunaamini Mungu hawezi kukosa stara kiasi hiki.

    sasa angalia M/Mungu anavyoeleza mambo kwa busara kabisa ndani ya Quran
    sura 17:32. “Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya.”

    ameeleza kwa kifupi na kwa namna inayoeleweka, Huyo ndiye Mungu wa kweli.Ni maneno unayoweza kuyasoma popote na mbele ya yeyote.
    Hakika Allah ndiye pekee ataweza kuwaonesha mwanga mkaufata, mimi ni mfikishaji tu.M/Mungu ameepukana na upungufu.

    Like

    • KELVIN says:

      JE KUFUNGA MWEZI WA RAMADHANI KWA KUUTANGAZA HADHARANI NA KUUANGALIA MWEZI UNAPOANDAMA PAMOJA NA KULA FTARI AU DAKU NI SAHIHI? SOMA BIBLA EZEKIEL7:4-7, MATHAYO 6:16-20,, TORATI 4:19.PIA ULICHO ANDIKA SI SAWA NIME KUJIBU HAPA HUWEZI KUFAHAMU NENO LA MUMGU MPAK UWE NA ROHO WAKE MTAKATIFU KWA SABABU MUNGU WAKO WATATU WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 5:8 WAKORINTHO WA KWANZA 2:9-12, WAKORINTHO WA KWANZA 12:3 OKOKA NAKULETE MENGINE ZAIDI AU SOMA COMMENTS ZANGU.MARKO 1616-20, WAKORINTHO WA KWANZA 6:1-2

      Like

  53. Abdul Majid says:

    Assalaam aleykum,
    ZITAMBUE KASORO NA TOFAUTI KUBWA KABISA NDANI YA BIBLIA YAKO.
    1.Je Yesu alistahili kurithi kiti cha enzi cha Daudi? (a) (LUKA 1:32)Ndiyo, malaika alimfunulia Mariamu. (b) Hakustahili,kwa sababu Yesu ni katika kizazi cha Yehoyakimu,angalia ( MATAYO 1:11,1 M/NYAKATI 3:16) Na Yehoyakimu alilaaniwa na Bwana kuwa hatakuwa na mtu wa kukaa katika kiti cha enzi cha Daudi (YEREMIA 36:30).Mhh!!Ajabu ya mungu wa Biblia hii.

    2.Ni nani alikuwa mtoto wa Zerubabeli katika kizazi cha Yesu?(a) (MATAYO 1:13)Abihudi. (b) (LUKA 3:27)Resa. Lakini majina ya watoto saba wa Zerubabeli ni haya hapa: i. Meshulamu, ii. Hanania, iii.Shelomithi, iv. Hashuba, v. Oheli, vi. Berekia, vii. Hasadia, viii. Yushabhesedi (1 M/NYAKATI 3:19-20). Ajabu,majina ya Abihudi na Resa hayamo kwenye list.

    3.Ni nani mwanafunzi wa kumi wa Yesu? (a)( MARKO 3:13-16) Thadayo;Yuda wa Yakobo hayupo kwenye list. (b)( LUKA 6:12-16) Yuda wa Yakobo; Thadayo hayupo kwenye list.

    4.Ni Nani alimuua Goliati? (a) (1 Samuel 17:23, 50)Daudi (b) (2 Samuel 21:19)Elihanani

    5.Je Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake?(a) (MWANZO 1:26)Ndiyo;(b)(ISAYA 40:18,25)Hapana, Mungu hafananishwi na chochote.(c)(ZABURI 89:6) Hapana.

    6.Wana wa Adini walikuwa wangapi?(a) (EZRA 2:15)Mia nne hamsini na wanne;454. (b) (NEHEMIA 7:20)Mia sita hamsini na watano;655.

    7.Nani alikuwa Baba yake Yusuf mume wa Mariamu mama wa Yesu? (a) (MATHAYO 1:16)Yakobo. (b) (LUKA 3:23)Eli.

    8.(a)(MITHALI 21:18)”Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki”; (b)Lakini ajabu! Yesu alikuwa mwenye haki,soma (MATAYO 27:19) na (MAT 27:24) (c)lakini ukisoma (MARKO 10:45)”Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

    9.Je Mungu alisema mwanadamu ataishi kwa muda wa miaka mingapi? (a)(MWANZO 6:3) Ndiyo, miaka mia na ishirini (b)(MWANZO 9:29)Hapana, Nuhu aliishi miaka mia kenda na hamsini(950).

    10. Je mtini alioulaani Yesu ulinyauka pale-pale? (a) (MATAYO 21:19)Ndiyo, ulinyauka mara. (b) Hapana aliulaani(Mark 11:14)ulinyauka usiku kucha mpaka asubuhi(MARKO 11:19-20).

    11..Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu walioachwa huru ni wangapi? (a) (EZRA 2:6)elfu mbili na mia nane kumi na wawili;2812. (b) (NEHEMIA 7:11)elfu mbili na mia nane kumi na wanane;2818.

    Baada ya kuwa tumeziona kasoro kubwa kabisa ndani ya Bibilia na kutofautiana kusiko kwa kawaida sasa tusome alichokisema Luka mmoja wa waandishi wakubwa kabisa wa Biblia kuhusu uandishi wake katika;

    Luka 1:1-3.”Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa kati yetu,kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo, nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu, Theofilo mtukufu.”

    Hapa tunajifunza mambo yafuatayo;
    i.Luka mwenyewe anakiri kuwa watu wengi wametia mikono yao na kutunga kwa taratibu kwa kadiri walivyosikia wala si kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu kama Wakiristu wanavyodai.

    ii.Luka anakiri kuwa yeye mwenyewe hakuwa shahidi aliyeshuhudia kwa macho yake na maelezo aliyoyakusanya yalitokana na mashahidi walioshuhudia kwa macho na si kuwa alifunuliwa na Roho Mtakatifu kama wakiristu wengi wanavyoaminishwa na viongozi wao.

    iii.Hakuandika, ili kiwe kitabu cha dini kama kinavyotumika sasa bali alimuandikia mfalme Theofilo mtukufu ili asome aburudike na ajue mambo yalivyokuwa zamani.

    -Je ewe Ndugu Mkiristu bado unaendelea kuamini kuwa Biblia ni neno la Mungu?
    -Je inayumkinikaje liwe neno la Mungu ambalo halikutoka kwa Mungu(si ufunuo) bali ni kwa kutunga na kusikia tu kwa watu? Tafakari bado unayo nafasi!
    -Isomeni Biblia lakini pia isomeni Quran ambayo haina kasoro ndani yake inshaallah mtapata mwanga!Allah anatuambia Quran imenyooka sawasawa haina kasoro (sura 17:1-2).

    Like

  54. Islam is a post-Christianity religion, found by Mohammad (s.a.w) , the prophet of Islam, in 610 A.D. It claims syncretism with other religions especially Jewish and Christianity which Muslims all over the world still propagate the same claims until today. But in the contrary, when they are asked inquisitive questions about their religion and belief, most of them become either furious or seem to know nothing about their religion and their destiny. Further worse, some can tell lies. Because their Prophet Mohammad (s.a.w) has been recorded in authentic Islamic tradition books, teaching Muslims to tell lies in defending their religion and faith before non- Muslims . It’s a problem!. So far, about 150 questions from the Islamic World which range from spiritual, social, economical and political, posed to Christianity have been, so far, clearly answered. Contrary to this, about 160 questions from the Christian World posed to the Islamic World, only one question has been, clearly, answered and that answer is: True, Muhammad ibn Abdullah ibn Abu Muttalib, was a real person who lived in Mecca, and died in Medina in 632 A.D. The rest questions, the Muslims World have no answers to them, because their religion is not only myth but also is full of fabricated stories of the ancient people. Do you know why? Visit here always………

    Like

  55. Abdul Majid says:

    Am very sorry 4u bt am not suprised, It is now obvious that when christians fail to defend their religious doctrines and teachings against muslims strong opposing points, they always panic and become anxiety, they r used 2 lose their temper. U know why !!! Christianity is made up of fabrication stories which contradicts one after another, Here I have more than 110 clear contradictions of which no true christian Priest or cleric can dare to come up with clear and satisifying answers to them. Thats why thousands and thousands of Intellectual christians in
    Europe and America are embracing Islam on daily basis.

    I am from now, ready to post those contradictions of the bible although some of them we have been posting and yet no any christian has managed to come up with answers for them and I am sure nobody will dare even to make a clear tackle of even a single contradictions out of twenty bible contradictions which we posted.come on what are u waiting it is about a month now ever since we made them appear 2u.mmmhhh! let shame be on u *1000,as u failed to bring the solution to the critical and serious contradictions facing what u believe 2be ur holy book.

    Once again ur proving ur failure by copying and pasting an article which was wrote by a white drunkered stupid man who know nothing about Islam and our holy Allah’s apostle Muhammad(S.A.W), mmh u are totally going astray my little kid.
    1.which authentic hadith which shows our holy Prophet is teaching us to tell lies?
    2.put here all those 160 questions and they will be clearly answered
    3.write down ur reply to strong 20 contradictions of the bible which we uploaded about one month ago.
    finaly say helo, 2 your fellow stupid to whom u copied that article.
    1.

    Like

  56. mhina says:

    Mr.Abdul Majid, u said: No any christian has managed to come up with answers (your 20 bible contraditions).Are you sure?..Mimi nitakujibu zote hizo kwa kiswahili ili tuwafaidishe watu wengi zaidi waweze kuona jinsi dini ya kiislamu na wafuasi wake walivyokuwa waongo.Nianze na Amani Rashid…..(1)JE,YUDA ALIKUFAJE? (a)(mathayo 27:5)alijinyonga (b) (matendo 1:18) alianguka kasi akapasuka matumbo….jibu: hiyo (mathayo27:5) inaelezea kifo cha yuda kuwa ‘ALIJINYONGA’ na hiyo (matendo 1:18) inamuelezea jinsi yuda ‘ALIVYOJINYONGA AU ALIVYOJIUA…Hapa inaonyesha wazi kuwa alijitupa mahali parefu na kupasuka,ndiyomaana maandiko yanasema:AKAANGUKA KWA KASI NA KUPASUKA MATUMBO YAKE YAKATOKA.Kinachotufurahisha ni kwamba waandishi wote hao kwa kuongozwa na roho mtakatifu wameandika ujumbe unaokubaliana kwamba, ni kweli kuwa yuda alikufa kwa kifo cha KUJIHARIBU YEYE MWEYEWE.Sasa tatizo liko wapi?!!……(2) YESU ALIPOKUWA ANAPITA FORODHANI ALIMUONA NANI AMEKETI? (a) lawi wa Alfayo (marko 2:14)( luka 5:27) (b) mathayo (mathayo 9:9)…….jibu:jibu la swali hili ni rahisi tu,kwa sababu, mathayo pia aliitwa lawi wa Alfayo,hili ni jina lake la pili kama lakikabila akiitwa lawi mtoza ushuru..au mathayo mtoza ushuru maana alikuwa mtoza ushuru.TATIZO LAKO LIKO WAPI NDUGU?!!……..(3) TOFAUTI NA YESU,JE, KUNA MWINGINE ALIYEPAA KWENDA MBINGUNI? (a)(yohana 3:13)hapana (b) (2falme 2:11) ndiyo, Eliya alipaa kwa upepo wa kisulisuli……jibu: kama ulivyojijibu wewe mwenyewe kwenye swali lako kwamba, Elia hakupaa mwenyewe kama alivyopaa bwana yesu bali yeye alikwenda mbinguni kwa msaada wa FARASI,GARI LA MOTO NA UPEPO WA KISULISULI ALIOLETEWA NA MALAIKA WA MUNGU….ni safari mbili tofauti kwa kuwa sio kweli kwamba kunguru anaeruka angani mwenyewe ujifananishe nae wewe ulioruka angani na parachuti!!..KAJIFUNZE KISWAHILI VIZURI NDIO UTULETEE HOJA ZAKO………(4)JE,BWANA YESU AKIJISHUHUDIA MWENYEWE USHUHUDA WAKE NI KWELI? (a) (Yohana 5:31) Si kweli (b) Yohana 8:14) Kweli………jibu: Ushuhuda wa bwana yesu anapojishuhudia mwenyewe ni kweli kwetu sisi tunaomuamini pamoja na mungu mwenyewe alie mtuma kwa kuwa sisi tunajua atokako na aendako…lakini ushuhuda huohuo akijishuhudia mwenyewe kwa watu wasiomuamini(km.waislamu) unakua sio kweli kwa kuwa watu hao(waislamu) hawamuelewi wala kuikubali ile kweli yake…’KWA SABABU NENO LA MSALABA KWAO WANAOPOTEA NI UPUUZI,BALI KWETU SISI TUNAOOKOLEWA NI NGUVU YA MUNGU.Soma(1wakorintho 1:18)…….(5) JE,YUDA ALIMBUSU BWANA YESU ILI WAMSULUBISHE? (a) (mathayo 26:48-50) ndiyo (b) (yohana 18:3-12) hapana hakumsogelea kabisa…….jibu:Kwanza nasikitika kwa kuwa najibu swali la uongo!!…hakuna jibu la yohana kwenye hiyo (yohana 18:3-12) lililosema’HAPANA HAKUMSOGELEA KABISA’…Pia uelewe kuwa dhumuni la roho mtakatifu ni kutuonyesha jinsi Yuda alivyomsaliti bwana yesu ili asulubiwe,tena chakufurahisha ni kwamba waandishi wote wameripoti ukweli wa tukio hilo…kwa hiyo mambo ya kubusiana na kukonyezana sio yamsingi sana kwetu kwa kuwa hata wangefanya hivyo wote katika ripoti zao kusingeongezeka kitu kwetu…mimi huwa najiuliza kwamba,hivi ingekuwa ni quran ndiyo twaichunguza na kuikosoa hivi,si tungekuwa tumekwisha ichanachana mapema tu……..(6) JE,YESU ALIJICHUKULIA MSALABA WAKE MWENYEWE MPAKA GOLGOTHA? (a) (yohana 19:17) ndiyo (b) (mathayo 27:31-32) hapana……jibu:bwana yesu iwe alisaidiwa au hakusaidiwa ujumbe wa kuelekea golgotha kwa ajili ya kusulubiwa umeonyeshwa na mitume wote kwa usahihi, na hii ndiyo iliyokuwa kazi ya roho mtakatifu….sasa kama lapa lake lilikatika njiani au watu walimcheka hayo sisi wakristo hayatukoseshi kile mungu wetu alichotukusudia.Hoja zako ni zakitoto mno!! Lakini kwa kuwa ni kazi ya mungu mimi nitaendelea kukujibu vyote……..(7) JE, NANI ALIMWAMBIA DAUDI AKAWAHESABU ISRAEL? (a) (2Samweli 24:1)) Bwana (b) (1Nyakati 21:1) Shetani……….jibu:Mungu ndiye aliyemwambia Daudi akawahesabu ISRAEL NA YUDA(sio israel pekee).Lakini tunaona katika ile(1nyakati 21:1) Shetani anamkengeusha Daudi na kubadili maagizo ya mungu kwa KUMSHAWISHI Daudi ili awahesabu ISRAEL PEKEE!!….Hapo tunaona jinsi shetani alivyokuwa mjanja wa kubadili maagizo sahihi ya mungu ili awapoteye wengi…lakini haya ni maagizo mawili tofauti,andiko la saweli likiwa ni agizo la mungu wakati andiko la nyakati likiwa kweli la shetani kumkengeusha Daudi mtumishi wa mungu,Sasa kama wewe ulifikiri biblia ilijichanganya ili umlaumu roho mtakatifu kama kawaida yako…BASI IMEKULA KWAKO!!……….(8) WANA WA HASHUMU NI WANGAPI? (a) (ezra 2:19)223 (b) (Nehemia 7:22) 328…………jibu:Kwa kawaida idadi ya watu huongezeka na kupungua kutokana na vifo na kuzaliana.Kwa hiyo ingekuwa jambo la ajabu kweli ya kwamba,idadi ya wana wa Hashumu wakati wa Ezra ibakie ileile mpaka kipindi cha Nehemia,wakati watu wa zamani walikuwa wakizaana mno!!.Pia huwezi kutafuta usahihi wa jambo la kiroho kama hili kwa kuchunguza mpaka idadi za watu kiasi hicho!! HIYO NI DALILI YA WAZI YA KUSHINDWA……..,…(9) NI LIPI JINA LA MAMA YAKE MFALME ABIYA? (a) (2nyakati 13:2) Maaka binti uriel wa gibea (b) (2nyakati 11:20) maaka binti Absalom lakini Absalom alikuwa na binti mmoja aliyeitwa Tamara (2 Samweli 14:27)…………jibu:Swali hili sikulielewa vizuri ulichotaka….kama ni la muhimu sana kwako utanitumia kwa utaratibu unaoeleweka.Naona kama umelijibu wewe mwenyewe ulieuliza……,…..(10) Simoni petro alipataje kujua kuwa yesu ndiye kristo? (a) (mathayo 16:17) Alifunuliwa na baba kutoka mbinguni (b) (yohana 1:40-41) Aliambiwa na ndugu yake Andrea……jibu:Hakuna tatizo lolote la kimaandiko hapo kwa kuwa mathayo alitoa jibu la kiroho lililotekelezwa kimwili na Andre, wakati wakati Yohana alitoa jibu la kimwili lililopangwa na Mungu kabla ya kutekelezwa.Hapo kwa sisi wakristo tunaelewa vyema jambo hilo na kusema MAANDIKO YAMETIMIA KWA MWILI NA ROHO….Maana katika imani yetu tunajua kuwa,Mwenyezi Mungu ndiye anaeanza kutuongoza kiroho halafu uhalisia wa kimwili wa tukio hufuata…..NAAMINI KUWA NIMEMALIZA KUMJIBU NDUGU AMANI RASHID.KESHO NITAKUMALIZIA NA WEWE NDUGU ABDUL MAJID….HALAFU NITAWAOMBA NAMIMI NIWAULIZE NYIE NA WAISLAMU WOTE DUNIANI MASWALI YANGU MATANO TU.Mbarikiwe.

    Like

  57. mhina says:

    MR.Abdul Majid….Hongera sana kwa kazi yako ya kumsingizia mungu mambo ya uongo.Umehoji vitu vifuatavyo…….(1) JE,YESU ALISTAHILI KURITHI KITI CHA ENZI CHA DAUDI? (a)alistahili (luka 1:32) (b) hakustahili kwa sababu anatoka kizazi kilicholaaniwa na Mungu (1nyakati 3:16)………….jibu: Kama ulivyojijibu wewe mwenyewe kwenye hiyo(luka 1:32) Hilo ndugu Abdul ndilo jibu la swali lako.Maandiko hayo yanasema,’HUYO ATAKUWA MKUU,ATAITWA MWANA WA ALIE JUU,NA BWANA MUNGU ATAMPA KITI CHA ENZI CHA DAUDI BABA YAKE…..Tumeona hapo, maneno ya malaika wa mungu akithibitisha kuwa bwana yesu kwa asili yake ni ya kiroho akiwa mwana wa mungu asie na dhambi yaani yeye ni MTAKATIFU KABISA KAMA ALIVYO MUNGU MWENYEWE….Tena Mungu anamwambia Mariamu kuwa atamrithisha bwana yesu kiti cha enzi cha daudi!!….Tatizo lako ndugu Abdul ni nini?.Bwana yesu alizaliwa kwa njia ya bikira ili aziepuke laana hizo na aweze kukomboa israel kutoka kwenye hizo laana za wakina yehoyekimu na hatimae aukomboe ulimwengu mzima kutokana na madhambi yetu na kutupatanisha na Mungu.Soma(mathayo 10:5-7) linganisha na(mathayo 28:19)………(2) NI NANI ALIKUWA MTOTO WA ZERUBABELI KATIKA KIZAZI CHA YESU? (a) (mathayo 1:13) Abihadi (b) (luka 3:27) Resa,LAKINI MAJINA YA WATOTO SABA WA ZERUBABELL NI HAYA(1nyakati 3:19-20) AJABU MAJINA YA ABIHUDI NA RESA HAYAPO KTK LIST……….jibu: Hili ndilo giza la macho walilokuwa nalo waislamu wengi kwa sababu,Zerubabeli huyo ulie mnukuu kwenye (mathayo 1:13) ni mwana wa SHELTIEL ona kwenye(ezra 3:2) wakati Zerubabeli uliyemnukuu kwenye ile(1nyakati 3:19-20) ni mwana wa PEDEYA,ona kwenye hiyohiyo(1 nyakati 3:19-20).Ijapokuwa majina yanafanana lakini ni koo tafauti kabisa!!!……….(3) NI NANI MWANAFUNZI WA KUMI WA BWANA YESU? (a) (marko 3:13-16) thadayo yuda wa yakobo (b) (luka 6:12-16) yuda wa yakobo, lakini wote hawapo katika list.ya wanafunzi wa yesu….,.jibu: Thadayo ndiye yuda wa yakobo,soma pia(luka 6:16)….Nae Yuda msaliti wa bwana yesu,nafasi yake ilichukuliwa na Mathiya,soma kwa makini(matendo 1:20-26).Sio wanafunzi hao tu, kwamba ndio waliokuwa wanafunzi wa bwana yesu, bali yeye aliendelea kuteua wengine wengi kwa nyakati tofauti.Biblia inasema: ‘AKATEUWA WENGINE SABINI’.Soma(luka 10:1)………..(4) NI NANI ALIMUUA GOLIATI? (a) (1 Samwel 17:23-50) Daudi (b) (2 Samwel 21:19) Elihanan……….jibu: Goliati maana yake ni MAJITU.Zamani kulikuwa na majitu makubwa mno.Daudi mtumishi wa mungu aliongoza jeshi lake kupambana na majitu au magoliati hayo.Goliati lililouliwa na Elihanani liliitwa MGITI. Soma(2 Samwel 21:19) Wakati Goliati au Jitu lililouliwa na Daudi lilikuwa ni mfilist mwenye vidole sita aliekuwa goliati mkubwa kuliko wote.Soma(1samwel 17:49-51).Acha kumsingizia roho mtakatifu mambo ya uongo asije akakuhukumu siku ya mwisho…………(5) JE,MUNGU ALIMUUMBA MWANADAMU KWA MFANO WAKE? (a) (mwanzo 1:26)ndiyo. (b) isaya 40:18-25) hapana mungu hafananishwi na chochote. (c) (zaburi 89:6) hapana………..jibu: kilichonishangaza na kunisikitisha ndugu Abdul katika swali hili ni kwamba umeamua kutumia mpaka nukuu za kuruan ili kushawishi wateule wa mungu wakuamini unachoandika!!.Neno ‘HAPANA MUNGU HAFANANISHWI NA CHOCHOTE’…Umelitoa kwenye msaafu ndugu!!!..Inasikitishakwelikweli, lakini nikujibu kuwa,Mungu alituumba kwa mfano wake katika hali za rohoni na kamwe sio kimwili kwa kuwa mungu ni roho….ndiyomaana biblia inasema……’AKAMPULIZIA PUMZI YA UHAI’.Soma'(mwanzo 1:26).Pia yale maandiko mengine uliyo nukuu yanaongelea mambo ya mamlaka ya kimwili kuwa mungu ndiye mwenye nguvu zote hodari asiefanana na yeyote.soma(zaburi 89:8)………….(6) WANA WA ADINI WALIKUWA WANGAPI? (a) (ezra 2:15) 454 (b) (Nehemia 7:20) 655………jibu: masuala yanayohusu idadi za watu hutofautiana kutokana na vifo pamoja na kuzaliana kwa watu.Tangu kipindi cha Ezra mpaka Nehemia kama tungepewa idadi moja ya watu inayofanana,basi hilo ndilo haswa lingekuwa ni tatizo la msingi sana la kuhoji waandishi..,……..(7) NANI ALIKUWA BABA YAKE YUSUFU MUME WA MARIAMU MAMA WA YESU? (a) mathayo 1:16) Yakobo (b) (luka 3:23) Eli…………jibu:Hebu angalia wewe mwenyewe ile(luka 3:23) inasema: ‘AKIDHANIWA’…Je,kitu kilichozaniwa na watu katika simulizi ile ya luka kinaweza kuwa ni sahihi na jibu la kweli la (mathayo 1:16) aliyetoa jibu la moja kwa moja kuwa ni Yakobo?….lazima ufahamu kuwa, pale luka hakutoa jibu yeye kama mtume wa mungu bali alikuwa anatoa simulizi za watu wanavyodhania jambo lile.Kwa hiyo jibu ni Yakobo ndiye aliyekuwa baba wa Yusufu………….(8) (mithali 21:18) ‘MTU ASIE HAKI NI FIDIA YA WENYE HAKI’ LAKINI AJABU BWANA YESU ALIKUWA MWENYE HAKI,Soma(mathayo 27:19) HALAFU AKASULUBIWA ILI AWE FIDIA YA WENGI,Soma(marko 10:45)………..jibu: Injili ni habari inayotangaza upendo wa mungu kwetu sisi wanadamu.Injili ni KUJITOA KWA AJILI YA WENGINE SIO KUTUMIKIWA.Mungu kwa upendo wake hakutaka sisi tujiokoe wenyewe kutoka kwenye makucha yake makali ya sheria zake kwa kuwa alikwisha jua kwamba kamwe hatutaweza kujiadhibu wenyewe kwa haki.Soma(zaburi 49:7-8).Yeye kwa upendo wake mkuu na waajabu alimleta bwana yesu ili awe fidia ya wengi.Kwa hiyo tunaona kuwa ukali wa mungu katika sheria zake,umedhihirishwa pia na upendo wake mwingi mno!!…ndiyo maana pia katika ile(mathayo 20:28) Bwana yesu tunamuona pamoja na heshima na ukuu wake wote,anaamua kudhihilisha tabia hiyo ya asili ya mungu kwa kusema’KAMA VILE MWANA WA ADAMU ASIVYOKUJA KUTUMIKIWA,BALI KUTUMIKA NA KUTOA NAFSI YAKE IWE FIDIA YA WENGI.Ndio maana utimilifu wa sheria ni upendo mkuu wa mungu kwa kutumikiana kila mtu na jirani yake.(luka 22:26-29)…na bwana yesu ndiye muanzilishi wetu wa tabia hiyo ya kiungu.Yeye ametusisitiza hivi: ‘MPENDANE KAMA MIMI NILIVYOWAPENDA………(9) JE,MUNGU ALISEMA MWANADAMU ATAISHI KWA MUDA WA MIAKA MINGAPI? (a) (mwanzo 6:3) Miaka 120 (b) (mwanzo 9:29) Nuhu aliishi miaka 950…………jibu: Pamoja na mungu kusema hivyo lakini bado kwa upendo wake mkuu na waajabu,akatuagiza hivi: ‘WAHESHIMU BABA YAKO NA MAMA YAKO ILI SIKU ZAKO ZA KUISHI ZIPATE KUWA NYINGI’.Soma(kumbuk 5:16).Mungu, pamoja na ukali wake wa maneno yake yaliyo matakatifu yasiyopaswa kugeuka ovyo na kumrudia yeyemwenyewe,huwa anatuwekea na njia ya kutokea katika maneno yake.Hivyo, pamoja na maneno yale ya mungu katika (mwanzo 6:3) bado wanadamu hufa mapema au huishi zaidi kufuatana na utii wa mtu katika neno lile la mungu la maisha kwa watu wote hata wapagani.Kibiblia wazazi ni sehemu ya mamlaka ya mungu.Biblia iko wazi mno, yatufundisha kuwa ‘KICHWA CHA MWANAMKE NI MWANAUME NA KICHWA CHA MWANAUME NI BWANA YESU NA KICHWA CHA BWANA YESU NI MUNGU MWENYEWE.Soma(1wakorinth11:3)………….,…..(10) JE,MTI ALIOULAANI BWANA YESU ULINYAUKA PALEPALE? (a)(mathayo 21:19) ndiyo (b) (marko 11:14) aliulaani (c) (marko 11:19-20) ulinyauka usiku kucha mpaka asubuhi……..jibu: Sasa…kama bwana yesu aliulaani mti fulani,ukanyauka palepale,naamini kuwa watakao kuja usiku watatoa ushuhuda wa usiku, Watakaokuja hasubui watatoa ushuhuda wa hasubuhi, lakini chamsingi ni kujua kuwa kweli bwana yesu aliulaani mti ule….ndivyo mitume wote hao,wakiongozwa na roho mtakatifu wameripoti ukweli huo…….mwisho ni ile (luka1:1-3)…….Luka aliyekuwa msomi wa fani ya udactari,alikuwa ni mmoja wa wanafunzi wa bwana yesu aliyeshuhudia mwenyewe mambo yote ya bwana yesu na kujia ukweli wote jinsi ulivyotokea.Yeye alipoona kila mtu anaropoka kuhusu mambo yale ya bwana yesu na kutaka kuandika bila ya utaratibu….ndipo yeye mwenyewe akaamua kujitoa kwa kuandika mambo yale aliyohubiri bwana yesu kwa mpangilio ulio sahihi.Luka analithibitisha hili kwa kusema: ‘KWAKUWA WATU WENGI WAMETIA MIKONO KUTUNGA KWA UTARATIBU HABARI ZA MAMBO YALE YALIYOTIMIZWA KATIKATI YETU’.Soma(luka 1:1)….kwa hiyo,luka kwa simulizi zile za vipande vipande vya watu alivyokuwa akisimuliwa na wale watu mbalimbali wa mwanzo waliokuwa wakishuhudia miujiza mbalimbali ya bwana yesu,soma(mathayo 14:32-33,8:27)…..hapo ndipo luka akaamua kuandika kwa utaratibu unaofaa wa kuhusu mambo yale yote yaliotokea.(luka 1:2).Pia luka hakumuandikia theofia mtukufu pekee ili aburudike bali ni kwa ajili ya watu wote.Soma(luka 24:47).HITIMISHO: Hakuna kasoro ndani ya biblia kwa kuwa hili ndilo neno pekee la mungu wa kweli.Ndugu majid ur 10+10=20 bible contraditions answered.lete hoja nyingine…..

    Like

  58. mhina says:

    Ndugu.Abdul majid na kila muislamu mwenye kuijua vyema dini yake,ninawaombeni sana sana mnijibu Vijiswali vyangu vitano tu, kwa majibu mazuri na yakweli yaliyojaa hekima za kiislamu zilizotoka kwa Allah, ili namimi angalau nifahamu na mambo ya upande wa pili kidogo yanavyoenda.VIJISWALI VYANGU HIVYO VITANO NI KAMA VIFUATAVYO…….(1) Mungu wa kweli hasemi uongo,akisema uongo basi ujue kuwa huyo sio Mungu wa kweli alietuumba wanadamu wote.Na pia hiyo dini yake itakuwa ni ya uongo.Lakini tunamuona Allah katika quran,amewaambia waislamu kuwa,nabii wao mhamad ametajwa katika torati na ijili.Sasa ndugu waislamu, nawaombeni mnionyeshe andiko moja tu,katika torati na andiko moja tu,katika injili, pasipo maelezo yoyote…ili tuyachambue hapahapa na kujua kama Allah alisema kweli au alisema uongo………..(2) quran inafundisha wafuasi wake kwamba, siku ya mwisho watazawadiwa na Allah mambo mengi sana ya kidunia kama ULEVI, MABIBI WAREMBO MNO TENA BIKIRA nk….Mambo ambayo kwa asili yake hapa duniani,tunaviita anasa za dunia hii ambazo shetani ndiye anaewashawishi wanadamu kupenda na kufanya mambo hayo…(a)Je, ni kweli kuwa bidii zoote za waislamu kuswali swala tano kwa siku zina lengo la kitabu chao na matumaini hayo ya kuja kulala na mabibi wazuri na kunywa ulevi huko mbinguni?…..(b) kwanini sasa Allah anawakataza waislamu wasifurahie mambo hayo hapa duniani akiyaita ni ya kishetani halafu tena anawa ahidi mambo hayo hayo wafuasi wake kule mbinguni?……(c) mbona sasa Allah anaahidi kuwa mambo hayo yapo huko mbinguni wakati mtume wake bwana yesu kama waislamu mnavyoamini anasema kuwa, mambo ya kupewa mabibi huko mbinguni HAKUNA.Soma(mathayo 22:28-31)……….(3) Muhamad anasema kuwa yeye ni msaidizi wa bwana yesu na ni nabii wa mwisho anaefaa kufuatwa (a) mbona sasa hakumsaidia bwana yesu kuihubiri injili yake kama walivyofanya wakina mtume paulo? Badala yake ameiletea dunia njia mpya ya uislamu na nguzo zake za kufuatwa,mambo ambayo hayapo kabisa katika torati ya musa wala injili ya bwana yesu. (b)kabla ya hii dini yake ya kiislamu na nguzo zake za kufuatwa, watu wa zamani kabla yake walikuwa na dini gani ya kuwafikisha kwa Allah kupata ulevi? Yaani wao walikuwa dini gani kwa kuwa bado nguzo za imani muhamad alikuwa hajaziandika.(quran 10:104,6:14)………….(4) Kama ni kweli Mhamad alipokea neno la Mungu wa kweli kule mapangoni: (a) mbona alikiri yeye mwenyewe kuwa alichezewa na mashetani yakimzuga akili yake? (b) mbona malaika yule kama ni kweli alitoka kwa mungu alitumia njia mbaya ya kumdhohofisha mtume kwa kumkaba na kumminya hali iliyomsababishia majasho na homa huku akijitetea kua hajui kusom.(c) mbona kila muhamad alipokuwa anapata ujumbe mzuri wa malaika (ufunuo) kutoka kwa Allah anapandwa tena na homa kali uku uso ukibadilika rangi…kwanini hali hizi zitokee?…mbona hakuna hata nabii mmoja katika historia zote za manabii aliewahi kuletewa ufunuo wa neno la mungu na malaika wa mungu alafu akabwe kama hivyo?,,……..(.5)Kwa kawaida kabisa ni kwamba Nabii ni mtu muhimu mno katika kuwaonyesha wafuasi wake njia ya kweli ya mungu na kuwapa matumaini wafuasi wake hao ujumbe wa ‘INAWEZEKANA KUSTAHILI MBELE ZA MUNGU KWA NJIA YAKE’.Nabii ni njia na njia ndiyo dini ya haki.Bwana yesu alisema yeye ndiye njia kweli na uzima.Swali langu hapa ni kwamba kama muhamad anadai kuwa yeye ndiye njia ya haki, mbona alikiri yeye mwenyewe kuwa hajui atakalofanyiwa na Mungu siku ya kiama wakati yeye ndio hiyo njia ya mungu?….mbona pia alishindwa hata kuwahakikishia wafuasi wake anaowaongoza katika hiyo njia? Mbona pia alishindwa kumhakikisha njia hiyo hata mwanae aliemzaa mwenyewe?……..KWA VISWALI VYANGU HIVI VICHACHE NDUGU WAISLAMU,NAWAOMBENI MNIJIBU VYEMA ILI NIWALETEE ZAID VIJISWALI VYENGINE.Nawashukuru…lakini nisipotosheka na majibu yenu nitaendelea kuhoji mambo hayohayo.

    Like

  59. chidy rakim says:

    Tatizo Bibilia hujuwi!!! 1.Kutabiriwa kwa nabii Muhammad ndani ya Bibilia! Kumbukumbu:18:18-20Katika ndugu zako (Israel).ndugu zao ni Waarabu….Kama wewe Musa. Kuzaliwa na Maisha yake Musa ni sawa ya Nabii Muhammad.1.Musa amezaliwa.na Baba na Mama2.Musa aliowa3.Musa alipata Utume akiwa mtu mzima4.Musa alipigana vita5.Musa alipewa amri na hukumu na Muhammad hivyo hivyo.N.B: Waandishi wa Bibilia wameondoa jina la Muhammad na kulitafsiri: ikiwa mnataka kuona ukweli, wende kwenye Google search: Online Hebrew Bible kisha soma Songs of Song:5:16 katika lugha ya KiHebrew kisha u highlight, copy and paste kwenye Online Hebrew to English Translations jina la Muhammad lipo. Na mara nyingi Muhammad ametabiriwa kupitiya inchi na mji wake atakapo zaliwa mfano Parani yaani Makka ya sasa. Kumkumbu:33:1-5……..Nchi yake ni Arabia kwa sasa ni Saudi Arab Isaya:21:13…..katika Agano Jipya ametabiriwa kwa kutumia neno la ( Nabii Yule ) ao ROHO wa Kweli.

    Like

  60. mhina says:

    (1)Sikuhitaji maelezo,bali nilihitaji nipewe andiko moja moja katika pande zote mbili(tor + injili) ilituyachambue kwa haki kwa mujibu wa biblia yenyewe.(2) .Sikuhitaji jibu la swali moja bali niliuliza maswali matano ili nijibiwe….Muislam wa kweli anaejua maandiko vizuri, namuomba anisaidie kujua hayo yote vyema.Hatuchokozani wala kushindana bali tunabadilishana mawazo kama ndugu.Aksanteni.

    Like

  61. chidy rakim says:
    MUHAMMAD S.A.W. KATIKA BIBLIA Kuja kwa Nabii Muhammad s.a.w. si jambo geni kwa watu wa Kitabu maana kumebashiriwa mara nyingi katika Biblia. Haya yanathibitishwa na Qur’an Tukufu inayosema hivi juu ya waaminio kwamba ni wale “Ambao wanamfuata Mtume, Nabii aliye Ummi, ambaye wao humkuta ameandikwa kwao katika Taurati na Injili. Huwaamuru yaliyo mema na kuwakataza yaliyo mabaya.” (7:158). 3 Maneno haya “Ameandikwa kwao katika Taurati na Injili”, yanaonyesha kwamba Nabii Muhammad s.a.w. si Mtume wa kitaifa bali ametumwa kwa mataifa yote ya wanadamu. Mtume Muhammad s.a.w. kwa kuwa ni m’bora wa mitume wote (Sura 33:41) naye alitumwa kwa watu wote (Sura 7:159) bishara zinazotabiri kuja kwake zinapatikana katika vitabu vya dini zote. Hapa vimetajwa Taurati na Injili. Katika vitabu hivyo mna bishara nyingi zenye kuwawezesha Mayahudi na Wakristo kumtambua Mtume Muhammad s.a.w. Hapa tutaeleza baadhi ya bishara hizo. BISHARA YA KWANZA. Siku ya mkutano katika Horeb, wana wa Israeli walipokataa kusikia sauti ya Mwenyezi Mungu. Mungu alimwambia Musa. “Wametenda vema kusema walivyosema, mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake. naye atawaambia yote nitakayomwamuru. “Hata itakuwa, mtu asiyeyasikiliza maneno yangu atakayoyasema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake. Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena kwa jina la miungu wengine, nabii yule atakufa.” (Kumbukumbu la Torati 18.16-20). Bishara hii tukufu inaonyesha mambo haya yafuatayo. (i) Wana wa Israeli hawatasikia tena sauti yenye nguvu ya Mwenyezi Mungu. (ii) Anayebashiriwa kufika ni Nabii. (ill) Ataondokeshwa miongoni mwa ndugu wa Waisraeli. (iv) Atakuwa mfano wa Musa. (v) Maneno atakayoyasema yatakuwa ufunuo wa Mungu. (vi) Atawaambia yote atakayoambiwa na Mungu. (vii) Atanena hayo kwa jina la Mungu. (viii) Asiyetaka kusikia maneno hayo ataadhibiwa. (ix) Nabii wa uwongo atakayesingizia kutumwa na Mungu atakufa. (x) Atakayesema kwa jina la miungu wengine atauawa. 4 Sasa ni watu wawili wanaosemwa kuwa wametabiriwa katika bishara hiyo. Wakristo wanasema ni Yesu, na Waislamu tunasema ni Muhammad s.a.w. Bishara yenyewe haitaji jina la mtu ye yote, ila tu imeeleza alama kumi za Nabii huyo. Basi tupeleleze alama hizo zinamwangukia nani katika manabii hawa wawili. (i) Katika bishara hiyo Waisraeli wanaambiwa kwamba hawatasikia tena sauti ya Mungu. Na inajulikana pote ya kuwa Yesu alikuwa Mwisraeli aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi (Mathayo. 1:1). Mtume Muhammad s.a.w. alikuwa Mwarabu. Hakuwa katika kizazi cha Waisraeli kilichonyimwa baraka za Mungu, kwa kukataa kwao kusikia sauti ya Mungu. (ii) Bishara inasema huyo anayebashiriwa kufika ni nabii. Wakristo wanaamini ya kwamba Yesu alikuwa “Mungu-Mwana” au Mungu Mwenyewe, nao hawataki kabisa Yesu aitwe nabii. Lakini Mtume s.a.w. aliitwa Rasuulullaahi (Mtume wa Mungu) na pia Nabiyyullaahi (Nabii wa Mungu). (iii) lkumbukwe kwamba nabii Ibrahim – baba wa manabii – ndiye aliyemzaa Ismaeli na Isihaka. Wazao wa Ismaeli ndio Waarabu, na wazao wa Isihaka ndio Waisraeli. Mtume Muhammad s.a.w. alitokana na Waismaeli ambao ni ndugu wa Waisraeli, kama inavyoagua bishara hiyo. Lakini Yesu mwenyewe ni Mwisraeli, wala hakutoka katika ndugu wa Waisraeli. Hivyo bishara hii si yake. (iv) Bishara inaeleza tena ya kuwa mtume huyo atakuwa mfano wa Musa. Nasi tunaona ya kuwa Mtume Muhammad s.a.w. ndiye anayeitwa mfano wa Musa katika Kurani tukufu (sura 73:16). Yesu angewezaje kujifanya kama Musa hali mwenyewe alikuwa chini ya Sheria ya Musa? (Mathayo 5:17, 7:12, Marko 10:19. Matendo 24:14). Hali ya Mtume Muhammad s.a.w. na ya Nabii Musa zinafanana sana. Nabii Musa alizaliwa na wazazi wawili wala hakulaumiwa katika kuzaliwa kwake. Tena Musa alioa, alipewa 5 Sheria mpya, alihama nchi yake baada ya kupewa utume, alipigana na adui zake, nao wakaangamia mbele ya macho yake, alikufa kifo cha kawaida, walitokea maimamu na mawalii katika umati wake, na mwishowe alikuja Masihi kusimamisha Sheria ya Musa. Hayo yote yalipatikana kwa Mtume Muhammad s.a.w. na hivyo wamefanana kabisa. Lakini hakuna hata alama moja ya hizo inayopatikana katika dhati ya Yesu sawa na itikadi za Wakristo. (v) Bishara inaendelea kusema: “Nami nitatia maneno yangu kinywani mwake”. Yaani Mungu atamteremshia maneno yake. Alama hii pia haionekani katika Yesu. Wakristo wanaamini ya kuwa Yesu alikuwa Mungu, kwa hivyo hakukuwa na haja ya kufunuliwa maneno kutoka kwa Mungu. Zaidi ya hayo, Kurani ndiyo Sheria ya pekee inayostahili kuitwa “Maneno ya Mungu”, maana haina hata neno moja lisilotoka kwa Mungu Mwenyezi. (vi) Mtume s.a.w. anaambiwa na Mwenyezi Mungu kufikisha yote aliyoteremshiwa (Kurani tukufu 5.68). Yesu aliwaambia wanafunzi wake ya kuwa hatawaambia yote (Yohana 16.12-13). Hivyo bishara hii haimhusu Yesu. (vii) Alama ya saba pia haionekani katika Yesu. Mtu anayesoma Injili anajua ya kwamba Injili yo yote haikuanzishwa kwa jina la Mungu. Yesu anasema mara kwa mara. “Bali mimi nawaambieni” (Mathayo 5:22. 28, 34. 39. 44). Luka anasema, ameandika Injili yake kwa sababu. “Nimeona vema mimi nami kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu, Theofile Mtukufu” (Luka 1:3-4). Hasemi kwamba alifunuliwa na Mungu, au ameongozwa na Roho Mtakatifu, wala hakuandika Injili hiyo ili watu wote waisome, bali alimwandikia mtu mmoja tu, Theofile. Paulo alisema. “Kwa habari za wanawali, sina amri ya Bwana. Lakini natoa shauri langu” (Wakorintho 7:25). Ni dhahiri ya kwamba lnjili za leo ni mkusanyiko wa maneno ya watu mbali mbali. Lakini Kurani inataja jina la Mwenyezi Mungu katika mwanzo wa kila sura, na inaonekana Mungu alikusudia 6 kutimiza alama hiyo wazi wazi. Tena Mtume s.a.w. kabla ya kuanza kazi yo yote alikuwa anataja jina la Mwenyezi Mungu. (viii) Waliokataa kusikiliza maneno ya Mungu yaliyotoka kinywani mwa Mtume s.a.w. waliadhibiwa hapa hapa duniani. Vita vikali vilivyoangamiza maadui wa Uislamu vilikuwa adhabu ya Mwenyezi Mungu iliyoahidiwa katika bishara hii, na bado kuna adhabu ya akhera itakayowawakia walio maadui wa haki. (ix) Wapinzani wa Uislamu wanasema ya kwamba Mtume s.a.w. alizua uwongo. Bishara hii inawajibu na kusema mtu ye yote atakayemzulia Mungu atauawa. Mtume s.a.w. alikaa miaka mingi duniani na akisha maliza kazi yake akafariki kifo cha kawaida. Lakini Yesu je? Tukifuata imani ya Wakristo kuwa aliuawa msalabani, tunashurutishwa kusema ya kuwa (Mungu apishe mbali) alikuwa mwongo, maana bishara yasema kuwa nabii wa uwongo ndiye atauawa. Hivyo kufaulu kwa Mtume s.a.w. na maendeleo ya kazi yake ni dalili zilizo wazi za ukweli wake. (x) Bishara inaeleza tena ya kuwa mwenye kusema neno kwa jina la miungu wengine “Nabii yule atakufa”. Kwa kuwa Mtume s.a.w. hakuuawa basi imethibitika ya kwamba yote aliyosema alifunuliwa na Mungu. BISHARA YA PILI. Katika kumbukumbu la Taurati 33:2-3 imeandikwa hivi, “Bwana alitoka Sinai, akawaondokea kutoka Seiri, akaangaza kutoka kilima cha Parani, na akaja na elfu kumi za watakatifu. Upande wa mkono wake wa kuume palikuwa na sheria ya moto moto kwao. Hakika awapenda hayo makabila ya watu, watakatifu wake wote wamo mkononi mwako, nao waliketi miguuni pako”. Hapa pameelezwa maonyesho matatu ya Mwenyezi Mungu. Musa alitoka Sinai. Seiri ni alama ya Yesu. Na Mtume Muhammad s.a.w. aliangaza kutoka kilima cha Parani. Wanazuoni wamekubali 7 ya kwamba Parani ni kilima cha Makka (Mu’jamul Buldaan). Biblia inasema. Ismaili “akakaa katika jangwa la Parani” (Mwanzo 21:21) na Mtume Muhammad s.a.w. ni mjukuu wa lsmaili. Mtume s.a.w. alipoondoka Madina kwenda kuiteka Makka alikuwa na masahaba elfu kumi. Katika Biblia ya Kiingereza hesabu ya watakatifu hao imetajwa kuwa “ten thousand saints” yaani “watakatifu elfu kumi”, kama tulivyofasiri hapo juu. Lakini katika Biblia ya Kiswahili cha Mvita (Mombasa). Wamefasiri maneno hayo kuwa “Makumi ya elfu”, yaani elfu zile zilikuwa si kumi moja bali makumi mengi, wapate kuwavuruga wasomao Kiswahili wasijue hesabu ya Masahaba watakatifu wa Mtume s.a.w. aliotokea nao Parani katika bishara ya Biblia. lnasikitisha kuona ya kwamba Mapadri hawajatosheka na kiasi hicho cha mageuzi. Katika tafsiri mpya ya Biblia (Union Version) ya mwaka 1952 kifungu hicho cha maneno wamekiandika: “Akaja Meribath kadeshi”, ili wavuruge kabisa bishara hiyo isiweze kufafanuka. Ni ajabu maneno kama Tirshatha (uk. 478), Darkoni (uk. 479) na mengine yameelezwa chini katika kurasa, na mengine yameelezwa mwisho wa kitabu cha Biblia, lakini neno Meribath-kadeshi hawakulieleza chini ya ukurasa ule wala mwisho wa kitabu. Ingawa ni jipya kabisa lakini limefanywa lionekane kama jina la mtu au Malaika au hivi. Wale wanaofikiri ya kwamba Biblia ya Union Version imefasiriwa vizuri sana katika Kiswahili cha kisasa, watasemaje juu ya uaminifu huu wa wafasiri? llikuwaje wanazuoni wakubwa wakubwa wa Kiyunani na Kiebrania na Kiswahili kushindwa kufasiri au kueleza neno Meribath-kadeshi? Inaonekana dhahiri ya kwamba dhamiri za mapadri zinawalaumu juu ya tafsiri zao zisizo sahihi, zinazovurugwa ili kuficha haki. Alama nyingine ni kuleta Sheria. Mtume Muhammad s.a.w. ndiye aliyeleta Sheria baada ya Nabii Musa. Na ile Sheria ilileta joto katika mioyo ya Waislamu, nao wakainuka katika miaka michache. Pia imeitwa “Sheria ya Moto Moto” kwa ajili ya kuunguza maovu, madhambi na mabaya yote. Wale waliojaribu kuipinga 8 Kurani wakaangamia wenyewe. Kweli, Kurani ikifuatwa sawa sawa, inaweza kuchoma dhambi za watu kama moto unavyochoma takataka. Je hamwoni Waarabu waliokuwa wakinywa ulevi kutwa mara tano waliacha wakawa wanasali kutwa mara tano? Mtume alizipenda sana kabila zote. Katika masahaba wake kulikuwa Waarabu wa makabila mbali mbali: Wahabeshi, Waajemi na Warumi, na Mtume s.a.w. aliwapenda wote. Hakuwaita mbwa na nguruwe watu wa mataifa mengine kama alivyowaita Yesu (Mathayo 7:6; 15:26). Masahaba wa Mtume s.a.w. pia walimpenda sana. Kwa hakika Mtume s.a.w. alipendwa na masahaba zake zaidi kuliko kila mtu anavyopendwa na wafuasi wake. Katika vita, kama mishale ilipigwa kutoka katika kila upande, masahaba walimzunguka Mtume kama kuta ili asipate kujeruhiwa. Hatuwezi kuwalinganisha na wanafunzi wa Yesu waliomtoroka wote wakakimbia na kumwacha Yesu peke yake katika matata (Mathayo 26:56. Marko 14:50). BISHARA YA TATU. Katika Wimbo ulio Bora (5:10) mmeandikwa “Mpenzi wangu ni mweupe tena mwekundu – mwekundu. Ndiye mkuu katika elfu kumi” (Biblia ya Kimvita). Huyu aliyetajwa hapa na Nabii Suleimani aliyekuwa mkuu katika watu elfu kumi si mwingine bali Mtume Muhammad. Maneno ya mbele ya haya yameeleza sifa zote za mwili wa Mtume s.a.w. kama ulivyokuwa. BISHARA YA NNE. Isaya 28:9-13 kinasema, “Atamfundisha nani maarifa? Atamfahamisha nani habari hii? Je! ni wale walioachishwa maziwa, walioondolewa matitini? Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu 9 ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni, huku kidogo na huku kidogo. La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa; ambao aliwaambia, Hii ndiyo raha yenu, mpeni raha yeye aliyechoka; huku ndiko kuburudika; lakini hawakutaka kusikia. “Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo, ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa”. Walioachishwa maziwa ni wana wa Ismaili ambao waliakhirishwa kupata ujumbe wa Mungu. Kurani tukufu iliteremshwa pole pole, amri juu ya amri, kama ielezavyo bishara hiyo. Baadhi ya sura zilishuka Makka na nyingine Madina (Huku kidogo na huku kidogo). Kurani tukufu iliteremshwa katika lugha ya Kiarabu ambayo ni “Midomo ya watu wageni na lugha nyingine” kwa wana wa Israeli. Mbele imeelezwa ya kwamba Mtume s.a.w. atakimbilia Madina kwenye raha, mapumziko na maburudiko, lakini watu wa Makka watazidi kukataa ujumbe wa Uislamu mpaka watashindwa, kuvunjwa na kunaswa, na kuchukuliwa. BISHARA YA TANO. Katika Isaya 21.13-17 mmeandikwa: “Hili ni neno zito lililo juu ya Arabia. Ninyi mtalala ndani ya msitu wa Arabuni, enyi Wadedani wenye kusafiri pamoja, Wenyeji wa nchi ya Tema walimletea maji yule aliyekuwa na kiu, walimlisha mkate wao yule aliyekimbia. “Kwani walizikimbia hizo panga, huo upanga uliofutwa, na huo uta uliopindwa, na hayo mazito ya vita. Kwani yeye Jehova ameniambia neno hili, katika muda wa mwaka mmoja, kwa kuandama hesabu ya miaka ya mwenye kuajiriwa, huo utukufu 10 wote wa Kedari utabatilika, na hao watakaosalia katika hesabu ya hao wenye kutumia uta, hao Mashujaa wa hao wana wa Kedari, watakuwa ni wachache kwa maana Jehova, yeye Mwenyezi Mungu wa Israeli, amenena neno hili.” 1. Aya 13 inatabiri juu ya “Hijra” yaani kuhama kwa Mtume Muhammad s.a.w. kutoka Makka hadi Madina. Tukio hili ni mojawapo katika matukio matukufu sana katika historia ya dini ya Kiislamu, maana Kalenda ya Kiislamu huanzia tangu wakati huo. Mtume s.a.w. alipotoka Makka kwa amri ya Mwenyezi Mungu na kuhamia Madina ambako alistawi sana na baadaye akiwa na masahaba wake watakatifu elfu kumi alirudi kuingia Makka bila kizuizi. 2. Maneno ya Aya 14 yanaeleza hali ya Mtume s.a.w. aliposafiri kuhamia Madina. Ikumbukwe ya kwamba Tema ndilo jina la nchi ambamo miji ya Makka na Madina yapatikana. 3. Maelezo ya aya 15, ni juu ya ile hali ya nchi yenye mateso na usumbufu juu ya Mtume s.a.w. ambayo watu wa Makka walimtendea hata maisha yake yakawa katika hatari katika mji huo alimozaliwa. Katika kitabu cha Maisha ya Mtume Muhammad, kilichoandikwa na marehemu Al-Haj F. R. Hakeem uk. 22 imesimuliwa hivi :- “Mwisho saa ilifika. Wakimkuta Mtume s.a.w. akielekea kuwa peke yake kabisa, Wakubwa wa Kikureshi walifanya mkutano katika Dar-un-Nadwa.. ambako mambo ya kiserikali yalifikiriwa na mashauri kukatwa. Walikutana huko na kushauriana jambo gani afanyiwe. Baadhi yao walifikiri afungwe kamba na atupwe katika chumba cha giza na aachwe bila chakula mpaka afe. Wengine walifikiri asafirishwe mbali sana. Lakini, mwishowe Abu Jahli aliwapa mawazo yake ya kwamba vijana wa ukoo mkuu wapewe panga kali, ambao watatumia kwa kumhujumu kwamba wote watamshambulia wakati mmoja ili pasiwe na kabila maalumu la Makureshi la kushtakiwa kwa kuua. 11 Bani Hashim (Kabila la Mtume, s.a.w.) lingeridhika, kwa hivyo kupewa pesa za damu badala ya kuwaadhibu. “Mpango huu ulikubaliwa na watu wote. Baadaye watu walio na silaha walijipanga nje ya nyumba ya Mtume s.a.w. tayari kumuua akitoka nje. Lakini Mwenyezi Mungu alimwepusha na hila zao mbaya na akamwepusha na panga zao zilizokuwa kali.” Hii ndiyo iliyokuwa hali ya mji wa Makka Mtume alipouhama, na hizi hasa ndizo hali zilizotabiriwa na maneno hayo ya Isaya. 4. Aya 16 yatabiri juu ya vita vya Badr, ambavyo Mtume s.a.w. na wafuasi wake wachache walipigana na kundi kubwa la maadui wa Uislamu mwaka mmoja baada ya Mtume kuhamia Madina. Katika vita hivi vilivyopiganwa karibu na mji wa Madina, Waislamu wachache waliokuwa na silaha haba waliwashinda maadui zao waliokuwa wengi sana tena mahodari wa vita. Hesabu ya Waislamu ilikuwa 313 hali maadui zao walikuwa elfu moja. Lakini kwa kudra ya Mwenyezi Mungu, mwenye uwezo wote, maadui wa Uislamu walishindwa vibaya sana na bishara iliyotajwa hapo juu ikatimia barabara. Pia ikumbukwe ya kwamba Kedar ni jina la mtoto mmoja wa Ismaili ambaye wazao wake waliishi katika sehemu ya Hijaz ulipo mji wa Makka. Wataalamu wa historia wamethibitisha kuwa Makureshi wa Makka (ambao ndio wale waliopeleka jeshi Madina kwenda kuwasaga Waislamu, lakini badala yake wakasagwa wao) walitokana na hao wazao wa Kedar. Na kule kushindwa kwao baada ya mwaka mmoja baada ya Mtume s.a.w. kuhamia Madina kunakamilisha bishara hii ya Isaya bila upungufu wo wote. 5. Ile aya ya mwisho, yaani 17, inatabiri ushindi wa Mtume s.a.w. juu ya maadui zake katika hivyo vita vilivyotokea mwaka mmoja baada ya Mtume kuhamia Madina. 12 Kwa jumla bishara hii nzima haina uhusiano wo wote na Nabii mwingine ila tu Nabii Muhammad s.a.w. Wala hapana ushahidi wa historia unaoweza kutufanya tuseme ya kwamba pana Mtume mwingine aliyehama mji wake kwa ajili ya maadui zake na kisha akawashinda hao hao baada ya mwaka mmoja. Hayo yote yalitokea kwa Mtume wetu mutukufu Muhammad s.a. w. pekee. BISHARA YA SITA. Katika Isaya 42:1-17 mmeandikwa maelezo kamili juu ya Mtume Muhammad s.a.w. nasi hatuna budi kuyanakili kama ifuatavyo. 1. Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye, mteule wangu. ambaye nafsi yangu imependezwa naye, nimetia roho yangu juu yake, naye atawatolea mataifa hukumu. 2. Hatalia wala hatapaaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu. 3. Mwanzi uliopondeka hatauvunja wala utambi utokao moshi hatauzima, atatokeza hukumu kwa kweli. 4. Yeye hatalegea, wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani, na visiwa vitaingojea sheri a yake. 5. Mungu Bwana anena, yeye aliyeziumba mbingu na kuzitanda; yeye aliyetandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake. 6. Mimi. BW ANA. nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono na kukulinda na kukutoa uwe agano la watu na nuru ya mataifa. 7. Kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa. 13 8. Mimi ni BWANA, ndilo jina langu, na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. 9. Tazama mambo ya kwanza yamekuwa nami nayahubiri mambo mapya, kabla hayajatokea nawapasheni habari zake. 10. Mwimbieni BWANA wimbo mpya, na sifa zake tokea mwisho wa dunia, ninyi mshukao baharini, na vyote viIivyomo visiwani, nao wakaao humo. 11. J angwa na miji yake na ipaze sauti zao, vijiji vinavyokaliwa na Kedari; na waimbe wenyeji wa Sela, wapige kelele toka vilele vya milima. 12. Na wamtukuze BWANA, na kutangaza sifa zake visiwani. 13. BWANA atatokea kama shujaa, ataamsha wivu kama mtu wa vita, atalia, naam, atanguruma, atawashinda adui zake. 14. Siku nyingi nimenyamaza kimya, nimetulia. nikajizuia, sasa nitapiga kelele kama mwanamke, aliye katika kuzaa, nitaugua na kutweta pamoja. 15. Nitaharibu milima na Vilima, nitavikausha vyote vimeavyo, nitaifanya mito ya maji kuwa visiwa, na kuyakausha maziwa ya maji. 16. Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua, katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza, nitafanya giza kuwa nuru mbeIe yao, na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Nitawafanyia haya wala sitawaacha. 17. Watarudishwa nyuma, wataaibishwa sana, hao wanaotumainia sanamu za mawe, na kuziambia sanamu za madini, Ninyi ndinyi miungu yetu. i. Maelezo yale yaliyo katika bishara hii yanamhusu Mtume Muhammad s.a.w. pekee. Aya ya kwanza tu yasema, “Tazama 14 mtumishi wangu”. Bishara hii inalingana sana na Kalima (Tashahud ya Kiislamu) inayosema: Nashuhudia kuwa hapana anayepasa kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, na nashuhudia ya kuwa Muhammad ni “Mtumishi wake” na “Mtume wake”. Wakristo wanasema Yesu alikuwa mwana wa Mungu au Mungu mwenyewe. Hivyo hawezi kuitwa “Mtumishi” wa Mungu. Huyu Mtumishi wa Mungu anayetajwa hapa si mwingine minghairi ya Mtume Muhammad s.a.w. ii. Kisha bishara inasema “Mteule Wangu” Ingawa maneno haya ya Isaya yalibashiriwa miaka mingi kabla ya kuzaliwa Mtume Muhammad s.a.w. lakini ajabu moja ni hii kwamba jina jingine la Mtume Muhammad s.a.w. ni “Mustafa” ambalo maana yake ni “Mteule”. iii. Bishara inaendelea kusema, “ambaye nafsi yangu imependezwa naye”, na katika Kurani tukufu tunasoma, “Hakukuacha Mola wako wala Hakukasirika” (93:4). Maneno haya ya Mwenyezi Mungu yanathibitisha wazi ya kuwa Mtume s.a.w. alipendwa mno na Mola wake. iv. lkiendelea mbe!e bishara hii inasema, “Nimetia roho yangu juu yake”. Akitimiza ahadi hii Mwenyezi Mungu anasema katika Kurani tukufu. “Na bila shaka hii (Kurani) ni uteremsho wa Mola wa walimwengu. Ameteremka nayo Roho mwaminifu juu ya moyo wako ili uwe miongoni mwa Waonyaji” (26: 193-195). Hii yaonyesha ya kuwa bishara hii yatabiri kuja kwa Mtume Muhammad s.a.w. wala si nabii mwingine. v. Kadhalika bishara inasema, “Naye atawatolea mataifa hukumu.” Ikumbukwe ya kuwa Manabii wote waliokuja kabla ya nabii Muhammad s.a.w. walikuwa manabii wa kitaifa, hivyo walipelekwa kwa mataifa yao pekee. Akitilia mkazo juu ya ujumbe wa kitaifa, Yesu aliwaagiza wanafunzi wake akisema, “Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wa Wasamaria msiingie, afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba 15 ya Israeli” (Mathayo 10:5). Akizidi kuutetea ujumbe wake wa kitaifa Yesu anasema, “Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli” (Mathayo 15:24). Hivyo Yesu hawezi kusemwa kuwa alileta hukumu kwa mataifa. Mtume aliyetolea hukumu mataifa ni Muhammad s.a.w. Yeye tu ndiye aliyetumwa kwa mataifa yote duniani. Mwenyezi Mungu anahakikisha ukweli wa jambo hili kwa kusema katika Kurani tukufu: “Hakika Tumekuteremshia Kitabu kwa haki ili upate kuhukumu baina ya watu kama alivyokufahamisha Mwenyezi Mungu” (4.106). vi. Tukiendelea mbe!e tunaona bishara inasema. “Yeye hatalegea wala hatakata tamaa hata atakapoweka hukumu duniani,” Ahadi hii pia Mwenyezi Mungu aliitimiza katika dhati ya Mtume Muhammad s.a.w. pekee. Kwani katika Kurani tukufu Mwenyezi Mungu anasema. “Bila shaka tumekupa ushindi ulio dhahiri”, (48.2). Wenye kusoma historia ya dini mbali mbali wanajua ya kuwa miongoni mwa manabii wa Mungu wanaojulikana ni Nabii Muhammad s.a.w. peke yake aliyewashinda maadui zake wote katika uhai wake. Kabla hajafariki dunia, nchi nzima ya Arabia ilikuwa chini ya uongozi wake. Hivyo tunaona mtumishi wa Mwenyezi Mungu anayetabiriwa hapa si mwengine minghairi ya Mtume Muhammad s.a.w. vii. Maneno ya kifungu cha tano ingawa hatukuandika hapo juu, lakini yanahakikisha kuwa bishara hii imetoka kwa Mungu. Aya ya sita katika bishara hii inasema “Mimi BWANA nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa” (Isaya 42.6). Ama sehemu hii ni bishara tukufu mno na ambayo muradi wake Mwenyezi Mungu aliutekeleza juu ya Mtume s.a.w. ili kuondoa tashwishi yo yote katika nyoyo za watu. Kuhusu jambo hili Mwenyezi Mungu akamfunulia Mtume wake akisema. “Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu”. (5.68). Na hivyo hasa ndivyo ilivyokuwa, maana kila adui mwasi aliyetaka kumdhuru Mtume s.a.w. Mwenyezi Mungu aliuzuia mkono 16 wake usimfikie Mtumishi wake wa haki. Mambo hayo hayawezi kusemwa juu ya Yesu. Wakristo wanasema Yesu alishikwa na maadui zake na akauawa juu ya msalaba. Kwa mujibu wa imani hii ya Wakristo inakuwa wazi sana kwamba bishara hii ya Isaya haimhusu Yesu asilani. viii. Maneno yaIiyoandikwa katika aya ya 8 ni haya. “Wala sitayapa masanamu sifa zangu”. Muradi wa maneno haya ni huu ya kuwa ibada ya masanamu haikubaliki na Mwenyezi Mungu na ya kwamba hapo atakapofika huyo Mtumishi wa Mungu sifa za miungu ya uwongo (masanamu) zitatoweka kwa njia iliyo bayana zaidi. Na kusema kweli hivi ndivyo ilivyotokea. Alipodhihiri Nabii Muhammad s.a.w. ibada ya masanamu ilikuwa imesitawi sana hususa katika bara Arabu. Katika nyumba ya Mwenyezi mungu, Al-Kaaba, mliwekwa masanamu yasiyopungua 360. Lakini Muhammad, Mtumishi wa Mungu, aliyachukia masanamu toka utoto wake. Wala hakupata kuyaabudu hata mara moja. Na wakati ulipowadia yeye alifanikiwa katika kuisitawisha dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu na akaitakasa tena nyumba ya Mungu kwa kuyavunjilia mbali masanamu yote yaliyokuwemo humo. Na pia kabla hajafariki dunia ibada ya masanamu ilifagiliwa kote Arabuni na watu wote walizama katika kumwabudu Mungu mmoja tu. Ufanisi huu alioupata Muhammad s.a.w. unaonyesha wazi ya kuwa bishara hii ya Isaya inamhusu yeye tu wala si nabii mwinginewe. ix. “Mwimbieni BWANA wimbo mpya.” Hapa ufasaha wa Kurani tukufu umetajwa kama wimbo. Kadhalika waandishi wengi wa Ulaya wakivutiwa na mpango wa maneno ya Kurani tukufu, wameiita Mashairi. Na katika maneno haya ya Biblia, Kurani tukufu imepewa mfano wa mashairi na kwa kuwa ni ufunuo mpya ndio ukaitwa “Wimbo Mpya”. Hapa ni lazima ifahamike ya kuwa Yesu hakuleta sheria yo yote mpya. Yeye mwenyewe anasema, “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua Torati au manabii, la, sikuja kutangua bali kutimiza” (Mathayo 5.:17). Kwa mujibu wa maneno haya ya Biblia, Yesu hawezi kusema alimwimbia BWANA wimbo 17 mpya, bali alikuja kutimiza sheria ya Musa. Kurani tukufu ndiyo Sheria mpya, na ndio wimbo mpya wa BWANA. x. Katika maneno haya, “Na waimbe wenyeji wa Sela”, Sela yaashiria kwenye mlima mmoja katika Madina. Neno Sela ni alama nyingine ya kuwa bishara hii inamhusu Mtume Muhammad (s.a.w.) pekee. xi. Maneno haya, “Ninyi mshukao baharini”, yanaashiria misafara ya wabashiri wa Kiislamu ambao walisafiri katika bahari ili kulieneza Neno la Mungu, Kurani Tukufu, miongoni mwa watu wa visiwa na nchi mbali mbali. Ikumbukwe ya kuwa Waislamu walifanya safari nyingi ili kuweza kuihubiri dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kweli ya kwamba Wahubiri wa Kristo pia walisafiri ulimwenguni kueneza dini yao. Lakini ipo tofauti iliyoko baina yao na Wabashiri wa Kiislamu. Waislamu walihubiri ili kutekeleza maagizo ya nabii mtukufu, Muhammad s.a.w. ya kuwa ni wajibu wa kila Mwislamu kuitangaza dini, lakini kwa upande wa Wakristo tunaona ya kwamba ni wao wenyewe walioamua kuhubiri duniani kote bila kuamrishwa na Yesu, bali kwa kufanya hivyo wakaasi amri za Yesu. Katika Mathayo (10;5-6). tunasoma, “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akisema. Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie”. Kwa mujibu wa maneno haya, ujumbe wa Yesu haukutumwa kwa ajili ya watu wa mataifa yote. Hivyo muradi wa msemo huu, “Ninyi mshukao baharini,” haumhusu Yesu wala wanafunzi wake, bali unaashiria safari za Waislamu kwani wao ndio waliopewa amri ya kuyahubiria mataifa yote ulimwenguni. Nasi tunaona visiwa kama vile Indonesia vikiwa mfano mwema miongoni mwa nchi zile zilizoupokea Uislamu kutokana na wabashiri wa Kiislamu waliofika huko toka Arabu. xii. Maneno ya aya ya 11 yanasema “Jangwa na miji yake na ipaaze sauti zao, vijiji vinavyokaliwa na Kedari, na wakaao katika majabali na waimbe, na wapige kelele kutoka juu ya milima.” Neno hili Kedari lilitotajwa hapa linaashiria ukweli kwamba nabii 18 anayebashiriwa katika bishara hii atakuwa Mwarabu, maana Kedari ni jina la mmoja wa wana wa Ismaili walioishi katika jimbo la Hijaz, Arabu. Kwa kuwa Yesu hakuwa Mwarabu bishara hii haimhusu. Bishara hii yamhusu Nabii Muhammad s.a.w. kwa sababu yeye ndiye aliyetokana na wazao wa Ismaili walioishi katika Hijaz. xiii. Katika Isaya 42:13 tunaambiwa ya kuwa nabii anayebashiriwa atapigana vita na maadui zake na ya kuwa yeye atawashinda wote. Historia inashuhudia ya kuwa nabii Muhammad s.a.w. aliwashinda maadui zake wote. Hivyo bishara hii inatimia katika dhati yake. 14. Ama maneno ya aya ya 17 katika mfululizo huu yanatueleza hali ya wenye kuabudu masanamu pindi watakaposhindwa na kuletwa chini ya himaya ya Mungu wa kweli, mwumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo baina yao. Bishara hii pia ilitimia sawa sawa katika dhati ya Mtume Muhammad s.a.w. Dini ya Mwenyezi Mungu ilipopata ushindi na maadui wa Waislamu wakaletwa mbele ya Mtume s.a.w., watu hawa walionekana dhalili na walioona haya sana machoni pa wenzi fungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufuwao. Yaani masanamu yao hayakuwafanyia cho chote, na mtu yule ambaye hapo mwanzoni walimwita yatima na mnyonge sasa Mwenyezi Mungu akampa ushindi juu yao, nao wamekuwa chini ya mamlaka yake. Ushindi kama huu hakuupata Yesu, hivyo bishara hii haimhusu. BISHARA YA SABA. Mojawapo ya bishara kubwa inayoashiria kuja kwa Nabii Muhammad s.a.w. ni hii. “Naye atawatwekea bendera mataifa toka mbali, naye atawapigia miunzi tokea mwisho wa nchi. Na tazama watakuja mbio mbio upesi sana. Miongoni mwao hakuna achokaye wala kukwaa; Hakuna asinziaye wala kulala usingizi. Wala mshipi wa viuno vyao hautalegea. Wala ukanda wa viatu vyao hautakatika; Mishale yao ni mikali na pinde zao zote zimepindika. Kwato za 19 farasi zao zitahesabika kama gumegume. na gurudumu zao kama kisulisuli. Ngurumo yao itakuwa kama ya simba, watanguruma kama wana-simba. Naam, watanguruma na kukamata mateka, na kuyachukua na kwenda zao salama, wala hakuna mtu atakayeokoka. Nao watanguruma juu yao siku hiyo kama ngurumo ya bahari. Na mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki, nayo nuru imetiwa giza katika mawingu yake” (Isaya 5:26-30). Maelezo ya bishara hii ni haya ya kwamba wakati utafika ambapo mtu mmoja atainua bendera nje ya Falastina (Palestine). Mtu huyu atayaita mataifa ya ulimwengu nao wataitikia wito wake na kumfuata upesi tena kwa wingi. Wale watakaomfuata wataacha uvivu na uzembe na watajitoa wakfu kwa imani yao. Watapigana vita na kwato za farasi zao zitatoa moto kama risasi. Watawashambulia maadui zao kwa kasi, mfano wa kisulisuli au kimbunga. Watawashinda maadui zao kwa njia ambayo hakuna atakayeweza kuwaokoa. Na watafanya haya yote kwa sababu gani? Kwa sababu wataona dunia imejaa giza ambalo lingeondoka tu kwa kila mmoja wao kujitolea kufa na kupona. Bishara hii nzima inamhusu Mtume Muhammad s.a.w. nayo ilitimia barabara katika dhati yake. Kurani tukufu pia imegusia jambo hili. Nabii Muhammad s.a.w. alidhihiri katika Makka, mbali na Falastina, na akainua bendera yake toka Madina, naye ndiye aliyetoa wito huu kwa uIimwengu wote. “Enyi watu, hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote,” (Kurani Tukufu: 7:159). Ni wito wake huu uliowavuta wake kwa waume kote duniani kama nguvu za umeme. Katika uhai wake Yesu hakumbatiza hata mtu mmoja nje ya nyumba ya Waisraeli. Vivyo hivyo. wanafunzi wake wote waliishi hatua chache tu kutoka maskani pa Yesu. Lakini wafuasi wa Mtume wa Uislamu mwanzoni tu, walitoka sehemu mbali mbali kama vile Yeman, Iran na Uhabeshi. Na miongoni mwa waliosilimu walikuwemo waliokuwa zamani 20 waabuduo masanamu, Mayahudi na hata Wakristo. Waaminio hao, (Mungu awe radhi nao), kwa kufuatia mwito wa Mtume s.a.w. walijitoa wakfu kwa dini yao na wakadumu katika imani katika kila hali hivi kwamba hata maadui wa dini ya Kiislamu wamelazimika kuusifu uthabiti na ushupavu wa masahaba hao wa Mtume s.a.w. Akitukumbusha jambo hili Mwenyezi Mungu anasema. “Mwenyezi Mungu amewaridhia nao pia wamemridhia,” (9:100). Wafuasi wa Mtume walilazimika kupigana vita kuilinda dini yao, nao humo vitani wakatumia pinde na mishale. Kwato za farasi wao wepesi zilikuwa kama risasi na gurudumu zao kama kinyamkela. Ukali huu wa majeshi ya Waislamu pia umetajwa katika Kurani tukufu. “Naapa kwa (Farasi) wakimbiaji wanaotweta. na kwa wale watoao moto kwa kupiga, tena kwa wale washambuliao wakati wa asubuhi, basi wao wanapeperusha mavumbi, kisha wanaingia ndani ya kundi” (100:2-6). Hizi ndizo sifa za majeshi ya Waislamu na ni ajabu vile zinavyolingana na bishara hiyo ya Isaya tuliyoitaja hapo juu. BISHARA YA NANE Bishara nyingine bayana juu ya kufika kwa Mtume Muhammad s.a.w. imo katika Isaya 62:2. “Nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BW ANA”. Ni wazi ya kuwa bishara hii inaashiria kufika kwa dini mpya itakayopewa jina na Mungu mwenyewe katika ufunuo wake. Madaktari wa Biblia wamekosea sana kwa kudhani ya kuwa bishara hii inahusu kuundwa kwa Kanisa la Kristo. Wanasahau kwamba majina kama “Wakristo” au “ukristo” au majina yale mengine mengi ambayo makundi mbali mbali ya Wakristo wanayatumia, si majina yaliyofunuliwa na Mwenyezi Mungu, bali ni majina waliyojitungia wao wenyewe. Waila bishara hii inasema juu ya jina litakalotoka katika kinywa cha Mungu. Dini ya Kiislamu pekee ndiyo iliyopewa jina “Islamu”, kwa ufunuo wa Mwenyezi Mungu, haya yanathibitishwa na Kurani Tukufu inayosema: “Yeye (Mwenyezi Mungu) aliwaiteni Waislamu tangu zamani na katika (Kurani) hii pia” (22.79). Aya hii ya Kurani Tukufu ina uhusiano dhahiri na bishara hiyo ya Isaya. 21 Ni kana kwamba Mwenyezi Mungu anasema, “Tulibashiri tangu zamani ya kuwa jina lenu hamtajichagulia ninyi wenyewe bali litatoka Kwetu Sisi. Na leo hii basi tunawaiteni Waislamu.” Jina hili “Islamu” linatokana na neno ‘Salm’ lililo na maana ya amani. Ikumbukwe ya kuwa katika bishara nyingine Nabii Muhammad s.a.w, ameitwa “Mfalme wa amani” (Isaya 9:6). Ama hii ni bishara ya ajabu mno. Kadhalika juu ya ukweli ya kwamba miongoni mwa dini zote ni Waislamu peke yao wanaotangaza ya kuwa wamepewa jina la “Islamu” na Mwenyezi Mungu ndani ya ufunuo wake – Kurani tukufu. Isaya alitabiri kufika kwa nabii ambaye wafuasi wake watapewa jina na Mwenyezi Mungu kwa njia ya ufunuo. Nabii huyu ndiye Muhammad s.a.w. na Mwenyezi Mungu kawaita wafuasi wake “Waislamu” na dini yake “Islam”. BISHARA YA TISA Injili ya Yohana inatuambia ya kwamba Mayahudi walitazamia ufikaji wa Manabii watatu. Waliwatuma watu kumwuliza Yohana Mbatizaji, “Wewe U nani? Naye alikiri wala hakukana, alikiri kwamba mimi siye Kristo. Wakamwuliza ni nani basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? akajibu, La,” (1:19- 21). Kristo, Eliya na Nabii Yule ndio Mitume watatu waliotazamiwa kufika, waliongojewa na Waisraeli. Injili inaeleza ya kwamba Yohana Mbatizaji ndiye Eliya, (Matt.17:10-13, Luka 1: 18), na Kristo ni Yesu. Sasa amebaki mmoja, naye ni Nabii Yule, ambaye si mwingine ila ni Mtume Muhammad s.a.w. maana baada ya Kristo hakuna mtu aliyedai kuwa bishara zake zimo katika Biblia, kisha akafaulu. isipokuwa Mtume Muhammad tu. BISHARA YA KUMI Katika Yohana 14.16 imeandikwa. “Nami nitamwomba Baba naye atawapa Msaidizi Mwingine, ili akae nanyi hata milele”. Tena Yesu alisema, “Hayo ndiyo niliyowambia wakati nilipokuwa nikikaa 22 kwenu. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote na kuwakumbusha yale niliyowambia”. (Yohana 14.25,26). Tena Yesu alisema, “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahamili hivi sasa. Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awaite kwenye kweli yote” (Yohana 16:12-13). Wakristo wanasema “Msaidizi Mwingine” aliyeahidiwa kufika katika Injili ya Yohana si Mtume Muhammad, bali ni Roho Mtakatifu. Waislamu tunajibu hivi:- (i) Kama Msaidizi huyo ni Roho Mtakatifu, Yesu asingesema, “Yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu,” (Yohana 16:7). Yesu asingesema hivyo kwa sababu huyo Roho Mtakatifu wa Wakristo alikuweko duniani siku zote hata kabla ya Yesu kuzaliwa. Yesu alipobatizwa, Roho huyo alimshukia (Math. 3:16). Tena kabla ya kuwaacha wanafunzi wake aliwapulizia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu” (Yohana 20:22). Ilmuradi wanafunzi wa Yesu walikuwa na Roho huyo kabla ya kufa kwa Yesu, au tuseme, kabla hajatengana nao. (ii) Zile alama zilizobainishwa na Yesu hazipatikani katika Roho Mtakatifu, kama (a) kuwaongoza watu kwenye kweli yote na kuwakumbusha maneno ya Yesu, (b) kumtukuza Yesu (Yohana 16:14). Mtume Muhammad s.a.w. ndiye aliyekuja miaka mingi baada ya Yesu akileta sheria yenye amri nyingi za Sheria za zamani, na mengi yaliyo mapya, ili kukamilisha Sheria. Kurani yenyewe inadai kuwa ni Sheria iliyo kamili (sura 5:4.) Tena Mtume s.a.w. alimtukuza Yesu na kumkinga na masingizio yote ya Mayahudi na Wakristo, akamwonyesha kama mtu mwema asiye na dhambi, na pia kuwa hakufa kifo cha laana msalabani. Ikiwa Wakristo wangali wanaongozwa na Roho Mtakatifu, mbona basi wanayo makanisa mengi yanayopingana? Je kila 23 kanisa lina Roho Mtakatifu wake? Kisha Roho Mtakatifu wa kila kanisa anakuwa adui wa Roho Mtakatifu wa kanisa jingine? Hata watu wa kanisa moja hawachelei kuwaita Wakristo wa kanisa jingine “Wapinzani wa Kristo na watu wa Shetani.” Au je, Yesu akitoka mbinguni atakwenda kwa nani na atamuacha nani katika wale ambao wamekwisha pata ubatizo au wanaopewa misa na sakramenti nyingine mara kwa mara, lakini wanaitwa na Wakristo wa kanisa jingine “Wapinzani wa Kristo na watu wa Shetani”? Hakika ni hii ya kuwa hawana dalili yo yote ya kuhakikisha kuwa yule Roho wa kweli aliyeahidiwa ni Roho Mtakatifu wanayedhani kuwa wanaye anawaongoza. Ni jambo wasiloweza kuhakikisha; yaliyobaki ni madai ya mdomo tu. BISHARA YA KUMI NA MOJA. Katika barua aliyoandika Yuda (Yuda 1: 14-15) tunasoma maneno haya, “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao akisema, angalia, Bwana alikuja na Watakatifu wake, maelfu maelfu, ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizotenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”. Maneno ya juu yamenakiliwa toka katika tafsiri mpya ya Biblia ya Kiswahili iitwayo “Union Version”. Katika tafsiri hii mpya wameandika “Bwana alikuja na watakatifu wake maelfu maelfu” Lakini katika tafsiri za zamani katika Kiswahili, mpaka mwaka 1949 walitafsiri “Elfu kumi za watakatifu wake”. Kila mtu atafahamu ya kwamba hayo si tofauti ya maneno tu, bali maana na mradi pia vimegeuzwa. Maana bishara hiyo inabashiri kufika kwa Mtume Muhammad s.a.w. pamoja na watakatifu elfu kumi, na ilitimia wakati Mtume alipoingia Makka na idadi hiyo ya watakatifu. Hakuna Nabii ye yote aliyetimiliwa na bishara hiyo isipokuwa Muhammad s.a.w. Ni kwa sababu hiyo mapadre wamependa kubadili maneno hayo 24 ili kuwadanganya na kuwavuruga wasomao Kiswahili. Juu ya hayo Injili za Kiingereza bado zina maneno “Ten Thousand of his saints” (Elfu kumi za watakatifu wake). BISHARA YA KUMI NA MBILI. Bishara hii yenye nguvu imo katika Mathayo 21:33-40. Hii ni mojawapo ya methali za Yesu ambamo ndani yake mna utabiri wa kufika Mtume Mtukufu. Bishara yenyewe ni hii:- “Kulikuwa na mtu mwenye nyumba naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungushia ua, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara akapangisha wakulima akasafiri. Wakati wa matunda ulipokuwa karibu akawatuma watumishi wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake. Wale wakulima wakawakamata watumishi wake, huyu wakampiga na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe. Akawatuma tena watumishi wengi kuliko wa kwanza, ikawa tena vile vile. Mwisho akamtuma mwanawe kwao, akisema watamsitahi mwanangu. “Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi haya na tumwue, tuutwae urithi wake, Wakamkamata wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu atawatendaje wale wakulima? Wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya, na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake. Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Kwa sababu hiyo nawambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake. naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika , na yeyote ambaye litamwangukia litamsaga tikitiki. Wakuu wa makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao. Nao walipotafuta kumkamata, waliwaogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii.” 25 Katika methali hii iliyo nzuri Yesu ameeleza historia ya mfululizo wa kuja kwa Mitume. Ni wazi hapa kwamba shamba la mizabibu ndiyo ulimwengu, wakulima maana yake ni walimwengu kwa jumla, matukio ambayo bwana wa shamba alitaka kuvuna ndiyo wema, uaminifu na ucha-Mungu, watumishi ndiyo manabii wa Mungu waliokuja duniani mmoja baada ya mwingine; mwana ndiye Yesu aliyekuja baada ya mfululizo wa manabii wengi. Mwana huyu aliadhibiwa na wakulima. Baada ya kusema mambo haya, Yesu ameendelea kunena juu ya “Jiwe” walilolikataa waashi, hilo limekuwa “jiwe kuu la pembeni.” Jiwe lililokataliwa ndiyo wazao wa Ismaili, waliodharauliwa na wana wa Isihaka. Kulingana na bishara hii ya Yesu, mtu mmoja angekuwa jiwe kuu la pembeni – “Muhuri wa Manabii,” katika lugha mashuhuri ya Qur’an tukufu – hangekuwa nabii wa cheo cha chini, bali m’bora wa manabii atakayeleta Sheria ya mwisho na kamili toka kwa Mwenyezi Mungu. Kuinuliwa kwa Nabii toka katika nyumba ya Ismaili lilionekana jambo geni, kwani wengi katika mfululizo wa manabii wa hapo mbele walitoka katika nyumba ya Isihaka (Israel). Lakini Yesu anasisitiza ya kuwa Mwenyezi Mungu ataondoa ufalme wake kutoka nyumba ya Israeli na kuwapa wana wa Ismaili, watakaotoa matunda yake; yaani wana wa Ismaili ndiyo watakaokuwa taifa litakalodumisha ucha-Mungu na ibada ya Mwenyezi Mungu duniani. Kila mtu anaweza kuona hapa ya kuwa hapana mtu yeyote aliyedai utume baada ya Yesu, na akafanikiwa, isipokuwa Mtume mtukufu Muhammad s.a.w. Ni yeye ambaye mafundisho yake yalihitilafiana na dini ya Mayahudi na akavunja kabisa nguvu za dini hiyo. Ni yeye ambaye taifa lake lilidharauliwa na kuchukiwa. Kama tulivyosema hapo mbele, nabii Muhammad s.a.w. ndiye mjumbe wa Mungu wa pekee aliyejaaliwa kushinda maadui zake wote katika uhai wake, hivyo ni yeye tu ambaye ndiye lile jiwe ambalo yeyote aliyeanguka juu yake alivunjika-vunjika na yeyote liliyemwangukia likamsaga tikitiki. Wakristo wamekosea sana kwa kudhani Yesu ndiye “Jiwe” linalotajwa hapa. Lakini wanasahau ya kuwa Yesu alikuwa Mwisraeli, hali yeye amesema “Ufalme wa 26 Mungu utaondolewa kutoka kwa Waisraeli na kupewa taifa jingine,” yaani Waismaili. Isitoshe, ikiwa jiwe ni Yesu, basi ingefaa kufahamishwa aliwasaga akina nani tikitiki? BISHARA YA KUMI NA TATU. Katika Mathayo 23:38-39 tunasoma “Angalieni nyumba yenu imeachwa hali ya ukiwa. K wa maana nawaambieni, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.” Aya hii inaashiria ya kuwa Yesu ataachana na watu wake nao hawatamwona tena mpaka wao watakaposema “Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana”. Kadhalika, hapa pamebashiriwa majilio mawili. Moja baada ya kifo cha Yesu, na hili lingekuwa kama Mungu mwenyewe kuja duniani. Jingine ni kuja kwa Yesu mara ya pili. Kama inavyobainishwa na bishara yenyewe, yule ajaye kwa jina la Bwana atafika kabla ya kurudi kwa Yesu mara ya pili. Tumekwisha eleza ya kuwa yule ajaye kwa jina la Bwana anafanana na Musa. Hivyo bishara hii ya Yesu ikiambatana na ukweli wa kuja kwa Mtume Muhammad s.a.w. na dini ya Kiislamu, inathibitisha ya kuwa katika mpango wa Mwenyezi Mungu. Yesu hakuwa nabii wa mwisho na wala kuja kwake hakukusudiwa kumfikisha mwanadamu kwenye kiwango cha mwisho cha maendeleo ya kiroho. Kazi hii angeifanya “Yule ajaye kwa jina la Bwana,” ambaye ndiye angekuwa msingi wa maendeleo makubwa ya kiroho. Ingekuwa upotevu dhahiri kufikiri ati baada ya kuja “Yule ajaye kwa jina la Bwana” Yesu angerudi tena ili apate sifa ya kuwa nabii aliye chanzo cha maendeleo ya upeo katika dini ya Mwenyezi Mungu. Yesu mwenyewe analiweka jambo hili wazi mbele ya macho yetu anaposema. “Hamtaniona kamwe tangu sasa mpaka mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana” (Mathayo 23:39). 27 Ikumbukwe pia ya kuwa Yesu hakuwa nabii mleta Sheria, bali alikuwa masihi wa nabii Musa na alikuja kutilia nguvu Sheria ya Musa. Hivyo katika bishara hii Yesu anawatangazia watu wake akisema. “Wala hamtamwona nabii na Masihi kama mimi mpaka atakapokuja nabii mfano wa Musa kwanza, nanyi muwe wenye kumkubali.” Hivi ni kama kusema hapana Masihi ila kwanza aje nabii mleta sheria mpya. Kadhalika maneno haya yatathibitisha ya kuwa mpango wa Mwenyezi Mungu wa kuleta manabii duniani katika muda uliowekwa si jambo lenye kikomo. Ama ndugu Wakristo wanaipotosha sana bishara hii ya Yesu ya kuendelea kwa unabii, kwani wao husema hapana nabii baada ya Yesu. Tukirudia sehemu ya pili ya bishara yenyewe, yaani kuja kwa Yesu mara ya pili, tunaona ya kuwa ni wale tu ambao kwanza watamkubali Nabii mfano wa Musa atakayetangulia kurudi kwa Yesu, ndio watakaomwona na kumtambua Yesu arudipo duniani. Asiyemkubali yule nabii aliye mfano wa Musa, hataweza kutambua kurudi kwa Yesu. Kwa nini? Kwa sababu Yesu arudipo duniani atakuwa miongoni mwa wafuasi wa yule nabii mfano wa Musa. Hivyo ni wazi kuwa watu miongoni mwa wale watakaokuwa wamemwamini yule nabii mfano wa Musa, wataweza kukubali na kutambua kuja kwa Yesu mara ya pili. Yesu ajapo mara ya pili hatakuwa nabii mwenye kujitegemea, bali atakuwa mfuasi mwaminifu na kielelezo kilicho bayana cha yule nabii mfano wa Musa. Na daraja la mwisho la wokovu wa mwanadamu halina chanzo chake ila ni pale alipofika yule nabii mfano wa Musa – na Yesu ajapo atakuwa masihi wa nabii huyo naye ataitilia nguvu Sheria yake. Baada va kutoa maelezo juu ya majilio mawili vanayoashiriwa katika bishara hii ya Yesu. sasa panabaki swali moja kujibiwa ili kutimiza muradi wa bishara yenyewe. Swali lenyewe ndilo hili. Je, ni mtu gani aliyedai unabii na akafaulu baada ya kifo cha Yesu? Ni ukweli unaokubaliwa na kila mwenye kujua ya kuwa hapana mtu hata mmoja aliyedai kuwa nabii wa Mungu kwa walimwengu na akapata ufanisi, baada ya Yesu, ila Muhammad s.a.w. Mtume 28 Mtukufu wa Uislamu. Nabii Muhammad s.a.w. ndiye aliyekuwa mfano kamili wa nabii Musa. Miongoni mwa ishara tukufu zinazotubainishia ukweli wa jambo hili, ni ile Sheria mpya, Kurani tukufu, aliyopewa Mtume Muhammad s.a.w. ili kuwa mwongozo kwa watu wote. Katika sifa hii manabii wawili, Muhammad na Musa (amani na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao), wanafanana. Nabii Musa alipewa Sheria ya Mungu -Torati, ambayo kwa kuitimiza Yesu alikuja. (Mathavo 5:17); lakini baadaye akabashiri kufutika kwa Sheria hiyo kwa kusema: “Kwa sababu hiyo nawaambia Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa jingine lenye kuzaa matunda yake” (Mathayo 21:43). Kwa hivyo, maneno haya ya Yesu aliyowaambia wana wa Israeli, hayapingi ukweli huu kwamba nabii Musa na nabii Muhammad wamefanana sana. Naam, na Muhammad s.a.w. ndiye nabii yule aliyetabiriwa na Yesu kuja kwa jina la Bwana. Nabii Muhammad s.a.w. alifunuliwa kila jambo kwa jina la Mwenyezi Mungu. Sura zote za Kurani tukufu zaanza kwa jina la Mwenyezi Mungu. Isitoshe yeye mwenyewe Mtume Muhammad s.a.w. alianza kila jambo kwa jina la Mwenyezi Mungu. Na kama kila mwanadamu afuate mfano huu mtukufu – kama itakavyokuwa katika siku za ushindi wa dini ya Kiislamu – basi hapo dunia nzima itajaa fahari ya jina la Bwana. Ndipo Yesu akawataka watu wake waseme, “amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana,” na kumkubali Mtume wa Uislamu. Ni wale tu miongoni mwa watu wa Yesu, watakaofuata maagizo haya na kusilimu, ambao watapewa nuru katika macho yao ya kiroho nao wataweza kumwona na kumtambua Yesu arudipo. Ni lazima ikumbukwe ya kuwa kuja kwa Yesu mara ya pili baada ya kufika yule nabii Mfano wa Musa. siyo maana yake ya kuwa ni Yesu yule yule wa Nazareti, ambaye atashuka kutoka mbinguni kama wadhanivyo Wakristo. La, hasha. Muradi sahihi wa kurudi kwa Yesu, au masihi, mara ya pili ni kwamba kutakuja nabii mfano wa Yesu kuja kutilia nguvu sheria ya nabii Yule, mfano wa Musa, kama vile Yesu mwenyewe alivyokuja kutilia nguvu sheria 29 ya Musa. Yaani, kama vile nabii Musa na Muhammad s.a.w. wanavyofanana kwa kuleta Sheria. vivyo hivyo Yesu na masihi wa nabii Muhammad wanafanana kwa kutoleta sheria – bali kutilia nguvu sheria iliyopo. Kama tulivyosema hapo mbele, kule kurudi kwa Yesu mara ya pili kunakotajwa katika bishara hii kunathibitisha ya kuwa mlango wa utume haukufungwa na hivyo manabii wa Mungu wataendelea kuletwa duniani pakiwa na haja. Na Yule mjumbe aliyetabiriwa kuja baada ya nabii aliye Mfano wa Musa, angekuja kufanya kazi kama ya Yesu na angekuwa mfano wa Yesu. Wale wanaosema ati ni Yesu yule yule wa Nazareti atakayeshuka toka mawinguni, wanakosea sana. Yesu alikufa fofofo. Kufuatia sheria za Mwenyezi Mungu za maumbile, wafu hawarudi tena duniani. Ni sheria hizi ambazo zimepiga marufuku kwamba mtoto azaliwe na kisha kurudi tena tumboni mwa mamaake. Hivyo ile ndoto ya kuwa Yesu wa Nazareti atarudi tena duniani na kuwa Masihi wa Nabii Muhammad s.a.w. haitatimia kamwe. Isitoshe, wazo hili la kipagani, lina maana ya kwamba Mwenyezi Mungu (Mungu apishe mbali) hawezi kuumba tena, kwani kashindwa kuumba nabii mwingine mfano wa Yesu hata ikamlazimu kumfufua Yesu, mwana wa Mariamu, na kumleta tena duniani awe masihi wa nabii Muhammad s.a. w. Bila shaka wazo hili lenye makosa litakataliwa na kila mwenye akili. Mtu anaweza kuuliza, na mambo yakiwa hivi basi Yesu atarudi duniani kwa njia gani? Kurudi au kudhihiri kwa Yesu mara ya pili, kungetokea kwa njia ya kawaida tu. Yeye angezaliwa kama vile walivyozaliwa manabii wengine wa Mwenyezi Mungu. Pia kuna alama nyingi, kama tutakavyoona baadaye, zilizotabiriwa ili kutujulisha wakati hasa atakapofika, na pia kutuwezesha kumtambua. Jambo lenye maana sana ni kukumbuka ya kuwa Yesu ajapo tena hatakuwa nabii mwenye kujitegemea, bali atakuwa mfuasi mwaminifu na kielelezo safi cha yule nabii Muhammad s.a.w. 30 KUJA KWA NABII MUHAMMAD S.A.W. Kwa fadhili za Mwenyezi Mungu bishara zote tulizozieleza katika kitabu hiki zilitimia barabara kwa kuja kwake nabii Muhammad s.a.w. Biblia na Kurani tukufu vyote vinasema nabii Muhammad ni wa damu ya Nabii Ibrahim a.s. Biblia yasema nabii Ibrahim alikuwa na wake Watatu-Sarah. Hajira na Katura. Hajira alimzaa Ismaili na Sarah akamzaa Isihaka. (Mwanzo. 16:10-12 na 17:19). Isihaka aliishi nchi ya Kanani na ndiye baba wa Mayahudi. Kufuatia ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Ibrahim manabii wengi na hata wafalme walizaliwa katika nyumba au kizazi cha Isihaka, kama vile Musa, Haruni, Joshua, Isaya, Daudi, Suleimani na Yesu (Mungu awe radhi nao). Ismaili aliishi katika nyika za Parani, yaani Arabu. Kufuatia ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Ibrahim, Ismaili alikuwa baba wa watoto 12 wanaume. Siku za utoto wa Ismaili, nabii Ibrahim aliamriwa na Mwenyezi Mungu kumchukua mwanawe pamoja na mkewe Hajira na kuwaacha katika bonde tambarare la Makka. Ibrahim akafanya hivyo, naye akamchukua mwanawe hali yu mdogo na kumwacha na mama yake pamoja na chakula kidogo katika bonde tambarare karibu na Kaaba. Kwa mara kadha Bi Hajira alimwuliza nabii Ibrahim kwa nini anafanya hivyo? Safari ya mwisho nabii Ibrahim akaitikia kuwa anafanya hivyo kwa amri ya Mungu. Hajira akasema kama ni hivyo, basi, Mwenyezi Mungu hawezi kutuangamiza. Nabii Ibrahim aliondoka pale na akiwa mbali kidogo na mkewe na mwanawe alielekea Kaaba na kuinua mikono yake juu akaomba dua hii, “Mola wetu, hakika mimi nimewakalisha baadhi ya wazao wangu katika bonde lisilozaa karibu na Nyumba yako tukufu, Mola wetu, ili wasimamishe sala. Basi Ujaalie mioyo ya watu ielekee kwao na Uwaruzuku matunda ili wapate kushukuru” (Kurani Tukufu 14:38). Baada ya nabii Ibrahim kuondoka, na chakula na maji kuwaishia Bi Hajira na mwanawe Ismaili walisikia sana kiu. Hapo Hajira akahangaika sana kutafuta maji. Katika kufanya hivyo 31 alipanda na kushuka vilima viwili mara kadha. Vilima hivi ndivyo Safaa na Marwa. Baadaye alijitupa kwa Mwenyezi Mungu na akaomba sana. Maombi yake yalikubaliwa na Mwenyezi Mungu akabubujisha chemchem ardhini karibu na mahali alipokuwa Ismaili. Maji hayo yalibubujika kwa mlio wa “Zam, Zam, Zam”. Mpaka hivi leo kisima hiki kitakatifu kinaitwa Zam-Zam. Baadaye Mwenyezi Mungu alimwamuru nabii Ibrahim kujenga tena Kaaba, ambayo ndiyo nyumba ya kwanza kujengwa kwa ajili ya ibada ya Mungu mmoja. Kazi hii aliifanya pamoja na mwanawe lsmaili ambaye sasa alikuwa mtu mzima. Walipokuwa wakijenga, nabii Ibrahim na Ismaili waliomba dua hii kwa Mungu: “Ee Mola wetu, Utupokelee, hakika Wewe Ndiwe Mwenye kusikia, Mwenye kujua. Ee Mola wetu, Utufanye tuwe tujitupao Kwako, na miongoni mwa wazao wetu pia Uwafanye watu wajitupao Kwako, Na Utuonyeshe njia za ibada yetu na Utuelekee, bila shaka Wewe ndiwe Mwelekevu, Mrehemevu. Ee Mola wetu, mwinue Mtume kati yao atokaye miongoni mwao, awasomee Aya Zako, na kuwafundisha Kitabu na hekima, na kuwatakasa. Hakika Wewe ndiwe Mwenye nguvu, Mwenye Hekima.” (Kurani Tukufu, 2′:128-130). Miongoni mwa watu waliovutiwa na Kaaba na kuhamia Makka ni kabila la Jurhum. Mtemi wao mkuu aliitwa Madhadh mwana wa Amr. Ismaili na mamaake Hajira (Mungu awe radhi nao) ndio waliokuwa wakaazi wa kwanza wa Makka. Ismaili alimwoa binti wa Mtemi huyu na akazaa naye wana 12. Majina yao ndiyo haya. Nebayothi, Kedari, Abduli, Milesamu, Mishma, Duma, Masa, Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kadema (Mwanzo. 25:13-16). Hawa ndio waliokuwa wakuu wa makabila ya Waarabu waliotawanyika katika Bara Arabu au Paran. Waarabu wengi hudai kuwa wa ukoo wa Kedari mwana wa Ismaili. Tangu hapo zamani Waarabu waliiheshimu sana Kaaba na mila ya Ibrahim nayo waliilinda sana. Baada ya kufariki Ismaili ulinzi wa Kaaba ukawa 32 mikononi mwa Nafishi (Nabit). Alipofariki Nafishi Kaaba ikawa inalindwa na babuye Madhadh, na hivyo kwa muda mrefu kabila lake Jurhum likawa ndilo lenye kutawala sehemu hiyo ya nchi takatifu. Utawala huu baadaye ulirudi mikononi mwa wazao halisi wa Ismaili kwa njia ya shujaa mmoja aitwaye Qusaiyy. Yeye alikuwa mtu mwenye maarifa sana na aliweza kuwakusanya watu wengi wa ukoo wa Ismaili chini ya serikali moja. Akaupa heshima zaidi mji wa Makka na kulinda kwa uangalifu sana nyumba ya Mungu yaani Kaaba. Ujasiri na maarifa yake yaliwafanya watu wake wampe jina la Kuraishi yaani mkusanyaji. Hilo ndilo jina la kabila miongoni mwao alimozaliwa Mtume Muhammad s.a.w. kama alivyoomba nabii Ibrahim a.s. Ni wazi kutokana na maelezo haya kuwa nabii Muhammad s.a.w. ni wa damu ya baba wa manabii, Ibrahim. Naye alikuja ulimwenguni baada ya Wana wa Israeli kumsahau Mwenyezi Mungu na kuyatupilia mbali mafundisho ya Musa. Kadhalika walivunja maagano ya nabii Ibrahim na Mwenyezi Mungu ya kwamba kila mtoto wa kiume ni lazima afanyiwe tohara. Hivyo ufalme wa Mwenyezi Mungu ukaondolewa kwao na ukapewa taifa jingine. Taifa hili ni taifa la wana wa Ismaili ambao waliyaheshimu maagano tuliyoyataja na wakawatahiri wanaume wao. Hii ni alama ya kimwili kuonyesha utii kwa Mwenyezi Mungu kama alivyofanya nabii Ibrahim. Na katika utii wa kiroho tunaona ya kuwa nabii Ibrahim na mwanawe Ismaili, baba wa Waarabu, waliomba Mungu ainue mtume miongoni mwa wazao wao atakayewafundisha Kitabu. hekima na kuwatakasa. Kama matokeo ya dua hii, Mwenyezi Mungu alimwinua nabii Muhammad s.a.w. kutoka miongoni mwa wazao wa Ismaili. Akampa kitabu (Kurani Tkufu) hekima na ucha – Mungu ili kuwaletea walimwengu utii wa kiroho, hekima, na utakaso ambao ndiyo matunda hasa ya ufalme wa Mungu ulioondolewa kutoka kwa wana wa Israeli. Mtume s.a.w. mwenyewe amesema, “Mimi ndiyo dua ya Ibrahim” (Jarir na Asakir). 33 Nabii Muhammad s.a.w. alizaliwa tarehe 20 April, 571 A.D. Kabila lake lilikuwa Kuraishi na ukoo wake Banu Hashim. Akiwa mtoto yatima alianza maisha yake kwa unyonge. Katika ujana wake alikuwa mwaminifu hata akaitwa “AL-Amin”. Ingawa ibada ya masanamu ilistawi sana wakati huo, yeye hakupata kuyaabudu hata mara moja na aliyachukia sana. Alipopata umri wa miaka 40 alipewa cheo cha utume. Na kama walivyotabiri Yesu na manabii wengine wa zamani, akapewa Sheria mpya (Kurani Tukufu). Yeye pamoja na wafuasi wake waaminifu walitaabishwa sana na maadui zao hata baadaye wakalazimika kuhamia Madina. Huko walistawi sana. Wakapigana vita na maadui wachokozi na kwa fadhili za Mwenyezi Mungu maadui hao waliangamia wote. Baadaye akiwa na wataktifu wake 10,000 nabii Muhammad s.a.w. aliushika mji wa Makka bila ya kumwaga damu. Maadui zake wote wakaletwa mbele yake hali ni wenye kukata tamaa. Yeye aliwasamehe wote. Kabla ya kuaga dunia alikuwa amepata ufanisi mkubwa ajabu. Wala hapana nabii mwingine aliyefanikiwa hivyo akiwa hai. Na alipofariki bara zima la Arabu lilikuwa limeingia katika dini ya Mwenyezi Mungu ya Uislamu, yaani “Kujitupa kwa Mwenyezi Mungu” kama alivyoomba nabii Ibrahim a.s. Naam, huyu ndiye Muhammad mtume na nabii wa Mungu aliyepewa Sheria na pia akahama mji wake kuepa uovu wa maadui na baadaye akafaulu sana na akafa hali yu Mfalme na mpendwa wa Walimwengu. Katika haya yote alifanana sana na nabii Musa – la, bali yeye alikuwa mfano halisi wa nabii Musa. Wale ndugu zetu wanaodhani kuwa nabii anayetabiriwa katika bishara ya Mathayo 23:39 ni nabii mwingine wala si nabii Muhammad s.a.w., basi watuambie ni nabii yupi aliyetabiriwa kuja kwa jina la Bwana baada ya Yesu? 34 SEHEMU YA PILI HADHRAT AHMAD A.S. MASIHI WA MTUME MUHAMMAD S.A.W. Madhumuni ya makala hii haitatimia kama nisitaje hapa, kwa ufupi, kuja kwa Masihi, mfano wa Yesu, katika umati wa Mtume Mtukufu Muhammad s.a.w., ambaye ameahidiwa na Mtume mwenyewe. Ikumbukwe hapa ya kuwa Mtume Muhammad s.a.w. amefananishwa na Musa ndani ya Kurani Tukufu. Kama nabii Musa alileta sheria mpya na Mtume Muhammad s.a.w. pia alileta sheria mpya. Mwenyezi Mungu anasema :- “Hakika Sisi Tumewatumieni Mtume aliye shahidi juu yenu kama Tulivyompeleka Mtume kwa Firauni” (Kurani Tukufu 73:16). Aya hii inatuambia wazi wazi ya kwamba Mtume Muhammad s.a.w. anafanana na nabii Musa. Kwa hiyo imelazimishwa ya kwamba kama alivyodhihiri Masihi mmoja katika umati wa Musa ndivyo hivyo atakavyotokea Masihi mwingjne katika umati wa Mtume Muhammad s.a.w. vile vile; na kwa ajili hii Mtume Muhammad s.a.w. alisema ya kwamba:- “Wawezaje kuangamia umati ambao mwanzoni mwake nipo mimi na mwishoni mwake atadhihiri Masihi”. (Ibni Maja). Kurani Tukufu vile vile inaashiria juu ya kufika kwa Masihi mmoja katika umati wa Mtume Muhammad s.a. w. Katika aya hii:- “Na anapotajwa mwana wa Mariamu kwa namna ya mfano (Yaani mfano wake atafika) ndipo watu wako wanaupigia kelele” (Kurani Tukufu 43:58). Sasa ni wazi ya kwamba wafuasi wa Mtume Mtukufu Muhammad s.a.w. waliahidiwa kuja kwa Masihi, mfano wa mwana 35 wa Mariamu. Agano jipya la Biblia vile vile linatuambia ya kwamba Masihi mwana wa Mariamu atarudi duniani mara nyingine (Mathayo 24:4-41). Sasa juu ya kuja Masihi mfano wa Yesu tunaona kuwa bishara hii ya Biblia, Kurani Tukufu na hadithi ya Mtume Muhammad s.a.w. ilitimia kwa ufikaji wa Hadhrat Ahmad a.s. wa Qadian. Kama tulivyoona, kuja kwa Masihi wa nabii Muhammad s.a.w. kumefananishwa na kurudi kwa Yesu mara ya pili. Kazi ya Masihi huyu ingekuwa kuimarisha na kutilia nguvu Sheria ya yule nabii mfano wa Musa. Tumeona kuwa nabii huyu si mwingine ila nabii Muhammad s.a.w. Na masihi wake si mwingine ila Hadhrat Ahmad. Hadhrat Mirza Ghulam Ahmad a.s. alizaliwa katika kijiji cha Qadian, India, mnamo Febuari 13, 1835. (14 Shawwal, 1250.) Babu zake walitokea Uajemi. Tangu utotoni Hadhrat Ahmad a.s. alionyesha alama za utukufu na alitumia wakati wake mwingi katika kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusoma Kurani Tukufu na vitabu vingine vya dini. Alichukizwa sana kuona Uislamu unavyotukanwa na maadui zake, hususa Wakristo na wafuasi wa dini ya Kibaniyani (Arya Samaj). Waislamu walikuwa katika hali ya nyuma na kutojali dini yao hivi kwamba walishindwa kuyapinga mashambulio maovu ya maadui wa Uislamu. Hadhrat Ahmad a.s. kwanza aliandika makala magazetini kuutetea Uislamu. Baadaye aliona nabii Muhammad s.a.w. katika ndoto. Jambo hili lilimtia moyo na akaandika kitabu maarufu sana kiitwacho Baraahine Ahmadiyya. Katika kitabu hiki Hadhrat Ahmad a.s. alitoa hoja madhubuti kurudisha mashambulio ya maadui wa Uislamu hata mtu yeyote hakuthubutu kuzijibu hoja zake. Katika mwaka wa 1890 Mwenyezi Mungu alimfunulia kwamba yeye ndiye Masihi aliyeahidiwa na pia Mahdi. Wakristo, Wa-Arya Samaj na mashekhe wa Kiislamu wote wakaungana 36 pamoia kumpinga Seyidna Ahmad a.s. alipotangaza jambo hili. AIifanya mijadala mingi iuu ya mas’ala ya dini na akawabwaga wapinzani wake wote vibaya sana kwa hoja zake zenye nguvu juu ya ubora wa dini ya Kiislamu. Watu waliompinga wakazidisha uovu wao hata wakamfikisha kortini kwa mashtaka ya uwongo ya kuua. Huu ulikuwa mwaka wa 1894 ambapo ile ishara mashuhuri ilivyotabiriwa zamani ilitimia kuthibitisha kufika kwa Masihi aliyeahidiwa. Ishara hii ilikuwa kupatwa kwa jua na mwezi katika mwezi wa Ramadhan. Hadhrat Ahmad akajulishwa kabla na Mwenyezi Mungu kuwa atashinda kesi yake. Hivyo ndivyo ilivyotokea na Colonel Douglas aliyeisikiliza kesi hiyo hakumpata Seyidna Ahmad a.s. na kosa lolote Jaji huyu mwenye haki alipewa jina Pilato. Jumuiya ya Ahmadiyya ikazidi kupata nguvu. Mwaka wa 1908 kikapigwa chapa kitabu chake mashuhuri kiitwacho “Yesu katika India” (Jesus in India). Katika kitabu hiki alithibitisha kwa ushahidi kwamba Yesu aliepuka kifo cha laana cha msalaba na akasafiri hadi Kashmir, India. Huko akawahubiria wana wa Israeli walioishi kule na baadaye akafa na akazikwa huko mtaa wa Khanyar, Srinagar. Kashmir. Kwa kufuatia ufunuo wa Mwenyezi Mungu. Hadhrat Ahmad aliligundua kaburi la Yesu. Hadhrat Ahmad a.s. alibashiri maafa ya tauni. matetemeko na vita vitano vikuu vya dunia. Maafa haya yote yalitokea kama alivvobashiri. Matetemeko ya dunia bado yanaendelea kadhalika vita viwili vimekwisha tokea na vingine vimebakia. Mwaka 1903 pakatokea nabii wa uwongo aliyeitwa Dr. J. A. Dowie wa Amerika. Mtu huyu alijidai kuwa yu Eliya aliyerudi mara ya pili duniani. Seyidna Ahmad a.s. alimwandikia barua na humo akamwomba Mwenyezi Mungu amwangamize yule aliye mwongo na mzushi baina ya watu wawili hao na amwache hai yule mkweli (wakati huo Hadhrat Ahmad alikuwa miaka 15 zaidi na akiwa na 37 afya si nzuri kuliko Dr. Dowie). Mzushi huyu wa Amerika alirudisha majibu ya ujeuri na matusi na tangu hapo utajiri wake na wafuasi wake wakaanza kupungua. Alikufa mwaka wa 1907 akiwa maskini asiye na rafiki wala wafuasi. Mji wake wa Zion aliouanzisha ulififia na mauti yalimvamia hali yu mwenda wazimu aliyepooza. Hadhrat Ahmad aliendelea na mahubiri kwa nguvu sana na wafuasi wake wakazidi kuongezeka. Katika mwaka wa 1904 alitangaza kwamba Krishna, Buddha na wengineo walikuwa ni mitume wakweli wa Mwenyezi Mungu, kwani kila taifa lilipelekewa mjumbe ila tu, mafunzo ya wajumbe hao kama vile ya Yesu yalichafuliwa na watu wa baadaye. Mwaka wa 1905, kulitokea tetemeko kubwa la dunia lililoleta vifo vingi katika sehemu kadha za India. Tetemeko hili lilipotukia Hadhrat Ahmad alikuwa akiandika maneno haya ya ufunuo wake “Mwonyaji mmoja alifika duniani, lakini dunia haikumpokea, lakini Mwenyezi Mungu atampokea na atadhihirisha ukweli wake kwa mashambulio makali.” Miongoni mwa bishara zake maelfu kuna utabiri juu ya mabalaa na maafa mengi ulimwenguni tangu mwaka wa 1914 ambayo mwisho wake ataangamizwa yule “Dajjal” aliyetajwa na nabii Muhammad (s.a.w.) – na huu ni utawala wa kinyama, kufuru, uasherati na madhambi – kisha mwishowe Uislamu utashinda na kutawala milele. Akiongea juu ya vita vya tatu vya dunia Hadhrat Ahmad alitabiri kuwa vitakuwa vikali hivi kwamba vitakaribia kuangamiza uhai wote ulimwenguni lakini Uingereza hata kama itapata hasara kubwa, itakuwa miongoni mwa washindi. (Haqiqat-ul-Wahi). Mnamo mwaka huo huo Hadhrat Ahmad alijulishwa na Mwenyezi Mungu kuwa umri wake umekaribia kwisha. Hata hivyo hakupuuza kazi zake tukufu za kuitetea dini ya Kiislamu na kubomoa misingi ya dini za uwongo. Alianza kuandika kitabu chake cha 80 kiitwacho “Paeghame Sulha” – yaani Ujumbe wa Amani, lakini tarehe 20 mwezi Mei 1908 Mungu alimkumbusha tena kwamba mwisho wake wakaribia. 38 Yapata saa nne u nusu asubuhi tarehe 26 Mei, mwaka wa 1908 alitamka maneno haya mara mbili “Mpenzi Mola Wangu” na akafariki mwenye umri wa miaka 74. Na huyu ndiye aliyekuwa Ahmad Masihi aliyeahidiwa kuja siku za mwisho kama mfano wa Isa mwana wa Mariamu. Jambo la kustaajabisha ni ule mlingano uliopo katika nyakati walizofika wajumbe hawa watukufu wa Mwenyezi Mungu, Musa, Yesu, Muhammad na Ahmad (amani na baraka za Mungu ziwe kwao wote). Tukichukua silsila ya nabii Musa tunaona yeye mwenyewe alizaliwa yapata 1275 B.C. Na masihi wake Yesu, akazaliwa yapata miaka 1269 baada ya hapo. Na tuchunguapo silsila ya nabii Muhammad s.a.w. tunakuta ya kwamba alizaliwa 570 AD., na Masihi wake aliyeahidiwa, Hadhrat Ahmad, akazaliwa 1835 AD., miaka 1265 baadaye. Hivyo tukilinganisha silsila hizi mbili tunaona pana muda sawa unaomtenganisha Yesu kutoka kwa Musa na Ahmad kutoka kwa nabii Muhammad s.a. w. Hii yatosha kwa wenye akili kutambua jinsi bishara tulizotaja zilivyotimia sawa sawa. Hapana shaka ya kuwa mtu anayemkataa nabii Muhammad anamkataa Yesu na Biblia yote kwa jumla, kwani bishara zote tulizozichunguza tumeona zimetufikisha kwenye ukweli usioepukika wa nabii Muhammad s.a.w. Sasa ni juu ya wenye akili kutafakari juu ya jambo hili na kutupilia mbali karaha zao zisizo na msingi ili kuifuatia njia iliyonyoka – “Islamu”. BISHARA ZA KUJA KWA MAHDI ALIYEAHIDIWA. 39 BISHARA ZA KUJA KWA MAHDI ALIYEAHIDIWA Hapa chini tunanakili baadhi ya bishara nyingi alizotabiri nabii Muhammad s.a. w. juu ya kufika kwa Masihi na Mahdi. Tunatumai ya kuwa b LikeLike
  62. chidy rakim says:

    BISHARA ZA KUJA KWA MAHDI ALIYEAHIDIWA
    Hapa chini tunanakili baadhi ya bishara nyingi alizotabiri nabii
    Muhammad s.a. w. juu ya kufika kwa Masihi na Mahdi.
    Tunatumai ya kuwa bishara hizi zitaondolea mbali shaka yo yote
    katika nyoyo za watafutao haki.
    1. Hakika Mwenyezi Mungu atamwinua kwa ajili ya umati huu
    mwanzoni mwa kila karne yule Atakayehuisha upya Dini na
    kuitilia nguvu” (Abu-Daud, Ja1ada 2, uk. 241). Hadhrat
    Ahmad a.s. ndiye mtu wa -pekee kudai kuwa Mujaddid wa
    kame ya kumi na nne.
    2. Masihi aliyeahidiwa ataitwa “Nabiyyullah” (Nabii wa Mungu)
    (Muslim, Jalada 2, uk. 515).
    3. Huyo Mahdi na Masihi atakuwa yule yule mtu mmoja (Ibni
    Majah, Jalada 2, uk. 257).
    4. Kuja kwa Yesu mara ya pili kutakuwa katika njia ya Imam
    kutokana na Waislamu wenyewe (Bukhari, Jalada 2, uk 490).
    5. Huyo Masihi ataua nguruwe na kuvunja msalaba. (Bukhari,
    Jalada. 2. uk. 159). Bishara hii inaonyesha ya kuwa Masihi
    atawaokoa Waislamu toka katika upotevu na kudhihirisha
    ubovu wa imani ya Kikristo.
    6. Huyu Mahdi atafutilia mbali vita vya kidini (Musnad Ahmad
    Ibni Hanbal, Jalada 2, uk. 411).
    7. Katika wakati wa Mahdi elimu itatapakaa na kuzidi mno, na
    watu watachanganyana zaidi. (Tirmidhi).
    8. Katika wakati huo, kutabuniwa njia mpya za usafirishaji na
    ngamia watakuwa wenye kuachwa (Mishkat-ul-Masabih).
    40
    9. Imani itapungua na hapatabaki cho chote katika Uislamu ila
    jina tu nayo Kurani tukufu itabakia maandiko matupu
    (Mishkat-ul-Masabih. uk. 38. Kanz-ul-Ummal. Jalada. 6. uk.
    43).
    10. Waislamu watakaposikia kufika kwa Mahdi basi yawapasa
    wafanye haraka kuungana naye hata kama katika kufanya
    hivyo itawalazimu kutambaa juu ya barafu ili kufika aliko
    yeye. (Kanz-ul-Ummal, pia maelezo ya Ibni Hanbal, Musnad,
    Jalada. 6. uk. 29. 30).
    11. Mataifa ya Kikristo yatakuwa yenye nguvu nyingi
    ulimwenguni. (Hujajul Karama. Tirmidhi na vinginevyo).
    12. Wakati huo mwezi na jua vitapatwa katika mwezi ule ule wa
    Ramadhani (Dar-Qutni. Sunan, Jalada. 8. uk. 188). Jambo
    hili lilitukia mnamo tarehe 13 na 28 mwezi wa Ramadhani
    mwaka 1894.
    13. Atakuwa na masahaba 313 (Ghayat-ul-Maqsud). Hivi ndivyo
    ilivyokuwa, na majina ya hao masahaba 313 yamehifadhiwa.
    14. Atakuwa mmoja wa mapacha (Ibni Arabi. Sharah Fusus-ul-
    Hikam). Hadhrat Ahmad a.s. alizaliwa pacha lakini dadake
    akafariki baada ya kuzaliwa.
    15. Atawakumbusha watu mafundisho ya Yesu (Kurani Tukufu.
    61:7).
    16. Wakati huo kutatokea tauni (Ikmal-ud-Din. uk. 348). Tauni
    iliambukia mwaka 1902 A.D.
    17. Masihi atadhihiri upande wa mashariki (Ibni Majah).
    18. Atadhihiri katika mahali paitwapo Kadaa (Jawahir- ul-asrar.
    uk. 56). Wenyeji wa zamani wa Kadian hupaita Kadaa.
    41
    19. Atatokana na ukoo wa Kiajemi (Bukhari. Bab-ul-fitan).
    20. Wakati huo kutakuwa na Manabii wa uwongo (Bukhari,
    Bab-ul-Fitan, Muslim Bab-ul Fitan).
    21. Uislamu utakuwa na karne tatu za utukufu, kisha utapaa
    mbinguni kwa miaka elfu moja (Bukhari. Jalada, 4 juu ya
    Kurani tukufu 86:2). Ndiyo kusema ustawi wa pili wa Uislamu
    utaanza mwanzoni mwa karne ya kumi na nne ya Hijrah.
    (Ahmad – The Promised Messiah and Mahdi. uk. 13, 14).
    Hapo juu tumetaja baadhi ya hadithi za Mtume Muhammad s.a.
    w. juu ya kufika kwa Masihi na Mahdi aliyeahidiwa. Masihi na Mahdi
    huyu atakuwa mfuasi wa Nabii Muhammad s.a.w. naye atakuwa
    ni mfano wa Yesu – hata ataitwa Isa bin Mariamu. Akitaja juu ya
    jambo hili Mtume s.a.w. alisema “Mtakuwaje atakaposhuka mwana
    wa Mariamu kati yenu naye ndiye Kiongozi wenu atakayetokana
    nanyi! (Bukhari).
    Hivyo kuja kwa Yesu mara ya pili si jambo lililo na shaka hata
    kidogo. Bali lilitimia katika umati wa “yule ajaye kwa jina la Bwana”
    yaani Muhammad s.a.w.; na umati huu ni wenye kudumu milele.
    Hata Mtume s.a.w. akasema: “Umati ulio na mimi upande mmoja
    na Masihi mwana wa Mariamu upande wa pili hauwezi kuangamia”.
    (Ibni Majah).
    Mwishoni mimi nawaomba watu wote kutafakari kwa bidii juu ya
    madhumuni ya kitabu hili; hususa juu ya sehemu yake ya pili.
    Mwenyezi Mungu Afumbue macho ya wote wanaoupenda haki,
    amin.
    AMANI NA BARAKA ZA ALLAH VIWE JUU YA MTUME

    Like

  63. mhina says:

    Sasa, ndugu chidy mbona hukujibu hata swali langu moja?…..Usijaribu kuyatetea mambo ambayo sio saizi yako,utazidi kuwatia waislamu wenzako aibu!!.BADO NAHITAJI MUISLAMU WA KWELI ATAKAEWEZA KUJIBU MASWALI HAYO YOTE MATANO….LAKINI SWALI LA KWANZA ANIPE MAANDIKO MAWILI TU,….ILI TUYACHAMBUE NA KUPATA JIBU HAPAHAPA KUWA DINI YA KWELI NI IPI?…..TUSIJE TUKAENDELEA KUPOTEZA KIZAZI CHETU KWA MAMBO YA KIPUUZI AMBAYO YAKO WAZI KABISA!!!.

    Like

  64. nkya says:

    Habari zako ndugu Mhina? naona ndugu umejibiwa swali lako la kwanza kwa urefu sana na ndugu yangu hapo juu lakini ujaridhika, sijaelewa ni kwanini amekutajia dalili nyingi sana za utabiri wa nabii wetu.
    labda na mimi nikujibu kama ifuatavyo:jibu la swali la kwanza
    waefeso1:12 nasi katika huyo tupate kuwa sifa ya utukufu wake,sisi tuliotangulia kumuekea kristo tumaini letu.
    1:13 nanyi pia katika uyo mmekwisha kuliskia neno la kweli,habari njema za uokovu wenu;tena mmekwisha kumwamini yeye,na kutiwa muhuri na roho yule wa ahadi aliyemtakatifu.
    1:14 ndiye aliye arabuni ya urithi wetu,ili kuleta ukombozi wa milki yakekuwa sifa ya utkufu wake.
    zingatia hii mr. nabii aliyetokea arabunu ni nani?
    wagalatia4:21 niambieni nyiynyi mnaetaka kua chini ya sheria! je amwiskii sheri?
    4:22 kwa maana imeandikwa Ibrahim alikua na wana wawili mmoja kwa mjakazi na mmoja kwa muungwana
    4:23 lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili,yule wa muungwana kwa ahadi.
    matayo 21:43 kwa sababu hivyo nawaambia ufalme wa MUNGU utaondolwea kwenu na kupewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
    zingatia ili mr. watapewa taifa lingine ambalo ni la arab.
    matayo23:36 amini nawaambieni ,mambo yote hayo yatakuja juu ya kizazi hiki.
    zingatia mr. kizazi icho cha arabuni.
    sasa kama unataka kuona jina la mtume kwenye torati na injili huwezi kuona kwa sababu ayo majina yalikua kwenye ile taurat ya nabii Mussa na Injili ya ya yesu na hivyo vitabu avipo tena sasa badala yake vipo ambavyo vimechakachuliwa na kufutwa jina lake. sasa kama unataka ushaidi wa jina niletee taurati ile ya mwanzo na injili nikusomee na kama uwezi basi walaumu waliyochakachua sio kusema Mwenyezi MUNGU ni muongo Astaghafirullah
    jibu la swali lako lapili:kwanza kabisa umesema uongo manake kwenye Quraan tukufu imeandikwa mvinyo na sio ulevi kama ulivyoandika wewe, inaonesha wazi kabisa kwamba wewe binafsi umeona tofauti ya ulevi na mvinyo ndio maana ukaona ukiandika mvinyo aitaeleweka kama unavyotaka wewe ieleweke ni ulevi ili uwapotoshe watu. sasa nikufafanulie mvinyo ni kinywaji kisicholewesha kama vile redbull ama shark ndio tafsiri halisi ya mvinyo sio pombe.
    ndio maana kuna aya nyingine Mwenyezi MUNGU anasema uko mtakunywa vinywaji vitamu vyeupe visivyolewesha wala kuleta maneno ya upuuzi.
    swali lingine unasema tumeahidiwa wanawake wazuri tena bikra wakati uku duniani mnaita ni anasa? kwetu sisi wanawake sio anasa tena tunawaheshimu sana, ndio maana tukaruhusiwa kuwaoa. sasa we unaesema wanawake anasa vp kuhusu mama yako aliekuzaa naye pia ni hvyo?
    Mwenyezi MUNGU mwenye hekima alimuumba Adam kwa hekima akaona kumueka peke yake si haki ndio akamuumbia mwanamke. sasa zile hekima alitumia kwa Adam ndizo anatumia kwa watu wa peponi wanawke wazuri tena ni bikra.
    zingatia mr. mwanamke bikra ana heshima kubwa sana ndio maana ukimtaja Maria unataja heshima yake ya bikra yaani bikira Maria. na kwa mwanaume yeyote angependa kuoa mwanamke mwenye heshima ya bikra sasa sijui mwenzangu kama ungependa kuoa gumegume! pia poleni sana manake peponi kwenu amna wanawake sijui mtaishia matendo ya kaumu Luuti!
    jibu la swali no3 Mtume yeye amekuja kumsadikisha yesu na kitabu chake na mitume waliotangulia na vtabu vyao. kama vile yesu alivyokuja kumsadikisha nabii Mussa lakini pia yeye alikuja na kitabu chake Injili? msidhani nalikuja kuitangua taurat bali kuitimiliza.. na ndio hvyo Mtume amekuja kumsadikisha yesu na kitabu chake lakini nae kaja na kitabu chake
    jibu la swali lingine: uislam ulikuepo tokea kipindi cha nabii Adam na watu walikua wakiswali kawaida ila Nabii wetu alikuja kuikamilisha dini tuu sio kuanzisha ndio maana ukitizama kabla yake Nabii Ibrahim alikuja akajenga Al-kaaba na watu walikua wakihiji na kuswali ata kbla yake.
    jibu la swali no4 Mtume aihisi amechezewa na shetani kwa sababu hakuwai kujua kama angetokewa na makaika na ndio sababu alipoona kutkewa na malaika akapata mshtuko na akuwerza kupata jibu kwa wakati ule kuwa ni kitu gani mpaka baade ndio alikuja kujua kuwa ni malaika,mshtuko ni kawaida kwa mwanadamu yeyote kuona kitu ambacho hakuwai kuona.
    jibu lingine: Mtume alikua akitka jasho na kupata homa wakati akishushiwa ufunuo kwa sababu ulikua unashushwa moja kwa moja kifuani kwake na malaika Mtukufu na ayo ni mambo ya kiroho.
    jibu la swali no5 Mtume alisema ajui ltakavyokua siku ya kiama kwa sababu sio yeye tuu bali akuna ajuaye habari ya siku ile ata Malaika wala yesu ushahidi huu apa chini
    matayo 24:36 walakini habari ya sikuile na saa ile hakuna aijuaye hata malaika walio Mbinguni,wala mwana ila baba pekee.
    apa tunaona kumbe ata yesu ajui. tuacheni ushabiki jamani hii ndio njia ya kweli isiyo na shaka

    Like

  65. mhina says:

    ‘SIO KUSEMA ALLAH NI MUONGO ASTAGHAFIRULLAH’…..Lakini cha kusikitisha ndugu Nkya,hivyo ndivyo ilivyo kwa upande wenu.Hebu thibitisha wewe mwenyewe katika ushahidi wa maandiko yenu mlioyatoa:(kumbukumbu 18:18-20).Katika maandiko hayo,tunamuona Mungu akimwambia Musa hivi: MIMI NITAWAONDOKESHEA NABII MIONGONI MWA NDUGU ZAO MFANO WA WEWE,NAMI NITATIA MANENO YANGU KINYWANI MWAKE NAE ATAWAAMBIA YOTE NITAKAYOWAAMURU’……Bwana yesu alipokuja,alithibitisha kuwa nabii huyo ni yeye na ni kweli kuwa Mungu alimtia maneno yake katika kinywa chake pale aliposema:…..HAYO MANENO NIWAAMBIAYO MIMI,SIYASEMI KWA SHAURI LANGU LAKINI NI BABA AKAAYE NDANI YANGU HUZIFANYA KAZI ZAKE.Soma(yoh 14:10).Wanafunzi wake nao wakamthibitisha bwana yesu kua ndiye aliyetabiliwa na Mungu katika torati ya Musa kwa kuambiana..TUMEMUONA YEYE ALIYEANDIKWA NA MUSA KATIKA TORATI NA MANABII,YESU MWANA WA YUSUFU,MTU WA NAZARETI.Soma(yoh 1:45).Pia soma(matendo 3:19-23).Hapo tumeona kuwa ukweli uko wazi kabisa!!.Lakini kwa kuwa mlikwisha jua kuwa hakuna ushahidi wa kweli katika biblia,unao onyesha kuwa,Mhamad ametajwa katika biblia,basi mkaamua kuvurugavuruga kwa kutoa maelezo mengi mno,ili kupoteza lengo!!.Katika maandiko yote ya biblia mliyonukuu,ukiyasoma kwa ufasaha kuanzia juu utaona ni MAELEZO YALIYOJAA UONGO MTUPU!!.Maelezo yenu yote hayamuhusu Mhamad na dini yake….sasa najiuliza,HIVI KWANINI WAISLAMU WENGI WANATETEA DINI YAO KWA MAELEZO YA UONGO!!!….Kwanza alieandika maandiko hayo yote mnayo nukuu ni Mtume paulo,na nyinyi siku zote mnampinga paulo kuwa ni mtume wa uongo….mbona tena mnatumia maandiko yake kumhalalisha mtume wenu mhamad?!!,…Yaani ni vichekesho vitupu vya kukwepa matope halafu kukanyaga mavi…..Eti mhamad ndiye roho wa kweli,Sasa kama ni hivyo,mbona hatuwasikii mitaani mkimuita Mhamad jina la Roho wa kweli?…mbona hakukaa ndani ya roho za watu?…Ukweli kumhusu roho mtakatifu,Bwana yesu anatuambia hivi: LAKINI HUYO MSAIDIZI,HUYO ROHO MTAKATIFU AMBAYE BABA ATAMPELEKA KWA JINA LANGU, ATAWAFUNDISHA YOTE NA KUWAKUMBUSHA YOTE NILIYOWAAMBIA.Soma(yoh 14:26).Hapa inatupasa kujiuliza kuwa, kama ni kweli mhamad ndiye msaidizi wa bwana yesu…mbona hapo msaidizi anatajwa kuwa ni ROHO MTAKATIEU’?…Labda waislamu wengi wangetamani kuliona jina la mhamad katika nafasi hiyo,lakini ukweli ni kwamba haikuwa hivyo kwa kuwa mhamad sio nabii,sio mtume wala sio msaidizi wa bwana yesu!!.Msinichukie ndugu zangu,mimi nawapenda sana sana lakini ninaamini silaha nzuri ya upendo ni kumfahamisha ndugu yako mambo ya ukweli kwa msisitizo…kwa kuwa hapa duniani tunapendana kwa muda tu,lakini tukija kutana siku ya mwisho mbele za mungu HAKIKA TUTAPENDANA MILELE.Lakini pia tunaona bwana yesu akisema:NA KWA JINA LANGU,HUYO MSAIDIZI ATAWAFUNDISHA YOTE,NA KUWAKUMBUSHA YOTE NILIYOWAAMBIA’…Lakini chaajabu ni kwamba,Mhamad hakufanya chochote kuhusu injili ya bwana yesu,na badala yake anatetewa na wafuasi wake(waislam) kuwa’MHAMAD AMEKUJA NA KITABU CHAKE NA MAMBO YAKE MWENYEWE!!.Hapa kamwe hatuongelei mambo ya kila nabii au kila mtume kuja na kitabu chake kama anakwenda darasani,HAPANA!!….Mimi naongelea maagano ya kweli ya Mungu ambapo biblia inasema,ni makuhani wawili tu,walioleta maagano ya mungu.Biblia inasema hivi:TORATI ILIKUJA KWA MKONO WA NABII MUSA BALI NEEMA NA KWELI (INJILI) ZIMEKUJA KUPITIA BWANA YESU.Soma(yoh 1:17).Sasa basi….kama nilivyoonyesha jinsi Mhamad alivyokuwa nje ya utaratibu wa mungu,akitetewa na wafuasi wake kuwa kaja na mambo yake mwenyewe,sasa kwanini ndugu zangu mnaendelea kuwa waislamu?!!……Jambo jingine la ajabu ni waislamu kutumia ile(waefeso1:14) na kusema kuwa yule yule paulo wanae muita mtume wa uongo…AMEWATABIRIA KUWA MHAMAD ATATOKEA UARABUNI…Baada ya wao kuona neno ARABU…Wakaamini kuwa huko ni kule uarabuni alikozaliwa mhamad!!!….ndiyo maana nilitahadhalisha kuwa kama mambo sio saizi yako ni heri uache kujibu usije ukaitia aibu dini yako zaidi.Ukweli ni kwamba ukisoma kwa utulivu maelezo ya mtume Paulo utagundua kuwa kamwe hakumzungumzia mhamad aliko zaliwa bali anazungumzia ARABUNI YA ROHONI.Katika (2wakorintho1:22)…Mtume paulo anafafanua vyema zaidi kwa kusema: NAE NDIYE ALIYETUTIA MUHURI AKATUPA ARABUNI YA ROHO MIOYONI MWETU….Sasa kama ni kweli Allah amewapofusha akili na macho kiasi hicho ndugu zangu KWANINI MNAENDELEA KUWA WAISLAMU?….Kwa ufupi ni kwamba:HAMKUJIBU HATA SWALI LANGU MMOJA…..Halafu pia niliuliza kuwa,mbona bwana yesu katika injili anasema kuwa mbinguni hakuna kupewa wanawake wala kunywa mabia lakini Allah anasema kuwa,huko atawapa wanaume mabibi wazuri tena bikira,sasa kwanini kauli yake inapishana na mtume wake,Bwana yesu kama nyinyi waislamu mnavyoamini?…hukujibu na badala yake mnajifanya mna hekima mbele za wanawake….Sasa kama ni kweli kuwa mna hekima za Allah,mbona hamuwaoi kwa utaratibu wa haki unaofaa,badala yake, muislamu mmoja anakuwa na wake wanne ndani ya nyumba,sasa…je,hivi hamjui kuwa hata wanawake nao ni wanadamu wenye wivu kama sisi wanaume?…ni haki gani hiyo ya kiroho aliyowafundisha Allah muifanye?hapo Pana haki na amani ya kiroho na mapenzi ya kweli au ni kufuata tamaa za mwili tu,na kuwasononesha wanawake?TUSIDANGANYANE KIASI HICHO NDUGU ZANGU!!….Alafu bado Allah anaonyesha upendeleo hata kule mbinguni kwake ,kwa kuwaahidi wavulana na wakina baba kuwa atawapa mabinti wazuri, Sasa mimi najiuliza kuwa wasichana na wakina mama nao watazawadiwa nini huko? Mbna wanaonekana hawapo katika listi ya Allah!!…je,huu sio upendeleo wa wazi mungu wenu anauonyesha?……Kuhusu utetezi wako wa jinsi mhamad alivyopokea ufunuo,umenishangaza mno mno!!…Yaani unamsingizia Mungu bila ya woga kuwa,ALIMVURUGA AKILI NABII WENU MHAMAD!!…LOH!!…Msiandike mambo msiyoyajua kwa kuwa nilikwisha kueleza huko juu kuwa,MUNGU NI MTAKATIFU MNO MNO NA PIA YEYE NI UPENDO.Mwanadamu yeyote anapokutana na Mugu kwa njia ya malaika au njia yoyote ile…Basi tunaamini kuwa,AMEKUTANA NA UPENDO MKUU.Yeye anatujua tulivyo dhaifu,kwa hiyo hata anapotutokea kwa njia zake,huja kwa hali nzuri za kutuwezesha sisi kupokea kwa usahihi kile alichotukusudia.Ndio maana katika maswali yangu nilieleza kuwa hakuna hata nabii mmoja aliyetembelewa na malaika wa mungu halafu eti avurugwe akili yake na kupandwa na mahoma kwa kisingizio kuwa yeye ni mdhaifu.Yule aliyempanda mhamad ni kweli alikuwa ibilisi,ndiyo maana hatayeye alijihisi hivyo.Shetani ndiye mwenye mchezo huo mchafu akiwa na lengo la kukuvuruga akili ili akudanganye vyema pasipo wewe mwenyewe kujitambua.Ndio maana biblia inamuita BABA WA UONGO!!.Yeye huwa ni muelevu mno kupita hata kawaida…anaweza hata kukuambia kuwa unapokanyaga chini unaua sisiminzi na viroboto wa mwenyezi mungu,kwa hiyo katika sala zako unatakiwa utubu kwa ajili ya wadudu wale….JAMBO AMBALO SIO KWELI KWA KUWA MUNGU WETU AMETUPA UHURU WA KUTEMBEA TUTAKAVYO.Kwa hiyo basi….kama Allah alishindwa kujitakasa na kuwa safi mbele ya nabii wake aliyemtuma yeye mwenyewe…..ataweza kweli kutakasika mbele ya wanadamu wote?…na pia,kama mhamad anaetegemewa na dunia nzima,akikutana na mungu wake kwa njia ya malaika,anashindwa kumtambua na kumuita Mungu,SHETANI!!….Huku kila wakati anapo ona ufunuo, homa zinampanda….Anaweza kweli kuwa nabii wetu wa kweli wa kumtumaini?….Mwisho ndugu zangu waislamu ni kwamba:Bwana yesu alijua kuwa, njia sahihi ya wanadamu wote ni yeye mwenyewe…MIMI NDIMI NJIA KWELI NA UZIMA.Lakini ni kweli kuwa katika ile(mathayo 24:36)…anasema kuwa hajui siku ya kiama au siku ya mwisho ni lini…na hii ni kweli kwa kuwa ajuae saa na siku ni YEHOVA MWENYEWE…..Lakini cha ajabu kwa upande wa mhamad…..Mimi siku hoji mambo ya siku ya mwisho kama anaijua siku ile bali nilihoji yeye kama njia mbele za watu anamatumaini gani?…lakini jibu lake ni kuwa’YEYE AKIWA NDIYE HIYO NJIA YA MUNGU KAMA ANAVYODAI MWENYEWE ANAKIRI KUWA HAJUI ATAKALOTENDEWA SIKU YA MWISHO….Sasa kama yeye mwenyewe anakiri hivyo,je…kwa wafuasi wake itakuaje?…..NARUDIA TENA NDUGU WAISLAMU KUWA HAMKUWEZA KUJIBU HATA SWALI LANGU MOJA…Lakini mimi niishie hapa na mungu awaokoe.

    Like

  66. Ibrabura says:

    Mhina, kubali na usikubali, lakini vitabu vya TAURATI NA INJILI hakuna tena hapa ulimwenguni. Vitabu viliyokuwepo siku hizi (kumbukumbu la taurati na injili kama ilivyoandikwa), haviwezi kusuluwisha hoja yako kwa sababu:
    1- Ukisoma dibaji ya Biblia kuna maelezo yafuatayo:
    1.1-“…maendelezo ya majina yote ya watu na ya mahali ilikuwa lazima yafikiriwe tena na mengine kutengenezwa jambo hili ilikuwa kazi kubwa sana kwa sababu yapo majina zaidi ya 3,500 tuliyotengeneza…”
    Je! Kwa maelezo hayo, jina la Muhammad s.a.w litabakia? Jiulize,tafakari chukua hatua!

    2- Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.
    YER.8:8
    Kwa kifungu hicho, Muhammad atasalimika kweli?

    3- Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya, kama yote
    yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
    Muhammad ataandikwa kumuacha Yesu hapo?
    Jiulize, tafakari na chukua hatua!

    Lakini, pamoja na ufedhuli wote uliofanyika, sura ya Muhammad ndani ya Biblia inaonekana waziwazi kabisa. Hii ikiwa na pamoja na kifungu cha Kumb.18:16-20, ambayo wewe, katika maelezo yako, umesahau kuzingatia vigezo muhimu vilivyotajwa juu ya huyo nabii.
    Umesahau kwamba, huyo nabii anaebashiriwa sio mwanaisraeli bali ni ndugu wa wanaisraeli. Mfano wake ni kwamba, ndugu yako wewe hawezi kuwa wewe bali, atakuwa ni mwengine. Mi nashukuru, mchangiaji mmoja hapo juu, chidy rakym, amebainisha vizuri sana.

    Mat.21:33-40 Yesu anasema:
    ”Kulikuwa na mtu mwenye nyumba naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungushia ua, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara akapangisha wakulima akasafiri. Wakati wa matunda ulipokuwa karibu akawatuma watumishi wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake. Wale wakulima wakawakamata watumishi wake, huyu wakampiga na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe. Akawatuma tena watumishi wengi kuliko wa kwanza, ikawa tena vile vile. Mwisho akamtuma mwanawe kwao, akisema watamsitahi mwanangu. “Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi haya na tumwue, tuutwae urithi wake, Wakamkamata wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu atawatendaje wale wakulima? Wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya, na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake. Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Kwa sababu hiyo nawambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake. naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika , na yeyote ambaye litamwangukia litamsaga tikitiki.
    Kifungu hiki, kama una nia ya kweli ya kutaka kujua kama Muhammad kabashiriwa kwenye Injili, bila ya shaka utakubaliana nami kwamba ufalme wa mungu umeondolewa kwa taifa teule la wanaisrael na wamepewa taifa jingine. Swali juu ya swali, ni taifa gani hilo waliopata hiyo baraka?
    Propaganda, hazina nafasi.

    Swali lako la pili, nakujibu kwa kuzingatia kifungu kifuatacho:
    43. Katika Bustani za neema.
    44. Wako juu ya viti wamekabiliana.
    45. Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
    46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
    47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
    QURAN 37:43-47.
    Biblia inasemaje! Je peponi kuna divai?
    ‘Kwa maana, nawaambia kwamba, tangu sasa sitakunywa tena divai hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
    LUKA 22:18
    Ndugu, unapotaka kusema jambo, lazima uwe na ushahidi nae. Sasa ni wapi kwenye vitabu vyote vya dini vinaposema kwamba wanawake ni anasa?
    Mchangiaji mmoja hapo juu amekuelekeza kama inavyotakiwa. Kuoa wanawake zaidi ya mmoja Biblia yenu imebariki. Nabii mmoja alikuwa na wake zaidi ya 700. Mbona yesu akumtenga nabii huyu, badala yake kasema hakuja kutengua manabii?
    Ndugu, asili ya ushetani ni kupinga maagizo ya mungu. Mfano wake ni kwamba mungu katoa amri kila mtu mwanamume atahiriwe, Paulo binadamu, kasema haisaidi kitu’

    Yesu kasema sheria haitatenguka mpka siku ya mwisho, Paulo kaja akayabisha yote. Sasa huu ndio ushetani.
    Ndugu usije ukajidanganya hata siku moja kwamba shetani hamjui mungu, never! Shetani kwa asili yake anamjua MUNGU lakini hatekelezi amri zake.
    Ndugu Mahubiri ya Yesu na Muhammad hayatofautiani, ila ni uvivu wako tu wa kuyaelewa na kuyafuatilia maandiko. Kifungu kinasema hivi; 28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye. 29 Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni. 31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema, 32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.
    Ndugu, YESU amejibu kulingana na swali lilivyoulizwa. Siku ya kiyama ni siku ya hukumu, yaani ni siku ya kutenganisha pumba na mchele. Ili kulielewa vizuri usiishie 31 nenda mpaka 32.
    Muhammad anazungumzia baada ya kupita ile hukumu kwa wale watakaojaliwa kuingia peponi, mambo watakayoyakuta huko.
    Ndugu, lazima ukumbuke kwamba Adam na Hawa walifukuzwa katika bustani ya aden huku wakiwa na mwili wao kwa mujibu wa biblia.

    18. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
    19. Vitabu vya Ibrahimu na Musa
    Quran 87:18-19
    Ndugu, Ibrahim amepokea kutoka kwa mungu, utaratibu wa tohara kwa wanaume, halafu Musa kapokea sheria kumi za mungu. Yesu, alisikika akisema yeye hakuja na kitu kipya bali kutimiliza.
    Ndo maana, alisema, sijaja kwa ajili ya wenye haki bali kwa wale waliopotea. Akiwa na maana kwamba, kabla yake, baada yake walikuwepo wachamungu ambao hawakuitaji kumsikiliza yesu.
    Kama unao utaratibu aliouleta yesu basi nifundishe sio mbaya. Na kama kuna watu ambao hawakuitaji kumsikiliza yesu kwanini hilo lisitokee kwetu? Ndugu, yesu hakuwa na hakuwai kutoa kitu kipya!

    Yesu aliposema mimi ni njia, anamaanisha ana ujumbe kutoka kwa mungu kwa watu wake. Sio wote, Hili vumbi la yesu, wala nyinyi mnaejiita wakristo, haliwahusu hata kidogo kwa ushahidi wa maandiko. Mtu wa wakati wa yesu, akiamini na kutekeleza basi ataingia peponi na kama hautaamini basi utaenda motoni.
    Kwa hiyo, minabii wote walikuwa njia ya kuelekea mbinguni kwa wakati wa utawala wao.

    Ndugu, uislaam haukuletwa na Muhammad. Ni mungu mwenyewe katika kuwafunnulia watu wamjue mungu na kumwabudu. Sasa ile njia ya kumwabudia ndo uislam.
    Kwa maana hiyo, kwa vipindi tofauti, mungu alikuwa anatuma nabii kwa ajili ya kutangaza ujumbe huo, ambao ni uislam.
    Shahada zote zilikuwa zinamlenga mwezimungu na mtume wa zama zile.
    Ukisoma biblia ya kiarabu, kifungu cha yesu kilichosema mjifunze kwangu …mpole na mnyenyekevu wa moyo, utakuta neno islam.
    Kwa kifupi dini ni moja wanatofautiana manabii tu.
    Na biblia imetuambia taifa kuu itakuwa arabuni
    Kutojua anachoenda kufanyiwa mbele za mungu Muhammad unaona ni makosa ila Yesu kutojua siku ya mwisho unaona kawaida! Acha ubabaishaji, hakuna binadamu aliyozaliwa na mwanamke aijuaye siri ya mungu kwa 100%.

    Ndugu, nabii hachaguliwi kwa kura, kama chaguzi za hapa duniani. Mungu uchagua manabii atakavyo! Wewe una mamlaka gani ya kujua nini mungu anafanya?
    Sasa kama utaratibu wa kuchaguliwa nabii ungekuwa mmoja, basi binadamu wote tungekuwa sawa, wote matajiri, wote maskini, kusingekuwepo mlemavu nk…..

    Kiumbe yeyote yule, jambo ambalo kwake ni geni lazima ashangae kwanza. Hata kuku wa vijijini kusikopita helikopta siku ikipita tu lazima atahangaika huku na kule. Lakini kwa wale wa jini, haaa ,
    Jiulize. Tafakari. Chukua hatua
    Muhammad ni Mtume wa mwisho

    Like

  67. mhina says:

    Ndugu.Ibrabura,Biblia takatifu imeandika kua, tusiongeze wala kupunguza maneno ya unabii wake, mpaka siku ya hukumu ambapo imefunuliwa katika ufunuo wake.Sasa huoni kuwa tukiongeza unabii wa mhamad mtume wenu mpendwa, tutakuwa tumekwenda kinyume na neno la Mungu?….je, tumuamini Mungu alie ahidi kulitunza neno lake milele na milele au tukuamini wewe mwanadamu ambae unatumia ushahidi wa uongo wa kwenye mitandao kusema neno la mungu silo la kweli?….Maana hata wale uliowataja kwenye dibaji,kamwe hawakuwa na lengo la kubadili neno la mungu zaidi ya kurekebisha tabia asili za kiswahili kwa kuwa,hata wewe ndugu ibra,unafahamu kuwa kiswahili cha kiunguja au cha kule kenya,matamshi yake kamwe hayako sawa na ya huku Tanzania.Mfano wa kile walichokifanya ni:Nuru kuitwa mwanga, kutwa kuitwa kucha,Wokofu kuitwa wokovu nk.Sasa tatizo lako ni nini hapo ndugu Ibra?!!!!…..Tena katika torati,Mungu aliahidi kuwa manabii wa uongo kamwe hawataandikwa katika neno lake takatifu yaani biblia.Sasa basi,kama nyinyi waislamu mmeona kuwa nabii wenu mhamad hajaandikwa katika biblia,kwanini msimuamini mungu kile alichosema? Pia kwanini msimuamini Mungu vile livyoahidi kuwa ‘ATASIMAMA KAMA MLINZI NA SHAHIDI MUAMINIFU KULITUNZA NENO LAKE MILELE.Soma(Zaburi 89:33-37)(Mhubiri 3:14).Je,Sisi wakristo tunaomuamini Mungu na kuzishika ahadi zake tumekosa nini mbele zenu?…au tuna makosa gani?!!….Maana tunaona kuwa hata yale mapigo aliyoyaweka Mungu kuwa,aliyaweka kwa ajili ya waharibifu wa neno lake na kamwe sio kwa ajili ya waaminio….kwa hiyo kamwe tusipende kukimbilia kuwahukumu watu wengine pasipo sisi kutimiza ule wajibu wetu wa kuliamini neno lake.Hata kama hayo yangekuwa kweli,hayatuhusu sisi…hilo ni fungu la mwengine mbele za mungu sio fungu letu.Huu ndio utetezi wangu katika neno takatifu la mungu,BIBLIA….Pia napenda nikufahamishe kuwa,kamwe haiwezekani kuandika kila kitu kinachotokea katika maisha ya mtu au watu…kwa hiyo,hata maisha ya mtume wenu mhamad yangeandikwa yote mpaka anapolala’anapopiga mswaki nk….mimi naamini tungeujaza huu ulimwengu!!…hizi hoja za kitoto ndugu ibra,jaribuni kuziacha.Kuhusu hoja zako nyingi ulizonipa,nilikwisha zijibu huko juu katika sehemu mbalimbali…..labda nikujibu baadhi ya zile ninazohisi sikuzijibu…….(1)kuhusu(kumbuk 18:18) naona ushahidi wa kuwa bwana yesu ndiye aliyetabiriwa….UMEJITOSHELEZA KABISA KABISA…TUSIPOTEZE MUDA KWA JAMBO HALISIA!!…..Kuhusu jiwe la pembeni na taifa teule la mungu,Biblia inatuambia hivi:BASI TANGU SASA NINYI SI WAGENI WALA WAPANGAJI,BALI NINYI NI WENYEJI PAMOJA NA WATAKATIFU,WATU WA NYUMBANI MWAKE MUNGU,MMEJENGWA JUU YA MSINGI WA MITUME NA MANABII,NAYE KRISTO YESU MWENYEWE NI JIWE KUU LA PEMBENI…KATIKA YEYE JENGO LOTE LINAUNGANISHWA VEMA NA KUKUWA HATA LIWE HEKALU TAKATIFU KATIKA BWANA.KATIKA YEYE NINYI NANYI MMEJENGWA PAMOJA KUWA MASKANI YA MUNGU KATIKA ROHO.Soma(waefeso 2:19-22)….Sasa ndugu ibra,kama mwenyewe ulivyoona ukweli wa mambo…sijui mhamad na hilo taifa lake la uarabuni utalichomeka wapi hapo!! Wakati sisi tukiwa kama mawe madogo,tunaungana na jiwe kuu ambaye ni bwana yesu kujenga hekalu la haki la mungu huko mbinguni.POLENI SANA KWA KUENDELEA KUDANGANYWA HUKO MITAANI……..Ndugu ibra naona hoja zako nyingi ulizotoa nilikwishazijibu huko juu.Labda nimalizie na somo kuhusu wanawake na ndoa inavyotakiwa kuwa:Ndugu Ibrabura unatetea ndoa za wake wengi kwa kutafuta jina la nabii sulemani alieoa wake 700.Ndoa ni nini?..ndoa ni makubaliano kati ya mwanamke na mwanaume kwamba waishi pamoja kwa uaminifu.Muanzilishi wa ndoa ya kwanza ni MUNGU MWENYEWE PALE EDEN.Neno lake linasema hivi:KWA HIYO MWANAUME ATAMUACHA BABA YAKE NA MAMA YAKE NAYE ATAAMBATANA NA MKEWE NAO WATAKUWA MWILI MMOJA.Soma(mwanzo 2:24).Hapa tunaona kuwa,Mwanaume kwa mujibu wa neno la mungu anatakiwa aambatane na mke mmoja(sio wake wengi) ili waweze kuwa kitu kimoja kiaminifu na cha haki.Pia tunaona kuwa kumbe mungu alimleta mwanamke ili awe kitu kinacholingana na mwanaume chenye kumridhisha ili kusudi kumsaidia katika kutimiza maagizo mengine yote aliyopewa na mungu.kwa hiyo basi,kwetu sisi wakristo,mwanamke sio kwa ajili ya tamaa zetu tu, bali ni mtu wa karibu mno mno hata mbele za mungu ndio maana tunatunza uaminifu aliouanzisha mungu kwao.Sasa kwa sababu wamekuwa mwili mmoja,wakifanya ngono na mtu mwingine yeyote atakae ongezeka,watakuwa wamevunja heshima ya ndoa,na kitendo hicho huitwa UZINZI.Istoshe ndugu ibra….kufanya mapenzi na mke zaidi ya mmoja ni kitendo cha ‘KUTOUWEZA MWILI(TAMAA MBAYA) AMBAPO UNAMPUNJA MKEO NA KUMSONONESHA MNO MNO MNO!!!…BADALA YA KUMUONYESHA UAMINIFU,UVUMILIVU NA UPENDO WA KWELI WA MUNGU.Kwa hali hiyo ndugu ibra unafikiri utaweza kumwambia mkeo NAKUPENDA MKE WANGU…Wakati unawake wenza watatu pembeni yake wanakukodolea mimacho??!!!….Kama sio utapeli huo utakuwa ni nini??…jamani nawaomba tusizishabikie tu,hizi dini zetu bali pia tuzipime kwa ufasaha kile dini inachofundisha.utakuta jijitu,huyo mke mmoja tu,hamuwezi lakini kwa kuwa ni mfungo wa ramadhani anaongeza wengine wawili ili ashindane na baba nanihii,ili aonekane kuwa nae ni kidume!!….sasa umawezaje kumbadilisha na kumpa akili mtu kama huyo wakati amekwisha leweshwa na mafundisho ya BABA WA UONGO.Ndugu ibra nimalizie na manabii wa zamani,Hapo nakubaliana na wewe kabisa kwamba walikuwa na tabia hiyo ya kuoa wake wengi…lakini utetezi wangu ni kwamba,walikuwa wakifanya vile kutokana na mazoea yao ya kizamani kwa kuwa hata mungu mwenyewe alikuwa akiendelea kuwakemea kuwaonyesha kuwa kamwe hapendezwi na mambo yale…WALA USIZIDISHE WAKE ILI MOYO WAKE USIKENGEUKE.Soma(kumbuk 17:17).Ndiyo maana hata huyo nabii suleman alie oa wake 700,alitambua makosa yake na kumrudia mumgu kwa kutubu’UISHI KWA FURAHA PAMOJA NA MKE UMPENDAE,SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO YA UBATILI,ULIZOPEWA CHINI JUA,SIKU ZOTE ZA UBATILI WAKO,KWA MAANA HUO NI SEHEMU YAKO YA MAISHA NA KATIKA TAABU ZAKO ULIZO ZITAABIKIA CHINI YA JUA.Soma(Mhubiri 9:9).Pia soma(mhubiri 2:1)(methali 5:16-18).Pia ndio maana tunamuona bwana yesu nae aliwakumbusha wanafunzi wake katika injili jambo lilelile la kwanza alilolisema Mungu kwa kuwaambia:HAMKUSOMA KWAMBA MUNGU ALIMUUMBA MTU NA MKEWE NAO WATAKUWA MWILI MMOJA,KWA HIYO ALICHOKIUNGANISHA MUNGU,MWANADAMU ASIKITENGANISHE.Soma(mathayo 19:4-6)…Njoo kwa bwana yesu ndugu yangu ibra…ili uwe kama paulo,tukufundishe vyema ukaihubiri injili mpaka misikitini!!.Asante sana.

    Like

  68. mhina says:

    ndugu ibra…katika utetezi wenu nyie waislamu,mnamtetea nabii wenu mhamad kua kile kiumbe kilicho mpa ufunuo kule mapangoni sio shetani bali ni malaika.Sasa mbona kimaandiko kuruani imeshindwa kujitetea hivyo badala yake maandiko ya mungu mnayatetea kwa akili na maarifa yenu?…pia mnasema kuwa ni kawaida kwa mwanadamu anapotokewa na jambo la ghafla kushituka….hiyo ni kweli lakini lazima mfahamu kuwa mhamad sio kwamba alishtuka tuu, bali pia alipatwa na homa kali,na wote sisi tunajua kuwa homa sio mshtuko tuu bali homa ni UDHAIFU WA MWILI AU MADHARA!!….Sasa ndugu ibra,hebu jiulize kwa akili zako mwenyewe kwamba,hivi sisi wanadamu tukishtuka kwa jambo fulani tunapata homa?.Mimi ninavyofahamu ni kuwa shetani akikuchezea ndio unapata homa kali na kuvurugikwa na akili iwe kwenye mibuyu au baharini nk.NAWEWE NIMEKUPA HII YA KUTAFAKARI,KUJIHOJI NA KUACHUKUA HATUA.

    Like

  69. mhina says:

    ndugu zangu waislamu na wafuatiliaji wote mimi naishia hapa.Lakini nawaaga kwa ujumbe wa maneno ya mtume petro ninayo yapenda mno!!.Petro anatutia nguvu za kiroho kwa kutusisitiza hivi: ‘MAANA,MWILI WOTE NI KAMA MAJANI, NA FAHARI YAKE YOTE NI KAMA UA LA MAJANI.MAJANI HUKAUKA NA UA LAKE HUANGUKA, BALI NENO LA BWANA HUDUMU HATA MILELE .NA NENO HILO NI NENO LILE JEMA LILILOHUBIRIWA KWENU.,…BASI,WEKENI MBALI UOVU WOTE NA HILA YOTE, NA UNAFIKI NA HUSUDA NA MASINGIZIO YOTE. KAMA WATOTO WACHANGA WALIOZALIWA SASA YATAMANINI MAZIWA YA AKILI YASIYOGHOSHIWA, ILI KWA HAYO MPATE KUUKULIA WOKOVU.Soma(1Petro 1:24-25,2:1-3)….Bwana yesu ndiye tumaini langu milele na milele.Thax.

    Like

  70. chidy rakim says:

    Petro Utume kapewa na nani kaka mbona upo gizani utume wa petro na paulo na sawa na wa kakobe

    Like

  71. Noor mohamed says:

    Ndugu zangu wakristo tumieni akili yesu hakufa msalabani kwa ajili ya kuondowa zambi zenu kwa kutumia damu yake. Nasema hivo kwa sababu

    1) kwa mujibu wa Biblia Yesu mwenyewe hakutaka kufa pale alipo anguka kifudifudi akainuwa mikono juu akaomba akisema Baba yangu ikiwa kama unanipenda kikombe hiki cha mauti kiniepuke sio kama nitakavo mimi ila kama utakavo wewe ewe baba ,

    Sasa ndugu zangu wa kristo huyu yesu ambae hakutaka kufa mpaka akaomba baba yake amuepushe , mnasemaje leo alijitowa afe kwa ajili yenu? Tumieni akili

    2) wakristu nyinyi hamumpendi yesu kama kweli mnampenda inakuwaje mnautukuza msalaba uliotengenezwa na maadui zake kwa ajili ya kumtesa na hatimae kumuuwa?

    Like

  72. Ibrabura says:

    Nilichojifunza kutoka kwako Mr.Mhina, hata kama umekimbia, ni kwamba, mazungumzo yako ni ya kutetea upande wako tu, yaani ili mradi upo kwenye kundi hilo basi hutaki kinyume hata kama utapewa hoja za msingi, hautairuhusu akili yako itafakari hoja hizo na kuupata ukweli, bali unakuwa na mtazamo hasi tu, Naomba tutafakari hoja au changamoto anayokupa mwenzio na sio kutetea kitu ambacho kiutash hakileti maudhui! Hata katika dini tunafundishwa kuongea vitu ambavyo tuna ushahidi navyo na si kila unachokisikia basi unakiamini!
    Quran Tukufu inadai Taurat n Injili. Sio ”Kumbukumbu la Taurat n Injili kama ilivyoandikwa!” Vitabu hivi haviaminiki (Kumbukumbu la Taurat n Injili kama ilivyoandikwa) kwa sababu vina mkono wa wanadamu kama Biblia yenyewe inavyojieleza kupitia DIBAJI na sehemu nyingine.

    -“…maendelezo ya majina yote ya watu na ya mahali ilikuwa lazima yafikiriwe tena na mengine kutengenezwa jambo hili ilikuwa kazi kubwa sana kwa sababu yapo majina zaidi ya 3,500 tuliyotengeneza…”

    Mhina, usitake watu walionuna wacheke. Hivi majina ya watu na ya maeneo yanakuwa na Uunguja, Utanzania na Ukenya? Tupe mfano wa jina lako! Acha kudanganya watu!

    Halafu nyie wakristo acheni unafiki! Mara agano la kale sio letu mara letu, nyinyi vipi? Baba yenu nani nyie? Janja yenu naijua, kinachowaponzeni nyinyi uroho, na mnakumbatia watendao maovu kwa kuleta fikra zenu ambazo hazikutoka kwa mungu. Ndo maana uzinzi, ulevi, ujambazi, kuuwa albino, na vingine vingi vibaya ambavyo mungu kakataza, mnavikumbatia kwa sababu na nyinyi pia mnausika. Eti ukiwa na imani tu bila matendo inatosha kuingia uzimani. Huyo Paulo wenu, kawauza nyie. Yeye alikuwa jambazi kubwa, kwa kuona hivyo, akaamua kwanzisha itikadi yake ili kuwapoteza watu wengi. Yaani, nyinyi kama mngekuwa wajanja mngetafakari maneno ya Yesu. Yesu aliwaonya wanafunzi wake juu ya akina paulo. Barnaba baada ya kumtambua huyu anaefuatananae kuwa ni yule alietajwa na yesu akantenga.
    Kwa hiyo, Mr. Mhina tunaposema Biblia sio yote neno la mungu hatukosei, PAULO anathibitisha hili katika 2WAK. 11:17.
    Mhina, kwa hali hiyo, Biblia inaposema kweli, tunakubali kwamba hapo imesema kweli. Na inaposema uongo, pia tunakubali kwamba hapo imesema uongo.

    Mhina, nikakukumbusha ya kwamba PENYE UKWELI UONGO UNAJITENGA. Tunapodai kwamba Kifungu cha KUMB.18:16-20 kinamhusu Nabii Muhammad saw, hatukurupuki. Kuna hoja za msingi zinazotufanya tuamini. Nikakutolea kipengele kimoja tu ambacho ni cha NDUGU YA WAISRAELI. Nimekupa mfano wake nikakuambia ndugu wa MHINA hawezi kuwa MHINA huyo huyo. Bali, atakuwa mtu mwingine. Kwa hiyo, kwa kipengele hiki kinamuondoa YESU katika kinyang’anyiro kwa sababu yeye ni Mwisraeli.
    Mhina, nilichogundua kingine kutoka kwako ni kwamba unaposoma vifungu unashindwa kuelewa, yaani unapita juu juu tu bila kuingia ndani.
    Kwa hiyo, kama utaendelea kupinga kumhusisha Muhammad kwenye huo ubashiri na usimhusishe Yesu kwa sababu vigezo vilivyotajwa hapo Yesu ananavyo, labda tafuta mwingine mwenye hivyo vigezo.
    MOJA KATI YA TABIRI ZA YESU JUU YA UJIO WA MTUME KUTOKA TAIFA JINGINE TOFAUTI NA ISRAEL
    Mat.21:33-40 Yesu anasema:
    ”Kulikuwa na mtu mwenye nyumba naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungushia ua, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara akapangisha wakulima akasafiri. Wakati wa matunda ulipokuwa karibu akawatuma watumishi wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake. Wale wakulima wakawakamata watumishi wake, huyu wakampiga na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe. Akawatuma tena watumishi wengi kuliko wa kwanza, ikawa tena vile vile. Mwisho akamtuma mwanawe kwao, akisema watamsitahi mwanangu. “Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi haya na tumwue, tuutwae urithi wake, Wakamkamata wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu atawatendaje wale wakulima? Wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya, na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake. Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Kwa sababu hiyo nawambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake. naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika , na yeyote ambaye litamwangukia litamsaga tikitiki.

    MHINA, ebu tuangalie kifungu hiki kipengele kwa kipengele kama kweli JIWE NI YESU:
    Mwenye nyumba ni mungu;
    Shamba ni ulimwengu;
    Wakulima ni wanadamu wakilengwa Waisraeli;
    Watumishi ni mitume na manabii;
    Mwanawe ni Yesu;
    Wakulima wengine ni taifa lingine ambalo ni Arabuni
    Jiwe walilolikataa waashi ni Ishmail aliedharauliwa na ndugu zake wana wa Isaka. Kipengele hiki, kinatimiza ahadi ya mungu mwenyewe
    Mwanzo 16:11-12
    11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako. 12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
    Mhina, aya ya 12 tunaona ahadi ya mungu kwa mtoto ishmail:
    Mkono wake utakuwa juu ya watu wote;
    Mkono wa watu wote utakuwa juu yake:
    Naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.
    Mhina, kama hauna nia ya kuwapotosha watu, utakubaliani nami kwamba, Muhammad ni kwa ajili ya watu wote, bila kujali dhehebu gani au dini gani katoka, kwa mujibu wa aya hiyo!
    Mtume wako Paulo, pamoja na ufedhuli wake wote lakini anafahamu vizuri tu juu ya maagano mawili ya mungu. AGANO MOJA LA ISHMAIL AMBALO ANARITHI KUTOKA KWA BABA, AMBALO NI AGANO KWA AJILI YA MATAIFA YOTE;
    AGANO LINGINE NI LA ISAKA AMBALO MUNGU AMEFANYA KWA AJILI YA UZAO WAKE TU
    MHINA, jambo ambalo hauna ushahidi nalo usililete hapa, utamaanika. Watu watakudai kifungu, utashindwa kujitetea. Hoja ya wanawake achananae, huna ujuzi nae. Hivi we ni nani mpaka ufikie hatua ya kuwadharau minabii, ambao mungu mwenyewe kawamini na kuwatuma kwa watu?
    Kuoa wake wengi mwenyewe mungu kabariki, wewe unaleta ukaidi. Sasa hapo ukiitwa shetwani utakataa?
    Mtu aliyelaaniwa na mungu ni YEHOAKIMU ambae ni kizazi kilichofikia mpaka yesu akatokea.
    Halafu, wewe usijifananishe na mwanamke. Kuna vitu vimetofautiana!

    We kaa ukijizuka, oh Muhammad hivi na hivi! Shauri yako. Wazungu unaowategemea sasa hivi wanasilimu na wanaenda kupigana sirya, shauri yako!!!

    Like

  73. Noor mohamed says:

    NDUGU MHINA na WAKRISTO WENZIO NAWAOMBENI MUWE WAKWELI MUWEKE WAZI IMANI YENU ILI MUELEWEKE!!!!! SWALI ; HIVI KWA IMANI YA KIKRISTO YESU NI MUNGU? AU NABII? IKIWA KAMA NI NABI, NA NDIE NABII YULE ALIEBASHIRIWA NDANI YA BIBLIA KWANINI BASI NDANI YA MAKANISA HATUSIKII KUTAJWA MUNGU, IKIZINGATIWA HUYU NABI YESU ALITUMWA NA MUNGU KUJA KUWAFUNDISHA WATU NENO LA MUNGU, WATU WAMJUE MUNGU, KWANINI MSIMUABUDU MUNGU KAMA NABII YESU ALIVO TUMWA KUJA KUFUNDISHA? NA BADALA YAKE MNAKESHA MKIMUABUDU YULE ALIETUMWA ?HIVI KWELI HUYU NABII YESU ALIKAIDI AGIZO LA MUNGU? ALIPOFIKA KWA WATU AKAWAMBIA MNIABUDU MIMI? BINAFSIYANGU SIAMINI NA IKIWA KWELI YESU NDIE NABI YULE KAMA BIBLIA INAVO BASHIRI NA SI MUHAMAD S.A.W KAMA UNAVODAI WEWE MHINA , JE UTAKUBALIANA NA WAISLAM KUWA YESU SIO MUNGU BALI NI NABII?

    Like

  74. Stev kei says:

    METHALI: Sikio la kufa……halisikii dawa!!!!!!!…teh..teh…teh…….na hiyo tafkr ya homa iliyompanda Muft mkuu mhamad ndiyo imewekwa kiporo mpk mfngo wa ramadhani uishe au???

    Like

  75. Noor mohamed says:

    SWALI LAPILI JE IKIWA KWELI YESU NDIE NABII YULE KAMA UNAVO DAI WEWE MHINA, UNAWAMBIA NINI WALE WAKRISTO WENZIO, AMBAO HUKESHA WAKIPAYUKA WAKISEMA : NANUKUU ………………………. YESU NDIE MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU. UTAKUBALIANA NA WAISLAM TUNAPOSEMA WOTE HAO WAMEKUFURU KWA KUMWITA MUNGU ASIEKUWA MUNGU………… NA KILA ALIEKUFURU NI KAFIRI NA KILA KAFIRI ATAINGIA MOTONI JAHANAM

    Like

  76. Stev kei says:

    thatha km mimi nikikujibu mathwali li hayo,ndio utabadili dini na kuwa mkristo au..teh teh teh..!!

    Like

  77. Stev kei says:

    Shekhe Ibra, sijui mwenzetu umesomea shule gani wewe!…..Kumbe kitabu chako kitakatifu(qurani tukufu) Imeshakufundisha kuwa Torati na injili sio neno la Mungu linaloaminika kwa sababu vina mkono wa wanadamu kama biblia yenyewe inavyojieleza kwenye dibaji na sehemu nyingine….ninachokishangaa hapa ni kwamba mbona tena unatumia kitabu hicho hicho tena cha wanaadamu kusema kuwa kimemtabiri muhamadi?..hivi huoni kuwa unakwenda kinyume na maneno ya Allah na imani yako kwa kuwa kwa kawaida neno la mungu likiwa kweli linamikono ya wanadamu iliyochafua halifai looooteee!!.Je, kinachokusumbua akili kwenye biblia ni nini mpaka ukifuate?…INAMAANA UMUAMINI ALLAH MANENO ALIYOKUTAHADHALISHA?….Maana kama ni hivyo kweli basi isingekupasa kabisa kuangaika zaidi ya kuendelea kumuabudu Allah then mwisho tukaona result kama ni Sisi wakristo au ni nyinyi waislamu!….maelezo ya huko juu yako wazi mno kwamba quruani sio neno la mungu..hata huyo aliepokea(muhamadi) alithibitisha hilo yeye mwenyewe kwa kusema’Nahisi nafsi yangu imechezewa na mashetani na yameniharibu(zuga)akili yangu!!!!!!!…tatizo liko wapi hapo waislamu!!!!!….muhamad kaweka wazi kabisa yeye mwenyewe!!!!!!…Tena cha kusikitisha’AKADHURIKA KWA KUPATA MAHOMA TELE… TELE…TELE…TELE…TELE…TELE…TELE…TELEEEEeeeehh!!!!!!!..Huyo mungu wenu mwenye madhara mpaka kwenye manabii wake mwenyewe katika biblia anaitwa SHETANI!!…wakati kwenu anaitwa…….loh!.VYATOSHA WATOTO WASIJE WAKAOGOPA.

    Like

    • Ibrabura says:

      Stev Kei, unatakiwa uwe makini na ufuatiliaji wa hoja. Mimi sijasema kwamba taurat na injili sio neno la mungu! We umeipata wapi hiyo? Al-quran inatufundisha tuviamini vitabu vyote alivyoteremsha na mwenyezi mungu.
      AL-QURAN 3:3
      ”Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati na Injili”
      AL-QURAN 17:55
      ” Na Mola wako Mlezi anawajua vilivyo waliomo mbinguni na katika ardhi. Na hakika tumewafadhilisha baadhi ya Manabii kuliko wengine; na Daudi tulimpa Zaburi.”
      Kwa maana hiyo vitabu vilivyotajwa hapo,TAURAT NA INJILI kwenye biblia yako havipo!
      Baada ya kupotea hivyo vitabu, wanadamu sasa, wakafanya mpango wa kutaka kuvirejesha kwa kumbukumbu. Kwa mpango huo vikazaliwa KUMBUKUMBU LA TAURATI NA INJILI KAMA ILIVYOANDIKWA NA MATAYO, MARKO, LUKA NA YOHANA.
      STEV kama utakuwa mkweli utajiuliza kwa nini kuna matoleo kibao ya biblia. Yaani hakuna uhakika. Wanakisia labda kifungu fulani kilisema hivi au vile. Kwa hali kama hii neno la mungu limepotea.
      Kipengele cha dibaji ya biblia imeweka wazi swala hili. Tumeona jinsi gani watu, sio mungu, walivyobadili majina ya watu na maeneo. Stev! sema kweli neno la mungu hapo lipo?
      Stev, mimi siifuati biblia! Mimi naifuata AL-QURAN na naviamini, TAURATI, INJILI, NA ZABURI.
      Lakini kitu kimoja lazima niseme kweli, Biblia inaposema kweli, mimi nakubari kwamba hapo biblia imesema kweli. Na inaposema uongo, pia nakubari kwamba hapo imesema uongo.
      Ndugu yangu, mi nakushauri usiangalie Muhammad saw kapataje utume, we angalia mafundisho yake yanaendana na hali halisi tuliyokuwanae leo? Haya mambo ya kutetemeka sijui kafanya nini itakusaidia nini? Hapa chini nakupa onyo usirudie tena na kauli za kipumbavu. Sasa Muhammad saw katetemeka Mungu wako wewe mzinifu na kahaba wakutupwa!
      Isaya 23:17” Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, Bwana ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia”.

      Yeremia 3:14
      Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni mume wenu; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni;

      Swala la ushetani, kama ungejuwa usingesema chochote, kwa sababu shetaniuana ushirika mkubwa na wakristo:
      1TIMOTEO 1:20
      20 Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
      JE, umekubari kuwa Paulo alikuwa anashirikiana na shetani? kazi kwako!
      Matayo 4:1
      Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
      Kumbe hapa ulikuwa ni mpango wa mungu wa kutaka kumjaribu yesu, akapatana na shetani hatujui kwa ujira gani,
      Stev, haya ni machache kati niliyokuwanae. Nakutakia uelevu mzuri.

      Like

  78. Mhina says:

    Mr.ibra.Mimi sija kukimbia kabisa…Maana nisipoihubiri injili kwako nitaihubiri kwa nani tena!!.Ninadiriki kurudi tena kwa ajili ya kazi ya mungu nikiwa kondoo.Na haya ndiyo tulioitiwa hapa duniani…..Umesema wewe mwenyewe kuwa vitabu vya tor na injili sio vile vya mwanzo,ila vimebadilishwa,tena ukaongezea kwa kusema kuwa HAVIAMINIKI!!!….Sasa basi…kwa ushahidi wa maneno yako hayo na ushahidi wa Mungu wenu Allh alivyowafundisha,Biblia haiwafai kwa imani hata chembe kwa kuwa neno la mungu ni takatifu lisilopaswa kuwa na mikono ya wanadamu…kamwe huwezi kuliamini nusu nusu au sehemu sehemu kwa kuwa maneno ya mungu hayaambatani na maneno ya wanaadamu,si ndivyo ndugu?….Sasa wewe mbona unakwenda kinyume na mawazo yako pamoja na mawazo ya Allah kuiamini biblia nusu nusu au vi..mstari..mstari hapo huoni kuwa unapotosha hata waislamu wenzako?!!..Pia mimi sio mwalimu wa dini wala mtaalam wa kitabu chenu cha quran lakini nabaki kujiuliza kuwa kama mhamad mtume wenu aliwahakikishia kuwa torati na injili ni sahihi kwa muongozo hivi kwa mfano yule mtume paulo mnaesema alibadili injil na torati alifanya hivyo wakati gani…maana kipindi kuruani inathibitisha usahihi wa torati na injili, paulo alikuwa amekwisha kufa zaidi ya miaka 200,iliyopita…tena ukimlinganisha paulo na huyo mtume wenu mhamad ni kama babu kikongwe na kijukuu chake au hata ni zaidi ya hapo!!!…ndugu ibra.Kujua historia za dini na vyanzo vyake ni muhimu sana sana kuliko kujaribu kukumbatia na kutetea mambo usioyajua vizuri.Hiyo kauli iliyokutia jazba hapo juu na kusema isirudiwe kwa kuwa ni YAKIPUMBAVU ndio kauli ya ukweli wenyewe na siku zote UKWELI UNAUMA!!.Hapo juu kamwe hukuambiwa kuwa mhamad alitetemeka, usijaribu kutia neno rahisi ili kuhalalisha upuuzi na upotofu wako!!.Kilichosemwa hapo ni kwamba MTUME WENU MHAMAD ALIKIRI YEYE MWENYEWE KUWA ALICHEZEWA NA MASHETANI WAKATI ALIPOKUWA ANAPOKEA NENO LA MUNGU KWA AJILI YA WANADAMU WOTE…Hili sio jambo dogo la kupuuzia ndugu ibra.hii ni KESI KUBWA MNO MNO KUPITA HATA MAELEZO!!.Wote sisi tunajua kuwa kazi kubwa iliyomleta shetani hapa duniani ni kupindisha neno la mungu kwa kuwavuruga waalimu,mitume na manabii….Sasa basi, kama muasisi wa quran amekiri kuwa alinaswa na mashetani wakati anapokea neno letu tunalo litegemea litufikishe mbingumi kuna usalama gani au kuna hekima gani au kuna mafundisho gani tena hapo atakayo tuletea halafu eti na sisi kwa urahisi tu…tupokee ujumbe wake bila ya kutafakari ukweli wa mambo!!….wewe ndugu ibra unaonekana ni mtu mwenye akili na maarifa lakini cha kusikitisha maelezo yako na utetezi wako unaonekana kuwa ni wakitoto kwa sababu unajaribu kutetea njia ambayo hata hiyo njia yenyewe haiwezi kujitetea kama unavyotaka wewe!!!.TANGU LINI UKWELI UKAFANANA NA UONGO?.Eti unasema tusitazame kilichompata mhamad bali alichofundisha!!…loh!…UMESOMEA SHULE GANI KAKA IBRA?!….Shetani sio zuzu kama unavyofikiri bali ni kiumbe wa roho mwenye busara,hekima,maharifa,ujuzi,ujanja kupita sisi wanaadamu ndio maana aliweza pia kumdanganya Mzazi wetu wa kwanza Adamu pale bustani ya eden…sembuse sisi!!.Yeye shetani anachofanya ni kutumia mambo yote ya kweli ya mungu kama mafundisho mazuri yanayovutia…ili aweze kukuangusha kwa jambo dogo tu,litakalo kuangusha usipate yote ya mungu kule mbinguni.Anaweza kukuacha upate yote ya mungu lakini njia akakufichia.Ni kama sisi wanadamu tunavyo mtega panya kwenye mtego ili aingie akale chakula chote mule ndani lakini akishiba na kutaka atoke anagundua looh!…kumbe amenaswa na mauti iliokua imejificha!!.Ndugu ibra.Bwana yesu ndiye pekee ni njia ya kweli.Yeye ni kweli kabisa MWANA WA MUNGU,NABII WA MWISHO WA MUNGU,NENO WA MUNGU…NA KWA HALI HIYO ANALIDHIHILISHA JINA LA MUNGU NA UTUKUFU WAKE KWETU SISI WANAADAMU AKIWA NDIYE NJIA YETU YA KWELI ILI TUSIPOTEE.Hata ndugu ibra.kama yakupatabu kuamini hivyo basi,mimi nakuomba uishike njia hii ili uweze kujinusuru…usiangaikie mathehebu na makanisa na tabia fulanifulani za waumini bali kumbatia njia ya biblia nae mungu atakuona na kukuvuta ili akuokoe.Bwana yesu yeye sie mwana wa mungu kwa mambo ya kufikirika kibinaadamu ila biblia insema kuwa ALIDHIHILISHWA NA MUNGU KWA UWEZA KUWA MWANA WA MUNGU KWA JINSI YA ROHONI YA UTAKATIFU…AMBAPO KATIKA YEYE,SISI WANAADAMU TUNAPOKEA NEEMA YA MUNGU NA KUJIDHIHILISHA KWAKE KWA NJIA YA IMANI….NDIO MAANA BWANA YESU ALITANGAZA HIVI: HAYA MANENO NINAYO WAAMBIENI SIYASEMI KWA SHAURI LANGU BALI NI BABA AKAAE NDANI YANGU HUZIFANYA KAZI ZAKE!!!!!….Mwili wa kristo ni HEKALU LA MUNGU.Nae kristo ndiye tumaini letu sisi wanaadamu wote, sio wakristo peke yao..HAPANA.HAPANA….Waislamu sio maadui zetu,adui wetu ni shetani pekee aliekuja kuweka uadui wa milele baina yetu.Na huyo shetani biblia inatufundisha kuwa atajibadili kwa Kupendeza,kuvutia nk…kwa lengo la KUPOTOSHA WASIO MTAFUTA MUNGU WA KWELI KWA BIDII…Mwisho ndugu ibra.ni mashtaka ya uongo unayoyabainisha kuhusu biblia.kwa mfano jina la mungu kukaa na kumfunua mfalme wa tiro ambae ni shetani kufanya ukahaba na mataifa.,..wewe ni msomi ndugu ibra.hivyo usitafute mashtaka ya uongo tena wa kitoto kabisa kujifanya hujaelewa eneo lile na hayo maandiko yako mengine uliyo yatoa.Wakristo kila kukicha tunajibu mashtaka hayo kutoka mitandao mbalimbali lakini mnajifanya kama hamjaona majibu!!.Soma kwa makini maandiko hayo kuanzia juu kabisa utaona papara zako za uongo za kutafsiri neno la mungu vibaya pasipo kuelewa vyema halafu eti unaniambia mimi ndiye ninae soma maandiko juu juu!!!!,….UKIJIHISI NI KWELI HUELEWI UTANIAMBIA NIKUFAFANULIE VYEMA AU TAFUTA KANISA HAPO JIRANI YAKO ILI WAKUSAIDIE KWA…Tuendelee kubadilishana mawazo ndugu….niko kwa ajili yako lakini siko tayari kujibu hoja nilizokwisha zijibu huko juu….

    Like

  79. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina;
    kwa kuwa ndg zangu waislam wamekujibu baadhi ya maswali mimi naomba niyajibu haya matatu;
    SWALI;.(3) Muhamad anasema kuwa yeye ni msaidizi wa bwana yesu na ni nabii wa mwisho anaefaa kufuatwa (a) mbona sasa hakumsaidia bwana yesu kuihubiri injili yake kama walivyofanya wakina mtume paulo? Badala yake ameiletea dunia njia mpya ya uislamu na nguzo zake za kufuatwa,mambo ambayo hayapo kabisa katika torati ya musa wala injili ya bwana yesu.

    JIBU; Ndug Mhina, naomba kwanza uelewe kuwa manabii wote walikuwa waislam na mtume amekuja kuuhuisha uislam uliokuwa umepotea kutokana na baadhi ya waandishi wa kiyahudi kutia mikono yao katika maneno ya Mungu.Kwa hiyo hata nabii Yesu mwenyewe alikuwa muislam kwani “islam” ni neno la kiarabu lenye maana ya “unyenyekevu” na bwana Yesu alisema “jitieni nila yangu na mjifunze kwangu kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu(muislam) wa moyo…” yaani kwa maana nyingine bwana Yesu alikuwa ni Muislam wa moyo kabisa kwa hiyo nawashangaa “ukiristo” ilikuwa ni dini ya washirikina wa Antiokia huko uturuki, ambayo pia Paulo alikuwa mfuasi wake.(Matendo 11:26)

    PILI; naona Mhina na wakiristu hamuelewi nini maana ya injili; Injili maana yake ni maneno au maufundisho aliyoyatamka bwana Yesu kwa kinywa chake, ntakushangaa saana unaposema Paulo kafundisha injili ya Yesu.Kwa kifupi Paulo hakufundisha injili ya Yesu bali alianzisha injili yake ambayo inapingana na injili ya Yesu, kwa nini nasema hivyo. Agano jipya ina vitabu 27, katika hivyo Paulo kaandika vitabu 22 vya biblia inayoitwa agano jipya ambayo ndiyo wakiristu wanaiita injili, cha ajabu zaidi katika vitabu vyote alivyoandika Paulo(mtume wa uongo) hakuna hata neno moja alilosema Bwana Yesu kwa kinywa chake.Ni vitabu vinne tu vya agano jipya ndivyo vina 10% tu ya maneno ambayo Bwana Yesu alisema kwa kinywa chake, yaani injili na 90% iliyobaki ni maelezo ya waandishi wa vitabu hivyo na si maneno ya Yesu mwenyewe.(soma Biblia inayoitwa Red lettered bible kwa ushahidi wa haya)
    Je utaendelea kusema paulo aliifundisha injili ya Yesu?hebu soma hapa chini uone Paulo mwenyewe anasemaje

    WARUMI 11:13 “Lakini nasema na ninyi,, mlo watu wa Mataifa. Basi, kwa kadri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa, naitukuza huduma iliyo yangu”
    kwa hiyo wewe usiyetahiriwa(mmataifa Mhina), Paulo mwenyewe anasema huduma anayoitoa si huduma ya Injili ya Yesu bali ni yake yeye mwenyewe sasa utasemaje alihubiri injili ya Yesu?

    TATU; Injili ya Paulo inapingana na injili ya Yesu na Mungu pia lakini tunaona maneno ya Allah kupitia kwa Mtume yanafanana na maneno na mafundisho ya Yesu hivyo tunashawishika zaidi kuwa mtume Muhammad hakuitangua injili ya Yesu bali Paulo alikuwa mpinga Yesu na hakuwahi kuihubiri injili ya Yesu bali injili yake mwenyewe kama anavyosema.

    MANENO YA PAULO YANAPINGANA NA MANENO YA YESU.
    Wakiristu kote duniani wameaminishwa na Paulo kuwa Taurati imepitwa na wakati, lakini angalia Bwana Yesu mwenyewe anavyosema;
    MATAYO 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la sikuja kutangua bali kutimiliza kwa maana, amin nawaambia mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya Torati haitaondoka, hata yote yatimeialisema;”

    Yesu anasema yote yaliyo ndani ya torati lazima yafuatwe na yazingatiwe milele kwa mfano aya ifuatayo ya torati;

    MAMBO YA WALAWI 11:7-8 “Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheuwi, yeye ni najisi kwenu. Msiile nyama yao wala msiiguse mizigo yao; hao ni najisi kwenu”

    QURAN SURA 5:3.”Mmeharimishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na mnyama aliye chinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na aliye kufa kwa kunyongeka koo, na aliye kufa kwa kupigwa, na aliye kufa kwa kuanguka, na aliye kufa kwa kupigwa pembe, aliye liwa na mnyama, ila mkimdiriki kumchinja. Na pia ni haramu kula nyama aliye chinjiwa masanamu. Na ni haramu kupiga ramli. Hayo yote ni upotovu”

    msikie Paulo sasa,
    WAKOLOSAI 2:16 “Basi mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi au sabato”

    Mungu anataka watu wale vyakula vizuri kwa afya zao Paulo anasema kila kitu kinafaa! tusihukumiane kwa kula na kunywa.

    ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………….
    SASA TUONE MUNGU NA YESU WANASEMAJE KUHUSU MTU ANAYEIACHA TORATI.
    MATAYO 5:18 “Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi (za torati) zilizo ndogo, na KUWAFUNDISHA WATU HIVYO, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni”
    Na Mungu anasema;

    KUMBUKUMBU 27:26 “Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kuyafanya.Na watu wote waseme amina”

    lakini tunaona Bwana Paulo akifundisha watu kula kila mtu anachohitaji hata kiti moto,Mbwa, mijusi, paka,panya n.k. Sasa hapo ndo nawashangaa wakiristu wanadai eti biblia yao huku baadhi wanayaamini na baadhi wanayakataa na yote yapo ndani ya biblia.

    SWALI:(b)kabla ya hii dini yake ya kiislamu na nguzo zake za kufuatwa, watu wa zamani kabla yake walikuwa na dini gani ya kuwafikisha kwa Allah kupata ulevi? Yaani wao walikuwa dini gani kwa kuwa bado nguzo za imani muhamad alikuwa hajaziandika.(quran 10:104,6:14)

    JIBU; Ndugu Mhina, kwanza naomba nikushangae kwa sababu unaonekana hata nguzo za imani ya kiislam huzijui; Nguzo za imani ya kiislam ni sita nazo ni 1.kumuamini Mwnyezi Mungu 2.Kuwaamini malaika wa Mungu 3.Kuamini vitabu vya Mungu 4.kuwaamini mitume wa Mungu 5. kuamini kuwa kuna siku ya kiyama 6. Kuamini kadari za M/Mungu
    je kuna nabii yeyote ambaye hakuzishika nguzo hizi za uislamu? kwa hiyo hata Yesu alizishika nguzo sita za kiislam kwa hiyo na yeye alikuwa muislam 100%.

    Lakini pia nani kakwambia peponi kuna ulevi kaka yangu? Pole sana maana hata biblia inasema hivi “watu wangu wamekuwa kama kondoo waliopotea kwa maana wachungaji wao wamewapoteza” nafikiri kosa sio lako ni la wachungaji waliokufundisha kuwa peponi kuna kilevi. naomba ninukuu Quran inasemaje kuhusu kinywaji cha peponi;
    QURAN SURA ASSAFFAT 37:
    46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
    47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

    Sasa ndugu Mhina naona hapo ulipitiwa kidogo ndg yangu naomba uwe unasoma ndiyo unakuja kuelezea mambo vinginevyo utakuwa kituko humu kwenye mtandao.Kama hujui jambo ni bora ukauliza au ukanyamaza kabisa.

    Swala la kuwa na wanawake wema peponi hilo halina ubishi na ndugu yangu Ibrabra amekujibu vizuri kabisa, hizo ni fadhila za Mwenyezimungu kwa waja wake wema sijui tatizo lako liko wapi?

    48. Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
    49. Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika

    SWALI; (4) Kama ni kweli Mhamad alipokea neno la Mungu wa kweli kule mapangoni: (a) mbona alikiri yeye mwenyewe kuwa alichezewa na mashetani yakimzuga akili yake?

    JIBU; Swali lako ni marudio lakini kueleweshwa ni haki yako ndg yangu, Kwa kifupi mtume hakusema kachezewa na mashetani lah! bali alisema “nahofia nisije nikawa nachezewa na shetani” alitumia neno “nahofia” kwa hivyo hiyo ilikuwa ni hofu ya kawaida kwa mwanadamu anapotokewa na jambo jipya maishani mwake.
    lakini baadae Allah alimshushia aya ifuatayo na kumuondoa hofu yake hiyo kama Allah anavyosema ktk QURAN.

    QURAN SURA YA 26:ASH-UARAA.

    210. Wala Mashet’ani hawakuteremka nayo(hii quran),
    211. Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

    kwa hiyo mashetani hawawawezi hata kuisogelea quran;

    SWALI; (b) mbona malaika yule kama ni kweli alitoka kwa mungu alitumia njia mbaya ya kumdhohofisha mtume kwa kumkaba na kumminya hali iliyomsababishia majasho na homa huku akijitetea kua hajui kusoma

    JIBU; Kabla hujauliza hili swali ungeisoma biblia vizuri, hakika ungeona aibu kuuliza swali hili Kwani ungejua kuwa uelewa wako ni mdogo,tunaona katika MATENDO (9:6-10) Paulo alipoteza fahamu siku tatu alipodai kutokewa na Yesu. Je kupoteza fahamu siku tatu na kutokwa jasho ni ipi adhabu kubwa zaidi?

    .SWALI; (c) mbona kila muhamad alipokuwa anapata ujumbe mzuri wa malaika (ufunuo) kutoka kwa Allah anapandwa tena na homa kali uku uso ukibadilika rangi…kwanini hali hizi zitokee?…

    JIBU; Ndugu Mhina kwanza unatakiwa ujue kuwa maneno ya Mungu yana nguvu kubwa kwani Allah anasema katika QURAN SURA YA 59;
    21. Lau kama tungeiteremsha hii Qur’ani juu ya mlima, basi bila ya shaka ungeli
    uona ukinyenyekea, ukipasuka kwa khofu ya Mwenyezi Mungu. Na hiyo mifano
    tunawapigia watu ili wafikiri.

    kwa hiyo hapo Allah anakupa challenge ili ufikiri, anasema mlima ungepasuka kwa hofu ya kupewa heshima ya kupokea maneno ya Mungu.Je hali inakuwaje kwa Mwanadamu.Na ndiyo maana quran ilishuka kwa nabii mwenye nguvu ya Imani kuliko manabii wote waliomtangulia kwani tofauti na hapo hakuna nabii angeweza kustahimili kuipokea quran.Kama Bwana Yesu anavyodai mwenyewe katika Biblia;

    YOHANA 16:12-13 “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa Lakini yeye atakapokuja huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe,lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”

    Kwa hiyo hata Bwana Yesu alijua kuwa yeye hastahili kuyanena maneno ya quran bali kuna Mtume ajaye ambaye ni nabii Muhammad ndiye ataweza kunena kila jambo kama alivyolisikia kutoka kwa Mungu na kulisema bila kupunguza na hiyo ndiyo Quran.Lakini pia alisema maneno hayo ya Quran wale mitume wake Yesu kwa sababu ya imani yao haba hawataweza kuyastahimili kwa maana alijua ni maneno yenye nguvu hivyo yanahitaji mtu mwenye nguvu ya imani pia.

    Kwa niaba ya waislam wote nakushukuru kwa maswali yako; lakini naomba uwe unasoma halafu unauliza “nahofia” usionekane kituko kwa wasomaji;
    Ahsante.

    Like

  80. Mhina says:

    Ndugu mhammad yhn…..naona unajitahidi kumtetea mwajina wako pamoja na dini yake kwa udi na uvumba.Ni jambo zuri na la haki kwako, nakupongeza sana lakini mbona sasa umejibu maswali yale kwa kutumia msaada wa biblia kwa 100%?…ndivyo mnavyofundishwa huko misikitini kwamba muitetee dini yenu kwa msaada wa kitabu ambacho chote mnadai kuwa HAKIAMINIKI KWA KUWA KINAMIKONO YA WANAADAMU?,..Mbona sasa ukiiondoa biblia,Quran inaonekana haiwezi kujitetea yenyewe?…mbona mimi situmii wala nitakapokujibu hoja zako sitatumia kitabu cha quran hata kidogo?…..Sasa basi, kwa kuwa hukujibu maswali yangu kwa hekima ya dini yako halafu ukaamua kunitengenezea hoja nyingine za kujibu ndani yake…..ni kwamba mimi kwa sasa niko kazini lakini nikirudi tu…baadae au usiku nitakujibu hoja zako zote zote ulizozichomeka kwenye maswali yale.UBARIKIWE NDUGU.

    Like

  81. Mhina says:

    Ndugu.Mhammad yohana….UKRISTO ni kuwa mwanafunzi na mfuasi wa bwana yesu…nayo injili sio dini fulani wala watu fulani katika itikadi fulani bali injili ni habari njema kwa watu wote hapa duniani inayotangaza KUFA NA KUFUFUKA KWA BWANA YESU KRISTO AMBAPO KATIKA YEYE TUNAIONA NJIA NA KUPOKEA HURUMA YA MUNGU.Hivyo, mwalimu, mtume au nabii yeyote katika injili asie ihubiri injili na kutangaza kifo cha bwana yesu pale msalabani kuwa ni ukombozi kwa wanaadamu, basi ujue mwalimu huyo au nabii huyo ni MUONGO!!….Mtume wenu anaongoza kwa kulikataa jambo hilo!!….Mtume paulo hakuleta dini nyingine bali yeye alitimiza kanuni zote za kuihubiri injili ya bwana yesu.Pamoja na wewe kutaka kudanganya watu kwa kumnukuu mtume paulo kwa mkato mkato…lakini yeyemwenyewe anaweka wazi kwa kusema: BASI TU WAJUMBE KWA AJILI YA KRISTO KANA KWAMBA MUNGU ANASIHI KWA VINYWA VYETU,TWAWAOMBA NINYI KWA AJILI YA KRISTO MPATANISHWE NA MUNGU.(2 Wakorintho 5:20).Paulo hakujiinua wala kuhubiri jambo lolote jipya katika injili zaidi ya kumuinua bwana yesu pekee.Sasa,kama ametuandikia ujumbe mwingi unaomhusu bwana yesu,tatizo lako ndugu Mhammad ni nini? Kwanza yeye alikuwa mwanasheria,kwa hiyo kazi aliyoifanya bwana yesu aliielewa vyema zaidi ndio maana kila mtume ilimpasa asimame kwenye eneo lake.Istoshe paulo kuwahubiria injili mataifa,kamwe halikuwa kosa bali yalikuwa ni maagizo ya bwana yesu mwenyewe :ENENDENI ULIMWENGUNI KOTE MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.Soma(Marko 16:15)….hii ni kazi yetu aliyotupa bwana yesu kuwahubiria injili wale wasioamini na kamwe sio kazi ya mtu fulani pekee.Kwa hiyo,tunaona katika ile (warumi 11:13)…paulo anathibitisha huduma yake hiyo aliyopewa na bwana yesu ya kuihubiri injili katika mataifa…unapofanya kazi ya utumishi au huduma yeyote ile uliyopewa na aliye juu yako unahaki kabisa ya kusema HII NI KAZI YANGU…Ili uitumikie vyema na kwa moyo..,..lakini chakusikitisha kwa waislamu kwa kuwa kazi yao ni kupinga kila kitu na kujifanya hawaelewi, basi hilo pia ni tatizo kwao…wakimtuhumu paulo kuwa anasema injili ni yakwake!!!!.Halafu ndugu.Mhammad wewe unasema kuwa ,uislamu ni’ UPOLE NA UNYENYEKEVU….Sasa kama ni kweli, mbona nyie kwa asilimia kubwa ndio mnaonekana sio wapole na wanyenyekevu?…mpo wangapi nyinyi? na huyo mwalimu wenu mpole na mnyenyekevu yuko wapi kwa sasa?…sisi bwana yesu tunaemuamini anaetufundisha upole na unyenyekevu AMEFUFUKA HAYUPO KABURINI TENA YUKO MBINGUNI ANAFANYA KAZI YA KUTUPATANISHA NA MUNGU KWA UPOLE NA UNYENYEKEVU….Sasa,nyie mnao mkataa bwana yesu mbona mko yatima na nyinyi mnakubali?….ndio maana hamueleweki kwa sababu mchungaji amekwisha kimbia kondoo wake lakini sisi bado ni kondoo wa mchungaji mwema.Soma(yohana 10:10-14).Pia unaposema uislamu ni upole na unyenyekevu basi inamaanisha kuwa mtu yeyote yule mpole na mnyenyekevu hata akiwa mpagani au haendi msikitini kila siku anakuwa na haki ya kujiita muislamu…na kama ni hivyo ni kheri mngeifunga hiyo miskiti yenu yote kwa kuwa huku mitaani kuna wapole na wanyenyekevu wengi mno,kwa hiyo hawa tayari wanavigezo vya kuwa waislamu maana wao pia ni ‘ISLAM’ > WAPOLE NA WANYENYEKEVU!!!…loh!..kumbe dini ya kiislamu ni rahisi tu…si ndivyo ndugu Mhamad na waislam wenzio?…..Sisi kwa upande wetu hakuna jambo la mzaha na lisilokuwa na maelezo ya kueleweka kama hivyo…hii ni njia maalum na imani ambayo chanzo chake ni mungu mwenyewe…na kamwe sio sifa fulani za mtu au tabia fulani fulani pekee!!…nikiendelea kukujibu hoja zako katika staili ya maelezo ni kwamba,Bwana yesu katika ile (mathayo 5:17)..alisema: Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii la, sikuja kutangua ‘BALI KUTIMIZA’…..Kwa hiyo mpaka hapo kwanza tunagundua kuwa MTIMIZA TORATI NI BWANA YESU…Sio sisi wanadamu hapana!…kwa kielelezo cha waisrael walivyoshindwa ni wazi kuwa hata sisi ni wadhaifu…hatuwezi kumtendea mungu vile anavyotaka katika torati yaani tufaulu kwa 100%…na jambo hilo tukilishindwa kwa mungu alie mtakatifu ATATUHUKUMU KWA KUWA YEYE NI MTAKATIFU KATIKA MANENO YAKE!!…injili ni huruma ya mungu kupitia bwana yesu, hivyo…Mungu alipomleta bwana yesu, hakumaanisha tena sisi wanadamu tuliowadhaifu kila wakati, tutimize mahitaji ya kutembea na kutimiza mahitaji ya torati, sivyo!!…bali ni bwana yesu ndie atimize kwa ajili yetu kama alivyosema yeye mwenyewe hapo juu…na kama nyie waislamu mnajaribu kutimiza kwa juhudi zenu wakati mnajua fika kuwa yodi na nukta kibao za torati mnaziacha, basi ni wazi kabisa kama ndugu.Mhamad ulivyoonyesha ile (kumbuk 27:26)…inasema: NA ALANIWE ASIYEYAWEKA IMARA MANENO YA TORATI HII KWA KUYAFANYA!!!!…..Kwa hiyo ndugu waislamu nyie mtakua ni wa kwanza kutangulia katika hukumu ya mungu siku ya mwisho!!.Inatisha sana lakini kama hamtabadilika basi ukweli wa maneno ya mungu nayo hayatabadilika mpaka yawahukumu.Nyie wenyewe mnalijua hilo wazi kuwa hamuwezi kutekeleza sheria za mungu kwa 100%…huku masikini sheria nyingine kama kuwa adhibu waizi kwa kuwa kata mikono au kuwapiga mawe wazinifu hamtekelezi sheria hizo za mungu kwa kuziita ni SHERIA ZA MAZINGIRA…Yaami mazingira yakikataa mungu mnamwambia hatuwezi!!!..loh!…shetani kaficha njia halafu kaweka mauti!!!!.Lakini tunaona kwa upande wa sisi wakristo, muendelezo wa mungu katika kuwakomboa wanaadamu unaendelea vyema kupitia kitabu kitakatifu cha biblia.Sisi bwana yesu ndiye mkombozi wetu wa kutukomboa kutoka katika mauti hayo ya haki ya neno la mungu.Biblia yaweka wazi kwa kusema: HUKUMU ZA BWANA NI KWELI, ZINA HAKI KABISA!!!.Soma(Zaburi 19:9).Kwa hiyo,ili bwana yesu aweze kutuokoa,yeye ndie iliembidi atimize sheria zote za mungu katika torati kikamilifu.Biblia kuhusu kile alichokifanya bwana yesu katika torati ya Mungu inasema: HATA ULIPOWADIA UTIMILIFU WA WAKATI, MUNGU ALIMTUMA MWANAE AMBAYE AMEZALIWA NA MWANAMKE, AMEZALIWA CHINI YA SHERIA KUSUDI AWAKOMBOE HAO WALIO CHINI YA SHERIA.Soma(galatia 4:4-5).Bwana yesu pekee ndie aliefaulu kwa 100% kutimiza mahitaji yote ya torati ya mungu kwa ajili yetu ili asimame mbele zetu akiwa ndie njia ya pekee.Kwanza alithibitisha kuwa ni kweli ya kwamba manabii na mitume walimuandika yeye kuwa ndiye mkombozi atakaekuja kufanya kazi hiyo,Pale alipowaambia wanafunzi wake hivi: HAYO NDIYO MANENO YANGU NILIYOWAAMBIA NILIPOKUWA NIKALI PAMOJA NANYI YA KWAMBA NI LAZIMA YATIMIZWE YOTE NILIYOANDIKIWA KATIKA TORATI YA MUSA NA KATIKA MANABII NA ZABURI.Soma(luka 24:44).Hapo tumeona kuwa kumbe MTIMIZA TORATI YA MUNGU NI BWANA YESU!!!…Halafu baada ya hapo ndipo anatupa njia ya unyenyekevu na upole mbele za Mungu….na kamwe sio kama waislamu wanavyojaribu kujinyenyekeza kwa upole katika ile torati ya Mungu, jambo ambalo halipo kabisa!!…kazi ya sheria za mungu sio kujinyenyekeza na kujipimia huruma wewe mwenyewe,..IA HASHA!!…Kazi ya sheria ni KUFUATWA KWA 100% KUSOMA DHAMBI NA KUHUKUMU…Kwa kuwa zinasimamia haki ya Mungu.Baada ya hapo, tunaona kuwa zile taratibu fulani fulani na miiko ya torati kuhusu mwili,kama kula,kutawadha nk….havina unajisi wa kutushtaki tena mbele za Mungu kwa kuwa, sheria zile na taratibu za torati za awali, bwana yesu amezikamilisha zote…Biblia inauliza: NI NANI AWEZAE KUWASHTAKI WATEULE WA BWANA?….Maana tumekuwa barua ya kristo iliyoandikwa mioyoni mwetu.Sio Paulo tu…hata bwana yesu mwenyewe alisema:HAKUNA KITU KILICHO NJE YA MTU AMBACHO KIKIMUINGIA CHAWEZA KUMTIA UNAJISI, BALI VILE VIMTOKAVYO NDIVYO VIMTIAVYO YULE MTU UNAJISI KWA SABABU HAKIMUINGII MOYONI ILA TUMBONI TU,KISHA CHATOKA NA KWENDA CHOONI.( Marko 7:15-23).Hali hii haitupi uhuru wa kula kila kitu ovyo ovyo…bali lazima tuchague vitu vinavyo tufaa kwa afya zetu pasipo kuwachafua na wengine.Paulo ameeleza kama alivyoeleza bwana yesu na kamwe hakuna hata sehemu moja paulo aliposema KULENI NGURUE….Acha uongo wako ndugu Mhammad!!.Sisi tumekuwa haswa ni wenye kujinyenyekeza tu, mbele za Mungu kwa kufuata sheria zake ndani ya mioyo yetu.Paulo anakazia jambo hili kwa kusema: ILI MAAGIZO YA TORATI YATIMIZWE NDANI YETU SISI TUSIOENENDA KWA KUFUATA MAMBO YA MWILI,BALI MAMBO YA ROHO.Soma(warumi 8:4)….Ndivyo pia alivyosema bwana yesu: MUNGU NI ROHO, NAO WAMUABUDUO YEYE IMEWAPASA KUMUABUDU KATIKA ROHO NA KWELI.Soma(yohana 4:24)….Pia ndivyo Mungu mwenyewe alivyoahidi kwetu: NITATIA SHERIA YANGU NDANI YA YAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAIANDIKA, NAMI NITAKUA MUNGU WAO NAO WATAKUA WATU WANGU.Soma(Yeremia 31:31-34)……Sasa ndugu. Mhammad na Waislamu wenzako, hebu nionyesheni hiyo dini ya Mtume paulo katika haya majibu yangu?!!…kwa ujumla ni kwamba, manabii wote wa Mungu katika biblia wameifua kweli ya Mungu kwa kutujulisha kuwa Sisi wanadamu ni watenda dhambi kwa asili yetu, hivyo kamwe hatuwezi kuishinda dhambi kwa uwezo wetu sisi wenyewewe pasipo msaada wa Mungu….Msaada pekee aliotupa Mungu ni kupitia Bwana yesu,ndio maana bwana yesu mwenyewe alilithibitisha jambo hili kwa kusema: MTU ATAKAYE KUIOKOA NAFSI YAKE, ATAIPOTEZA NA MTU ATAKAE IPOTEZA NAFSI YAKE KWA AJILI YANGU ATAIOKOA.Soma(mathayo 16:25)…..Ndugu.Mhammad, nimalizie kwa kukushangaa sana!!…Wewe umesema kua umejibu maswali yale kwa niaba ya Waislamu wenzio, hivi ni kweli?….kama ndivyo mbona sasa umetia aibu wenzio?….yaani umeweweseka na kujichanganya ukitumia vitabu vya imani zote…Yule Mtume paulo mnaesema anahubiri injili za kimashetani ndie huyo huyo ulie mfananisha na mtume wenu mhamad katika upokeaji wake wa neno la Mungu ijapokuwa wala havifanani kabisa kabisa!!!…wewe ulikuwa unajibu ilimradi uondoe ile aibu ya yale maswali lakini chakusikitisha ni kwamba wale ndugu zako walishindwa kujibu yale maswali mawili na wewe umeshindwa kabisa kujibu yale matatu ulioyachagua wewe mwenyewe!!!……LABDA UJARIBU TENA KUJIBU PASIPO KUTUMIA MSAADA WA KITABU MSICHOKIAMINI….YAANI BIBLIA TAKATIFU NIONE KAMA UTAWEZA!!!…Njooni kwa bwana yesu…Mbarikiwe.

    Like

  82. Ibrabura says:

    Mhina, mimi nilikuwa najibu kila swali lako kutokana na jinsi ulivyo uliza! Moja kati ya maswali yako, ulitaka uthibitishiwe japo kwa aya moja moja kutoka kwenye taurat na injili, ili Mwenyezi Mungu asionekane muongo, juu ya ujio wa Nabii Muhammad saw ukinukuu kifungu cha Al-quran kinachosema:
    157. Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanaye mkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili, anaye waamrisha mema na anawakanya maovu, na anawahalalishia vizuri, na ana waharimishia viovu, na anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyo kuwa juu yao. Basi wale walio muamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa pamoja naye – hao ndio wenye kufanikiwa. QURAN 7:157.
    Kwa upande wangu mimi, katika kulijibu swali ili nimetafuta TAURATI na INJILI kama inavyoelekeza hiyo aya, sikuvipata. Ikanibidi sasa, nifungue kitabu kiitwacho bibilia. Mwanzoni mwa kitabu nikasoma dibaji, nikapata maelekezo ya kwamba kuna MAJINA YA WATU NA YA MAENEO ZAIDI YA 3500 YALIYOTENGENEZWA. Nikajiuliza, hivi kweli jina la Muhammad nitalikuta kwa mtindo huu? Nikaendelea mbele, nikakuta pameandikwa KUMBUKUMBU LA TAURATI. Sikujali kwa sababu shida yangu ni TAURATI.Mbele kabisa nikafungua Kijitabu cha YEREMIA 8:8 kikaniweka sawa tena kama vile vya kwenye dibaji.
    Nilipogeukia upande wa INJILI nilijuwa kwamba sasa mambo yatakuwa shwari. Haa!!! nilipocheki vizuri nikaona pameandikwa INJILI KAMA ILIVYOANDIKWA NA….Sikupata shida nilijua hii siyo yenyewe. Paulo na yeye anadai ANENALO ANENI AGIZO LA BWANA…Paulo tena katika kuwafanya watu wamjue mungu anamshirikisha shetani timot 1:20.
    Mhina! Biblia kwa jinsi ilivyo ni kama karanga. Ukizimenya utakutana na mzima na mbovu. Kwa kigezo hicho nimetumia katika kukujibu hoja hiyo. Halafu, sisi waislamu tunatumia QURAN TUKUFU pamoja na HADITH ZA MTUME. Tofauti na hapo hatutumii kitabu cha aina yoyote.
    Lakini, kwa kuwa nyinyi ni wabishi wa kuelewa inatubidi tuwachape kwa kutumia kitabu chenu.
    Mhina! kitu kimoja nimengundua kutoka kwako, kwamba hii mada imekushinda na unatafuta sehemu ili ujishikilie. Kama we kidume tiririka na hizo aya nilizotoa kwenye kumbukumbu na injili kama ilivyoandikwa. Utaweza wapi! Usiwe mbishi! Eti we ni mwanakondoo….thubutuu!!! we ni nguruwe na mbwa kwa mujibu wa Yesu.
    Eti mmeambiwa muhubiri injili kwa kila kiumbe, sasa mbona…Kifungu chenyewe hakinauhakika kwa sababu Marko inaishia kwenye 16:8 sasa hii 16:9-20 inatoka wapi kama si kipachiko?
    Wayahudi waliyo mkubali yesu wana injili moja tu ya matayo katika agano jipya mbona imetofautiana sana na injili matayo mlizokuwa nazo nyie?
    Halafu, Mhna kwa nini unataka kutugombanisha na Yesu? Sisi tunamwamini sana, kwa sababu ni mmoja kati ya mitume wa mwenyezi mungu kwa wana wa Israeli. Mafundisho yake yanafaa kufuatwa. Lakini, yeye si wakusikilizwa peke yake na wengine pia lazima wasikilizwe na wafuatwe. Kwa kinywa chake yesu, alisikika akisema “yafaa mimi niondoke, maana nisipoondoka mimi huyo msaidizi hatokuja. Ina maana huyu msaidizi anatakiwa na yeye asikilizwe na afuatwe! Mnakwama wapi wakristo?
    MWISHO KABISA YESU ALIKUJA KWA AJILI YA WANA WA ISRAELI WALIOPOTEA AKIWA NA MAANA KWAMBA KUNA WENGINE AMBAO HAWAKUPOTEA. HAKUJA NA TARATIBU WALA SHERIA MPYA!

    Like

  83. Mhina says:

    Bwana Ibra.Mimi naona nikuachie hapohapo kwa kuwa ninapozitazama hoja zako,nakuona kuwa unamitazamo yenye matatizo makubwa sana!!.

    Like

  84. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina,
    Nizitangulize shukurani zangu kwa Allah kwa kuwa sasa naona umeanza kuelewa mafundisho matakatifu ya uislam. Allah anisaidie Inshaallah nikueleweshe zaidi na mwisho upate kumtambua.

    KWANZA; Naomba nianze kwa kuelezea maana ya uislam, yaani unyenyekevu, Ndugu Mhina mtu yeyote hawezi kuwa au kuitwa au kujiita mnyenyekevu kama hamjui Allah. Huyo anaitwa sheitwan au kafiri. Hakuna upole au unyenyekevu kama wewe hujawa muislamu , Ni kama Allah anavyotuambia katika aya zifuatazo.
    QURAN SURA YA 2.
    45. Na tafuteni msaada kwa kusubiri na kwa kuswali; na kwa hakika jambo hilo ni
    gumu isipokuwa kwa wanyenyekevu,

    Kwa hiyo Allah anatupa condition ya unyenyekevu ni lazima mtu awe anaswali na awe na subira.na pagani hawezi kuswali.Pia Allah anasema katika aya ifuatayo;

    QURAN SURA YA 22.
    32. Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika
    unyenyekevu wa nyoyo.

    katika iyo aya ya 22 Allah anaelezea maaana ya unyenyekevu wa Moyo kama alivyokuwa Bwana Yesu na manabii wote waliokuwa waislam kwamba mtu mnyenyekevu lazima azitukuze ibada za Allah.Sasa pagani hana sifa ya kuzitukuza ibada za Allah kwa hiyo hawezi kuwa mnynyekevu.

    QURAN SURA 7
    205. Na mkumbuke Mola Mlezi wako nafsini kwako kwa unyenyekevu na khofu, na bila
    ya kupiga kelele kwa kauli, asubuhi na jioni. Wala usiwe miongoni wa walio
    ghafilika.

    kwa hiyo ndugu Mhina, Unyenyekevu sio kuongea kwa sauti ya chini,au kula umeinama au kucheka huku umeshika mdomo, au kumsalimia mtu kwa kupiga magoti. Hapana ndugu yangu, Unyenyekevu ni lazima umjue Mungu yaani uwe muislam ndiyo matendo yako sasa kama muislamu uthibitishe unyenyekevu wako.

    PILI; Kuna kauli ambayo wakiristu wengi hawaielewi, kauli hii inasema hivi;

    MARKO 16:16 Akawaambia enendeni ulimwenguni mwote,mkaihubiri injili kwa kila kiumbe.
    Hizi ni kauli ambazo zilikuwa zikitumika kwa maana nyingine lakini watu wakieleweshwa maana nyingine.
    Bwana Yesu hapa alisema injili ihubiriwe ulimwenguni. Neno “ulimwenguni” linamaanisha Ulimwengu wa Israeli kwa sababu yeye alikuwa mtume kwa ajili ya watu wa Israeli tu.Ukisoma aya ifuatayo katika biblia itakusaidia kutambua kuwa neno ulimwenguni lilikuwa na maana gani;

    LUKA2:1 Siku ile amri ilitoka kwa kaisari Augusto ya kwamba iandikwe orodha ya majina ya watu wote wa ulimwengu.

    Hapo Luka anatwambia kuwa mfalme aliagiza watu wa ulimwengu wote waorodheshwe majina yao, huyu alikuwa mfalme wa taifa la israeli kwa hiyo alikuwa anamaanisha watu wote wanaoishi katika ulimwengu wa israeli wahesabiwe. Usitake kuniambia kwamba na mababu zako huko mwanza,kigoma,sumbawanga, marangu, eldorate, kampala n.k walihesabiwa, hapana! .Kwa hiyo biblia inaposema ulimwengu wewe ndugu mkiristu wa Tanzania, Uganda, Kenya,marekani n.k ujue haumo.

    Biblia ikitumia neno “ulimwengu” inamaanisha kitu tunachokiita “nchi” kwa lugha ya sasa, na ndiyo maana ukisoma cover page za biblia imechorwa ramani ya ulimwengu wa zama hizo ambamo tanzania,uganda,rwanda,burundi n.k hazimo.Lakini pia biblia inapotumia neno “nchi” huwa inamaanisha kitu tunachokiita “ulimwengu” kwa lugha ya sasa ikiwa inamaanisha dunia nzima.kwa hivyo ni jinsi lugha inavyobadilika wakati mwingine kutokana na nyakati. Kwa hiyo basi Bwana Yesu angesema enendeni katika nchi, hapa tungeamini moja kwa moja kuwa na sisi tunausika na maagizo hayo.Na ndiyo maana ukisoma katika kitabu cha MWANZO 1:1-2 “Inasema Mungu akaumba nchi” ikiwa inamaanisha dunia au ulimwengu.

    Lakini pia kama, ilikuwa inamaanisha injili ihubiriwe kwa kila kiumbe sasa mbona hatuwaoni wakiristu mkiitekeleza hii amri,mbona mbuzi,ng’ombe,miti,mawe,mbwa,mijusi n.k nao hamuwahubirii injili kwa sababu nao ni viumbe pia.Je hamuoni kuwa hii amri haiwahusu kwa sababu bila shaka mngekuwa mnaitekeleza kwa kuyahubiri mawe,kuku,mbwa n.k

    Lakini pia kuna kauli nyingine ambayo wakiristu wanashindwa kuelewa pia nayo ni hii hapa chini.
    MATAYO 28:19 Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi

    Watu wanaotaka kupotosha, hapa wanasema eti kauli hii inamaanisha mataifa hata huku kwetu Tanzania,Kenya,Misri, n.k tumo, Ndugu wakiristu Biblia inaposema “mataifa yote” ni tofauti na kusema “mataifa wote”. Biblia inaposema “mataifa yote” inamaanisha yale mataifa 12 ya Israeli tu ambayo mimi na wewe hatumo.Lakini kama Bwana Yesu angekuwa anamaanisha kwamba hata sisi tumo basi ingetumika kauli hii “mataifa wote” na si “mataifa yote”.

    Ndugu Mhina, Hata Ukisoma biblia ya Kiingereza kwenye METHEW 28:19 limetumika neno ” Nations” na siyo “Gentiles”.Maneno haya yote kwa kiswahili yanatamkwa kama “Mataifa” lakini yana maana tofauti kabisa.Kwa sababu biblia inapotumia neno “Nations” inakuwa inamaanisha “mataifa ya Israeli” lakini inapotumia neno “Gentiles” inamaanisha “mataifa wote” ambao mimi na wewe tumo, na waganda na wakenya n.k wamo pia.

    Either, Kuhusu sisi ,watanzania wazimbabwe, wahindi n.k Bwana Yesu aliwakataza wanafunzi wake kuhubiri injili yake katika mataifa na hii inathibitisha kuwa alikuwa mtume kwa ajili ya mataifa ya israeli; ukisoma
    MATAYO 10:5 “wala katika njia ya mataifa msiende….bali ishikeni njia ya kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya israeli”

    Hapo hata biblia ya kiingereza katika MATHEW 10:5 imetumia “Go ye not to the Gentiles….” Haijatumia neno “Nations”.

    kwa kifupi zipo aya nyingi sana ambazo Bwana Yesu aliwakataza wanafunzi wake kwenda kwa “matiafa” yaani “gentiles”.ambao ni mimi na wewe.

    PILI; Umesema pia kuwa Bwana Yesu ndiye amekuja kutimiza torati na manabii kwa ajili yenu, hapo Bwana Yesu alikuwa anamaanisha kuwa amri za torati zitaendelea , kwa sababu katika ufafanuzi wake alisema hata mbingu zidondoke amri hizo hazitaondoka. pia Yesu alisema katika maneno yafuatayo kuwakanya wale waliokuwa wakiiacha sheria;

    MATAYO 23:25 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria , yaani adili, na rehema na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache. viongozi vipofu wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia. na rehema na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala

    Kwa hiyo unapodai kuwa, Bwana Yesu ndiye anayewatimizia sheria za Mungu halafu nyie mkae tu, mpumzike na kula bata duniani halafu kesho muingie peponi, unakuwa unajidanganya kwani ingekuwa hivyo Bwana Yesu asingewasisitiza kwa kauli hiyo hapo katika MAT 23:25 kuwaambia Mafarisayo, bali angewaambia wasifanye mambo ya sheria,wapumzike tu kwani yeye amekuja kuitimiza na kufanya Sheria kwa ajili yao ili awakomboe.

    Lakini pia hata kama nyie hamuwezi kuzitekeleza sheria za torati kwa 100% siyo sababu ya kusema kuwa hazipo kwani hata hiyo mnayoiita iinjili hamuitekelezi yote pia kwa 100%(ukitaka ushahidi nitakupa).Kwa hiyo Mungu ndiye anayejua udhaifu wa mwanadamu wewe unatakiwa kujitahidi kufanya ukishindwa kufanya baadhi ya maamrisho basi Mungu yeye anaona na kwa hakika ni msamehevu lakini siyo kupinga eti kisa umeona huwezi kufanya 100% basi imekufa haipo.

    Lakini pia mnadai Bwana Yesu ni njia ya kuelekea Mbinguni, lakini ajabu njia yenyewe hamuifuati kwa sababu Yesu mwenyewe aliishi chini ya torati na alizitekeleza sheria zote lakini nyie mnaojiita wafuasi wake mnaishi nje ya amri za torati.Sasa kuna haja gani ya kujiita wafuasi wa Yesu au yeye kumuita njia na hali hamumfuati? Sasa Yesu alikuwa ana maana gani alipowaambia wanafunzi wake “nyinyi mwaniita mwalimu na Bwana nanyi mwanena vyema…” Hivi mwanafunzi gani asiyemfuata mwalimu wake.au Mwanafunzi gani anayesema mwalimu wangu ameshanifanyia mtihani kwa hiyo mimi sisomi au ni mwalimu gani anamfundisha mwanafunzi halafu anamfanyia mtihani huku mwanafunzi wake akila bata? Hakika hii ni fikra potofu kabisa ndugu wakiristu ya kusema mwalimu Yesu ametekeleza majukumu yake ya kufundisha lakini pia kwa sababu vichwa vya wanafunzi wake ni vizito ametekeleza majukumu ya wanafunzi wake kwa kuhofia kwamba hawawezi kufanya kwa 100%.hii ni fikra potofu kuliko zote ambazo nishawahi kuzisikia duniani.

    Mwisho, Ndugu Mhina Kutumia vitabu vyote siyo dalili ya kujichanganya, bali nataka kukufanya uelewe zaidi, kwa sababu nikitumia maneno Ya Quran tu, Mathalani,waislamu tunaposema Yesu sio Mungu, nautumia ushahidi wa Quran ambao uko wazi lakini wewe kama mkiristu unakataa na unatumia Biblia ambayo unaiamini kutoa ushahidi wako, kwa hiyo mimi mwenyewe lazima niisome biblia ili nione kama unasema kweli halafu nilinganishe na Quran. na hii ni kawaida kwa mtu yeyote anayetafuta ukweli, huwezi kutafuta ukweli kwa kuangalia upande mmoja tu kwani hata mahakamani hawahukumu kesi mpaka wasikilize pande zote mbili na hiyo ndiyo jinsi ya kutafuta haki na ukweli.

    Kwa mjadala huu nimeufunga kwa upande wangu labda ukija na hoja mpya nitakujibu.

    Like

  85. Mhina says:

    ndugu.Mhammad yohana….Usifunge mjadala ambao haujaisha,wewe ukishindwa,mpasie hata shekhe wako hapo pembeni ili akusaidie.Nashukuru Mungu ya kwamba umeanza kuijua injili ipasavyo mpaka hata mtume paulo naona hukumlaumu tena!!…..Eleweni waislamu kuwa bwana yesu kamwe hajawahi kuwa na dini au njia inayoitwa ISLAM au kwa kiswahili UNYENYEKEV, kwa kuwa hiyo sehemu tu ya sifa zake maana sisi wote tunatambua kuwa unyenyekevu ni sifa tu ya kibinaadamu na kamwe sio njia au dini fulani.Sasa kama nyie waislamu mnachukulia hiyo sifa ya moja ya unyenyekevu kuwa ndiyo kiwakilishi cha kumzungumzia bwana yesu kuwa alikuwa muislamu(mnyenyekevu) basi hivyo vitakuwa ni vichekesho vikubwa sana nilivyowahi kuvisikia!!.Hii ni kwa sababu zamani hakukuwa na dini inayoitwa UNYENYEKEVU au kwa kiarabu ISLAM…Hapo mmepotoshwa waziwazi ndugu zangu.Bwana yesu yeye alitumia torati ya Mungu kupitia nabii Musa, Zaburi na manabii.Hakuna ibada za Allah ambazo bwana yesu alizitekeleza hata kidogo.Bwana yesu katika biblia takatifu,kwenye ibada zake za kawaida hapo zamani tunamuona anatumia vitabu ambavyo vimo katika biblia ambavyo havihusiani na Uislamu.Hapo ilikuwa ni kabla ya ukombozi aliotuletea kwa njia ya injili…yaani ulikuwa ni wakati wa yeye kutimiza torati,zaburi na manabii.Hivyo hata katika ibada zake za kawaida tunamuona akitumia chuo cha nabii isaya kilichokuwa ndani ya biblia pekee.Tunasoma katika biblia hivi: AKAENDA NAZARETI, HAPO ALIPOLELEWA, NA SIKU YA SABATO AKAINGIA KATIKA SINAGOGI KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YAKE, AKASIMAMA ILI ASOME, AKAPEWA CHUO CHA NABII ISAYA AKAKIFUNGUA CHUO,Soma(Luka 4:16-17)….Hicho chuo alichokifungua na kukisoma bwana yesu katika ibada yake hiyo, kipo katika biblia pekee….sasa waislamu inawapasa kujiuliza kuwa huo uislamu wa zamani wa bwana yesu ulitoka wapi?!!…..Lakini unaweza kugundua pia kwamba wakati ambapo mhamad mtume wa waislamu analeta dini yake mpya ya UNYENYEKEVU USIOELEWEKA > UISLAMU Pamoja na zile taratibu zake mpya(nguzo)….Manabii wote pamoja na bwana yesu mwenyewe walikuwa wamekwisha kufa zaidi ya miaka 400 iliyopita!!….tena chakusikitisha ni kwamba hata yule mtume wetu paulo wanaedai kuwa alichakachua neno la Mungu hakuwepo kabisa kabisa maana nae alikwisha kufa zaidi ya miaka 200 na zaidi kabla ya Mtume wa waislamu na dini yake kuzaliwa!!!.Hizi ni kumbukumbu za ajabu sana sana halafu eti leo mtu anakuja kirahisi tu kupinga neno la Mungu la kweli na kutoa sababu za kipuuzi!!….Eti zamani ulimwengu uliitwa ULIMWENGU WA ISRAEL na nchi iliitwa DUNIA NZIMA!!!….loh!!..Sasa kama maelezo yako hayo yangekuwa ni kweli ndugu.mhammad, mbona tukisoma ile (luka 2:8) tunaona inasema:’Na katika ‘NCHI’ ileile walikuweko wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku….hebu sasa jiulize wewe mwenyewe kuwa, MBONA WALE WACHUNGAJI HAWAKUKAA KATIKA MIPAKA YA DUNIA YOTE ILI KUCHUNGA HAO KONDOO ZAO NAWAKATI WEWE UNASEMA KUWA NCHI KWA MUJIBU WA BIBLIA NI DUNIA YOTE?…MBONA HAPO BIBLIA INASEMA WALIKAA KATIKA NCHI ILEILE?,..JE, WACHUNGAJI WAKICHUNGA KONDOO ZAO WANAKAA KATIKA MIPAKA YOTE YA DUNIA AU KATIKA MIPAKA YA NCHI/MIJI YAO PEKEE?…..Lakini mimi nafahamu kuwa lengo lako lilikuwa ni kuonyesha kuwa bwana yesu ni mtume wa israel pekee,yaani yale makabila 12 ya watoto wa yakobo ulitaka uwaite ulimwengu wote!! ajabu kwelikweli.Lakini hata kama ingekua ni kweli kuwa bwana yesu ni mtume wa israel pekee….mbona nyie waislamu mnasema kuwa bwana yesu ni mtume wenu halafu hapohapo tena ndugu.mhammad unaniambia kuwa mimi na wewe hatuhusu?…pia mbona quran na nyie wenyewe mnakubali kuwa injili ya bwana yesu na torati ya musa ni vitabu sahihi kwa muongozo wa wanadamu wote halafu hapohapo mnasema tena injili ni kwa ajili ya israel pekee?..je,hicho sio kigeugeu cha watu walioshindwa?……ndugu mhammad hujui kua quran yako katika(al-imran 3:2-3) imekuambia hivi: …..(Mungu) ameshafunua torati na injili kwa ajili ya kuwaongoza wanadamu na kwa ajili ya kutofautisha kati ya jema na baya!!!…sasa hapa napo sijui utasema wanaadamu ni waisrael pekee na watu ni sisi wote!!…ni ajabu kwelikweli kumbe hata kuruani inavikubali vitabu vya torati,zaburi na injili ya bwana yesu kuwa ni muongozo kwa watu wote lakini chaajabu ni kwamba hapohapo waislamu wenyewe wana pingana maneno yao na kitabu chao wenyewe!!!!!….Pia kwa ujumla hakuna kitu kinachoitwa Mataifa yote >Israel pekee na Mataifa wote>Dunia nzima!!!….biblia ipo wazi kabisa yote hata ukisoma(matendo 4:12) inasema: WALA HAKUNA WOKOVU KATIKA MWINGINE AWAYE YOTE,MAANA HAPANA JINA JINGINE CHINI YA MBINGU WALILOPEWA WANAADAMU LITUPASALO SISI KUOKOLEWA KWALO….bwana yesu ndiye njia pekee ya watu wote hapa duniani….wewe ndugu mhammad bado huelewi wala kuikubali injili ya bwana yesu nawakati wewe unaakili timamu,sasa hebujiulize itakuwaje kwa wanyama na viumbe wengine?…huoni kuwa wakristo tuna kazi kubwa mno!!….lakini bwana yesu aliposema kuwa injili ihubiriwe ulimwenguni kote kwa kila kiumbe alimaanisha kuwa injili yake ienee kote kote duniani kila pembe ya dunia na kamwe sio kama unavyotafsiri wewe…lakini hata hivyo viumbe na wanyama wanaweza kudhihilishiwa injili ya bwana yesu kwa kuonyeshwa upendo na matunzo mema kwao badala ya kuwa mkatili kwa kuwatesa!!…huu upendo wa kweli unapatikana kwa bwana yesu pekee…..halafu katika ile (mathayo 23:25) tunamuona bwana yesu akiwaonya mafarisayo na waandishi(wanasheria) kufuata vyema kile wanachofundisha katika torati ya Musa…wakati ule wanasheria hao pamoja na bwana yesu mwenyewe kwa wakati ule bado alikuwa yupo chini ya torati ya Musa…pale ilikuwa bado bwana yesu hajamaliza ile kazi ya kuishi na kuitimiza ile torati ya Musa na kutuleta katika njia ya Mungu ya kufuata sheria za Mungu kwa roho na wala sio eti sisi wakristo tukae bila ya sheria za Mungu huku tukila bata…Hizo ni kejeli ulizotupatia sisi wakristo ndugu.Mhammad!!….Sasa nimalizie na mambo ya sheria.Ndugu.Mhammad unasema kuwa inatupasa katika sheria za Mungu tujitahidi kwa nguvu zote tukishindwa Mungu atatusamehe yeye mwenyewe kwa huruma wake….lakini biblia takatifu inakataa utaratibu huo wa Allah wa uongo kwa kuwa Allah yeye sie Mungu wa kweli alie mtakatifu…hii ni kwa sababu kwetu sisi wakristo biblia inatuambia kuwa hizi ni sheria takatifu za Mungu alie mtakatifu pia!!.Hivyo sisi wanaadamu wote tunatakiwa tufuate, tutii na kuzitekeleza kwa 100%.Hii ni kwa sababu sheria za Mungu hazikuja kwa imani bali zilikuja kwa MALIPIZI,Yaani ni jino kwa jino,Uhai kwa uhai nk.Mtu anaeshindwa kufuata na kutekeleza sheria zile za Mungu HUFA PASIPO HURUMA KWA NENO LA MASHAHIDI WAWILI AU WATATU.Soma(kumbuk 17:6-7) (waebrania 10:28).Kwa hiyo haiwezekani hata siku moja eti, Mungu mwenye haki kamilifu halafu awe na huruma wakati huohuo!!.Ndio maana biblia inasema: AMELAANIWA MTU YULE ASIYEYASHIKA NA KUTII MAMBO YOTE YALIYOANDIKWA KATIKA KITABU CHA SHERIA!!!…Soma(kumbuk 27:26) pia (galatia3:10)…hapo Mungu wetu ameweka wazi kabisa kuhusu msimamo wake katika sheria zake, lakini pia tunaona ya kwamba sisi wanaadamu kwa asili yetu ni wadhaifu mno tusioweza kuzitekeleza sheria zile za Mungu kwa 100%.Hapo ndugu mhammad hatuwezi kupona bila msaada wa Mungu mwenyewe na huruma yake kwetu…Pia huruma ya Mungu haiwezi kututia na kutupitisha tena katika yaleyale ambayo hatuyawezi basi kama ni hivyo ungekuwa ni unafki mtupu wa kujidanganya sisi wenyewe.Biblia inasema: IKIWA NI KWA NEEMA HAIWI KWA MATENDO YA SHERIA TENA AU HAPO NEEMA ISINGALIKUWA NEEMA,Soma(warumi 11:6)..hapo ndipo huruma wa Mungu kupitia bwana yesu ndipo unapodhihilika kwetu…lakini ndugu.Mhammad,hata ukiuchukua ule mfano wako wa mwalimu utauona ukweli ulipo kwa kuwa hivi Mwalimu anaekufundisha masomo ambayo anajua fika kuwa sio saizi yako(huyawezi)halafu anakwambia uendelee tu,kujifunza kwa kuwa hata kama ukishindwa kujibu mitihani siku ya mtihani basi wale watakao kusahishia watakupa maksi za bure na kukuonea huruma…na yule mwalimu anae kuambia, hapana usiendelee maana utafeli rudia tena dalasa la awali ili ujue vyema ndipo upite kufanya mtihani hapo ni mwalimu yupi yuko sahihi??!!!…njoo kwa bwana yesu ndugu.UBARIKIWE.

    Like

  86. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina,
    Awali ya yote nimshukuru Allah aliyenijaalia uhai na afya, lakini zaidi ya yote akanijaalia kuwa muislam, hivyo sina budi kusema alhamdulillah kwa neema hizo kwani wapo wengi kama mimi bado hawajazipata neema hizi.Allah awajalie inshaallah.

    Pili, niingie mojo kwa moja kwenye mada kwa kunukuu maneno yako katika mada mojawapo ;
    “Ndugu.Mhammad yohana….UKRISTO ni kuwa mwanafunzi na mfuasi wa bwana yesu..” Kaka yangu Mhina hii inaonesha ni jinsi gani ambavyo bado unahitaji msaada kwa sababu bado unababaika sana . Ndugu Mhina, Ukisoma Biblia nzima hutakuta neno UKIRISTO sasa wewe hiyo tafsiri ya ukiristo umeitoa kitabu gani?Naomba uniambie iko sehemu gani ktk biblia ili nami niitafute niisome nipate kufaidika.

    Lakini pia historia ndani ya Biblia haioneshi kama wanafunzi wa Yesu waliitwa WAKIRISTO, labda kama ipo nitaomba unioneshe kwa maana wewe ni msomi wa biblia kidogo.Nnachojua Ukisoma matendo 11:25-26 ndio kwa mara ya kwanza utakuta neno wakiristo, lakini ukisoma chini katika sherehesho/maelezo ya msitari huo wameandika hivi “neno hilo ni la kupanga tu, walilotumia wapagani wa Antiokia” sasa ndugu yangu biblia inaonesha wakiristo walikuwa wapagani wa antiokia, wewe unathubutu vipi kusema wakiristu walikuwa wanafunzi wa Yesu? Yesu hakuwahi kuwaita wanafunzi wake wakiristo hiyo hata uende Bethlehem leo au Galilaya watakwambia.

    Lakini ndugu yangu bado unakataa kwamba manabii wote kuanzia Ibrahim, Musa,Nuhu, mpaka Yesu hawakuwa Waislam,ajabu zaidi umeshindwa kuniambia kwa kutumia ushahidi wa biblia dini yao ilikuwa ni ipi? Hapo wakiristo wengi wameshindwa kuthubutu kulijibu swali hili kwa sababu biblia nzima haisemi manabii hao walikuwa na dini gani! na ndio maana wakakimbilia kusema dini haimuingizi mtu mbinguni lakini ajabu ukimuuliza mtu anakwambia mimi dini yangu ni ukiristu! Kumbe hii yote ni aibu kwa sababu biblia kuna mambo mengi ya msingi imeyaacha.

    Lakini tunapokuja upande wa Quran tukufu yenyewe haijacha kitu imeeleza waziwazi kuwa manabii wote waliopita walikuwa waislamu.
    QURAN SURA YA 2
    132. Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi
    Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu,
    wanyenyekevu.
    133. Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub(Yakobo) mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu
    nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako,
    Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake.

    Kwa hiyo ndugu yangu, kabla Bwana Yesu hajazaliwa Duniani dini ya Uislamu ilikuwepo, na tunaona watu waliitwa waislamu, tofauti na ukisoma biblia utaambiwa watu waliitwa wakiristu kwanza hapo antiokia miaka takriban zaidi ya 20 baada ya Nabii Yesu kuondoka duniani.Je Ndugu Mhina utaendelea na maneno yako ya kifedhuli kuwa uislamu ni dini ngeni? je huoni kwamba kwa ushahidi ulio wazi kabisa ukiristu ndiyo dini ngeni?Kwa hiyo ndugu yangu kutokujua siyo kosa ila nakushauri utuulize tunaozijua dini hizi zote mbili kwa ufasaha tutakupa majibu mazuri.Biblia haiwezi kukwmbia ni ipi dini walikuwa nayo manabii wote akiwemo na nabii yesu mwenyewe.

    TATU; Swali lingine ulihoji kwamba waislam wamekuwa mayatima kwa sababu mtume wetu mtukufu kafa,lakini nyinyi sio mayatima kwa sababu Yesu bado yuko hai anawaunganisha kwa Mungu.
    JIBU; Ndugu Mhina Uislam haikuwa Dini ya nabii Muhammad, hapana kabisa! Uislamu ni dini ya Allah na Nabii Muhammad ni mjumbe tu wa Allah kwa ajili ya kufundisha uislam. Kwa hiyo kufa kwake au kuwa hai kwake hakuizuii Dini ya Allah kuendelea. Na kama kufa kwa mtume kungetufanya kuwa mayatima kama unavosema basi hiyo ingekuwa shiriki kwani tungemfanya mtume kuwa mungu; Tizama Allah alikwisha tuonya kabla katika Quran;

    QURAN SURA YA 3;
    144. Na Muhammad hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwisha pita kabla yake Mitume. Je,
    akifa au akauwawa ndiyo mtageuka mrudi nyuma? Na atakaye geuka akarudi nyuma
    huyo hatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu atawalipa wanao mshukuru.

    Ndugu Mhina sisi waislamu hatuamini kama mnavyoamini nyie kwamba maombi mpaka yapitie kwa yesu halafu yaende kwa Mungu kwani hiyo ni shiriki kubwa.Kwa sababu Muhammad (S.A.W) Alikuwa mtume wa Allah tu kama walivyokuwa mitume wengine, hivyo kufa au kuwa hai kwake hakumzuii Allah kupokea maombi ya waislam kwa sababu Allah yuko hai milele wala hafi;Soma aya ifuatayo;

    QURAN SURA YA 2;255. Mwenyezi Mungu – hapana mungu ila Yeye Aliye hai milele, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala.

    Sifa hizo za Allah hawezi kuwa nazo Bwana Yesu, Yesu hakuwa hai milele kwa mujibu wa biblia inaonesha alikufa siku tatu, yeye alizaliwa na mwanamke, pia ukisoma biblia bwana Yesu alikuwa akishikwa na usingizi na akilala kwa hiyo hizo sababu zinatosha kabisa kumfanya asiwe Mungu pia zinaondoa hiyo fikra kwamba maombi yenu yanapitia kwa Yesu ambaye anawapatanisha na kuwaunganisha kwa Mungu. Kwa sababu fikiria hivi alipokuwa hajazaliwa watu walipatanishwa na nani kwa Mungu wao? Lakini pia alipokufa siku tatu ni nani aliyekuwa mpatanishi wa watu kwa Mungu? Na je alipokuwa amesinzia ni nani alikuwa anawapatanisha kwa Mungu?

    Either, sisi waislam tunaamini kila nabii alikuwa ni mpatanishi wa wanadamu kwa Mungu lakini siyo kwamba bila maombi kupitia kwa manabii basi hayakubaliki kama wakiristu wanavyofanya shiriki hii kwa kumsingizi Yesu. Waislam Tunaamini walikuwa wapatanishi kwa maana ya kwamba Mungu aliwatuma ili watufundishe tumjue kuwa yeye ndiye aliyetuumba na tumuabudu na baada ya hapo wao wanakwenda zao na Mungu anabaki.

    Ndugu Mhina, nimekushangaa uliposema nimeacha kumpinga Bwana Paulo,kuacha kwangu kumpinga Bwana paulo ni kuwa mkiristu kwa maana nyingine kitu ambacho ni kumkosea Mungu wangu aliyeniumba.Kosa kubwa alilofanya Bwana Paulo ni kule kuwafundisha watu kuwa Bwana Yesu ni Mtume na nabii lakini pia ni Mungu katika utatu mtakatifu. Hebu ona Allah anavyotuambia katka Quran kuhusu Yesu;

    QURAN 4:171. Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu, wala msimseme Mwenyezi
    Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa
    Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka
    kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu.
    Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka
    Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika
    ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.
    172. Masihi hataona uvunjifu kuwa mtumwa wa Mwenyezi Mungu..

    Lakini pia Allah anatuambia katika quran kuwa; Yesu hakuwafundisha watu wamuite Mungu, au hakuwaambia watu wamuabudu bali aliwaambia watu wamuabudu Mungu mmoja tu wa mbinguni na yeye ni mtume na mjumbe wake tu.

    QURAN 5:72. Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi (Issa) mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu,
    Mungu wangu ndiye Mungu wenu. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu,
    hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio
    dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.

    Ndugu Mhina, hii ni pointi ya muhimu sana kama wewe unataka kujua kama Allah ni mkweli au la. Ni ukweli usioepukika kuwa Ukipekua Biblia nzima hutakuta sehemu ambayo Bwana Yesu alisema Yeye Ni Mungu au sehemu alipowaambia watu wamuabudu yeye baadala ya Mwenyezimungu kama tunavyoona watu wanaojiita wakiristu wakifanya hivi leo. Badala yake mafundisho haya tunayakuta kwa Mtu anayeitwa Paulo akiwafundisha watu kuwa na Yesu mtume pia ni Mungu aliyevaa mwili wa binadamu.

    Ndugu Mhina ukisoma maneno yafuatayo ya Bwana YESU na maneno y ALLAH kwenye Quran kwa mawazo yaliyo huru utaona kuwa hayatofautiani kabisa.

    Yohana 20:17 “usinishike maana sijapaa kwenda kwa Baba. lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie ya kuwa ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu”

    Mimi ningekuwa mkiristu mpaka hivi leo, hii kauli moja tu ingenitosha kabisa kuamini kuwa Yesu hakuwa Mungu bali alikuwa nabii tu. Wala hakuna haja ya kuzunguka kwenda sehemu nyingine kwa sababu ni kauli ambayo wazungu wanasema “it is a simple explicity statement” ni kauli fupi yenye maana ya wazi.

    NNE;Ndugu Mhina kuhusu luka 2:8 “inaposema nchi ileile” hata ukiitafsiri kwa maana tunayoitumia hivi sasa ya “nchi” utagundua kuwa kuna kosa pia kwa sababu hata mimi nitakuuliza kama ulivyo niuliza “je wachungaji wa kondoo walikuwa wametapakaa nchi nzima kila pembe ya nchi ya israeli wakichunga kondoo?”utagundua kuwa siyo kweli, kwa hiyo kama wewe unaamini kuwa haiwezekani wachungaji kukaa dunia nzima wakichunga basi unalazimika pia kukubali kuwa hawakutapakaa nchi/mji nzima wakichunga kondoo kwa sababu pia itakuwa haiwezekani.Kwa hiyo kwa sababu ni kauli ambayo kwa uhalisia haileti maana tukubaliane sote kwamba kuna makosa ya lugha.

    Tukiachana na hiyo tukirudi katika hoja ya msingi, kuhusu Bwana Yesu kutumwa kwa ajili ya ulimwengu mzima yaani dunia nzima hili hata walioandika Biblia hii hawaamini kama kuanzia (Marko 16:9-20)ni maneno ya Yesu na ndio maana utakuta katika Biblia nyingi kama New American standard Bible na nyingine nyingi zinaishia marko16:8.

    Lakini ndugu Mhina ukiangalia kwa makini hata biblia uliyo nayo bila shaka ukisoma kuanzia marko 16:19-20 yamewekwa kwenye mabano kiaina […] lengo na madhumuni ya kufanya hivyo ni kuwa ni maneno ambayo katika biblia hayakuwemo bali yameingizwa na watu tu! wakidai kuwa ni maneno ya Yesu. Lakini kwa mkiristu wa kawaida mambo hayo huwezi kuyajua lakini kwa sababu wewe una shauku ya kufahamu hebu kaulize au tafuta biblia mbalimbali utagundua kitu ninachokwambia.utagundua kuwa biblia nyingi zimeishia msitari wa 8.

    SWALI;mbona nyie waislamu mnasema kuwa bwana yesu ni mtume wenu halafu hapohapo tena ndugu.mhammad unaniambia kuwa mimi na wewe hatuhusu

    JIBU; Ndugu Mhina hakuna sehemu tulikosema Yesu ni mtume wetu, kama ipo naomba uinukuu niione. Waislam tunasema Bwana Yesu alikuwa ni mtume muislam kwa ajili ya taifa teule la Israeli kama manabii waliomtangulia walivyokuwa. Na kama yeye mwenyewe alivyosema kumwambia mwanamke mmoja katika MATAYO 15:24 “Sikutumwa bali kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya israeli” sasa mimi na wewe ni kondoo wa Israeli? lakini Bwana Yesu akaendelea kusema kuwa chakula cha watoto wa israeli si vyema tukakila sisi mbwa wa mataifa? sasa wewe nafasi yako iko wapi ndg yangu?

    SWALI;?…pia mbona quran na nyie wenyewe mnakubali kuwa injili ya bwana yesu na torati ya musa ni vitabu sahihi kwa muongozo wa wanadamu wote halafu hapohapo mnasema tena injili ni kwa ajili ya israel pekee?..je,hicho sio kigeugeu cha watu walioshindwa?

    JIBU; Ndugu Mhina, Ni kweli kabisa injili na torati ni vitabu vya Allah na ni muongozo kwa watu wa israeli, lakini hakuna sehemu quran inaposema torati na injili ni muongozo kwa wanadamu “wote” kama ulivyonakiri wewe.

    QURAN SURA YA 3;
    47. Maryamu akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa
    mwanaume? Mwenyezi Mungu akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba
    apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.
    48. Na atamfunza kuandika na Hikima na Taurati na Injili.
    49. Na ni Mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia:
    Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi..

    Kwa hiyo ndugu Mhina, hakuna sehemu yoyote tulikosema torati au injili ni muongozo wetu waislam (kama ipo naomba uinukuu uiweke kwenye majibu yako),sema wewe hujatuelewa tu.Tunachokisema ni kuwa hivyo vyote ni vitabu vya Mungu lakini ni mwongozo kwa ajili ya watu wa Israeli tu. kabla ya kushuka quran ambayo ni mwongozo wa kwa dunia nzima.

    QURAN3:93. Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israili isipo kuwa alicho jizuilia
    Israili mwenyewe kabla haijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome
    ikiwa nyinyi ni wasema kweli.

    QURAN 3:44. Hakika Sisi tuliteremsha Taurati yenye uwongofu na nuru, ambayo kwayo
    Manabii walio nyenyekea kiislamu, na wachamngu, na wanazuoni, waliwahukumu
    Mayahudi;

    Kwa hiyo ndugu Mhina ni kweli kabisa kuwa Bwana Yesu ni Mtume wa kiisalamu na ni mtume kwa ajili ya kondoo wa Israeli kwa ushahidi wake mwenyewe katika biblia lakini kwa maneno ya ALLAH katika Quran tukufu,na zaburi injili na torati ni vitabu vya Allah na ni muongozo kwa wana wa israeli kabla ya quran.

    Wallahu a’alam!
    wabillah tawfiq.

    Like

  87. Mhina says:

    Ndugu.Mhammad yohana na waislamu wenzio wote…Nawashukuruni sana kwa mawazo yenu mnayoyatoa.Mimi ninachokiomba kwenu ni kwamba msikate tamaa, yaani tuendeleeni mimi na nyie mpaka kieleweke…..Ndugu zangu.UKRISTO kimaelezo ili muelewe vizuri….Ni matokeo ya utume wa bwana yesu uliopokelewa na waliomuamini kuwa ndiye MASIYA MPAKWA MAFUTA AU KRISTO Kwa lugha ya kigiriki, ikimaanisha ‘MKOMBOZI ALIETIMIZA AHADI ZA MUNGU. Hivyo basi, WA>KRISTO maana yake ‘WAKWAKE BWANA YESU AU WAFUASI WA BWANA YESU,Kama nilivyoelezea hapo juu.Hata huyo mtume Paulo mnaemsingizia kuwa ndiye alieleta ukristo,anafafanua maana ya ukristo wazi kwa kutuambia: MAANA NINYI NYOTE MMEKUWA MMOJA KATIKA KRISTO YESU, NA KAMA NINYI NI WA…KRISTO, BASI MMEKUWA UZAO WA IBRAHIMU, NA WARITHI SAWASAWA NA AHADI.Soma(galatia 3:28 -29)….Mahali pengine Paulo mtume wa Mungu anasema: NI NANI ALIYEFAHAMU NIA YA BWANA, AMUELIMISHE?….LAKINI SISI TUNAYO NIA YA KRISTO (yaani Masiya ambaye ni bwana yesu).Soma(1wakorintho2:16).Pia ndio maana ndugu.Mhammad hata kitabu chenu wenyewe, kinatufagilia sisi wakristo kwa kusema: UTAWAONA WALIO KARIBU ZAIDI KWA URAFIKI NA WAAMINIO NI WALE WANAOSEMA SISI NI WAKRISTO.(Quran 5:83)….Sasa ndugu.Mhammad kumbe hata mwajina wako unaemuamini katika dini yake ya uislamu amekufundisha jinsi wakristo tulivyokuwa waumini wa kweli mbele za Mungu….mbona wewe unajifanya unielewi!!!…..Hoja yako nyingine ndugu.Mhammad umeniuliza hivi: KAMA BWANA YESU NA MANABII WA NYUMA HAWAKUWA WAISLAMU,JE…DINI YAO ILIKUWA NI IPI, MBONA WAKRISTO MNABABAIKA KUTOA MAJIBU MNAPO ULIZWA HIVYO?….jibu: Hapana ndugu Mhammad, kamwe sisi wakristo hatuwezi kubabaishwa na swali lolote lile la Waislamu…labda ulimuuliza mkristo mwenye ufahamu mdogo….Mimi nilichogundua na kujifunza kwako na waislamu wenzio ni kwamba, nyinyi mnapenda sana kushikilia majina badala ya kujua maana ya hayo majina, kama nilivyokuonyesha hapo juu nini maana ya ukristo.Swali lako hili pia LINAUGONJWA HUOHUO!!!.Hebu tujiulize ni nini maana ya neno ‘DINI’ Kabla ya kuichunguza na kuipata hiyo dini ya kweli.Loooh!!.Kumbe tunagundua kuwa neno ‘DINI’ Maana yake ni ‘NJIA’…Na kamwe sio eti Sifa fulani kama UNYENYEKEVU>ISLAM Kama waislamu wanavyoimanishwa huko Misikitini!!!….Ndio maana Sisi Wakristo siku zote tunawasisitiza watu NJIA ambayo ndiyo haswa maana ya DINI…na kamwe sio eti kuleta udini na umadhehebu ambao tukiendelea hivyo tutashindwa kuelewana na kuihubiri kazi ya Mungu mwenyewe.Sisi wote Wakristo na Waislamu pamoja na hata wale wasioamini ni ndugu, kwa hiyo anachokihitaji Mungu wetu ni sisi kukaa kwa pamoja wote ili kuambiana ukweli watu wake wapate kuokolewa.Hivyo, Ukweli ni kwamba Uisilamu sio dini bali ni Mojawapo tu, ya sifa za dini au sifa za hiyo njia ya kweli.Lakini kwa maelezo hayo mazuri tunaona kuwa ukristo ndio dini ya kweli > NJIA.Kivipi?…Bwana yesu aliweka wazi kwa kusema:MIMI NDIMI NJIA YA KWELI NA UZIMA!!.Wapi?..Pitia kwenye(yohana 14:6)…..Kama haitoshi, bwana yesu akasisitiza tena kwa kusema: MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU, YEYE ANIFUATAYE HATAKWENDA GIZANI KAMWE BALI ATAKUWA NA NURU YA UZIMA.Soma(yohana 8:12)…Hapa ndipo pia tunapo pata chanzo cha hii njia kwa kuwaona manabii wote wa nyuma pamoja na bwana yesu mwenyewe kabla ya kutuletea hii njia, walitumia torati na zaburi kuwa njia waliopewa na Mungu katika nyakati zile…na wala sio kama waislamu wanavyoimanishwa eti kuchukua kasifa ka hii njia kamili ya Mungu(UNYENYEKEVU) halafu eti kukaita ndio DINI AU NJIA NA NGAO YA WANAADAMU WOTE!!!..Maajabu hayo.Hebu wewe muislamu jiulize mwenyewe Kuwa, hao manabii wa nyuma pamoja na bwana yesu mwenyewe walitumia njia gani ya vitabu zaidi ya hivi niliovielezea maana kipindi hiko bwana muhamad na kuruani yake walikuwa hawajazaliwa wala kujulikana kama watazaliwa…halafu eti tunaambiwa na waislamu kwamba walikuwa na dini yenye kijisifa kinacho maanisha UNYENYEKEVU!!….Hoja nyingine uliyonipa ndugu.Mhammad ni wewe kutaka kuelezewa uungu wa bwana yesu…lakini nilikwisha kueleza vyema Mwanzo wa hoja zangu zote,hivyo, hainipasi kurudia mambo niliyokwisha yajibu huko juu.rudi juu ukajifunze zaidi na kama hutoelewa,mimi sintoshangaa kwa kuwa hata mtume wako mhamad alikiri kuwa elimu ya roho haijui…je, itakuwaje kwa wewe muumini wake!!…..hoja yako nyingine ulitaka tukubaliane kwamba ile(luka 2:8) ilikuwa na matatizo ya kilugha….lakini kwa kuwa mimi nasimamia neno la kweli kutoka kwa Mungu mwenyewe siwezi kukubali mchezo huo mchafu wa kubadili na kukosoa maneno ya Mungu ovyo ovyo asije yeye mwenyewe akanihukumu siku ya mwisho.Istoshe ukweli utabaki pale pale kwa kuwa,kwa nyakati za zamani za mifugo mingi na maeneo mapana, lilikuwa ni jambo la kawaida kuwaona wachungaji wakilinda mipaka yao ya nchi kwa ajili ya ulinzi wa mifugo yao lakini sio eti wafanye ulinzi katika mipaka ya DUNIA NZIMA!!.Kama hujaamini kajaribu kumsoma Ibrahimu na lutu katika agano la kale ili uone jinsi walivyogawana miji kwa ajili ya malisho ya wanyama wao….Pia ndugu.Mhamad bado huamini kuwa bwana yesu amekuja kwa ajili ya watu wote kwa kunukuu ile(mathayo 15:24) inayomnukuu bwana yesu akisema: SIKUTUMWA ILA KWA KONDOO WALIOPOTEA WA NYUMBA YA ISRAEL…JIBU: Tunaona tangu mwanzo katika biblia, enzi za mitume na manabii Mungu wetu akilitumia taifa la Israel kuwa Taifa lake teule kwa ajili ya KUENEZEA UTUKUFU WAKE kabla ya kutuletea sisi wa Mataifa NURU YA WOKOVU….Katika biblia tunamuona mtumishi mmoja wa Mungu aitwae Siemoni,nae alikuwa ni mtu wa haki mcha Mungu.Yeye alijiliwa na roho wa Mungu na kusema: KWA KUWA MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU WAKO ULIOUWEKA TAYARI MACHONI PA WATU WOTE NURU YA KUWA MWANGAZA WA MATAIFA NA KUWA UTUKUFU WA WATU WAKO ISRAEL.Soma(Luka 2:30-32).Kwa hiyo,ilikuwa ni lazima neno la Mungu linenwe kwa israel kwanza halafu ndipo injili ienee ulimwenguni kote ndio maana bwana yesu alisema maneno yale ili kutuonyesha kuwa Mungu wetu ni Mungu wa mipango na taratibu maalum.Lakini kumhusu bwana yesu kwetu sisi, Mungu wetu alikwisha weka wazi tangu zamani kwa kusema: NIMEKUWEKA ILI UWE NURU YA MATAIFA UPATE KUWA WOKOVU HATA MWISHO WA DUNIA.Soma(Matendo 13:47).Pia ili niondoe utata wa upinzani wa ndugu yangu.Mhammad, kuhusu yeye kusema kwamba bwana yesu hakuja kwa ajili ya watu wote kwa sababu ya kutoiamini injili katika agano jipya…basi nitanukuu maneno ya Mungu mwenyewe kupitia manabii wa zamani katika agano la kale.Tunaona kuwa,tukisoma(isaya 52:10)….Tunamuona Mungu wetu akiweka mambo wazi kabisa kuhusu wokovu wake kwa watu wote wa dunia hii kwa kusema kupitia kinywa cha nabii isaya: BWANA AMEWEKA WAZI MKONO WAKE MTAKATIFU MACHONI PA MATAIFA YOTE,NA NCHI ZOTE ZA DUNIA ZITAUONA WOKOVU WA MUNGU WETU.Kwa hiyo ndugu waislamu wote,Mungu wetu alimleta mtumishi wake bwana yesu kwa hatua maalum.Kwanza ni kuziinua kabila za yakobo na kuwarejeshea watu wa israel utukufu wake aliowapatia.baada ya hapo, sisi wa Mataifa tunapokea nuru ya wokovu wake.Ndio maana Mungu akasema: ZAIDI YA HAYO NITAKUTOA UWE NURU YA MATAIFA UPATE KUWA WOKOVU WANGU HATA MIISHO YA DUNIA.Soma kwa makini(isaya 49:6)….Hoja yako ya mwisho ndugu.Mhammad unasema: HAKUNA WAISLAMU WANAOSEMA BWANA YESU NI MTUME WAO…Ukweli ni kwamba wako, tena wengi mno!!…lakini hatakama wewe unataka useme hivyo ili nisikunase katika hoja zangu, mimi bado nabaki kujiuliza, kama hivyo ndivyo kweli: unamaanisha kuwa bwana yesu hana maana yeyote mbele za waislamu kuhusu ile injili yake?…kwa kuwa alichotuletea bwana yesu ni injili pekee na kamwe sio eti kumsifusifu ovyo kuwa alirusha tiara au kipande cha karatasi kikageuka ndege, mambo hayo kamwe sio ya msingi kwake na mbele za Mungu aliemtuma bali injili yake ndio zawadi na tumaini pekee la sisi wanaadamu.Nauliza tena…UKO WAPI UMUHIMU WA BWANA YESU MBELE ZA WAISLAMU WANAOIKATAA INJILI YAKE NA KUJARIBU KUMPACHIKA VIJISIFA VYA UNAFKI HUKU WAKIIKATAA INJILI YAKE?!!….Mimi ninamuomba Mungu abariki kondoo wake waliopotea ili waisikie sauti yake na kuukubali wokovu huo kwa hiari ya mioyo yao wenyewe…Maana biblia inasema: WATAISIKIA SAUTI YANGU NA KUJA KWANGU NA KUNIKUBALI.Kitu cha ajabu ndugu zangu waislamu ni kwamba, kuruani hiyohiyo mnayoiamini, inawafundisha kuviamini vitabu vyote alivyoteremsha Mwenyezi Mungu.Tunaona katika (Al-QURAN 3:3) inasema: AMEKUTEREMSHIA KITABU KWA HAKI KINACHOSADIKISHA YALIYOKUWA KABLA YAKE NA ALITEREMSHA TAURATI NA INJILI….Pia ukisoma(AL-IMRAN 3:2-3) inazungumzia hayo hayo!!!!.Kwa hiyo basi,hata kama mkijitetea kuwa vitabu hivyo vimepotea iweje neno la Mungu alilowaandalia watu wake eti liharibiwme na wanadamu kirahisi rahisi namna hiyo??.,.mbona sisi wakristo tunavyo vitabu hivyo lakini nyinyi hamvitaki kuviamini?…inamaana nyinyi mmepoteza mausia yote ya mungu na misingi yake halafu eti mnasema quran ndio kila kitu..sasa hilo ni neno gani la Mungu lisilokuwa na misingi ya manabii wa Mungu wanaofundisha kwa kutumia ujumbe wao kwa mfano injili ya bwana yesu?…..Yaani ukweli wangu ni kwamba, nilichogundua katika dini ya kiislamu ni kwamba iko hivi: TORATI+ZABURI+INJILI = NI VITABU VYA KALE VYA MANABII VILIVYOPITWA NA WAKATI (VYA ISRAE PEKEE)……Halafu Quran na Mtume wake Mhamed wanasimama mahali pa bwana yesu na injili yake….NA HUYU NDIYE MPINGA KRISTO AMBAYE BIBLIA ILIMTABILI KUJA KWAKE MIAKA ZAIDI YA 2000 ILIYOPITA IKISEMA KUWA ATASIMAMA MAHALA PA BWANA YESU!!!!!!!……Ndugu ya mhammad yohana na waislamu wenzio, mimi bado nipo hapa pamoja na nyinyi nawaomba tuendeleeni kubadilishana mawazo, lakini pia tazameni dini yenu kwa jicho la pili,maana ninachokiona mimi ni nyinyi kuongozwa na watu wenyesura nzuri za kibinaadamu lakini kumbe WAMEVAA KINYAGO CHA SHETANI MIOYONI MWAO.Mungu awaokoe…

    Like

  88. Noor mohamed says:

    Kabla ya kuendea na mijadala, wakristo twambieni yesu kwanu ninani? Nabi au Mungu maana naona hamuelewiki mara yeye ndie nabi yule, mara ni Mungu mkuu na mwokozi wenu, mara yeye ndio njia ya kwenda kwa Mungu, mara ni mwana wa Mungu, ivi mkoje tumieni akili , Mungu ni mmoja, hakuzaa wala hakuzaliwa Ebu nijibuni swali hili: Mama na mwana nani alie juu ya mwenzie? Mtoto amtii mama au mama amtii mtoto? Hii inanipa taabu ninapo fikiria kuwa Mungu wenu yesu anawajibika kumtii na kumnyekea mama yake MARIA . PIA NAJIULIA KAMA MARIA NDIE ALIE MZAA MUNGU WENU YESU , JEE MUNGU WA MARIA NA MWANAE YESU NI NANI? BILA SHAKA ATAKUA NI ALLAH MUNGU WA MBINGU NA ARDHI, MUNGU WA MASHARIKI NA MAGHARIBI, MUNGU YAKOBO NA DAUDI, NA IBRAHIM NA ISKHAKA, MUNGU WETU SOTE MIMI NA WEWE MUNGU ALIE HAI NA AMBAE KAMWE HAWEZI KUSULUBIWA MSALABANI NA WATU ALIE WAUMBA HUYU NDIE MUNGU WAKWELI

    Like

  89. Noor mohamed says:

    Masahihisho sio Mungu Yakobo, bali mimetaka kusema Mungu wa Yakobo

    Like

  90. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina;
    Sifa zote njema zinamstahiki Allah, Mola wa viumbe vyote;sina budi kumshukuru kwa neema zake hasa hii neema kubwa kabisa ya kunifanya niwe muislam.Kwani wengi bado wapo katika upotofu na Allah akipenda atawaongoa inshaallah.

    Nikiingia kwenye mjadala moja kwa moja,Ndugu Mhina, Naomba nikumbushe maswali yangu kwenye mada iliyopita halafu ninakiri majibu yako Halafu utapima mwenyewe kama umejibu au hujajibu? akili yako mwenyewe itakuhukumu.

    SWALI LANGU; Ni kitabu gani umetoa tafsiri ya dini ya UKIRISTO?

    JIBU LAKO;Ndugu zangu.UKRISTO kimaelezo ili muelewe vizuri….Ni matokeo ya utume wa bwana yesu uliopokelewa na waliomuamini kuwa ndiye MASIYA MPAKWA MAFUTA

    CHANGAMOTO YANGU;Ndugu zangu mimi nilitaka kujua hawa jamaa waliipata wapi hii dini inayoitwa UKIRISTO mbona Biblia haijasema kuwa kuna dini inayoitwa Ukiristo?Lakini pia niliuliza hivi wale wanafunzi wa Bwana Yesu yeye aliwaita WAKIRISTO kwa ushahidi wa Biblia? bahati mbaya kabisa majibu ya Mhina ni kama nilivyoyanakiri hapo juu.Hata Bwana Yesu akija saa hz ukamwambia hawa ni wakiristo atakuuliza wakristo ndio akina nani mbona sikuwaacha? Itabidi umfunulie MATENDO 11:25 umwambie hawa walikuwa washirikina wa Antiokia ambao sasa ni wafuasi wako.Bila shaka Bwana Yesu atasema inna lillahi wa inna ilayhi rajiuun! hakika huu ni msiba.NduguMhina naomba uiache Biblia ijitetee yenyewe,iache biblia ijibu maswali inayoulizwa usiisaidie, kama haina majibu sio kosa lako kwani hukuitunga wewe.

    SWALI LAKO;Mhammad hata kitabu chenu wenyewe, kinatufagilia sisi wakristo kwa kusema: UTAWAONA WALIO KARIBU ZAIDI KWA URAFIKI NA WAAMINIO NI WALE WANAOSEMA SISI NI WAKRISTO.(Quran 5:83)….

    JIBU LANGU; Ndugu Mhina, Allah anasema ole wao wanaozijadili aya zake bila elimu! Nakuhofia usije ukawa miongoni mwao ukaja kuangamizwa siku ya kiyama. Kwa kifupi Aya hii iliteremka Madinna kwa sababu ulikuwa ni mji wa wakiristo na mayahudi kabla ya Mtume kuhamia .Mtume alipofika Madinna wale waliokuwa wakiristo wengi wao walimuamini na kumpokea na wengi walibadili dini na kuwa waislamu.Lakini mayahudi wengi walimkataa na ndiyo waliokuwa wanaongoza kwa kumfanyia uadui na walifanya fitina hadi kutaka kumuua lakini Allah hakuwajaalia. Hapo ndipo Allah akashusha aya hiyo kumwambia mtume kuwa watu ambao wapo karibu kwake na kwa waaminio pia ni wakiristo. Mmoja wa walio badili dini ni swahaba mkubwa kabisa wa Mtume aliyeitwa Salmaan Al farsy.
    .Lakini hata hivyo aya hii haiishii hapo ulipoishia wewe naamini kabisa ungeimalizia ungeelewa nini maana yake; Mimi nakuwekea uisome

    QURAN SURA YA 5
    82. Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini
    ni Mayahudi na washirikina. Na utawakuta walio karibu mno kwa urafiki (na waaminio) ni wale wanao sema: Sisi ni wakiristo. Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na
    wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi.

    83. NA WANAPO SIKIA yaliyo teremshwa kwa Mtume utaona macho yao yanachururika
    machozi kwa sababu ya Haki waliyo itambua. Wanasema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini.
    Basi tuandike pamoja na wanao shuhudia.

    SWALI;UKO WAPI UMUHIMU WA BWANA YESU MBELE ZA WAISLAMU?

    JIBU; Ndugu Mhina, Umuhimu wa Yesu kwa waislam ni mkubwa mno. Allah amemfanya nabii Issa kuwa ni mfano wa kuigwa kwetu sisi waislamu kwa sababu Allah alimjalia kuwa nabii mwenye imani kubwa na alikuwa mtu mwenye subira mno pia Allah alimjalia kumpa wanafunzi waliompenda na kumsikiliza mno, hayo mambo yote yanastahili kuigwa na kila anayejiita muislamu,Na haya si maneno yangu bali ni maneno ya Allah ndani ya Quran tukufu;

    14. Enyi mlio amini! Kuweni watumishi wa Mwenyezi Mungu, kama alivyo sema Isa
    bin Mariamu kuwaambia wanafunzi wake: Nani wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu?
    Wakasema wanafunzi: Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu! Basi taifa moja la Wana
    wa Israili liliamini, na taifa jingine lilikufuru. Basi tukawaunga mkono walio
    amini dhidi ya maadui zao, wakawa wenye kushinda.

    SWALI;unamaanisha kuwa bwana yesu hana maana yeyote mbele za waislamu kuhusu ile injili yake?

    JIBU; Kwa bahati mbaya kabisa hayo ni maneno yako siyo ya Waislamu.Injili ya Yesu ni mfano wa kuigwa kwa waislam wote kwani hayo ni maneno ya Allah. lakini siyo Injili ya Paulo mliyo nayo nyie kwani katika hivyo vitabu takribani 23 hamna hata doti ya neno alilolitamka Bwana Yesu;Kibaya zaidi ni maneno ya Mtu ambaye alikuwa adui mkubwa wa wanafunzi wa Bwana Yesu.Aliyeamua kuwa chui na kujivika ngozi ya Mbuzi akijifanya katumwa.Pia Sisi waislamu tunaamini hakuna mtume hata mmoja ambaye kabla ya utume wake alikuwa adui wa Mungu hata katika Biblia historia inaonesha hivyo,Paulo alikuwa adui wa Mungu.Hata hivyo Vitabu vinne tu vya biblia agano jipya luke,marko,matayo na yohana humo ndiyo kidogo utakuta baadhi ya maneno ya Yesu ambayo ni 1/10 tu ya vitabu hivyo.Sasa ndugu yangu utaniambia wewe una injili ya Yesu kweli???? hebu acha utani Bwana!!Sema hivi nina sehemu tu ya Injili ya Yesu hapo utaeleweka.

    SWALII;manabii wote wa nyuma pamoja na bwana yesu mwenyewe kabla ya kutuletea hii njia, walitumia torati na zaburi kuwa njia waliopewa na Mungu katika nyakati zile…Hebu wewe muislamu jiulize mwenyewe Kuwa, hao manabii wa nyuma pamoja na bwana yesu mwenyewe walitumia “njia gani ya vitabu” zaidi ya hivi niliovielezea maana kipindi hiko bwana muhamad na kuruani yake walikuwa hawajazaliwa

    JIBU; Mimi nilikuuliza dini ya manabii waliopita kwa ushahidi wa biblia yako! Bahati mbaya kabisaaaaa mpaka kesho biblia yako haina jibu! lakini wewe unaniambia kwamba walitumia “njia ya vitabu” . Hivi kuna dini inaitwa vitabu? Hivi hapo utasema umejibu swali? mimi nilitegemea labda uniambie isaya au yeremia au kumbukumb inasema dini yao ilikuwa inaitwa vitabu vya zaburi na torati!!! hapo ningekuelewa saana au ungesema yeremia au nehemia au habakuki inasema manabii hao walikuwa wakiristu!! hapo ningekupongeza sn ndg yang! Hebu iache biblia ijitetee bwana, usipende kuisaidia Bwana ina maana wewe una busara kuliko mungu wako wa biblia?

    Halafu Umesema mimi muislamu nijiulize hivi manabii walitumia njia gani? Mimi muislam sina haja ya kujiuliza kwa sababu Allah ashaniambia katika quran kuwa manabii walikuwa waislamu wa ukweli! wewe mkiristo ndiyo unatakiwa kujiuliza kwa sababu mungu wako hakukwambia ktka kitabu chako!

    SWALI;Kitu cha ajabu ndugu zangu waislamu ni kwamba, kuruani hiyohiyo mnayoiamini, inawafundisha kuviamini vitabu
    vyote alivyoteremsha Mwenyezi Mungu.

    JIBU; Vitabu vyote tunaviamini na vyote vimetoka kwa Allah, na Quran ndicho kitabu cha mwisho na ni laana kuvikataa! na ndiyo maana Sisi waislam sheria zote zilizo ndani ya quran zinafanana na sheria za torati na injili ya Yesu kwani na yenyewe haipingani na torati.Lakini nyie mnazipinga sheria hizi na kudai kuwa ni mapito huku mkizibeza kwa kutumia injili yenu wenyewe.

    SWALI;iweje neno la Mungu alilowaandalia watu wake eti liharibiwme na wanadamu kirahisi rahisi namna hiyo??.

    JIBU; Ndugu yangu, nina wasi wasi sana na elimu yako ya biblia kwani usingeuliza swali hili. Ukisoma biblia utaona kuwa Bwana Yesu amewatahadharisha sana wanafunzi wake na waandishi na farisayo, maeneo mengi tu (niulize kama hujui nitakwambia ukasome wapi ndani ya biblia) kwani wanatumia kalamu kulipotosha neno la kweli la Mungu.sasa hebu hapa unijibu hivi bwana Yesu aliwataadharisha na nini kama kweli neno la Mungu watu hawawezi kulibadili?Pia ndugu yangu Ibrabra alikuonesha katika dibaji ya biblia yenu jinsi walivyotengeneza baadhi ya majina ambayo hayakuwemo, lakini pia nilikuonesha marko 16 jinsi gani biblia zenu zinavyotofautiana kuna nyongeza na mapunguzo mengi! Lakini pia kuna Biblia nyingine hasa wanazotumia wakatoliki zina vitabu 73 na nyingine zina vitabu 66 tu. Hivi wewe unataka ushahidi gani zaidi ya huo?

    SWALI;NA HUYU NDIYE MPINGA KRISTO AMBAYE BIBLIA ILIMTABILI KUJA KWAKE MIAKA ZAIDI YA 2000

    JIBU; Ndugu yangu, hebu kwanza naomba upunguze jazba kwa sababu jazba zina kufanya uonekane kichekesho, kwa sababu zinapunguza busara yako mpaka 0%. Ndugu Mhina, Mtume amezaliwa miaka 570 baada ya Yesu sasa hiyo miaka 2000 wapi na wapi na Mtume wetu mtukufu? mimi nafikiri labda ulitaka kuwamaanisha hawa manabii wenu ambao kila kukicha wanaongezeka kama uyoga akina Kakobe, Mwingila, Buberwa kule Mwanza, n.k kwa sababu hao ndio waliokuja miaka 2000 baada ya Yesu. na kweli ukiangalia sifa zote alizosema Bwana Yesu katika Matayo wanazo.Kwa sababu bwana Yesu alisema “na watafanya miujiza mingi kana kwamba walio wateule ili wawapoteze watu wengi” hizo sifa hasa mnazo nyie na wengi mmewapoteza kweli.. kwa kufanya miujiza ya uwongo ili muwadanganye watu….mara ooh kikombe cha miujiza kule loliondo, kinaponesha kila ugonjwa! pale kweli shetani aliwapoteza walio wengi, mara tunaombea vipofu,viziwi na viwete kumbe waaaaaaapi! wizi mtupu.mbinu zote nazijua vizuri kuliko hata wewe.

    SWALI;Kumbe tunagundua kuwa neno ‘DINI’ Maana yake ni ‘NJIA’…Na kamwe sio eti Sifa fulani kama
    JIBU; Ndugu yangu kusema maneno usiyoyajua utaumbuka bure! Dini ni neno la kiarabu kwa 100% lenye maana ya “mfumo wa maisha ya imani ya mwanadamu kwa mungu wake” maana nyingine neno hili linamaanisha “malipo anayoyategemea mwanadamu kwa mungu wake”.Acha kudanganya watu dini maana yake siyo njia hata Kamusi ya kiswahili haitoi tafsiri hiyo.Hebu kama una ushahidi wa kamusi yoyote ya kiswahili inayotafsiri hivyo uniambie. Njia kwa kiarabu ni “siratwaa” au “sabiil”.Kwa hiyo mfumo waYesu wa maisha ni uislamu au unyenyekevu kwa Mola wake.Quran imetoa tafsiri pana ya neno unyenykevu na nimeshakuwekea ushahidi najua akili yako imeelewa lakini mwili wako hautaki, baadala yake unaendelea kushikilia eti unyenyekevu ni neno moja tu.wewe hiyo tafsiri unaipata wapi?????

    Ndugu Mhina unyenyekevu ni term pana sana katika mas-hala mazima ya kiimani,mtu hawezi kuwa mnyenyekevu pasipo kumjua Allah hata awe mrembo au handsome vipi!Lakini Allah kaelezea katika aya ifuatayo mtu mnyenyekevu anatakiwa awe na sifa gani!Najua ulielewa ila hapa nakuelewesha zaidi kwa sababu kila swali lako Quran ina majibu!

    33:35. Hakika Waislamu wanaume na Waislamu wanawake, na Waumini wanaume na Waumini
    wanawake, na wat’iifu wanaume na wat’iifu wanawake, na wasemao kweli wanaume na
    wanawake, na wanao subiri wanaume na wanawake, na wenye hushui wanaume na
    wanawake, na watoao sadaka wanaume na wanawake, na wanao funga wanaume na
    wanawake, na wanao jihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanao msifu
    Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume na wanawake, Mwenyezi Mungu amewaandalia
    msamaha na ujira mkubwa.

    Hao ndio waislamu na hiyo ndiyo tafsiri ya unyenyekevu, na hiyo ndiyo dini ya Yesu yaani mfumo wa maisha wa Yesu na Mtume Muhammad na manabii wote waliotangulia na hayo ni maelezo yaliyo wazi kabisa kwa muulizaji.

    Wwahaadha ssalaaam!
    Wabillah tawfiq!

    Like

  91. alfa says:

    kijana acha unafk,hujasoma waniaminio mimi watatenda haya kwa jina langu?halafu babu wa loliondo na nyie si mliiga mkatoa vijamaa vyenu eti navyo vimetoka kwa mungu?niny mtaishia kuiga kila k2 hata msivyovijua,shetan hana mpango na nyie c kashawapata,yesu anatoa angalizo kwa kanisa ambalo ndo linalohusika c niny waongo,cc tulikataa watu wa mataifa ndo mlioribarik jambo mkiwatukana watumish wa mungu kila cku,mtaumbuka,yesu amewapa uwezo wamuaminio kutenda hayo na yanafanyka na wachaw wanarudisha tungul zao,mmejaa ghadhab na chuk mafundisho ya kishetan visa vya kutunga tu,mhad angeish dunia ya leo angeitwa mhalifu kama alivyojiita mwenyewe jina la utani,na matund yak tunayaona,kwel waislam wanyenyekevu,nyie wanyenyekevu sana,balaa la dunia!vp yule mtoto wa kike mliemtandika risas ya kichwa alikataa kuolewa nini?kapona bab watakoma,niny wenyewe kwa wenyewe mnaitana makafir na mnakatana masikio kila siku ntashangaa nini ukiita kafir,mmelaaniwa na ndo hamuish malalamish kwa sababu mtume wenu kafa na anasubir hukum

    Like

  92. alfa says:

    mara muhamd ndo roho mtakatif mara jibril(shetan aliemtokea mhd pangon)ndo roho mtakatif mara musa kamtabil mud kwen torat achen ubabaishaj nafas ya yes mnatak kumuweka mshkaj asijua anakwenda wap,kaenda jehanam coz kule ndo gizan hamuelew!au ndo kiapo ntautetea hata kufa,tumeipokea injil ya yesu huku tunaipinga,hamna say niny zaid ya kuoa watoto wadogo na uganga tu,washirikina kibao,mtakunyw makombe mpaka mfe,nampa pole mungu wa walalamish,washirikina waongo na weny chuk,hutoa sadaka hata kuwajengea ndugu zao waganga lakin hawamtolei mungu wao asiejiweza,wanampigania,musa na israel walipiganiwa na bwana soma bible vizur wale malaika wawil walivyopigana,na sehem nyngne waliuzunguka ukuta ukaanguka na adui zao wakatiwa mikonon mwao,pia hawakupigana wasambaze dini bal wapewe nch ya ahad ambayo mpaka leo waislam mnaendelea kuwasumbua mmeumbuka babu,mpiganien asiyejiweza hallah back!muhalif amekufa babu,bt kaacha kizaz chak kinasumbua dunia babu,wazungu ni wapelelez weny akil babu imekula kwenu tena myahud da!

    Like

    • Muhammad Yohana says:

      nafurahi sana ninapoona! ninafundisha halafu wakiristu wanapanic! Hiyo huwa naipenda kwa sababu huwa najua ukweli umewaingia hadi wanakosa hoja wanaanza kutukana! mimi sitakata tamaa kwani hiyo ndiyo sunna ya manabii wote! walitukanwa, walipigwa wakakebeiwa n.k lakini yote ni kwa sababu walisema ukweli, walikataza mabaya na wakaamrisha mema!Lakini kama manabii wangefika wakatangazia watu walewe, wacheze kamari, waende disko bila shaka wasingebugudhiwa kwa sababu roho za watu hupenda waambiwe upuuzi ndio wafurahi lakini wakiambiwa ukweli wanachukia kwa sababu unawagusa.
      Alhamdulillah namshukuru Allah! kwa kunijalia kufikisha ujumbe wake hata kama makafiri wanachukia;Kwa sababu wasingechukia ningejua hawakunielewa!

      Like

  93. alfa says:

    halaf unaniambia manabi wote walikuwa waislam mbna majamaa niny waongo jaman tumewachoka na din yenu ya kutunga.daudi alikuwa akiabudu msikiti gan pamoja na israel wote?musa je si myahud?eliya na elisha na samwel pia jaman si wayahud hawa tena samwel amekulia kwenye mahekalu yao jaman,suleman mjenz wa hekal ambalo tunaona aliingia na kuomb wingu likashuka kutoka mbnguni jaman,kwa msisitizo zaid hukusoma daud alipoomba bwana asimuondolee roho yak takatifu wandugu,muache uzush bandugu mmefulia

    Like

    • Muhammad Yohana says:

      Alfa tunakuomba kwanza usipanic! pili usidandie train kwa mbele utasagwa tikitiki!
      Sasa tunakuomba utwambie kwa ushahidi wa biblia yako walikuwa wakiristu?
      Tunakuomba utumie nguvu ya hoja usitumie msuli! kama huna hoja u quit! or stay quiet! thats all!

      Like

  94. Mhina says:

    Ndugu.Mhammad,Mimi nilikwisha kupa maana ya Ukristo kuwa ‘KRISTO’ ni neno la kigiriki lenye maana ‘MESIYA’ ambaye ndiye Bwana yesu mwenyewe.Kwa hiyo, WA..KRISTO, maana yake, wakwake bwana yesu ambaye ndiye huyo masiya.Tatizo lako ni nini hapo ndugu??.Kama tatizo ni hiyo lugha ya kigiriki mbona hushangai lugha ya kiarabu ya ISLAM Kwa kiswahili kubadilika na kuwa UNYENYEKEVU?…Mbona hapo hukuwahoji mashekh kuwa imekuwaje!!.Neno Kristo ni sawa na kusema Masiya kwa kigiriki, na Masiya huyo anajulikana kuwa ni bwana yesu mpaka kwenye quruan yako unayoiamini.Tatizo lenu waislamu ni kwamba, nyinyi mmezoeshwa kukariri mambo kuliko kuyaelewa vyema hayo mambo.Pia nikujibu kuwa wakati bwana yesu atakaporudi kamwe hatapata tabu kututambua sisi wafuasi wake kwa sababu,biblia inasema, atakuja na utukufu mwingi utakao muwezesha kutabua kabila zote, lugha zote na jamaa zote za dunia hii kutoka kila pembe ya dunia.Lakini pia, yeye zaidi ya yote ataangalia ile kweli yake kama ipo mioyoni mwetu na kamwe sio majina au madhehebu yetu.Hii ni tofauti na nyinyi waislamu ambapo kwa mujibu wa Quran, Allah ataangalia waislamu wanaojua kiarabu pekee.Sasa sijui ndugu mhammad na waislamu wenzio wote kama tayari mnakijua kiarabu. Pia nikujibu kuwa wale wanafunzi wa bwana yesu wa mwanzo nao walikuwa ni wakristo kwa sababu walikuwa wafuasi wa bwana yesu, na maana ya ukristo ni kuwa mfuasi na mwanafunzi wa bwana yesu kama sisi.Lakini kumbe mtume mhamad alisema, MAYAHUDI NA WASHIRIKINA NI ADUI ZANGU LAKINI MARAFIKI NA WAAMINIO WA KWELI NI WALE WANAOSEMA KUWA SISI NI WAKRISTO!!…..Hapo pako wazi wazi hata kwa mtu asiesoma, ya kwamba, mtume wenu aliwasifu na kuwatambua wakristo kuwa ni watu wa Mungu wa kweli, lakini cha ajabu ni kwamba ndugu waislamu wanajaribu kuendelea kumpinga hata mtume wao wenyewe na kutofautiana nae kimawazo!!….Pia swala la kuwafanya wale wakristo wa mwanzo waliotokwa na machozi na kusilimu kuwa ndio hao wakristo halisia, halileti mantiki kwa sababu hata kama ni hivyo, bado mtume mhamad alionyesha kuwa liko jina la ukristo linalobeba waumini wa kweli mbele za Mungu…na cha ajabu ni kwamba waislamu wote duniani wanalipinga jina hilo kwa kusema ni jina la kipagani la mtume paulo na dini yake…sasa kama ni hivyo kweli, mbona mtume wenu AMELITUKUZA MBELE ZA MUMGU WAKATI NI JINA LA KIPAGANI?!!…..Hoja yako nyingine ndugu Mhammed yohana, umeandika bila ya aibu kwa kusema: AllAh AMEMFANYA NABII YESU KUWA MFANO WA KUIGWA KWETU SISI WAISLAMU!!….JIBU: Kumbe kwa mujibu wa dini ya kiislamu ni kwamba, bwana yesu hana maana yeyote ile zaidi ya kusifiwa sifiwa na kutumika kama mfano tu!!….na hii ni kwa sababu, wao waislamu wamepoteza misingi yote ya neno la Mungu kupitia manabii wake, kama Musa,daudi,Sulemani…Wakaona kwamba, ili kuficha hiyo aibu ni kheri wachukue sifa zao pekee na pia ni kheri wasingizie kuwa vitabu vya manabii hao vimeharibiwa na Mayahudi na wakristo jambo ambalo sio kweli.Ndipo pia kwa niaba ya manabii wote hao zaidi ya 40, akasimamishwa nabii mmoja tu, aitwae Mtume mhamad tena kutoka hukooo uarabuni na kitabu chake alichokipata mapangoni kwa staili ya kubanwa na mashetani kama alivyokiri yeye mwenyewe katika kitabu chake mwenyewe eti ili awalishe neno la Mungu munia nzima na kuwaingiza Mbinguni watu wote kwa hiyo njia yake!!!…hivi kwa mtu mwenye akili timamu inaingia akilini hiyo?!!….ndio maana huko juu ndugu.Mhammad yohana ulikiri wewe mwenyewe kuwa injili,torati na zaburi ni vitabu vya israel pekee halafu quruani ndilo neno la Mungu kwa watu wote!!.Tatizo la waislamu hapa ni kwamba vitabu hivyo vya manabii wa Mungu hawanavyo kwenye quruani yao….ndio maana mimi ninauliza hivi: NI DINI GANI HIYO INAYOKOSA MISINGI YA MANABII WAMUNGU ZAIDI YA 40 ALAFU ETI INASIMAMISHWA NA MTUME MMOJA TU,…Maana ndugu yangu Mhammed yohana alikwisha tuambia huko juu kwamba torati,zaburi na injili ni kwa israel pekee na quruani pamoja na mtume mhamad ni kwa ajili ya dunia nzima!!…ndipo hapo nilipomuona ndugu.mhamad yohana akibadilika kama kinyonga mara ya pili ya majibu yake kwa kusema hivi: VITABU VYOTE TUNAVIAMINI KWA SABABU VYOTE VIMETOKA KWA AIIAh ,NA QURUANI NI YAMWISHO!!!….Lakini hatakama ndugu.Mhammad umebadilika kiasi hicho bila ya aibu ukijitahidi kutetea dini yako, mimi nitakupa swali hili: KAMA NI KWELI VITABU VYOTE MNAPASWA KUVIAMINI MBONA PALE MWANZO ULISEMA KUWA VITABU VYA TORATI, ZABURI NA INJILI VILIKUWA VYA ISRAEL PEKEE HALAFU QURUANI NDIYO KITABU CHA WANAAMDAU WOTE? Ndivyo mnavyomtetea Mungu wenu kwa uongo kiasi hicho?!!…Pia kama sasa umevikubali vitabu vyote hivyo vya manabii, je, unakubaliana na mimi kwamba bwana yesu amekuja kwa ajili ya watu wote na sio tena kama ulivyokuwa ukikataa huko juu?…maana wewe mwenyewe umekiri kuwa ni laana kuvikataa vitabu hivyo vya manabii wote wa zamani,lakini hata hivyo kinachosikitisha ni kwamba nyinyi waislamu hamnavyo tena hivyo vitabu vya torati,zaburi na injili mkidai kuwa vilishabadilishwa na mayahudi na kupotezwa kabisa…sisi wakristo tukiwaambia tunavyo vyote hivyo, nyinyi mnadai kuwa sivyo kwa kuwa hivi vyetu vimechakachuliwa na mayahudi jambo ambalo halina ukweli wowote.Kwa hiyo ndugu.Mhammed kama ulivyokiri wewe mwenyewe kuwa usipoviamini vitabu vile ni laana….kwa hiyo nyinyi waislamu ni laana mbele za Mungu kwa kuwa hamviamini vitabu vile kutoka kwa wakristo na pia nyinyi wenyewe hamnavyo, si ndio maana yake ndugu? Poleni sana ndugu zangu.Ndio maana siku zote ninasema kuwa quruani kamwe sio neno la Mungu la kweli maana halina mausia yoyote ya misingi ya manabii wa zamani wa Mungu zaidi ya kuwapa manabii wale vijisifa vijisifa tu,ilimradi neno hilo nalo lionekane eti nalo ni la kihistoria!!!.Hapo ndipo yule Mpinga kristo alietabiliwa na biblia miaka 2000 iliyopita kuwa atakuja kutokea wakati wowote katika hii dunia na kuchukua mahala pa bwana yesu.Bwana yesu ndiye nabii wa mwisho wa mungu aliepaswa kuongoza dunia yote kwa kutumia injili yake.Lakini mahalipake hapo, amekaa mtume mhamad na quruani yake akitaka yeye ndie afuatwe na dunia nzima akijaa sifa zote zile za mpinga kristo zilizoonyeshwa katika biblia.sifa hizo ni kama ifuatavyo: ATASIMAMA MAHALA PA BWANA YESU + ATAKATAA KWAMBA BWANA YESU SIE MWANA WA MUNGU + ATAKATAA KWAMBA BWANA YESU HAKUSULUBIWA MSALABANI + ATAKATAA KWAMBA YESU SIE KRISTO = Hapo tunaona kuwa hata kama wapo wapinga kristo wengine wadogo wadogo lakini Mtume mhamad wa waislamu ametwaa 100% ya utabiri huo!!!.jiokoe wewe muislamu acha mambo ya udini, njoo upitie njia ya kweli ya Mungu ambayo ni bwana yesu…ndio maana hata vitabu vyote vya nyuma vya manabii vilimtabiri yeye na injili yake na kamwe sio eti mtume mhamad wa waislamu……..Hoja nyingine ndugu.Mhammad ulisema kuwa ‘HAKUNA NJIA ILIYOITWA NJIA YA KITABU ILIYOTUMIWA NA MANABII WA ZAMANI.JIBU: Ajabu ni kwamba wewe mwenyewe unapingana na hata dini yako mwenyewe kwa kuwa kuhusu manabii na wakristo wa zamani quruani yako mwenyewe unayoiamini ilikuwa inawaita WATU WA KITABU!!….Ambao ndio waliokuwa wamebeba maana ya dini au njia.Wewe ndugu unatafsiri maana ya neno dini kuwa ni’ MFUMO WA MAISHA YA IMANI YA WANAADAMU KWA MUNGU’…Sasa na mimi nikuulize hivi: katika ‘NJIA’ tunayo itumia kumuabudu na kumfuata Mungu wetu….huo sio mfumo wa maisha yetu ya imani mbele za Mungu??.,..uoni kuwa imeleta maana ileile ya neno dini?..hapo cha msingi ni kuangalia aina ya hiyo njia ambayo kwa maelezo yetu tunajua ni njia ya dini.Lakini tunaona kwamba ukiliweka neno la unyenyekevu la waislamu lenye kutaka limaanishe maana ya neno dini, utagundua kua haiwezekani kabisa kwa sababu neno lenyewe maana yake ni sifa isiyojitosheleza yenyewe mpaka ilundikiwe msaada wa maneno ya pembeni.Kwa hiyo basi, bado mimi nasisitiza kwamba uislamu maana yake sio dini bali ni kajisifa tu, ka dini ambako bado kanahitaji msaada wa maneno ya kusaidiwa kwa kuwa hakajitoshelezi kenyewe.Hivyo uislamu sio dini ya kweli wala sio maana ya neno dini.Mimi niliuliza hivi: HAO MANABII WA MUNGU WA ZAMANI TUNAOAMBIWA KUWA WALIKUWA WAISLAMU HIVI WALITUMIA KITABU GANI CHA HUO UISLAMU? NA PIA MBONA HATUKIONI KIKITUMIKA HII LEO KWA WAISLAMU WENZAO WA WAKATI HUU….AU MUNGU AMEBADILIKA YEYE NA NENO LAKE LILE LA AWALI.NAKAMA NI HIVYO KWANI HAWA WOTE WAITWA WAISLAMU WAKATI VITABU VYAO NI TAFAUTI….YAANI WALE MANABII WA MWANZO NA HAWA WAISLAMU WA SASA?……Hoja ya mwisho kwa leo ni kuhusu biblia yenye vitabu 66 na ile yenye vitabu 73.Jibu lake ni rahisi sana kwa sababu hapo idadi ya neno la Mungu ni ileile katika biblia zote hizo ila mpangilio wa namba ndio tofauti.Neno la Mungu katika biblia hizo HALIJAZIDISHWA WALA KUPUNGUZWA.Mfano wake ni kwamba utakuta kuwa biblia yenye vitabu 66 imeligawa kumbukumbu la torati katika vijitabu vidogo dogo 10 wakati biblia yenye vitabu 73 imeligawa kumbukumbu hilo hilo la torati katika vijitabu vidogo vidogo 13 sasa huoni kuwa neno la Mungu litakuwa ni lilelile lakini namba za jumla za vitabu lazima zatatofautiana?…huo ni mpangilio wa waandishi wa biblia ambao kamwe hauwezi kwa mgawanyo huo wa namba kwenye neno hilohilo kuathili kwa kupunguza au kuongeza chochote kwa kuwa mpangilio wa namba hauhusiki na neno lenyewe la Mungu.Njoo ni kwa bwana yesu ndugu waislamu.Mungu awabariki.

    Like

  95. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina,
    Shukrani zote zinamstahiki Allah aliyemtuma Mtume wake kwa haki ndani ya dini ya kweli ili ishinde dini zote, hata kama washirikina watachukia.

    Ama baada ya Kumshukuru Allah(S.W), Naomba niitumie fursa hii kuwasilisha mada juu ya kwa nini waislamu tunasema nabii Yesu,alitumwa
    kwa mataifa ya Israeli na si dunia nzima kama wenzetu wa upande wa kushoto wanavyoaminishwa na watu wasiojua au kwa makusudi
    wanaotaka kupotosha ukweli.Kwa leo nitatumia ushahidi wa kitabu chao wenyewe kinachoitwa biblia kwa sababu kwa upande wetu Quran iko
    wazi kabisa;

    Kama kawaida, naomba nianze kunukuu hoja alizotoa ndugu Mhina ili kuhalalisha kuwa Nabii Yesu alitumwa kwa ajili ya Dunia
    nzima, halafu nitoe uchambuzi;

    HOJA YA MHINA; “Lakini kumhusu bwana yesu kwetu sisi, Mungu wetu alikwisha weka wazi tangu zamani kwa kusema:
    NIMEKUWEKA ILI UWE NURU YA MATAIFA UPATE KUWA WOKOVU HATA MWISHO WA DUNIA.Soma(Matendo 13:47).”

    JIBU;Kwa uelewa wake wa biblia anataka kutwambia kwamba hayo maneno ni utabiri wa Bwana Yesu toka zamani, kweli kama
    huyu ndiye mchambuzi wenu wa biblia wakiristu nawapa pole kubwa, kwa sababu knowledge yake ya biblia iko chini mno.
    Kwa kifupi kabisa maneno hayo aliyatamka bwana Paulo katika injili yake akidai kuwa yeye amewekwa awe nuru ya mataifa wala
    siyo Yesu.Paulo aliendelea kudai kuwa neno la Bwana Yesu lilitakiwa kuhubiriwa kwa Wana wa Israeli kwanza halafu kwa mataifa.
    Ndugu zangu,Maneno hayo katika MATENDO 13-46-47 yanafanana kwa karibu
    sana na yale yaliyopo kwenye MATENDO 18:5-6 pale Paulo alipowahubiri wana wa Israeli Lakini wao wasimsikilize kwa sababu
    walimjua kuwa ni muuawaji wa wanafunzi wa Yesu tokea zamani kwa hiyo ikawa ni vigumu kwao kumpokea kwa sura nyingine kama mtume
    Paulo aliwajibu hivi “kwa kuwa hamkunisikiliza basi kuanzia leo NAGEUKIA mataifa”(MATENDO 18:5-6).

    Ndugu Mhina, ukisoma GALATIA 2:7 Paulo huyu-huyu anadai kuwa Bwana Yesu alimpa Injili ya wasiotahiriwa ambao
    ni mataifa kama Petro alivyopewa injili ya waliotahiriwa. Sasa je mbona alikuwa anawahubiri waliotahiriwa na hali hiyo injili yao
    yeye hakupewa?Je aliwahubiri kwa kutumia injili ya wasiotahiriwa hali wao wametahiriwa?
    Kwa nini basi aliwahubiri na walipokataa akawalaani na hali akijua kuwa yeye hakuwa Mtume wao? Na kama kweli
    angekuwa ni mtume rasmi kwa ajili ya mataifa ni kwa nini asubiri waisraeli wamkatae ndipo aamue kuyaendea Mataifa?Je Yesu
    alimwambia waliotahiriwa wakikutaa tu nitakufanya uwe mtume wa mataifa?Waswahili wanasema siku zote njia ya mwongo ni
    fupi! na siku zote msema uwongo kuna siku tu atajisahau! na hapo ndipo tunaona uwongo mwingine wa Paulo;

    Lakini Je unajua ni kwa nini Paulo alikimbilia kwa mataifa?? mhhh! usijali nitakwambia, ni kwa sababu Biblia ishasema mataifa hawana akili!
    kila kitu wao wanapokea wala hawatafakari tofauti na waisraeli hivyo Paulo alilijua hilo.Paulo alipofika kwa mataifa ndipo
    akasema “Injili ilibidi ihubiriwe kwa wana wa israeli kwanza halafu kwa Mataifa hivyo mimi ni mtume wa mataifa” mataifa kama
    kawaida wakasema ndiyoooooooooooo! ndiyo mpaka sa hizi wakiristu wameshikilia kauli hiyo!

    Lakini mimi na wewe tupate bahati ya kutafakari maneno ya Bwana Yesu.Hivi ni kweli Bwana Yesu alisema mkikataliwa
    na wana wa israeli ndiyo mwende kwa mataifa kama Paulo alivyofanya? Hebu tumsikilize Bwana Yesu aliwaambiaje wanafunzi
    wake tusije tukaangukia pua!

    MATAYO 10:22-23 “Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu, lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye
    atakayeokoka Lakini watakapwafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawambia, Hamtaimaliza miji
    ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu”

    Hapo tunaona Bwana Yesu akiwaasa wanafunzi wake wawe wavumilivu kwani watakataliwa, watachukiwa, watatukanwa
    na zaidi watafukuzwa mijini lakini anawaomba wavumilie wasiache kuwahubiri waisraeli, hasa watakapofukuzwa mji mmoja
    wa israeli wahamie mwingine na waendelee kufundisha neno lake kwa wana wa Israeli tu kwani mpaka anarudi yeye miji hiyo
    itakuwa haijaishaaaaaa!

    Kwa maneno hayo ya Yesu, tunaona kuwa kama Bwana Paulo angekuwa kweli ni mtume wa Yesu tunaona kwanza alikosa
    uvumilivu ambao Bwana Yesu aliuagiza na pili hakufuata amri ya Yesu aliyowaambia ya kuwa wakiwafukuza mji mmoja wa israeli
    waende mwingine kwani tunaona yeye kukataliwa tu mji mmoja akaona ni bora aje kwa mataifa lakini tatu Bwana Yesu alisema miji
    hiyo haitaisha mpaka atakaporudi yeye.Je? Paulo wakati anakuja kwa mataifa miji yote ya Israeli ilikuwa imeisha? jibu ni hapana kwa
    sababu Yesu alisema haitaisha mpaka atakaporudi.Je wakati Paulo anayaendea Mataifa BwanaYesu alikuwa amesharudi? Obvious hapana
    Je hujauona uwongo wa Paulo mpaka hapo? si nyie mnajiita wasomi sasa mbona kitu kidogo mnashindwa kung’amua.
    Ndugu msomaji maswali ni mengi lakini yote nakuachia utafakari! uone hawa ndugu zetu wanavyodanganywa kwa sababu ya kutotaka
    kuisoma biblia na kusubiri kusomewa hivyo wanashindwa kuujua ukweli!

    HOJA YAKOYA PILI; baada ya hapo, sisi wa Mataifa tunapokea nuru ya wokovu wake.Ndio maana Mungu akasema
    ISAYA 49:6 ZAIDI YA HAYO NITAKUTOA UWE NURU YA MATAIFA UPATE KUWA WOKOVU WANGU HATA MIISHO YA DUNIA
    .Soma kwa makini(isaya 49:6)….Hoja y

    HOJA YANGU; Ndugu Mhina, mimi nitaendelea kukushangaa sana unapoamua kulihubiri neno la mungu wako kwa propaganda
    za uwongo! Ndugu wasomaji wa blog hii hebu kaisome hiyo ISAYA 49:6 aya hii iko wazi na kila mtu ataielewa! Maneno hayo
    yalisemwa na Mungu na alikuwa akimwambia Nabii Isaya hivyo ni maneno yanayomhusu nabii Isaya wala siyo Yesu.Siku zote
    nakwambia iache Biblia yako ijisemee! wewe siyo msemaji wa biblia unaihurumia nini?

    HOJA YAKO YA TATU;Ulinukuu ISAYA 50:12 BWANA AMEWEKA WAZI MKONO WAKE MTAKATIFU MACHONI PA MATAIFA
    YOTE,NA NCHI ZOTE ZA DUNIA ZITAUONA WOKOVU WA MUNGU WETU

    HOJA YANGU; Maneno hayo, Mungu anaahidi kuwa dunia nzima watauona utukufu wake ni kweli kabisa lakini ahadi hiyo
    anapewa nabii isaya na siyo Yesu.Tuoneshe ahadi aliyopewa Bwana Yesu.

    Baada ya kuona kuwa wakiristu wanababaika kwa kushindwa kuitumia Biblia yao kutuonesha ni wapi Bwana Yesu, katumwa kwa
    ajili ya Dunia.Nimeona ni bora niwaondoe kwenye giza rafiki zangu wakiristu kwa kuzieleza hoja zilizo
    wazi kabisa ndani ya Biblia zinazoonesha kuwa Yesu ni nabii kwa ajili ya wana wa Israeli tu kwa uwazi kabisa wala siyo kiubabaishaji!

    HOJA ZANGU ZA MSINGI ZINAZOONESHA KUWA YESU NI MTUME KWA AJILI YA TAIFA LA ISRAELI TU!

    Ndugu wakiristu, Kwanza kabisa Yesu alipozaliwa Malaika aliwatokea watu mbali mbali akiwaambia kuwa kuna mtoto kazaliwa na mtoto huyo ni nani
    .miongoni mwao ni hawa mamajusi ambao tunaona wakisema;
    MATAYO 2:2 “Yu wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?”
    Kwa hiyo ndugu zangu, hoja hii moja tu inanitosha kabisa kuwaelewesha wakiristu kuwa Bwana Yesu alikuwa mfalme wa Wayahudi na si mfalme wa
    ulimwengu kama wakiristu wanavyodai kwani tukiwauliza wanatoa wapi maneno hayo katika biblia wanababaika sana.Sasa je
    ndugu yangu Mhina, ndugu yangu mtanzania wewe ni Myahudi? hadi huyo Yesu awe mfalme wako kama unavyomuimbia kila siku kanisani?
    Je wewe una elimu kuliko hao mamajusi? la hasha!

    Lakini pia tunaona kuwa vitabu vya manabii vilikwisha kutabiri kuzaliwa kwa Bwana Yesu kama alivyoambiwa Herode na makuhani wa jerusalem;
    MATAYO 2:6 “Nawe Bethlehem katika nchi ya Yuda hu mdogo kamwe katika wajumbe wa Yuda; kwa kuwa kwako atatoka mtawala
    atakayewachunga watu wangu Israeli”
    Neno hili la Mungu mwenyewe kupitia vinywa vya Manabii lilishatabiri zamani kuwa mtoto atakayezaliwa atakuwa ni mchunga kondoo wa taifa
    lililopotea la Israeli.Ndugu, Tena hapo Bahati nzuri Mungu mwenyewe ndiye anasema sasa nyie mnampinga Mungu?
    Je wewe nafasi yako mtanzania, mkenya, mrwanda,m-ethiopia,mbulgaria,mmarekani iko wapi hapo?

    Lakini pia Yesu mwenyewe alikuwa akijitambulisha mara nyingi kuwa ametumwa kwa ajili ya wana wa israeli tu na siyo kwa ajili ya
    mataifa kama pale alipomwambia mwanamke mkananayo;
    MATAYO 15:24 “Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”
    Kauli hii ni fupi sana na yenye maana kwa mtu mwenye akili; Hapa bwana Yesu anadhihirisha kuwa hakutumwa bali kwa wa-israeli tu.
    Je wewe unayebisha unataka Bwana Yesu atumie kauli gani ndiyo ujue kuwa wewe si katika kazi yake? Je ina maana Yesu aliposema
    “sikutumwa ila kwa israeli” kauli mtu mswahili anashindwa kuilewa au ataka kumfanya Yesu aonekane mwongo?na kama alitaka neno
    lienee kwa wana wa-israeli kwanza halafu kwa mataifa kwa nini hapo ajibu hivyo?

    Ndugu wakiristo, tunaendelea kuona yule mwanamke alipomkazania sana BwanaYesu akamwambia;
    MATAYO 15:26 “Akajibu akasema si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa”
    kwa hiyo kwa mujibu wa Yesu sisi wa mataifa ni ‘mbwa’ halafu waisraeli ni ‘watu’.Kwa hiyo angekuwa ametumwa kweli kwa mataifa
    asingetuita mbwa kwa sababu mtume hawezi kutumwa kwa mbwa kama , kwa sababu angelazimika kwanza yeye mwenyewe awe mbwa(Mungu apishe mbali)
    halafu ndo atumwe kwa mbwa wenzie sasa.kitu ambacho Mungu alipisha mbali kabisa!

    Ndugu Mhina, Bwana Yesu hakuishia hapo kuonesha dhamira yake kuwa hakutumwa kwa mijibwa ya Mataifa bali aliwaambia wanafunzi
    wake na kuwakataza tena na tena wasiende kwa midogi ya mataifa pale aliposema katika;
    MATAYO 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu wala situpe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao,
    wakaruka na kuwararua.”
    kilicho kitakatifu ni neno la injili, alitumia lugha ya fumbo lakini lengo ni kuonesha kuwa sisi watu wa mataifa sio lengo la kuja kwake.

    Ndugu mhina, Bwana Yesu hakuishia hapo bali akaendelea kutia msisitizo tena pale alipowaambia wanafunzi wake kuwakataza wasiende kwa mataifa;
    .Kwani ni haramu sisi mbwa kupewa kilicho kitakatifu katika;
    MATAYO 10:5 “Hao thenashara akawatuma akiwaambia katika njia ya mataifa msiende wala katika mji wowote wa samaria
    msiende bali ishikeni njia ya kuwaendea kondoo wa nyumba ya Israeli waliopotea, na katika kuwaendea hubirini mkisema
    ufalme wa Bwana unakaribia”

    Pamoja na ushahidi huo wote wa Bwana Yesu,Wakiristu kwa kutafuta kujipachika pachika kwa Bwana Yesu wanautumia
    msitari huu ufuatao kuwa ndipo alipotoa ruhusa ya kuyaendea mataifa kwa wanafunzi wake, kitu ambacho siyo kweli kabisa;
    MATAYO 28:19-20 “Basi enendeni katika mataifa yote mkawafanye kuwa wanafunzi wangu mkiwabatiza kwa jina la Baba
    la mwana na la Roho mtakatifu”

    Nilishaelezea maana hasa halisi ya maneno haya hapo juu lakini si vibaya nikirudia japo kwa ufupi;Ukiangalia hapo
    neno lililotumika ni “mataifa yote” ukichukua Biblia za kiingereza zimetumia “all Nations”. Kitu cha ku-note hapa
    ni kwamba kama msitari huu ungekuwa unatuhusu sisi mataifa hapo lingetumika neno “mataifa wote” na si “mataifa yote” kwani
    “mataifa yote” maana yake ni yale mataifa 12 tu ya Israeli, na kama kweli hiyo amri ingekuwa inatuhusu hata Biblia za kiingereza
    zisingetumia neno “all Nations” bali sasa zingetumia neno “all the Gentiles”.Kwa hiyo kwa kifupi hapo Bwana Yesu alikuwa akimaanisha
    wanafunzi wake wayaendee yote mataifa 12 ya Israeli kwani siku ya hukumu wataketi katika viti 12 wakiyahukumu mataifa hayo na siyo wewe mtanzania;

    Lakini kwa mkiristu yeyote anayebisha, kwa sababu binadamu huwa hatupendi kuambiwa ukweli!
    Wanafunzi wa Yesu, walielewa kuwa Bwana Yesu aliwakataza kwenda kwa mataifa na ndiyo maana hata Bwana Yesu alipokwisha
    kuondoka duniani waliendelea kujilinda wasije wakahubiri Injili kwa watu wa mataifa, na baadhi ya wanafunzi wa Yesu walioyaendea mataifa
    walikuwa wakisutwa na wenzao;
    Hebu we mbishi soma msitari ufuatao utaelewa;

    MATENDO 11:19`”Basi wale waliotawanyika kwa sababu ya Ile dhiki iliyotukia kwa habari ya Stefano wakasafiri kwa Fineoiki na Kiproni
    na Antiokia, WASILIHUBIRI lile neno ILA kwa WAYAHUDI peke yao”

    Baada ya Yesu kuondoka kulitokea njaa hivyo wanafunzi wakaenda Feneoiki,Antiokia na Kiproni ambayo ilikuwa ni miji ya wamataifa kule
    hawakuhubiri Injili isipokuwa kwa wayahudi peke yao, kwani bado walikuwa wanakumbuka maneno ya Yesu alivyowakataza;Je wewe mbishi
    jiulize kama kweli Bwana Yesu pale kwenye MATAYO 28:19-20 Alimaanisha wakayahubiri mataifa tofauti na ya israeli mbona wanafunzi wa
    Yesu wenyewe hawakufanya hivyo?Na waliojaribu kufanya hivyo walifanya kwa siri na walipogundulika wale wenzao walikuwa wakiwasuta na
    kuwaonya; Hebu soma hapa chini wewe mbishi.

    MATENDO 11:23 “Na Petro alipopanda kwenda Yerusalem, wale walio wa tohara wakashindana naye wakisema uliingia kwa watu
    wasiotahiriwa ukala nao”

    Hapo tunaona Petro akionywa na wanafunzi wa Yesu kwa kukaa na watu wa mataifa na kula nao tu.Je mtu usiyeruhusiwa hata
    kula nae utaruhusiwa kum-hubiri.kwa hiyo walikuwa hawaruhusiwi kabisa hata kuongea nao kwani wao ni wateule.

    Pia tukisoma GALATIA Tunaona Paulo mwenyewe akiudhihirisha unafiki wa Petro na Barnaba kwa kuwa walienda kuwafundisha
    watu wa mataifa kwa siri;
    GALATIA 2:12-13 “Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa
    Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa. Na hao wayahudi wengine wakajigeuza
    pampja hata na Baranaba pia akachukuliwa na unafiki wao”

    Hii inadhihirisha uongo wa Paulo kwa kujitia mtume wa mataifa kwani hapo tunamuona akiwalaumu wenzake waliokuwa wakienda
    kwa mataifa kufundisha, lakini tukisoma katika MATENDO 18:5-6 Tunamwona yeye huyu-huyu aliyewasuta wenzie kwa kupinga amri
    ya Yesu ya kutowaendea mataifa akiyaendea tena bahati mbaya kabisa baada ya ujumbe wake kukataliwa na waliokuwa wanamjua
    kama muuwaji!

    Mwisho ndugu Mhina, unapokuwa unamtetea Yesu ni lazima uweke ushahidi wa maneno yake mwenyewe kwanza kama nilivyofanya mimi
    hapo juu siyo unakimbilia mara ooh! hata mtu mmoja alisema! ooh mara fulani alisema!! mmmmm! hapanaa kwa sababu kila mtu alisema lake
    wengine walisema ana mapepo je na hao tuwasikilize? Ni bora tumuache Yesu aseme mwenyewe kwanza halafu tuwaangalie wengine wanamsemaje,
    hapo tutaenda sawa kabisa kuhusu utume wake na kuhusu yeye mwenyewe kwa ushahidi wa biblia hapo tutakuelewa;

    Aidha Quran tukufu iko wazi kwamba Yesu alikuwa ni mtume kwa wana wa Israeli na hilo liko wazi;Kama kuna waislam wanasema Yesu
    alikuwa mtume wetu pengine wako sawa kwa sababu Yesu alikuwa ni mtume muislam kwa ushahidi wake ndani ya
    Biblia tumeona akisema, pia kwa sababu mitume wote ni wa Allah na sisi hatubagui hata mmoja baina yao, na waislam wote tuko sawa.

    wwahaadha ssalaaam!
    wabillah tawfiq.

    Like

    • alfa says:

      kijana naitwa alfa rashd ukipenda cal me king,kijana hata mumtetee vp hasimami hyo babu kashaoza,musa elia wamesepa yesu kapaa mwana.watu tunaring mwana na yesu wetu,wapinga kristo hamjasoma maneno haya kila anayekataa ya kuwa yesu ni mwana wa mungu huyo ndie mpinga kristo,na yesu alisema hvi,yohana 17:1-2,maneno haya aliyasema yesu akainua macho yake kuelekea mbinguni akisema,baba saa imekwishafika,umtukuze mwanao mwana wako nae atakutukuza wewe,kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili,ili kwamb wote uliompa awape uzima wa milele,sasa mudy ye hana mwil au we huna?pia soma yohana 17;4-5,yesu anasema,na sasa baba unitukuze mimi pamoja nawe kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.kuhusu swala la kwamb yeye atatolewa awe nuru ya mataifa listen ths kiduchu,sikia mwana,yohana 17:20 yesu anasema wala si hao tu ninaowaombea bli na wale watakaoniamini kutokana na neno lao,ninayo mistar ming ya kukupa kijana ngja nimsalimie shmej ak i wl b back na kapu la mistar na madongo yangu.

      Like

    • alfa says:

      lm back mpendwa ktk bwanaaa!alpha the don kiler,napata raha sana kusikia hoja za kitoto zinanipa raha kujibwaga,umeshajibiwa nami nakuongeza maarifa ndugu yangu na rafk yangu,ndani ya moyo wangu nashuhudiwa hvyo beibe!hollah!hyo GALATIA 2 anzia hapa 2:11-15.lakini kefa alipokuja antiokia,nalishindana nae uso kwa uso,kwa sababu alistahili hukumu.kwa maana kabla hawajaja, watu kadha wa kadha walitoka kwa yakobo,alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa;lakini walipokuja wao,akarudi nyuma akajitenga,akiwaogopa waliotahiriwa,na hao wayahud wengine wakajigeuza pamoja nae,hata na barnaba akachukuliwa na unafki wao,lakini nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kwel ya injil,nalimwambia kefa mbele ya wote,ikiwa wewe myahud wafuata destur za mataifa,wala si za wayahud kwa nini unawashurutisha mataifa wafuate destur za wayahud,sisi tulio wayahud kwa asili wala si wakosaji hali tukijua ya kuwa mtu haesabiwi hak kwa matendo ya sheria bli kwa imani ya kristo yesu.ndugu mzozo uliozuka hapa haihusian na tafsir ak

      Like

    • ndugu kwa akil yako hv jua hutuama kwenye maji machafu?sasa hyo ni quran imesema hvyo,nao hudai jajmaa anaiweza mpaka scienc,utumbo kibao ntakupa nkikaa poa,hyo ndo sayans wanayomsifia hyo jamaa anayejifany mtume. says:

      tatizo mungu wenu muongo na muoga dat y anawafundish kutetea dini kwa kusema uongo.maneno ya isaya unadai ya paul.hv kwa nini niny waongo kupita kiasi,hapo huwa naamini mnakijua mnachokifanya,wapinga kristo na mungu wao anayewaitia maut,hv mnamsifia mwanasayans wenu anaedai kuwa jua hutuama kwenye maji machafu,mpandikiz wa chuk,na mnampasifa kwa kuoa mtoto hvi nyie mpoje!!!.i feel so much sry,bt i lv u all najua mungu hana upendeleo,atafanya jamb kwa kila aliyemkusudia.be blesd.

      Like

  96. alfa says:

    mwana moyon nna raha kinoma mwanangu,nadhan mungu amekupitisha ktk mikono mipya c kubishana bali kufunguliwa,na huu ni wakat wako utakaotoka gizani kwa maana nuru imekuzukia au co,4gve smtime, coz i lke jokes bt lm seriouz in ths,au co brada,isaya 9:6 kwa ajili yako na yangu mtoto amezaliwa tumepewa mtoto kidume na uweza wa kifalme utakuwa begani begani mwak,naye ataitwa mshaur wa ajabu,mungu mwenye nguvu,baba wa milele mfalme wa amani maongeo ya enz ak na aman hayatakuwa na mwisho kamwe.ngoja nipate raha zangu nikujibie hoja moja kwa kurasa 4.i wl b back kisha ntamchambua mudy au thio chalii.wait najua wameshakujibu ila ntakufundisha kwa kuwa jehova lvz u dat y hujawah kumeet smbdy lke me.i lv u niga,najua hayo yanayofanyka ni upofu 2,imeandikwa wakat utafka anybod wh kils u atadhan anamtolea mungu ibada,na kwel hudhan hvyo.ndugu ntayafungua bt nayapangilia kiupendo,lv iz wht we had.

    Like

  97. Juma says:

    Mimi nitaiamini bible mpaka aya hii iondoke: 8:8 yeremia: MWASEMAJE, SISI TUNA AKILI, NA TAURATI YA BWANA TUNAYO, LAKINI TAZAMA KALAMU YA WAANDISHI WAMEIFANYA TAURATI KUA NI UONGO. Haya kama kitabu cha waklisto kina uongo ndany, je ni mungu gani ane ongea uongo,? na kutaka watu wafuate uongo huo.?!!!!

    Like

    • alfa says:

      labda daka na hili mwana,taurat tunayo lakn kalamu ya waandish imeifanya kuwa uongo,moja kwa moja ni yale mapokeo yao waliyokuwa wakipokezana ambyo hata mfalme wa wafalme yesu aliwasema juu ya hlo,na mbka leo hii wanayo mapokeo yao na biblia bt mapokeo yao yapo palepale so elewa brada

      Like

    • alfa says:

      halaf mwana achen ulev wa kiroho,unapoambiwa ishmail atatoa maseyd 12 na iska kabila 12 elewa kwa nini wameitwa seyd na wengne kabila,pia elewa maana ya agano la kudumu ntalifanya kwa yakobo,tena la milele,sas ishmail ambaye ni pundamwitu ni yule ambaye si mrith wa baraka hz za ibrahimu,yule aliyekataliwa tangu mwanzo,kusimama mbele ya ndugu zake daima haimaanish kama pared inamaanisha uadui kati yake na wana wa agano,na hli ni neno la kiroho,usifikiri punda mwitu ni waarabu wote sivyo mwana,waarabu waliompokea kristo wamehesabiwa hak warith katika kristo,wale waliokataa ndio punda mwitu,na hao ndio mkono wao utakuwa juu ya watu wote na mkno wa watu wote utakuwa juu yao,angalia syria wenyewe kwa wenyewe,mara wanalipua makanisa,mara wanashambulia serikal,mara wanataka miji yao,yaani mara alshabab mara alqaida mara boko haram,wanashambulia tu wakimtolea mungu wao ibada,wape na wenzio walioandika pumb huko juu.

      Like

  98. alfa says:

    ile hoja ya watoto wadogo et y akataliwe ndo awageukie mataifa,unahtaj elimu ya roho,mungu akisema jambo ni lazime litimie na alitimizaye huwa hajui kwa wakat ule kwamb analitimiza,israel iliandikwa wao watatazama wasielewe, lile neno jiwe walilolikataa waash 2 b jiwe la pembeni unakumbuka?afta dat wale waliokwenda gizani yani wewe na mimi nuru imetuzukia,boy hyo elimu ya rohoni yani ilikuwa lazima yatimie,injil ihubiriwe kwanza israel na yuda,kisha wageukiwe mataifa na ndo ilivyokuwa,den uokovu unatoka kwa wayahud mwanangu ktk bwana!blin!!!,nsubiri nikuandikie kitabu frm the holy bible agano la kale na utimilivu wak agno jipya,jins watu wa mungu waliosh miaka tofaut walivyoongozwa na roho ktk habar hii,tchatcha roho mtakatifu aliyemuomb daud anekuwa mudy chacha da!e bna mc u brada mida shem ako anaanda nthothi welkam ka vp,nkirud tena i thnk afta a week ntakuwa read.

    Like

    • alfa says:

      pia israel wote wataokoka maana wataangukia toba mwana mungu hawatup wana wa agano mwana ila wapinga kristo wajipange,mak lv preach peac co chuk.

      Like

    • alfa says:

      tatizo unaposoma elewa usikariri,janja ya kuchukuwa nusu mstar ukaishia kat ili uendelee kupiga stor humu mwana noma!ukielewa kubali, co ligi mpendwa,hata kimoyomoyo co mbya,baada ya kukupa kitab hki utakuwa huru. mpendwa ktk bwana.manak naona mnazunguka mlemle 2.one day 2ngemeet ningefurah sana.

      Like

    • alfa says:

      it’z me alpha a.k.a don killa baibe!mwana kwani hyo aya ambayo unataka itoke imeandikwa na nani?kama una uelewa ni kwamb ilo limekuwa onyo kwa waandish wa sheria za kiyahud ambao walikuwa wanahukumu kwa sheria tofaut na maagizo ya torat yao,bas elewa hlo ni neno la nabii mwana da!kwa maana nyingne ni mapokeo yao ambayo yalikuwa tofauti na taurat yao mwana,then mudy mwenyewe ametukir weny vitabu ni sisi na jewz,ask us upewe uelewa.

      Like

  99. Mhina says:

    Ndugu.Mhammad yohana….Mbona sasa unaanza kuukwepa mjadala kwa kushindwa kujibu yale niliokuuliza huku ukileta hoja mpya ambazo zitatutoa kwenye mstari?!!…kilichobadilika ni nini tena!!…hebu twende kwa utaratibu uleule wa kiistarabu….yaani inamaana kuwa yale yote niliyokuuliza ulishindwa kuyajibu au?!!…mimi hapa nitayajibu yale yaliohusu ule mjadala wetu, halafu hizo hoja zako mpya sitazijibu mpaka na wewe unijibu yale niliokuuliza kwanza ili twende kwa utaratibu unaofaa na kueleweka na watu wote….Hoja yako ya kwanza umenukuu ile(matendo 13:47)……Katika andiko hili kamwe mimi sikusema kwamba bwana yesu ndie aliesema maneno ya hilo andiko kwa kuwa, yale maandiko yote aliyoyasema bwana yesu kuhusu injili yake kuwa ihubiriwe ulimwenguni kote TAYARI WEWE ULIKWISHA YAKATAA KWA SABABU ZAKO ZA UONGO UNAZOZIJUA WEWE MWENYEWE.Ndio maana mimi nikajaribu kutumia maneno ya Mungu mwenyewe ili ndugu yangu wewe upate kuamini na kuelewa vyema.Kwa hiyo katika hiyo(matendo 13:47) ni maneno aliyoyaandika mtume paulo akimnukuu Mungu mwenyewe katika ile (isaya 42:6) ambapo Mungu kupitia kinywa cha nabii isaya alisema maneno haya kumhusu bwana yesu: MIMI, BWANA, NIMEKUITA KATIKA HAKI, NAMI NITAKUSHIKA MKONO, NA KUKULINDA, NA KUKUTOA UWE AGANO LA WATU NA NURU YA MATAIFA…Kwahiyo ndugu.Mhamad, wewe ndie ukuelewa kabisa kwa sababu maneno yale kamwe sio ya bwana yesu wala Mtume paulo bali ni maneno ya Mungu mwenyewe yaliyonukuliwa na mtume paulo….ndio maana Mtume paulo alianza kunukuu kwa kusema ‘KWA SABABU NDIVYO TULIVYO AMRIWA NA BWANA’…..hoja yako nyingine ulijaribu kunukuu maandiko yangu haya:(isaya 49:6) (isaya 50:12)….Pasipo hata aibu, eti ukaamua kunipinga Mimi mkristo kwa kudai kuwa mimi sijui biblia pamoja na huyo mwalimu wangu alienifundisha, kwa kuwa maandiko hayo ni ya Mungu kamwambia nabii isaya na kamwe sio ya bwana yesu….huku ukiwashawishi wanaotufuatilia wadhibitishe uongo wangu….JIBU LANGU: Sasa Mimi nitakusaidia zaidi wewe na hao wanaotufuatilia ili wote kwa pamoja muelewe kwamba ni kweli bwana yesu amekuja kwa ajili ya watu wote na pia yale maandiko yote yanamuongelea yeye, kwa kua naona sasa unaweweseka mpaka unataka uwe mwalimu wa biblia ili uwapotoshe watu vizuri…Ndugu.Mhammad, wewe huna misingi wala fahamu yeyote ile ya biblia.Neno la Mungu linasema hivi: MAANA UNABII HAUKULETWA POPOTE KWA MAPENZI YA MWANADAMU BALI WANAADAMU WALINENA YALIYOTOKA KWA MUNGU WAKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU.Soma(2 petro 1:21)….Nae mfalme daudi alithibitisha jambo hilo kwa kusema; ROHO YA BWANA ILINENA NDANI YANGU NA NENO LAKE LIKAWA KINYWANI MWAMGU.Soma(2 samweli 23:2)….Nilichokusudia katika maandiko hayo ni kukuonyesha kuwa Mwenyezi Mungu, AMEONGEA NA SISI KUPITIA MANABII WAKE.Yeye alikuwa anatupa habari zinazo mhusu bwana yesu pamoja na mambo mengi ya maisha yaliopita, yaliyopo na yajayo kupitia vinywa vya manabii wake.Biblbia inatuambia kuwa, manabii wale walitabili mambo mengi sana yanayomhusu bwana yesu kupitia roho wake…’USHUHUDA WA YESU NDIO ROHO YA MANABII.Soma(ufunuo 19:10) (1petro 10:13)….Na kumhusu Mungu mwenyewe katika mambo yale anayotutabiria kwa nyakati zake, ili kutufahamisha kilichopita, kilichopo na kijacho, yeye anatangaza hivi: TAZAMA MAMBO YA KWANZA YAMEKUWA, NAMI NAYAHUBIRI MAMBO MAPYA, KABLA HAYAJATOKEA NAWAPASHENI HABARI ZAKE.Soma(isaya 42:9).Kwa hiyo ndugu.Mhammad, Mungu aliongea na sisi kupitia vinywa vya manabii wake na kamwe sio eti kusema: MUNGU ALIMWAMBIA NABII ISAYA PEKEE!!!…Sasa hebu jihukumu mwenyewe hapo kwa kutoajibu kwamba ninani kati ya mimi na wewe anaepaswa kuchekwa na watu wanaopitia kwenye blog hii!!…lakini mimi sitakuhukumu kwamba watu wakucheke kwa kuwa, mimi naamini kwamba, lengo lako ni kujifunza na kujua zaidi.Katika mambo yote hayo nilio kuelezea, ndipo tunapowaona malaika wa Mungu wakipewa jukumu la kuleta habari njema hizo za Mungu kwetu.Biblia inasema hivi: MALAIKA AKAWAAMBIA, MSIOGOPE, KWA KUWA MIMI NINAWALETEA HABARI NJEMA YA FURAHA KUU ITKAYOKUWA KWA WATU WOTE, MAANA LEO KATIKA MJI WA DAUDI AMEZALIWA KWA AJILI YENU MWOKOZI NDIYE KRISTO BWANA.Soma(Luka 2:10)…..Hapo pia kuna vitu vya msingi vya muhimu mno vinavyotosha kabisa kujibu na kuhoji hoja za ndugu.Mhamad yohana…Kwanza tumeona kuwa neno la Mungu limesema kuwa HABARI NJEMA ITAKAYOKUWA KWA AJILI YA WATU WOTE, NA KAMWE SIO ISRAEL PEKEE….PILI TUNAONA KUWA, MWOKOZI NDIYE KRISTO YESU…kama alivyotufagilia mtume mhamad wa waislam!!!(MASIYA)…..TATU….TUMEONA JINSI MALAIKA WALIVYOPELEKA UJUMBE WA MUNGU KWA UPOLE NA UPENDO….Sio kama wale malaika jibiliiii wa kiislamu walivyo mminya + mtia kabari + mbana + mtia homa mtume wao mhamad kule mapangoni!!!..Namalizia kwa kukuomba ndugu.Mhamad hebu jibu ile hoja yangu ulioikwepa kama ilikushinda kujibu basi niambie ili nikusamehe ndipo tuendelee na hoja mpya.Poleni sana waislamu wote lakini mimi nitaendelea kuwahubiria injili ya bwana yesu mpaka mtaokoka kwa hiari yenu wenyewe maana palipo nuru ya ukweli basi lile giza la uongo hufifia kana kwamba LIMEKUFA!!.

    Like

  100. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah, na niwatakie rehema mitume wake watukufu.

    Ammma baad!
    Ndugu Mhina, wallah nazidi kupata raha sana! ninapoona ukiangaika kulitafuta neno UKIRISTO kwenye Biblia nzima usilione! Pia unatafuta kwenye Biblia nzima hakuna sehemu Bwana Yesu aliposema hawa wafuasi wangu ni WAKIRISTO.Inna lillah wa inna ilayh rajiuun! hakika huu ni msiba kweli.Hiyo nimekwambia nenda hata kwa baba zenu warumi huko vatican hautapata.

    Sasa huo ndio upofu wenyewe ambao Bwana Yesu alishatabiri zamani kuwa itafikia zama watu wapotofu watakuwa na mwongozo lakini usiwaongoze kwenye kweli yote! pale aliposema wanayo macho lakini hayaoni sasa ndiyo nyie ambao kwa bahati mbaya mnayo biblia lakini haina majibu ya maswali inayoulizwa!!!!.Poleni sana ndg zng.

    Pili,Ndugu Mhina mimi nilisema Bwana Yesu ni mfano wa kuigwa kwa waislamu, ukashangaa saana. Ukiamini kuwa sisi waislamu kwa kusema hivyo tunamvunjia heshima Yesu.Ndugu yangu Mhina, mimi sikushangai bali nakusikitikia na kuwasikitikia wakiristu wenzako kwani uelewa wenu wa maneno ya kiroho ni mdogo mno. Ndugu Mhina, Mungu aliwatuma manabii wake ili wawe mfano wa kuigwa kwetu, kwani Manabii huishi maisha yao wakiwa na imani kubwa ya kiroho,Huishi maisha ya kumpenda Mungu, huvumilia mambo na mikasa mingi, huvumilia shida na muda wote wao huishi maisha ya kumtegemea Mungu wao aliyewatuma. Hivi nikuulize kuna ubaya gani sisi kuiga maisha yao?Kwa hiyo kila muislamu anatakiwa aangalie manabii waliishi vipi, walimuabudu vipi Mungu wao ili aweze kuishi maisha ya kumpendeza Allah, kwetu sisi waislam kila nabii ni mfano wa kuigwa , hata Nabii Muhammad mwenyewe kwetu ni mfano wa kuigwa.Na ni sunna kuishi kama manabii!! Sasa nyie wakiristu vipi? Kuna ubaya gani kuwafanya manabii wa Mungu mfano wa kuigwa?Au nyie ndo mmefanya shetani mfano wa kuigwa?

    Bahati mbaya kabisa kwako neno hili limekuwa zito, na ndiyo maana hata Bwana Yesu alikuwa akiongea nanyi kwa mifano kwa maana hamuelewi na mna vichwa vigumu! Kumbe niliposema Yesu ni mfano wewe ulifikiri mifano kama hilo lipicha la kubumba ambalo mmeweka hapo juu mkiamini kuwa ndiye Yesu, au mifano ya yale masanamu mnayo yaabudu kule makanisani. kumbe niliposema ni mfano wa kuigwa ulifikiri lipicha flani la mfano ambalo halina uhai! Kweli hapo ndipo ninapobaini jinsi tunavyotofautiana akili na uelewa! yaani mimi naongea maneno ya Mungu kiroho wewe unapokea kimwili!

    Bahati mbaya nyie Yesu sio mfano wa kuigwa kwenu, na ndiyo maana hamuishi kama alivyoishi Bwana Yesu bali mmechagua maisha yenu mengine kutoka kutoka kwa mababa zenu America na Ulaya! Ndiyo maana mnaingia na mabendi ya miziki makanisani na kuanza kuimba miziki eti mnamsifu! Hivi unaweza ukanionesha msitari hata mmoja ndani ya biblia ambao Yesu alisema mfanye ibada kwa kumsifu tena kwa nyimbo na mangoma! au unaweza ukanionesha sehemu yoyote katika biblia ambako Yesu alienda kupiga miziki kwenye sinagogi?Unataka kuniambia hiyo Kama si kazi ya shetani ni nini!.

    Pia Bwana Yesu aliwakataza wanafunzi wake kuomba kwa kupayuka payuka kitu ambacho tunaona ni tofauti na nyie mnaojiita wafuasi wa Yesu, kwani kupayuka na kupiga makelele ndiyo imekuwa Ibada yenu mkiamini kuwa mkicheza mziki sana mnawafurahisha malaika mbinguni.Hii yote ni kwa sababu hamtaki kumfanya Yesu kuwa mfano wa kuigwa katika maisha Yenu!

    Sisi waislamu ibada zetu ni sawa kabisa na ibada alizofanya Bwana Yesu, hivyo sisi kwetu ni mfano wa kuigwa kweli, siyo kama nyie mnaopiga magoma na kurukaruka makanisani kama wakongomani! Eti mnamwabudu Yesu Hivi Yesu aliwaambia mumuabudu eeeh! Hebu naomba unioneshe kwenye Biblia ni sehemu gani Bwana Yesu alisema mumuabudu????Kama siyo kazi ya Shetani ni nini? Mimi ninavyojua hakuna kabisa sehemu ambayo Bwana Yesu alishawahi kusema aabudiwe! Bali alikuwa akiwaambia wanafunzi wakeshe wakimuomba Mungu wakiziungama dhambi zao n.k. lakini siyo kama nyinyi mnavyofanya!

    Bwana Yesu alikuwa akisali kama waislamu kwa kusujudu paji la uso akiliweka chini na kumuomba Allah kwa unyenyekevu kabisa na manabii wote walifanya hivyo kama biblia inavyoonesha maeneo mbali mbali na alikuwa hapigi magoma na madisco kama nyie mnaojiita wafuasi wake kumbe wafuasi wa shetani.Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake jinsi ya kutawadha na kukaa na udhu muda wote kwa lengo la kujitakasa lakini nyie ni tofauti kabisa, hivi mnafuata mafundisho ya shetani gani?? Bwana Yesu alitahiriwa kama amri aliyopewa baba yetu Ibrahimu na Mungu sasa nyie mbona mnajiita wasiotahiriwa na mnabeza amri za Mungu mnaziita za kimwili? hii yote kwa sababu hampendi kuishi kama Yesu na kama Mungu alivyoagiza.Bwana Yesu alifunga saum ili kujitakasa zaidi, kama sisi waislamu lakini nashangaa nyie mnakejeli maisha ya Bwana Yesu na hamtaki kumweka katika maisha yenu.Zaidi ya yote Bwana Yesu akawaambia muwe waislamu kama yeye alivyokuwa muislam ili mpate uzima wa milele lakini bado hamtaki eti mnasema ni kijisifa tu, nyie kweli ndiyo wapinga Yesu wakubwa. Eti mnajifanya mnasalimiana “Tumsifu Yesu Kristo Mtumishi wa Bwana” hivi nikuulize hiyo salamu mliitoa wapi?? kama siyo kuchanganyikiwa tu hamjui hata mafundisho ya Yesu.Angalieni Bwana Yesu alikuwa akiwasalimia wanafunzi wake salaam nzuri kabisa “Shalom Haloom” kwa kiebrania ambayo maana yake ni sawa kabisa na sisi waislamu tunavyotakiana Heri kwa kiarabu tunaposema “Salaam Aleikum” hayo ni maamkizi yenye maana moja kwa lugha tofauti “Amani iwe kwako”. Lakini nyie mnaaga maamkizi ya kishetani kabisa!! Hivi hujui unaposema tumsifu Kristo unamaanisha kumsifu mungu jua??? mbona maarifa yenu madogo nyie!! yako wapi mafundisho ya Yesu makanisani???Badala yake mnafuata mafundisho ya wanadamu jambo ambalo hata Yesu alilikemea sana!

    Eti unatamba unanipa maana ya neno KRISTO, ndug yangu mimi kigiriki nakifahamu kuliko wewe kama unabisha naomba nikupe exercise ndogo tu ya kigirik au kiebrania/kiramaic kama utaweza kuchomoka.Kwanza naomba nikurekebishe ile siyo MESIYA kama unavyotamka wewe ni MESIH inayotokana na neno masah yaani futa au paka, au pangusa. na hiyo KRISTO siyo kigiriki bali ni Kiswahili kwa kigiriki ni CHRISTOSIS huyu alikuwa ni mmoja wapo wa miungu saba wa warumi aliyekuwa akiabudiwa siku ya jumapili na warumi .Hawa watu walikuwa na miungu saba iliyokuwa ikiabudiwa kila siku ya wiki na mungu wa saba aliitwa christosis.Wagiriki kwa kutaka kupotosha ukweli wakimtumia adui wa Yesu Paulo wakalibadilisha jina la MESIH kwenda CHRISTOSIS ili mungu wao aabudiwe na kila mtu. na Wazungu walipoipokea wakabadilisha zaidi wakaita CHRIST.Hawa wagiriki walikuwa wakimuabudu mungu huyu CHRISTOSIS yaani mungu jua.Na hawa WAKIRISTO yaani wafuasi wa mungu jua walikuwako huko Turky na katika baadhi ya dola za kirumi.soma hata hao waliotafsiri biblia yako wamekuwekea hapo kwenye maelezo ya chini ya MATENDO 11:25-26 .Kwa hiyo na nyie mkaiga eti WAKIRISTO. Maskini ndivyo mnavyoangamia hivyo kwa kukosa maarifa.Kumbe wenzenu walifanya hivyo ili kumfanya mungu wao CHRISTOSIS aabudiwe kupitia jina la MESIH ambaye walitaka asitajwe tena na wao warumi waitawale Dunia zaidi na nyie mkafyata mkia.Shetwaan aliyelaaniwa anafanya kazi yake kupitia mikono yenu.Kumbe nyie ni wafuasi wa mungu jua na ndiyo maana staili ya maisha yenu inatofautiana sana na ile ya Yesu.Ukisoma katika Quran huwezi ukakuta neno KRISTO kwa sababu kitabu chetu Allah mwenyewe ndiye aliyekiteremsha na ameapa kukilinda na kila aina ya madhara ya wanadamu bali utakuta neno MASIH Mwana wa Mariam.

    Paulo kwa kutaka kueneza utamaduni huu wa kuabudiwa “mungu jua” mungu wa warumi ambao ndio walikuwa mabosi wake yeye kama jemedari wa jeshi waliyemtumia kuuwa wanafunzi watukufu wa Bwana Yesu. Alizidi kuwahakikishia warumi kwamba sasa imani yao hiyo inazidi kuota mizizi na karibu sasa itahubiriwa dunia nzima pale alipowaandikia Barua yake inayoitwa “waraka wa paulo kwa warumi”. Hebu soma uone alivyowaambia.

    WARUMI 1:8 “Kwanza namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristu kwa ajili yenu nyote kwa kuwa IMANI YENU inahubiriwa Dunia nzima”

    Hapo alikuwa akiwapa ripoti mabosi wake, na wakoloni wa Israeli kipindi kile waliokuwa wakimtumia kama kibaraka wao ili waendelee kuitawala Israeli na Dunia nzima kwa kueneza imani yao hiyo na kumfanya mungu wao huyo aabudiwe Dunia nzima kitu ambacho tunaona kwa 60% walifanikiwa.

    Mafanikio hayo yote ni kwa sababu pia Paulo alitumia hila nyingi kama anavyojieleza yeye mwenyewe;
    2WAKORINTO 12:16 “Lakini na iwe hivyo, mimi sikuwaelema; bali kwa kuwa mwerevu naliwapata kwa hila”

    Jamani nafikiri hicho ni kiswahili rahisi sana, Hila kila mtu anajua maana yake.Kama hujui hila maana yake ni ulaghai au uwongo. Kwa hiyo Paulo anaendelea kueleza mwenyewe jinsi alivyotumia uwongo na ulaghai ili aisambaze imani ya warumi kama anavyosema hapa chini;
    1WAKORINTO 9:20-23 “Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi ili niwapate wayahudi, kwa wale walio chini ya Sheria nalikuwa kama chini ya sheria(ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria) ili niwapate walio chini ya sheria;Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria(si kwamba sina sheria mbele za Mungu…) ili niwapate hao wasio na sheria,Nalikuwa kama mnyonge kwa wanyonge ili niwapate wanyonge, nalikuwa hali zote kwa watu wote ili niwapate wote.”

    Mbaya zaidi ni hapo anaposema alikuwa hali zote kwa watu wote ili awapate wote,Ndugu wakiristo kumbuka kuwa enzi hizo pia walikuwepo mashoga, wavuta bangi,wezi n.k. Sasa hebu fikiria hivi hali ilikuwaje alipofika kwa makundi kama hayo? hasa alipofika kwa mashoga?Haya ndiyo mambo tunayowambia wakiristu kila siku,halafu mnaanza kulalamika eti tunawatukana, sasa kama ni ukweli tusiuseme?Kwa hiyo Kwa mtindo huu Paulo aliweza kuwapata wafuasi wengi wa “mungu jua” yaani wakiristu kwa kuwalaghai kuwa Kristu ndiyo tafsiri ya Masih.Sasa hebu nikuulize hivi majina huwa yana tafsiri? yaani ushawahi kuona mtu anatoka Tanzania anaitwa upendo anafika America anaitwa “Loveness”, wapi na wapi ndugu yangu mbona hamtumii akili nyie wagalatia???Kwa mtindo huu naamini kweli njia ya kwenda uzimani ni nyembamba mno kwani shetani amejikusanyia wafuasi wengi mno.

    Lakini kama Paulo angekuwa Mtume wa kweli kutoka kwa Mungu isingemlazimu yeye kutumia hila na uwongo kama tulivyoona!!la hasha, Bali angeendelea kuwa na msimamo mmoja kwa watu wote na siyo kuwa hali zote kwa watu wote.Hebu mwangalie Yesu, alikuwa na msimamo wake ule ule hata alipopelekwa kwa Pilato na Herode hakubadilika hata kidogo, Mtume Muhammad pia alipigwa mawe mpaga kanzu yake ikalowa damu lakini aliendelea kuwa na msimamo mmoja kwa watu wote, na hii ndiyo sifa ya mitume wote wa Mungu.

    Ndugu Mhina ukachemsha zaidi pale uliponiambia kuwa mnaamini Yesu ndiye Mtume na Nabii wa Mwisho! Hivi mbona unaongea tu maneno ilimradi umeongea?Mbona nyie kila siku mnapata mitume na manabiii wa kila namna na kila sampuli! mara ooh Apostle and Prophet of god TB Joshua huyu ndo baba yenu mnakoenda kuchukua akina beerzebuli ili mje kuzuga watu, mara ooh Mtume na nabii J.Mwingila, mara hata wewe tutakuja kusikia baada ya muda ni nabii ilimuradi tu mkono uende kinywani na watoto washibe na mke apate hela ya kwenda saluni, sasa hebu naomba uniambia iko wapi hapo nafasi ya Yesu ya kuwa nabii wa mwisho kama ulivyosema.Ndiyo maana hata Bwana Yesu alishasema kuwa wengi siku hiyo watasema tulifanya unabii kwa jina lako, kwa jina lako tukatoa mapepo, kwa jina lako tukafanya miujiza mingi n.k lakini nitawaambie tokeni machoni pangu hata siwatambui!Alishasema atawakana nyie.

    Ndugu Mhina, Uliniuliza swali kwamba ni ipi nafasi ya Yesu kwa waislamu na wewe naomba nikuulize ni ipi nafasi ya nabii Ezekieli kwenu, pia ni ipi nafasi ya nabii Nuhu kwenu tatu ni ipi nafasi ya nabii Lut kwa wakiristu naomba jibu lako.

    Ndugu Mhina, ukatoa dalili za mpinga Yesu kwamba zote anazo Mtume wetu Mtukufu(Mungu apishe mbali) ukisema mojawapo ni kukataa kwamba Yesu kasulubiwa.Ndugu Mhina na wakiristu wote naomba muelewe kabisa kuwa Yesu hakusulubiwa hata kidogo! kwa sababu kusulubiwa ni laana hata biblia yenu inasema hivyo, sasa utasemaje kipenzi cha Mungu asulubiwe??Hivi Mhina utaendeleaje kusema unampenda Yesu na hali unakubali kuwa kalaaniwa pale msalabani pamoja na wale wezi na wanyang’anyi! hebu na wewe tumia hizo akili ndogo alizokujalia Mungu kwanza punguza kidogo kutumia akili ya mchungaji wako wa kanisani, Allah katika quran anasema wazi haiwi na haitokuwa yeye kumlaani kipenzi chake, bali Allah anasema alimnyanyua kwake wakati makafiri wa Jerusalem walipotaka kumfanyia kitendo hicho na akawapoteza macho yao wakaona wamemsulubisha lakini kumbe Allah ana uwezo mkubwa kuliko wao.

    Kwa hiyo nyie wakiristo wote yaani wafuasi wa mungu jua wote ni wapinzani wa Bwana Yesu, kwa sababu Mnaungana na makafiri wa Jerusalem kufurahia laana ya Yesu pale mtini tena wakiristu wanaenda mbali zaidi kabisa kwa kuupenda kwa mapenzi ya kupindukia msalaba ambao wanaamini ndipo yesu alikatia roho kule Golgota. Hivi wewe kisu kimemuua baba yako unayempenda hebu niambie utakipenda kweli???Mbona mnafanya unafiki kwa Yesu???

    Hata hivyo ushahidi ni mwingi mno ambao unathibitisha kuwa Bwana Yesu hakusulubiwa; Ukisoma katika biblia Yesu anasema ombeni nanyi mtapewa, na anaendelea kuwambia wanafunzi wake kuwa chochote watakachoomba Mungu atawapa kwani hakuna mzazi awezaye kumpa mtoto wake jiwe na hali amemuomba andazi.Ukiendelea kusoma katika Matayo unaona kwamba Bwana Yesu aliomba mara nyingi Mungu amuepushie na kikombe cha kusulubiwa.Je si tutakuwa wadhalimu tukisema Bwana Yesu kasulubiwa na hali alimuomba Mungu amuepushie kikombe hicho???Je nyie wakiristu mnataka kumaanisha kwamba Yesu aliomba dua ikakatiliwa? Acheni ufedhuli nyie!Acheni kujifanya mnampenda Yesu halafu mnamtukana eti kalaaniwa pale msalabani kwa ajili ya dhambi zenu.Ushahidi upo mwingi kuhusu suala hili ila tu naomba nikuulize Mhina swali moja; Hivi mwili wa ufufuo yaani mwili uliofufuka huwa ni mwili wa roho au ni mwili wa kawaida?Hebu nijibu swali hili kwanza.

    Lakini pia hebu ndugu Mkiristu angalia chanzo cha uokovu wako ambao unategemea kifo cha Yesu pale msalabani, mbona chanzo chake ni shetwani aliyemuingia Yuda na Yuda akamsaliti Yesu?Hivi unakubali kabisa chanzo cha uokovu wako ni shetwani aliyelaaniwa. Halafu kuthibitisha kwamba hamjitambui mnamwita Yuda msaliti wa Yesu halafu nyie mnajiita wafuasi wa Yesu na hali mnatakiwa Yuda mumpe utakatifu kwa sababu alimsaliti Yesu ili nyie mpate kuokoka.Halafu nyie mbona mnakuwa wakosefu wa shukurani kwa Yuda na shetwani???Wao walifanya vile ili nyie muokoke halafu nyie mnawaita wasaliti! Kwa hiyo pia nyie ni wasaliti wa Yesu kama alivyo Yuda na shetwani aliyemuingia.Mnatakiwa mumshukuru shetwani kwa kufanikisha uokovu wenu basi!si ndiyo hivyo? Hebu acheni kumpa nguvu shetwani ndugu zangu kwa sababu huko aliko bila shaka anajisifu kwani amepata wanaomsapoti wengi kwa alichokifanya.Hebu angalia hata hao waliowapoteza wanawasuta kwa kuwaambia Enyi wagalatia msio na akili ni nani aliyewaroga ya kuwa Yesu aliyewekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulubiwa?? Kweli wazungu wamewapoteza halafu nimeamini mzungu akianzisha kitu hata kama ni kibaya nyie akili yenu haipimi kabisaa! mnakuwa akina ndiyoo mzeee!

    SWALI LAKO: KAMA NI KWELI VITABU VYOTE MNAPASWA KUVIAMINI MBONA PALE MWANZO ULISEMA KUWA VITABU VYA TORATI, ZABURI NA INJILI VILIKUWA VYA ISRAEL PEKEE HALAFU QURUANI NDIYO KITABU CHA WANAAMDAU WOTE?

    JIBU LANGU;Ndugu Mhina, swali lako linatosha pia kuwa jibu la swali lako; Ni kweli vitabu vyote tunaviamini kwa sababu ni vitabu vilivyotoka kwa Mungu kama manabii wote tunavyowaamini kwamba wametoka kwa mungu, na tunaamini zaburi alipewa nabii Daudi(A.S) kwa ajili ya wana wa Israeli na Torati alipewa Musa(A.S) kwa ajili ya wana wa Israeli na Injili alipewa Yesu(A.S) kwa ajili ya wana wa Israeli na Quran tukufu alipewa mbora wa daraja, mbora wa mitume wote na mwisho wa mitume, Mtume Mustafa Muhammad ibn Abdullah (S.A.W) kwa ajili ya Ulimwengu mzima. Na sheria za Mungu ndani ya quran ni sawa na zile walizopewa manabii hao katika vitabu vyao.

    Ndugu Mhina, nafikiri nimekupa ushahidi wa kutosha wa manabii hao kutoka ndani ya biblia jinsi walivyokuwa wakijitambulisha wenyewe, Hata Bwana Yesu mwenyewe umeona ndani ya Biblia sehemu nyingi anajitambulisha kuwa amekuja kwa ajili ya Taifa la Israeli na ndiyo maana hakuna hata siku moja alifunga safari kwenda kwa nchi tofauti na Israeli kwenda kufundisha labda alikuwa anapita tu kama njia na kwenda zake na hata alikuwa akikutana na watu wa mataifa alikuwa akiwasaidia lakini huku akiwaambia kuwa yeye hakutumwa kwa ajili yao bali kwa ajili ya wana wa Israeli tu.Na sisi wa mataifa alikuwa akituita mbwa na nguruwe.Na alikuwa akisema mwenyewe mara nyingi tu kwamba mbwa hata siku moja hawastahili kupata kilicho kitakatifu yaani Injili, sasa mbona leo hii mbwa ndo wako msitari wa mbele kudai Yesu alitumwa kwa ajili yao?au ndio tena kiherehere cha mbwa hicho walichosema waswahili?Mara nyingi Bwana Yesu aliwakataza wanafunzi wake wasitupe lulu zao kwa mbwa yaani mataifa kwa sababu hawana akili.Hivi wewe Mhina ulitaka Yesu atumie kauli gani ndiyo sasa uelewe?Hebu sasa nikuulize unijibu unafikiri labda angetumia neno gani ili uelewe kuwa hakutumwa kwa ajili yako?Hebu sasa nione kama utalijibu swali hili.

    Ndugu Mhina, katika swali nililokuuliza kuhusu dini ya manabii wa zamani kwa ushahidi wa Biblia yako naona umechemka, mpaka ukatafuta jibu ndani ya Quran tukufu ukisema eti dini yao walikuwa watu wa kitabu? Hivi nabii Nuhu,Ibrahimu, Yakub, Isak, na Ismail walitumia kitabu gani kati ya zaburi,torati na Injili? Hebu naomba unitajie hiyo njia ya vitabu walivyotumia.Tuone kama na nyie wakiristu mnavitumia ili tujue kama Dini Yenu ndiyo dini ambayo ina misingi ya manabii wa zamani kama ulivyojitamba! Kwa sababu sisi Quran inasema hao wote walikuwa waislam kwa uwazi kabisa!

    Ndugu Mhina, mimi ndiyo maana naendelea kusema sisitahili kabisa kujadili na wewe labda uniletee mkubwa wako wa kanisa hapo kidogo tutajadili hoja, lakini siyo wewe.Hivi wewe unamiini dini ya kweli mpaka iwe na vitabu vya manabii wa zamani??? Sasa kama hicho ndo kipimo, hivi unaweza kuniambia ni kipi kipimo cha ukweli wa dini za manabii hao ambao Mungu aliwatuma bila kuwepo vitabu vya manabii waliowatangulia? Kwa mfano nabii Nuhu,Lut n.k kwa sababu wao pia hawakuwa na vitabu vya manabii waliowatangulia??Je nyie wakiristu mnaamini kuwa hao ni manabii wa uongo kwa sababu hawana vitabu vya manabii waliowatangulia??mbona akili yako ya kufikiria inakuwa finyu mno!!!
    Hata hivyo nyie wakiristu vitabu hivyo mlivyo navyo kalamu za waandishi zimeshakoroga kwa kiasi chake. Kwa ushahidi mwingi tu ambao tunaendelea kukupa!

    Ushahidi mkubwa mmojawapo niliokupa ni ule wa idadi ya vitabu ndani ya Biblia , ambao kwa kudhihirisha kuwa huna elimu yoyote kuhusu dini yako umesema eti idadi ya vitabu ni ile ile ila tofauti ni mipangilio tu! Hivi hujui kwamba wasomaji wa Blog hii wanaojua biblia wanakushangaa sana.

    Kwa kifupi ni kwamba Biblia asilia ilikuwa na vitabu 73.Biblia hii ilitumiwa na waroman Catholic mpaka mwaka 1940 alipojitenga Askofu Marthin Luther Sr. kutoka kanisa hilo, na kuamua kukimbilia Ujeruman na kuanzisha dhehebu iliyojulikana kama Protestants ambalo vijikanisa vyenu vingi vimezaliwa.Askofu huyo aliorodhesha sababu 95 za kujitenga kutoka kanisa Katolik mojawapo ya sababu ilikulwa ni kuvikataa vitabu sita ambavyo vimo ndani ya Biblia akidai kuwa vina maneno ambayo siyo maneno ya ufunuo wa Mungu bali ni maneno ya watu tu.Stori ni ndefu ukitaka mkasa kamili niambie nitakujulisha kwani najua hufahamu lolote na ndiyo maana unaamua kutetea tu bila ushahidi.Labda naomba nikupe exercise moja ndogo tu kama kweli hoja yako ni ya kweli kwamba biblia ni ile ile naomba uninakirie kwenye biblia yako uliyonayo MAKABAYO 1:1-8 naomba uniambie kutoka kwenye biblia yako yenye vitabu 66 maneno yaliyopo kwenye fungu hilo tunayapata wapi na ni yepi? Hebu naomba uifanye hiyo exercise kwa sababu bado unaonekana unaongea mambo usiyokuwa na elimu nayo.

    SWALI:HAO MANABII WA MUNGU WA ZAMANI TUNAOAMBIWA KUWA WALIKUWA WAISLAMU HIVI WALITUMIA KITABU GANI CHA HUO UISLAMU?

    JIBU; Ndugu Mhina,Manabii hupewa funuo mbali mbali, funuo hizo zikiandikwa huitwa vitabu.Manabii waislamu waliotangulia kuna waliotumia zaburi ,taurati na injili na hawa walikuwa ni kwa ajili ya Israeli tu.Allah alipomtuma mtume Muhammad kwa walimwengu wote ndipo alipompa Quran.Lakini wote waliishi maisha ya kiislam na walikuwa waislam.

    SWALI;NA PIA MBONA HATUKIONI KIKITUMIKA HII LEO KWA WAISLAMU WENZAO WA WAKATI HUU….AU MUNGU AMEBADILIKA YEYE NA NENO LAKE LILE LA AWALI.

    JIBU;Leo hii inatumika Quran ikiwa ni kwa ajili ya ulimwengu mzima tofauti na zamani manabii walitumwa kwa ajili ya taifa teule la Israeli, na Mungu hajabadilika na neno lake ni lile lile.Na ujumbe wa manabii wote ni ule ule kutangaza kuwa Mungu ni mmoja, na kuamrisha watu mema na kuwakataza mabaya.

    SWALI;NAKAMA NI HIVYO KWANI HAWA WOTE WAITWA WAISLAMU WAKATI VITABU VYAO NI TAFAUTI….YAANI WALE MANABII WA MWANZO NA HAWA WAISLAMU WA SASA?

    JIBU;Majina ya vitabu walivyopewa ni tofauti lakini neno la Mungu ni lile lile! Na wote wataitwa waislam nitakupa ushahidi zaidi kwa kutumia biblia yako,Mungu akinijalia kwa sababu inaonekana una hamu hasa ya kujua kuhusu manabii wa zamani na dini zao kwa ushahidi wa biblia au hata kwa ushahidi wa quran tukufu, lakini kwa leo kwa kifupi majibu ya maswali yako ndiyo hayoo.

    Mwisho najua wakiristu mnachukia saana!Lakini sisi waislamu lazima tuseme ukweli hatujali mnaumia kiasi gani lengo tunataka tuwaepushe na moto wa jehannam siku hiyo ya kiama msije mkasema hamkuambiwa.

    Wwahaadha ssalaam!
    Wabillah tawfiq!

    Like

    • alfa says:

      alph don killa baibe!nakiandaa kile kitab uckonde,ila nataka kukushaur muendelee kumuenz jamaa yenu hyo a.k.a muhalfu,lakni nahuzunika kwamb hamna hoja zaid ya pumba tu,kwanz mmemtosa kiongoz wenu,kama hamjamtosa nataka kuckia cku moja mmeanz ubakaj tena,oa mtoto wa miaka sita muingilie afkishapo 8 yearz,imagne anafanyiwa mdogo sa hzi,tena aolewe na kijana ka mimi lm ninteen year co abov 35,hvi utakubal wewe unayejifany unamuenz na kumtetea hata kwa uongo huyo jamaa,wanigeria waislam et wanaomb umr wa kuolewa bint usiwe 18 kisa iman yao inaruhusu ndoa za miaka sita na ukatil kwa watoto wa miaka 8,kumuingilia mtoto wa miaka 8 ni ubakaj,wewe mungu atakujalia watoto,mtoto wako afike miaka 6 m2 akuambie anamuoa lakn miaka nane kama kawa,uko tayar kumuenz kiongoz wako kwa hlo.injil zote zinazungumzia uokovu wa yesu kuran ni janja ya shetan.blinblan!!!

      Like

  101. Mhina says:

    Bwana Yohana, kama uliruka ukuta na kwenda upande wa pili, basi imekula kwako, maana hata ukipinga vipi, haitawezekana tena kwamba, bwana yesu asiwe” KRISTO”…..MASIYA MPAKWA MAFUTA WA MUNGU AMBAE NI MKOMBOZI WA WATU WOTE. Hata ukitafsiri kwamba sijui ‘MESIH/PAKA/PANGUSA/…..hayo yote kamwe hayawezi kumuondoa bwana yesu mahali hapo halafu eti akae mtume wenu mhamad!!…Mimi nilikuuliza hivi: KAMA NI KWELI JINA LA WAKRISTO NI JINA LA KIPAGANI LISILOAFAA KUTUMIWA KWA IMANI YA KWELI MBELE ZA MUNGU, MBONA MTUME WENU MHAMAD ALILIBARIKI JINA HILO KWA KUSEMA KUWA WATU HAO WANAOJIITA WAKRISTO NI WAAMINIO WA KWELI MBELE ZA MUNGU??!!….ukaanza bla..bla..bla, ambazo, zote zilishindwa kutoa utetezi kamili.Wewe mwenyewe ilikupasa kujiuliza kuwa, mtume wako, angewezaje kulisifu jina la kipagani halafu eti aseme: HAO WANAOJIITA WAPAGANI NI WAAMINIO WA KWELI MBELE ZA MUNGU!!!!!….Basi kama ni hivyo kweli…nayeye alikua ni MPAGANI.Lakini ili nikusaidie ndugu yangu ni kwamba, biblia ilimuweka wazi mpakwa mafuta huyu hata kabla ya kuzaliwa kwa huyo paulo mnaemsingizia, kwa kusema: UMEIPENDA HAKI UMEICHUKIA DHULUMA.KWA HIYO MUNGU, MUNGU WAKO, AMEKUPAKA MAFUTA, MAFUTA YA FURAHA KULIKO WENZAKO.Soma(zaburi 45:7)…Nae Paulo alipokuwa akihubiri injili, ilikuthibitisha kuwa alikuwa akimhubiri bwana yesu ambae ndie masiya yuleyule wa biblia alinukuu maneno yaleyale ya(zaburi 45:7)…thibitisha katika (ebrania 1:9).Istoshe, katika biblia takatifu hakuna hata mahali pamoja ambapo mtume paulo kafundisha mambo ya sijue mungu wa jua au miungu saba au sijui kristosis.LAHASHA!!…Bali yeye wakati wote katika injili yake alikuwa akisisitiza mambo ya Mungu mmoja/bwana yesu na imani moja. Kwahiyo basi, Elimu mpya ambayo ndugu mhamad anataka kutuletea ni mawazo ya kidunia kutoka kwenye mitandao ya internet ya watu waliokosa imani na kukosa hoja za kimaandiko.kama ni kweli ndugu mhamad, wewe ni mtu wa Mungu na Muislamu wa kweli kwanini basi umeamua kuacha hoja za vitabu tunavyo viamini, halafu ukaamua kukimbilia mambo ya uongo ya kidunia, ambayo hayamo katika kitabu chako cha imani wala biblia yangu ya imani yangu?!!…je hizo sio dalili za mtu alieshindwa!!!…hebu nionyeshe ushahidi wa kimaandiko wa quran yako au biblia yangu kuhusu injili ya paulo ya Mungu jua au Mungu saba au tv joshua kuwa ni nabii wa wakristo nk nk nk..!!.Umetoa wapi maelezo hayo, kwenye biblia au quran,hebu tupe maandiko yanayoweza kuthibithsha maneno yako!!.Siku zote nimekuwa nikisisitiza kwamba ni makosa makubwa mno kuchanganya neno la Mungu na siasa za dunia.Kwa hiyo ndugu. Mhamad kwetu sisi wakristo hatuwezi wala haturusiwi tena ni kosa kubwa mno kuchanganya neno la Mungu na maneno ya wanadamu ili kutafuta ushahidi wa kujitetea badala ya kutumia kitabu chako cha imani.Ushahidi na utetezi wa neno la Mungu hautafutwi kwenye vitabu vya kihistora kwenye mitandao bali neno la Mungu lenyewe ndio linalohitajika kujitetea kutoka kwenye hicho kitabu chake!!.UMESOMA WAPI WEWE MAMBO YA DINI? MBONA KAMA HUJIELEWI??….Yaani unajisahau na kupiga stori mpaka kwenye mambo ya Mumgu!!!!….Sehemu moja katika maelezo yako, ulisisitiza kwa kusema: STORI NI NDEFU UKITAKA MKASA KAMILI NIAMBIE NITAKUJULISHA KWANI NAJUA HUFAHAMU LOLOTE!!!!!….Hapo katika hayo maneno yako mimi ninakukubalia kwa 100% kwamba kama mwenzangu unaacha mijadala ya vitabu vyetu vya dini halafu eti unaanza kupiga stori za uongo za kidunia…NIKWELI NDUGU UTANISHINDA KWA SABABU MIMI SINA NINACHO JUA KATIKA IMANI YANGU ZAIDI YA KUIAMINI BIBLIA PEKEE. Halafu, hiyo tabia ya nyinyi waislamu kumnukuu kwa mkato mkato mtume paulo katika injili anazoandika na kujenga hoja za uongo hivi mtaacha lini tabia hiyo? Yaani ni vichekesho vitupu!!.Kwa mtu aliekwenda shule akikagua hayo mambo uliyomzushia mtume paulo kwa kusoma biblia kutoka mwanzo wa hoja mpaka chini…ataishia kucheka na kushangaa!!!.YOTE NI UONGO MTUPU.Pia lazima uelewe ndugu kuwa manabii wa mwanzo kabisa kama wakina Nuhu,Ibrahimu na wengineo wale walikuwa ni wajumbe wa Mungu ambao hawakutumia vitabu bali Mungu aliwasiliana nao moja kwa moja kupitia malaika zake….ndipo nao wakatuandikia maneno yale ya Mungu kuwa ni msingi wa imani yetu, yaani nilazima nasisi tutumie maneno yake ya kuwa ni msingi wa kuendelezwa na vizazi vyote vijavyo…ndio maana sisi wakristo tunafuata na kutunza maneno yale ya awali ya manabii kuwa ni msingi wetu wa imani ambayo chanzo chake ni Mungu mwenyewe.Pia kwa njia hiyo ndipo tunapoziona nafasi za wakina Nuhu,Ezekiel,Ibrahimu kwa sisi wakristo kuwa na vitabu vyao na kuvifuata….lakini tunaona katika dini ya kiislamu mambo kuwa ni tofauti kabisa.Yaani vitabu vyote vya Mungu kupitia manabii wake, havifuatwi wala quruani nayo haina….badala yake tunaambiwa ni mtu mmoja tu anapewa nafasi ya kuleta neno la Mungu kwa watu wote huku maneno yote ya nyuma ya Mungu kupitia manabii wake tunaambiwa hayapo wala sio yakwetu!!!.Dini gani sasa hiyo isiokuwa na misingi ya neno la mungu la asili!!….istoshe, kuwa mfano wa manabii sio kwa njia ya mdomo na kutoa vijisifa sifa tu,bali ni kufuata vitabu vyao vyote lakini tunaona kuwa waislamu hawanavyo kabisa kabisa hivyo vitabu vya hao manabii.Sasa kwa akili za mtu aliekwenda shule, inawezekanaje kupata tabia na mfano wa mtu ambae huna kitabu cha maelezo yake yanayomuelezea mtu yule!!!!.UONGO MTUPU.Ndio maana hata sheria za kweli za Mungu kupitia nabii Musa hazifanani na zile za uongo za kiislamu ijapokuwa wao wanasema sheria zao zinafanana, ukiangalia hata utekelezaji wake ni tofauti kabisa.Mungu wa waislamu katika sheria zake anasamehe dhambi za waumini wake bweleleeee!!…wakati sheria za Mungu kupitia nabii Musa imasema kuwa pasipokumwagadamu hakuna ondoleo la dhambi.Hizo ni sheria tofauti na dini tofauti kabisa!!!.kilichofanana hapo ndugu mhamad ni nini hebu jiulize mwenyewe!!…kwanza huko kufanana kwake mlikudhibitisha wapi na wakati nyinyi hamna vitabu vile vya awali??!!UONGO MTUPU.Mimi niishie hapa.Mungu awaokoe kutoka gizani.

    Like

  102. alfa says:

    naitwa alpha a.k.a don kiler baibe!mwana umechemka vbaya mpendwa ktk bwana,mungu ana destur ya kuwatoa watu wak wakajaribiwe na shetani,baba wa uongo haimaanish kuwa ndo amemsamehe,mungu ni mungu wa maarifa mwana,hukumbuk amewatoa israel mara ngapi?kumbuka wana wa mungu ni mali ya mungu na shetani anajua hilo,kwa hyo mungu anavyowatoa kwa mashetani anataka wajifunze na wamjue baba yao ni nani,watambue umuhimu wa yule aliyewatafuta na kuwaokoa,hamtoi kwa malaika hata siku moja maana malaika ni watakatifu,naye shetan anajua waz ya kwamb hawa c wake hvyo huwashambulia na kuwatesa,mwisho wa watu hawa humrudia mungu wao,c rahsi mwana wa mungu aliyepigwa na ibilis kwa namna yoyote ukamkuta kwa waganga wenu huko mbagala au ameenda kutafuta uchawi wenu unaoanzia kushoto,atamrudia baba ak na kutubu ndipo afunguliwe,mfano watu wamatambiko wasipofany hvyo mambo yao huenda mrama maana miungu yao imewaacha hvyo watarud tu,ndivyo wana wa mungu walivyo,ndo mana wameitwa wana wa agano,

    Like

  103. alfa says:

    mpendwa ktk bwana pia until 2day majini ni waislam utasikia maulana,mara sheh yahya mara maimuna,na hao maskan yao ni pamoja na wahalifu,ngoja nikuambie k2 mdogo,nna kitab naanda kwa ajili yenu nyote ntawatumia kama mtakuwa ok!majini ni jesh la kuzimu na hakuna aliye mwema,nakupa ushuhuda wa kwel and if u want nijulishe nikupeleke moja ya familia za kiislam na ushahd utaupata kwa jiran zake kwa muda wako,kuna ndugu alipewa kinga na waalimu wenu,manak nyie mungu hana uwezo wowote so lazma mjiking kidogo,yule ndugu baada ya kupewa neno la mungu sahihi aliamua kuachana nayo akaisalimisha ikiwa imeandikwa lugh zenu,watumish hawakuielewa ndipo akaja kijana anayeelewa akasoma(jini makata naomba umlinde huyu anaekuva umuepushe na balaa zote mpaka atakapokwenda jehanum)hao ndo majini wazur,na kuna mwingne mshkaj wang anakabwa kinoma na lijini lake linamtaka aende mskitini,haya madude yakiwa msikitin hakuna nguvu ya mungu hvyo yanakula raha tu kumuabudu shetani,mahal ambapo mungu alie hai anaabudiwa yanakimbia.

    Like

    • Muhammad Yohana says:

      Ndugu Alfa;
      Katika wakiristu wote, ambao wanachangia humu wewe ndo point zako ni dhaifu kuliko wote, kwanza unawaaibisha kwa sababu hata kiswahili hujui, pili hujitambui, tatu hujui kupangilia hoja, nne maelezo yako hayana mwelekeo, tano hujui unachokichangia,; Kwa ujumla unawaaibisha wakiristu wenzako mnaonekana nyote mko hivyo.Kwa upande wangu sihitaji hata kujadili na wewe kwa sababu watu watajua tuko level moja, labda nitakutafutia kitoto changu kidogo cha miezi 3 ndo mtajadili kwa sababu pengine thinking capacity yenu inakaribia kulingana.

      Like

  104. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Mhina,
    Shukran zote zinamstahiki Allah Mola wa viumbe vyote, Mola ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa, Mola ambaye amemtuma Mtume wake kwa haki na akampa Quran kuwa Mwongozo katika maisha ya wanadamu.

    Ammaa baa’ad!
    SWALI; Yaani unajisahau na kupiga stori mpaka kwenye mambo ya Mumgu!!!!….Sehemu moja katika maelezo yako, ulisisitiza kwa kusema: STORI NI NDEFU UKITAKA MKASA KAMILI NIAMBIE NITAKUJULISHA KWANI NAJUA HUFAHAMU LOLOTE!!!!!

    JIBU;Ndugu Mhina, Kwanza kabisa nikuombe kitu kimoja, hebu Kabla hujaandika hoja yako tafakari kwanza vinginevyo unawapa watu faida. Hivi Ndugu Mhina, tunaposema a certain scene is a story, hivi unashindwa kuelewa what is a story!!!! Dont u know that even ur bible contains some stories??Dont you!!?For ur information about 95% of ur Bible are stories?Naomba labda nikuelimishe kwanza stori maana yake ni “maelezo ya matukio ya mambo yaliyopita”.Huwezi ukawa religous person while u know nothing about the background of ur belief , if that happen, that is what we call blindness in belief which is too bad.Hivi niliposema stori we ukajua stori maana yake ni ‘alf lela ulela!!!” no! no! my friend, we dont think that way!!!

    Tunapoyataja makanisa ya wakiristu wanaojiita “born again” utakuwa mwizi wa fadhila usipozungumzia mtu aliyeitwa Martin Luther King Sr.,so when i said that it is a story yeah! it was real a story.Hata hiyo biblia unayoitumia sa hz wewe kama sio mkatolic ambayo ina vitabu 66 ndani yake ni matokeo ya Bwana huyu otherwise you could all have been catholic christians and ur bible could probably have contained 73 books.Lakini pia, mimi nashindwa kuelewa umekwama wapi ndugu yangu kwani unapokuwa mkiristu huwezi kulikwepa neno hili kwa sababu kawaida stori ni maelezo ambayo huanza na “hapo zamani za kale”, au “hapo zamani” n.k.Kwa mtu ambaye ni msomi mzuri wa biblia atagundua kuwa maeneo mengi biblia imeanza kwa mtindo huo kwa mfano YOHANA 1:1″Hapo mwanzo kulikuwako na Neno….” hii ni stori, au biblia inapoanza hivi “Zamani za mfalme Herode” hii ni stori au ukisoma MWANZO 1:1 utakuta “Hapo mwanzo” hii ni stori kwa hili hata waandishi wa vitabu vya fasihi simulizi wanajua, kwani stori yoyote lazima ianze kwa mtindo huo.Kwa hiyo ndugu Mhina kama unanishangaa mimi kwa kukupa story ya mambo uliyokuwa huyajui kuhusu dini yako, basi jua ni ufinyu wako wa elimu ya dini yako kwani ungeanza kumshangaa mungu wako anayekupigia story kwenye kitabu chako kitakatifu.Au unataka kumaanisha kwamba na mungu wako alijisahau akakupigia stori??? Hebu naomba urudi darasani kwanza ukasome ndugu yangu,ukishindwa waite walimu wako tujadili hoja za msingi na wewe uwe mtazamaji!

    SWALI;Pia kwa njia hiyo ndipo tunapoziona nafasi za wakina Nuhu,Ezekiel,Ibrahimu kwa sisi wakristo kuwa na vitabu vyao na kuvifuata.

    JIBU; Naomba uniambie nabii Nuhu alikuandikia kitabu gani ambacho unakifuata wewe mkiristu? otherwise niruhusu niseme umepitiwa.

    SWALI;inawezekanaje kupata tabia na mfano wa mtu ambae huna kitabu cha maelezo yake yanayomuelezea mtu yule!!!!.UONGO MTUPU

    JIBU;Katika maswali yote uliyouliza tangu tuanze mjadala, naomba nikupongeze kwani hili ndo swali la msingi kuliko yote! Ndugu Mhina na hapo ndipo utagundua ukweli wa Mtume wetu mtukufu, kwani Allah alikuwa anamfunulia maisha ya manabii ambao mwenyewe alitaka tuwafanye mfano wa kuigwa.Allah alikuwa akimpelekea ufunuo Mtume wake Mtukufu kupitia kwa Malaika Jibril(Gabriel), Allah alikuwa akimtolea mifano ya maisha mbalimbali ya manabii waliomtangulia, alikuwa akimwambia shida walizopata manabii waliomtangulia akina Musa, Issa, Yohana,Zakaria n.k hivyo kumtaka awe na subira kwa yote yatakayomkuta kwani hata manabii waliomtangulia wamepata shida.Lakini Pia Allah katika quran katupa mifano ya watu walioishi kabla yetu ambao Allah aliwatumia Mitume wawaonye na wao wakawakataa kwa kufanya kiburi ,kwa hiyo Allah ameeleza madhara yaliyowapata kwa mfano watu wa Nuhu kisa chao Allah amekieleza vizuri kabisa ndani ya Quran, kisa cha Nabii Nuhu Allah amekielezea vizuri kabisa kwa ufasaha na madhara yaliyowapata wale wanaume waliokuwa wakiwaendea wanaume wenzao na kuwaacha wanawake, pia Allah ameekielezea sana kisa cha Nabii Musa kwa urefu kabisa jinsi Firauni na watu wake walivyokuwa wamezidi kwa uovu na Allah akawagharikisha kwenye Bahari.Kisa cha nabii Ibrahim na watu wake Allah amekielezea kwa ufasaha kabisa.Kisa cha nabii Issa Allah amemfunulia Mtume wake kwa uhakika kabisa na kusaidia kumuondolea nabii Issa kashfa wanazompa wakiristu na Baadhi ya mayahudi wanaodai eti Nabii Issa kalaaniwa kwa ajili ya dhambi zao, pia hao wanaomfanya Mungu Allah amewakemea vikali mno kupitia ufunuo wake kwa Mtume wake mtukufu.Hayo mambo yote Allah alikuwa akimueleza mtume wake mtukufu kupitia malaika Jibril.

    Ndugu Mhina na hiyo ndiyo maana ya kuwa Mtume wa Allah, Unapokuwa mtume hutakiwi kwenda kwa watu kuuliza mambo yalivyokuwa hapana! Mungu mwenyewe ndiye anayetakiwa kukujulisha hata kama hujasoma kitabu chochote.Na hii ni tofauti kidogo na Biblia kwani katika biblia tumeona jinsi gani mikono ya waandishi ilivyokichezea kitabu kwa asilimia kubwa kwani hata Luka mwenyewe anakiri hilo katika LUKA 1:1-4, na pia tumeona ni jinsi gani Martin Luther alivyotoa siri za kanisa nyingi pale alipogundua kuwa baadhi ya vitabu ni kazi ya mikono ya wanadamu na wala siyo ufunuo,Kumbuka huyu alikuwa Askofu kule Vatican kwa Papa kabisa katika kanisa la st.Peter ambalo mwasisi wake ni mwanafunzi wa Yesu, lakini pia hata hao waliofasiri biblia pia wamekiri kwenye dibaji kuwa majina mengine ambayo yapo kwenye biblia walilazimika kuyaongeza, kitu ambacho tafsiri yake ni kukosoa mapungufu ambayo waliona pengine mungu wao anayo kwa kusahau baadhi ya majina hivyo wao ikabidi wayaongeze, Lakini pia kuna biblia za kingereza zinazoitwa king james version, kuna King James Version I na King James Version II, Ukisoma King James Version I Utagundua kuwa JOHN 1:1 Haimo waliitoa kwa sababu walijua chanzo cha msitari huo kuwa siyo ufunuo bali yalikuwa ni maneno ya mwana falsafa mmoja aliyeitwa Philos maneno hayo aliyaongea tu akiwa anajibu swali la mwanawe mdogo aliyemuuliza kuhusu mungu, hivyo akaamua kumpa falsafa hiyo, mwandishi wa kitabu Cha Yohana akacopy na ku-paste kama lilivyo.Katika King James Version II walilazimika kuurudisha msitari huo baada ya mjadala mkali uliofanyika huko Ujerumani.

    SWALI;kwanza huko kufanana kwake mlikudhibitisha wapi na wakati nyinyi hamna vitabu vile vya awali??!!UONGO MTUPU

    JIBU; Ndugu Mhina, hata ili swali linafuata kwa ubora katika mlolongo wa maswali yako, Hakika ungekuwa unauliza maswali kama haya tokea mwanzo ungeshautambua uislam kwa uwezo wa Allah,Ndugu Mhina hapo ndipo utagundua ukweli wa Mtume, Kwanza kabisa Mtume alipohamia Madinna alipokimbilia kutafuta hifadhi baada ya kutaka kuuwawa na mabedui wa Mji aliozaliwa wa Makka, alikuta mayahudi na wakiristo ndiyo watawala wa mji ule, Mtume alipoanza kufundisha kwa muda wa miaka mitano karibia mji mzima wakiristu wote walisilimu na baadhi ya mayahudi, kwa hiyo karibia 95% ya mji ule wakawa waislamu hivyo Mtume akatangaza dola ya Kiislam, hivyo Madina ukawa mji wa kwanza Duniani kuishi chini ya sheria za kiislam.Kesi zote zilikuwa zinahukumiwa kwa sheria za kiislamu. Mayahudi wengi walimkataa Mtume lakini walikuwa wanalazimika kuleta kesi zao kwa Mtume Mtukufu kwa sababu ndiye aliyekuwa mtawala kwa kipindi hicho,Walipomletea kesi mayahudi mara nyingi Mtume alikuwa akiwaambia kafunue torati msitari flani flani, hapo mtakuta hukumu ya kosa hilo, walikuwa wakikuta ni hivyo kweli. kesi za namna hiyo ziko nyingi mno hasa ukisoma hadithi za Mtume.Jambo hilo lilikuwa likiwashangaza sana Mayahudi kwani Mtume alikuwa anajulikana kuwa hajui kusoma, lakini alikuwa akijuaje hukumu ziizo ndani ya Kitabu chao tena hadi anajua msitari na sura, wakaanza kumuita mchawi na wengine wakasema anadanganya anajifanya hajui kusoma kumbe anajua n.k.

    Wakiristu wengi waliweza kutambua kuwa mtu huyu alikuwa anapata ufunuo kutoka kwa Mungu, hasa waliokuwa Mapadre na wasomi wakubwa wa torati,hivyo wengi wlisilimu,Hapa chini nimekuwekea baadhi ya matukio ambayo Allah alimpa ufunuo mtume walipomjia Mayahudi na kesi zao;
    QURAN SURA YA TANO(AL-MAIDA)
    42. Hao ni wasikilizaji kwa ajili ya kusema uwongo, na ni walaji mno vya haramu!
    Basi wakikujia, wahukumu baina yao au jipuuze nao. Na ukijipuuza nao, basi wao
    hawatakudhuru kitu. Na ukiwahukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika
    Mwenyezi Mungu anawapenda waadilifu.

    43. Na huwaje wakufanye wewe hakimu nao wanayo Taurati yenye hukumu za Mwenyezi
    Mungu? Kisha baada ya hayo wanageuka. Na hao si wenye kuamini.

    Mayahudi wakajenga tabia ya kuwa wanamuuliza maswali, mbalimbali kuhusu torati yao. Pale pale Allah alikuwa akimshushia ufunuo Mtume wake Mtukufu hebu soma ufunuo huu ndani ya Quran;
    QURAN SURA YA TATU(AL-IMRAN)
    93. Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israili isipo kuwa alicho jizuilia
    Israili mwenyewe kabla haijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome
    ikiwa nyinyi ni wasema kweli.
    94. Na wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu baada ya hayo, basi hao ndio
    madhaalimu.
    95. Sema: Mwenyezi Mungu amesema kweli. Basi fuateni mila ya Ibrahim mwongofu,
    wala hakuwa miongoni mwa washirikina.

    Kama unavyoona hapo katika aya ya 93 Allah anamuambia Mtume aseme kuwaambia wana wa israeli waliokuwa wamekuja kuhojiana naye kuhusu masuala ya vyakula akawaambia Leteni taurati muisome mtakuta humo vyakula vilivyo halalishwa na vyakula vilivyoharamishwa.Kupitia uwezo mkubwa wa Mtume wa kuyaeleza mambo ambayo alikuwa hajayasoma popote Wakiristu wengi walisilimu na wakawa vipenzi vyake, Wakiristu waliokuwa Syria(Sham) walipopata habari kuwa Madinna kuna mtu anayedai kuwa yeye ni mtume wa Mungu walifunga safari mpaka Madinna makundi kwa makundi, walifanya mijadala sana na Mtume na Mtume alikuwa akiwakaribisha kwa wema kabisa, tena kuna kipindi aliwapa msikiti wakafanya ibada zao kwa siku tatu na walipomaliza mjadala wengi wao hawakutaka kurudi Syria, walijitoa waambatane na Mtume kila mahali, wengine walirudi na Mtume akawapa walimu wa Quran, hata wakiristu wa Yemen ilikuwa hivyo hivyo mpaka Mtume anafariki nchi nyingi za wakiristu walikuwa wameshasilimu kwa sababu maswali yao yalikuwa yakijibiwa kwa ufasaha kabisa.

    Kwa chuki mayahudi na warabu wa nyumbani alikozaliwa mji wa Makka wakawa wanamwita mchawi lakini Allah akawa anajibu hoja zao katika funuo mbalimbali;Hebu kwa mfano soma hapa chini;
    QURAN SURA YUSUF(10)
    2. Je! Imekuwa ajabu kwa watu kwamba tumemfunulia mmoja wao kuwa: Waonye watu,
    na wabashirie wale walio amini ya kuwa watakuwa na cheo cha juu kwa Mola wao
    Mlezi? Wakasema makafiri: Hakika huyu ni mchawi dhaahiri!

    SURA YA 38;
    4. Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri
    wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
    5. Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.

    Basi Allah alivyoona wanamfanyia hivyo akamshushia aya za kumfariji na matukano yao pale alipomwambia kuwa asisikitike kwani hata mitume waliotangulia waliitwa wachawi kwa sababu ya miujiza waliokuwa wakiifanya na hiyo ni kweli kwani hata Yesu ukisoma ndani ya Biblia kuna waliomwita mchawi, Hasa alipowasomea chuo cha nabii Isaya wakasema amejuaje mambo ambayo hakufundishwa huyu;Pale alipomwambia;

    SURA 51. SURAT ADH-DHAARIYAAT
    52. Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni
    mchawi au mwendawazimu.
    53. Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
    54. Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
    55. Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

    Kwa hiyo ndugu Mhina huo ndiyo Uwezo mkubwa Allah aliomjalia Mtume wake mtukufu,ambaye alikuwa hajui kusoma, lakini anayajua yaliyoandikwa na anajua yako wapi kwa Elimu aliyopewa na ALLAH.Lakini watu waliokuwa na elimu na watawala wakamjengea chuki lakini wapi Hawakufanikiwa, wengine wakamuita mtunga mashairi kwa sabab Quran yote kuanzia mwanzo mpaka mwisho imepangwa katika mfumo wa vina na mizani kama mashairi, Wengine wakamuita mganga wa kienyeji;
    Lakini Allah akawapa aya kuwakataza wasimuite hivyo;

    SURA 52. SURAT ATT’UR
    29. Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala
    mwendawazimu.
    30. Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari

    SURA 69. SURAT AL-H’AAQQAH
    40. Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
    41. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
    42. Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
    43. Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote

    Ndugu Mhina, wapo walioendelea kudhani Mtume Mtukufu wa Allah ameitunga hii QURAN lakini Allah alikuwa anawajibu kupitia ufunuo kwa kupitia kwa malaika wake;

    SURA 52. SURAT ATT’UR
    32. Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
    33. Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
    34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
    35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

    Mwisho, sisi waislam hatumlazimishi mtu kuutambua ukweli, ila Allah akuongoze uuone ukweli ndugu yangu,kwani hakika moto wa jahannamu unawasubiria wale ambao wamepokea habari za mtume lakini wamefanya kiburi;Nafikiri wewe mwenyewe ni shahidi jinsi ulivyopata ugumu kuzijibu hoja zangu na pengine ukalazimika kudanganya kitu ambacho siyo kizuri hasa unapokuwa unamwambia mtu ili aitambue imani yako;Na maswali mengi wewe mwenyewe umekuwa shahidi jinsi ulivyokosa majibu yake, kwa hiyo ndugu yangu Mhina, lengo siyo nani kashinda nani kashindwa hapana, lengo ni kueleza ukweli kwani uongo hauwezi kusaidia kitu kuifanya imani ionekane kuwa ya kweli, kama imani ni ya kweli haitaji mtu kutumia nguvu nyingi kuelezea ukweli wake.Wengi tulikuwa wabishi hata zaidi yako lakini Allah mwenyewe ndiye anayejua kilichotokea mpaka maisha yetu yakabadilika na sa hizi tunaifanya kazi yake kwa uwezo wake, kwa hiyo ndugu yangu nakushauri isome vizuri imani yako na uislam usome ili upate kuutafuta ukweli zaid;

    Allah ndiye mjuzi zaidi;
    Wwahaadhaa ssalaam;

    Like

    • alfa says:

      don kil baibee!!ndugu acha kutapatapa,kinachotakiwa ni ushahid wa kimaandiko na siyo bla bla bla za vichochoroni,mi naona hujajibu hoja ya msingi,toa maandiko ya miungu saba ya paul co hadith za vichochoroni,kama hadith zipo nying,nnachotaka ni maandiko na c bla bla bla zako mjomba,kama ulivyomnukuu yohana,umetoa ktk maandiko na co hewan,halafu unasema nuhu ameandika kitab gani,umeambiwa hvi,manabii wa mwanzo walipata ufunuo kutoka kwa bwana hvyo wakatuandikia sisi,mfano( DAUD alisema,roho wa bwana alinena ndani yangu),hao ndio waliotuandikia habar za mungu,pia ndugu yangu,yesu alikuja kutimiza maandiko ambayo alikwisha kutabiriwa na c kama niny mnavyodai alishushiwa kitab kipya,hvyo bsi ufunuo ule waliopewa manabii wa kale ndio aliokuja kuutimiliza,kwa hiyo huo ufunuo mpya wa muhammad c wa mungu alie hai ni wa mungu wenu nyie(allah).kama ufunuo wote ulishakamilika huo ufunuo mpya umetoka wapi.mmeishiwa sera bandugu!

      Like

    • alfa says:

      coz ukitaka hadith ziko kibao,hujui kuna baadh ya vitabu vya kiislam vimezuiliwa visitoke?ndo mana nakuambia hadith za nini twend kimaandiko ndugu,jibu hoja ipasavyo,nadhan umeishiwa sera umebakiza ubish wa jadi kijana.

      Like

  105. Mhina says:

    Ndugu.Mhammad, Mimi nasikitika ya kwamba, elimu yako uliyokuwa nayo, bado haikusaidii kuwa Mwalimu mzuri wa mambo ya dini zaidi ya kuwa mpotoshaji mkubwa!!…Na kama wewe sio mpotoshaji, hebu tuonyeshe kimaandiko stori za biblia zinazohusu elimu ya Mtume paulo kuhusu Mungu jua, Miungu saba pamoja na yule mtume wa tv joshua ya kwamba ni baadhi ya mitume waliofuata kwa wakristo baada ya bwana yesu.Kabla hatujaendelea, hebu niweke sawa ili namimi mkristo niweze kuijua biblia yangu vizuri kama unavyoijua wewe….kwa kuwa watu wote wenye dini na akili timamu, wanafahamu waziwazi kwamba, habari za kimaandiko za vitabu vya dini, kamwe hazichanganywi na habari au stori zinazotoka katika vitabu vya kidunia.Hivi ni vitu viwili tofauti kabisa ,ndio maana kuna mambo ya kidunia yanayojibiwa kidunia na kuna Mambo ya Mungu yanayojibiwa ki Mungu kwa kutumia vitabu vya Mungu pekee.Na kama kusingekuwa na utaratibu huu…basi pia kusingekuwa na umuhimu wa kuwa na vitabu vya dini kwa kuwa, tungeweza kuchanganya stori zote za vitabu vya dunia halafu tukavifanya kuwa ni stori zetu za kidini katika kujitafutia uhakika wa majibu yetu mbalimbali!!!.Ndugu.Mhd, Mimi nilichojifunza kwako ni wewe kuwa mwepesi wa kutafuta Makosa ya mwengine lakini makosa yako mwenyewe huwa huyaoni….SASA HEBU NA WEWE NIONYESHE KIMAANDIKO HOJA ULIZOMTUNGIA MTUME PAULO KATIKA BIBLIA UNIONYESHE KUWA ZIKO MAHALA GANI…PIA UNIELEZE KAMA KUNA UHALALI WA KUJIBU HOJA ZA KIDINI KWA KUTUMIA STORI ZA VITABU AMBAVYO SIO VYA DINI ZETU.Halafu pia ukaniuliza hivi: naomba uniambie nabii Nuhu alikuandikia kitabu gani ambacho unakifuata wewe mkristo.JIBU: Katika historia za Manabii wote, Mungu amejifunua zaidi mno pasipo mipaka wala kipimo kwa manabii wakuu wawili ambao ni Nabii Musa na Bwana yesu.Ili nikujibu swali lako, Tutamuongelea Nabii Musa ambaye Mungu kwa upande wa agano la kale, alimuongoza kiroho na kumpa jukumu kubwa zaidi la kuandika vile vitabu vitano vya mwanzo ambavyo ni mwanzo,kutoka,walawi,hesabu na kumbukumbu la torati.Musa alipozaliwa na kuwa mtu mzima hakuviandika vitabu vile kwa hali za kawaida bali aliweza kuviandika kwa uweza wa kiroho na kiungu ndio maana aliweza kutambua yaliyopita,yaliopo na yajayo, yaani habari za vitabu na mambo ya Adamu,Nuhu pamoja na yote yaliyotokea kabla ya hapo akiongozwa na Mungu mwenyewe katika kuyajua yote hayo.Wakatifulani Mungu alikuwa anampa nabii Musa uwezo wa kiungu kabisa kabisa…Mungu alimwambia Musa hivi: ANGALIA NIMEKUFANYA WEWE KUWA KAMA MUNGU MBELE YA FARAO.Soma(kutoka 4:10)…..Musa akamwambia Bwana ee Bwana, Mimi si msemaji tokea zamani wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako, Maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.Bwana akamwambia: NI NANI ALIYEKIFANYA KICHWA CHA MWANAADAMU? AU NI NANI AFANYAYE MTU KUWA BUBU AU KIZIWI AU MWENYE KUONA AU KUWA KIPOFU?….SI MIMI BWANA? BASI SASA ENENDA, NAMI NITAKUWA PAMOJA NA KINYWA CHAKO, NA KUKUFUNDISHA UTAKALOLINENA.Soma(kutoka 4:10-12).Hapo tumeona jinsi nabii Musa alivyokuwa akitumika kwa kiasi kikubwa mno mbele za Mungu na kuweza kuwa msingi wa vitabu vile vya mwanzo vikiwemo vya maelezo ya Adamu, Nuhu nk.Ndipo sisi wakristo tunapopata misingi zaidi ya manabii kuanzia hapo na kwenda mbele….lakini sio eti kusema HAVITUMIKI TENA KAMA WANAVYOFANYA WAISLAMU!!….,….Mwisho ndugu.Mhmd.ni kwamba, katika maelezo yako huko juu, umeonyesha jinsi Mtume wenu mhamad alivyopata ufunuo mwingi wa manabii wa nyuma kama wakina Musa,Daudi pamoja na bwana yesu…yaani mpaka na yeye kwa kuona umuhimu wa elimu hizo, akawaandikia elimu hizo za manabii na nyinyi waislamu katika kitabu chenu cha imani yaani quran ambapo humo kuna injili,torati na zaburi na pia hata quruani yenyewe inakuunga mkono katika maelezo yako yote uliotupatia kwa kusema: MUNGU AMESHAFUNUA TORATI NA INJILI KWA AJILI YA KUWAONGOZA WANADAMU NA KWA AJILI YA KUTOFAUTISHA KATI YA JEMA NA BAYA.(Al-imran 3:2-3).Pia soma(al-quran 3:3). Hapo ndugu.Mhd,Tumeona wazi kwamba wewe maelezo yako huko juu ukilinganisha na kitabu chako cha imani yaani quran, tunaona kwamba uko sahihi kabisa….SASA NDUGU NAOMBA UNIAMBIE SABABU ZA WEWE NA WAISLAMU WENZAKO WOTE DUNIANI ZA KUSEMA KWAMBA INJILI, TORATI NA ZABURI PAMOJA NA MITUME WAKE AKIWEMO BWANA YESU NI KWA AJILI YA ISRAEL PEKEE…..Wakati hapo, wewe na quran mmethibitisha kwamba hata waislamu wanafaidika mno mno katika vitabu hivyo!!!!!!!.Ubarikiwe ndugu.

    Like

  106. Mhina says:

    halafu ndugu.mhamad.ulidai kwamba nilikwepa kujibu hoja zako….hizo hoja za kitoto za kumsingizia mambo ya ungo mimi naona sikuwa na haja ya kuzijibu kwa sababu kwa mtu aliekwenda shule akitaka ajue uongo ulioandika basi ataanza kuyasoma maandiko hayo ya paulo kuanzia juu mpaka chini na kamwe sio kama unavyo mnukuu wewe kwa mkatomkato alafu unamzushia uongo!!.Pia ulidai kuwa niliandika uongo sasa hebu kama ni kweli nionyeshe huo uongo wangu mahali popote nilipoandika ili niweke mambo sawa.

    Like

  107. Mhina says:

    NDUG.MHAMAD KWAKUWA UNACHELEWA SANA KUNIJIBU KWA SABABU YA KUISHIWA MAJIBU PAMOJA NA HOJA ZA MAANA ZA KIMAANDIKO,…..BASI MJADALA WETU NAKUOMBA UISHIE HAPA ILI TUWAPE NAFASI WENGINE KUCHANGIA MAWAZO YAO.HATA HIVYO NIKUSHUKURU SANA KWA KUWA TUMEBADILISHANA MAWAZO VIZURI NA KWA AMANI. MIMI NAAMINI HAKUNA MSHINDI KATI YETU BALI WASHINDI WATAKUWA WAFUATILIAJI KATIKA KUUJUA UKWELI WA MAMBO ULIPO. UBARIKIWI.

    Like

  108. Kaka Mdachi says:

    Nimeipenda sana Wakristo wenzangu, endeleeni kutupakulia mavitu ili tuzidi kujiamini zaidi.

    Like

  109. ndugu kwa akil yako hv jua hutuama kwenye maji machafu?sasa hyo ni quran imesema hvyo,nao hudai jajmaa anaiweza mpaka scienc,utumbo kibao ntakupa nkikaa poa,hyo ndo sayans wanayomsifia hyo jamaa anayejifany mtume. says:

    quran inadai jua hutuama kwenye maji machafu,kitab cha allah vi2ko kibao,ntakupa mistar yake ngoja n2lie.

    Like

  110. Hassan says:

    sija ona hoja ya kisomi hapa

    Like

  111. Rich says:

    Sizitaki mbichi hizi !!.

    Like

  112. Rich says:

    ndugu waislamu hebu nisaidieni hili: mnasema kwamba manabii wa zamani wa mungu walikuwa waislamu wakitumia biblia yaani vitabu vyake ambavyo ni zaburi,torati na injili…..sasa mpaka hapo tu, hamuoni kuwa mtume mhamad amewatoa katika njia ya asili ya kweli, yaani biblia halafu akawaletea njia na dini yake mpya inayokataa vitabu hivyo vya asili vya Mungu eti akidai kuwa vitabu hivyo ni vya wale waislamu wa mwanzo tu(manabii au israel). Pia kama mtajitetea kwa kusema kuwa neno la Mungu ni lilelile yaani quran ni sawa na torati,zaburi na injili(biblia) ila majina ya vitabu ndiyo tofauti, kama alivyojitetea bwn. Mhamad yhn hapo juu kidogo….. :Nivipi sasa waislamu waseme kuwa ujumbe wa torati,injili na zaburi ni kwa ajili ya manabii waislamu wale wa mwanzo tu(israel)? Hivi hiyo njia mpya ya mhamad ktk quran imeficha nini au imeleta nini jipya ili kutengua ile njia ya asili ya Mungu ambayo manabii wote wa mwanzo na sisi wa sasa inatubidi tuitumie nikimaanisha torati,zaburi na injili ambavyo ni vitabu vya BIBLIA??!.Halafu mbona kunatofauti kubwa mno kati ya mafundisho ya Mhamad ktk quran na mafundisho halisi ya manabii ktk torati,zaburi na injili? .Hebu mwalimu wa kweli wa kiislamu ajaribu kunisaidia kwa lengo jema tu.Amani iwe juu yenu watu wa Mungu.Asanteni.

    Like

    • alfa says:

      kusoma robo mstari ili kupotosha maana,kutunga yasiyokuwepo na kudai yameandikwa,c unajua wakristo wachanga hawajui kitu,ni kuwapotosha tu,si ndo pundamwitu a.k.a wapinga kristo,tunamkubali israel na wale watoto kumi na wawil ambao ni taifa la israel ila tunawachukia waisrael,usipotuelewa kivyako,kuanzia muhammad isaka si mrith wa hak wala hana ahad ya kanaani,tunapinga ahad ya mungu kwa ibrahm,hakuna cha uzao wake kuish kanaani,tutaendelea kushndana na mungu wa israel ingawa mungu wetu haeleweki,mtakoma tu!

      Like

    • Shafii says:

      HOJA YAKO:”ndugu waislamu hebu nisaidieni hili: mnasema kwamba manabii wa zamani wa mungu walikuwa waislamu wakitumia biblia……..”

      JIIBU LA HOJA:Hebu naomba unukuu sehemu ambako muislam yeyote kasema manabii wa zamani walitumia bibilia, mbona unakurupuka kijana?! Hakuna nabii wa kweli hata mmoja aliyetumia biblia, bali biblia imetengenezwa tu na watu wasio mananabii, kama una ushahidi wowote kwamba kuna nabii hata mmoja alitumia biblia naomba utupe pengine tutaelimika zaidi. Mungu aliwapa manabii Zaburi, torah, injil na Quran tukuf basi, hakuna nabii hata mmoja aliyepewa biblia bhana.

      HOJA YAKO:hamuoni kuwa mtume mhamad amewatoa katika njia ya asili ya kweli, yaani biblia halafu akawaletea njia na dini yake mpya inayokataa vitabu hivyo vya asili vya Mungu

      JIBU LA HOJA;Kama ni hivyo basi hata nyie Yesu aliwatoa katika njia ya asili ya mwanzo pale alipopinga maneno yaliyo kwenye vitabu vya torat waziazi na kuwaletea njia mpya.
      KWA MFANO; Torat inasema jino kwa jino lakini Yesu alisema mkipigwa kofi l a kushoto geuza upigwe na kulia. je hamuoni kuwa alikiuka maneno ya torarati na kuyapinga waziwazi? hivyo hastahili kuitwa nabii na mtume au mkombozi wa kweli!

      KKW
      kWA

      Like

    • Shafii says:

      HOJA YAKO:”ndugu waislamu hebu nisaidieni hili: mnasema kwamba manabii wa zamani wa mungu walikuwa waislamu wakitumia biblia……..”

      JIIBU LA HOJA:Hebu naomba unukuu sehemu ambako muislam yeyote kasema manabii wa zamani walitumia bibilia, mbona unakurupuka kijana?! Hakuna nabii wa kweli hata mmoja aliyetumia biblia, bali biblia imetengenezwa tu na watu wasio mananabii, kama una ushahidi wowote kwamba kuna nabii hata mmoja alitumia biblia naomba utupe pengine tutaelimika zaidi. Mungu aliwapa manabii Zaburi, torah, injil na Quran tukuf basi, hakuna nabii hata mmoja aliyepewa biblia bhana.

      HOJA YAKO:hamuoni kuwa mtume mhamad amewatoa katika njia ya asili ya kweli, yaani biblia halafu akawaletea njia na dini yake mpya inayokataa vitabu hivyo vya asili vya Mungu

      JIBU LA HOJA;Kama ni hivyo basi hata nyie Yesu aliwatoa katika njia ya asili ya mwanzo pale alipopinga maneno yaliyo kwenye vitabu vya torat waziazi na kuwaletea njia mpya.
      KWA MFANO; Torat inasema jino kwa jino lakini Yesu alisema mkipigwa kofi l a kushoto geuza upigwe na kulia. je hamuoni kuwa alikiuka maneno ya torarati na kuyapinga waziwazi? hivyo hastahili kuitwa nabii na mtume au mkombozi wa kweli!

      HOJA YAKO:eti (mTUME mUHAMMAD)akidai kuwa vitabu hivyo ni vya wale waislamu wa mwanzo tu(manabii au israel).
      JIBU:Hata Yesu alizikataa waziwazzi amri za taurati na kudai kuwa ni kwa ajili ya watu wa zamani, hivyo tuseme basi na yeye alikuwa muongo mkubwa? Kwa mfano pale alipoulizwa kuhusu sheria ya talaka mbona alijibu kuwa talaka walipewa amri watu wa Musa tu, je huko si kuyapinga maneno ya asili?naomba unipe mfano ni wapi mtume anapingana na amri ya vitabu vya zamani kama tulivyoona mifano ya wazi bwana Yesu wa Biblia akifanya hivyo.

      Like

      • Rich says:

        Ndugu yangu: Biblia ni neno tu, lenye maana hiyohiyo inayomaanisha mkusanyiko wa hivyo vitabu vya torati + Zaburi + Injili, kasoro quran peke yake kama ulivyojaribu kutudanganya !!. Lakini kama wewe hulitaki hili jina la biblia kwa kuogopa kuwa mkristo na kubatizwa….basi husihofu kwa hilo, nikubali kama unavyotaka kua, manabii wa zamani walitumia vitabu vya torati, zaburi na injili, ambavyo mpaka hii leo vinatumiwa na sisi wakristo kwa ajili ya muongozo wa kidini. Hivyo, swali limebaki pale pale kuwa, “WAISLAMU HAMUONI KUWA HIVYO VITABU VYA ASILI VYA KWELI, BWANA MHAMAD AMEVIKATAA NA KUWAANZISHIA NINYI WAISLAMU MUONGOZO MPYA WA UONGO?. Istoshe, kama kitabu cha quran kilikua ni kimojawapo cha vitabu hivyo vya nyuma vya manabii kama ulivyotuambia hapo juu, inawezekana vipi, na wakati quran iliandikwa miaka zaidi ya 570 , baada ya manabii wote wa nyuma kua walikwisha kufa !!, waliitumia wakati gani quran na wakati kipindi kile, hata huyo Muandishi wenu na nabii wenu Mhamad alikuwa hajazaliwa wala hajulikani kama atazaliwa mtume kama yeye?!!!!!!!….acha kujaribu kutetea mambo ambayo sio saizi yako, ndio maana alihitajika mwalimu mkubwa wa kiislamu lakini sio wewe maana wewe bado ni mchanga. Utetezi wako wa pili pia ulikuwa ni pumba tupu kwa kua, Bwana yesu alikuja kutimiza au kukamilisha kazi ya torati na manabii na kamwe yeye hakuja kurudia rudia yaleyale kama alivyofanya mtume wenu mhamad. Kwa elimu zaidi ya kile alichokifanya bwana yesu, jaribu kufuatilia zaidi mijadala iliyoendelea huko chini then utapata elimu na ufahamu zaidi. Pia kama ni kweli bwana yesu hakustahili kuitwa nabii au mtume kama ulivyotuambia hapo mwisho wa majibu yako, je, huoni kuwa maneno yako hayo na msimamo wako huo, unapingana na hata dini yako mwenyewe unayoiamini ikimuita bwana yesu kua ni nabii wa kweli wa Mungu yaani “NABII ISA??!!!!!…..tazama sasa, ulijiona mjuaji kumbe ulikuwa unazidi kukufuru, uwe makini kijana mwenzangu, bwana yesu ndiye njia pekee. Hebu tazama viroja vya nabii wako, sheria za awali zilisema ni jino kwa jino halafu yeye anarahisisha kwa kusema kuwa, wanaosamehe bila ya kuadhibu wanafanya vyema au kheri, yaani inakuwa ni kafara yao wenyewe na sio kufuata amri ya Mwenyezi Mungu,!!!!. Soma(quran sura almaida 5:45). Halafu anaendelea kubadilika hapohapo kwa kuwalaani ninyi waislamu wenyewe msiozitekeleza sheria hizo za jino kwa jino kwa kuwaambia ninyi ni “MADHALIMU” Yaani ni watu wabaya kama mapagani yasio na dini,!!!!!…..kwa kuwa ninyi mnazitetea sheria hizo lakini hatasikumoja hatuwaoni mkizifuata sheria hizo, kwa mfano: kuwapiga mawe wazinifu mpaka kufa, kuwakata mikono waizi na nk. Hebu ndugu yangu ijapokuwa sitakuwepo tena kwenye blog hii, lakini ingekuwa ni vizuri ukawapa majibu watu wote watakao pitia kwenye blog hii, ili nao wajifunze zaidi. Kazi kwako.

        Like

  113. alfa says:

    ruhusu kutetea dini kwa kusema uongo na kuzusha tukujibu rich

    Like

  114. Rich says:

    nafikiri ndugu alfa hukutenda vyema..kwa hiyo basi, ninaomba mhusika wa blog hii angefuta hayo maelezo yako pamoja na haya yakwangu ninayoyaandika hapa ili nafasi ile ibaki kwa mwalimu wa kiislamu au muislamu yeyote mwenye uelewa mzuri ili kama ndugu tujadiliane na kujifunza zaidi kwa upendo na amani ili tupate kufahamu vyema misingi haswa ya dini zetu na pale watu walipojikwaa.Ubarikiwe ndugu alfa na wafuatiliaji wote.Asanteni na amani iwe juu yenu.

    Like

  115. alfa says:

    vitab vya mwanzo vyote,zabur,injil,na torat,warith ni wakristo na ndugu zao jews,kitu ambacho quran imepindua na kudai ni makafir tena ni haki kuwauwa,mfano ktk hadith zao zinasisitiza uhalal wa chuki dhid ya wana wa ufalme,wakristo na wayahud,kwa akili za kawaida watakubali kusoma hvyo vitabu?

    Like

  116. erwin says:

    katika ulimwengu wa sasa hakuna haja ya kulumbana yupi bora na yupi kafiri.tazama wakristu wanaishi,kuoa na kuolewa na waislamu ktk jamii moja na kuishi pamoja na kugawana natumizi yote ya factors of production.
    kwa hali hio na kwa mani yangu mijadala mingi ingeangalia yafuatayo:
    kama hakuna dini je cc sote tungeishi vp?
    chanzo cha dini ni nini?
    dini ni moja tu ukristu.hapo mngetueleza ss akina yakhe historia yote ya ukristu na changamoto zake mpaka sasa kuna mfumuko wa madhehebu
    pia vivyo hivyo kwa uislam na waislam.hapo wakristu watoe changamoto na pia waislamu watoe zao.
    kama tuna dini mbili je hao wafuasi wa dini hizo mbili waishije pamoja ili kujenga jamii moja yenye amani,umoja,mapendo,uvumilivu na uhuru wa kuabudu,pamoja na kufuata misingi bora iliyojengwa juu ya imani yadini husika.

    Mwisho ni maoni yangu.napenda sana kufuatilia mijadala yenu ila kashfa na mausi sijapenda tujiheshimu tunapochangia.

    samahani km nimewakera.

    Like

  117. Rich says:

    nafikiri hoja zote zilizotolewa hapa hazihusiani na udini au thehebu la mtu bali ni jamii ya mawazo ya watu mbalimbali wakichunguza kitabu sahihi cha Mungu kinachofaa kwa muongozo wa wanadamu ndiomaana wote kwa pamoja tunajadiliana.Hebu mimi niendelee kuomba kujibiwa hiyo hoja yangu hapo juu….

    Like

    • alfa says:

      sisi tunaposhndwa kabisa mamb na mateso au ki2 chochote yesu ndiye tunayemtwika mizigo,hata uponyaj,kuinuliwa na mamb meng 2,wenzetu wanapata wap msaada,HEBU TUKACHUKUE SENSA WAGANGA NA WATABIRI WA NYOTA MBAGALA,PWANI,PAMOJA NA WALE WANAOTOKA MAHAL PENGINE KUJA DAR WATEJA WAO NI WAKINA NANI ZAIDI?TEMBELEA MBAGALA NA MAENEO MENGINE,CHUNGUZA MAENEO AMBAYO HAWA JAMAA NI WENGI CHEK RATE YAKE COMPARE NA CHRSTIAN,TUCHUNGUZANE MATENDO NA SIO MANENO,JANGA LA ULIMWENGU,HUSIFIA HATA MAMB YA AIBU KUJITETEA,UNAWEZA KUKAA MBELE ZA WA2 KUJISIFU MUNGU AMEMPENDA KIONGOZI WAKO AKIWA NA MIAKA HAMSINI KAOA SIX YEAR BABY?,HII NI SIFA KWEL YA KUITETEA,MARA KAUA WAYAHUDI 603,C MUUAJI,KUNA CHA KUTETEA HAPA,MITUME WA KRISTO WALIUAWAWA KWA AJIL YA INJIL KAMA YESU MWENYEWE,CO WALIUA NO,GUD BYE,SIRUD MPAKA NIONE NDUGU ZETU WANA HOJA YA KUNIKONVICE.JAMAA ANGEISH LEO ANGEITWA MUALIFU WA KIVITA,HATA KA NDO SIASA KWA STAA BASI,YESU ATAWALE AMAN ITAKUWEPO C MFUMO FULANI,ANGALIEN NCHI ZA WATU FULANI,NAKUPENDA KA NAFS YANGU,YA NINI MABOMU?

      Like

  118. alfa says:

    Kuna mu alinimaind kisa nilifungulia mzik gar yangu,gospal music,cku yao et ckukuu yao!kisa jina la Mungu wa Miungu,mfalme wa wafalme,Baba wa milele,mfalme wa salem{amani},YESU KRISTO,hafanani na hadith zilizotungwa za mtu mwingne ambye cye bal uongo tu na
    upotoshaji,huyu ni mwokozi na ndo tafsir ya jina lake,na co mwekundu au dume la ngamia ambaye hajui mpaka aone tena anakosea,tuacheni wayahudi tulionunua na damu ya Mwana wa Mungu aliye hai,mwache israel aongezeke yuda ndiye mwamba,bethlehemu hawi mdogo kamwe,watoto wa Mungu kwa agano la rohoni,mamb ya roho hamtayaweza mpaka roho mtakatifu wajameni,PRAISE TRINITY,I LV U MY SAVIOR,NAKUPENDA MWAMBA WANGU NA NGUVU ZANGU,JEHOVA NI SIFA ZANGU,WASTAHIL PEKE YAKO JESUS CHRIST,HALELUYAAA!.Na hili ndilo kanisa ambalo malango ya kuzimu hayataliweza,limesambaa kwa damu za watakatifu,BORN AGAIN,liv in JESUS,AMEN.Nc dayz al pipo bila dini zenu wala nini,ful lv in jesuz.

    Like

    • Shafii says:

      Ndugu alfa vip ulisema unaandaa kitabu kuhusu majini na utakiweka mtandaoni vp hakijaisha au umeogopa jinsi tunavyopindua hoja zenu zilizo dhaifu.tunaomba basi utuwekee ili waislamu wote tuelimike ndugu. mbona unashindwa kitu kidogo hicho.

      Like

  119. TEACH ME THE REAL WAY TO FOLLOW, FOR KINGDOM OF GOD!

    Like

    • Shafii says:

      QURAN SURA 61:AS-SAFFAT
      11. Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na fanyeni Juhudi katika Njia ya
      Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu. Haya ni bora kwenu, ikiwa nyinyi
      mnajua.
      12. Atakusameheni dhambi zenu, na atakutieni katika Mabustani yapitiwayo na mito
      kati yake, na maskani nzuri nzuri katika Bustani za milele. Huko ndio kufuzu
      kukubwa.
      13. Na kinginecho mkipendacho, nacho ni nu itokayo kwa Mwenyezi Mungu, na
      ushindi ulio karibu! Na wabashirieni Waumini!

      Like

  120. mhina says:

    Nimewaandikia haya katika habari za watu wale “WANAOTAKA KUWAPOTEZA”. Soma(1yohana 2:26). Ni nani aliye “MWONGO” ila ni yeye “AKATAAYE KUWA YESU NI KRISTO (AKANAYE). Huyu ndiye “MPINGA KRISTO”!!!!!! > YEYE ANAYEMKATAA BABA NA MWANA (AMKANAYE). Kila amkataaye Mwana > HANA BABA, amkubalie Mwana > ANAYE BABA PIA. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo “NA LIKAE NDANI YENU”. Ikiwa hilo mlilolisikia linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa “NDANI YA MWANA NA NDANI YA BABA” > NA HII NDIYO AHADI ALIYOTUAHIDIA, YAANI UZIMA WA MILELE. Soma(1Yohana 2:22-25)…..Ndugu wasomaji wote mliobahatika kusoma hapa, nafikiri nyinyi wote mmeona jinsi tabia za mpinga kristo hapo juu zilivyowekwa wazi na biblia takatifu, lakini lamuhimu zaidi ninalotaka nilielezee kwa wale ndugu zetu wote wenye kutatizwa na mateso na kifo cha bwana yesu pale msalabani, ni kwamba: YEHOVA Mungu wetu ni wa ajabu sana katika kazi zake, tofauti kabisa na akili zetu na mawazo yetu tunayoyawaza na kuyafikiria kibinadamu, maana akilizake”HAZICHUNGUZIKI wala maarifa yake “HAYATAFUTIKANI. Yeye aliyachagua mambo ya dunia hii, ambayo kwa hekima za kibinadamu yanaonekana ni ya kipumbavu, ili awaaibishe wale wanaojiona wanahekima, tena akachagua vitu vinavyoonekana ni dhaifu ili aviaibishe vile vyenye nguvu, halafu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, yaani vitu ambavyo havipo ili aviaibishe vile vilivyokuwepo.Mungu alifanya hayo yote kwa lengo moja tu ” ILI IMANI YETU ISIWE KATIKA HEKIMA YA WANAADAMU BALI KATIKA NGUVU ZAKE YEYE MWENYEWE.!!!!!.Soma(1wakorintho 1:27-31) pia(1korintho 2:5). Hapo ndipo pia tunamuona bwana yesu ambaye nae alisulubiwa katika udhaifu lakini anaishi kwa nguvu za Mungu huko mbinguni akituombea, ambapo na sisi wanadamu katika yeye tu dhaifu lakini tutaishi milele pamoja nae huko mbinguni kwa uwezo wa Mungu na hekima yake ileile aliyotuandalia sisi tunaomuamini na kumpokea kwa imani.Soma(2wakorintho 13:4). Hii ni kwa sababu, katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu naye alipenda kuwaokoa kwa upuzi wa lile lile neno linalohubiriwa na kukataliwa.Soma(1wakorintho 1:21)….na hapo ndipo wanapo nasika ndugu zetu wengi kutoka katika dini mbalimbali wanaposhindwa kutambua siri hii ya Mungu na hatimaye kuikataa injili ya bwana yesu na kupotezwa na shetani kwa kufuata akili na hekima zao za kidunia, na ndipo pia hapohapo neno la Mungu tunaliona likiendelea kutimiza unabii wake katika siku hizi za mwisho kabla bwana yesu hajaja kutunyakua: “NITAIHARIBU HEKIMA YAO WENYE HEKIMA NA AKILI ZAO WENYE AKILI NITAZIKATAA.Soma(1wakorintho 1:18-19) halafu ilinganishe na (Isaya 29:14). Hitimisho:Pasipo bwana yesu: HAPANA NJIA WALA IMANI YA KWELI YA WOKOVU INAYOTOKA KWA MUNGU…Ndiomaana biblia inatufundisha kuwa, imani ya kweli huja kwa neno la kristo.Soma(warumi 10:17). Hii ni kwa sababu ndani ya kristo, Mungu wetu ametuwekea hazina zake zote za HEKIMA,UTAKATIFU PAMOJA NA UKOMBOZI.Soma(1wakorintho1:30-31). Kwa hiyo ndugu,kumkataa bwana yesu na kupinga kazi ya Mungu aliyoifanya pale msalabani ni “KUSHAMBULIA SEHEMU YA UTAKATIFU WA MUMGU” na hiyo ni kazi ya shetani na wafuasi wake anaowaendesha kiroho pasipo wao wenyewe kujijua.NJOO KWA BWANA YESU,MWALIMU WA AMANI YA KWELI.Mbarikiwe.

    Like

  121. Prosper says:

    Mtakatifu Mohamedi (St. Mohamed S.A.W) sijawahi kumsikia!! Tofauti yake na Yesu ni kwamba: Mohamedi yupo kaburini kama ambavyo na babu yangu alikufa na kuzikwa, LAKINI YESU KRISTO baada ya kufa ALIFUFUKA, hayupo kaburini, alishinda ADUI wa MWISHO ambaye ni mauti…… Sina muda wa kulumbana, YESU Pekee ndiye Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6).

    Like

    • ndugu prosper unaposema mtakatifu mohamedi(st.mohamed s.a.w) ndo kwanza nasikia kutoka kwako na wala sijasikia jina hilo kutoka kwenye kinywa cha muislam yeyote ispokuwa ni wewe tu ndo uliyosema hayo! kwa taarifa yako waislam hawana shida na SAINT zenu! swala la MTUME MUHAMMAD(S.A.W) kufa wewe lisikutie shaka kwani MUHAMMAD(S.A.W) hakujitangaza kwamba ye ni mungu! (ambaye hafikwi na umauti) bali yeye ni mtume na muonyaji,kwa wanadamu na yeye ni binadamu na alistahili kufa kama manabii na wanadamu wengine kwa hiyo usishangae kuona kwamba mtume alikufa sasa tunapokuja kwenye swala lako la kusema YESUalikufa na kufufuka (yaani aliyashinda MAUTI)mimi na jambo linanitatiza katika hili kwamba sisi sote tunafahamu ya kwamba m/mungu ndiye aliyeumba kila kitu kilichopo duniani na mbinguni yakiwemo UHAI NA UMAUTI hivi ni kweli yesu aliyaumba mauti ili akapambane nayo kaburini? baada ya kufa pale msalabani kama ulivyosema hapo juu nanukuu ‘LAKINI YESU KRISTO BAADA YA KUFA ALIFUFUKA,HAYUPO KABURINI ALISHINDA UADUI WA MWISHO AMBAYE NI MAUTI’ yaani hapa naona mungu anasumbuliwa na vitu alivyoviumba mpaka uvumilivu umemshinda akaamua kupambana navyo na njia ya kupambana mauti ni yeye apigwe mpaka afe aende kaburini akapambane alafu awadhihirishie watu kwamba yeye ameyashinda mauti ili watu wamwamini yeye ni mungu? na kama ni kweli YESU aliyashinda mauti kama adui wake basi leo tungeshuudia wimbi la wakristo wamwanio yesu kwamba ni mungu wao aliyeshinda mauti kama adui wa mwisho wanaishi duniani bila kufa kwa maana mungu amepapmbana na kifo na kushinda!

      Like

  122. mhina says:

    Hayo ndugu Prosper, ni kweli kabisa kabisa!!!….Adui wa mwisho ni ‘MAUTI’ yanayokamilisha lile kusudi kuu la mwisho la yule mwovu, yaani shetani. Ni kweli isiyofichika ya kwamba,Muhamad alifanikiwa kwa kiasi kikubwa mno kuupa ulimwengu zile kweli kuu za kifalsafa,lakini alikosa uwezo wa Mungu(mambo ya kiroho) yaani kuwapa walimwengu ‘UZIMA WA MILELE’ ndio maana yeye mwenyewe mpaka hii leo bado anaendelea kubaki kaburini. Lakini tunaona kwa upande wa bwana yesu,kwa kuwa alifufuka kutoka kaburini siku ya tatu baada ya kifo chake, kwa hali hiyo ‘ALIMSHINDA ADUI WA MWISHO AMBAYE NI MAUTI.Ndiomaana baada ya hapo akatupa ahadi hii: NA KWA SABABU MIMI NI HAI,NINYI NANYI MTAKUWA HAI.Soma(yohana 14:19).Hapo tunajifunza tofauti ya kwamba,Bwana yesu anao uwezo juu ya mauti,hivyo anaweza kuwa tumaini letu kutuokoa toka mautini na kutupa uzima wa milele kama kweli tutamruhusu aishi ndani yetu,ndiomaana akasema hivi: ‘NA TAZAMA MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE,HATA UKAMILIFU WA DAHARI’.Soma(mathayo 28:20)….Tena akaendelea kutuahidi hivi: NYUMBANI MWA BABA YANGU MNAMAKAO MENGI,KAMA SIVYO,NINGALIWAAMBIA,MAANA NAENDA KUWAANDALIA MAHALI,BASI MIMI NIKIENDA NA KUWAANDALIA MAHALI,NITAKUJA TENA NIWAKARIBISHE KWANGU ILI NILIPO MIMI NANYI MUWEPO.Soma(Yohana 14:1-4).Ndugu mliobahatika kusoma mahali hapa, hakuna mauti tena katika yesu kristo bali ni uzima wa milele tu,ndiomaana neno la Mungu katika injili lilitimiza unabii wake kwa kututangazia ushindi kwa kuiuliza mauti hivi: KU WAPI,EWE MAUTI KUSHINDA KWAKO? UWAPI,EWE MAUTI UCHUNGU WAKO?.Soma(1wakorintho15:55).Pengine wewe msomaji unaweza kufikiri kwamba hizi ni hadithi lakini ukweli ni kwamba,huu ni ukweli mkuu wa siri za Mungu katika neno lake anazoendelea kuzitimiza katika injili.Kitakacho wagharimu watu wengi ni hali yao ya kukataa imani ya kumpokea bwana yesu awe bwana na mwokozi wao, na kamwe si jambo jengine.Sisi tumesimama katika kweli ya Mungu pasipo mashaka hata chembe,hata chembe kabisa kabisa!!.Taabu ni jinsi ya kuwasaidia wale wasioijua kweli ya Mungu ili nao waelewe vyema.Lakini kwa imani naamini Mungu atawasaidia na kuwapa ufahamu wa kweli wale wanaomtafuta kama fedha.Injili ninayoiandika hapa,sio suala la kusema, eti sijui paulo ndie alieandika hivi na vile>HAPANA.Hii ni injili ya Mungu mwenyewe iliyotimia kupitia mitume wake aliowachagua kwa neema yake yeye mwenyewe.Tunamuona Mungu mwenyewe kupitia kinywa cha Hosea anatabiri hivi: NITAWAKOMBOA NA NGUVU ZA KABURI,NITAWAOKOA NA MAUTI,EWE MAUTI YA WAPI MAPIGO YAKO? EWE KABURI KUWAPI KUHARIBU KWAKO? KUJUTA KUTAFICHWA NA MACHO YANGU.Soma(Hosea13:14)….Nae nabii isaya anakazia haya kwa kusema: AMEMEZA MAUTI HATA MILELE,NA BWANA MUNGU ATAFUTA MACHOZI KATIKA NYUSO ZOTE NA AIBU YA WATU WAKE ATAIONDOA KATIKA ULIMWENGU WOTE MAANA BWANA AMENENA HAYO,KATIKA SIKU HIYO WATASEMA: TAZAMA HUYU NDIYE MUNGU WETU,NDIYE TULIYEMNGOJA ATUSAIDIE,HUYU NDIYE BWANA TULIYEMNGOJA, NA TUSHANGILIE NA KUFURAHIA WOKOVU WAKE.Soma(isaya25:8-9).Hitimisho: je, bado wewe ndugu muislamu utaendelea kumkataa bwana yesu na kuendelea kumshikilia mtu ambaye amekwisha kufa siku nyingi?KAZI KWAKO!!.Basi ndugu zangu Wakristo,muimarike,msitikisike mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana siku zote kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika bwana…Wote tuseme: ‘HUYU NDIYE MUNGU WETU,NDIYE TULIYEMNGOJA ATUSAIDIE,NA TUSHANGILIE NA KUFURAHIA WOKOVU WAKE!!!.Jumaapili njema na mbarikiwe.

    Like

    • Ndugu Mhina,
      Kwanza kabisa nimshukuru Allah(S.W) na niwatakie rehema na amani mitume wake.
      Baada ya shukrani hizo nianze kuzijibu hoja za ndugu yangu Mhina moja baada ya nyingine kwa kunukuu baadhi ya vipengele na kuvitolea majibu ya msingi;
      1. HOJA YA MHINA: “Hayo ndugu Prosper, ni kweli kabisa kabisa!!!….Adui wa mwisho ni ‘MAUTI’ yanayokamilisha lile kusudi kuu la mwisho la yule mwovu, yaani shetani……… lakini(Mtume Muhammad) alikosa uwezo wa Mungu(mambo ya kiroho) yaani kuwapa walimwengu ‘UZIMA WA MILELE’ ndio maana yeye mwenyewe mpaka hii leo bado anaendelea kubaki kaburini”

      JIBU LANGU: Tatizo kubwa ulilonalo ndugu yangu ni kwamba hata biblia yako tu yenyewe inakushinda kusoma na kuilewa baadala yake unaandika mambo ambayo huna ushahidi nayo,Ndugu Mhina sijui imani hii ya kuwa kifo ndiyo mwisho wa kila kitu kama nilivyokunukuu hapo juu umeipata kitabu gani?kwa sababu hata ndani ya biblia hamna. Sisi waislamu tunaamini kuna maisha baada ya kifo na kifo siyo mwisho wa mwanadamu. Kwa mujibu wa biblia pia, tunaona kuwa kuna maisha ya milele baada ya kifo. Lakini quran inaenda deep zaidi pale inapotuambia kuwa watu wakosefu wataingia motoni na watu wema wataingia peponi na humo wataishi milele, biblia vile vile inatwambia kuwa watenda mema watapata uzima wa milele na waovu wataingia jehanam. Kumbe vitabu vyote viwili vinatambua kuwa baada ya kufa kuna maisha ya milele kwa watenda mema, licha ya kuwa kila siku tunashuhudia watu ambao ni watenda mema wakizikwa makaburini .Kwa imani hiyo ya vitabu vyote viwili, sidhani kama kuna haja ya mtu msomi wa vitabu hivi kushindwa kulitambua hilo na kuendelea kudhani kuwa kila aliyeko kaburini hana uhai. Mtu yeyote anayeendelea kuamini kuwa watu walio makaburini hawana tena uhai huyo hafai kuitwa mkiristu wala mwislamu bali anastahili kuwa mfuasi wa dini isiyokuwa hizo kwani vitabu vyote vinakubali maisha baada ya kifo.

      Kutokana na imani hiyo waislamu wote tunashawishika kusema Mtume wetu Muhammad(S.A.W) alikufa lakini baada ya hapo anao uhai wa milele peponi, Wakiristu pia wanaamini kuwa Bwana Yesu alikufa na baada ya hapo anao uhai wa milele peponi, Vivyo hivyo pia Nabii Musa, Nabii Yohana, Nabii Yakobo,Nabii Ibrahim pamoja na watu wote wema wako hai na wote wako peponi na wote wana maisha ya milele.

      Ndugu Mhina, najua na naamini kabisa kuwa elimu yako y a kiroho ni ndogo mno, lakini siyo lazima kila mtu ajue udhaifu wako, basi uwe unajaribu hata kuuliza watu wenye elimu za mambo ya kiroho watakusaidia ndgu yangu.
      2. HOJA YAKO TENA: lakini(Mtume Muhammad) alikosa uwezo wa Mungu(mambo ya kiroho) yaani kuwapa walimwengu ‘UZIMA WA MILELE’ ndio maana yeye mwenyewe mpaka hii leo bado anaendelea kubaki kaburini”

      JIBU LAKO TENA; Baada ya kuwahakikishia wakiristu wote kuwa kipenzi cha Allah yuko hai peponi, sasa tuone kwa ushahidi wa Qurani tukuf je ni kweli Mtume wa Allah alishindwa kuupa ulimwengu uzima wa milele?
      Allah Sub-hana wata’ala(S.W), anatuambia katika Quran tukuf kama ifuatavyo;
      QURAN 4:13 “Hiyo ni mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na anaye mt’ii Mwenyezi Mungu na Mtume
      wake, Yeye atamuingiza katika Pepo zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.”

      Kwa aya hiyo tu iko wazi kuwa yeyote atakayempokea Mtume katika maisha yake na kumtii Allah(S.W),Allah atamtia peponi na humo atadumu milele na huko ndiko kufuzu kukubwa kabisa; Sasa ndugu wakiristu kumtii mtume maana yake ni kuwa muislam na kufuata mafundisho na maadili yake, hiyo ndiyo njia pekee ya kuingia peponi na si vinginevyo. Siyo kwa Yesu kufa kifo cha laana msalabani pamoja na wanyang’anyi wawili kama wakiristu mnavyomkashifu na kumtukana yesu kipenzi cha Allah. Kufa msalabani biblia inatwambia ni kitendo cha laana maana imeandikwa amelaaniwa kila aangikwaye mtini (msalabani), kwa hiyo sisi waislamu kwa kuwa tunampenda sana Yesu Muislamu mwenzetu na Nabii wa Allah hatuamini kuwa yeye kalaaniwa pale msalabani kwa ajili ya dhambi za watu wanaomkosea Mungu. Yaani wewe uzini, uibe, n.k halafu Yesu aadhibiwe kwa ajili ya upuuzi wako!!!!!? Hiyo ni imani potofu mnayotakiwa kuiacha mara Moja kabla Allah hajashusha adhabu yake juu yenu.
      Allah atulinde na atuepushe na kumkashifu Yesu kuwa kafa kifo cha laana pamoja na wanyang’anyi pale msalabani na atuongoze sote Inshaallah.

      Like

  123. CONRAD says:

    Watumishi wa Mungu mtumikie kwa dhati na siyo kujidanganya

    Like

  124. GEOFREY says:

    NDG MHINA NIMEFURAHISHWA SANA NA COMMENT ZENU ZENYE UPENDO NA UNYEYEKEVU WA HALI YA JUU SANA, NA HII NDO AMRI AMBAYO YESU ALITUACHIA TUIFUATE.NDG ZETU WAISLAM IFIKE MAHALI MUWE WAWAZI NA KUKIRI KUWA DINI YENU INAPOTOSHA UMMA WENU,IMEJAA CHUKI,VISASI HASIRA NA KILA AINA YA UOVU. SIWALAUMU KWANI HIZO NDO SIFA ZA ALLAH(SHETANI) WENU.

    Like

    • Khamis says:

      Ndugu GEOFREY,
      kwani kwenye biblia hakuna, chuki, visasi na hasira? naomba ukatae kwamba kwenye biblia hakuna vitu hivyo halafu mimi nikupe ushahidi kwamba kwenye biblia vitu hivyo vimejaa tele.(naomba ubishi please au mkiristu yeyote akusaidie kubishi)

      Like

  125. GEOFREY says:

    Daah nimefurahishwa sana na hoja za wenzetu waislam kuwa YESU alikuwa muislam, Na hayo ndo mafundisho wanayowadanganya waumini wao misikitini. Mbona YESU alikuwa na upendo ilhali waislam ni jazba na chuki tupu? Acheni kutoa hoja za kitoto ni ukweli kuwa mohamed alipewa utume na kigoli wake bi khadija.

    Like

  126. GEOFREY says:

    Je waislam mnaweza mkanipa jibu kwanini mtume alibaka?

    Like

    • alfa says:

      ebu itazame jumapili na watu wake,wazur kuanzia th way walivyovaa,wana nyuso za furaha hata ka wamelala njaa,na biblia zao mikononi,wakikuona ubarikiwe zenye furaha na upendo,ingia makanisani ukasikilize injil inayoelekeza mioyo ktk upendo na amani,kiasi na uvumilivu,pia kusamehe ili kufunguliwa vifungo vya muovu shetani,ijuma ni tofauti sana,watu wenye sura za kikauzu,ngita usoni,hasira na usongo,mahubiri ni haya(naswara na mayahudi ni adui mkubwa kwa muislam)na mengine mengi sitayasema coz yanasikitisha xana na nawaonea huruma coz i lv ma frnds althoug they hat me,lm a christian,i blv in lv ka Mungu anavyowapenda hata watu wabaya na kuwaokoa,say piece,preach lv.

      Like

    • alfa says:

      halaf mi nadhan pia ndugu ze2 inatakiwa wajue kuwa Mungu hana mipaka,kwa matendo na waseme kwa dhati,kukataa uungu wa Kristo ni kumpa Mungu mipaka na kulipinga neno lake kwa nguvu,kama 2 unaamini Jehova anatenda mamb yake nje ya upeo na uwezo wa mwanadamu kufikir au kutafsiri,kwa nini ukatae aliweza kuzaliwa kama mwanadamu akawa mwana na at the same time father?

      Like

    • SWALEHE says:

      Je ndugu GEOFREY na wakiristu wenzio mwajua kwamba Paulo alikuwa shoga na hanith !? anayekataa aje na ushaidi na mimi nitaleta ushaidi kutoka ndani ya biblia.

      Like

    • SWALEHE says:

      Je ndugu GEOFREY na wakiristu wenzio mwajua kwamba Paulo alikuwa shoga na hanith !? anayekataa aje na ushaidi na mimi nitaleta ushaidi kutoka ndani ya biblia.

      Like

  127. alfa says:

    nawashangaa xana,nadhan mungu wa wakristo ndiye mungu coz yeye ndiye pekee asiyetafsirika kwa fahamu za wanadamu kama wao pia wanavyoamini ingawa wanaamini kinafiki lakini hapohapo wanapinga kisa kwa fahamu zao hatafsiriki,umeshasema Mungu na matendo yake ni juu ya fahamu zetu,unashangaa nini Mungu kuwa ktk hali tatu wakat mmoja?mwokoz Yesu,mfariji Roho mtakatifu,hakimu Baba,kukataa kwako inamaanisha mungu wako hana uwezo ulio juu za fahamu zako kwa hyo ni dhaifu,i don worship th weakest but the strongest,mungu anayeponya na kuokoa mpaka kesho,injil ni halis kwa waiaminio,polen na hadith za uongo zinazowafundisha chuki na uadui,uongo kwa kisingizio eti ni uongo wa faida,ndo maana waongo na wapindua maandiko na watunz wa hadith za uongo ili kutetea dini za giza.

    Like

    • alfa says:

      je ni ALLAH ama JEHOVA?nifuatilie,alikuja ktk KRISTO,huyo ROHO MTAKATIFU mwenye nguvu,injil yake inaponya magonjwa,inatia hekima na maarifa,msamaha na kiasi,uvumilivu na upendo{kumbuka maovu wanayotutendea hawa,fanya wangetendewa wao,japo moja ya kumi ya wanayowatendea wafuas wa MFALME MKUU,ingekuwaje?},tazama mwamba wetu ana huruma na habadiliki,amewasamehe israel kwa kumkataa kwao,kwa sababu aliapa hatawaacha kamwe,MUNGU WETU ALISEMA HIVI,TAZAMA UTAFIKA WAKATI WATAKAPOSEMA,AHIMIDIWE BWANA ALIYEWAKUSANYA WANA WA ISRAEL KUTOKA MATAIFA ALIMOWATAWANYA NA TENA KUTOKA MISRI,BAADA YA HASIRA ZA MUNGU WETU KUWAKA JUU YA ISRAEL KWA KUWA WALIMKATAA MFALME WAO NA BABA YAO KISHA KUMSULUBISHA NA KUWATESA NDUGU ZAO,MWAKA 7O AFTER JEHOVA KUPAA WAKATAWANYWA DUNIA NZIMA KWA FEDHEHA NA MATESO,MPAKA MWAKA 1967 BWANA AMEWARUDISHA WATU WAKE MAHALI PAO KWA MKONO WA CHUMA,(VITA),NA KAMA ALIVYOSEMA KTK NENO LAKE,ATAWAFUKUZA ADUI ZAO POLEPOLE HUKU AKIWAPA NGUVU WAO SIKU KWA SIKU,NILITEGEMEA NIMUONE ALLAH AKIWATETEA WAARABU,KIMYA.

      Like

    • alfa says:

      JEHOVA PEKE YAKE NENO LAKE LITASIMAMA,HAKUNA MWINGINE AWEZAYE KUOKOA KTK MKONO WAKE,SHAUR LAKE PEKE YAKE NDO LINATIMIA NA NENO LAKE LINATENDEKA,vitabu vya hawa jamaa vinatumika zaidi kuchochea chuki na uadui na lugha walioichagua ndo inayotumiwa na waganga pamoja na hicho kitabu chao,hii inajibu kwamb lugha wanayodai ya mbinguni c kwel ni ya mashetan kuzimu coz waganga ni vibaraka wa mapepo na majin ni ndugu zao,wanadai yapo mazur yanawalinda,lakin mwisho wataingia nayo Jehanam.coz majin ni malaika waas so mashetani hayo.

      Like

  128. alfa says:

    Bwana Yesu asifiwe wana wa Mungu aliyehai,ninayofuraha kuona mko makini na janja ya yule mwovu kutaka kuwapotosha,neno la Mungu wetu ni hai na halisi,na hakuna jina lingne litupasalo kuokolewa kwalo mataifa isipokuwa Yesu,niambieni ni nani mwingine anayehuisha na kuponya,anayefariji na kuinua isipokuwa Yesu,naongea kwa ujasiri bila uoga,yeyote asiye na Yesu,mchunguze hakosi mganga,na ibada za wafu ili mamb yaende vizur,matambiko na ibada za mizimu,bt mwisho wataangamia pamoja nao,una bahat uliyemfahamu Kristo,huna haja ya makombe wala chale,AHIMIDIWE MUNGU WA PEKEE WA KWELI(JEHOVA SHAMA NI LAKE JINA),nasi tu uzao wa ibrahmu kweli kweli ktk imani pamoja na israel,neno la bwana limetimia,tu weng kama nyota za mbinguni.

    Like

  129. Ndugu Mhina,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah(S.W) na niwatakie rehema na amani mitume wake.
    Baada ya shukrani hizo nianze kuzijibu hoja za ndugu yangu Mhina moja baada ya nyingine kwa kunukuu baadhi ya vipengele na kuvitolea majibu ya msingi;
    1. HOJA YA MHINA: “Hayo ndugu Prosper, ni kweli kabisa kabisa!!!….Adui wa mwisho ni ‘MAUTI’ yanayokamilisha lile kusudi kuu la mwisho la yule mwovu, yaani shetani……… lakini(Mtume Muhammad) alikosa uwezo wa Mungu(mambo ya kiroho) yaani kuwapa walimwengu ‘UZIMA WA MILELE’ ndio maana yeye mwenyewe mpaka hii leo bado anaendelea kubaki kaburini”

    JIBU LANGU: Tatizo kubwa ulilonalo ndugu yangu ni kwamba hata biblia yako tu yenyewe inakushinda kusoma na kuilewa baadala yake unaandika mambo ambayo huna ushahidi nayo,Ndugu Mhina sijui imani hii ya kuwa kifo ndiyo mwisho wa kila kitu kama nilivyokunukuu hapo juu umeipata kitabu gani?kwa sababu hata ndani ya biblia hamna. Sisi waislamu tunaamini kuna maisha baada ya kifo na kifo siyo mwisho wa mwanadamu. Kwa mujibu wa biblia pia, tunaona kuwa kuna maisha ya milele baada ya kifo. Lakini quran inaenda deep zaidi pale inapotuambia kuwa watu wakosefu wataingia motoni na watu wema wataingia peponi na humo wataishi milele, biblia vile vile inatwambia kuwa watenda mema watapata uzima wa milele na waovu wataingia jehanam. Kumbe vitabu vyote viwili vinatambua kuwa baada ya kufa kuna maisha ya milele kwa watenda mema, licha ya kuwa kila siku tunashuhudia watu ambao ni watenda mema wakizikwa makaburini .Kwa imani hiyo ya vitabu vyote viwili, sidhani kama kuna haja ya mtu msomi wa vitabu hivi kushindwa kulitambua hilo na kuendelea kudhani kuwa kila aliyeko kaburini hana uhai. Mtu yeyote anayeendelea kuamini kuwa watu walio makaburini hawana tena uhai huyo hafai kuitwa mkiristu wala mwislamu bali anastahili kuwa mfuasi wa dini isiyokuwa hizo kwani vitabu vyote vinakubali maisha baada ya kifo.

    Kutokana na imani hiyo waislamu wote tunashawishika kusema Mtume wetu Muhammad(S.A.W) alikufa lakini baada ya hapo anao uhai wa milele peponi, Wakiristu pia wanaamini kuwa Bwana Yesu alikufa na baada ya hapo anao uhai wa milele peponi, Vivyo hivyo pia Nabii Musa, Nabii Yohana, Nabii Yakobo,Nabii Ibrahim pamoja na watu wote wema wako hai na wote wako peponi na wote wana maisha ya milele.

    Ndugu Mhina, najua na naamini kabisa kuwa elimu yako y a kiroho ni ndogo mno, lakini siyo lazima kila mtu ajue udhaifu wako, basi uwe unajaribu hata kuuliza watu wenye elimu za mambo ya kiroho watakusaidia ndgu yangu.
    2. HOJA YAKO TENA: lakini(Mtume Muhammad) alikosa uwezo wa Mungu(mambo ya kiroho) yaani kuwapa walimwengu ‘UZIMA WA MILELE’ ndio maana yeye mwenyewe mpaka hii leo bado anaendelea kubaki kaburini”

    JIBU LAKO TENA; Baada ya kuwahakikishia wakiristu wote kuwa kipenzi cha Allah yuko hai peponi, sasa tuone kwa ushahidi wa Qurani tukuf je ni kweli Mtume wa Allah alishindwa kuupa ulimwengu uzima wa milele?
    Allah Sub-hana wata’ala(S.W), anatuambia katika Quran tukuf kama ifuatavyo;
    QURAN 4:13 “Hiyo ni mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na anaye mt’ii Mwenyezi Mungu na Mtume
    wake, Yeye atamuingiza katika Pepo zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.”

    Kwa aya hiyo tu iko wazi kuwa yeyote atakayempokea Mtume katika maisha yake na kumtii Allah(S.W),Allah atamtia peponi na humo atadumu milele na huko ndiko kufuzu kukubwa kabisa; Sasa ndugu wakiristu kumtii mtume maana yake ni kuwa muislam na kufuata mafundisho na maadili yake, hiyo ndiyo njia pekee ya kuingia peponi na si vinginevyo. Siyo kwa Yesu kufa kifo cha laana msalabani pamoja na wanyang’anyi wawili kama wakiristu mnavyomkashifu na kumtukana yesu kipenzi cha Allah. Kufa msalabani biblia inatwambia ni kitendo cha laana maana imeandikwa amelaaniwa kila aangikwaye mtini (msalabani), kwa hiyo sisi waislamu kwa kuwa tunampenda sana Yesu Muislamu mwenzetu na Nabii wa Allah hatuamini kuwa yeye kalaaniwa pale msalabani kwa ajili ya dhambi za watu wanaomkosea Mungu. Yaani wewe uzini, uibe, n.k halafu Yesu aadhibiwe kwa ajili ya upuuzi wako!!!!!? Hiyo ni imani potofu mnayotakiwa kuiacha mara Moja kabla Allah hajashusha adhabu yake juu yenu.
    Allah atulinde na atuepushe na kumkashifu Yesu kuwa kafa kifo cha laana pamoja na wanyang’anyi pale msalabani na atuongoze sote Inshaallah.

    Like

  130. mhina says:

    Ndugu Mhamad, nimepitia kwenye blog hii, kwa bahati nzuri nimekuona umerudi tena, ni sawa kabisa, tena namuomba Mungu akubariki sana, na pia aufunue ufahamu wako zaidi ili uijue kweli ipate kukuweka huru. Mimi kwa jicho langu la rohoni ninaamini kuwa wewe ndugu Mhamad, ni kweli unampenda Mungu ndiyo maana umekuwa mdadisi wa mambo.Hebu sasa nianze kukujibu lawama ulizonitupia……naanza kwa kukunukuu, umesema”SIJUI IMANI YA KUWA KIFO NDIYO MWISHO WA KILA KITU UMEIPATA KITABU GANI, KWA SABABU HATA NDANI YA BIBLIA HAMNA”.Mwisho wa kukunukuu……JIBU LANGU: Ndugu yangu mhamad, ukiandika mambo ya uongo,utamkosea hata Mwenyezi Mungu ila ukiandika mambo ya ukweli basi hutamkosea Mungu bali utamfurahisha.Nasema hivyo kwa kuwa mimi kamwe kamwe sikuandika kuwa, kifo ndiyo mwisho wa kila kitu ila mimi niliandika kuwa”ADUI WA MWISHO NI KIFO” au tuseme”MAUTI” …Na hili kamwe sio kwa mujibu wa mawazo yangu bali ni kwa mujibu wa biblia takatifu,hebu thibitisha wewe mwenyewe kwenye (1wakorintho15:26).Haya ndiyo mafundisho ya biblia neno la kweli lenye uzima unalolikataa wewe na waislamu wenzako.Biblia inatufundisha wazi wazi kwamba,Pamoja na kuwa watu wote tutakufa lakini bado katika ufufuo wa mwisho,kutakuwa na mauti ya pili, yaani kwenye ziwa la moto.Wale wote waliomkataa bwana yesu na kukosa neno lake la kweli kama wewe ndugu mhamad, mtakataliwa ili muungane na baba yenu shetani katika ziwa lile la moto,soma(ufunuo 20:14-15).Lakini sisi wote tuliompokea bwana yesu kuwa ni bwana na mwokozi wetu,tutachukuliwa kwa ajili ya uzima wa milele.Ukweli ni kwamba, dhambi huleta mauti, na mauti huleta adhabu ya Mungu, lakini kwa kuwa sisi tumemkubali bwana yesu kuwa ni bwana na mwokozi wetu, na kwa kuwa yeye aliyashinda mauti na kufufuka siku ya tatu kama biblia takatifu inavyotufundisha,basi kama nilivyoeleza huko juu ya kwamba, hatupo tena mbele ya adhabu ya Mungu, ndiyo maana biblia yalithibitisha hili kwa kusema”SASA,BASI, HAKUNA HUKUMU YA ADHABU JUU YAO WALIO KATIKA KRISTO YESU, KWA SABABU SHERIA YA ROHO WA UZIMA ULE ULIO KATIKA KRISTO YESU IMENIACHA HURU, MBALI NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI.Soma(warumi 8:1-2). Hapo ndugu yangu mhamad, utagundua kuwa, sheria ile ya dhambi na mauti, ni ile sheria takatifu ya Mungu inayodai malipizi, yaani torati ya Musa inayosema”mshahara wa dhambi ni mauti” au “AMELAANIWA YEYOTE ASIYESHIKA NA KUTII SHERIA ZA MUNGU KIKAMILIFU”.Soma(kumbuk 27:26).Hapo kinachonisikitisha kwa ndugu zangu nyinyi waislamu ni kwamba, kwanza sheria hizo za quran ni za mhamad na dini yake ya kule uarabuni alizopewa na vibwengo kule mapangoni na kamwe sio sheria zile takatifu za asili za Mungu kupitia nabii Musa.Pili hatakama mkijitetea kwa kusema ni zilezile, basi mtagundua kuwa kama yanenavyo maandiko matakatifu”waislamu wote pamoja na mtume wenu mhamad, mmelaaniwa ninyi kwa kushindwa kuyashika yote yaliyoandikwa kwenye kitabu cha sheria za Mungu kwa 100%. Hapo sihitaji kelele zako maana hata wewe mwenyewe roho yako ni shahidi kwamba, mambo mengine hamuyatekelezi kwa sababu ya kitu mnachokiita eti”MAZINGIRA MAGUMU!!.Sasa nikuulize ndugu Mhamad kuwa, je, unahitaji nikusaidie kukuonyesha baadhi ya hizo laana zilizowapata ninyi waislamu?,yes…tukiachana na mambo ya kuchoma sehemu anazoabudiwa Mungu,hasira kali na jazba isiyo ya kidini, kuhisi mnaonewa na kupunjwa kila kitu,kulala misikitini kama mko kwenye misiba,kufanya ibada za kuwalaani mayahudi na wakristo wakati wote badala ya kuwaombea wamjue Allah, hizi ni baadhi tu,lakini kubwa kuliko ambayo hata wewe ndugu mhamad nakupa pole kwa kuwa laana hii hata wewe unayo ni kulichanganya neno takatifu unaloliamini wewe mwenyewe na elimu ya hali nyingine usioiamini kwa kutafuta usawa wa majibu ili ufanye usawazo na kujiridhisha wewe mwenyewe!!.Hilo ni kosa kubwa mno mno,ndiyo maana sisi wakristo hatutakiwi kumtia mtume wenu ndani ya bibli kwa kisingizio eti naye ni nabii wa mwisho, kwani kwa kufanya hivyo tutalaaniwa.Msingi wako dhaifu huo na elimu yako ndogo ya imani mimi siwezi kukulaumu kwa kuwa,najua umefundishwa huko misikitini maana tunaona kwa mfano mdogo tu…ile tv yenu ya kiislamu, badala ya kutumia kitabu cha ibada kuwafundisha watoto mambo mema ya kiroho ya Allah, wao wanakwenda kuchukua vitabu vya komfuu na kareti ili kuwafundisha watoto ukatili wa kupigana matokeo yake jitoto likiwa kubwa linawaza kupiga watu mitaani badala ya kufikiria jinsi ya kuishi na watu vizuri na kuwasamehe!!…jamani hebu tujiulize, dini na mambo ya komfuu ni wapi na wapi?!!,Allah akifundisha komfuu misikitini hivi na wale wakina Anod,cheknoris na wale wahindi wakina sijui amita bachari na mithunchakaribota hivi nao watafundisha nini hapa duniani?!, mbona Allah anaonekana anaingilia fani za watu pamoja na imani za wengine?,kweli siyo laana kuu hii?!!.Basi ndugu yangu mhamad,mimi nimalizie na kukupongeza sana kwa ushauri wako mzuri kwangu kuwa wewe unajua wazi kwamba, elimu yangu ya kiroho ni ndogo mno,mimi nakubaliana na wewe kwa kuwa kamwe mimi siyo mwalimu wa dini, mimi siyo mchungaji wala mimi siyo padre au askofu bali mimi ni mkristo mchanga mno katika mambo ya kidini na ni kweli kabisa kama ulivyosema kuwa inanibidi nijifunze zaidi mbele ya viongozi wangu wa dini haya mambo ya kiroho, nimepokea ushauri wako mzuri sana lakini pamoja na madhaifu yangu hayo unayoyaona, mimi naamini kwa uwezo wa Yehova,Mungu ninaemuabudu mwenye uwezo na nguvu tele tele…ninacho kitu cha kukusaidia wewe na waislamu wenzako ambao kwa kweli mpo kinyume kabisa na njia pamoja na maagano ya Mungu kupitia manabii wake.Mimi ninaamini kuwa “lile tahira na zuzu la chuo kikuu linalokuwa la mwisho darasani, ukilipeleka chekechea linaweza kufundisha hata kuchaguliwa liwe mwalimu mkuu”…hivyo na mimi nitaendelea kugawa kile Mungu anachonipa pasipo kukata tamaa au kujiona siwezi kwa kuwa kila mtu amejaliwa kiwango chake.Njoo kwa bwana yesu ndugu kwa kuwa bado lango halijafungwa.Ubarikiwe.

    Like

  131. Ndugu Mhina.
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah kwa kunijalia neema ya uhai na afya, zaidi nimshukuru kwa kunipa neema kubwa kabisa kuliko zote kwa kunijaalia mimi kuwa miongoni mwa waislamu, kwa ufupi kabisa niseme Al-hamdulillah.

    Nikiingia katika mada, naomba nianze kwa kunukuu na kujibu hoja zako walau kwa kifupi kadri Allah atakavyonijalia.
    HOJA YAKO: “je, unahitaji nikusaidie kukuonyesha baadhi ya hizo laana zilizowapata ninyi waislamu?,yes…tukiachana na mambo ya kuchoma sehemu anazoabudiwa Mungu,hasira kali na jazba isiyo ya kidini, kuhisi mnaonewa na kupunjwa kila kitu,kulala misikitini kama mko kwenye misiba,kufanya ibada za kuwalaani mayahudi na wakristo wakati wote badala ya kuwaombea wamjue Allah,…”

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina, kwanza kabisa naomba utambue kuwa umehama katika hoja ya msingi na kukimbilia ktk matukio, nadhani ingekuwa vema zaidi kama hoja zetu zingelenga zaidi katika kulinganisha bible na quran na hapo tungesaidia kuelimisha uma unaofatilia blog yenu hii.
    Pamoja na hayo bado ninayo majibu ya msingi kuhusu hoja zako, nikianza na swala la kuchoma nymba za Ibada. Dini ya kiislamu hairuhusu kabisa matendo ya namna hiyo, bila kujali nymba hiyo ni ya dini gani.
    Lakini pia ni lazima sote tujue kwamba hatuwezi kuu-hukumu uislam kwa kuangalia matendo ya baadhi ya waislam au kuutuhumu ukiristu kwa kuangalia matendo ya baadhi ya wakiristu, kwa sababu matendo ya kuharibu nyumba za ibada tumeona Raisi wa nchi ya Msumbiji hivi karibuni akiamuru kuwa misikiti yote nchini humo ivunjwe kwa sababu nchi hiyo ni ya kikiristu na kweli misikiti imevunjwa na sote tumeshuhudia.
    Lakini pia, tumeshuhudia wakiristu wa Urusi wakifanya mauaji ya Kimbali kwa waislam wasio na hatia wa nchi ya Bosnia miaka ya tisini.Mbali na hapo tumeshuhudia pia katika miaka ya nyuma kidogo wakiristu wa dhehebu la Katholic(Christian Crusaders) wakiwauwa kinyama wenzao wa madhehebu ya Protestant na kuwavunjia nyumba zao za ibada kwa unyama na ukatili mkubwa.Kwa hiyo je hayo matukio yoote tuyaite laaana kwa wakiristo na ukiristo pia? Je ni haki tuseme ukiristo umelaaniwa?Naomba tutumie busara ktk kujibu hoja za msingi badala ya kukurupuka na kuanza kuongea mambo usiyoyajua.

    Ndugu Mhina, Pili umesema sisi tunahisi tunaonewa ktk kila kitu, unaposema kila kitu siafikiani na ww kabisa, lakini naweza sema uonevu kwa waislamu hususan hapa Tanzania ni wa kihistoria toka enzi ya mkoloni, kwa hilo nisingependa kulifanya mada lakini yapo matukio mengi yanayodhihirisha hilo ukitaka tulijadili tutalijadili pia, lakini pia hiyo siyo kwa waislamu tu hata wakiristu mmekuwa mkihisi kuonewa katika baadhi ya masuala pia, kwa mfano suala la kuchinja, kama unakumbuka limeleta mgogoro sn hadi watu kufa, hii yote imetokana na baadhi ya wakiristu kuhisi wanaonewa. Je na hiyo ni laana iliyoukumba Ukiristu na wakiristu pia?

    Ndugu Mhina, Umeleta pia hoja ya kulala msikitini kama tuko msibani kuwa ni laana kwa mtazamo wako. Ndugu yangu naomba utambue kuwa kulala msikitini ni jambo miongoni mwa mambo ya kheri mno, kwa sbabu kuna watu wanalala guest house wakifanya uzinifu, wengine wanalala kwenye kumbi za disco na mabaa, na wengine kwenye ushenzi na upuuzi mbalimbali wa kidunia.Kwa hiyo ndugu Mhina kama unasema kulala msikitini ni laana je hao wanaolala katika hizo sehemu nilizoainisha hapo juu ndio waliobarikiwa???
    Ndugu yangu, mimi binafsi Wallah natamani hata ningeamishia makazi yangu msikitini ili niweze kufanya ibada zote za usiku kwa sababu ninapolala nymbani mara nyingi ibada za usiku hunipita.Binafsi nimetenga siku ya Alhamis kwa ajili ya kulala msikitini kila ninapopata wasaa.Ndugu yangu kulala msikitini kuna faida kubwa mno kwa wachamungu kwani nyumba ya Allah haitakiwi kuachwa na upweke, kama yanavyoachwa upweke makanisa mpaka siku ya j.pili au j.mosi. Watu hawaendi makanisani mpaka j.pili mimi nadhani hiyo ndiyo laaana kubwa kuliko zote.Makanisa yanakuwa na masanamu ndani yake masaa 24 katika siku sita za wiki, watu wanaingia kwa ajili ya kupangusa masanamu vumbi tu na kutoka mpaka siku ya j.pili ndo mungu anaabudiwa ndani ya kanisa, Ndugu Mhina hiyo ndiyo laana nambari 1, kufanya nyumba ya mungu wenu magofu.

    HOJA YAKO. Ndugu Mhina pia umesema pia kuwa sisi waislamu tunawaombea laana ya Mungu mayahudi na wakiristu, hiyo siyo kweli ndug yangu, ingawa ni kweli kuwa inaruhusiwa kabisa kumuombea laana mtu yeyote aliyewafanyia dhulma waislamu kwa makusudi na kwa kujua kuwa hicho anachokifanya ni dhulma, kwa sababu Allah anasema dua ya mtu aliyedhulumiwa ni “mustajaba” yaani ni dua inayokubalika.Lakini Pia kuna dua ya kuwaombea msamaha kama wametenda dhuluma kwa waislam lakini bila kujua kuwa wanachokifanya ni dhuluma.Hao inaruhusiwa kabisa kuwaombea msamaha kwa Allah.
    Mfano mzuri kabisa ni kisa maarufu kinachomhusu Mtume wetu Mtukuf Muhammad bin Abdullah(S.A.W) pale alipopigwa mawe katika mji wa Twaif huko Makka pale alipoenda kuwafundisha masuala ya kiimani, Mtume alipigwa mawe mpaka mwili mzima ukalowa damu. Walipokuja malaika wakamwambia “ewe Mtume wa Allah amuru adhabu yoyote iwapate watu hawa, hata ukiamuru tuikutanishe milima miwili ili watu hawa wote wafukiwe ndani yake sisi tutafanya” Mtume akasema “hakika hawa watu nimewasamehe kwani katika vizazi vyao watakuja kutoka watu wanaompenda Allah hivyo nimewasamehe,” Na kweli waislamu wote tu mashaidi kuwa katika kizazi hicho wametoka mashekhe wakubwa mno katika uislamu.
    Lakini pia hata biblia yenu imetoa laana mbali mbali kwa watu wasiotii sheria za Mungu
    “AMELAANIWA YEYOTE ASIYESHIKA NA KUTII SHERIA ZA MUNGU KIKAMILIFU”.Soma(kumbuk 27:26).
    Kwa hiyo ndugu yangu swala la laana kwa watu wakosefu hilo lipo tu, na hakuna jinsi unavyoweza kulipinga.
    Ndugu Mhina, wewe na wakiristu wenzenu pia ni mashahidi kuwa biblia yenu hiyohiyo imeendelea kuwapa watu laana mpaka Yesu mwenyewe biblia inadai kafa kifo cha laana. Yaani uokovu wenu umetokana na laana alizopata yesu msalabani.Waislamu tunafadhaika sana kwa jinsi wakiristu mnavyomtukana na kumkashifu Yesu(Rehma na amani ziwe juu yake) aliyekuwa nabii wa Allah na mwislamu mwenzetu. Wallah hilo ni jambo ovu mno, wallah hilo ni tusi kubwa mno kwa mtu aliyekuwa mtakatifu kufa kifo cha laana kwa kuingikwa mtini, wallah msipoacha laana za Allah zitakuwa juu yenu.
    Allah atuongoze wote inshaallah.

    Like

  132. mhina says:

    Mr.Mhamad, nilikwisha kueleza huko juu ya mijadala yetu kwamba, tatizo kubwa ulilonalo, ni wewe kutafuta makosa ya mwingine lakini makosa yako huwa huyaoni.Huko juu ya michango yako,ulielezea mambo mengi mno machafu tena ya uongo yanayohusu wakristo na makanisa yao lakini mimi nikanyamaza.Lakini hata kama yalikuwa ya ukweli,kamwe,wateule wa Mungu hatufanyi kazi za kutetea makanisa bali tunatetea neno la Mungu ambalo ni Biblia kwa maana ni kweli kuwa wanadamu hawakosi mapungufu yao.Sisi tunaishi kwa neno la Mungu pekee na kamwe hatuishi kwa ajili ya watu au kanisa fulani.Lakini mimi kusema kuwa waislamu wote na Mtume wenu mhamad mmelaaniwa haikuwa kwa sababu ya yale maelezo yangu niliyokusaidia bali nilisema kuwa mmelaaniwa kwa misingi ya kweli kabisa ya neno la Mungu na misingi ya sheria zake.Hebu sasa tujiulize kuwa,je, ni kweli au ni uchokozi na maudhi?….Mungu mwenyewe anasema hivi: “NA ALAANIWE ASIYEYAWEKA IMARA MANENO YA SHERIA KWA KUYAFANYA”!!!!!.Halafu tunamuona Yakobo ambaye alikuwa anayajua sana mambo ya sheria za Mungu na utakatifu wake,nae alisisitiza kwa kusema”MAANA MTU YEYOTE AKISHIKA SHERIA ZOTE ILA AKAJIKWAA KATIKA MOJA, BASI AMEKOSA JUU YA ZOTE”!!!…Sasa,hebu wafuatiliaji wa blog hii angalieni, Siku zote ndugu zetu waislamu wanadai kuwa wao ni watenda sheria,tena pasipo woga wanasisitiza kuwa sheria za Manabii wa Mungu ndiyo hizo hizo zilizokuwa kwenye quruani yao, wao huwa wanasema hivyo kwa lengo la Kumlinda na kumtunza nabii wao mhamad ili asionekane kuwa ameleta sheria mapya zinazopingana na zile za kweli za Mungu.Lakini sasa tazama ibilisi huyu jinsi anavyokosa balance yake ya uongo na hatimaye anaelekea kuanguka!!!,huku ataka na huku ataka lakini kote ni kuchungu!!.Maana sheria za quruani zikiwa ni tofauti na zile za Mungu kupitia nabii Musa(na ndivyo ilivyo) basi,tena waislamu watakuwa wamepotoshwa, nakama ni zilezile kama wanavyoamini wao wenyewe”BASI WAMELAANIWA WOTE KWA KUSHINDWA KUTII NA KUSHIKA SHERIA ZOTE”,…Kama Mwenyezi Mungu mwenyewe alivyoahidi na kamwe si kwa matakwa ya mimi Mhina….sasa sijui kosa langu ni nini,wakati wote ni wanadamu na kazi yetu ni kupeana maarifa tu,!!.Wao waislamu wanajua wazi kwamba masheria kibao hawayatekelezi kwa sababu ya “MAZINGIRA”….Sasa ni dini gani hii unayoiinamia msikitini mara tano kwa siku,kumbe kimaandiko ilikwisha kufa siku nyiiiingi!!!…jamani waislamu,msipende kufuata mambo pasipo udadisi wa kina ndugu zangu.Tende na halua kutoka uarabuni haziwezi kuwapeleka mbinguni…hojini maswali ya msingi viongozi wenu pasipo woga,hapo ndipo mtakapogundua udhaifu wenu.Mimi naamini kabisa hata nyinyi kufika kwenye blog hii ya kikristo ni moja ya hatua kubwa kwenu ya kupata point za kuwahoji viongozi wenu.Sasa baada ya hayo,napenda ndugu mhamad kukuhakikishia kuwa kamwe sisi wakristo hatuna laana za kimaandiko kama nyinyi,kama uliwaona baadhi ya wakristo wana laana basi hizo ni laana zao za kushindwa kutii na kufuata kanuni za kweli ya biblia.KIVIPI?….Ukweli ni kwamba, bwana yesu alikuja kutimiza torati na manabii kwa ajili yetu, ili sisi wafuasi wake tusishtakiwe na hata yodi au hata nukta moja ya sheria za Mungu kama nyinyi zitakavyo washtaki mbele za Mungu siku za hukumu.Wakristo hatukatai,ni kweli kabisa kwamba,sheria za Mungu zinaeleza mapenzi ya Mungu, lakini tunafahamu pia kwa ajili ya watu wote waliochini ya hizo sheria”ZINAWALETEA HUKUMU YA MUNGU”.Hivyo, Mungu kwa mapenzi yake mwenyewe kwa sababu ya kutupenda sisi wote,alituandalia mchungaji wa kutuokoa tangu zamani ambaye ni bwana yesu.Siku zote mchungaji ni mtu wa kujitoa kwa ajili ya kondoo wake.Unabii wa ajabu wa Mungu kupitia kinywa cha nabii isaya,ulitoa sauti ya ajabu mno yenye matumaini yanayomuelezea huyo Mchungaji jinsi atakavyojitoa kwa ajili yetu”NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”!!!…SISI SOTE KAMA KONDOO TUMEPOTEA, KILA MMOJA WETU AMEGEUKIA NJIA YAKE MWENYEWE, NA BWANA MUNGU AMEWEKA JUU YAKE MAOVU YETU SISI SOTE.Soma(isaya 53:5-6).Hebu sasa tujiulize kuwa je, fumbo hilo la Mungu la mchungaji na kondoo wake alilolitabiri maelf ya miaka hata kabla ya bwana yesu kuzaliwa na injili kuandikwa lilitimia kweli?…..Bwana yesu alisema, amekuja kutimiza torati na manabii.Siku zote, mchungaji mwema, anapochunga kondoo wake porini,wakati panapotokea simba kutaka kuwala wale kondoo wake, basi kwa kuwa yeye ni mchungaji mwema tena ni wakweli na muaminifu,utamuona anajitoa yeye mwenyewe kupambana na yule simba hata mpaka mauti yamfike ilimradi tu,ahakikishe kuwa hakuna kondoo atakae potea kwa kuliwa na yule simba.Sasa, Simba ni shetani halafu mchungaji mwema ni bwana yesu,mwisho,Porini ni humu duniani mnamotawaliwa na shetani katika mambo yetu mengi.Kuhusu huyu shetani biblia inamuita”mshtaki wetu kama simba angurumaye kutaka kutumeza”.bwana yesu nae anajiita”mchungaji mwema asiekimbia kondoo wake hata kifo kimfike” nao kondoo wa mchungaji mwema ambae ni bwana yesu ni sisi wakristo….hivyo ningekushahuri vyema ndugu mhamad ujiunge katika zizi hili salama wewe na waislamu wenzio…karibuni sana,maana bwana yesu atakapokuja,biblia inasema”NDIVYO ATAKAVYO WASITUSHA MATAIFA MENGI, WAFALME WATAMFUMBIA VINYWA VYAO MAANA MAMBO WASIOAMBIWA WATAYAONA NA MAMBO WASIO YASIKIA WATAYAFAHAMU.Soma(isaya 52:15)(warumi 15:21).Ubarikiwe.

    Like

  133. Ndugu Mhina,
    Nizitangulize shukrani zangu kwa Allah sub-hana wata’aala(S.W) ambaye uhai wangu umo mikononi mwake, na niwatakie rehema mitume wote na watu wema wote waliotutangulia.
    Ama baada ya kumshukuru Allah, Ningependa nianze kuijadili mada hii kwa kunukuu hoja zako na kuzitolea majibu ya msingi;
    Kwanza kabisa ni lazima sote tukubaliane kuwa Biblia ni kitabu cha mwongozo kwa wakiristu hivyo basi maneno yote yaliyomo ndani ya biblia, sheria na amri zote zilizomo ndani ya biblia ni mwongozo kwa wakiristu kwani ndio waaminio wa biblia. Kwa sisi tuliobahatika kuwa waislam mwongozo wetu ni Quran tukuf.
    Baada ya kulitambua hilo, kwenye biblia kuna kipengele ambacho ndugu yangu amekinukuu kinachosema “BASI WAMELAANIWA WOTE KWA KUSHINDWA KUTII NA KUSHIKA SHERIA ZOTE”
    Kipengele hiki kimo ndani ya biblia ambayo ni mwongozo wa wakiristu, na wakiristu hao hao wameshindwa kabisa kuufuata mwongozo huu kwa sababu wao wanazikataa sheria za Musa wa ndani ya biblia yao kwa kudai kuwa laana zote amezichukua mwokozi wao yesu kristu kwa kutimiza torati. Wakiristu wanajichanganya na wanashindwa kuelewa msitari huu wa biblia, kwa sababu huwezi kusema Yesu kachukua laana za watu wote na hali yeye aliziishi na kuzitii sheria za zote, na biblia inasema asiyezitii sheria zote ambao ndio wakiristu wenye biblia.
    Kinachonishangaza ni kwamba ndugu Mhina anaposoma kipengele hiki anasema kinawahusu waislamu na ili hali kipo ndani ya biblia ambayo ndiyo mwongozo wao na wao hawafuati sheria ambazo biblia yao ishasema asiyezifuata kalaaniwa.Sasa hii haingii akilini, yaani sheria zipo ndani ya biblia yenu, na nyie hamzifuati na biblia inasema asiyezifuata amelaaniwa . Je ndugu Mhina huoni kuwa una jaribu kuukwepa ukweli??? Na ilihali roho inakusuta!!?
    Sisi waislam mwongozo wetu ni quran, na hakuna sehemu quran inaposema “wamelaaniwa wote kwa kushindwa kutii sheria zote za torat” hakuna, hakuna!!!!!! Hebu tuone Allah anatuambia nini kuhusu torati.

    QRUNA 5:44. “Hakika Sisi tuliteremsha Taurati yenye uwongofu na nuru, ambayo kwayo
    Manabii walio nyenyekea kiislamu, na wachamngu, na wanazuoni, waliwahukumu
    Mayahudi; kwani walikabidhiwa kukihifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nao wakawa
    ni mashahidi juu yake.”

    Ndugu yangu Mhina, quran iko wazi kabisa kuwa torati walipewa manabii wa kiislam waliokuwepo kabla ya Mtume wetu mtukufu ili uwe mwongozo kwa mayahudi. Kwa hiyo ndugu yangu Mhina biblia inakulaani wewe usiyeziweka sawa sheria za torati na siyo muislam we vip ndg yang? Muislamu halaaniwi na biblila hata siku moja, yaani hiyo ondoa katika akili yako.

    HOJA YAKO YA PILI: “basi kwa kuwa yeye ni mchungaji mwema tena ni wakweli na muaminifu,utamuona anajitoa yeye mwenyewe kupambana na yule simba hata mpaka mauti yamfike ilimradi tu,ahakikishe kuwa hakuna kondoo atakae potea kwa kuliwa na yule simba.Sasa, Simba ni shetani halafu mchungaji mwema ni bwana yesu,”
    JIBU LA HOJA YAKO:Ndugu Mhina, Kwa hoja hiyo unamaanisha kuwa mchungaji wenu yesu alikufa wakati akipambana na simba(shetani) ili simba asiwatafune nyie kondoo, kwa maana hiyo basi simba yaani shetani alimzidia nguvu mchungaji mpaka akamuua, hivyo kondoo wakabaki bila mchungaji.sasa Ndugu Mhina na wakiristu wote ni lazima mtafakari kama mchungaji wenu alitolewa uhai na simba wakati akiwalinda msiliwe, je inakuwaje mchungaji akishauliwa,?????????????? Jibu ni kwamba simba anawatafuna kondoo kirahisi mno na huku kondoo wengine wakikimbia huku na huku kwa sababu mchungaji ashatoa uhai wake kwa ajili ya kondoo aliowapenda.Hivyo simba yaani shetani anajilia tu makondoo.
    Mi nadhani mchungaji huyo alikuwa ni mjinga wa mwisho, kwa sababu huwezi kupambana mpaka mauti ya kufike ili kondoo wako wasipotee sasa ukishakufa si wataliwa na kupotea tu bila direction yoyote. Mi naamini kabisa mchungaji wenu huyo alikuwa hajajipanga.
    Hebu angalia Allah alivyomchungaji wa kweli katika quran.
    QURAN 2:255. Mwenyezi Mungu – hapana mungu ila Yeye Aliye hai milele, Msimamia mambo yote
    milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni
    na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake?
    Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika
    vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni
    na duniani; na wala haelemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na
    ndiye Mkuu.”

    Allah anatuambia kuwa haelemewi na kuvilinda viumbe vyake, anao uhai wa milele, anayajua yaliyo mbele na nyuma yake. Sub-hanalllah ewe ndugu mkiristu unasubiri nini kumpokea mchungaji huyu asiyelemewa na kuuwawa kama alivyokufa mchungaji wenu, mnasubiri nini ndugu zangu, muda unaenda hivyo na kifo kinakaribia.Jitahidini fanyeni hima mfe mkiwa waislam Allah atakusameheni na atawatieni peponi iwapo mkifa mkiwa waislam.Inshaallah
    Allah atuongoze sote inshaallah tuione haki na tuifuate.

    Like

    • Rich says:

      hapo mimi ninakushangaa ndugu mhamad kwa kukataasheria za torati ya Musa za jino kwa jino wakati ninyi siku zote mnasema kuwa sheria za torati ni sawa na zile zenu za quran. Hebu pia soma quran yako katika sura 5:45. Kwa hiyo basi, ni kweli kuwa biblia ni muongozo wa wakristo lakini huoni kuwa ile misingi ya sheria za jino kwa jino imerecodiwa na mtume wenu Mhamad hata katika quran yenyewe?!!….na kama ingekuwa sio lazima kutekeleza sheria za Mungu ili usilaaniwe, mbona sasa ninyi waislamu siku zote mmekua mkidai mahakama ya kadhi ili kuzitekeleza sheria hizo za Mungu ili msipate laana ya Mungu? Pia mbona sasa waislamu wenzenu huko uarabuni wanajitahidi kuzitekeleza sheria za jino kwa jino ili wasipate laana ya Mungu?….tafakari hayo ndugu.

      Like

  134. mhina says:

    ndugu mhamad, Mimi kwa imani yangu inayotoka ndani ya biblia,kamwe siamini kwamba, quruani ni “Kitabu cha muongozo kwa wanadamu” ila hicho ni kitabu cha muongozo kwa waislamu, kama ulivyothibitisha hata wewe mwenyewe.lakini tunaona kuwa, Biblia ni “kitabu cha muongozo kwa wanadamu wote”.Ndiyo maana pia hata hiyo quruani yenyewe inatambua hilo na kusema”MUNGU AMESHAFUNUA TORATI NA INJILI KWA AJILI YA KUWAONGOZA WANADAMU NA KWA AJILI YA KUTOFAUTISHA KATI YA JEMA NA BAYA.(quran al-imran 3:2-3).Hapo tumeona, kumbe quran ni ya waislamu lakini biblia siyo kitabu cha wakristo kama ndugu mhamad anavyotaka kutumaanisha ila biblia ni muongozo kwa ajili ya wanadamu wote.Kwa hali hiyo ndugu mhamad, ndiyo maana mimi siwezi kukukosoa kwa kutumia kitabu cha quruani bali ninatumia kitabu sahihi cha biblia, maana quruani siyo neno la Mungu bali ni maneno ya wanaadamu yaliyopatikana katika hali na mazingira ya kutisha mno mno”NAJIHOFIA NAFSI YANGU KUCHEZEWA NA MASHETANI YALIYONIZUGA AKILI YANGU”. Maneno hayo yalisemwa na muasisi wa kitabu hicho wakati kitabu hicho cha quruani alipokuwa amekipokea kule mapangoni!!.Halafu ndugu mhamad, kama ni kweli hivyo ulivyosema kwamba, biblia na maneno yake yote ni muongozo wa wakristo pekee…mbona wewe mwenyewe huko juu ya michango yako, pamoja na waislamu wenzako wengi mno tena mpaka viongozi wenu wa dini, mbona huwa mnatumia muongozo wa biblia pamoja na nabii Musa wa biblia kusema kuwa ile(kumbuk 18:18) ilimtabiri mtume wenu mhamad kuwa ndiye nabii atakaefuata?!!, kama hiyo haitoshi, bado waislamu pamoja na viongozi wao wa dini hutumia injili ya (yohana14:16,17) Wakidai kuwa huyo msaidizi,huyo roho wa kweli ndiye nabii wao mhamad, kuwa biblia kitabu tunachoambiwa na ndugu mhamad kuwa hakiwahusu wao lakini wanakiamini kuwa kimetabiri hivyo.je,hizo siyo imani tofauti na miongozo tofauti? Kwanini utabiri wa nabii Musa wa biblia kuhusu mtume wenu mnaukubali wakati sheria zake katika biblia hiyo hiyo mnadai kuwa haziwahusu!!!.au kuna Musa mapacha wa kiislamu na wa kikristo katika biblia yetu?,Hapo tumeona jinsi waislamu wanavyoendelea kutofautiana wenyewe kwa wenyewe, na hii ni kwa sababu ya ile laana ya kuchanganya changanya maandiko ya imani tofauti.Ukweli ni kwamba, kitabu cha quruani hakijitoshelezi halafu pia, sio neno la Mungu.Masheria wanayoyafuata ni ya mhamad mwenyewe, ndiyo maana alivyogundua mambo ni magumu, akawafukuza waislamu wote kwenye dini yake kwa kuwaambia”NENDENI MKAWAULIZE WENYE KUMBUKUMBU ZA VITABU VYA MWENYEZI MUNGU VYA KALE IKIWA NINYI HAMJUI !!!!!!.Soma(quran 16:43).Kumbe mlishashauriwa na muasisi wenu mjifunze kutoka kwetu, sasa kelele za ubishi za nini??….Mwisho nimalizie kuhusu lile somo la mchungaji wetu bwana yesu ambaye yeye baada ya kifo chake….alifufuka siku ya tatu, ambapo hayupo tena kaburini.Yeye anaishi na pia ataishi na sisi milele na milele ambapo hata mtume mhamad wa waislamu anasubiri afufuliwe na bwana yesu hiyo siku ya mwisho.Ukweli ni kwamba, ule mfano wa mchungaji mwema, nilimuandikia ndugu yangu mhamad baada ya kumgundua kuwa ni mzito wa kuelewa mambo au anajifanya haelewi ili ailinde dini yake iliyokwisha kufa ili isife.Huko juu ya michango yandu nilielezea vizuri tu, kimaandiko kile alichokifanya bwana yesu, lakini ndugu mhamad anajifanya hakuelewa hata jambo moja halafu eti anajifanya anakuja kishangaa hicho kimfano cha mchungaji mwema!!.Nilikwisha sema huko juu kwamba injili ni “mungu ndiye anaetoa kwa ajili yetu njia ambazo hata tukifa katika ulimwengu wa mwili anakuja tufufua kama washindi ili tuishi nae katika ulimwengu wa roho, kwa kuwa ulimwengu huu wa mwili ni wakupita tu, lakini katika ulimwengu wa roho tutafufuliwa na kuishi milele, ndiyo maana hata bwana yesu ijapokuwa alikufa kimwili lakini siku ya tatu akafufuka kama mshindi wa mauti ili atutangulie na kutusubiri katika uzima wa milele.Mimi ndugu mhamed niishie hapa kwa sababu naona unarudia mambo ambayo nilikwisha yatolea majibu huko juu.Usichelewe kuja kwa bwana yesu ndugu.

    Like

  135. mhina says:

    ndugu mhamad.Mimi nawashangaa nyinyi waislamu….kama mnasema kuwa manabii wa zamani wakina daudi,suleman,Musa,bwana yesu nk, walikuwa waislamu…mbona sasa walitumia torat,zaburi,injili, ambavyo ni vitabu vya biblia takatifu ya wakristo???!!!……je, hivi ndani ya biblia kuna mambo ya waislamu au wakristo??!!…..wewe si ulituambia kuwa vitabu vya biblia ambavyo ni torat, zaburi na injili ni vitabu vya muongozo kwa ajili ya wakristo pekee sasa, kama mitume wa zamani walitumia vitabu vyetu hivi vya kikristo, huo uislamu wao mnaoutaja ulitokea wapi??….hebu nijibu hapa kama kweli nyie mnajua kuchezea akili za watu.

    Like

  136. Mohamed Ally says:

    itakuwa ni jambo zuri watu wakafahamu ipi imani ya kweri kati ya uislam na ukristo

    Like

  137. Ndugu Mhina,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah sub-hana wata’ala aliyenipa uhai na afya na kunijalia niweze kuwaelimisha ndugu zetu Wakiristu na kuwatoa kwenye giza na kuwaleta kwenye nuru ya uislamu.

    Baada ya shukrani hizo, nataka kumpa majibu ya mambo yanayomtatiza ndugu Mhina kwa kifupi kadri Allah atakavyonijalia. Naomba nikunukuu ndugu yangu kama ilivyo ada.
    HOJA YAKO:”ndugu mhamad, Mimi kwa imani yangu inayotoka ndani ya biblia,kamwe siamini kwamba, quruani ni “Kitabu cha muongozo kwa wanadamu” ila hicho ni kitabu cha muongozo kwa waislamu”

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina, mbona unaendelea kuwaaibisha wakiristu wenzako ndug yangu, Unasema huamini kuwa quran ni mwongozo wa wanadamu bali ni mwongozo kwa waislamu kama nilivyokunukuu hapo juu, hivi naomba nikuulize, kwani waislamu siyo wanadamu????????????
    Lakini pia umesema biblia ni mwongozo kwa wanadamu, hivi samahani ndugu yangu unaweza kunionesha andiko ndani ya biblia linalosema “biblia ni mwongozo wa wanadamu”. Hakika biblia yenyewe haisemi hivyo sasa wewe kwa nini unapenda kujibu maswali kiujanja.Kwa nini unapenda kujitungia majibu?hii ni kwa sababu unajua kuwa biblia yako mwenyewe haijitoshelezi.
    Ndugu Mhina, Naomba ujue biblia si mwongozo kwa wanadamu kwa sababu yenyewe haisemi hivyo, bali nyie wakiristu ndio mnaitumia kama mwongozo wenu ingawa yenyewe haiwatambui na pia yenyewe haisemi sehemu yoyote kuwa mfanye hivyo.
    Ni kweli kabisa quran ni mwongozo kwa waislam ambao ni binadamu pia na kama quran yenyewe inavyosema:
    Quran sura Baqra
    2. Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni mwongozo kwa wachamungu(waislam),
    3. Ambao huyaamini ya ghaibu na hudumisha Sala, na hutoa katika tuliyo wapa(sadaka).
    4. Na ambao wanayaamini yaliyo teremshwa kwako(Muhammad), na yaliyo teremshwa kabla yako;
    na Akhera wana yakini nayo.
    5. Hao(waislam) wapo juu ya uwongofu utokao kwa Mola wao Mlezi, na hao ndio walio
    fanikiwa.”

    Kwa hiyo ndugu yangu, quran haikuongozi wewe kafiri, Hapana! Quran ni mwongozo kwa mtu aliyeamuamini Allah na Mtume, akashika sala na akatoa zaka na sadaka na akafanya matendo mema.

    Tukirudi kwa upande wa wakiristu ni lazima Quran yenyewe ituambie imekuja kuwafanyia nini wakiristu! Hebu tuiulize na itupe jibu!
    QURAN SURA YA 18 AL-KAHF
    1. Kuhimidiwa ni kwa Mwenyezi Mungu, ambaye amemteremshia mja wake Kitabu, wala
    hakukifanya kina Kasoro.
    2. Kimenyooka sawa, ili kitoe onyo kali kutoka kwake, na kiwabashirie Waumini
    watendao mema kwamba watapata ujira mzuri.
    3. Wakae humo milele.
    4. Na kiwaonye wanao sema: Mwenyezi Mungu ana mwana.
    5. Wao hawana ujuzi wa jambo hili, wala baba zao. Ni neno kuu hilo litokalo
    vinywani mwao. Hawasemi ila uwongo tu.

    Ukisoma kwa umakini iyo aya ya nne(4), utagundua kuwa quran ni kitabu kilichokuja kuwaonya nyie wakiristu mnaosema Mungu ana mtoto. Kwa hiyo ndugu yangu quran ni mwongozo kwa wachamungu yaani waislamu na ni maonyo kwa wanaosema mwenyezimungu ana mwana Yesu yaani wakiristu wanaosema Yesu ni mwana wa Mungu.Kiwaonye muache kauli hizo.Sasa vipi ndugu Mhina unashindwa kuelewa wapi nikusaidie ndugu yangu!!!Quran inajieleza yenyewe na wala siyo kama biblia ambayo inahitaji mtu wa kuisaidia kuongezea maelezo.

    HOJA YAKO NYINGINE: “pamoja na nabii Musa wa biblia kusema kuwa ile(kumbuk 18:18) ilimtabiri mtume wenu mhamad kuwa ndiye nabii atakaefuata?!!, kama hiyo haitoshi, bado waislamu pamoja na viongozi wao wa dini hutumia injili ya (yohana14:16,17) Wakidai kuwa huyo msaidizi,huyo roho wa kweli ndiye nabii wao mhamad, kuwa biblia kitabu tunachoambiwa na ndugu mhamad kuwa hakiwahusu wao lakini wanakiamini kuwa kimetabiri hivyo.je,hizo siyo imani tofauti na miongozo tofauti?”

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina, Nashukuru sana kwa swali hili, kwa maana huwa linawatatiza wakiristu wengi. Kwanza kabisa naomba uelewe kwamba sisi waislamu huwa tunayachukulia maneno yoyote yale kutoka katika kitabu chochote kile kuwa yapo sahihi endapo tu hayapingani na maneno ya Allah ndani ya Quran, maneno hayo huwa tunayachukulia kuwa ni ya kweli kabisa.
    Katika biblia pia tunaamini kuwa yapo baadhi ya maneno ya kweli aliyoyasema Bwana Yesu lakini tu endapo maneno hayo hayapingani na quran kwa sababu quran ni ufunuo kutoka kwa Mungu mwenyewe na biblia ni maneno ya waandishi mbali mbali waliosikia kutoka kwa watu na wenyewe wakaandika kwa ushahidi zaidi soma (luka 1:1-4).Hivyo basi kama maneno yapo kwenye biblia na yanapingana na Quran basi maneno hayo hatuyaamini.
    Kwa hiyo basi, kwa nyie mnaotumia biblia kama mwongozo na mnaiamini ingawa yenyewe haiwatambui ni vema muutumie mwongozo huo uwalete kwenye Nuru ya Uislam.Na ni kweli kabisa hiyo (Yohana 14:16-17) ni kweli kabisa inamtabiri Mtume Muhammaad kwa sababu haipingani na maneno ya quran.Lau kama Yohana 14:16-17 ingepingana na maneno ya Allah kwenye quran basi tusingeiamini.

    HOJA YAKO TENA:” Mwisho nimalizie kuhusu lile somo la mchungaji wetu bwana yesu ambaye yeye baada ya kifo chake….alifufuka siku ya tatu…”

    JIBU LA HOJA: Sasa ndugu Mhina kama simba alimtafuna mchungaji wenu na kumuua kwa siku tatu, hivi hao kondoo, si alikuta washapotea kweli kwa maana siku tatu ni nyingi mno kwa kondoo kubaki bila mchungaji.Huyo mchungaji wenu alimezwa na shetani kwa siku tatu bila kupumua! Je huoni kwamba shetani alimzidi nguvu huyo mchungaji kwa siku tatu mfululizo! JE Kama mchungaji amekuwa dhaifu kiasi hicho mbele ya shetani(simba) je itakuwaje kwa kondoo!Ndugu zangu wakiristu hebu tumieni tu walau hata akili ya mtoto wa chekechea, hamuoni kuwa mpo kwenye upotovu uliopitiliza?
    Tena shetani huyo hakuanzia hapo ndgu yangu maana tukisoma katika Matayo tunaona ni jinsi gani shetani alivyomburuta yesu nyikani kwa siku saba mfululizo bila kujitetea akipelekwa huku na huku akihojiwa maswali mbalimbali! Je wakati huo kondoo walibaki na nani ndugu yangu? Sasa Ndugu yangu Mhina, mbona biblia yenu inampa nguvu sana shetani kuliko mchungaji yesu!!!? Tafakari bado nafasi mnayo!

    SWALI LAKO: “ndugu mhamad.Mimi nawashangaa nyinyi waislamu….kama mnasema kuwa manabii wa zamani wakina daudi,suleman,Musa,bwana yesu nk, walikuwa waislamu…mbona sasa walitumia torat,zaburi,injili, ambavyo ni vitabu vya biblia takatifu ya wakristo???!!!……”
    JIBU LAKO: Ndugu Mhina,hebu naomba kwanza ujue unachokiongea usiwe unakurupuka tu na kuandika bila kuelewa unachokiandika.Taurat,zaburi na injili ni vitabu vilivyokuwepo kabla ya wakiristu na si vitabu vya wakiristu kama unavyosema na nina uhakika nikikuuliza uthibitishe utashindwa, hata biblia yenyewe inathibitisha hivyo ukisoma Katka (matendo 11:25) utaona kuwa watu wa kwanza kuitwa wakiristu walipatikana hapo antiokia ambayo ni Uturuki kwa sasa. Na hivyo vitabu mlivyo navyo kwenye biblia yenu siyo taurat,zaburi wala injili bali ni baadhi tu ya maneno yaliyokuwa ndani ya vitabu hivyo ndiyo yapo kwenye biblia. Hebu unioneshe ni andiko gani linalosema Daudi, Ibrahim au Suleimani walikuwa wakiristu. We ndugu yangu vipi? Lakini quran inatuambia hivyo kuwa hao wote walikuwa waislamu na nimeshakupa aya nyingi za quran zinazosema hivyo huko juu sasa unachokataa ni nini ndugu yangu?Mbona biblia yako inashindwa kujitetea kuwa walikuwa wakiristu wewe ndo unaisaidia ndugu yangu? Biblia inatakiwa kukusaidia wewe siyo wewe uisaidie.
    Allah akusaidie ndugu yangu kwa kuwa unapenda kujifunza, akusaidie uione haki na uifuate na akujaalie uingie katika nuru ya uislamu Inshaallah.

    Like

    • Rich says:

      hatujasema kuwa wakristo ndio walioanzisha na kuandika vitabu vya torati zaburi na injili ila point hapo ni kwamba, misingi ya vitabu hivyo vya kidini vya Mungu kupitia manabii wake ndivyo vimekuwa msingi wa dini na njia ya wakristo sawa sawa na manabii wale wa mwanzo. Kwa hali hiyo, swali litabaki palepale kuwa, wale manabii wa zamani huo uislamu wao ulitoka wapi? Kama waislamu wanavyotaka kutudanganya!!!…je, vitabu vya torati, zaburi na injili vinatumika na waislamu au wakristo leo hii? Acha kujibu maswali kwa hila na ujanja wa kiongo. Pia kama ni kweli kuwa vitabu vya torati, zaburi na injili katika biblia yetu ni vya uongo…hebu ninyi waislamu tuonyesheni hivyo vyakwenu vilivyo sahihi lakini hatutaki kuonyeshwa hadithi za uongo za kutunga kutoka kwenye quran.

      Like

  138. mhina says:

    Ndugu,Mhamad…Mimi napata tabu kwako, kwa kuwa wewe unaonekana hujakomaa kifikra!!, bado ni mchanga wewe, hujui kitu…au kama ni kweli kuwa hiki ni kiwango chako cha ufahamu wa mambo ya kiimani basi hiyo njia yako ya quruani itakua inakufubaza akili zako….Nianze kwa kusema kwamba ni kweli kuwa waislamu ni wanadamu, lakini tunapozungumzia suala la imani, tunatambua kuwa, sio wanadamu wote kuwa ni waislamu.Hapa tunazungumzia suala au kipengele cha imani au “HAO WALIOUKUBALI HUO UISLAMU”. Pia utaona kuwa tunaposema “biblia ni muongozo wa wakristo” hapo tutakuwa tunazungumzia “wakristo, yaani”hao walioukubali huo ukristo” lakini tunaposema “biblia ni muongozo wa watu wote” hapo tunawazungumzia watu wote kabisa,hata wapagani wanatakiwa waifuate biblia ili iwaongoze.Sasa kwa hali hiyo pia, utaona kwamba, unaposema quran ni kwa ajili ya waislamu, basi utaona kuwa unazungumzia jamii ileile ya kiislamu iliyosilimishwa na dini hiyo ya kiislamu na kamwe sio muongozo wa watu wote. Halafu wewe unasema kuwa biblia sio muongozo wa wanadamu wote kwa kuwa haisemi hivyo!!….jibu: biblia imethibitisha mara nyingi mno kuwa ni muongozo kwa ajili ya watu wote.biblia inasema kuwa “WALA HAKUNA WOKOVU KATIKA MWINGINE AWAYE YOTE KWA MAANA HAKUNA JINA JINGINE CHINI YA MBINGU WALILOPEWA WANADAMU LITUPASALO SISI KUOKOLEWA KWALO. (matendo 4:12). Ni jina la bwana yesu pekee ndilo liwezalo kuwaokoa wanadamu wote, hakuna jina jingine chini ya jua.Pia yeye mwenyewe alisema” mimi ndimi njia na kweli na uzima, mtu haji kwa baba ila kwa njia ya mimi.soma(yohana 14:6)…Lakini kubwa kuliko zote, nimegundua kumbe uislamu ni dini ya ajabu na vichekesho mno mno mno…ngoja ndugu mhamad nikunukuu ulivyosema”SISI WAISLAMU HUWA TUNAYACHUKULIA MANENO YEYOTE YALE KUTOKA KATIKA KITABU CHOCHOTE KILE KUWA YAPO SAHIHI ENDAPO TU, HAYAPINGANI NA MANENO YA ALLAH NDANI YA QURAN, MANENO HAYO TUNAYACHUKULIA KUWA NI KWELI KABISA”. Mwisho wa kukunukuu. Jamani…jamani…jamani!!!!, kama ni kweli uislamu uko hivyo kama anavyotuambia ndugu mhamad, basi itakuwa kumbe wanaopotea, wanapotea wao wenyewe kwa upumbavu wao wa kukosa maarifa, sijawahi kulijua hilo, ni ajabu kwelikweli!!!!!!.Ukweli kutoka moyoni mwangu, sijawahi kusikia dini ya ajabu na vituko kama uislamu!!.Kaka mhamad, unasema ukweli au umechanganyikiwa kidogo??!!….kama ni hivyo kweli basi tena, quran sio neno la Mungu kaabisa kabisa bali ni maneno ya wanadamu yanayosaidiana na maneno ya wanadamu wowote wale ili kulinganisha maandiko na kutafuta usahihi, Mimi kwa upande wangu hainishangazi sana maana nilijua na kuamini hivyo, tangu zamani sana ila kilichonishangaza ni kuona kuwa kumbe quran yenyewe inafundisha hivyo waziwazi, halafu kumbe waislamu wenyewe wanalijua hilo na kulikubali!!!!!…Mungu wangu Mungu wangu, poleni sana ndugu zangu. Allah yeye hayaamini maneno yake mwenyewe kwa kuwa”HAYAJITOSHELEZI”…Hivyo ametoa ruhusa kwa waislamu wakatafute maneno duniani popote, tena kwa mtu yeyote halafu wanakuja yalinganisha na yale ya Allah katika quran waone kama yanakubaliana…yakikubaliana ndipo uhakika wa neno takatifu la Allah unakubali na yale maneno mapya ya wanadamu kuwa nayo pia yanastahili.Hii maana yake ni kwamba neno la Allah katika quran halijaweka mipaka yake, hivyo basi, waislamu wakienda kwa wakristo na kuchukua ile(kumbuk 18:18) na ile (yohana 14:16) pamoja na maelezo yake yote, halafu tukayapachika ndani ya quruani ili iwaongoze waislamu, inakuwa sio kosa kwa mujibu wa Allah kwa kuwa maandiko hayo yanakubaliana na maneno ya Allah anavyotaka, hivyo, maneno hayo yanakuwa ya “KWELI KABISA KWA MUJIBU WA UTARATIBU WA ALLAH!!!. Ngoja nikuwache hapo. Kuhusu somo la mchungaji ndugu mhamed, nakuomba urudi tena kule mwanzo kabisa ili ukajifunze zaidi kile alichokifanya bwana yesu kimaandiko kwa ajili yetu.Naona unarudia kuhoji mambo kama vile ndio tunaanza mjadala wakati maelezo ya huko juu, ukichanganya na michango mbalimbali niliyochangia basi, ungekuwa umekwishanielewa nilichotaka kukielezea kwa mfano huo wa mchungaji mwema…..Mwisho kabisa ni jibu lako la lile swali langu lililohusu Manabii wa nyuma.kwa ufupi ni kwamba, swali lile limekushinda!!…hapa, mimi nitakusaidia wewe pamoja na waislamu wenzako wote ili mjionee wenyewe jinsi dini yenu ilivyowapotosha!!, pia jinsi mtume wenu kipenzi kutoka uarabuni alivyowapotosha!!!…ndiyo maana hata nyinyi wenyewe mnajaribu kutetea mambo msiyoyajua masikini……… Ndugu mhamad, ukweli ni kwamba, nyakati za mwanzo, hakukua na manabii waislamu wala manabii wakristo. Wakati ule wa mwanzo, Mungu alimuongoza nabii Musa kuandika torati pamoja na vile vitabu vitano vya mwanzo. Zaburi akapewa daudi,wakaja manabii na mwisho kabisa akamalizia bwana yesu na injili. Hivi ndivyo vitabu vya asili vya Mungu wa kweli anaepaswa kuabudiwa pekee, katika historia yetu yote sisi wanadamu. Manabii wote hao wa nyuma, walikaa kwenye mahekalu yao na masinagogi yao ya asili, wakitumia vitabu hivi vya biblia kuwa muongozo wao. Bwana yesu ambaye ndiye aliyekuwa wa mwisho, kazi yake kubwa ilikuwa ni moja tu, “KUTIMIZA ZILE AHADI ZA MUNGU ZILIZOMO NDANI YA VILE VITABU VYA MWANZO VYA MANABII”.Soma(mathayo 5:17) linganisha na (luka 24:44). Baada ya bwana yesu kukamilisha kazi hiyo….ndipo akaachia injili ya Mungu kwa ajili ya watu wote. vile vitabu vya mwanzo vya manabii, vikabaki kuwa msingi wa wale wote wanaofuata injili ya bwana yesu, ili viwasaidie wajue kule walikotoka. Zaidi ya hapo kwenda mbele, injili ya bwana yesu ilianza kuhubiriwa israel kwanza halafu ikaja ulimwenguni kote.Wakristo ni wafuasi au wanafunzi wa bwana yesu, yaani ni wale waliompokea na kumuamini.Biblia inasema “TORATI NA MANABII, VILIKUWEPO MPAKA KIPINDI AMBACHO YOHANA MBATIZAJI ALIKUJA, NA TANGU WAKATI HUO ALIPOKUJA YOHANA MBATIZAJI MPAKA LEO HII “HABARI NJEMA ZA UFALME WA MUNGU ZINAHUBIRIWA”.Soma(luka 16:16). Kwa hali hiyo, ni kweli kabisa ndugu mhamad kama ulivyosema kuwa kulikuwa na wakristo wa kwanza kwenye ile (matendo 11:25), kwa kuwa ni lazima kuwe na wakristo wa awali kwanza, halafu ndio waongezeke mpaka kufikiwa sisi wa mataifa. Sisi wakristo ndio tumekuwa warithi wa maagano yote ya Mungu ambayo yanaonekana katika biblia takatifu(torati,manabii,zaburi,injili). Sisi tunaonekana tukiwa ndani ya jengo lile lile la awali la manabii wa Mungu, ambapo tumeona kuwa ni jengo ambalo Mungu mwenyewe alilianzisha enzi na enzi. Kwa hali hiyo, tunakuwa na haki kabisa ya kuwaita manabii wa mwanzo “MABABU ZETU au “WAKRISTO WENZETU”….Maana wote sisi, pamoja na wao tupo katika jengo moja la Mungu tukiunganishwa na bwana yesu mwenyewe, ndiyo maana biblia inatuambia “MMEJENGWA JUU YA MISINGI YA MITUME NA MANABII, NAYE KRISTO YESU MWENYEWE NI JIWE KUU LA PEMBENI, KATIKA YEYE, JENGO LOTE LINAUNGANISHWA VEMA NA KUKUA HATA LIWE HEKALU TAKATIFU KATIKA BWANA, KATIKA YEYE NYINYI MMEJENGWA PAMOJA KUWA MASKANI YA MUNGU KATIKA ROHO”.!!!!!. Soma (waefeso 2:20-22). Na kwa sababu bwana yesu ndiye nabii wa mwisho wa Mungu, Pia kwa sababu jengo hili la Mungu ni kubwa na lenye thamani, basi yule wa mwisho ni lazima akae mlangoni ili kuhakikisha wote wanaotaka kuurithi uzima wa milele wanapitia kwake. Hivyo bwana yesu akatangaza hivi: “MIMI NDIMI MLANGO, MTU AKIINGIA KWA MIMI “ATAOKOKA”.Soma(Yohana 10:9). “Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiisha vitu vyote, ili kwamba “MUNGU AWE YOTE KATIKA WOTE.Soma(1wakorintho 15:28). Hitimisho: ndugu mhamad, nafikiri umeona kwa uwazi kabisa njia ya kweli jinsi ilivyo wazi wazi pasipo maandiko kubabaisha babaisha watu wake. Hii ni tofauti kubwa sana ukilinganisha na dini yenu ya kiislamu. Alichokifanya mtume wenu mhamad ni kuja kuvamia mambo ambayo alikua hayaelewi vizuri.Kama wewe msomi wa leo hii unapata tabu ya kupambanua ukweli wa mambo, je, kwa mtu asiye soma kwa wakati ule unafikiri ni kwa nini asibebwe na malaika wa giza mwenye nguvu za giza?….malaika hawa waovu hukimbilia nafsi ya mtu na akili za mtu ili kumvuruga mhusika asijitambue, lakini pamoja na hayo mhamad alipata fahamu ya kilichomtokea kule mapangoni ambapo kwa kawaida mashetani hukaa kwa wingi…NAJIHOFIA NAFSI YANGU KUCHEZEWA NA MASHETANI NA KUNIZUGA!!!….Ndipo akaanza kuyasilimisha majini hayo ili yawe waislamu apate kuabudu nayo…tena jambo la kusikitisha, kwa kawaida sura za maandiko zinaonyesha jina la huyo muhusika alieandaa ujumbe huo, kwa mf:torati> Musa, injili > bwana yesu….lakini chakusikitisha ni kwamba kwenye quran kwa kuwa majini na mashetani ndiyo yaliyoandaa, basi utasikia…SURA YA MAJINI.!!. Ndugu mhamad. Njooni kwa bwana yesu angali kweupe ndugu zangu. Wewe unaonekana kuwa bado ni mchanga katika mambo haya ya imani…kwa hiyo basi, mimi naishia hapa.Sita jibu kwa sasa hoja zako kwa kuwa naona unarudia yaleyale.Mungu akujalie wewe na waislamu wenzako”MUIJUE KWELI ILI IPATE KUWAWEKA HURU. Kwaheri ndugu yangu mhamed yohana.

    Like

  139. Ndugu Mhina,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah subhanahu wata’aala, aliyemtuma mtume wake wa kweli ili wanadamu tupate kufaulu siku ya mwisho.

    Ama baada ya shukrani hizo naomba nizijibu hoja za Ndugu yangu Mhina, kwa sababu kijana huyu ana moyo wa kujifunza na kutaka kujua kwa sababu maskini ufahamu wake wa mambo ya kiroho bado ni mdogo kama alivyothibitisha yeye mwenyewe huko juu hivyo ni vema tumsaidie kijana wetu ili siku ya mwisho Allah atakapomuuliza kama quran inavyotwambia hapa chini.

    QURAN SURA MULK.
    “6. Na kwa walio mkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jahannamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo!
    7. Watakapo tupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka.
    8. Inakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara likitupwa kundi (La watu)humo walinzi wake huwauliza: Kwani hakukujieni mwonyaji?
    9. Watasema: Kwani! Ametujia mwonyaji, lakini tulimkataa, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote. Nyinyi hamumo ila katika upotovu mkubwa!
    10. Na (watu wa motoni)watasema: Lau kuwa tungeli sikia, au tungeli kuwa na akili, tusingeli kuwa katika watu wa Motoni! »

    Kwa hiyo ndugu yangu Mhina, siku ya kiyama ukiulizwa kwani hakukujia mwonyaji ? bila shaka utakiri kuwa nilikujia na nikakuonya na nikakufundisha basi hukutaka kusikia, basi ukisikia na ukafuata itakuwa heri kwako ndugu yangu.

    Baada ya kunukuu aya hizo za quran naomba ndugu Mhina uelewe kuwa vitabu vyote duniani, maandishi yoyote yale ,hakimu wake ni quran hivyo quran ndicho kitabu pekee kinachoweza kuthibitisha ukweli au uongo wa jambo flani au wa maandishi flani.Hivyo basi maandishi yoyote yanayopingana na quran hayo ni ya uongo na hayana asili ya Mungu ndani yake.
    Nitakupa mifano katika hili kwa sababu hata Yesu inasemekana alifundisha kwa mifano kwa sababu watu walikuwa na vichwa vizito :
    Mathalan, Biblia au kitabu chochote kile kinaposema Yesu alitundikwa msalabani na kufa kifo cha laana kama wezi na wanyang’anyi, Ili mimi muislamu nithibitishe shutuma hizo ni lazima nirudi kwa hakimu wangu quran na nimuulize je ni kweli jambo hili au ni uzushi, quran ikinambia ni kweli mimi nakuwa sina hiari ya kukataa lakini quran ikiniambia ni uongo sina haki ya kusema ni kweli pia.
    Au Biblia au kitabu chochote kile kinaposema Yesu ni Mungu, ni lazima kwanza nirudi kwa mwongozo wangu niulize je ni kweli Yesu ni Mungu au ni uongo ? Quran inaposema ni uongo mimi sina hiari ya kukataa.na lazima mimi kama muislamu nitambue kuwa maneno hayo ni uongo kwani yanapingana na Maneno Ya Allah.
    Lakini kwa upande mwingine Allah anaposema mathalan kula nguruwe ni haramu, halafu na biblia au kitabu kingine chochote kikasema hivyo, basi lazima niamini kuwa maandishi ya kitabu hicho ni ya kweli kwa sababu hayapingani na kweli ya Allah ndani ya Quran.
    Kwa hiyo ndugu Mhina, Allah ndani ya quran anapotuambia kuwa Yesu alitabiri kuwa atakuja Mtume Muhammad(S.A.W) na nikafunua kitabu chochote kile nikaona Utabiri wa Yesu kuhusu Nabii Muhammad mimi muislamu sina hiari ya kusema maneno hayo ni ya uongo na ili hali hayapingani na maneno ya Allah.
    Sasa ndugu Mhina hebu naomba uniambie hapo hujaelewa wapi ndugu yangu nikusaidie !hebu nambie ndugu yangu niko tiyari kabisa kukusaidia ili siku ya mwisho usije ukapata adhabu ya moto wa jehannam ndugu yangu.

    HOJA YANGU : Ndugu wakiristu wote, ndugu wana-forum wote ndugu waislamu mabibi na mabwana, nimewaita nyoote ili mshuhudie uwongo wa kijana wenu Mhina ambaye wakiristu wamemwamini na kumtuma anavyowatia aibu jamani.Naomba kwa makini kabisa mzisome hoja mbili za Ndugu yenu Mhina nilizonukuu hapa chini halafu kisha mtafakari ;

    HOJA YA KWANZA: « Ndugu mhamad, ukweli ni kwamba, nyakati za mwanzo, hakukua na manabii waislamu wala manabii wakristo »

    HOJA YA PILI : Kwa hali hiyo, tunakuwa na haki kabisa ya kuwaita manabii wa mwanzo “MABABU ZETU au “WAKRISTO WENZETU”….

    Baada ya kuzitafakari hoja hizo, mtajigundua ni jinsi gani wakiristu mnavyotapatapa kwa kukosa uhakika na dini yenu. Hoja ya kwanza anasema hakukuwa na nabii mkirisito yoyote hapo mwanzo, lakini hoja ya pili anakula matapishi yake mwenyewe kwa kusema manabii wa mwanzo walikuwa wakiristu wenzao.Sasa ndugu Mhina ni lipi jibu sahihi kati ya hayo mawili ndugu yangu.Mbona unataka kula kotekote mbele na nyuma kama nge ??? vipi mbona unatapatapa ndugu yagu ?yaani huku hauko na kule hauke maana kote ni kumekuwa kwa moto.
    Kwa bahati mbaya kabisa hawezi kuiuliza hata biblia yake, kwa sababu anajua kuwa biblia yake haitampa jibu hivyo anaamua kujitungia ka-biblia kadogo kutoka kichwani ! Sasa ndug yangu kweli kama biblia ni mwongozo wako kwa nini isikwambie mababu zako akina Suleiman, Ibrahim, Yakobo , Isack, Yesu, walifuata dini gani ili na wewe uwafuate ndugu !!

    Kwa upande wetu sisi waislamu hatuna shida kabisa quran iko wazi 100% inatuambia kuwa akina Yesu, Ibrahimu, Isack, Suleiman woote walikuwa waislamu na sisi tunaishi kwa kufuata mienendo yao na tunapita njia ile ile ya Uislamu waliyopita wao !

    Je ndugu wakiristu mnataka kujua mababu zenu walifuata dini gani kuelekea mbinguni ? Hebu soma baadhi ya aya zifuatazo ndani ya quran tukuf :

    QURAN SURAT AL-BAQRA.
    130. Na nani atajitenga na mila ya Ibrahim isipo kuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini Sisi tulimteuwa yeye katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema.
    131. Na Mola wake Mlezi alipo mwambia: Silimu, Nyenyekea! Alinena: Nimesilimu, nimenyenyekea kwa Mola wa walimwengu wote.
    132. Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu.
    133. Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake. »

    Tukisoma biblia( matendo 11 :25) inatwambia Wakiristu wa kwanza walipatikana Antiokia miaka mingi kabisa baada ya Yesu, Musa na manabii wote wa mwanzo !Sasa ndugu yangu andiko hilo huwa hulioni ?mbona unajifanya hamnazo kaka ?Paulo alianzisha ukiristu baada ya Yesu kuondoka duniani.
    Ndugu Mhina mimi Napata mashaka sana kama huwa unatenga muda walau kidogo na kusoma biblia maana ungekuwa unafanya hivyo ungeshajua kuwa ukiristu ni dini ya kipagani iliyokuwepo huko Rumi ya Antiok soma ufafanuzi wa (Matendo 11:25) chini ya ukurasa huo wa biblia utapata maelezo mazuri kabisa.Paulo akakopi na kupaste.

    Ndugu Mhina, Naomba nimalizie na sura ifuatayo katika quran;

    QURAN SURA YA 3 AL-IMRAN
    “20. Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea
    Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na
    wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi
    juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake. »

    kwa hiyo ndugu Mhina mimi nimeusilimisha uso wangu kwa Allah, je wewe umeslimu, ukisilimu umeongoka aidha ukikengeuka ukakataa mimi ni juu yangu kufikisha tu na Allah ni mwenye kuniona .
    Mwisho naomba usome ndugu yangu na utafakari, yasije mauti yakakukuta bado upo katika hali ya ukafiri.Allah akutoe kwenye giza akulete kwenye mwanga Inshaallah.

    Like

  140. mhina says:

    Ndugu.Mhammad, unaonekana bado unahamu ya kusaidiwa. Hilo ndilo tatizo lako, yaani unajikaza kutetea dini ambayo ulikuwa unaiamini miaka mingi, matokeo yake sasa, baada ya wewe kugundua ukweli “UNAJISIKIA KUFAKUFA”!!.Mimi ninakushauri kuwa usikate tamaa kwa kuwa bado mlango upo wazi kwa ajili yako………Mimi nikuulize hivi: kama ni kweli unavyosema kuwa, quran inajitosheleza katika maneno yake, tena ni neno la kweli la Mungu, kwanini Allah amewapa tena kazi ya kupekua pekua vitabu vya imani ya kikristo ili mtafute yale maandiko yatakayo fanana na neno lake katika quran?…je, inamaana Allah hajiamini?. Hebu msikilize wewe mwenye mtume wako mhamad jinsi anavyo waamuru nyinyi waislamu kutafuta msaada kwenye vitabu vya wakristo: “NENDENI MKAWAULIZE WENYE KUMBUKUMBU ZA VITABU VYA MWENYEZI MUNGU VYA KALE IKIWA NINYI HAMJUI!!!!!. Soma(quran 16:43). Haya ni maajabu kwelikweli, kitabu badala kiwasaidie waumini wake, kinatoa ushauri kwa waumini hao kwamba watafute ukweli kwenye vitabu vya wakristo. Sasa kama ni kweli vitabu hivyo vya kale vilichafuliwa, hivi mtume wenu angeweza kuwapa ushauri huo kweli?!!…mbona hutumii akili yako vizuri ndugu.mhammad!!. Hapo utagundua kuwa, wakulaumiwa sio mtume mhamad ila wakulaumiwa ni nyinyi waislamu msiotaka kuupokea ushauri wake, ndio maana pia, kuna andiko aliwaonya hivi: “MSISHINDANE NA WATU WALIOPEWA KITABU KABLA YENU.!!!. Hebu sasa niendelee kumalizia kukusaidia lile somo la manabii wa zamani, maana inaelekea ulinielewa vyema sana, lakini uliona kuwa ukikubali hivyo mbele za wana blog, basi itakuwa ni aibu kwako na kwa dini yako kwa ujumla. Lakini mimi naamini kuwa hapo kamwe hapakwepeki….Ndugu mhamed, nianze kwa mara nyingine kukuonya kuwa, kamwe usipende kuandika mambo ya uongo mbele za macho ya watu kwa kuwa unapofanya hivyo, unajiaibisha wewe pamoja na hiyo dini yako unayoiamini…..Mimi sikusema manabii wa zamani walikuwa wakristo wenzetu kwa kuwa nilifahamu wazi kuwa kipindi ambacho manabii hao, yaani wakina Ibrahimu,Musa, Daudi nk, waliishi, ilikuwa , injili ya bwana yesu iletayo ufuasi wa ukristo, bado haijakamilika, lakini nilichosema mimi ni kuwa “TUNA HAKI YA KUWAITA WAKRISTO WENZETU AU MABABU ZETU”….Kwa kuwa ndiyo kazi aliyoifanya bwana yesu kuunganisha watu wote wawe mmoja au jamii moja mbele za Mungu, ndiyo maana bwana yesu anaitwa “Baba wa amani” kwa kuwa, tumepoke neema na baraka za Mungu ndani yake, ndiyo maana, neno la Mungu linasema”NA KAMA NINYI NI WA KRISTO, BASI MMEKUWA UZAO WA IBRAHIMU, NA WARITHI SAWASAWA NA AHADI.Soma(galatia 3:29). Ili tuelewe vizuri hapa, inatupasa kuikumbuka hiyo ahadi ya ibrahimu aliyopewa na Mungu tangu mwanzo. Mungu alimuahidi Ibrahimu baba yetu, hivi:”UTAKUWA BABA WA MATAIFA MENGI”.Soma(mwanzo 17:4). Lakini pamoja na kukujibu hivyo ndugu Mhamad. Utagundua wewe mwenyewe kuwa, lengo haswa la swali lile lilikuwa ni sisi kutaka kujua kama vitabu vya injili, torati na zaburi, walivyovitumia manabii hao wa zamani kama kweli vinawahusu waislamu au kama ni kweli hao manabii wa zamani walikuwa waislamu. Hapo jibu la uhakika tumeshalipata kwamba, kamwe manabii wa zamani hawakuwa waislamu, kwa kuwa hawakutumia muongozo wa kiislamu ambao ni quran, bali wao, walitumia biblia ya wakristo ambayo ndiyo yenye hivyo vitabu vya torati,zaburi na injili. Kwa hiyo basi, “DINI YA KIISLAMU NI DINI YA UONGO NA UPOTOSHAJI KWA MUJIBU WA MAANDIKO NA UKWELI WA MAMBO!!!!. Ndugu Mhamad, mimi naanza kukuonea huruma kwa kuwa, wewe ni mtumzima mwenzangu lakini unaaibika kwelikweli, jasho litakuwa linakutoka hakika, maana mimi mhina nabaki kujiuliza kuwa, hivi hiyo jamii uliyoialika katika blog hii, ili watutizame watakuwa wanakuonaje?…..maana mfano wake ni kama mtu alievaa tai kubwa shingoni pamoja na ile miwani kubwa kama ya comedy huku akiwa uchi wa mnyama, halafu akaelekea sokoni huku mwenyewe akijihisi amependeza pale alipowaona watoto na wakina mama wanamtazama na kushangaa, kumbe wao walikuwa wanaushangaa ule uchi wake yeye hajijui !!!!. Ndugu Mhamad. Nilichogundua kwako ni kwamba, wewe ni mchanga sana katika mambo ya kiimani, unakiu sana ya kulishwa na kondoo wa bwana, kwa hiyo basi, mimi nimeona niendelee na wewe mpaka hapo utakapo shiba ili uje kuondoka kwenye blog hii kwa amani ukiwa umejaa injili ya bwana yesu, maana naamini utakwenda kuwasaidia waislamu wenzako huko misikitini….sikweli ndugu? au sivyo!!…Sasa nimalizie na ile (matendo 11:25). Waislamu wengi, pamoja na huyu ndugu.Mhamad, wanapenda kutumia andiko hili kushutumu neno ukristo kuwa ni dini ya kipagani ya Paulo aliyoianzisha huko Antiokia jambo ambalo sio kweli….ukweli ni kwamba, yule mwanafunzi Stefano alipouliwa kwa sababu ya kushikilia imani ya kikristo, kulitokea vurugu na manyanyaso makubwa sana yerusalemu. Hivyo, wanafunzi wengi wa bwana yesu walitoka Yerusalemu kuelekea huko Antiokia ya siria iliyoko kaskazini mwa yerusalemu, soma(matendo 11:19). Hapo, Wayahudi wengi walikuwa wameishi Antiokia tangu kujengwa kwa jiji hilo mwaka wa 300 k.w.k. Sasa Paulo kwa kuwa yeye ndiye aliyepokea utume wa mataifa kutoka kwa Mungu, Soma(matendo 9:15) (warumi 1:5), ilimbidi awafuate wanafunzi wote na kuanza kuwatia moyo ili waendelee katika bwana wakiwa wamejaa kusudi la moyo. Hapo ndipo utaona umati mkubwa wa wakristo wa kwanza, umati ule ukaongezeka kwa bwana, soma(matendo 11:22-24). Wayahudi ilibidi ndiyo wawe wa kwanza kuitwa “WAKRISTO” au Wafuasi wa bwana yesu lakini tatizo lao ni kwamba, wao walimkataa bwana yesu kuwa ndiye “MESIYA au “KRISTO”. Waislamu wengi sana, tena hata viongozi wao wa dini, wanafikiri kuwa, jina hili KRISTO” ni la kipagani alilolianzisha Mtume Paulo, lakini ukweli ni kwamba jina hilo, lilitoka kwa Mungu mwenyewe….”MESIYA” ambaye ni “MPAKWA MAFUTA WA MUNGU.Soma(Zaburi 45:7). Ndugu waislamu, mimi naamini kuwa, kwa maharifa haya ya kielimu ninayowapa, angekuwepo hai mtume wenu mhamad, basi angekuwa amekwisha amini na kubatizwa, lakini sijui kwanini huyu mfuasi wake Mhamad yohn anakuwa mzito kufanya hivyo wakati ukweli anaushuhudia waziwazi!!. Basi, mimi naamini siku moja atakuwa ni mwenzangu katika bwana.Asante ndugu.Mhamad.

    Like

  141. Ndugu Mhina,
    kwanza kabisa nimshukuru Allah mwingi wa rehema mwenye kurehemu.Allah ambaye ni mlinzi wangu mwenye uhai wa milele.
    Ama baada ya shukrani hizo, niingie kwenye mada moja kwa moja ili nimsaidie ndugu yangu Mhina pamoja na wakiristu wengine waliojaliwa kufatilia majadiliano haya.
    Baada ya sote kushuhudia kushindwa kwa juhudi za ndugu yetu, na kijana wetu Mhina za kuwafanya manabii wa zamani pamoja na wafuasi wao kuwa ni wakiristo, pamoja na kuhangaika sana huku na huko, tumeshuhudia akibadili kauli mara kwa mara, kitu ambacho kinatufanya tuendelee kuona hawa wakiristu wanavyotanga tanga kwa sababu dini yao imekosa mwelekeo.Maskini biblia yenyewe kimyaaaaaaa! haiwezi tena kuwasaidia ila wao sasa ndo wanatafuta njia za kuisaidia, kutafuta maneno, kuchomekachomeka huku na kule basi ili muradi tu waunge unge.Lakini pamoja na hayo yote ukweli unabaki pale pale.
    Mwanzoni Ndugu Mhina alisema hivi “Ndugu mhamad, ukweli ni kwamba, nyakati za mwanzo, hakukua na manabii waislamu wala manabii wakristo”
    Jamani hii ni kauli ya wazi kabisa, aliyoitoa yeye mwenyewe, mwanzoni kwamba hapo mwanzo hawakuwepo manabii wakiristo.Lakini sasa tuendelee kumuona kwenye kauli ya pili anavyozidi kuwakoroga hata wakiristu waliomtuma.
    NUKUU : “lakini nilichosema mimi ni kuwa “TUNA HAKI YA KUWAITA WAKRISTO WENZETU AU MABABU ZETU”
    Sasa kama umeshasema kuwa mwanzoni hakukuweko na manabii wakiristo ndugu yangu, ni kwa nini sasa muwaite wakiristu wenzenu na hali mnajua kabisa kuwa huko mwanzoni hawakuwepo manabii wakiristo na wewe mwenyewe umekiri?Biblia kimyaaaaaaaaaaa!! Hii yote ni kwa sababu tu wakiristu mmeshakuwa wafa maji, hivyo hamna jinsi zaidi ya kutapatapa tu.Simba yule aliyekula mchungaji wenu sasa amevamia zizi hivyo anajilia tu makondoo!hamna pa kwenda ndugu zangu njooni katika uislamu.ooh mara hawakuwa wakiristo, oooh mara wakiristo wenzetu!! Sasa jibu ni lipi ndugu mbona hutaki kuchagua moja. Chagua moja bwana maana yote hayawezi kuwa majibu.
    Sasa ili tuendelee kuwafahamisha na kuwafafanulia vizuri wakiristu kuwa ukiristu ni dini ngeni na ya uongo, Na ili tuwajulishe kuwa wafuasi wa kweli wa Bwana Yesu hawakuwa wakiristu, bali walikuwa waislam pamoja na yeye Yesu mwenyewe akiwa muislam katika maisha yake ni lazima kwanza tuangalie Biblia yenyewe hiyo (matendo 11:25-26)inasemaje hapa chini.
    25 Kisha Barnaba akasafiri kwenda Tarso kumtafuta Sauli. 26 Alipompata akaja naye mpaka Antiokia. Na wote wawili wakakaa huko kwa mwaka mzima, wakiwafundisha wengi walioamini katika kanisa la Antiokia. Hapo Antiokia ndipo waamini waliitwa ‘Wakiristo’ kwa mara ya kwanza”
    Sasa jamani mimi naamini sote ni watumiaji wa Kiswahili wazuri, hapo biblia inasema “kwa mara ya kwanza” watu waliitwa wakiristo hapo Antiok baada ya Yesu kuondoka duniani, kwa wale wasiojua kiswahil, neno “kwa mara ya kwanza” maana yake ni kwamba haijawahi tokea huko nyuma watu wakawa wakiristu. Ila kwa mara ya kwanza hapo ndipo wakaitwa wakiristo .Sasa labda tutoe mfano kidogo wa lugha nafikiri ndo tutaweza kuelewana kwa maana hata Yesu inasemekana alivyoona watu hawaelewi alitumia mifano: Mathalani mtu akisema Afrika Kusini imepata raisi mweusi kwa mara ya kwanza mwaka 94, hii inamaanisha hapo nyuma hakuwahi kuwepo rais mweusi, kwa hiyo hata biblia inaposema “kwa mara ya kwanza watu waliitwa wakiristo hapo antiok mamiaka kibao baada ya Yesu,sasa mbona Ndugu Mhina unaipinga biblia yako mwenyewe!!!!?Jamani hiki si kituko cha karne!!!yaani wakiristu biblia yenu mnaanza kuikimbia sasa na kuyakana maneno yake.Ukiristo kwisha habari yake!!
    Kwa ushahidi na ufafanuzi zaidi wa lugha hapa chini nimenukuu biblia nyingine niliyonayo hapa na yenyewe inasema hivi.
    Matendo 11.26 Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. HukoAntiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
    Watu kuitwa wakiristu ilikuwa haijawahi kuwepo, hata Yesu mwenyewe hakuiacha dini hii ya uongo na ya kishetani ya ukiristo.wafuasi wa Yesu walikuwa waislamu ila alipokuja huyu mtume wa uongo Paulo akawafanya wakiristo.
    Hebu tuangalie Quran tukuf, inatwambia wanafunzi wa Yesu walikuwa na dini gani?
    SURA AL-IMRAN 3:52. “Isa(Yesu) alipo hisi kuwa kati yao pana ukafiri alisema: Nani wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu? Wanafunzi wake wakasema: Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na shuhudia kwamba sisi hakika ni Waislamu.”
    Ewe ndugu yangu Mkiristu unataka upewe ushahidi upi tena zaidi ya huo? kama wanafunzi na wafuasi wa kweli wa Yesu wenyewe wanakiri kwamba ni waislamu,ni nini basi kinakuzuia wewe unayejiita mkiristu usiingie katika dini hii!!Dini ya Mitume na manabii wote wa M/Mungu?Nini kinakuzuia ndugu yangu? Ewe ndugu yangu Mkiristu, wafuasi wa Yesu walikuwa waislamu, na waislamu walikuwepo hata kabla ya Yesu mwenyewe na quran inatuthibitishia hilo wala sisi hatuna haja ya kuhangaika, na wakati tunaye Allah anayesema wazi kabisa, huku akiwakemea hawa wanaobishana mambo wasioyajua.

    QURAN SURA 3AL-IMRAN
    “66. Angalieni! Nyinyi mlibishana katika yale mliyo yajua. Mbona sasa mnabishana katika yale msiyo yajua? Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui.
    67. Ibrahim hakuwa Yahudi wala Mkristo, lakini alikuwa mwongofu Muislamu, wala hakuwa katika washirikina.”

    Ibrahim hakuwa mkiristu kama mlivyo nyie, Kijana Mhina, quran iko wazi mno ndugu yangu, wazi mno yaani imerahisishwa kiasi kwamba hata mtoto akisoma anaelewa sasa wewe mtu mzima unakwama wapi ndugu?? Kwa hiyo Allah anawaambia wakiristu katika( aya ya 66-67) kuwa mnabishana msiyoyajua, Ibrahim hakuwa mkiristu wala Yahudi, bali alikuwa Muislam na mwongofu.Kwa hiyo ndugu yangu Mhina, naamini kabisa hata hapo ulipo unazidi kushangaa maajabu ya Quran jinsi inavyochambua mambo kwa uwazi kabisa kabisa, na jinsi inavyowasuta wakiristu mnaobishania msiyoyajua. Enyi ndugu wakiristu, ukiristu ni dini ya uongo tena ya mashetani, iliyoletwa na mtume wa uongo Paulo. ajabu zaidi hata hao waandishi wa agano la kale hawatambui dini ya ukiristo na ndiyo maana soma usomavyo agano la kale hutaona neno kiristo, wala ukiristo au wakiristo, sasa kumbe hata biblia yenu yenyewe inawasuta na dini yenu mpya , dini ya mashetani ambayo haikuwepo toka mwanzo.

    Ndugu Mhina, umekuwa ukisema uwongo mwingi tu hata huko nyuma ulipokuwa ukijadili na wakina Ibrabra mimi nimekuwa nikikufatilia ndugu yangu, umekuwa ukiisingizia biblia yako mwenyewe maneno hata ambayo haijayasema kwa mfano nakunukuu hapa chini katika moja ya hoja yako huko juu.
    NUKUU “Na kwa sababu bwana yesu ndiye nabii wa mwisho wa Mungu, Pia kwa sababu jengo hili la Mungu ni kubwa na lenye thamani, basi yule wa mwisho ni lazima akae mlangoni ili kuhakikisha wote wanaotaka kuurithi uzima wa milele wanapitia kwake”
    Ndugu Mhina, kwenye kauli hii ulisema Yesu ni nabii wa mwisho wa Mungu, kama nilivyokunukuu hapo juu hivyo Mtume wetu Mtukuf Muhammad (S.A.W) hafai kuwa Nabii wa mwisho wa Mungu, Hapa sasa naomba tuelewane lugha kwanza, nabii wa mwisho maana yake hatakuja nabii mwingine baada yake, hiyo ndiyo maana halisi ya neno hilo sasa sitaki uanze kujikoroga tena, kama ulivyofanya huko juu, lakini kwa bahati mbaya kabisa Biblia yako haisemi kwamba Yesu ni nabii wa mwisho wa Mungu, badala yake inasema kama ifuatavyo hapa chini.
    Matendo 11:27 “wakati huu manabii walitoka Yerusalemu wakaenda Antiokia. 28 Na mmoja wao, jina lake Agabo.”
    Ndugu yangu Mhina, tukio linaloelezewa hapo juu lilitokea wakati Yesu ashaondoka duniani zamani sana ,Sasa hapo mbona biblia yako yenyewe inakusuta?biblia inaonesha kabisa kuwa walikuwepo manabii baada ya Yesu,sasa kumbe Yesu sio na wala sio nabii wa mwisho wa Mungu na biblia yako inatambua hilo ,hapo ulijitungia tu baada ya kukosa pa kukimbilia maana kila unapokwenda waislmu tunapiga, kila ukijaribu tunapiga kichwa kama nyoka, sasa unakosa mwelekeo.
    Sasa baada ya kuona kuwa biblia yenyewe inakiri kuwa Yesu sio nabii wa mwisho wa Mungu bali biblia inasema walikuwepo manabii hata baada ya Yesu kuondoka, sasa tuone Quran inatwambia nabii wa mwisho ni nani?

    QURAN SURA AL-AHZAB
    “ 33:40. Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi
    Mungu na ni Nabii wa Mwisho, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.”

    Kwa hiyo ndugu Mhina usisumbuke na kubabaika, usitape tape na kuhangaika, Muhammad(S.A.W) ndiye nabii wa mwisho wa Mwenyezi Mungu.na quran ndicho kitabu pekee kinachoweza kukutoa kwenye giza na kukuleta kwenye mwanga.

    Ndugu Mhina umekuwa ukinakiri tena kwenye maneno matukufu ya quran na kutafsiri kama unavyotaka lakini kamwe neno la Quran,na Allah ashasema atailinda na wala neno lake halitabadilika , Ndugu Mhina nitakunukuu katika aya moja uliyodai umeitoa ndani ya quran.
    16:43 “ENDENI MKAWAULIZE WENYE KUMBUKUMBU ZA VITABU VYA MWENYEZI MUNGU VYA KALE IKIWA NINYI HAMJUI!!!!!.”
    Kwanza kabisa hiyo aya umenukuu vibaya ili kujiridhisha mwenyewe.Lakini pamoja na hayo Aya yenywe nimeinukuu hapa chini.
    16:43. Nasi hatukuwatuma kabla yako ila watu wanaume tulio wapa Wahyi (Ufunuo).
    Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui.
    Ndugu Mhina huna elimu ya kutafsiri na kuyatambua maneno ya Allah hivyo unajaribu kupotosha ukweli, lakini wapi ukweli upo pale pale, hapo walikuwa wanaambiwa makafiri wa makka waliokuwa wakikataa ufunuo wake, hivyo Allah anawaambia wawaulize watu wenye ukumbusho yaani waislam ikiwa wao hawajui! ina maana Allah alikuwa anawadirect makafiri kwa waislam wenye ukumbusho kama hawajui kuliko kubishania uwongo kama unavyobisha ndugu Yangu Mhina, bila elimu yoyote.
    Sasa tuone kwenye aya inayofuata wenye ukumbusho ni akina nani kama si waislam;
    16:44 Kwa Ishara za wazi na Vitabu. Nasi tumekuteremshia wewe Ukumbusho ili uwabainishie watu yaliyo teremshwa kwao, wapate kufikiri.
    Kwa hiyo, watu wenye ukumbusho ni Mtume ambaye ameteremshiwa ukumbusho, pamoja na maswahaba zake aliowapa elimu ya ufunuo huo pamoja na waislamu wote, na ukumbusho unaokusudiwa hapo ni quran tukuf,kwa sababu quran imekusanya vitabu vyote vya Mungu vya kale na kuviweka pamoja! sasa ndugu yangu unashindwa kuelewa nini! Allah anasema amemteremshia mtume Ukumbusho, na anawaambia makafiri waulize watu wenye ukumbusho! Hebu sasa nikuulize kwa utaratibu ndugu yangu, ni wapi panakutatiza, tatizo lako unanukuu nusu msitari alafu unatoa tafsiri kama kweli una nia ya kujifunza ni kwa nini basi usisome hata aya inayofuata ili upate kuelimika?kama hujui unabisha si uniulize mimi mwenye ufunuo na ukumbusho? Kuliko kuwauliza hao wachungaji wako wasiojua kitu?wao ukiwauliza lazima watakwambia uongo kuhusu uislamu ili muradi utoe sadaka tu!! Wao wazidi kuneemeka, wanajua wakikwambia ukweli utawakimbia makanisa yatabaki magofu.

    Ndugu Mhina, udogo wako wa elimu ya dini yenu, unatia aibu mno, tena mno ndugu yangu, na ndio unaokufanya utuletee marudio ya mada ambazo tumeishakuelimisha mno huko juu, lakini sisi tutaendelea kukuelimisha tu ndugu yetu, kwa sababu Allah ashasema sisi waislamu tumetolewa kwa ajili ya kuelimisha watu.

    Ngoja nikunukuu hapa chini, ili nione utakavyojitetea kwa kula matapishi yako tena.
    HOJA YAKO :“Hapo jibu la uhakika tumeshalipata kwamba, kamwe manabii wa zamani hawakuwa waislamu, kwa kuwa hawakutumia muongozo wa kiislamu ambao ni quran, bali wao, walitumia biblia ya wakristo ambayo ndiyo yenye hivyo vitabu vya torati,zaburi na injili…”
    Ndugu Mhina, kama unasema manabii wa zamani walipewa taurat,zaburi na injili hivyo walikuwa wakiristo, kweli kama ufahamu wako umeishia hapo, hakika hili ni janga la kikiristo, na ukiristo duniani.
    Mimi swali langu ni moja tu Hivi Nabii Ibrahim alitumia vitabu gani kati ya hivyo ulivyoorodhesha hapo juu? Au Nabii Nuhu na nabii Adamu walitumia vitabu gani ili tujue kuwa walikuwa wakiristu? Sasa kwa hiyo kumbe ikigundulika hawakutumia vitabu hivyo utakuwa umeisha jijibu kwamba hawakuwa wakiristo. Hili tumeshakujibu sana na najua ushaelewa sema bado una aibu jinsi utakavyowaangusha wakiristo wenzio, lakini naamini kabisa akili yako ishakubali.Hebu turudi katika quran kwanza tuone Allah anawaambia nini watu kama nyie.

    QURAN 3:65. Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnabishana juu ya Ibrahim, na hali Taurati na Injili hazikuteremshwa ila baada yake? Basi hamzingatii?
    Unaona ndugu Mhina, Allah anajua kuwa nyie mnabishana msiyoyajua juu ya manabii wa kale.Taurat na injili na zaburi pia vimeletwa baada ya Ibrahimu miaka mingi mno na yeye alikuwa muislam.sasa problem iko wapi ndugu?kwa hiyo Allah anajua kabisa jinsi mnavyopenda kubishana katika mambo msiyo na ufahamu nayo.

    Ndugu Mhina, nimekuelimisha vya kutosha ila kwa leo naomba nimalizie kwa kunakili aya ifuatayo kutoka ndani ya Quran.
    SURA 3 AL-IMRAN:
    “64. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na
    nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na
    chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi
    Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudi- eni ya kwamba sisi ni Waislamu.”

    Ewe ndugu mkiristo, usitegemee kabisa kuingia peponi kama wewe ukifa katika ukafiri, yaani wewe ni kwenda jikoni tu, siku ukifa, Kwa hiyo ndugu zangu hii bahati mliyoipata ya kuwafikishia ujumbe wa Allah wengine hawaipati, kwa hiyo jitahidini fanyeni hima mfe mkiwa waislam.
    Wallahu a’aalam, wabillahi tawfiq.

    Like

    • alfa says:

      mhamad unanifurahish sana,huna hoja baba!anyway moyon umeipata,hebu anz upya kufuatilia huo mjadala toka mwanz mpaka mwisho ulipoishia wewe,najua ni udin unakusumbua lakin kwel umeshaijua,ubarikiwe.

      Like

    • alfa says:

      suala la wanafunz kuitwa wakristo jibu utalipata utakaporudi kuanza kusoma huu mjadala,na kwamb paulo alihubir antiokia,ni kweli,lakin wapo walioamini tayar ambao walikimbilia huko,mi nnachokiona ni kwamb ndug mhumad yohna unajifany ka huelewi,nakuomb urudie kusoma upya mjadala huu,manak unarudia v2 vilevile,UBARIKIWE NDUGU YE2.

      Like

  142. Salim says:

    Ahsante sana kaka Yohana,umetufumbua macho weng! Allah akuzidishie elimu, manaake wakiristo wengi huwa hawapendi kusoma hata biblia yenyewe, lakikini sasa naamini kabisa wamekuelewa.Allah akuzidishie kaka

    Like

  143. Salim says:

    QURAN SURA AL-MAIDA
    59. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Hivyo mnatuchukia kwa kuwa tumemuamini Mwenyezi
    Mungu na tuliyo teremshiwa na yaliyo teremshwa kabla, na kwa kuwa wengi katika
    nyinyi ni wapotofu?
    60. Sema: Je! Nikwambieni yule ambaye ni mwenye malipo mabaya zaidi kuliko hayo
    mbele ya Mwenyezi Mungu? Ni yule ambaye Mwenyezi Mungu amemlaani na
    amemkasirikia, na amewafanya miongoni mwao manyani na nguruwe, na wakamuabudu
    Shet’ani. Hao ndio wenye mahali pabaya na wamepotea zaidi njia iliyo sawa.

    Like

    • alfa says:

      halaf mbna hoja zinarudiwa tu,anyway mi najua ujumbe umefika maana kama unahtaj kuelewa anz toka mwanz mpaka mwisho,Mungu akutie nguvu Mhina tuihubiri injil kwa upendo ili weng wapate kuijua kweli,manak weng wamepotea,kutoa sadaka kwa majini huku wakiikana nguvu halis ya Mungu mwokoz wetu,nawapenda na naendelea kuwaombea watumish wa Bwana tusonge mbele,roho nying hazijakombolewa bdo.AMEN

      Like

  144. alfa says:

    salim ndugu yangu,iman ya mkristo imejaa ktk upendo,na ndo amr kuu,je ni nani mweny upendo kat ya hawa?nitaenda kati yao wasio amini kwa upanga niwaangamize kama hawatak kuslimu,(muhammad)na huyu nitahubir wokovu kat yao,nitawaombea msamaha watakaponipiga kwa mawe maana hawajui watendalo{stephano},mara ngap tumetukanwa na kudhihakiwa,na ikitokea tumetenda mabaya ni mara moja kwa zenu alfu,na kwa kutokujua.

    Like

  145. alfa says:

    salim ndugu yangu,iman ya mkristo imejaa ktk upendo,na ndo amr kuu,je ni nani mweny upendo kat ya hawa?nitaenda kati yao wasio amini kwa upanga niwaangamize kama hawatak kuslimu,(muhammad)na huyu nitahubir wokovu kat yao,nitawaombea msamaha watakaponipiga kwa mawe maana hawajui watendalo{stephano},mara ngap tumetukanwa na kudhihakiwa,na ikitokea tumetenda mabaya ni mara moja kwa zenu alfu,na kwa kutokujua.na din yak ndo inayofundisha chuk na mauaji kwa sababu mwasisi wak ananuka damu za wanadamu watakatif kwa wasio watakatifu,tengeneza na bwana acha propaganda.

    Like

  146. alfa says:

    shafii young boy unamapenz na majin kiasi hki,hzo habar za majini ndugu wameshawaelezea nadhan kama ishu ni kuelewa umeshaelewa,huwa sirudii hoja zilizojibiwa tayari,au unahtaj aya za aibu ndugu,scienc ya walev ndo huamin jua latuama kweny maj machafu,lakin Musa alisema bwana amelifanya tufe la dunia,scientist provd dat,najua hii hujasisitiza ving vya msing vimepewa majib,suala uelewe co ligi,BARIKIWA SALIM

    Like

  147. alfa says:

    shafii young boy unamapenz na majin kiasi hki,hzo habar za majini ndugu wameshawaelezea nadhan kama ishu ni kuelewa umeshaelewa,huwa sirudii hoja zilizojibiwa tayari,au unahtaj aya za aibu ndugu,scienc ya walev ndo huamin jua latuama kweny maj machafu,lakin Musa alisema bwana amelifanya tufe la dunia,scientist provd dat,najua hii hujasisitiza ving vya msing vimepewa majib,suala uelewe co ligi,BARIKIWA SHAFII.na hamna mlichopangua zaid kujing’ata tu.bwana akutie nguvu in yo day ma frnd.

    Like

  148. Salim says:

    QURAN: SURA 5 AL-MAIDA
    72. Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi(Yesu) mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.

    73. Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja. Na ikiwa hawaachi hayo wanayo yasema, kwa yakini itawakamata adhabu chungu wale wanao kufuru.

    74. Je! Hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha? Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.

    75. Masihi mwana wa Maryam hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwisha pita Mitume kabla yake. Na mama yake ni mwanamke mkweli. Wote wawili walikuwa wakila chakula. Angalia jinsi tunavyo wabainishia Aya, kisha angalia vipi wanavyo geuzwa.

    76. Sema: Je! Mnawaabudu, badala ya Mwenyezi Mungu, wale ambao hawawezi kukudhuruni wala kukufaeni? Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

    77. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu bila ya haki. Wala msifuate matamanio ya watu walio kwisha potea tangu zamani, na wakawapoteza wengi, na wenyewe wakapotea njia iliyo sawa.

    Allah anawaambia, Enyi wakiristo acheni ibada ya kumuabudu Masihi mwana wa Maryam, hiyo ni kufuru ndugu zangu, Muabuduni M/Mungu aliyeumba mbingu na nchi.Mwenyezimungu ni Mmoja tu , na Mungu wa Yesu ndiye Mungu wangu na wewe, hata Yesu mwenyewe anasema katika (Yohan 20:17), mnapinga hata maneno ya Yesu?

    Like

  149. alfa says:

    hamna k2 kipya hapo,bdo naendelea kusema,ni marudio hayo,somen toka mwanz mkishapata majibu 2lie,c lazma uonekane kweny ukurasa,biblia ni habar inayoonyesha mwanzo wa mtu,anguko lake na mpango wa Mungu kumkomboa mwanadamu,na mwisho wa mwanadamu hapa duniani na maisha baada ya hayo,ukisoma robo mstar ni uwendawazmu,mtu mwenye ufaham awe na biblia na aisome kwa uelewa,hki kitabu cha watu wote na muongozo wa maisha,hoja zako ni hewa na zimejibiwa vzuri tayari,endelea kumuamin mtu aliekufa ka bibi zangu na babu zangu,kaoza na anasubir kuhukumiwa na Kristo hata mkibadil maandiko,BARIKIWA SALIM

    Like

  150. mhina says:

    ndugu.mhamad, Wewe unataka tuanze tena kufundishana mambo mengi ambayo tulikwisha yajadili huko juu jambo ambalo sio zuri kwangu kwa kuwa mimi ninatumia simu ndogo sana ya mkononi kuyaandika mambo yote haya….huwa inanichukua hata usiku wa manane ili kukamilisha yote. Lakini kwa busara kabisa, ngoja nianze kukujibu tena: Mimi binafsi katika hoja zako, nilichokiona ni kuwa asilimia 99.9, ya hoja zako, hazina maana yeyote zaidi ya kutafu visababu vidogo vidogo ili kupoteza ukweli halisi wa msingi mkubwa wa ule ukweli tuliokuwa tunautafuta kwa pamoja.Wewe umeweka udini udini zaidi kuliko hata kuelewa maana ya hata hayo majina ya dini unayoyatumia…..”Uislamu maana yake ni “UNYENYEKEVU”…Kwa hiyo basi, waislamu maana yake ni “WANYENYEKEVU”.Swali: inatosha kweli kukazania kuwa manabii wa zamani walikuwa wanyenyekevu pasipokuonyesha kuwa huo unyenyekevu wao ulitumia muongozo gani wa vitabu ili nasisi tufuate nyayo zao?. KRISTO maana yake ni “MESIYA” ambaye ni bwana yesu. Kwa hiyo, wakristo maana yake ni wanafunzi au wafuasi wa huyo mesiya ambaye ni bwana yesu. Mpaka hapo, kwa kutumia maana halisi za dini zetu, utagundua kuwa, uislamu sio dini ila ni sifa ya dini, na ndiyo maana jina hilo la “UNYENYEKEVU” Linaonekana ni la asili kwa mtu yeyote anae mpenda Mungu.Hata mimi mhina ukiniita mnyenyekevu ninakubali lakini ni lazima nionyeshe muongozo wangu wa huo unyenyekevu wangu kama ni kweli unatoka kwa mungu au kwengine.Kwa hali hiyo, ndugu mhamad…Mimi ukiniambia kuwa manabii wa zamani wote walikuwa “WANYENYEKEVU” Kwa maana halisi kama hiyo, kamwe mimi siwezi kukataa, tena nitakwenda mbali zaidi kukubali kuwa hata sisi wakristo wote ni wanyenyekevu lakini swali la msingi ni kujiuliza kuwa, unyenyekevu huo kwa kutumia muongozo gani haswa? Wa Allah wenye kutumia kitabu cha mtume mhamad alichokipata kwa mazingira yake yeye mwenyewe, au muongo wa mitume wote na manabii wa Mungu waliotumia torati,zaburi na mwisho injili ya bwana yesu kwa ajili yetu sisi wakristo? Hapa ndipo penye tatizo na tofauti zetu ndugu mhamad, lakini kwa kuwa wewe unajua wazi kuwa umepotoshwa katika huo muongozo wako, ndiyo maana unashindana na mimi si kwa kuangalia miongozo ya vitabu vyetu bali wewe unakimbilia kwenye majina ya udini ambayo hata mtu mwenye maarifa sahihi akiangalia tafsiri halisi za majina ya hizo dini, atagundua kuwa ukweli upo palepale tena haujasogea hata kidogo!!!. Mimi nakubali kabisa kuwa hata tangu Adamu mpaka bwana yesu, manabii na waumini walikuwa “WANYENYEKEVU”.Tena nirudie kwa kusema kuwa hata mimi mhina ni “MNYENYEKEVU…Hivyo, ndugu mhamad, wala tusishindane kwa jambo dogo na lakipuuzi, lakini ni lazima sisi wote kwa pamoja tujue kuwa, katika huu unyenyekevu wetu ni lazima ufuate nyayo, njia na muongozo wa vitabu vya manabii wa nyuma wa mungu na kamwe si vinginevyo!!.Sasa, biblia inakubali kuwa hao wanyenyekevu wote wa nyuma, yaani manabii na mitume wa Mungu walitumia, torati, zaburi na mwisho ikaja injili kupitia bwana yesu jambo ambalo hata quran inaliunga mkono….tatizo hapo ni nini ndugu yangu mhamad linalokufanya wewe na waislamu wenzako kufuata muongozo huu halali wa Mungu katika huu “UNYENYEKEVU WETU!!!!,…Huyu nabii mpya aliyejitenga peke yake na muongozo wake usioeleweka alichomekwa na nani ili nae atuongoze??!!…tena jambo la ajabu ni kwamba, anatukataza tusitumie vile vitabu vyote vya mwanzo vya wanyenyekevu wenzetu waliopewa na Mungu halafu anasema kuwa kitabu chake pekee ndicho kifuatwe na wanadamu wote?,HATARI KUBWA. Nilichojifunza kwa ndugu yangu Mhamad ni kwamba, kumbe wakati mwingine inatupasa tuihubiri injili kwa hali na mazingira haya ya kitoto mno mno, ili tuweze kueleweka na wengine.Kwa hiyo basi, mimi bado nasisitiza kuwa “unyenyekevu” siyo dini wala sio njia bali hiyo ni sifa ya kawaida tu, na kama kuna mtu anaetaka kuipamba sifa hiyo kwa kuweka taratibu zake mpya za kuwaongozea watu, ili kupindisha ukweli wa mambo, basi huyo “AMELAANIWA NA MUNGU KWA MUJIBU WA MAANDIKO MATAKATIFU. Quran hiyohiyo inayopingana na kila jambo la Mungu wa kweli inasema”MUNGU AMESHAFUNIA TORATI NA INJILI KWA AJILI YA WANADAMU WOTE KUTAFAUTISHA JEMA NA BAYA,!!!.Tatizo ni nini hapo ndugu mhamad?!!. Halafu ndugu mhamad, unasema kuwa mimi nitakula matapishi yangu, yapi hayo?…niliposema kuwa sisi wakristo na Manabii wa kale, tumekuwa kitu kimoja au mmoja,…. ni katika Yesu kristo aliyetuunganisha kwa mwili wake ili sisi tuwe mwili mmoja katika yeye.Haya ni mambo ya kiroho ambapo wewe mtu unaependa kupokea kila jambo kimwili na kulielewa kimwili pekee, ni lazima upate tabu kunielewa kwa urahisi.Biblia inasema kuwa, “jengo lote, yaani (manabii na sisi wakristo, limeunganishwa kupitia yeye.soma(efeso 2:19-22), tena kama haitoshi, Mungu mwenyewe anamwambia ibrahimu: NIMEKUWEKA WEWE UWE BABA WA MATAIFA MENGI. Sasa ndugu mhamad, wivu wako hapo unatoka wapi mimi kusema kuwa “TUNA HAKI YA KUWAITA WAKRISTO WENZETU AU MABABU ZETU”?!!…Huoni kuwa tukonao pamoja katika ulimwengu wa roho kwa Mujibu wa Mungu mwenyewe? Istoshe, kwani wewe hujui kuwa alichokifanya bwana yesu ni kutimiza torati ileile walioitumia wale manabii wa mwanzo, na kamwe sio kuondoa na kuleta vitu vipya na vigeni kama alivyofanya nabii wako mhamad??, UNASHANGAZA KWELIKWELI WEWE!!…ndiyo maana hata nilikua naona uvivu kukujibu haraka mtu ambaye unaonekana kuwa maarifa yako yamezidi udogo.Nikuulize, hivi wewe unaelewa maana ya “BABA” Katika nyumba moja??!!.Acha kupoteza Muda kwa mambo ya kijinga bwana, tafuta hoja zenye uzito unaotufaa. Pia ukauliza kuwa manabii wa Mungu kama’Nuhu, ibrahim, Adamu…walitumia vitabu gani?, swali hili nilikwishalijibu pia huko juu halafu wewe unataka turudie!!…hao ni manabii wa Mwanzo ambao, Mungu aliongea nao moja kwa moja kupitia malaika ili awape ujumbe wake, wauhifadhi kwa kutuandikia sisi tuliofuata tupate msingi wa mausia yake.kazi ya kuandika vitabu vile vitano vya mwanzo alipewa nabii Musa pekee. Kwa upande wako mimi nakushangaa mno kwa kuwa, wewe mwenyewe huko juu, ulituambia kuwa vitabu vya kale haviwahusu kwa kuwa vilikuwa ni kwa ajili ya israel pekee…lakini hapo juu umebadilika tena kama kinyonga baada ya wewe kugundua umuhimu wa vitabu hivyo, umebadilika kwa kusema kuwa “vitabu vyote vya kale vimehifadhiwa katika quran na mtume wenu, sasa hivyo vitabu ni vya nini ndani ya quran wakati wewe ulisema kuwa haviwahusu!! …. Kuhusu ile (matendo 11:25-26). Nilikwisha ielezea vyema sana.Narudia tena….Waumimi wale wa Antiokia walikuwa kundi kubwa la kwanza kuitwa “wafuasi wa bwana yesu(wakristo) kwa sababu wayahudi walimkataa bwana yesu, tena kwa ushahidi wa hata maneno ya bwana yesu mwenyewe.Bwana yesu aliwaambia wayahudi “KWA SABABU HIYO, NAWAAMBIA UFALME WA MUNGU UTAONDOLEWA KWENU, NAO WATAPEWA TAIFA LINGINE LENYE KUZAA MATUNDA YAKE. Soma(Mathayo 21:43). Ukweli ni kwamba hata ukisoma injili zote nne, utaona jinsi wayahudi wanavyo mkataa bwana yesu na kumpinga katika kila jambo hata kufikia hatua ya kumuua pale msalabani. Ndio maana hata Paulo, aliwaambia wayahudi hivi: ILIKUWA NI LAZIMA NENO LA MUNGU, LINENWE KWENU KWANZA, LAKINI KWA KUWA MNALISUKUMIA MBALI, NA KUJIONA NAFSI ZENU KUWA HAMKUSTAHILI UZIMA WA MILELE, ANGALIENI, TWAWAGEUKIA MATAIFA.Soma( matendo 13:46). Pia hili tulikwisha lijadili vizuri huko juu ya kwamba, Mataifa ndiyo waliopokea nuru ya wokovu. Mpaka hii leo, Wayahudi wanamkataa bwana yesu kama nyie waislamu sasa unafikiri kwa hali hiyo, kunaweza kukawa na Wakristo wengi kupita wale wakristo wa mataifa, eti kwa kisingizio kuwa wao walikuwa wa kwanza kukutana na bwana yesu?! Si kweli ndugu mhamad na wewe unalijua hilo. Biblia inasema kuwa jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni, bwana yesu ndiye jiwe kuu la pembeni. Wewe ndugu mhamad, unafanya kazi ya kupingana pingana na kutetea udini sana katika maelezo yako, huku ukirudia rudia mambo yote ya nyuma tuliyo yafafanua,!!. Mwisho ni ile (matendo 11:27-28)….ndugu mhamad, Mimi nilikuwa ninamuongelea bwana yesu kama nabii mkubwa na wamwisho aliyetumwa kwa ajili ya watu wote…ukiondoa hivi vinabii na vimitume vidogodogo vya maeneo fulanifulani ambavyo hata hivi leo bado wanaendelea kuongezeka. Na wewe nikuulize hapa: kama nyinyi waislamu mnajua kuwa manabii na mitume wanaendelea kuongezeka au wapo(hawavumi lakini wamo) mbona na nyinyi pia mnasema kuwa mtume wenu ni mtume na nabii wa mwisho baada ya bwana yesu??, kwanini sisi wakristo hatukuhoji hivyo unavyo nihoji wewe?, ni kwa sababu tunaelewa upesi kuwa mnazungumzia nabii yule mkubwa kabisa aliyetumwa kwa ajili ya watu wote. Hata wanafunzi wa bwana yesu wanao ni wale 12, lakini ukweli ni kwamba waliongezeka wakawa zaidi ya 80. Biblia inasema “AKATEUWA WENGINE 70, Je, ndugu mhamad, wewe ulikuwa unawajua vizuri hao wengine sabini alio wateuwa bwana yesu? Au ulikuwa unawajua wakina matayo tu??….acha hoja za kitoto unapoona umezidiwa ndugu. Njooni kwa bwana yesu njia isiyo kuwa na mashaka hata kidogo, hata hata hata chembe ndugu yangu.Asante na ubarikiwe….lakini ukifukua mambo yaliyopita huko juu basi mimi sintokujibu maana ni vizuri nafasi iliyobaki, tukajifunza kutoka kwa ndugu zetu wengine. NAOMBA UFAHAMU KUWA HAPA MIMI SISHINDANI ILA NAJARIBU KUBADILISHANA MAWAZO NA MTU YEYOTE KAMA WEWE. Usikubali kumkosa bwana yesu katika maisha yako ya hapa duniani kabisa kabisa.

    Like

    • alfa says:

      naomb tuwaze kama watoto wa Mungu,inanshangaza wazinz,walevi,na waasherat wanavyomfikir Mungu,na hapo ctakubal kuwa Mfalme wangu na Mungu wangu ndiy Mungu wa waislam,watu najis wa roho wanafikir Mungu ni mchafu!wanadai amewaandalia wanawake weny makalio makubwa,watawatumia watakavyo,mito ya maziwa na kila chakula watakula,yaani hawa jamaa hawajui Mungu ni mtakatifu,uchafu haupo ktk maskani ake?wanawaza mapenz ya mwil mamb ya roho hawatak kufaham,ndo maana wanawaza wanawak na vyakula v2 vinavyoharibika,kwa hyo wanaswal ili wakafany uzinz na ulev na ulaf kwa Mungu mtenda dhamb.achaneni na uongo tafuten kweli.

      Like

      • ondoa dhana potofu na fikra mgando na chuki binafsi dhidi ya uislamu!alfa hivi ni wewe unayewaambia waislmu wa muamini YESU kuwa ni mungu? mungu ambaye amepigwa na viumbe vyake alivyoviumba mpaka akabakiwa na chupi ya ndani? alafu aseme kupigwa kwangu ni uwokovu wenu! alfa niache kidogo! kama uokovu unapatikana kwa kuamini hilo? mi basi! ALLAH AMETAKASIKA NA HAYO! haimkiniki kwa m/mungu kuchezewa kiasi hicho ni aibu kubwa

        Like

    • alfa says:

      naomb tuwaze kama watoto wa Mungu,inanshangaza wazinz,walevi,na waasherat wanavyomfikir Mungu,na hapo ctakubal kuwa Mfalme wangu na Mungu wangu ndiy Mungu wa waislam,watu najis wa roho wanafikir Mungu ni mchafu!wanadai amewaandalia wanawake weny makalio makubwa,watawatumia watakavyo,mito ya maziwa na kila chakula watakula,yaani hawa jamaa hawajui Mungu ni mtakatifu,uchafu haupo ktk maskani ake?wanawaza mapenz ya mwil mamb ya roho hawatak kufaham,ndo maana wanawaza wanawak na vyakula v2 vinavyoharibika,kwa hyo wanaswal ili wakafany uzinz na ulev na ulaf kwa Mungu mtenda dhamb.achaneni na uongo tafuten kweli.MUNGU NI MTAKATIFU NAYE NI ROHO,WAMUABUDUO HUABUDU KTK ROHO NA KWELI,JESUS Z THE TRUE WAY.

      Like

  151. alfa says:

    siku moja nlishangaa sana,kiongoz wa dini ya hawa jamaa alikuwa anawahubir wenzak mskitini,akadai swala wanazofany zitakuwa a.c makaburini,upepo mwananaa,na jamaa wakaamini pale makaburin wataendelea kupata a.c safi,hawakujiuliza na hizo mait zinazofukuliwa vipi?a.c zao mbna hazionekan zaid ya mifupa tu,siamin msemo dhaifu,sikio la kufa halisikii dawa,ila Bwana wa majesh humvuta yeyote amtakaye,WATAKUWA WALIOFUNDISHWA NA MUNGU,NA YAKOBO NIMEMPENDA ESAU NIMEMCHUKIA,NIMEWACHAGUA HAMKUNICHUGUA,tafuten uokovu mumuone Bwana live na nguvu zake,waliobak wanahadith tu.JESUS SHALL CME 2 TAK THE CHURCH,ATAWAKOMBOA ISRAEL NA VITA YA MPINGA KRISTO,NA ATAHUKUMU ULIMWENGU MZIMA NA LUSIFA NDANI.PRAISE THE KING,WORSHP THE LORD OF SALVATION,WE WORSHIP YOU JESUS,WE WERSHOP JEHOVA ALIETUKOMBOA.

    Like

    • alfa says:

      NAOMBA WASOMAJI MFUATILIE MJADALA HUU TOKA MWANZO MPAKA MWISHO NA MUANDIKE HOJA ZINAZOELEWEKA KA MNATAKA UFAFANUZ,KURUDIA V2 VILEVILE NI KUPENDA MALUMBANO WAKAT HAPA SI TUNAELIMISHANA,MBARIKIWE WAPENDWA WOTE MNAOCHANGIA MADA ZENU,MUNGU AFANYE JAMBO MAISHAN KWENU HASA WANAOPINGA UOKOVU,MSIISHIE KUTAZAMA,SAFINA IKIONDOKA MACHOZ HAYATAKOMA JAMANI,ACHENI HADITH NJONI MUONJE MJUE WEMA WA BWANA,NGUVU ZAK NA UOKOVU WAKE KTK UHALISI WAK NA SI HADITH,NENO LA BWANA NI HALISI NA LINATENDA MAMB YA KUTISHA,NAYE BWANA HUJIFUNUA KWA WATU WAKE,HASA WALE WALIO WACHANGA KTK UFALME,KUBALINI MTII MTAKUWA NA CHA KUSEMA,WAACHENI WENYE HADITH ZAO,MTAFUTEN BWANA,NAWAPENDA NA MBARIKIWE NYOTE.

      Like

  152. mhina says:

    Mimi naishia hapa. Aksante ndugu mhamad yohana kwa ushirikiano wako. Naamini kuwa pamoja na uchanga wangu wa kutoyajua maandiko vizuri, hutakosa cha kujitafakari wewe na waislamu wengine.Ubarikiwe. Mimi naamini kuwa sina cha kuchangia chochote tena kwenye blog hii zaidi ya kuwa mtazamaji tu. Kwaherini wafuatiliaji wote.

    Like

  153. Ndugu Mhina,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah kwa kunijalia afya na uzima na zaidi kunifanya niwe muislamu.
    Pili nikushukuru sana ndugu Mhina kwa sababu sasa naona unaanza kuelewa nini maana ya uislamu na inshaallah kidogo kidogo ndgu yangu usichoke kujifunza huenda Allah siku moja akakuingiza katika nuru ya uislam.

    Ndgu Mhina, nashkuru kwa kuwa kwa sasa umetambua kuwa manabii wa zamani walikuwa wanyenyekevu yaani waislamu, na wala hawakuwa wakiristo, niseme kwa dhati kabisa nimefrahi sana kusikia hilo, lakini kwa bahati mbaya kabisa bado kuna tatizo kidogo pale unaposema hata nyie wakiristo ni wanyenyekevu hapana ndugu yangu, hapo utakuwa unakosea kabisa ndug yangu kwa kujaribu kuwapa sifa hii watu ambao hawana sifa hii. Ndugu Mhina Wakiristo ni watu waliomkataa Mwenyezi Mungu, badala yake wakasema Mwenyezimungu ana mtoto na mtoto wa Mungu nae ni Mungu. Ndugu Mhina watu wa namna hiyo hawawi waislam, wanyenyekevu bali wao huitwa makafiri na wala sio waislam, wanyenyekevu. Hebu tuone Allah anawaambia nini.

    QURAN SURA 4:AN-NISAI
    “171. Enyi Watu wa Kitabu! Msipite mipaka katika dini yenu, wala msiseme kuhusu Mwenyezi Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa(Yesu) mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu. Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.”

    Enyi wakiristo komeni kusema utatu , itakuwa heri kwenu, Mungu si wa tatu katika watatu, hapana Mungu ni Mmoja tu.sasa hebu tuangalie sura ifuatayo je ili tujue wakirito ni akina nani?

    QURAN SURA 5:AL-MAIDA
    “17. Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu. Sema: Ni nani mwenye kumiliki cho chote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika ardhi? Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi Mungu. Huumba apendavyo. Na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu.”

    Kwa hiyo ndugu wakiristo, Allah anasema nyie mmekufuru yaani kwa maana nyingine nyie ni makafiri na wala sio wanyenyekevu kwa maana mngekuwa kweli nyie ni wanyeyekevu msingekuwa ni imani potofu ya mungu katika watatu.Imani hii ya mungu katika utatu hata Yesu mwenyewe hakuwahi kuifundisha, bali huyo kafiri mkubwa Paulo ndiye aliyepandikiza imani hii baada ya kuona mbinu ya kuwauwa wanafunzi wa Yesu imeshindikana.

    Ndugu Mhina, baada ya kuona kuwa nyie, sio wanyenyekevu bali makafiri, nikunukuu hoja zako kasha nizitolee majibu.
    HOJA YAKO:“kwani wewe hujui kuwa alichokifanya bwana yesu ni kutimiza torati ileile walioitumia wale manabii wa mwanzo, na kamwe sio kuondoa na kuleta vitu vipya na vigeni kama alivyofanya nabii wako mhamad”

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina, kwanza naomba kabla hujaleta hoja, uwe unapitia biblia yako walau hata kwa uchache, Kwa kifupi biblia yenu inaonesha Yesu kapinga maneno ya taurati wazi wazi, kwa mfano sehemu moja anasema;
    Matayo 5:38 Mmesikia kwamba ilisemwa: Jicho kwa jicho, jino kwa jino. 39 Lakini mimi nawaambieni, usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la pili. 40 Mtu akikupeleka mahakamani kutaka kukuchukulia shati lako, mwache achukue pia koti lako.
    Je ndugu Mhina, unataka kuniambia huko si kupinga torati, je torati inasema ukipigwa kofi upande wa kulia geuzia shavu la kushoto? Kwa hiyo Yesu wa biblia ndiye anayeonekana kuondoa na kuleta vitu vipya tofauti na vile ilivyokuwa ndani ya torati na kamwe si quran tukuf.
    Na sasa tuone quran tukuf inatwambiaje Ndugu Mhina Halafu tupime nani kati ya Yesu wa Biblia na Mtume Muhammad ni nani aliyetengua maneno hayo ya torat.

    QURAN SURA 5:AL- MAIDA
    45. Na humo(kwenye torat) tuliwaandikia ya kwamba roho kwa roho, na jicho kwa jicho, na pua kwa pua, na sikio kwa sikio, na jino kwa jino, na kwa majaraha kisasi. Lakini atakaye samehe basi itakuwa ni kafara kwake. Na wasio hukumu kwa yale aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhaalimu.
    Sasa Ndugu yangu Mbona bwana yesu anapinga torati kwa wazi kabisa, lakini sisi hatuamini kama Yesu aliipinga torati bali ni waandishi wa biblia ndio ambao kwa lengo lao lile lile la kutaka kumkashifu Yesu kuwa alipinga torati wanajaribu kumchafua bwana Yesu ili aonekane kasema kinyme na torati.Ndugu Mhina huo ni mfano tu lakini zipo kauli nyingi mno ndani ya biblia zinazoonesha Yesu kapinga torati, pamoja na kuwa alisema amekuja kutimiza.

    HOJA YAKO TENA:Kwa hiyo basi, mimi bado nasisitiza kuwa “unyenyekevu” siyo dini wala sio njia bali hiyo ni sifa ya kawaida tu,

    JIBU LA HOJA: Nduku yangu Mhina, Unyenyekevu, yaani uislam ndiyo njia sahihi nay a pekee kabisa itakayokufanya uende mbinguni, na siyo kitu kingine, hata Yesu mwenyewe alilitambua hilo na ndiyo maana aliendelea kuwasisitizia hata wanafunzi wake wawe wanyenyekevu soma(Marko 10:13)”msipojinyenyekeza na kuwa kama watoto wachanga hamtauona ufalme wa mbinguni” sehemu nyingine anasema katika (matayo 11:29) “jitieni nira yangu na mjifunze kwangu kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu”, kwa hiyo ndugu Mhina unyenyekevu siyo kijisifa tu, kama wewe unavyodhani bali Yesu alitambua kuwa unyenyekevu ni sifa kubwa mno hivyo akawa anawasisitizia kila mara wanafunzi wake wasiache njia hiyo.Lakini hatuoni akiwaambia wanafunzi wake wawe wakiristo, hata siku moja, Kama Yesu angejua Ukiristo ni jambo kubwa basi angewaambia kuweni wakiristo lakini wapi, mwenzenu hakuwahi kusema hivyo, ila Paulo ndiye aliyeleta dini hii ya kigeni ambayo ni ya uongo hata Yesu haitambui, na wala hakuwahi kuisikia, na wala hakuiacha.

    HOJA YAKO:”Quran hiyohiyo inayopingana na kila jambo la Mungu wa kweli inasema”MUNGU AMESHAFUNIA TORATI NA INJILI KWA AJILI YA WANADAMU WOTE KUTAFAUTISHA JEMA NA BAYA,!!!.Tatizo ni nini hapo ndugu mhamad”

    JIBU LANGU: Kwanza kabisa naomba ujitambue jinsi ulivyochanganyikiwa na kukosa mwelekeo, hata hujui maneno unayoyaandika kwa sababu, umeshasema quran inapinga kila jambo la Mungu wa kweli halafu hapo hapo unatoa aya ndani ya quran ambayo unaamini kuwa ni ya kweli, sasa wapi na wapi ndugu!!!
    Pili hiyo aya haisemi kwamba torat imeshuka kwa ajili ya watu wote, kama ulivyojaribu kudanganya hapo juu.
    Pamoja na kuwa umeshajichanganya lakini tatizo lako lingine bado liko pale pale ni kwamba unapenda kunukuu nusu msitari halafu ukajifanya unatoa tafsiri bila kujua ni maneno yapi yanayoendelea, hiyo aya nainukuu vizuri kabisa hapa chini inasema hivi;

    Quran sura 3:AL-IMRAN
    “3. Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati na Injili
    4. ziwe uwongofu kwa watu wa Kabla yake, Na akateremsha Furqani (quran). Hakika walio zikanusha aya za Mwenyezi Mungu watakuwa na adhabu kali. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye kulipa.”

    Kwa hiyo ndugu, yangu ni kweli kabisa torat,injil na zaburi ilikuwa ni mwongozo kwa waislam waliopita kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w) lakin Allah alivyotimiza nuru yake ya dini hii ya Uislam kwa Mtume Muhammad akampa Furqan au quran ili uwe mwongozo kwa waislam Na iwakanye na kuwaonya watu makafiri wakiwemo wakiristo na mayahudi ili waachane na imani potofu ya kumuabudu mungu-mtu Yesu na waingie katika nuru ya Uislamu.

    HOJA YAKO : “Sasa ndugu mhamad, wivu wako hapo unatoka wapi mimi kusema kuwa “TUNA HAKI YA KUWAITA WAKRISTO WENZETU AU MABABU ZETU”?”

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina hapa nafkir, tutaparudia sana tu ndugu yangu kwa sababu ndipo panapothibitisha uongo wa dini yenu ya kikiristo.Ndugu Mhina wewe mwenyewe unajishuhudia unavopata shida mno kujitahidi kuzunguka na kukotoa lakini wapi unakwama.Hebu sasa naomba unipe kauli moja na yenye kueleweka, hao manabii wa zamani (a)walikuwa wakiristo? Au (b) mna haki ya kuwaita wakiristo wenzenu ingawa wenyewe hawakuwa wakiristo? Ukinipa jibu moja kati ya hayo mimi nitaacha kabisa kuuliza swali hili na itanisaidia kujua dini yao ilikuwa ipi ili niwafuate, hebu ndugu yangu samahani nipe jibu moja kati ya hayo maswali mawili hapo juu kwa maana naona huko kote ulikopita unazunguka mbuyu bila ku-specify jibu lako.

    HOJA YAKO“vitabu vyote vya kale vimehifadhiwa katika quran na mtume wenu, sasa hivyo vitabu ni vya nini ndani ya quran wakati wewe ulisema kuwa haviwahusu!!

    JIBU LANGU: Ndugu Mhina, hapo umeuliza swali zuri, ni kweli kabisa quran imejumuisha funuo zote zilizotangulia, ingawa hata manabii waliotanguliwa walipewa kwa ajili ya wana wa Israeli tu, lakini kwa ajili ya Ulimwengu sasa Allah amemtuma Mtume wake na akampa Quran yenye sheria sawa kabisa na sheria zilizokuwepo mwanzo, Ndugu Mhina hata biblia yenu inatambua kabisa kwamba manabii wa mwanzo walitumwa kwa watu wa Israeli
    EZEKIELI 4: Naye akaendelea kuniambia: “Mwanadam, nenda, uingie katikati ya nyumba ya Israeli, nawe lazima uwaambie maneno yangu. 5 Kwa maana hutumwi kwenda kwa watu wa lugha ngeni wala walio wazito wa ulimi, kwa nyumba ya Israeli, 6 si kwa vikundi vya watu wengi sana wa lugha ngeni wala walio wazito wa ulimi, ambao maneno yao huwezi kuyasikia ukayafahamu.kiwa ningekutuma kwao, watu hao wangekusikiliza wewe.

    Ndugu Mhina, huo ni mfano mmoja tu ndani ya biblia unaomhusu nabii Ezekiel, ambaye anapewa amri ya kuwaendea wana wa Israeli tu, na siyo kwa watu wanaotumia lugha asiyoifahamu yeye, yaani watu wa matiafa mengine akina sisi.Hebu tuangalie tena aya inayofuata kutoka ndani ya biblia.

    YONA 3: “Ndipo neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, na kusema:2 “Ondoka, uende Ninawi lule mji mkubwa, ukalitangazie neno ninalokuambia.”

    Ndugu Mhina, Hiyo amri anapewa nabii Yona aende Ninawi, sasa naomba nikuulize Tanzania kuna sehemu inaitwa ninawi? Ninawi ni mojawapo ya miji mikongwe huko Palestine ambako ndio makaazi ya wana wa israeli. Sasa kumbe hata biblia yenu inatambua kuwa manabii wa mwanzo walitumwa kwa ajili ya wana wa israeli.

    Hata Bwana Yesu mwenyewe anasema katika biblia (Matt. 15:24). “Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya lsraeli” sasa wewe mtanzania umeshaambiwa hakutumwa bali kwa kondoo wa Israeli wewe unataka mpaka akwambieje ili ujue hakutumwa kwa ajili yako?, tena sehemu nyingine ametutukana na kutuita mbwa soma (Matt. 15:26) ” Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa ” Binafsi siamini kama huyu ni Yesu wa kweli anayeporomosha matusi kwa watu wasiokuwa waisraeli, ni nabii gani ana matusi kiasi hiki! Yaaani sisi wasio waisraeli ndio mbwa? Halafu bado mnaendelea kulia makanisani, mkombozi wetu, mkombozi wetu, waapi nyie mshaitwa mbwa!!!! kwa hiyo ndugu Yangu Mhina haya sio maneno yangu bali ni maneno niliyoyatoa ndani ya biblia kitabu chako mkiristo yanayothibitisha kabisa kwamba manabii hao wa mwanzo walitumwa kwa ajili ya Wana wa Israeli.
    Soma hata kisa cha Musa
    (Kumb 1:1 )Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia, 2 Neneni na wana wa Israeli, mkiwaambia, Wanyama hawa ndio wanyama wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote walio juu ya nchi. “

    Lakini shangaa nyie wakiristo mnaodai kuwa mnafuata amri za manabii wa zamani, inapofikia aya kama hizo zinazohusu makatazo na sheria mnaanza kuruka viunzi na kudai haziwahusu bali zilikuwa ni kwa ajili ya wana wa Israeli, kwa mfano kama amri hiyo hapo juu inayohusu maswala ya vyakula vya nyama, amri ya kutahiriwa aliyopewa nabii ibrahim na amri nyingine nyingi tu kibao zimo ndani ya biblia yenu na huwa mnazikana mnapobanwa.
    Kwa mfano mzuri msome huyu mmiliki wa blog hii mosespk Click kwenye kipengele cha TEACHING/MAFUNDISHO hapo juu, utaona jinsi anavyoelezea agano la kale lilivyokwisha pitwa na wakati; na hapa nimemnukuu kidogo kwenye kichwa cha habari;

    By Mosespk “AMRI KUMI, TORATI NA AGANO LA KALE YOTE YAMESHAONDELEWA!
    Mungu alitabiri kwamba ataondoa agano la kale na kufanya agano jipya lililotofauti……….”
    Ndugu Mhina, huyu ni mkiristo mmojawapo tu ambaye kwa ushahidi wa biblia anaamini kabisa kuwa mambo ambayo yapo kwenye agano la kale ambalo nyie wenyewe mnadai ni vitabu vyenu vya wakiristo, yeye anasema vishaondolewa , sasa ni zama za agano jipya. Sasa mimi nawauliza wakiristo kama vitabu hivyo vishatolewa inakuwaje sasa mnaendelea kuvitumia kanisani? Lakini inapofikia vipengele vinavyowabana mnadai vimetolewa je huu si unafiki na ukigeugeu?
    Nikiendelea kumnukuu huyu mchungaji wa magomeni anayemiliki blog hii anasema

    By Mosespk “Misitari hii yaonya kwamba agano jipya linadumu bali agano la kale limebatilika”
    Ndugu Mhina, huyu ni mkiristo tena mchungaji na mwenye elimu ya dini kuliko wewe , mwenzio anaamini kabisa kuwa agano la kale lishabatilika zamani? Swali langu ni kwanini basi wakiristo mnaendelea kubebelea vitabu hivi ambavyo vishabatilika kila siku makanisani?Kumbe nyie mnatembea na vitabu vilivyobatilika na mnavitumia kwa ajili ya wokovu wenu?Du hii ni hatari sana , hii ni picha kamili kwamba na imani yenu imebatilika kwa sababu ya kutumia vitabu vilivyobatilika.

    Ndugu Mhina wakiristo wengi mno wanaamini kuwa agano la kale ilikuwa ni kwa ajili ya wana wa Israeli tu, na ndio maana wanapinga amri zinazokataza kula nguruwe pamoja na amri nyingi zilizo kwenye agano la kale wakidai Yesu, katengua amri hizo na kawaruhusu wale kila kitu.

    SWALI LAKO:Na wewe nikuulize hapa: kama nyinyi waislamu mnajua kuwa manabii na mitume wanaendelea kuongezeka au wapo(hawavumi lakini wamo) mbona na nyinyi pia mnasema kuwa mtume wenu ni mtume na nabii wa mwisho baada ya bwana yesu??, kwanini sisi wakristo hatukuhoji hivyo unavyo nihoji wewe?”
    JIBU LAKO: Ndugu Mhina, sisi hatuamini kama manabii wanaongezeka, hapana ndug yangu hakuna sehemu mimi nimesema hivyo labda uninukuu kama kuna sehemu nimesema kwamba waislamu tunaamini kuwa manabii wanaongezeka, kwa kurahisisha mjadala naomba nijinukuu nilivosema kwenye mjadala uliopita ili usiwapotoshe watu kwa uongo wako, kwa sababu nyie wakiristo ni kawaida yenu kusingizia waislamu.
    NUKUU “Sasa baada ya kuona kuwa biblia yenyewe inakiri kuwa Yesu sio nabii wa mwisho wa Mungu bali biblia inasema walikuwepo manabii hata baada ya Yesu kuondoka, sasa tuone Quran inatwambia nabii wa mwisho ni nani?”

    Hivvyo ndo nilivosema na baada ya hapo nikatoa aya ndani ya quran inayosema Muhammad ni Nabii wa mwisho. Sasa ndug yangu mbona unataka kulazimisha kufunga goli kwa mkono?Wewe ndo ambaye siku moja nilikwambia ukiristo una manabii kibao baada ya Yesu ukaruka mita 10 ukidai hayo ni matukio ambayo wewe huwezi kuyachanganya na dini yako sasa mbona biblia yenyewe inakusuta, inakwambia no! Yesu sio nabii wa mwisho. Kwa kifupi kabisa biblia haijasema nabii wa mwisho ni nani bali quran ndiyo inasema kwa uwazi kabisa kuwa nabii Muhammad ndiye nabii wa mwisho.

    Ndugu Mhina, kwa kuwa naona umekaukiwa na hoja, bali umebaki na maneno ya kubuni buni tu Naomba nimalizie mjadala wangu kwa leo na Aya ifuatayo.

    QURAN SURA 44:AL-FAT-HI
    29. Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele
    ya makafiri, na wanahurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama na kusujudu
    wakitafuta fadhila na radhi za Mwenyezi Mungu. Alama zao zi katika nyuso zao,
    kwa athari ya kusujudu. Huu ndio mfano wao katika Taurati. Na mfano wao katika
    Injili..”

    Kwa hiyo Allah anatuambia sisi waislamu kwamba hata manabii waliotangulia akina Yesu, Musa, Harun, Ibrahim walikuwa wakisali kwa kuinama na kusujudu kama waislamu, ambavyo nyie wakiristo mnasali kwa kupiga miziki.Pili Allah anasema sisi tuna nguvu dhidi yenu makafiri, kwa hiyo hata hoja zenu ni lazima ziwe dhaifu mbele ya hoja za waislam na mwisho Muhammad ni Mtume wa Mwenyzimungu, asiyemkubali na kumkataa. Ajiandae kwa ajili ya kuingia moto wa jehanam.
    Allah atuongoze Inshaalllah.

    Like

  154. mhina says:

    Ndugu Mhamad…Mimi nimekwishamaliza mjadala na wewe.Tuwaachie wafuatiliaji ili wachunguze kwa roho zao na kujifanyia maamuzi wao wenyewe.Usiendelee kuitetea dini yako kwa hoja za kitoto. Lakini kubwa zaidi ninataka ujue kuwa mimi ninakupenda sana sana wewe na waislamu wenzako wote, pamoja na tofauti zetu za kiimani. Mimi siwaoni kua nyinyi ni makafiri au ni watu wabaya ila ninawaona kama ndugu zangu wa karibu. Hii ndiyo sheria yetu sisi wakristo,Yaani upendo kwa watu wote.Aksante sana ndugu yangu Mhamad yohana, Mungu akubariki.

    Like

  155. Ndugu Mhina,
    Kwanza nimshukuru Allah aliyenijalia mimi kunipa uhai na afya lakini zaidi akanijalia kuwa muislam.
    Kwa kifupi niseme nakushukuru sana hasa kwa moyo wako wa kupenda kujifunza na kutaka kujua uislam tabia ambayo wakiristo wengi huwa hawana, naamini kabisa kwa uwezo wa Allah utakuwa umejifunza mengi kuhusu uislam na kwa kiasi chake kama Allah amekujalia utakuwa umetambua ukweli wa dini ya kiislam.

    Ndugu Mhina, naomba utambue kuwa propaganda nyingi mno zimetungwa na baadhi ya wakiristo wasioutakia mema uislam kujaribu kupotosha, hivyo basi naomba kupitia fursa hii tuliyonayo ukiwa na swali lolote kuhusu uislam usisite kuuliza walau kupitia blog hii, sisi kwa uwezo wa Allah tutakusaidia.

    Mwisho, Ndugu Mhina, neno kafiri siyo tusi ndugu yangu, bali ni neno la kiarabu linalomaanisha mkanushaji, au anayekataa, lakini zaidi maana yake ni mtu mkaidi au mwenye kiburi.
    Allah atujalie sote tuwe na moyo wa kujifunza zaidi inshaallah.

    Like

  156. alfa says:

    ubarikiwe kaka,nimefurah sana,kwa mfuatiliaj anajua hoja zilizochoka zisizo na mashko ni zipi,2kiondoa udini hata mwenyewe unajua kwamb ilibd uendelee kuwepo ili mrad 2,kafir even christian wanalo kwa asiyeamini,na ukae ukijua co silaha hilo neno,kama ni kwa mpingaji hata budha iman yao inapingwa na wasioamin so nao watawaita hvyohvyo makafir.KAKA UNANIFURAHISHA,ILA WAFUATILIAJ WATAONA KAMA KWELI MLIKUWA NA HOJA YOYOTE JUU YA WAKRISTO,C WEWE!UBARIKIWE KAKA,ACHA WAFUATILIAJ WAJIONEE NDUGU.BWANA AKUPE FAHAMU NA UJASIR WA KUAMUA. MERR CHRSMAS MA BRO.

    Like

  157. Ndugu Alfa,
    Naamini wewe ni mkiristo unaependa kujifunza na kujua ukweli, ila kwa bahati mbaya kabisa, hujajipanga kuufahamu ukweli ndugu yangu,lakini ndugu yangu Mhina ametuielewa na ametambua ukweli wa uislam, lakini ndugu Alfa nashindwa kuelewa bado unakwama sehem gani ili mimi nikusaidie. watu kama nyie Allah amewasema katika, quran;

    QURAN SURA 2:AL-BAQRA
    “170. Na wanapo ambiwa: Fuateni aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu; wao husema: Bali tutafuata tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawaelewi kitu, wala hawakuongoka? 171. Na mfano wa walio kufuru ni kama mfano wa anaye mpigia kelele asiye sikia ila wito na sauti tu — ni viziwi, mabubu, vipofu, kwa hivyo hawaelewi.”

    Kwa hiyo ndugu Alfa watu kama nyie ambao sisi waislamu tumewafikishia ujumbe halafu mkakataa kata kata kukubali na mkaendelea kufuata dini mlizowakutanazo baba zenu hata kama ni za upotofu, basi Allah anasema nyie ni viziwi, vipofu kwa hiyo hata tukiwaambia hamtaelewa, lakini wapo wakiristo wazuri wanapofikishiwa ujumbe wa Allah hawafanyi ubishi bali wanaingia moja kwa moja kwenye uislam, na hao Allah kawataja;

    QURAN SURA 5:AL-MAIDA
    “82. Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni Mayahudi na washirikina. Na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanao sema: Sisi ni Wakiristo. Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi.
    83. NA WANAPO SIKIA yaliyo teremshwa kwa Mtume utaona macho yao yanachururika machozi kwa sababu ya kweli waliyo itambua. Wanasema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini(uislam). Basi tuandike pamoja na wanao shuhudia.
    84. Na kwa nini tusimuamini Mwenyezi Mungu na kweli iliyo tujia, na hali tunatumai Mola wetu Mlezi atuingize pamoja na watu wema? «

    Ndugu yangu Alfa, ni kwa nini basi unakubali kuendelea kubaki kwenye giza? Allah amewasifia wakiristo ambao hawafanyi kiburi, tena hao ni viongozi wa kikiristo ambao wao wanapoiona kweli ya uislam, basi macho yao hujawa na machozi na hukubali kuingia katika dini hii, vip ndugu yangu bahati hii unaichezea ?

    Allah anaelezea siku atakayowatia watu motoni, basi walinzi wa motoni watawauliza watu wa motoni.

    SURA 67 : SURAT AL-MULK
    « 6. Na kwa walio mkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jahannamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo!
    7. Watakapo tupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka.
    8. Inakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara likitupwa kundi(la watu) humo walinzi wake huwauliza: Kwani hakukujieni mwonyaji?
    9. Watasema: Kwani! Ametujia mwonyaji, lakini tulimkadhibisha, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote. Nyinyi hamumo ila katika upotovu mkubwa!
    10. Na watasema: Lau kuwa tungeli sikia, au tungeli kuwa na akili, tusingeli kuwa katika watu wa Motoni!
    11. Watakiri dhambi zao. Basi kuangamia ni kwa watu wa Motoni! »

    Kwa hiyo ndugu yangu Alfa, Allah amekupa akili ya kutafakari bado ukiwa mzima wa afya, na ametutuma sisi waislam tuwaonye nyie wakiristo,na tuwafikishie ujumbe wake na siku ya mwisho atawauliza je aliwajia mwonyaji ?Alfa utasema ndiyo, alinijia kaka Yohana ila mimi nikaleta kibri, moto wa jahannam utakuwa unaunguruma kwa hasira, basi kama hautabadilika nina hofu usije kuwa miongoni mwa watu watakaokuja kujuta mno siku ya mwisho.

    Ewe ndugu alfa, siku zinakwenda na mauti yanakaribia kwa kila mtu ni vizuri ukautumia muda huu kutafakari, na kama ukiweza ukatafuta msikiti wa karibu ukatoa shahada yako na ukasilimu.
    Mwisho ndugu Alfa, sisi waislam usitutakie xmass njema kwa sababu maana ya kristmass wakristo mnaamin ni siku aliyozaliwa Yesu, Ambavyo sisi waislamu hatuamini kabisa kama Yesu alizaliwa tarehe 25/12/, lakini isitoshe sisi waislamu hatuwezi kufanya kitu ambacho hata historia yenyewe inaonesha Yesu hakufanya wakati akiwa hapa duniani, hakuna maandiko yoyote yanayothibitisha kwamba Yesu alisherehekea birthday yake, na waliofanya hivyo ni mbinu za kutaka kuwapotosha watu wengi kwa kufanya mambo ya uongo. Ukimuuliza mkiristo yeyote kwa nini unasherehekea christmass atakwambia ni siku aliyozaliwa mtoto Yesu, lakini ukimuuliza je una uhakika Yesu kazaliwa tarehe 25/12 atakwambia Yesu hakuzaliwa tarehe 25/12, sasa kumbe ile amri ya usiseme uongo mnaivunja huku mnaona.

    Ukitaka kujua tarehe 25/12 kilitokea nini soma Yeremia 52:31, hapo ndo utajijua jinsi mkiristo unavyoingizwa chaka.

    (Yeremia 52 :31 ) “Hata ikawa, katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na tano ya mwezi, Evil-merodaki, mfalme wa Babeli, katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, akamwinua kichwa chake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani.”

    Kwa hiyo ndugu wakiristo ni vema mjue kabisa hilo ndilo tukio lilotokea tarehe 25/Desemba na siyo kwamba ni siku aliyozaliwa Bwana Yesu, Lakini pia zimekuwepo tamaduni za kuchonga na kupamba miti ya christmass lakini hata biblia yenu imekemea vikali mambo kama hayo nashangaa kuona wakiristo hamsomi hata biblia yenu hebu soma

    (Yeremia 10 :3-4) :“Mila za watu si chochote, wanakata mti kutokana na msitu, na mchongaji anauchonga kwa patasi yake, wanaupamba kwa fedha na dhahabu, wanaugandanisha kwa nyundo na misumari ili usipate kutikisika”

    Kwa hiyo nyie mnafata mila za watu tu, ambazo hata biblia yenu ishasema si chochote, mila za kuchonga miti mkaipamba mkaita miti ya kristmass. Kwa bahati mbaya kabisa umekuwa ni msiba mkubwa sa hizi kila nyumba ya mkiristo unakuta imepambwa miti hii, kitu ambacho bwana Yesu mwenyewe hakuwahi kufanya wala wanafunzi wake hawakuwahi kusherehekea christmass wala ndani ya biblia yenyewe hakuna hata neno christmass
    Ndugu wakiristo somo la christmass na chanzo chake ni pana sana ila kwa mkiristo yeyote anayetaka kujifunza nakaribisha mjadala inshaallah sisi waislamu tupo kwa ajili ya kuwaelimisha nyie wakiristo.
    Ndugu wakiristo, sisi waislam hatuko pamoja nanyi katika kuvunja amri moja wapo kati ya zile kumi, yaani kusema uongo eti Yesu kazaliwa 25 Dec.sisi tunasema huo ni uongo unaostahili kulaniwa na si kazi ya Yesu bali ni kazi ya watu wenye nia mbaya na Yesu.
    Kwa hiyo enyi waislam ni haram kumtakia mkiristo kristmass njema iwapo utafanya hivyo utakuwa umeshiriki dhambi ya uongo.
    Acheni imani hizo rudini kwa Allah atawasameheni dhambi zenu inshaallah.

    Like

    • ALFA says:

      Kaka nilijua lazima utakurupuka ndugu na tatizo mlilonalo ni kukosa ufahamu,uokovu wak haupo ktk cku wala tarehe,ni kwa neema ndan ya iman ktk kristo,ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwokoz ndugu yangu,usitumie maandiko kutengeneza chuk baina ya watu ili hal kwel unaifahamu,mbna hampend aman?mi c wa hadith kaka,nnachokuona unapenda ligi ndo maana ukiishiwa hoja unaanza kuingiza chuk mlizonazo kwa hoja za kitoto sana,ila kwa sababu we u wa thaman mbele za mungu,na roho yako ni ya thaman sana,nnachokuomba tafuta faragh na mungu kwa mwez mzima,weka fikra zako ziwe huru,ukajimimine mbele za bwana akuambie yakupasayo na njia ya kwenda.kwa mtu aliezoea hadith jamb hli ni geni ila fanya na utajua injil c hadith,ni pumz ya mungu na uweza wake.nawapenda na Bwana akubariki,umaanishe na usijihesabie hak unapokwenda kujimimina mbele zake.NIMEISHIA HAPO MUNGU WANGU AKUTANGULIE UFUNGUKE.

      Like

  158. Ndugu Alfa,
    Kwanza nikupongeze sana kwa kujitokeza, kujaribu kujibu hoja, lakini kabla sijaendelea naomba nikunukuu;

    HOJA YAKO: “uokovu wak haupo ktk cku wala tarehe,ni kwa neema ndan ya iman ktk kristo,ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwokoz ndugu”

    JIBU LAKO: Ndugu Alfa, Nakubaliana na wewe kabisa kwamba christmass ni kumbukumbu/maadhimisho ya kuzaliwa Yesu, lakini swali langu ni moja tu; Je ni kweli historia au maandishi matakatifu yanaonesha Yesu aliwahi katika maisha yake kuadhimisha kuzaliwa kwake? Lakini pia je kwa ushahidi wa maandiko wanafunzi watukufu wa Bwana Yesu waliwahi kuadhimisha kuzaliwa kwa Bwana Yesu? Kama jibu ni hapana je nyie mlipata wapi maadhimisho haya? Kama si mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake nyie mlitoa wapi ndugu?

    Nilijua hautapata jibu ila kwa sababu sisi tupo kwa ajili ya kuwaelimisha, kwa kifupi tutawapa maelezo ya chanzo cha krismass;
    Kwa ushahidi wa maneno yangu tafuta kitabu cha “The compact History of Roman Catholic church”

    Ndugu Alfa, tukisoma katika Biblia tunaikuta tarehe 25 December, kuwa ni sikukuu iliyokuwa inasherehekewa na wapagani wa Babeli ambako Waisraeli walichukuliwa mateka. Hivyo sikukuu ya 25 Desemba ilikuweko kabla hata ya Kuzaliwa Yesu, na ilikuwa sikukuu ya wapagani wa Babebli wakisherehekea kuzaliwa kwa Mtoto wa Mungu JUA aliyeitwa TAMUZ.

    Ndugu Alfa, ukisoma kitabu hicho cha roman catholic church kinasema kuwa, Kulikuwa na Mfalme wa babeli aliyeitwa Nimrodi, na mke wake Nimrodi ambaye pia aliitwa Malkia wa Mfalme jina lake aliitwa Semiramis, baada ya Mfalme Nimrudi kufariki, Mke wa mfalme akapata mimba nje ya Ndoa.kwa sababu kupata mimba nje ya ndoa ilikuwa ni aibu hata kama mmeo amefariki, Ilimlazimu mwanamke huyo kuficha kitendo hicho cha mke wa mfalme kubeba mimba wakati mume wake amefariki, akatunga UONGO kuwa Mume wake HAKUFA ila alibadilika kuwa Jua (SUN), hivyo mionzi ya Jua wanayoiona ndiyo iliyomdunga Mimba. Wababeli kwa kuwa walikuwa waabudu mizimu waliamini Uongo huo na kuanza Kuliheshimu Jua (SUN) kama Mungu wao.

    Usiku wa kuamkia Tarehe 25 Desemba, Semiramis akazaa Mtoto aliyemwita TAMUZ, ambaye baba yake ni Mungu Jua. Imani yao ilienda mbali zaidi hadi kuamini kuwa tendo la Semiramisi kuzaa na Mungu jua yeye pia ni Mungu Mke na Mtoto wao Tamuz akaitwa Mungu Mwana. Kuanzia kipindi hicho wapagani wa Babeli tarehe 25 mwezi wa 12, waliweka sherehe kubwa ya kuzaliwa kwa Mungu Mwana Tamuz.

    Ndugu Alfa, tukiachana na maelezo ya kitabu hicho cha kiroma Biblia yako pia inatoa maelezo juu ya jambo hilo la kufanya sherehe ambayo mfalme aliitumia kufungua baadhi wafungwa, kama msamaha wakati wa sikukuu – kwa ushahid zaidi soma Yeremia 52:31

    Nabii Yeremia aliandika kitabu hicho zamani kabla ya Yesu kuzaliwa, taifa la babeli lilikuwa na Desturi ya kuweka huru wafungwa katika siku hii ya Kuzaliwa kwa Tamuz tarehe 25 Desemba. Enzi hizo haikuwa inaitwa Krismass huenda iliitwa Tamuz–Mass.

    Ndugu Alfa na wakiristo wote, naomba mjue kuwa baada ya Yesu kuzaliwa, hapakuwa na Sikukuu ya Krismass hata mitume hawakuwahi kusherehekea sikukuu hii, soma hata biblia yako uone ni wapi iliadhimishwa siku ya krismas,bali tunaona baada ya miaka mingi kupita karibia zaidi ya miaka 300 Mfalme Constatino wa Dola ya Kirumi aliyekuwa anaabudu JUA aliamua kuwa Mkristo, lakini hakutaka kuacha Desturi za kuifanyia sherehe miungu yake. Hivyo akaamuru sherehe ya kuzaliwa Mungu Mwana Tamuz iendelee kusherehekewa ila wakristo waambiwe kuwa ni siku ya kuzaliwa Yesu Kristo. Kulingana na kitabu cha Historia ya kanisa la RC, ambacho hata mimi ninacho, kinachoitwa “The Compact History of Roma cathoric church” kinaeleza juu ya tangazo la Mfalme Constantino kwa wakristo kuanza kuadhimisha sikukuu za kipagani ikiwemo Ibada ya JUA ya siku ya Kwanza (SUN-DAY) yaani siku ya Mungu jua badala ya Ibada ya Siku ya SABA ambayo ni jumamosi, historia inaeleza kuwa alitoa maagizo hayo akiwa bado mpagani (Kabla ya kubatizwa), tangazo hilo lilitolewa mwaka 325AD.

    Ndugu Alfa, Historia inasema, ilikuwa ni mwaka 336AD, ndipo kanisa lilipoamua kwamba, badala ya kuwa na sikukuu ya kipagani mjini Rome iliyojulikana kama “Natalis Solis Invincti” au The Birthday of the invincible/unconquered Sun, iliyosherekekewa tarehe 25 Desemba, sasa tarehe hiyo iwe si kwa kuzaliwa jua, bali iwe siku ya kuzaliwa mwana (son) wa Mungu – Yesu Kristo. Kwa mara ya kwanza kanisa lilikuwa linaendesha Misa tu, lakini baadaye mtindo wa sherehe za kipagani ikaingizwa hadi leo inaendelea – ikitawaliwa na Vinywaji (Vileo), Vyakula na starehe za kila namna.

    Ndugu Alfa na wakiristo wote, naomba muelewe sisi waislamu hatuipingi krismass kwa sababu ya uadui na chuki kama ndugu alfa ulivyoeleza bali ni kwa sababu ya chanzo chake ambacho ni upagani, ni sherehe iliyotoka kwa mapagani wa kiroma ambao waliamua kuingiza mila hizo katika ukiristo.

    Maneno hayo si yangu bali nimeyatoa katika kitabu cha kanisa kongwe na kanisa ambalo makanisa mengine yamezaliwa kanisa la waroma wenyewe nilichokitaja hapo juu, naomba ukitafute ndugu yangu ili ujionee mwenyewe.

    Maelezo hayahaya kama ulibahatika kutazama TBC siku ya krismass wakati wanaeleza chanzo cha krismass basi utakuwa huwezi kupinga ukweli huu kwa maana walitoa maelezo haya walikuwa ni wakiristo wenyewe kupitia TBC na wala hayakuwa maelezo ya waislam.

    Mwisho naona unapenda kuongelea suala la Hadithi katika uislam, ni imani yangu hujui nini maana ya hadithi katika uislam ila samahani kama una idea yoyote, naomba uelezee ili mimi nikusaidie utakapokwama, kwa maana naona huelewi unachokichallenge hasa kuhusu hadithi, kwa hilo nipo tiyari tulijadili ili nikueleweshe kwa kina.

    Allah akufungue macho ndugu yangu Alfa,uuone uongo wa ukiristo na siku moja utoe shahada na uwe muislam inshaallah.

    Like

    • alfa says:

      ndugu mhamad.mi cna muda wa kujadiliana na wewe,uelewa wako bado,au labda quran imekufanya udumae fikra na mawazo kiasi hcho,mtu yeyote atakaefuatilia mjadala huu toka mwanzo mpaka hapo ulipofikia,unaonyesha bdo sana,fikra zako hazipo huru ndo maana toka ulipokuwa na mhna mpaka sasa bdo hujaonyesha kupevuka,hebu tuwaachie wafuatiliaj ndugu yangu,umeshakir kuwa uokovu ni kwa neema ndani ya iman ktk Kristo na si cku wala hyo miungu jua yako,naokolewa kwa neema na iman ndani ya Yesu,sasa ka kuna mkrist mweny iman ktk jua sawa.NAOMBA UWAACHIE WAFUATILIAJI SASA,USHAURI WANGU NILIOKUPA UUFANYIE KAZI,NA JITAHIDI KUWEKA FIKRA ZAKO HURU UNAPOJIFUNZA.UBARIKIWE SANA MUNGU AKUTIE NGUVU,NAWAPENDA WOTE ILA NAONA INATOSHA,AHSANTE KAKA.

      Like

  159. Ndugu Alfa,
    Nizitangulize shukrani zangu kwa Allah.

    Pili nikushukuru na niwashukuru wakiristo wote mliochangia ktk mijadala mbalimbali, shukrani za pekee kwa Ndugu Mhina pia.

    Ndugu zangu, naomba mjue kuwa lengo letu sisi waislam si kubishana wala kutafuta mshindi, hapana ndugu yangu, lengo letu ni kutoa elimu kwa watu wamtambue Allah(S.W) na watambue kuwa Allah ndiye aliyeumba kila kitu na wajue kuwa Allah peke yake ndiye anayestahili kuabudiwa.
    Pia lengo letu ni kuondoa na kuyafutilia mbali mafundisho yote ya uongo na propaganda chafu zinazotungwa na baadhi ya viongozi wa kikiristo kwa ajili ya kuuchafua uislam.
    Mwisho tunaomba mtumie fursa hii pekee, kuhusu ujumbe wa Allah tuliowapa kupitia blog hii kwa ajili ya kujifunza zaidi kuhusu uislam, badala ya kusikiliza maneno ya watu wasioutakia mema uislamu.

    Tuko tiyari kayapatia majibu kila aina ya maswali mtakayokuwa mkiuliza kuhusu uislam hasa kupitia blog hii.Tunaomba msichoke kadri mtakavyojaliwa.

    Wabillah tawfiq, wahaadha ssalaam.

    Like

  160. Enyi ndugu wakiristo,

    Sisi Waislamu tunaamini kwamba Bwana Yesu a.s. alikuwa Nabii wa Mungu. Na manabii wote ni watukufu na wapendwa wa Mwenyezi Mungu. Wanatoka kutoka koo takatifu.

    Kwa hiyo sawa na mafundisho ya dini ya Kiislamu tunamheshimu Nabii Isa a.s. (Yesu) na pamoja uzao wake na tunaamini kabisa wote walikuwa watukufu. Kinachotushangaza sisi waislam ni wakati tunaposoma Biblia, tukaona Biblia inamfedhehesha na kumchafua Yesu (A.S) vibaya mno. Licha ya kuwa biblia inatambua kuwa Bwana Yesu alikuwa ni Nabii na Mtume wa Mungu, Biblia hiyo hiyo inadhalilisha ukoo na uzao wa Bwana Yesu.

    Ewe ndugu Mkiristo, ukisoma Biblia katika ;
    (MATAYO 1:5), Utakuta inasomeka hivi; Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu.“

    Ewe ndugu Mkirsto,Ukisoma tena biblia katika:
    (YOSHUA 2 :1) inasema hivi ; Rahabu alikuwa kahaba.

    Ewe Ndugu Mkiristo, Rahabu ni katika uzao wa Yesu, na hapo biblia inasema alikuwa kahaba

    Hivyo ndivyo biblia inavyoanza kumtukana Yesu, kwa kutukana ukoo wake kwamba walikuwa makahaba; waislam tunasema INNA LILLAH WA INNA ILAYH RAJIUN, ni msiba ndugu zangu.

    Enyi ndugu wakiristo biblia yenu haihishii hapo katika swala zima la kumtukana Yesu, bali inaendelea;

    “Yuda alimzaa Peresi na Zera kwa Tamari (Mathayo1:3).”

    Kaitka kitabu cha ukoo wa Yesu cha Mathayo kinatwambia kwamba Tamari ni miongoni mwa mabibi wa Yesu.Lakini hebu ndugu Mkiristo soma hapa chini uone Tamari hasa kazi yake ilikuwa ni nini?

    “Tamari alikuwa kahaba na mzinifu. (Mwanzo38:13-18).”

    Enyi ndugu wakirsto , hakika matusi ya biblia kwa ukoo wa Bwana Yesu hayaishii hapo bali ukisoma kitabu hicho hicho cha Matayo kinatwambia;

    “(MATAYO 1:6). Daudi alimzaa Sulemani kwa yule mke wa URIA Beth Sheba”

    Sasa naomba tuangalie huyo URIA alikuwa nani katika kitabu cha Samweli;

    “(2 SAMWELI 11:2-5).mkewe URIA alipata mimba ya zinaa. “

    Enyi ndugu wakiristo Biblia yenu inaonesha kuwa hawa mabibi wote wa Yesu Kristo walikuwa makahaba na wazinifu. Lakini sisi Waislam hatukubaliani na Biblia bali tunaona kwamba ni taka taka na uchafu na ni malengo ya kumdhalilisha Yesu.Hivyo basi kwa sababu sisi waislam tunampenda Yesu, hatuko tiyari kuona uzazi wake ukidhalilishwa na biblia, kwani sisi tunaye Allah na Allah ashatwambia kuwa ukoo wa Yesu ni ukoo mtakatifu, soma QURAN SURA 19:29

    Enyi ndugu wakiristo, naamini kabisa kama kweli mnampenda Yesu, mtakubaliana na mimi kwamba biblia ilichokifanya kwa ukoo wa Yesu mtakatifu wa Mungu sicho bali ni upuuzi na uzandiki wa hali ya juu, sisi waislamu hatuamini na wala hatuwezi kukubali kwamba Yesu(A.S) katokea katika koo na familia za makahaba na wazinzi, bali tunaamini katokea katika koo za watu wema kama (quran 19:29) na (Quran 5:75) inavyotwambia kwamba uzao wake ulikuwa umebarikiwa na wala haukuwa uzao wa wazinzi kama biblia inavyosema.

    Ndugu wakiriso, kama kweli mnampenda Yesu mlango uko wazi, karibuni katika uislam mtakutana na watu wanaompenda Yesu ambao hatuko tiyari kuona Bwana Yesu nabii wa Mungu akidhalilishwa kwa namna yoyote ile.

    Karibu tujadili.

    Allah atupe ufahamu, Inshaallah.

    Like

  161. shaaban says:

    A. ALAYKUM shukran kwako ndugu muhammed yohana ila ndugu yangu alfa alikuwa na fujo sana huko juu ila alhamdulillah ametulia ila namshangaa sasa kwa nini anaukimbia mjadal wakati alikuwa na hamu nao sasa….naamini huu ndio muda muafaka kwake kuuliza yale maswali yake ili inshaallah tumsaidie…..wabillah taufiq

    Like

  162. Ni kweli Kabisa unavyosema ndugu Shabani hawa ndugu zetu wanahitaji msaada mkubwa mno wa kiroho, hivyo ni bora tuutumie muda wetu kuwasaidia isije ikafika siku wakatulaumu kuwa hatukuwaambia.Na sisi tunataka tuwasaidie waepuke na adhabu za Allah siku ya mwisho, kwani Allah anasema Katika Quran.

    SURA 25. SURAT AL FURQAN
    22. Siku watakayo waona Malaika haitakuwa furaha siku hiyo kwa wakosefu. Na watasema: Mungu apishe mbali!
    23. Na tutayaendea yale waliyo yatenda katika vitendo vyao, tuvifanye kama mavumbi yaliyo tawanyika.
    24. Watu wa Peponi siku hiyo watakuwa katika makaazi bora na mahali penye starehe nzuri.
    25. Na siku zitapo funguka mbingu kwa mawingu, na wateremshwe Malaika kwa wingi,
    26. Ufalme wa haki siku hiyo utakuwa wa Arrahman, Mwingi wa Rehema, na itakuwa siku ngumu kwa makafiri.
    27. Na siku ambayo mwenye kudhulumu atajiuma mikono yake, na huku anasema: Laiti ningeli shika njia pamoja na Mtume!
    28. Ee Ole wangu! Laiti nisingeli mfanya fulani kuwa rafiki!
    29. Amenipoteza, nikaacha Ukumbusho, baada ya kwisha nijia, na kweli Shet’ani ni khaini kwa mwanaadamu.

    Enyi wakiristo hayo si maneno yangu bali ni maneno ya Allah aliyetuumba sisi wanadamu, akaumba mbingu na nchi na kila kilichomo, Allah anasema siku hiyo itakuwa ngumu mno kwa makafiri na Allah anasema siku hiyo watu watajiuma mikono na waseme laiti ningelimkubali Mtume Muhammad, sub-hana llah, mtakuwa mmechelewa ndugu zetu,kwa hiyo lazima mjue kuwa Mwenyezimungu ni mmoja na dini ya kweli ni moja nayo ni Uislamu, na mtume wa mwisho Ni Muhammad ibn Abdullah (S.A.W),na hakuna jinsi nyingine ya kumpenda Yesu bali ni kuwa muislam.Bali mkikataa kuitikia wito huu Allah anasema katika quran.

    QURAN SURA 29. SURAT AL A’NKABUT
    68. Na nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye mzulia uwongo Mwenyezi Mungu au anaye kanusha Haki inapo mjia? Je! Si katika Jahannamu ndio yatakuwa makaazi ya makafiri?

    Kisha Allah haishii hapo bali anasema;

    SURA 32. SURAT ASSAJDAH
    22. Na ni nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye kumbushwa kwa Ishara za Mola wake Mlezi, kisha akazikataa? Hakika Sisi tutajilipiza kwa wakosefu.

    Enyi wakiristo, sisi tumewakumbusha kwa ishara zote mkikataa au mkikubali, sisi kazi yetu ni kufikisha ujumbe wake Allah tu;

    Fanyeni hima muusome uislam, muelewe wala msikimbilie maneno ya kuambiwa na baadhi ya viongozi wenu wasioutakia mema uislam, tafuteni quran na vitabu vingine mjisomee wenyewe kwa Uwezo wa Allah mtaipata nuru Ya Uislam.

    Allah awaongoze kwa uwezo wake na mapenzi yake awalete kwenye nuru ya uislamu Inshaallah.

    Like

  163. Rich says:

    kaka, hizo hukumu ulizozitaja, sisi wakristo hazituhusu kabisa. Ila, hizo zinawahusu waislamu wote mbele ya Mungu wao Allah atakazozitekeleza kule jehanam kwake kwenye vitanda vya kulalia na mabibi wazuri aliowaandalia nyie wafuasi wake kama malipo yenu. Allah amenishangaza sana, yeye aliteremsha sheria zinazoitwa “sheria za israel pekee” lakini kupitia nabii wake Mhammad, akazijaza kwenye kitabu kitakatifu cha waislamu(quran) wakati anajua wazi kuwa sheria hizo na vitabu hivyo sio vyakwao!, halafu tena, akateremsha sheria zinazoitwa, sheria za waislamu, akachanganya madawa kwenye kitabu kimoja hichohicho cha quran huku akisema kuwa, sheria hizo za pande mbili ni sawa..tena zinafanana kabisa!. Kama Allah anasema kweli, ni kwanini yeye atoe miongozo miwili ya sheria zinazofanana katika kitabu kimoja halafu eti awape watu mafungu hayo wakati watu wote hao ni wanaadamu aliowaumba yeye mwenyewe!!. Kama sheria hizo zinafanana iweje zirudiwe mara mbili kwenye kitabu kimoja?…haya ni maajabu ya Allah katika muongozo wake kwa waislamu!.

    Like

  164. Rich says:

    nabii ni mtu anaetumwa na Mungu kwa ajili ya watu ili kuwafikishia watu hao ujumbe wa Mungu. Bwana yesu ni nabii aliyetumwa na Mungu ili kutuletea injili. Waislamu wanadai kua bwana yesu ni nabii wao, (wanamuita nabii isa). Sasa kama ni nabii wao mbona wanaikataa injili yake kwa kusema kuwa ni ya israel pekee!!

    Like

    • alfa says:

      kitu nlichojifunza ni kwamb ndugu zangu waislam c kwamb hawaelewi,ila hubishana ili kutimiza matakwa ya dini,wanadai wanapigania dini na hapo pana tatizo,kuna mmoja huko juu alidai kwamb kanisa limejengwa juu ya mwamb ambaye Bwana Yesu alimuita shetani,lakini akaruka sababu ambayo ilimfanya Bwana amkemee ambayo ni hii,BWANA YESU ALIZUNGUMZIA HABARI ZA KIFO CHAKE NA KUFUFUKA KWAKE KAMA ILIVYOTABIRIWA NA MANABII WA KALE WAKISEMA(ALICHUBULIWA KWA AJIL YETU,AKAUTOA UHAI WAKE KWA FIDIA YA DHAMB ZETU,PETRO ALIPINGA,NDIPO BWANA AKASEMA NENDA NYUMA YANGU WE SHETAN MAANA HUYAWAZI YA MUNGU BALI YA WANADAMU,NI VIZURI WATU WOTE WAWE NA BIBLIA ILI WAPATE MAARIFA,KWA SABABU NABII ASEMAYE UONGO ALIYETABIRIWA AMEKWISHA KUJA ILA BADO HUKUMU YAKE TU,HUJIENEZA KWA UONGO,UZUSHI.dat y nimewapa ushaur wa mwisho uwapasao,usitetee dini kwa hoja zisizo hai,kana kwamb unajadil na mtoto,nimemalizana nao labda nione hoja itakayonigusa.

      Like

    • shaaban says:

      amani iwe kwako ndugu……sasa yesu ni nabii ama mungu??? mbona sasa wakristo wenyewe kwa wenyewe mnajichanganya???? njoo kwenye uislam ndugu yangu….no contradiction.

      Like

    • takbir! takbir! ndugu zangu waislamu endeleeni kuwapa dawa’a hawa wakristo leo rich anakubali kwamba yesu si mungu bali ni nabii wa m/mungu alikuja duniani kuleta injili! ah aha ha ha ha ha ha chezea QURANI wewe waulize marekani na europe utaipata habari yake wazungu kokoko wanaukimbilia uislam wanaachana na ukristo

      Like

  165. alfa says:

    kitu kingine huwez kumfananisha muhammad na Emmanuel(Mungu pamoja nasi)wala Musa,kuna m2 amedai eti muhammad amekufa yuko mbinguni ka Musa na wakristo wanavyoamini kuhusu emmanuel,hawafanani hata kidogo,muhammada hayupo mbinguni,amekufa ameoza yupo anasubiri hukumu na hatujui kwamb wapi,pazur ama pabaya,ila Musa alinyakuliwa kwenda mbinguni alipokufa,hamna kabur la Musa wala Eliya,Yesu aliutoa uhai wake kisha akautwaa akapaa akaenda mbinguni,watu tuliobak pamoja na muhamad hamna awezaye kuhukumu juu yao,wameoza makaburini nao wanasubri saut ya emmanuel watoke humo kwa jins ajuavyo Bwana,wakirudiwa na uhai ili kuhukumiwa.

    Like

    • alfa says:

      halaf wanadai muhammad alihubir dini nch fulan ya kiarabu,asilmia tisini na tano wakawa waislam,na baadh ya wayahud wakasilimu,mbele ya upanga hata myahud ataleta unafki kuokoa roho yake,hujasoma kweny quran mauaji ya zaid ya wayahud 600 ktk mji alioutaja yanavyopewa sifa?nenda ziara israel utawakuta wayahud wakikristo weng tu wanaamin kwamb Kristo amekuja,na watakuelezea namna wanavyojipanga kutimiza neno,HALITASALIA JIWE JUU YA JIWE,MSKITI ULIOJENGWA JUU YA HEKALU LA SULEIMAN LAZIMA UVUNJWE NA HEKALU LISIMAME UPYA NA MICHANGO INAENDELEA KWA KAZI HYO,HII INATOSHA KUKUONESHA HAKUNA MYAHUDI MWENY IMAN KTK UISLAM LABDA KA ANATAFUTA K2 KUJILINDA NA MAADUI ZAO,leo hii kuhubir injil arabun ni kosa,lakin amerika na nch za ulaya wako huru waislam na miskiti wanajenga,kumbatiza mtu arabun ni kifo lakn kumsilimisha mzungu newyork hamna kesi,dini ya ajab sana hii,inawalazimisha watu kuelekea kuzimu na eti Allah anawalazimisha wa2,silimuni ama mfe!Mungu we2 halazimish,amewapa watu uwezo wa kuchagua,Allah katoka wap?

      Like

    • shaaban says:

      Amani kwako ndugu….hivi unaamini kama mussa alikufa?? au alipaa kama yesu kama alikufa atakuaje mbingini wakati kaburi lake liko palestine muda huu,kwa hiyo na yeye anasubiri hukumu si ndo unavyomaanisha au???…..kua muelewa rudi huko juu usome vizuri ndo upost hayo maelezo yako….kwa

      Like

    • shaaban says:

      Toaga na ushahidi basi ndugu yangu kwa sababu hua unaongea bila evidence
      “hamna kaburi la Musa wala Eliya:” mmh kweli au hayajulikani yalipo???

      Like

  166. Rich says:

    ooh mara vitabu vya nyuma vilikuwa vya israel pekee, halafu quran imekuja kwa ajili ya watu wote….mara tena, ooh, vitabu vya nyuma vya manabii vimeandikwa vyote na mtume wetu mhammad katika quran, hivyo, sheria zile zote za manabii wa nyuma zinafanana na ni sawa kabisa na sheria za Mhamad, mara tena ooh manabii wa nyuma wote walikuwa ni waislamu wenzetu wakiswali kama sisi, mara tena ooh, hapana walitumia vitabu vya Muongozo tofauti yaani tor, zab, injil, na sisi leo hii tunatumia quran!!!!!!…dini hii haieleweki chimbuko lake na kusudi lake hata kidogo, ijapokuwa itatetewa kwa nguvu kubwa mno mno.Inanisikitisha sana. Hebu bwana mhamed yhana jaribu kutetea dini yako kwa maelezo yanayoeleweka tafadhali…yaani watu watumie biblia biblia halafu waswali kama waislamu wanavyoswali misikitini!!, sijawahi sikia hiyo…na kama vitabu vyao ni tofauti kutokana na nyakati zao, iweje ibadazao ziwe sawa? Pia kama vitabu vyao vinafanana na ibada zao zinafanana , iweje Mungu awatenganishie vitabu vyao katika jambo lilelile linalofanana wakati Mungu wao ni huyohuyo mmoja?!, maajabu maajabu ya mzee Rajabu.

    Like

  167. Rich says:

    hakuna kufuru kubwa ya waislamu nisioipenda kama ile kufuru yao ya kusema kuwa ” Manabii wote wa Mungu waliopita yaani wakina Musa, daudi, ibrahimu baba wa imani, mpaka bwana yesu, eti ni manabii wadogo ila nabii mkubwa kuliko wote tena nabii aliyetukuta, Rais wa manabii wote ni huyu ndugu yao mpendwa Mhammad akiongozwa na Mungu wao Allah sub ana uwa taaaaaalah!!!!…hapa wanaharibu na kupotosha kabisa kabisa njia na kusudi la Mungu kwa watu wote. Naandika haya lakini naumia mno moyoni mwangu kuona kuwa kumbe hapa duniani kuna wanaadamtu ambao wako gizani kabisa bila ya wao wenyewe kujielewa.

    Like

  168. Rich says:

    eti mtu na akili zake timamu, anakwenda kuchukua maandiko ya mwanzo yaliyoandikwa maelf ya miaka halafu anakuja kuyaoanisha na maandiko ya injili ili asingizie kuwa bwana yesu katukanwa na biblia!!, umesoma shule gani wewe?, hivi unajua umbali wa miaka ya mwanzo na miaka ya vitabu vya joshua mpaka nyakati alizozaliwa bwana yesu urefu wake?, mbona sasa hukuchukua na andiko la ibrahimu alivyotembea na mjakazi wake na kumzaa ismail ambae nyie waislamu mnasema ni uzao wa Mtume wenu mhamad?, je, muhamad anaweza kuwa salama kwa njia hiyo pasipo kuonekana katukanwa?. Kwa upande wa bwana yesu, mimi nitakujibu kuwa hausiki katika kizazi hicho cha kibinaadamu kwa kuwa yeye alizaliwa kiroho kwauwezo wa roho mtakatifu kupitia bikira. Sasa sijui nabii wako itakuwaje kwa upande wake!. Uwezi kumhukumu mtu kupitia maisha ya watu wengine hata kidogo, maana kila mwanadamu aliletwa na mungu kwa makusudi yake mwenyewe. Babu yake mhammad alikuwa mchawi na mpagani, mbona hapo hukuilalamikia quran kuwa imetukana ukoo wa mhamad?.

    Like

  169. Rich says:

    jamani ndugu zangu waislamu, hebu itazameni quruani jinsi ilivyomtukana raisi wa manabii wote mtume wenu mhamad, yaani imemuelezea kuwa ni muuaji aliyeua zaidi ya wayahudi 600, pia imemuelezea kuwa ni mtume aliyewaoa watoto wadogo wa miaka 6-8, ambapo, kiukweli huu ni umri wa watoto wetu wa shule za primary na chekechea, je, ndugu waislamu, huo sio ubakaji ulioelezewa na quran dhidi ya rais wenu wa manabii aliyetukuta mtume wenu mhamad?’ tena quran haikutaja ukoo au ndugu zake ila imemlenga mojakwamoja rais wenu wa manabii kua ndiye mhusika mwenyewe. Haya sio matusi wapendwa???

    Like

  170. Rich says:

    eti tamari alikuwa bibi wa yesu, tuonyeshe kimaandiko sehemu ya biblia inayoweka wazi kuwa bibi yake yesu aliitwa tamari!!….au unataka namimi nikufukulie bibi yako wa kihistoria aliyekufa miaka elfu kumi iliyoita kuwa alikuwa ni mchawi?, kwanza hivi unamjua bibi yako aliyemzaa bibi yako akamzaa bii yako aliyemzaa bibi yako akamzaa bibi yako aliyemzaa bibi yako akamzaa bibi yako..mara elf kumi…unayajua maisha ya huyo bibi yako wa mwisho yalivyokuwa?!!

    Like

  171. Rich says:

    nakupa muda bwana mhamad yohn unijibu hoja zote huko juu mpaka hapa chini nione kama upo sahii au janja ya nyani tu, ukimaliza nitakuhoji mambo mengine.

    Like

  172. alfa says:

    hawa jamaa wanatafuta kasoro ambazo hazipo kwa wakristo bal kwao,dat y mi nimewaambia,tatizo lao ufahamu ama kukurupuka kukosoa bila kuangalia anajikosoa ye mwenyewe au vp,YESU HAUHUSIK KTK UZAO WA KIBINADAMU,NI KAZ YA ROHO MTAKATIFU KUPITIA BIKIRA,MUHAMAD UKIMFUATILIA SI HATARI!!!,BIBLIA IMEONYESHA MAISHA YA MITUME WOTE,NGUVU ZAO,NA MAHAL WALIPOKOSEA IL KANISA TUJIFUNZE KUPITIA MAISHA YAO KWA UWEZO WA ROHO,QURAN IMETUNGWA DAT Y INAONGEA BILA KUJITAMBUA,MANABII WOTE WALIZALIWA NA WANADAM NA BINADAM HAWEZ KUWA MIA KWA MIA MKAMILIFU,LABDA KAMA KWENU NINY HAWA JAMAA WALIKUWA MIUNGU,MUNGU WA ELIYA NDIYE MUNGU WANGU,YULE ALIYEZUNGUMZA NA ISRAEL KTK WINGU AMEZUNGUMZA NA MIMI KTK KRISTO,ALITUMIA WINGU KUFICHA ROHO AK,AMETUMIA MWIL KUFICHA ROHO AKE,halafu hawa jamaa wanajifanya wanaposwal wanaangalia kibra,ukiwauliza wanadai mbna daniel alifanya hvyo.DANIEL ALIANGALIA MASHARIK AMBAKO KUTOKANA NA MAHAL ALIPOKUWEPO,KULIKUWA JERUSALEM,KAMA KIBRA NI MASHARIK HAWA JAMAA WANAANGALIA CHNA NA INDIA.

    Like

  173. alfa says:

    HALAFU CKU HZI HATUMUABUDU MUNGU JERUSALEM WALA MLIMA SAYUNI,WAABUDIO HALIS HUMUABUDU BWANA KTK ROHO NA KWELI,TENA KUNA WAZUSH WENGINE WANADAI KUMUABUDU BWANA KTK ROHO NA KWELI NI KUABUDU MUNGU MMOJA,HUU UZUSH MTUPU,TANGU HAPO ISRAEL WALIKUWA WAKIABUDU MUNGU MMOJA NA BWANA YESU ALILIKUTA HLO,KTK ROHO MTAKATIFU LAZIMA ISHARA ZIWEPO,WATU WATANENA,WENY KARAMA YA KUFASIR WATAFASIR UJUMBE ILI KULITIA MOYO KANISA AU KULIJENGA MAANA NI MUNGU ANAZUNGUMZA NA KANISA,WATU HAWATAABUDU KWA MAZOEA BALI KADR ROHO ANAVYOONGOZA,NA WENG WATAMIMINWA MBELE ZA BWANA,NA KUTABIRI PAMOJA NA WATU KUMUADHIMISHA BWANA KWA MATENDO MAKUU TOKEA ROHON MAANA NI MSUKUMO WA NDANI,HAPO ISHARA NA MIUJIZA BWANA ANAWEZA AKATENDA HATA BILA KUWEKEWA MIKONO.NI MUNGU ANAKUWEPO KTKAT YA KUSANYIKO LA WATU WAKE,so msipotoshe maana mtukuzeni Mungu pamoja nami,HALELUYAH!!!

    Like

  174. alfa says:

    MMOJA AKADAI,TUNAJUAJE KAMA YESU ALIVYOJARIBIWA NA SHETANI ALIANZA KUHUBIR MANENO YA SHETANI,HATUSEMI TUNAJUAJE,MAANDIKO YANASEMAJE?SHETAN HATAMSHINDA MUNGU CKU YOYOTE!YESU ALIMSHNDA SHETANI KWA MAANDIKO HATA KA SHETAN NAYE ALITUMIA MAANDIKO KTK KAZ YAKE YA UPOTOSHAJ KA WAISLAM WANAVYOJARBU KUFANYA CKU HZI LAKN YESU ALIMSHNDA KWA MAMLAKA,SASA VP MUHAMMAD ALIPOJIKUTA ANAZUNGUMZA MANENO YA SHETAN,YALE AMBAYO GIBRIL HAKUMUAGIZA?MSIBADIL VIFUNGU,QURAN IMEFANYIWA MAREKEBISHO MENG NA AYA NYING ZIMEONDOLEWA,ILI KUJIDEFEND HAWAISH KUTUNGA UONGO USIO NA USHAID KUHUS BIBLE.KAMA KUNA MABADILIKO KUHUSU BIBL.

    Like

    • Ndugu Rich,
      Naomba kwanza kabla hujajadili ujue unachokijadili otherwise utaaibika kama ndugu zako wanavyoaibika kila siku humu kwenye blog,.

      Ndugu Rich usitake kuchekesha walionuna ndugu yangu, hivi uliambiwa na nani kwamba manabii waliopita walitumia biblia?

      Ndugu rich unaposema biblia maana yake ni Kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo na hiyo ndiyo biblia, pungufu ya hapo hata kwa msitari mmoja au pungufu ya kitabu kimoja katika hivyo haiwezi itwa biblia.

      Hivyo basi lazima ujue kwamba kuna tofauti kubwa kati ya biblia na torati na injili na zaburi.Nabii daudi hakutumia biblia bali alitumia zaburi, nabii Musa hakutumia biblia bali alitumia torah. Hivyo basi unaposema manabii walitumia biblia hebu nambie walitumia biblia gani ambayo haina kitabu cha Matayo, Marko, Yohana,Matendo n.k? Hivi unataka kuniambia nabii Musa, Daudi,Suleman, Ibrahim, Nuhu walitumia biblia yenye Matayo, Matendo,Marko, Galatia? Ndugu Rich kwa ushahidi gani utajaribu kusema hao walitumia biblia? Mbona hata unashindwa kutumia akili ya chekechea tu ndugu yangu?

      Ndugu Rich ni lazima pia ujue kuwa hata Bwana Yesu hakutumia Biblia na hata hilo neno biblia Bwana Yesu hakuwahi kulijua wala kulitamka katika maisha yake, bali hata neno biblia lenyewe hata ndani ya biblia yenyewe halimo, which means hata biblia yenyewe haitambui kama ni biblia.

      Ndugu Rich, sisi waislam ndio maana tunatambua na kuviheshimu vitabu vyote vitakatifu kama zaburi,torah na injili lakini sio biblia, kwani biblia yenyewe hata Yesu haijui,bali hata yenyewe haijatambui kama inaitwa biblia.

      Ndugu Rich, kama hujui naomba nikufahamishe, Biblia ni neno la kutunga tu lisilo na maana yoyote ile ya kiroho na ndio maana hata Bwana Yesu hakuiacha wala hakuwahi kuifundisha biblia.Biblia ni neno la kigirik lenye maana ya Biblos yaani mkusanyiko wa vitabu vyovyote vile.wala Mungu hakuwahi kumpa nabii yoyote kitabu cha Biblia hebu ndugu Rich kama unajua niambie ni Nabii gani alipewa kitabu cha biblia? Kama si uongo wa makafiri wa kikiristo? Sisi waislam hatupo tiyari kushiriki dhambi ya uongo.

      Ndugu Rich, Ni kweli kabisa kwamba sisi waislam tunaamini Bwana Yesu alipewe Injili, lakini labda wakiristo hamjui nini maana ya injili ila mimi ntawafahamisha inshaallah. Injili maana yake ni ufunuo aliokuja nao Bwana Yesu kutoka kwa Allah kwa ajili ya wana wa Israeli. Kwa hiyo maneno yote aliyoyasema Bwana Yesu pamoja na mafundisho yake hiyo ndiyo injili kwa ajili ya wana wa Israeli.

      Lakini ukisoma biblia inayoitwa agano jipya ambayo ndo wakiristo wengi wanaaminishwa kuwa ndiyo injili, agano hili ni compilation ya vitabu 27 kati ya vitabu 73 vya biblia. Katika agano jipya hilo ukitafuta maneno aliyoyasema Bwana Yesu au mafundisho ya Bwana Yesu ni asilimia 1% tu ya maneno yote yaliyomo ndani ya agano jipya maneno yaliyobaki yaani 99%ya agano jipya lote ni ya waandishi wa vitabu hivyo vya agano jipya na wala siyo maneno ya Yesu na wala siyo Injili ya Yesu bali ni watu wanaomsemea Yesu. Ukiangalia vitabu 13 alivyoandika Paulo akaita Injili hakuna hata nukta moja ya neno la Yesu. Je hiyo ndiyo injili ya Yesu au upotoshaji mkubwa, sisi hatuamini upuuzi huo kutunga vitabu mkaviita injili.

      Ndugu Rich nitazijibu hoja zako zote ila kwanza naomba uondoe ujingana ububusa kichwani mwako eti manabii walitumia Biblia, Hebu nioneshe nabii gani alitumia biblia ndugu.Kama si kukaririshwa kama toto jinga.Hebu acha utoto na ubishi wa kijinga, tumia akili bwana wewe ni mtu mzima.

      Nitajibu kila hoja uliyoandika ila naomba siku nyingine hoja zako zote uziweke page moja ili nikujibu vizuri kaka.Usiogope.

      Ahsante.

      Like

    • mpalestina says:

      MUNGU HATAJARIBUWAJE NA SHETANI???????????????????????

      Like

  175. alfa says:

    katika waislam nnaowapenda mmojawapo ni wewe,smtime unanyuut kabisa,hv hujui kama Daud alikuta tayar maandiko yamewekwa tayar ktk gombo la chuo,naye kabla ya kuandika kwa uwezo wa Roho mtakatifu alitumia hayo maandiko aliyoyakuta,SAMWEL,JOSHUA,ESTA,MUSA,wameandika sehemu ya maandiko wakiongozw na Roho yeye yule,kusema walitumia biblia mean walitumia maandiko ambayo yalikuwa tayar na hayo maandiko matakatifu utayapata ktk Biblia,maana bibl ni mkusanyko wa maandiko matakatifu,hata YESU alipokuja alisoma ISAYA 61,KISHA AKAWAAMBIA HLI NENO LIMETIMIA LEO,agano ni injil ya Yesu mwenyewe ambayo ameileta kupitia mitume wake,ROHO MTAKATIFU ambaye BABA alimpeleka kwa Daudi naye akaandika kwa israel ndiye ambaye YESU alimleta nae akawafunulia mitume yawapasayo kuandika,manake sasa ni kwa mataifa yote na c israel pekee ka mnavyodai,ilikuwa lazima andiko litimie,JIWE WALILOLIKATAA WAASH LIMEKUWA JIWE KUU LA PEMBENI,wangekubal asingekuwa YESU maana andiko halijatimia!NIMEKUTOA UWE NURU YA MATAIFA BY ISAYA.

    Like

    • Ndugu Alpha,
      Swali langu kwako ni simple tu je nabii samweli alisoma Marko, Matayo, Yohana ? je bwana Yesu alisoma waebrania,wagalatia, wafilipi, warumi na wakorinto ? Au je kwenye hivyo vitabu vya Paulo vyote kuna hata doti ya neno alilolitamka Bwana Yesu .Ndugu Alpha soma vitabu vyote vya Paulo uone kama utakuta neno la Yesu hata moja, je na hiyo utaita injili ya Yesu ndugu Yangu na hali hakuna hata neno moja la Yesu? Hizo ni barua alizoandika Paulo akiwaandikia watu wa maeneo mbalimbali kwanza hata nyie watanzanina haziwahusu, Kwa sababu ukisoma vitabu vya Paulo anavyoita injili ni mabarua aliyokuwa akiwaandikia washikaji zake na nyie mkachukua eti vitabu vitakatifu vyenu mnatumia makanisani hata huku Tanzania, hebu soma baadhi ya barua halafu ujihukumu wewe mwenyewe kama aliandika kwa ajili yako mtz au kwa sababu ya kisebengo chako basi na wewe unajipachika tu.

      1 TIMOTHEO
      1Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
      2.Kwa Timotheo, mwanangu mwaminifu katika imani:

      Hapo anamwandikia Timotheo rafiki yake, je wewe mtanzania ni timotheo, Huo waraka umeandikwa unaenda kwa Timotheo, sasa wewe kiherere cha nini ndugu Alfa.

      WAEFESO 1
      Salamu
      1.Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu Kwa watakatifu walioko Efeso walio waaminifu katika Kristo Yesu.

      Sasa wewe ndugu mkiristo unayesoma kitabu hiki kwa nini unasoma yasiyokuhusu, kwani wewe ni mtakatifu uliyeko efeso, sasa mbona mnaingilia mambo yasiyowahusu. Waraka umeandikwa kwa watakatifu wa efeso na wewe ni mtanzania unautumia, je huoni unajishushua ndugu yangu alpha.

      WAGALATIA
      salamu
      1.Paulo, mtume, si mtume wa wanadamu aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu 2. na ndugu wote walio pamoja nami, Kwa makanisa ya Galatia:

      Huo waraka unaenda kwa makanisa ya Galatia, wewe vip ndugu yangu mtanzania! Au labda huku tanzania kuna sehemu inaitwa galatia mi sijawahi isikia? Duh makafiri mnachekesha kweli hata Paulo atawakana nyie kwa maana alikuwa hajui kama mpo.Hakuna waraka wa paulo kwa wanadamu wote duniani hapana duh ni kichekesho kweli.

      Like

  176. alfa says:

    HALAFU NDUGU UKISOMA KI2 UKIELEWA USITAFUTE KAKOSEA WAPI,TAFUTA KAMAANISHA NINI,KA SISI TUNAVYOFANYA.HALAFU WAISLAM HUWA WANAKOSOA K2 KINACHOWAHUSU WENYEWE ILI WAJILINDE,HVI SHERIA ZA MUSA WALIPEWA AKINA NANI?SASA JE HAWA JAMAA C NDIO WANAFUATA SHERIA WALIZOPEWA WAYAHUDI?HAPO HAWASEM KA ZINAWAHUSU WAYAHUD PEKEE,ILA KUDANGANYA WATU KUHUSU YESU NAMBAR MOJA,HAWA WATU BNA,MAANDIKO YAMESEMA HYO NDIE MATAIFA WATAKAYEMTAFUTA,TENA NDIYE NURU YA MATAIFA,TENA PALE WALIPOAMBIWA NINY C WA2 WANGU,WATAAMBIWA WANA WA MUNGU ALIE HAI,YESU NDIE AMEWAPA UWEZO KUWA WANA WA MUNGU,WALOMWAMIN,HAKUNA ATAKAYEKWENDA KWA BABA ILA KUPITIA MIMI NA SIYO HAKUNA MUISRAEL ATAKAEKWENDA KWA BABA ILA KWA MIMI,MKAHUBIR KWA MATAIF YOTE NA KUWAFANY WOTE WAWE WANAFNZI WANGU,TATIZO LAKO UNAONGEA V2 VIDOGO NA AMBAVYO VIMEKWISHA JADILIWA NA MAJIB UNAYO,UKIULIZW UNAJIGONGAGONGA,HUWA POWERFUL ANSWERZ,HOJA ZAKO PIA HAZIGUS,MARA YESU KATUKANWA,MARA ISRAEL PEKEE,

    Like

  177. alfa says:

    halaf kwa uzush c mchezo,mara injil ya barnaba, kuifuatilia iliandikwa na muislam mpotoshaj,aliingiza uongo ambao waongo wenzake walipokubaliana hawakuuweka,mara kimya!!,hawa jamaa hawaish kutunga mamb madanganyifu,halaf janja yao ni kusingizia wakristo maovu yao wenyewe,UNAJUA ALLAH YE ANAMAIND KIARABU,VIPI ALIPOMTUMA ISA ISRAEL HAKUMUAGIZA AANZISHE MADRASA?,AU ALLAH KACHANGANYA MADAWA?,NIMESOMA SEHEMU,YESU TAFSIR YAKE NI MWOKOZ,ISA DUME LA NGAMIA,AU MWEKUNDU MWEKUNDU,C TUNAMJUA MWOKOZ (YESU)C MWEKUNDU AU DUME LA NGAMIA HUYO NI WA WAISLAM.

    Like

  178. Ndugu Rich,

    Kwanza kabisa niseme nashuhudia kwamba hapana Mungu ila Allah na Mtume Muhammad ni mjumbe wake na Mtume wa mwisho na ni mbora wa Mitume wote hata kama makafiri wakichukia.

    Ndugu Rich, naona bado una tongo tongo za ujinga na chuki za kikiristo dhidi ya uislam ila usijali naamini kabisa baada ya mijadala hii utakuwa umeelimika vya kutosha na tongo tongo zitakuwa zimekutoka.

    Ndugu Rich, Umesema quran inasema Mtume Muhammad aliua mayahudi 600 naomba uniambie ni aya ipi inasema hivyo.

    Pili ukasema quran inasema Mtume alioa watoto wa miaka 6-8, naomba pia uniambie ni aya gani inasema hivyo.Kwa kifupi utakuta hakuna aya zinazosema hivyo, ila mimi ninachojua ni kwamba Mtume alioa wake 9 na mmoja Zainab bint Jahsh alikuwa ni mwanamke Myahudi ambaye alisilimu.

    Ndugu Rich, mwanamke ambaye mtume alioa akiwa na miaka 9 ni mmoja tu naye ni mama wa wauminI Wote wa kiislam Bibi Aisha bint Abibakry Ssiddiq.

    Ndugu Rich tunapozungumzia swala la umri katika masuala ya kuoa na kuolewa ni wazi kabisa kwamba utakuwa ni ujinga na upuuzi kulinganisha umri waliokuwa wakiolewa mabinti miaka 1500 iliyopita na sasa hivi. Kwa miaka hiyo lilikuwa ni jambo la kawaida kabisa kwa binti kuolewa akiwa na umri wa miaka hiyo.

    Ndugu Rich, kama wewe ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 30 na kuendelea bila shaka ukimuuliza mzazi wako wa kike miaka aliyoolewa na Mzee bila shaka utagundua kuwa kama wangeoana leo, Mzee wako bila shaka angeozea jela, kwa sababu sasa hivi watu washenzi wanaompinga Mungu hawaangalii tena sababu za kibailogia kama kigezo cha mwanamke kuolewa ila wanachokiangalia ni sababu tu za kidunia, mara utasikia ooh mara huyu bint ni mdogo hastahili kuolewa ukimuuliza sababu ya udogo wake atakawambia bado anasoma shule ya msingi au sekondari(o-level) au mwingine atakwambia mwanangu mpaka amalize form six mara ooh ni chekechea n.k. Lakini jitu jinga kama hilo ukiliuliza je Mungu anasema binti aolewe akimaliza form six? Kwa ujumla jibu halitapatikana ni sababu tu za kidunia.

    Ndugu Rich, Watu washenzi na wapuuzi zaidi ukiwauliza binti anatakiwa aolewe wakati gani watakwambia mpaka afikishe miaka 18. Mtu wa namna hiyo ukimuuliza je kuna kitabu chochote cha dini yoyote mathalan Biblia ya wakiristo kinachosema mtoto wa kike aolewe akiwa na miaka 18?Jibubusa hili litakwambia hapana. Ukiliuliza je Mungu amesema mabinti wasiolewe mpaka miaka 18? Atakwambia hapana , ukimuuliza je amri hii umepata wapi basi kama biblia yako haisemi hivyo? Jibu atakwambia Serikali inakataza.Sasa je wewe mkiristo unafuata serikali au unafuata biblia yako? Bibilia kimyaaaaaa.wakiristo mtababaika hivyo lakini mwisho wa siku mtakwama kwa sababu biblia yenu imekaa kimya na haisemi mwanamke anatakiwa kuolewa wakati gani.

    Ndugu Rich, Mtume Muhammad ndiye kiigizo bora zaidi kwa maisha bora zaidi Duniani na kesho akhera.Hivyo basi sisi waislam katiKa suala zima la kuoa hatuangalii mara alitakiwa awe kidato cha pili hapana kwani Mungu hana mpango na hicho kidato cha pili n.k na ndiyo maana hajakitaja katika vitabu vyake vitakatifu.

    Ndugu Rich, katika uislam mwanamke anapobalehe au kwa lugha nyingine mwanamke anapovunja ungo maana yake huyo siyo mtoto tena bali ameingia utu uzima, hiyo ndiyo kanuni sahihi ya kupima ukubwa au udogo wa mtu na siyo kufikisha miaka 18.

    Ndugu Rich, Sayansi ya sasa (Modern Science) inathibitisha kabisa kwamba mwanamke anapofikisha miaka 9 anaweza akawa amebalehe kulingana na sababu za kiafya, chakula na maumbile pia. Hivyo ni kweli kabisa Bi Aisha aliolewa na mtume akiwa na miaka 9 na hadithi inathibitisha kabisa kwamba alikuwa aishavunja ungo hivyo aishaingia utu uzima kwa hiyo basi alistahili kuolewa.

    Lakini pamoja na sababu hizo za kibailogia, kwa miaka hiyo 1500 iliyopita hakukuwepo tuition, chekechea wala sekondari au college hivyo sababu za kijingajinga kama hizo eti mtoto anasoma hazikuwepo hivyo wanawake wengi walikuwa wakiolewa katika umri huo na lilikuwa jambo la kawaida.

    Tukiachana na Mtume, turudi sasa kwa wakiristo tuangalie mtume wenu Paulo ambaye hakuoa, hapa kuna swali la msingi sana je amri hii aliipata wapi ya kutooa? Kwa sababu wakiristo wanaamini katika andiko linalosema “hapo mwanzo mliumbwa mke na mume hivyo mtu atamuacha babaye na mamaye na ataambatana na mweziwe na wote watakuwa mwili mmoja”
    Sasa ndugu zangu kama amri inasema mwanzo aliumbwa mume na mke na wala si mume peke yake, je hamuoni kuwa huyu bwana alivunja amri hii ya biblia inayowataka watu waoane?Sisi tunaona huo ni upuuzi kabisa! Tena kibaya zaidi Paulo anasema “kuhusu habari ya wanawali hapo sina amri kutoka kwa baba ila nawashauri muwe kama mimi” yaani msioe. Je nyie wakiristo mkifuata ushauri wa kafiri huyo hamuoni kuwa mnavunja amri ya biblia inayotaka watu waoane? Na je mkifuata kweli ushauri wake na hawa wanawake wataolewa na nani? Au mnataka wajioe kama siku hizi tunavyoona makanisa yenu yanasapoti ndoa za jinsia moja na ushoga?

    Lakini pengine na yeye alikuwa miongoni mwa hao akina “si riziki” kwa sababu alishasema “nalikuwa hali zote kwa watu wote ili niwapate wote” kwa hiyo alipokuwa kwa makahaba alikuwa kahaba, alipokuwa kwa mashoga….jibu unalo wewe mkiristo ! mwenzio tiyari ashasema alikuwa hali zote kwa watu wote.

    Huyo bubusa anayesema hakuna yahudi aliyesilimu asome aone miongoni mwa wake za mtume mmoja Zaynab bint Jahsh alikuwa ni yahudi pure na ndugu zake walimfuata kumchukua kwa kila mbinu akakataa katakata kwa mapenzi aliyokuwa nayo kwa Mtume.

    Naomba utulie ndugu yangu kila hoja yako ina majibu ya mazuri na ya kutosha.

    Allah awape mwanga, msome na mtambue haki na muifuate.

    Like

  179. Rich says:

    Kaka yohana mudi, umenitukana kuwa mimi ni mshenzi na mjinga, lakini oky, mimi ninakuheshimu kwa kuwa naamini umenizidi sana umri. Nianze kama alivyouliza kaka Alfa kuwa, nyinyi waislamu mnasema kuwa sheria za wakina nabii Musa na vitabu vyao ndizo hizo mnazozifuata tena hazijabadilishwa hata kidogo, ni sawasawa kabisa mpaka walivyokuwa wanaswali, waliswali kama ninyi waislamu, tena mnadai kuwa mtume wenu mhamad hajabadili kitu. Swali langu hapa….mbona tena mnasema kuwa vitabu vile vya mwanzo na sheria zake za Muongozo ni kwa ajili ya israel pekee…wakati hapohapo mdadai kuwa ni sheria zilezile za manabii hao wa nyuma ndizo mnazozitumia kwa usahihi nyinyi hivi sasa?, Mimi nilichogundua hapa ni kwamba, bwana yesu pekee ndiye nabii ambaye ni adui wa Allah, kwa kuwa utagundua kuwa ikiingizwa injili yake tu, akiwa nae kama nabii wa nyuma aliyeleta ujumbe wa Mungu, basi utaona kuwa kupitia jina lake lenye nguvu za haki…Maadui wote wanaompinga Mungu wa kweli katika wokovu wake ‘ hukataa maandiko yote ya manabii na kuanguka katika jina la bwana la haki…kwa kusema kwao kwamba’ maandiko hayo ni ya upande fulani pekee!!…( na huu ndio ujumbe wetu sisi wakristo kwa watu wote hapa duniani wanaosoma mahali hapa ya kwamba ‘ MWANA WA MUNGU AMEKUJA ILI KUIDHI HIRISHA HAKI YAKE, NA KILA AENDAE KINYUME NAE, BASI JIWE HILI LITAMSAGASAGA NA KUMTUPA SHIMONI.!!!!!!. Kaka yangu mhd yhn, mimi sina nguvu ya kubishana na wewe, lakini nimesimama kwenye mhimili wa Mungu wenye nguvu mno kiasi ambacho ungejua alau kidogo basi ungetamani mno tuwe pamoja katika njia yangu ya kweli na haki. Wewe mwenyewe huko juu nilikushuhudia ukikubali kuwa, manabii waliopita walitumia torati, zaburi na mwisho ikamalizia injili kupitia bwana wetu yesu kristo…hili jambo ni kweli kabisa, hata sisi wakristo tunafahamu hivyo kupitia elimu ya biblia. Biblia ni mkusanyiko wa vitabu vyote vya Mungu kupitia manabii wake wote waliokuja kwa nyakati zao tofauti. Mwenyezi Mungu alitimiza mkusanyiko huo, ili kwa upamoja wake, wanaadamu wake wote watakaofuata wawezekupata muongozo wake pasipo sababu wala masingizio yoyote kama hayo mnayoyatoa ninyi waislamu. Hapa utaona kuwa, ndiyo maana alivyomalizia bwana yesu, kutuletea ujumbe wake wa mwisho kutoka kwa Mungu, alisema ‘IMEKWISHA(IMETIMIA). Kaka unaswali na mimi hapo? Maana hapo utagundua kiukweli kwamba hata quran yako unayoiamini wewe mwenyewe haikuitwa quran hapo kabla mpaka wale wakina nanihii, kuanza kukusanya kusanya nyaraka zake ambapo kwa pamoja ndipo ziliitwa ‘quran neno kamili la Mungu wenu Allah.Tusijaribu kupotosha watu jamani. Aliekwambia kuwa kunatofauti katika maneno ya Mungu kupitia manabii wake ni nani?, we mwandawazimu nini!!. Kaendelee kuwadanganya waislamu wenzio huko misikitini, lakini sio sisi wakristo kupitia blog hii. Kama ninyi waislamu mnasema kuwa hamviamini vitabu hivi vyote vya Mungu vinavyoleta maana ya neno ‘biblia’ basi tena, sisi wakristo hatuwezi kuwa na dawa ya kuwasaidia kwa kuwa, hilo ni tatizo la Umasikini wa kumuamini mwenyezi Mungu katika kazi zake. Mini niliuliza kuwa, kama ninyi waislamu mnafundishana huko misikitini kwamba, ufunuo wa bwana yesu ni maneno ya Mumgu yaliyokusudiwa unabii wake kwa ajili ya Taifa la israel pekee, huo unabii wake kwenu ninyi waislamu mpaka mnamuita ‘Nabii isa’ umetoka wapi?, ni wa nini sasa?, je, inamaana kuwa viongozi wa kiislamu hawajui maana ya neno ‘nabii wetu isa’ kwenye kitabu chao cha ibada!!!. Ndugu waislamu, hebu jiulizeni maswali hayo ya msingi kabla ya kukimbilia kuswali swala tano huko msikitini!!. Hivi inawezekana kweli kitabu changu cha ibada cha biblia, kiwe na jina la nabii kwa mfano ‘mtume mhamad wa waislam, kikiniambia kwamba ni mtume wangu halafu eti mimi nipinge???, aoooo!! angalia sasa, kwa uongo wenu mnaaibika…baibo takatifu inasema kuwa, kila ampingae kristo ni muongo, huu mnaouona ndiyo uongo wenu ndugu zetu waislamu. ukimpinga na kumkwepa bwana yesu katika dunia hii, ni lazima utakuwa ni muongo unaeutetea uongo!!. Nijibu sasa ili nione.

    Like

  180. Rich says:

    eti inawezekana kwa mtoto wa miaka 9 kuolewa…mbona na nyinyi waislamu hamfuati nyayo za mtume wenu za kuwatia mimba na kuwaozesha watoto wenu wenye umri huo? hivi kwa akili za kawaida za kibinaadamu inawezekana kweli kutafuta vitoto vinne vyenye miaka 9 halafu unaviweka ndani kuwa vijike vyako vyote kisa eti unauwezo wa kuvitunza wakati wewe mwenyewe unamiaka 40? Kama sio ubakaji na unyanyasaji wa watoto itakuwa ni nini? Tena wewe ni nabii ulietukuta wa wanadamu wote!!!…acha ujinga wako mwandawazimu mkubwa wewe. Maisha sio kubalehe kwa msichana pekee bali maisha ni heshima ya mtu, uadilifu wa mtu na upendo wa kweli wa mtu katika fikirazake bwana!!. Ukiona mtu yeye kazi yake ni kuviwahi mapema vitoto vya kike eti vimeshakomaa ili avile…basi ni sawasawa na mkulima anayeangusha maembe tosa shambani kwake kwa tamaa yake ya kwenda kuyauza maembe hayo na wakati hayajaiva vya kutosha kwa 100%. Wewe fikiria mwenyewe hiyo nyumba wewe baba mzima unakaa na katoto ka miaka 9 halafu eti unakaonyesha uchi wako na kushauriana nae mambo magumu ya maisha wakati yeye ndio kwanzaaaaa ameanza kubalehe na kutoka primary au chekechea hivi karibuni. Hili jambo kwa kweli hata mimi nisie na elimu nyingi haliwezi kuniingia akilini!!. Huo unaitwa ubakaji wa kisiasa na kiutu uzima. Hata madaktari huwa wanasema kuwa umri wa kubeba mimba kwa usalama kwa mama nl lazima uanzie miaka ’18 chini ya hapo unaweza kusababisha kifo cha binti kwa kutokwa na damu nyingi. Je…mhamad mtumewenu hakuyajua hayo!! Yeye alitukuta utume wake kwa mambo ya vita na ngono chafu pekee, sio mambo ya Mungu kamwe.

    Like

  181. Rich says:

    mambo yote yaliyoandikwa huko juu kuhusu mtume wenu ukichanganya na upuuzi huu tunaomalizia sisi wadogo, kwa mtu mwenye akili timamu kamwe hawezi kuwa muislamu. Pasipo ushawishi wa maneno ya mtu ataelekea kwenda kubatizwa upesi upesi. hebu fikiria wewe mwenyewe, uwe na vitoto vinne vyenye miaka 9+10+9+11 ndani ya nyumba yako ukiviita wake zako!!. Tujiulize kwa akili zisizohitaji siasa wala ubishi wala kutetea dini kwamba : kama ukiwa na majimama majitu mazima mawili tu, ndani ya nyumba yako, yanaanza kuoneana wivu na kuchukiana dhidi yako, itakuwaje sasa kwa hivi vijitoto pale vitakapokuwa vinakutazama ukielekea chumbani na kimoja wapo huku ukiwa umeviweka kiporo vile vitatu kwa ajili ya kesho na kesho kutwa?. Jamani narudia tena tusipende kudanganyana kama watoto wadogo. kwanza mapenzi yanauma kwelikweli kwa kuwa yanatabia ya kutia wivu rohoni mwetu..na kimsingi kuoneana wivu mbele za Mungu wa kweli ni dhambi kubwa mno, ndio maana kwa heshima ya ndoa kwa mwanamke, Mungu mwenyewe alilikataza jambo hilo na kuliita UZINZI. Sasa ni kwanini Muhamad alifanya uzinzi halafu anawafundisha wafuasi wake nao wafanye wakati jambo hilo kibinaadamu haliingii akilini wala halipendezi mbele za watu?? Jamaa alitumwa na mungu wa kweli huyu ili awafundishe wanadamu uchafu huo au ilikuwa ni hadithi zake za maisha!!.Maajabu makubwa haya. Hakuna mwanadamu yeyote katika dunia hii awe wa kike au wa kiume, ambaye anaweza kufurahia mapenzi kwa kushea na wenzake wengine…kama mnawazoesha na kuwafanyia wanawake hivyo ndugu waislamu, eti kwa kisingizio kuwa dini ya mhamad imesema, pasipo kutumia akili ya kuitafakari kwa haki dini yenu basi nyinyi mtakuwa ni mateka wa mtumewenu kule jehanam.

    Like

  182. Rich says:

    kiukweli kubalehe kwa msichana au mvulana sio sababu ya kukimbilia kumpeleka akapandiwe na mijibaba au akapandie mijimaa, ukifanya hivyo utamuua sasa hivi,!!. Wakati huo wa balehe ya awali kiukweli anakuwa bado ajaanza kujitambua vizuri. Utamkuta ndio kwanzaaa ananuka kikwapa cha kubalehe. Hapo kwanza ni lazima apate mafundisho ya mwili wake ili aweze kujua jinsi ya kujitunza, ukilichukua jibaba lenye miaka 40 tena eti ni nabii wa Mungu akalale nae, hakika uo ulikuwa ni ubakaji kabisa hakuna cha mazingira wala nini. Maana kama ni kweli mazingira yanamabadilliko basi utagundua kuwa wale watoto wa miaka ile ya zamani ndio kabisaaaa walikuwa wanachelewa kubalehe tofauti na hii leo vitoto vidogo vinaota ndevu na mvi. Sasa hebu tujiulize kuwa, kama vitoto vya sikuhizi vinavyo balehe mapema kwa sababu ya kula mikate ya blue band, vikifikisha miaka 9 bado tunaviona kuwa havipaswi kukimbilia ndoa, je, itakuwaje kwa wale watoto wa zama zile ambao walikuwa wanachelewa kubalehe kutokana na mazingira ya wakati ule??. Ukikaoa kakiwa na miaka 9 wakati ule basi lazima itakuwa kama hakakuwa kamalaya basi wewe mwanaume inaelekea ulikabaka na kukalazimisha, lakini yote hayo pia yanaweza kwenda kwa pamoja kwa pande zote mbili za hao wahusika na sifa zao hizo.

    Like

  183. Rich says:

    jamami bwana yesu pekee ndiye astahiliye kwa kuwa yeye, hakupigana vita kumwaga damu wala kutoa roho ya mtu hata mmoja. Ndio sababu hata waislamu wanamtambua mpaka kwenye kitabu chao cha ibada. Lakini sisi katika biblia, hakuna jina la mtu anaeitwa Mhamad. Atokee muislamu yeyote sasa hivi anionyeshe jina la nabii wake ndani ya biablia tuone?

    Like

  184. Rich says:

    huko juu hakuna hata mkristo mmoja alieshindwa au kuaibika ila tatizo ni kwamba nyinyi ni wabishi msiokubali kushindwa ndio maana huwa mnaachiwa uwanja ili mjione kuwa mmeshinda. Istoshe sisi wakristo kazi yetu hapa sio kushinda na na nyinyi bali tunataka tuwafahamishe habari njema za wokovu wa bwana wetu yesu kristo nabii wa mwisho na wakweli. Kama swala ni ushindi basi utagundua kuwa sisi wakristo tulikwishashinda tangu zamani sana miaka 2000 iliyopita kwa kifo cha bwana wetu yesu kristo pale msalabani.

    Like

  185. Rich says:

    kila jambo linaloelezewa kuhusu uislamu ni aibu tupu kutoka huko juu mpaka hapa chini. Ukienda kwenye unabii wa mtume wao > utakutana na swala la majini na mashetani yaliyomdamganya kule mapangoni,!!, ukija kwenye sheria zake > hazieleweki zimetoka wapi na kwamba zina kusudi gani haswa, maana sheria za Mungu zilezile za mwanzo zisingeweza kurudiwarudiwa upya eti kwa tofauti tu, ya hao waletaji na si tofauti ya sheria zenyewe. Hapo tunaweza kujiuliza kuwa, katika sheria zile za mwanzo, mungu alisahau kitu gani mpaka ampe mhamad kuzirudia tena vilevile katika kitabu hikohiko ili kufundishia waislamu wa wakati huu. Tukija kwenye mambo ya ndoa kama tulivyoona kuwa ni aibu na ubakaji mtupu!!…yapo mambo ya ajabu mengi sana huko juu. Anaetaka kujifunza ni lazima aanze mwanzo mpaka mwisho ndipo atafaidi sana

    Like

  186. Rich says:

    bwana mhamad yohana mi naenda zangu kulala nakuachia bwana alfa akunyooshe.kama vipi nitakucheki kesho kwenye blog hii.

    Like

  187. Rich says:

    sheria ya mhamad inasema kuwa ukiwa na uwezo unaweza kuoa hata vitoto vinne vyenye miaka tisa tisa ilimradi uwe na uwezo wa kuvitunza.!!

    Like

  188. Ndugu Rich,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah sub-hana wata’ala aliyenijaalia neema miongoni mwa neema kubwa kabisa ya kunifanya kuwa muislam, kwa uchache wa shukran, niseme al-hamdulillah.

    Ama baada ya kumshukuru Allah, nikupongeze sana ndugu yangu Rich kwa vile umeonesha kabisa una moyo wa kujifunza na kutaka kujua na Inshaallah Allah atakufumbua macho, na atakutoa kwenye giza na kukuleta kwenye nuru kupitia blog hii Inshaallah.

    Ndugu Rich, Kuhusu suala la umri wa kuoa na kuolewa naomba tusitumie akili zetu za kibinadamu, kwa sababu akili za binadamu wakati mwingine huwaza mambo yasiyompendeza Mungu, bali ni vema tukalijadili kwa kutumia ushahidi wa vitabu vyetu vitakatifu na maisha ya mitume waliotangulia. Kwani hao Mungu aliwapa ufahamu mkubwa mno ambao mimi na wewe na binadamu wengine hawakupata.

    Ndugu Rich, naomba unapojadili mada hii ni vema ukaja na vielelezo either kutoka kwenye bible ambao ni mwongozo wako na si kwa kudhani dhani tu, na kutumia kauli za watu wasiokuwa na funuo zozote kutoka kwa Mungu, au kwa kutumia mitazamo ya watu ambao pengine hawatambui hata uwepo wa Mungu.

    Ndugu Rich, sisi waislamu tunachokitaka kutoka kwenu mtwambie ni je Biblia yenu wakiristo inasema ni umri gani au ni wakati gani binti anatakiwa aolewe? Ukinipa jibu moja tu kutoka ndani ya Biblia kuanzia leo nitakuja kanisani kwenu kubatizwa, Kwa sababu nitajua Mungu aliyetuumba anataka tuishi maisha ya namna gani na akina Hawa(eva), kwa sababu kama Mungu ametuumba ni lazima atupangie taratibu za maisha.

    Ndugu Rich, naomba usiwe na ujinga kama ujinga walionao watu siku hizi wanaodai eti kuna mimba za utotoni, huu ni upuuzi usioweza kuelezeka ndugu yangu. Hivi kweli ndugu Rich kwa akili yako mtoto anaweza kubeba mimba? Huu ni upuuzi mkubwa, mwanamke yeyote anayebeba mimba huyo ni mtu mzima kwa sababu angekuwa mtoto asingeweza beba mimba.

    Ndugu Rich, moja wapo ya sababu za kipuuzi wanazotumia watu kusema eti kuna mimba za utotoni na za kipuuzi mno na hazina mashiko na ni sawa kabisa na hoja zako ulizotoa eti mwanamke anaweza kufa kwa sababu ya kutokwa na damu Nyingi, mara eti mfuko wa uzazi unaweza kutoka na asizae tena, mara anaweza pata kifafa cha mimba. N.k , Ndugu Rich hivi na wewe unakubaliana na upuuzi na ujinga huu ndug yangu. Hivi ni wanawake wangapi wenye umri zaidi ya miaka 18 tumeshuhudia wakifa kwa kutokwa na damu nyingi, wakipata kifafa cha mimba na kufa, na wengine wakitokwa na mfuko wa uzazi na wasizae tena, mimba kukaa vibaya n.k. Tena hebu ndugu Rich na wewe tumia akili yako tu ya kawaida hivi ni mabinti wangapi wameweza kuzaa kwa usalama kabisa bila matatizo yoyote na ili hali umri wao ni chini ya miaka 18? Ni wanawake kibao wamezaa wakiwa na umri wa miaka chini ya 15 tumewashuhudia wakizaa kwa usalama kabisa na wananawake wengi tu ambao wamepoteza maisha yao wakati wa kujifungua kutokana na sababu mbalimbali na wakati umri wao ulikuwa zaidi ya miaka 18.

    Sasa ndugu yangu Rich, naomba tuache ubishi wa kipuuzi naomba uniambie biblia inasema mwanamke anatakiwa kuolewa akiwa na umri gani, ili niweze kujua kuwa Mtume wangu alifanya kosa la jinai?

    Ndugu Rich, hili suala naomba nyie wakiristo mliache kama lilivyo kwa sababu hamliwezi kabisa na mtume wenu Paulo aishasema kuwa yeye kuhusu suala la wanawake hajapewa amri na Baba yake, sasa kama amri hajapewa na ni mtume wenu basi nyie wafuasi wake hamna haki ya kulizungumzia kwa sababu Baba yenu aliye mbinguni hakuwapa misingi labda alisahau, basi mtuache tuwafundishe sisi ambao tulipewa amri kupitia kwa mtume wetu.

    Pili ndugu Rich, umeuliza kuwa sisi waislam mbona basi hatuwaoi wanawake wenye umri huo? Ndugu Rich suala hilo nshakwambia sisi hatuangalii umri bali tunaangalia sababu za kimaumbile ambazo ndizo sababu za asili, hivi ndgu yangu hata sayansi ya Darasa la sita hukusoma nini? Kwa sababu nakumbuka wakati tunasoma sayansi tulisoma sababu zinazofanya utambue kuwa mtu flani wa jinsia flani ameingia utu uzima, hebu tafuta kitabu cha sayansi darasa la sita tu,uone kama mle wameandika miaka 18, hapana bali utakuta wanaeleza sababu za kimaumbile.

    Lakini pia kuna hoja ya kipuuzi inayotolewa siku hizi eti mwanamke akiwa na miaka 18, ndiye anakuwa anajitambua na kujua maisha na kadhalika. Huu ni upuuzi, kujitambua kwa mtu siyo umri kwani jitu linaweza likawa hata na miaka 60 lakini bado halijajitambua na halijui maisha bora hata ya mtu mwenye miaka 15, tumeshuhudia ni watu wangapi wazima hawajitambui na hawana muelekeo kabisa kimaisha na ni umri wao ni zaidi ya miaka 50. Kwa hiyo ndugu yangu Rich suala la mtu kujitambua au kutojitambua ni suala la Kipawa anachojaliwa mtu na Allah, kwani unaweza ukawa na umri mkubwa lakini busara zako unazidiwa na mtu wa chekechea. Na ndio maana hata bwana Yesu kwa kulitambua hilo alisema “ewe baba tunakushukuru kwa kuwa mambo haya umewanyima watu wazima na ukawafunulia watoto wachanga” kwa hiyo ukubwa si busara na wala si chochote bali busara ni kipawa kutoka kwa Mungu. Na ndiyo maana Bibi Aisha(r.a) ni mwanamke mwenye elimu kubwa ya dini ya kiislamu kuliko watu wote baada ya Mtume na saydina Abibakry ambaye ni baba yake, pamoja na kuwa alikuwa na umri mdogo kwa kipindi kile.

    Ndugu Rich, umetoa pia sababu za vyakula kwamba kipindi kile lishe na vyakula vilikuwa siyo kama sasa hivi, Ndugu Rich naomba usifananishe maisha ya Uarabuni kipindi cha miaka 1500 iliyopita na maisha ya sehemu yoyote ile duniani, kwani ukisoma hata vitabu vya historia vya wazungu utagundua kuwa bala Arab ndilo bara liloendelea mapema zaidi kuliko sehemu yoyote ile duniani, kwa hiyo usishangae vyakula unavyokula wewe leo wenzio walikula miaka 1500 iliyopita. Nitakupa mifano kulithibitisha hilo na utajua kuwa wenzetu waliendelea mapema kabisa,

    Mfano 1: wakati wewe huku Tanzania mwaka 1888 ukijulikana kama bara la giza katika zama za “dark stage” wana historia wanasema zama za mawe Uarabuni tiyari walikuwa wakifanya kazi kwa kutumia chuma mwaka 650 kipindi cha mtume.

    Mfano2: wakati sehemu zote duniani wakifanya biashara kwa kubadilishana “butter trade”, Uarabuni tiyari walikuwa na fedha yao iliyojulikana kama dinari na dirham kipindi cha mtume kwa ajili ya biashara.

    Mfano3; wakati huku afrika na maeneo mengine duniani mkichezea bao dhahabu na almasi miaka ya 1900, wenzenu uarabuni kipindi cha miaka 650 kipindi cha Mtume wanatumia dhahabu na almasi kwa ajili ya mapambo, na ushahidi ni kwamba Mtume alikuwa na pete ya dhahabu.

    Mfano4: wakati watu wanatembea zaidi ya km10 kwa mguu, tiyari kipindi cha mtume Allah amewaruzuku watu vipando, kama ngamia na farasi;

    Kwa hiyo ndugu Rich, usifananishe chakula unachokula sasa hivi wewe kwa ubora kama chakula alichokula mtume na maswahaba zake, hivyo basi hiyo ilikuwa ni sababu tosha ya kuwa binti anaweza kubalehe kwa miaka 9 tu, kwa sababu maisha yao yalikuwa mazuri.

    Ndugu Rich, unajua ni kwa nini Paulo hakuoa na ili hali Biblia ishasema “hapo mwanzo waliumbwa mwanaume na mwanamke ili waishi pamoja”? na akaendelea kukiri kuwa yeye kuhusu wanawake hajapewa amri? Sasa kama mungu wake hakumpa amri kuhusu wanawake basi moja kwa moja hiyo amri ya kutooa yaani kuwa “ruhubani” ni lazima tujue kuwa aliitoa kwa shetani. Na ndio maana siku hizi mapadre wanaona wenyewe kwa wenyewe, vidume kwa vidume nab ado wanaingia kanisani kuwaongoza wakiristo, hiyo yote ni kwa sababu mungu wenu wafuasi wa paulo hakuwapa amri juu wanawake hivyo mnatumia amri ya shetani.na tumeshuhudia wengine wanajifanya hawaoi kumbe wanavibaka vifanyakazi vyao kwenye mahekalu, na wake za watu kwa kisingizio eti mchungaji hawezi kuchunga kondoo bila kuwala, duh hii ni hatari sana, ushauri wa Paulo huo.

    Rudi kwa Allah ndugu yangu Rich, Utapata mafanikio hapa duniani na kesho akhera.
    Wabillah tawfiq.

    Like

  189. Rich says:

    acha uongo wako ndugu yangu. Huwezi kamwe kumuozesha binti yako wa miaka 9 kwa jibaba lenye miaka 40. Acha kumsingizia Mungu kila kutu kua hajasema wakati akili na maarifa ya kufanya maamuzi sahihi amekujalia. Kwa mfano hatuwezi kuwapa watoto wadogo na wakina mama wafanye kazi ngumu au waendeshe magari barabarani kwa kuwa kufanya hivyo ni hatari kwa misha yao. Lakini hebu tujiulize kuwa, hivi jambo hilo hatujui kwamba ni sahihi kuliunga mkono eti mpaka Allah atufundishe!!, Kwakeli haifai kabisa binti yako wa miaka 9 aolewe na jibabu la miaka 40, hata ukiwachunguza kwenye mapenzi yao utaona kuwa ni unyanyasaji wa kimwili na kimapenzi mtupu mtupu. Utamuona yule binti kwa kuwa anafanya mapenzi na mtu kama baba yake au babu yake basi anakua mnyonge na mwenye mawazo wakati wote, huku yeye mwenyewe kiroho akiogopa na kuamini kabisa kuwa jambo hilo sio zuri. Lakini kwa uoga wake anajikaza ili alizoee jambo hilo la ajabu!!. Atakuwa wakati wote ni msichana mdogo mwenye mawazo huku akijiuliza nafsini mwake kwa siri kuwa usiku wa leo hili babu tena nabii la Mungu litanifanya kitu gani jamani!!. Lazima jamani tuwe wa kweli na tuanze kubadilika kumfuata bwana yesu mwokozi na nabii wa Mungu wa kweli. kujaribu kutetea ujinga ambao hata akili zetu unaukataa ni jambo la hatari ndugu zangu. Sisi wakristo biblia inatuambia kuwa pamoja na kuongozwa na maandiko inatupasa pia kutumia akili + hekima + maharifa na busara, pale tunapofanya maamuzi yetu. Kwa nabii tena aliyetukuta kwa ajili ya dunia nzima kufanya mambo kama yale kwakeli ni aibu kubwa kwake na kwa wafuasi wake wote kuthibitishwa kuwa kamwe yeye hakua nabii wa kweli wa mwenyezi Mungu!!!!. Eti mimi niwe na miaka 40 halafu niwaache wakina mama rika langu na kwenda kukababua kanuka jasho ka miaka 9 kaliko balehe hivi karibuni, kweli ni halali jamani mambo hayo??. Sisi wakristo upuuzi huo kamwe hatuwezi kumsingizia Mungu kwamba eti hajatufundisha kwa kuwa tayari sisi kupitia maharifa ya neno lake takatifu tunajua jambo jema na baya. Hiyo ndiyo kazi kubwa ya neno la Mungu lenye uzima kwa watu, yaani kuwafundisha na kuwajenga wanadamu kutambua jambo jema na jambo baya. Mwisho ni kwamba, jamaa limenishangaza kwelikweli kwa kuwa alipoona nimemuuliza hoja ngumu na za msingi, yeye akaamua kuziacha zote halafu eti anakimbilia hoja hii ambayo kwa akili yake alifikiri ataweza kuitetea!!. Hebu tujibu na zile hoja nyingine za mambo ya bwana yesu na mambo ya sheria, mbona umeziacha ndugu yetu??, poleni sana ndugu zetu waislamu.

    Like

  190. Ndugu alpha,

    Kwanza kabisa nakushukuru kwa sababu, hivi sasa kidogo umeanza kuuliza vitu vya msingi, hii inaonesha kidogo akili yako inaanza kukomaa sasa na kwa uwezo wa Allah unakaribia kuiona nuru ya Allah na Mtume wake.

    Ndugu Alpha, nafurahi sana kuona sasa wewe mwenyewe umeanza kutambua kuwa Petro alikuwa shetani na aliitwa jina hilo si na waislamu bali na Bwana Yesu mwenyewe na sababu hasa ya kumuita mtoto wa watu shetani, Yesu alisema kuwa Bwana Petro alikuwa akiwaza mambo ya binadamu na si mambo ya kiroho, na kwenye hilo hilo shetani ndo kanisa likajengwa, yaani kwa maana nyingine Yesu alimaanisha kuwa kanisa litasimama juu ya misingi ya kishetani shetani, nashkuru sana kwa kuwa hata ndugu Alpha amekiri.

    Ndugu Alpha, nimeona umecomplain mambo mengi saana kuhusu uislam lakini mojawapo hasa la msingi ambalo bado hasa hujalitambua ni kuhusu sheria ndani ya torati na mahusiano ya sheria hizo na zile za waislam ndani ya Quran tukuf.Ndugu Alpha sisi waislam tunaamini kweli kuwa sheria za torat na za injili ni sheria za Allah alizoteremsha kwa ajili ya watu au wana wa israeli.

    Ndugu Alpha tofauti na nyie wakiristo mnavyoamini kwamba injili imekuja kuipinga torati, sisi waislamu hatukubaliani kabisa na suala hilo bali tunaamini sheria za injili ya Bwana Yesu, na sheria za torati na sheria za Quran zote ni funuo za Mungu kwa Manabii wake na tunaamini quran ndiyo sheria ya mwisho kabisa kwa ajili ya ulimwenugu wote.

    Ndugu Alpha, Mtume Muhammad alipokuwa mtawala wa Makka na Madina au Hijaaz kama ilivyokuwa ikijulikana enzi hizo, na kwa kuwa maeneo hayo wakaazi wake wengi walikuwa waarabu na mayahudi, basi Mayahudi walishindwa kuelewa kama wewe unavyoshindwa kuelewa sasa hivi, walishindwa kuelewa kama sheria za quran ni mpya au ni sawa na zile walizokuwa wakipewa na manabii wao waliomtangulia Mtume? Na mara nyingi walipofanya makosa yapasayo hukumu za Allah mayahudi walienda kwa Mtume kutafuta hukumu, na wengine walikuwa wanafiki kama ilivyo kawaida ya Mayahudi hivyo basi walitaka kujua je kama Mtume atawahukumu kwa hukumu mpya au ile ile ya manabii waliopita?

    Kutokana na majaribu hayo Allah alimshushia Mtume wake ufunuo ndani ya quran kama ifuatavyo hapa chini;

    QURAN SURA 5:AL MAIDA
    42. Hao ni wasikilizaji kwa ajili ya kusema uwongo, na ni walaji mno vya haramu! Basi wakikujia, wahukumu baina yao au jipuuze nao. Na ukijipuuza nao, basi wao hawatakudhuru kitu. Na ukiwahukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda waadilifu.

    Ndugu Alpha, kwa vile Allah alishatambua kuwa hao mayahudi walikuwa wanafiki na walikuwa wakisikiliza si kwa ajili ya kufahamu bali kwa ajili ya kuleta ubishi na kwa ajili ya kupotosha basi Allah anamwambia Mtume awahukumu au aachane nao kwani Allah alijua kuwa mayahudi pamoja na kuwa walimwendea mtume ili awahukumu, tiyari hukumu zilezile ambazo Mtume angewahukumu nazo wao pia wanazo kwenye torati, hivyo basi wether mtume angewahukumu au angewaacha watumie hukumu waliyonayo ndani ya torati yote ni sawa. Ndugu Alpha , aya hiyo inatosha kukuonesha kuwa hizo sheria ziko sawa.

    Ndugu Alpha, Allah hakuishia hapo bali aliendelea kumfahamisha Mtume kuhusu habari za Mayahudi, jinsi walivyokuwa wanaleta janja ya nyani. Hebu soma aya ifuatayo hapa chini uone Allah alivyoendelea kumfahamisha Mtume Muhammad;

    AL-QURAN SURA 5 ALMAIDA;
    43. Na huwaje wakufanye wewe hakimu nao wanayo Taurati yenye hukumu za Mwenyezi
    Mungu? Kisha baada ya hayo wanageuka. Na hao si wenye kuamini.

    Kwa hiyo Allah anamwambia Mtume , kuwa hao Mayahudi kama wanayo taurati basi sheria hizo za torati zinatosha kabisa kuwahukumu kwani sheria hizo ni sawa na zile wanazofuata kwa Mtume.

    Ndugu Alpha, Mfano mzuri ni katika hadithi ya Mtume inayoeleza kuwa siku moja Mayahudi walimfuata Bwana Mtume Muhammad, baada ya mayahudi wawili kukutwa wakifanya zinaa na ili hali mmoja wao alikuwa kwenye ndoa,Basi walipofika kwa Bwana mtume aliwauliza je taurati yenu inatoa hukumu gani juu ya swala hili, Mayahudi wakamwambia hukumu yake ni mawe, basi mtume akawaambia kumbe hukumu mwaijua halafu mwaja kwangu kutafuta nini sasa, basi wale wazinifu walipigwa mawe mpaka wakafa.

    Kwa hiyo ndug Alpha, hizo ndizo sheria za Allah ziko sawa kabisa na sheria za torati na zile za Injili ya Bwana Yesu.

    Lakini kwa upande wenu wakiristo mnanishangaza kitu kimoja, kwani ukimuuliza mkiristo yoyote duniani atakwambia sheria za agano la kale amabazo ndizo anazoamini kuwa ni sheria za torati zimepitwa na wakati yaani ni zilipendwa, tena kwa ujinga na upuuzi zaidi atakwambia laana aliyoipata Bwana Yesu pale alipotundikwa mtini imeondoka na sheria zote za torati, sisi waislamu hatukubaliani na upuuzi huo kabisa, eti Bwana Yesu kalaaniwa yaani nyie tukiwaita wapuuzi mnasema tunawatukana, hivi mtu una akili yako utasemaje Bwana Yesu kahingikwa mtini na ili hali unajua kuwa kitendo cha kuhingikwa mtini ni laana na hawatundikwi mtini isipokuwa watu waliolaaniwa, sasa wewe utasemaje Yesu kalaaniwa kwa ajili ya dhambi zako ? Yaani dhambi utende wewe halafu Mungu wako Yesu atundikwe mtini na alaaniwe ! yaani mungu wako alilaaniwa ndugu yangu na wewe unakubali suala hilo, kweli waislam tunasema Inna-li-lah wa inna ilayh rajiun, hakika huu ni msiba mkubwa yaani watu mungu wao anatundikwa kwenye mti pamoja na wanyang’anyi na wezi ! Sasa mungu huyo atawezaje kuwahukumu watu na hali yeye mwenyewe ashahukumiwa kwa kuninginizwa kwenye mti ndugu yangu ?mungu wenu alikuwa dhaifu kiasi gani ndugu zangu hadi anapigwa mijeledi ? huu ni msiba,

    Halafu eti baada ya Yesu kutundikwa ndipo laana ya torati ikaisha, lakini huu ni upuuzi wa wazi kabisa unaofanywa na wakiristo, kwani kila siku na mara nyingi naangalia mahubiri ya Mz. Wa upako, Mch. Rwakatare, na Mwingira na nimeshuhudia mara nyingi wanapohubiri wanatumia agano la kale ambalo kwao limepitwa na wakati, na Bwana Yesu ameshaondoka na laana zake pale mtini.sasa swali langu linakuja ndugu yangu Alpha hivi utawezaje kuhubiri kitu ambacho kimepitwa na wakati ?

    Ndugu Alpha huko juu nilimnakiri mchungaji Moses PK, anayemiliki blog hii, alipokuwa akichangia mojawapo ya mada kwenye blog hii amesema hivi, naomba nimnukuu tena.

    By Mosespk “AMRI KUMI, TORATI NA AGANO LA KALE YOTE YAMESHAONDELEWA!
    Mungu alitabiri kwamba ataondoa agano la kale na kufanya agano jipya lililotofauti……….”
    Ndugu Alpha, huyo bwana ni mchungaji mkubwa na mwenye elimu yake ya dini kuliko hata wewe mwanafunzi, yeye anadai hata zile amri kumi zishaondolewa yaani kwa mfano ile amri inayosema usizini au usiibe au usisime uongo sasa zishaondolewa hivyo kusema uongo ruksa, kuiba ruksa, kuzini ruksa n.k lakini jambo la kushangaza utakuja kuta hata yeye biblia yake bado inalo agano la kale ndani yake, sasa je ni ya nini basi kama sheria zake zimepitwa na wakati ?

    Tena mchungaji huyu anaendelea kwa kusema ;

    By Mosespk “Misitari hii yaonya kwamba agano jipya linadumu bali agano la kale limebatilika”

    Sasa kama agano la kale limebatilika, ni kwa nini basi mnapohubiri mara nyingi mnatumia agano la kale ?

    Ndugu Alpha, muda si mrefu ulikuwa unatetea hapa kwamba hiyo ni biblia yenu na biblia ya manabii waliopita na wote walikuwa wakiristo wenzenu, je kama kweli ufunuo waliopewa wakiristo wenzenu ulibatilika hamuoni kwamba hata imani yenu ya ukiristo nayo ni batili ?

    Hilo jambo liko wazi kabisa ndugu yangu alpha kuwa nyie wakiristo hamjielewi hasa mnachokisimamia, na ndio maana utaona kila mara mnaanzisha vitu vipya kwenye dini yenu.

    Ndugu Alpha, ninayo mengi sana ya kukusaidia lakini soma kwa uhakika kwanza halafu kama kuna sehemu hujaelewa naomba usisite kuuliza kwa sababu shetani amewachukua wakiristo na amewafanya marafiki zake, hivyo ndugu yangu mi nataka nikurejeshe kwa Allah inshallah ;

    Karibu tujadili ndugu,
    Wabillah tawfiq.

    Like

  191. Ndugu Rich,

    Nakushukuru na nakupongeza sana kwa sababu naona sasa wewe mwenyewe umekiri kuwa sasa imefikia sehemu sasa biblia na mungu wako wamekwama na baadhi ya vitu wameviacha hawakueleza, nafurahi sana kuona sasa umetambua kuwa mungu wenu alisahau kuwapa baadhi ya amri hivyo akawaacha muishi mnavyotaka na kila mmoja kwa akili yake anavyoona.

    Lakini ndugu Rich, kama kweli mungu wenu anafikia sehemu anawaambia sasa ameshindwa hivyo basi kila mtu atumie akili yake, hamuoni kuwa mungu wenu ni mnyonge mno na hawezi kuchukua maamuzi juu ya viumbe aliowaumba. Kwa maana nyingine anazidiwa hata wanaotengeneza simu kwa sababu wao wanaweka menu book inayoonesha ni jinsi gani simu inatakiwa kutumika, je itakuwaje kwa Mungu aliyetuumba asitwambie tunatakiwa kuishi namna gani.

    Lakini ndugu Rich,kweli kama inafikia kipindi mungu wenu anawaacha kama watoto wakiwa waliofiwa na baba yao hivyo kulazimika kutumia akili na nguvu zao wenyewe kwa ajili ya kutafuta mahitaji yao je huyo ni mungu sahihi anayestahili kuabudiwa kweli ndugu yangu!

    Lakini pia kama kweli Mungu alikuwa anaona ya kutuacha wanadamu tutumie akili zetu, ni kwa nini basi akaleta kwenye maandiko matakatifu akikataza mambo machafu ikiwemo wizi, zinaa, uongo , ugomvi n.k. Ni kwa nini basi Mungu huyu hakutuacha tutumie akili zetu? Kwani wewe ndugu Rich bila Mungu wako wa biblia kusema kuwa wizi hauruhusiwi unataka kuniambia akili yako ingeshindwa kutambua kama wizi ni mbaya? Au unataka kuniambia watu wasio na dini hawajui kuwa wizi ni mbaya?

    Ndugu Rich utaona kuwa pamoja na kuwa Mungu alijua kuwa kila mtu mwenye akili timamu anatambua kuwa wizi ni mbaya lakini hakusita kukataza kupitia maandishi yake matukuf, vivyo hivo pamoja na kuwa Mungu huyu huyu alitambua kuwa sisi binadamu tunajua kuwa zinaa ni mbaya na ni uchafu, lakini Mungu huyu huyu hakusita kutufahamisha kuwa zinaa ni uchafu, pamoja na kuwa alijua kuwa kila mtu mwenye akili timamu analitambua hilo. Vivo hivo katika masuala mazima ya kusema uongo kila mtu mwenye akili timamu anatambua kuwa ni jambo baya lakini Mungu hakusita kulikataza suala hili.

    Ndugu Rich, tunaona kuwa pamoja na kuwa Mungu alijua kuwa ametupa akili ya kutambua jema na baya lakini pia hakuacha kutuambia jema lipi na baya ni lipi na hakusita kukataza kupitia maandishi matukufu.

    Sasa kama hivyo ndivyo ilivyo nilitegemea pia, mungu wenu atwambie kuwa kuwaoa wanawake wenye umri mdogo ni jambo baya hata kama wamebalehe. Kwa hili hata kama ametupa akili za kutafakari lakini basi mbona kwa hili mtume wenu anasema hakupewa amri? Na hivyo mnalazimika mtumie akili zenu? Hapa utaona kuwa mungu wenu alikuwa na mapungufu makubwa na mimi naamini kabisa mungu aliyemtuma Paulo alisahau, hivyo Paulo analalamika kuwa katika mambo yooote hilo tu mungu alisahau kumpa amri, du mungu wenu yehova ndugu yangu mbona anatia aibu sasa.

    Ndugu Rich, sisi waislam hatuamini kama Mungu wa kweli anaweza kusahau baadhi ya amri, bali tunaamini kila amri ametoa na tunaruhusiwa kutumia akili zetu lakini bila kukiuka amri za Allah, kwa mfano Allah anaposema wizi ni uovu,wewe muislam unatakiwa kutumia akili kujua ni kwa nini Allah kasema wizi ni uovu, na siyo kwamba eti mungu asahau halafu atuache sisi tutumie akili zetu na ilihali yeye kasahau huu ni ujinga ndugu zangu wakiristo.

    Ndugu Rich, suala la kutumia akili zetu katika masuala ya kiroho bila amri ya Mungu mwenyewe, hilo ni jambo baya mno kwa sababu kila mtu kuna jinsi akili yake inavyomtuma; Nitatolea mfano baadhi ya mambo ambayo watu wanatumia akili zao bila amri ya mungu, mambo hayo ni maovu lakini wao kwa sababu wanatumia akili zao na akili zao zinawatuma kuwa ni sahii huna jinsi ya kuwazuia; kwa mfano;

    Siku hizi tumeshuhudia madada wengi wakivaa nusu uchi, maziwa kila kitu njenje, kwetu sisi waislam Allah kakataza uchafu kama huo lakini kwa wakiristo kwa sbabu wanatumia akili zao na mungu hakuwapa amri basi wao ni sahihi, sasa haya ni madhara ya kutumia akili badala ya amri na sheria za Mungu.

    Ndugu Rich, tumeshuhudia sa hizi uko America watu wameruhusiwa kuvuta bangi hadharani, kwa sababu akili zao zinawatuma kuwa ni sahihi na kwa sababu hasa wengi wao ni wakiristo, na mungu wao wa biblia hajakataza, basi akili zao zimeona ni sawa.

    Lakini pia kule india tumeona wanawake wengi wakitoa mimba, pamoja na maeneo mengine mengi duniani imeruhusiwa kabisa na serikali zao, hasa maeneo ya wakiristo wengi kama Amerika n.k, wametumia akili zao na kwa sababu mungu wa biblia yao hasemi kama kutoa mimba ni haramu, lakini sisi Allah hayo mambo yote kashayasema ndani ya quran lakini kwa sababu nyie wakiristo mungu wenu amewaacha wapweke basi mnatumia akili zenu tu kwa sababu mungu wenu uwezo wake umeishia hapo hivyo mnalazimika kujiongeza.

    Ndugu Rich, hayo ndiyo madhara ya kutumia akili hasa kwa wakiristo wengi ambayo yote hiyo ni sababu wao wamekuwa mayatima na mungu wao amewaacha wapweke.

    Ndugu Rich,mimi bado niko na wewe ndugu yangu, naomba andiko takatifu linalosema mwanamke mdogo haruhusiwi kuolewa hata kama amebalehe. Na nakuahidi ukinipa andiko hilo mimi leo nabatizwa na nakuwa kafiri wa kikiristo, lakini kama hakuna basi jua munugu wenu anayo mapungufu makubwa hivyo hastahili kuendelea kuabudiwa.

    Allah akufahamishe ndugu yangu Rich.
    Wabillah tawfiq.

    Like

  192. Rich says:

    Kaka mhamad, sheria inayotuongoza sisi wakristo kuonyesha muda halisi unaofaa kwa ajili ya wakati muafaka wa binti au mvulana kufunga ndoa ni ‘TAMAA’ Ikimaanisha kuwa ni wakati ule tamaa ya ngono inapomuwaka muhusika, na kamwe sio wakati wa’BALEHE’ kama ninyi waislamu mnavyofundishwa na Allah. Biblia inatuambia kuwa, kwa ajili ya ‘TAMAA’ oeni maana ni afadhali kufunga ndoa kuliko ‘KUWAKA TAMAA MBAYA ZA MWILI’ Soma( 1wakorintho 7:9). Kipindi halisi kinachofaa kwa ndoa sio wakati wa kubalehe kama Allah anavyofundisha nyinyi waislamu, bali ni kile kipindi ambacho mwili unawaka tamaa ya kufanya tendo la ndoa kutoka kwa mhusika mwenyewe. Hii ni kwa sababu, unaweza kumuona binti au kijana amebalehe kimwili lakini kiakili na kiroho anakuwa bado hajawa tayari kufanya maamuzi hayo ya kuoa au kuolewa ambayo ndiyo yatakayo muwezesha kukabiliana vizuri na changamoto zote za ndoa pale atakapokuja kuishi na mume wake. Sasa, unapokuja kumlazimisha kwa kigezo kimoja cha balehe pekee pasipo kumpa muda wa kujifunza mambo ya ndoa na changamoto zake, unajikuta wewe mzazi unampachika binti yako jibabu lenye miaka 40 pasipo kujua athari zake kiakili na kiroho kwa binti yako. Binti huyo anakuwa ni kweli amebalehe kimwili lakini kiakili na kiroho katika kuchagua na kufanya maamuzi yeye mwenyewe kwa msukumo wa uwezo wa mwili wake anakuwa bado kabisa. Huu unaitwa ubakaji na unyanyasaji kwa sababu yeye mwenyewe kama binti mdogo ambaye ndio kwanza anamiaka 9, haiwezekani hata kidogo kwa kutumia kigezo kimoja cha balehe yake, eti ukamtwike akalale kitandani na mtu kama baba yake mzazi au babu yake, kwakweli hiyo siyo sawa kabisa bali hizo ni sheria za unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji,!!!. Najua ukweli unauma ndugu zangu waislamu lakini ni lazima mbadilike. Hata kama ni Allah aliewapa sheria hiyo ya kishenzi, kwa kuwa sheria yenyewe sio adilifu na ya Mungu wa kweli inayoweza kutunza heshima ya ndoa na watu wake, basi sisi wakristo tunaiweka sheria hiyo, katika kundi la sheria ya ubakaji na unyanyasaji dhidi ya wanawake au tuseme kuwa hiyo ni sheria ya uzinzi au ngono, na kamwe sio sheria ya ndoa. Tena mtume wenu mhamad angekuwa anaishi mpaka leo hii, basi tungemkamata na kumtia jela kwa makosa ya kutunga na kutumia sheria ya unyanyasaji na ubakaji kwa watoto na wakina mama. Hii ni kwa sababu, heshima ya ndoa sio kulaliana pekee kama nyinyi waislamu mnavyofikiri ila heshima ya ndoa ni kuheshimiana pande zote mbili kwa upendo wa kweli kabisa pasipo unafki. Bwana yesu alituambia kuwa tuwapende wake zetu kama sisi tunavyojipenda wenyewe, tena akasisitiza kwa kusema kuwa, upendo ndio haswa maana yote ya torati na manabii wote wa Mungu, Soma(mathayo 7:12). Kwa hali hiyo, sisi wakristo, tunajikuta tunapotii neno la Mungu, basi mioyo yetu haitushutumu wala kutuhukumu kwa kuwa tunafanya mambo yanayopendeza machoni pa Mungu wetu, na kama ndugu yohana, kunawakristo uliowaona huko mitaani au nchi yoyote, wanapayukapayuka kwa mambo ya ovyo na ya aibu, basi hao ujue kuwa ni wakristo wasiofuata sheria za Mungu ambapo kimsingi neno la Mungu lina sheria zote na taratibu zote zinazofaa kumuongoza mwanadamu katika maisha yake. Mtume wenu mhamad ndiye aliyevunja sheria zote za Mungu kwa kuwafundisha ninyi mambo ya ajabu tena yanayosikitisha mno mno. Yeye hakubahatika kwenda shule hata darasa la vidudu (awali), halafu eti anafanikiwa kuwadanganya nyinyi waislamu ambao wengine mmefika hata mpaka chuo kikuu,!!. Amefundisha waislamu vitu vingi tofauti kabisa ambavyo hata haviwezi kukubaliana na akili za kawaida za kibinadamu. Kwa mfano, ninawauliza nyinyi waislamu hivi: kama wewe mwanaume wa kiislamu hupendi mke wako awe na wanaume wengi zaidi ya wewe mwenyewe kwa sababu ya wewe kutaka kulinda heshima yako ya ndoa, iweje tena wewe umletee mkeo wake wenza watatu ndani ya nyumba wakati unajua wazi kuwa jambo hilo ni baya kwa mkeo kama wewe mwenyewe usivyotaka yeye akufanyie?!!, kwa nini eti mimi nisiyependa kufanyiwa jambo fulani baya linalotia wivu na kusononesha roho yangu, huku likiondoa heshima ya ndoa, ninapenda tena jambo hilo hilo baya kumfanyia mke wangu?, je, heshima ya ndoa inaangaliwa kwa upande mmoja pekee? Jibu ni kwamba ‘HAPANA’kwa kuwa sheria ya upendo wa kweli haujifikirii kibinafsi kwa upande mmoja bali ni upendo na kufikiriana kwa pande zote, ndiyo maana bwana wa amani mtetezi wa wanyonge akaitangazia dunia yote hivi ‘ WATENDEENI WATU WOTE MAMBO YA HAKI KAMA NINYI MNAVYOPENDA KUTENDEWA NAFSINI MWENU,.Huu pekee ndiyo upendo wa kweli wa Mungu ambao bwana yesu pekee ndiye aliyeufundisha,!!!!!. Yule aliyemtokea mtume wenu kule mapangoni ndiye aliyemfundisha mhamad mtume wenu upendo wa uongo wenye ubinafsi wa siri rohoni mwa watu, ndio maana hata ndoa zenu huwa hazidumu kama ndoa za wakristo, unakuta jibaba lina wake wanne ndani ya nyumba lakini bado halitosheki, kila mara yeye kazi yake ni kuwakorofisha wakeze na kugawa taraka kama karanga, ili awabadilishe na kuoa vibinti vingine vidogo, yaani ni mambo ya tamaa tupu, wakati bwana wa amani kwa upande wetu sisi wakristo anasema kuwa alichokiunganisha Mungu basi mwanadamu asikitenganishe ovyoovyo,!!. Tena pia inatupasa kujiuliza kwa haki kabisa ndani ya mioyo yetu kuwa, tangu lini kitoto cha miaka 9 kinachoanza kubalehe hivi karibuni kikalale kitandani na babu yake mwenye umri wa miaka 40 halafu eti kitegemewe kuzaa watoto na kuwalea halafu kiwe na uzoefu wote unaohitajika kushughulika na matatizo yote ya ndoa??!!, maanatumeshaonyeshwa na waislamu kuwa kigezo chao cha ndoa ni kubalehe pekee tofauti kabisa na sisi wakristo wenye kigezo cha tamaa inayojumuisha mambo ya akili na utiyari wa rohoni wa mhusika, kumpa elimu ya ndoa kwanza na kumuacha ajisikie kuwa yuko tayari na anao uwezo wa kukabiliana na changamoto za ndoa. Hivi nabaki kujiuliza kuwa, wale wanafunzi wote wa kule primary wa darasa la tatu mpaka la saba kwa mujibu wa dini ya kiislamu wanatakiwa wafungishwe ndoa hata kama hawajamaliza shule kwa kuwa tayari wao wana kigezo cha balehe ya miaka 9, !!!. mwisho kabisa ni kwamba, kaka mhamad, mimi nilikuuliza maswali ya msingi ya kisheria huko juu, lakini kwa sababu wewe unajifanya hukuyaona ukaamua kuyakwepa, basi naomba ukae tayari ili mimi nikuulize tena hapo chini nitayaandika tena baada ya muda kidogo.

    Like

  193. Rich says:

    kaka mhamad, wewe ulituambia kuwa, sheria za Mungu kwa manabii wa kale yaani wakina nabii Musa, daudi nk, ndizo sheria hizo hizo mnazozitumia nyinyi waislamu leo hii pasipokubadilisha kitu au neno lolote, tena mnasisitiza zaidi kuwa mtume wenu mhamad hajabadili chochote mpaka hata walivyokuwa wanaswali na nyinyi hii leo mnaswali hivyo hivyo wakiwa ni waislamu wenzenu kama ninyi. swali langu hapa ni kwamba, kama hayo mnayosema ni kweli, mbona tena huwa mnatuambiaga sisi wakristo kuwa sheria zile za manabii wa kale haziwahusu nyinyi bali zile ni sheria kwa ajili ya israel pekee? Wakati hapohapo mlikwishatuambia kuwa zinawahusu tena pasipo kubadilishwa mnazifuata vilevile kwa ukamilifu wake leo hii kama wao walivyokuwa wakizifuata?. Pia wewe ulituambia huko juu kuwa bwana yesu sie nabii wa waislamu bali ni nabii wa wana wa israel pekee, lakini mbona sasa maneno yako hayo yanapishana na kitabu chako kinachowafundisha waislamu wote kuwa bwana yesu ni nabii wa waislamu akiitwa nabii wenu isa? Hebu nisaidie mimi mkristo kuniweka sawa ili nielewe mnachotaka kumaanisha kwa faida ya watu wote. Nakusubiri jibu lakini naomba majibu yanayoeleweka kwa uwazi wake kabisa maana hapa nimehoji mambo ya sheria za Mungu na watumiaji wanaopaswa kuzitumia, sikuhoji mambo ya nani kaleta na kwa wakati gani. Nataka jibu linalohusu hizo sheria na matumizi yake pekee ili nielewe kuwa ni kweli zinawahusu au haziwahusu.

    Like

  194. Ndugu Rich,
    Nakushukuru kwa maswali yako mazuri, ila naomba kukutaarifu kuwa maswali yako kuhusu sheria ni sawa kabisa na yale aliyouliza ndugu alfa, pamoja na wakiristo wengine pia wakitaka kujua uhusiano uliopo kati ya sheria za quran tukuf na zile za bible na torati. Kwa kifupi ni kwamba nimeshayajibu maswali yako yote nilipokuwa nikijibu hoja za alfa hapo jana naomba upitie majibu niliyompa ndugu alfa siku ya jana tarehe 7 kwa sababu naona yeye amebaki kimya labda amenielewa ila wewe kwa kuwa hujanielewa naomba uyasome utapata faida kubwa mno ndugu yangu. Pamoja na majibu hayo pia kuna maswali niliyaweka nina imani utawasaidia wakiristo kuyajibu ili wapate faida pia.Nitafurahi sana iwapo utasoma na kuuliza maswali kupitia majibu niliyowapa hapo juu kupitia kwa alfa. Ila ukitaka nirudie kujibu majibu yangu yatakuwa yale yale halafu tutajaza space bila sababu za msingi.
    Nakushukuru nitarejea badae kaka.

    Like

  195. alfa says:

    UNAJUA NILIDHANI UNAUELEWA WA KUTOSHA,KAMA SIVYO UNAFANYA KUSUDI BT UNAELEWA(HIV MANENO YALIYOSABABISHA YESU AMKEMEE PETRO NI YAPI,WAISLAM WANASEMAJ KUHUSU KUSULUBIWA KWA YESU,PETRO ALIPOKEMEWA ALIAMBIA NI KWA NINI BWANA ATASULUBIWA,NAYE AKAWA SHAHID WA MAMB HAYO YOTE,JE WAISLAM MNASEMAJE KUHUSU MATESO YA KRISTO KWA WOKOVU,C NINYI MASHETAN ALIOWAZUNGUMZIA BWANA YESU?KWA NINI MNAJIKOSOA WENYEWE?HALAFU NDUGU NAPENDA UNAVYOENDELEA KUJITUTUMUA INGAWA TUNAJUA HUJABAKIZA K2,UNAJIBU KWA KUKWEPAKWEPA,C 2NAKUENJOY SANA,MAJIB YAKO AJIBIWE MTOTO,UMEULIZWA KADR UNAVYOJITEGA,UISLAM NI JANJA YA UDANGANYIFU,HAMNA JIBU LA KIUTU UZIMA ULILOTOA,KIDOGO LABDA MJADALA ULIPOANZA,AFTA HAPO HUNA HOJA,KUKAA KIMYA KWANGU NI V2 UNAVYOANDIKA NA KUJIHUKUMU MWENYEWE NA DINI YAKO,HEBU MUELEWE BWANA YESU,UTAJIELEWA WE NDO MWENYE MAWAZO YA BINADAM KUTOKA KWA LUCIFER

    Like

  196. Ndugu Rich,
    Kuhusu suala la ndoa, niseme nafurahi san asana sana ndugu yangu kuona sasa umelielewa, namshukuru Sana Allah aliyenijaalia uwezo wa kuwa mwalimu mzuri mpaka vijana wa kikiristo sasa wananielewa.

    Ndugu Rich, wallah ungejibu vizuri kama leo tiyari tungeshaelewana zamani saaana ndugu, yangu.
    Kumbe kigezo cha binti kuolewa ni kuwaka tama! Na siyo umri, sasa kumbe hapo tumeelewana ndugu yangu, sasa kumbe jibu ulilijua halafu unaanza kuhoji swala la umri, sasa kama ni tamaa na si umri ni vipi sasa swala la umri lilikuwa linakusumbua ndug yangu? Kumbe hata mungu wa biblia yako hatambui swala la umri bali anachokitambua ni mwili kuwaka tama, sasa vipi unahoji kuhusu umri ndugu yangu na wakati kigezo ni tama ya mwili?Mwanzoni ulisema umri sasa hizi umebadilisha kigezo kimekuwa ni tama ya kimwili na siyo umri tena basi mi nafikiri kama ni mgonjwa tunaweza sema ameanza pata nafuu.

    Ndugu Rich, kwa sababu sasa Allah kwa uwezo wake amekufanya ukatambua kigezo cha kuolewa mwanamke si umri bali ni tama za mwili, ni vema sasa nikufahamishe kuwa kwa kuwa wewe inaelekea hujasoma sayansi hata ya darasa la sita, inaelekea hujui ni wakati gani mwili wa mwanamke huanza kuwaka tamaa.

    Ndugu Rich, kwa sababu mimi Alhamdulillah Allah kanijalia elimu na ufahamu wa biology kidogokidogo naomba kushare na wewe elimu hii huenda ukajua ni wakati gani mwili wa mwanamke huanza kuwaka tamaa.

    Ndugu Rich, mwili wa mwanamke hauwaki tamaa isipokuwa mpaka awe amebalehe au awe amevunja ungo.kwa sababu mimi sipendi ubishi wa kipumbaf usio na facts kama ulio nao basi naomba nikueleweshe ndugu yangu kwa kukupa facts za kibiologia.

    Ndugu Rich, mwanamke anapobalehe,au kitaalam anapofikia “puberty stage” mwili wake hupata mhemko unaotokana na kuzalishwa kwa wingi kwa “testeterone hormones” testerone hormone husababisha tezi ndogo ndogo ambazo hutengeneza mafuta ndani ya mwili wa binti hivyo huwa ni sababu mwanamke huyu huanza kuwa na hisia za kufanya mapenzi, na mwili wake huanza kuwaka tamaa , hivyo basi kipindi cha mwili wa mwanamke kuwaka tamaa hakimtokei mpaka awe amefikia puberty stage yaani awe amevunja ungo. Kibiologia mwanamke hali hii ya mwili kuwaka tamaa huwa ni mara nyingi kuanzia miaka 6 – 8 na kuendelea, na kwa wanaume ni kuanzia miaka 9-12 na kuendelea.

    Ndugu Rich, mimi nashindwa kuelewa biology yako umeisoma wapi, ama kweli ujinga ni mzigo, kumbe bado wale maadui watatu aliowapiga vita nyerere bado wapo hapa tanzanial, yaani ujinga, maradhi na umasikini.

    Ndugu Rich, huko juu umeeleza kuwa kitoto kidogo kinakuwa kinuka jasho, hiyo sayansi umeipata wapi ndug yangu, mtu mzima ndiye mnuka jasho kwa sabbu za kibiologia na jasho la mtu mzima husababishwa na hormone hizohizo za testeterone ambazo huzalisha mafuta yanayoitwa “seburm” kitaalam ambayo hutunzwa na kutolewa katika vinyweleo vya ngozi kama jasho la utu uzima, na jasho hilo ndilo huwa na tabia ya kutoa harufu, mara nyingi hutokea kupitia kwapani, na sehemu nyingine za mwili zenye vinyweleo vingi.

    Ndugu Rich, kwa kuwa umetambua kuwa sabbu ya mwanamke kuolewa siyo umri kama ulivyokuwa uking’ag’ania naamini kabisa umejigundua kuwa ulikuwa na ubishi wa kipuuzi, lakini sasa kwa kuwa baada ya kusoma biblia yako na kukuta inaeleza sababu zile zile nilizokuwa nikukwambia yaani sababu za maumbile “biological reason” yaani mwili kuwaka tamaa, mimi kazi yangu ilikuwa ni kukufahamisha tu kuwa mwili wa mwanamke unaanza kuwaka tamaa pindi anapobalehe na nimekupa sababu za kibiologia hapo juu.

    Hivyo basi biblia yako imekupa jibu sawa na nililokuwa nikikwambia, nakushauri pitia maandiko ya biblia yako kabla hujaleta hoja humu ndani.

    Kwa sasa namalizia kwa kusema mimi na wewe sasa ndugu Rich tumepata ushahidi kamili kuwa Bibi Aisha mama yetu waumini wa kiislam alistahili kuolewa na Bwana mtume Mtume Muhammad, kwa kuwa maumbile yake yalikuwa yanaruhusu kufanya hivyo.

    Ndugu Rich, kwa ushahidi wa kibiologia niliouweka hapa kwenye presentation hii, naomba utafute kitabu chochote cha biology au sayansi darasa la sita utaona ukweli wa maneno niliyoandika humu.

    Nakushukuru ndugu yangu, karibu.

    Wabillah tawfiq.

    Like

  197. alfa says:

    KUNA HOJA ZINGINE KUTETEA AIBU,LAKIN HATA ALIEZOEA KULA WATU HUWA HAACHI,UNATETEA UBAKAJI?HEBU OA WEWE MTOTO WA MIAKA SITA,HATA MKITETEA,UNYANYASAJ HUU WA WATOTO WA KIKE HATA ARABUNI KWA ULIMWENGU HUU UMEFEL,WE C UNA WATOTO,MAY B FRM YO FRIEND O BRO AU WE MWENYWE,MWANGALIE BINT WAKO WA MIAKA 6,HALAFU LINGANISHA NA UNACHOKIZUNGUMZA,MI NASEMA HATA WALA WATU HAWAACHI,UCTETEE UOVU KAKA,WALA USIMTETEE M2 MWOVU,NASHKURU UMENISAIDIA KUFAHAMU UELEWA WENU ULIVYO.2CJAZE NAFAS KA ULIVYOSEMA,UMEAMUA KUPUNGUZA UMR WA KUBALEH TOKA 11-14 MPAKA 6 _8 KUTETEA UBAKAJI,SA TUJADIL NINI TENA?UONG C PART OF LFE,ET UNATETEA DINI,BARIKIWA.

    Like

  198. Ndugu wakiristo,
    Baada ya kuzijibu hoja zenu zote kwa ufasaha na kuondoa madukuduku mliyokuwa nayo na baada ya ndugu alfa na Rich kunielewa, ni matumaini yangu makubwa kuwa huko waliko wanatafuta misikiti iliyo karibu ili wakamkiri Allah na mtume wake kwa kutoa shahada na kuwa waislamu,Ndugu waislam naomba mtoe taqbir kwa mafanikio haya, ama baada ya utangulizi huo naomba nirudi katika mwendelezo uleule wa kuonesha ni jinsi gani biblia inavyomkashifu Bwana Yesu, na ili hali Quran tukufu inamtukuza na kumnyanyua daraja za juu mno ili tuweze kuwasaidia wakiristo wengine waliobaki.

    Kwanza kabisa kabla sijaendelea na mjadala nawaomba ndugu zangu wakirsto muwe na moyo wa uvumilivu kwa ukweli niitakaowaambia ingawa najua mtaumia na mioyo itawaenda mbio lakini mtulie huo ndio ukweli na hautabadilika.

    Ndugu wakiristo, tukianza na kitabu cha Luka chapter4, tunaona mara baada ya mtoto Yesu kuanza kuhubiri, biblia inatwambia ghafla lilikuja bonge la muibilisi, yaani kubwa la maibilisi wote duniani likamnyakua kama vile mwewe anyakuavyo vifaranga vya kuku, na kumpeleka nyikani, wazazi wake wasijue yuko wapi maskini na hata ndugu na jamaa pia wengine walishaweka matanga tiyari wakijua mtoto yesu amekufa kwa maana hilo li-baba la maibilisi wote duniani lilikaa nae kwa masiku arobaini, yaani 40 days oclock. Kwa bahati mbaya kabisa, biblia inatwambia kuwa katika mission hiyo ya ibilisi kumteka mtoto yesu ibilisi alifanya featuring na Roho mtakatifu, na huyo roho mtakatifu ndiye aliyemchoma yesu kwa ibilisi, akimwambia kuna bwana mdogo mmoja hivi anajifanya anahubiri siku hizi hivyo mimi nitakuletea ndugu yangu shetani umtest kidogo.

    Enyi ndugu wakiristo hapo tunajifunza mambo mengi lakini kubwa zaidi tunajua na kutambua ni jinsi gani huyu mungu roho takatifu alivyokuwa rafiki kipenzi wa ibilisi hadi wakashirikiana kumteka mungu mwana yaani kamungu katoto ambako ni ka-yesu.Lakini pia tunajifunza ni jinsi gani nguvu ya yesu wa biblia kiroho ilivyokuwa ndogo hadi anazidiwa na kutekwa na ibilisi kwa siku 40 bila kujitetea.

    Luka 4:1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi jangwani, 2mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na Ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula cho chote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.

    Ndugu wakiristo biblia inaonesha kuwa ji-ibilisi lilimlea na kumfundisha mambo mbalimbali ambayo bwana Yesu alikuwa hajawahi kuyasikia kwa masiku yote hayo, mwisho biblia inasema kutokana na kwamba siku hizo zote kazi na masomo ya shetani yaani training ya shetani kwa yesu ilikuwa ngumu mno hivyo alishikwa na njaa karibia kufa. Ndugu masiku 40 siyo mchezo tena fikiria siku za zamani zilivyokuwa ndefu tofauti na siku hizi siku moja utafikiri saa moja, zamani ukiambiwa siku ni siku kweli yaani pengine labda siku moja ya zamani unaweza kuta ni sawa na siku mbili za leo.

    Ndugu wakiristo, tukiachana na habari za Ibilisi labda pia tuangalie baadhi ya kauli za Bwana Yesu ndani ya biblia kwa watu halafu tupime na tuone je bwana Yesu ndani ya biblia kweli alikuwa na busara au alikuwa na vielement vya ki-ibilisi;

    Ndugu wakiristo, ukisoma Matayo 7:6 utagundua bwana Yesu kawatukana na kuwadhalilisha na kuvunja utu wa watu ambao sio wana wa Israeli yaani mimi na wewe ndugu yangu, mtanzania mwenzangu Bwana na mwokozi wako kakuita nguruwe wewe, lakini jambo la ajabu mnachukia mkiitwa makafiri lakini bwana Yesu kawaita manguruwe na mijibwa koko, nyooote haa kimyaa, hakuna anayelalamika, mimi ningekuwepo kipindi hicho akayasema maneno haya wallah tusingeelewana, huwezi ukaniita mimi nisiye muisraeli nguruwe halafu nikakuchekea. Ndugu wakiristo nguruwe ni najisi soma hata biblia yenu inasema nguruwe ni najisi, sasa we mwenyewe kubwa jinga ni najisi kwa Yesu wa biblila halafu bado wewe unamwita mwokozi wako, na yeye ashasema hajaja kwa ajili nguruwe bali kwa ajili ya kondoo. Sio nyie manguruwe na majibwa. Ndugu wakiristo soma hata (Mathayo 15:27) utaona matusi ya yesu bado yanaendelea juu ya watu wa mataifa.

    Biblia inaendelea kumdhalilisha bwana Yesu, pale inapoonesha kuwa alikuwa na mijitusi kuliko hata mateja wa mtaani pale alipowatukana hata hao manabii waliomtangulia ambao nyie wakiristo mnawatetea manabii hao na kuwaita wakiristo wenzenu, Bwana Yesu alisema

    (YOHANA 10:8)“wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi.”

    Wakati nyie mkisema hao manabii waliotangulia ni wakiristo wenzenu, bwana yesu anakuja na kauli tofauti pale anaposema wote waliomtangulia ni wevi na wanyang’anyi.yaani ina maana hata akina Suleman, Daudi, Ibrahim, Yakobo,Isaka n.k woote walikuwa wevi na wanyang’anyi.

    Bwana Yesu, hakuishia hapo bali aligeuzia matusi yake hata kwa wanafunzi wake pale aliposema;
    ”Enyi wazao wa nyoka” (Mathayo 12:34)
    Yaani alipoona masikini watu wanamuuliza maswali katika hali ya kutaka kufahamu alikuwa akikosa majibu na kuanza kuwatukana, Hivi ndugu yangu wewe ukiitwa mzao wa nyoka, utajisikia vizuri kweli kwa akili yako ya kawaida, kwa sababu unapoitwa uzao wa nyoka ina maana hata baba na mama yako na wao ni majoka, sasa ndugu yangu si matusi hayo kweli.

    Ndugu wakiristo bwana yesu ndani ya biblia hakuishia hapo bali biblia inaelezea kuwa siku moja wanafunzi wake walimfuata wakimuomba awaoneshe miujiza sasa soma hapa chini majibu aliyowapa ndugu yangu halafu upime kama kweli huyu alikuwa mtu muungwana kweli kama unavyoaminishwa au biblia inaonesha yesu alikuwa mtu mwenye mijitusi na majivuno.

    Matayo 12:
    38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.
    39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

    Masikini wanafunzi wamemwendea kwa nia nzuri ya kutaka kufahamu na kujua, lakini yeye anaingiza mambo ya zinaa, yaani jibu haliusiani na swali, wao hawajamuuliza kuhusu mambo ya zinaa lakini yeye kwanza mawazo yake yamemtuma kwenye zinaa, hivi watu wanaomba ishara wewe unawaita kizazi cha zinaa, sasa kama ni kizazi cha zinaa ina maana hata Yeye bwana Yesu alikuwa kizazi cha zinaa kwa sababu hao ni ndugu zake kwa ushahid wa (yohana 20:17)mayahudi ni ndugu zake, na wao tiyari ni kizazi cha zinaa, kwa hiyo biblia inatwambia hata yeye Yesu ni kizazi cha zinaa pia.

    Ewe ndugu Mkiristo, bwana Yesu hakuishia hapo kuwaita majina ya ajabu ajabu wanafunzi wake bali kama tulivyokwisha ona jinsi Petro alivyoitwa Shetani, masikini Petro alikuwa akimpenda sana Yesu lakini kosa moja tu jamaa akamwita Shetani,Yaani Yesu ndani ya biblia alikuwa akiwaza mambo ya matusi matusi tu, na kutukana watu wanaomuuliza maswali ya msingi, yaani ni kama vile alikuwa hajiamini kabisa kwa maana siku zote mwalimu ambaye huwa hajiamini akiulizwa swali kidogo tu darasani lazima atukane.

    Ndugu mkiristo ukisoma Matayo 17:17, utaona tena bwana Yesu anadondosha matusi mengine kwa wanafunzi;
    MATAYO 17: “17 Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini?”
    Yaani bwana Yesu alikuwa asiulizwe swali tu na wanafunzi wake jibu lake lazima liambatane na matusi.sasa kumbe kama wanafunzi wako unasema ni kizazi kisichoamini na kilichopotoka watawezaje sasa kutangaza injili yako na hali hawaamini na wamepotoka?

    Ndugu wakiristo mada hii ni pana sana ila nakaribisha maoni yenu
    Kwa sasa namalizia kwa kusema Qur’an inamtukuza Yesu, Biblia inamtukana Yesu.we are proud that we love Allah, Muhammad and Jesus ibn Mariam , karibu tujadili;

    Wabillah tawfiq;
    Wahaadha ssalaam.

    Like

  199. alfa says:

    HAUNA SERA,RICH ALIKUJIB KWA UKARIMU,CKUTEGEMEA KA UNGEONGEA TENA,UNAJIAIBISHA KAKA,KWA HAPO HAKUNA MWENYE AKILI ATAKAECHANGIA UPUUZ WAKO,MAANA KAMA RICH ANGEENDELEA BILA HEKIMA,NINGEWAONA WOTE VICHAA,ILA C KOSA LAKO,UMECHOKA NA HUNA HOJA YA MSING YA KUTETEA WALA KUPINGA,KAPUMZIKE MJOMBA.

    Like

  200. alfa says:

    WATU WAZIMA USITUFANYE WATOTO,NAMSHUKURU KAKA MUHNA KWA KUONYESHA UKOMAVU,NA NDUGU RICH KWA BUSARA ZAKE,PIA NDUGU ZETU WAISLAM WOTE KWA KUONYESHA USHIRIKIANO,TUNAWAPENDA,TENA C USON TU NA ISIWE MOYON ET KWA SABABU YA IMAN ZENU NO,NAMUOMBA BWANA AWAPE MIOYO LAINI,MJUE PENDO LA MUNGU KWA WANADAMU,MUNGU ALITUPENDA KWANZA,AKATUCHAGUA,NA HUTUPIGANIA,ONDOEN MAWAZO YA KUDAI MNAMPIGANIA YEYE PAMOJA NA DINI YAKE,HAJAWAH KUPIGANIWA BAL AMEWAPIGANIA WATU WAKE CKU ZOTE,NA PENDO LAKE AMELIDHIHIRISHO KWA KRISTO,ALIPOFANYIKA MWANADAM MWENYE HAK NA KUUTOA UHAI WAKE KAMA SADAKA KWA AJIL YA WANADAM WOTE,DAMU ILIYOMWAGIKA MARA MOJA KWA ONDOLEO LA DHAMBI,HATUHTAJ KONDOO WALA MBUZ KAMA KILA MWAKA,NA HII NI KWA WATU WOTE!!!USIJIHESABIE HAK KWA KUDHAN UNAMPENDA MUNGU NA KULIKATAA PENDO LAKE,NA UKIISHIWA HOJA POSITIVE KAPUMZIKE.AHSANTEN COZ 2MEBADILISHANA MAWAZO VYA KUTOSHA.

    Like

  201. Rich says:

    Kaka mhamad, hivi kwanini waislamu wenzako hawajitokezi ili kukusaidia ndugu yangu, mpaka unaweweseka na kuaibika namna hiyo jamani?!!!…hebu angalia sasa unavyobabaika na kufedheheka kiasi hicho ndugu yangu. Wewe umetoka kwenye balehe ya vitoto vya miaka 9 , uliyo tuonyesha huko juu kwa mujibu wa dini yako ya kiislamu….ukaendelea kuporomosha miaka ya balehe za watoto mpaka sasa kufikia miaka 6-8 kwa mujibu wa wanasayansi,!!!!. Haya ni maajabu kwelikweli. kwanini sasa unajaribu kuchanganya neno la Allah na elimu za kidunia ulizofundishwa mashuleni?!, Sasa hapo tushike na kuamini usahihi upi ndugu yangu,!!. Kama kweli wewe ni msomi mzuri kupita sisi, huoni kuwa elimu yako ya shule pamoja na elimu yako ya dini, zote kwa pamoja zinakufundisha wewe kuwa na mchezo mchafu usiozingatia heshima za ndoa na haki za watoto wadogo kwa kutuonyesha sisi kwamba, vibinti vidogo vyote kuanzia miaka 6+7+8+9 vinatakiwa kuolewa, kwa sababu mmoja tu, aliowapa Allah kuwa, vibinti hivyo vimekwisha kubaleh !!. Kwakweli hali hii ndiyo niliyoielezea huko juu kuwa, tatizo la mtume wenu mhamad lilikuwa ni kuendeshwa mno na tamaa ya ngono kuliko jambo lolote lile maishani mwake, ndio maana akawa anatunga sheria zake anazozijua kuwa zingeweza kumtimizia haja zake. Yeye alikuwa na mchezo wa kuchuma maembe ambayo hayajakomaa(vidakwa) kwa kisingizio kuwa tayari yamekwisha kuwa maembe kwa sababu hayafanani tena na majani ya muembe,!!!!. Ndugu yangu mhamad yohana, mimi naamini kabisa kwa sasa kuwa, wewe mwenyewe umetambua kuwa quran kamwe kamwe kamwe sio neno la Mungu wa kweli, ila ni hadithi za uongo za mtu fulani aliejiita nabii wa Mungu, aliepandwa na mapepo makali yenye nguvu mno, yaliyomsaidia achanganye maneno ya uongo ya maisha yake ya kidini pamoja na elimu za kidunia ili kujitafutia uhakika wa jambo, kama ulivyo fanya wewe hapo juu ya hoja zako!!. Maana mtoto wa nyoka ni nyoka. Huo umri wa miaka 6 wa mtoto mdogo uliotuonyesha sisi wakristo hapo juu ni umri wa shule za darasa la kwanza au lapili, kwa hiyo, sisi wakristo tukikuona unakatamani katoto ka umri huo, tutakukamata halafu tukutie jela ukanyee mavi yako kwenye ndoo na masela gelezani kwa kuwa wewe tutakuita ni ‘MBAKAJI’!!. Uondoe upesi akilini mwako, huo ujinga uliouandika hapo juu…Mwandawazimu mkubwa wewe!!!. Sasa ndugu yangu unanipandisha hasira ijapokuwa nitajitahidi kujikaza maana nikikatazama kabinti kangu kenye miaka 7 jinsi kalivyo, alafu wewe unatufundisha kuwa inampasa amlale babu yake mwenye miaka zaidi ya 40, kwakweli ninaona kama unanitusi mimi!!. Dini ya ajabu sana hiyo. Nimalizie ndugu yangu kuhusu yale maswali yangu mawili tu, niliyokuuliza ukasingizia kuwa uliyajibu kupitia kaka Alfa, sio kweli kuwa uliyajibu pale ila ulitoa maelezo ya ovyoovyo ya hadithi za mtume wako tofauti kabisa na lengo la maswali yale. Najua kuwa huyawezi, tena yamekushinda kabisa.Mambo mengi sana uliulizwa na kuhojiwa huko juu kabisa ya hoja zako lakini mchezo wako ni huohuo wa kutetea dini kwa kulazimisha mambo ya uongo na yasiyo na msingi!!!. Eti unatoa sababu kuwa unaogopa utaijaza hii blog utakapo nijibu hayo maswali yangu mawili, kwani kazi ya hii blog ni nini kama sio kujazwa??, kwani tunalipia hapa!!, vipi ndugu yangu wewe!. Ndio maana hata hapo juu umetoa lawama za kimaandiko za kitoto kabisa ambazo hata nyingine zilikwisha jibiwa vizuri huko juu. yaani umeandika hoja kama mtoto mdogo asiejua kitu na ndio kwanzaaa anae anza kuuliza maswali,!!!. Sasa hebu jibu hayo maswali yangu mawili, kwa ufupi tu, ukilenga jibu la kile nilichouliza halafu ukimaliza na mimi nikilidhika na kuona kuwa sina cha kuhoji kuhusu hivyo viswali vyangu viwili, basi na mimi nitakujibu huo utoto wako hapo juu kwa 100% kwa kuwa nimesha upitia vyema kabisa. Haya, twende kazi ndugu yangu…

    Like

  202. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Rich,
    Kwanza nakushukuru sana kwa kujitokeza kutoa mchango wako, lakini pia samahani sana kwa kukukwaza kutojibu maswali yako kama ulivyotaka na hii imetokana na kuwa mwanzo niliona kama yanafanana sana na aliyo uliza ndugu alfa hivyo nikahisi utaweza kuelimika kupitia majibu niliyompatia ndugu yangu alfa, lakini kwa sasa nimeyapitia kweli nimeona kuna utofauti kidogo katika jinsi ya uulizaji, hivo ni haki yako kupewa majibu ya msingi ili usipoelewa uulize tena mpaka uelewe inshaallah.

    SWALI LAKO; swali langu hapa ni kwamba, kama hayo mnayosema ni kweli, mbona tena huwa mnatuambiaga sisi wakristo kuwa sheria zile za manabii wa kale haziwahusu nyinyi bali zile ni sheria kwa ajili ya israel pekee?

    JIBU LAKO: Manabii wengi waliomtangulia Mtume wetu Muhammad(S.A.W) walitumwa kwa ajili ya taifa tukutu la wana wa Israeli, ingawa wapo manabii waliotumwa hata kabla ya kuwepo kwa taifa la israeli ambao ni akina nabii Nuhu,Lutu, Ibrahim na wenigineo, manabii hao wote walikuwa ni manabii waislam kwa ushahidi wa quran yetu tukufu na wengi wao waliotumwa kwa ajili ya kuwaendea wana wa israeli. Manabii wengine walitumwa kwa ajili tu ya makundi flani ya watu ndani ya Israeli kwa mfano soma kuhusu nabii Yona ambaye ndani ya quran tukuf ametajwa kama nabii Yunus aliyetumwa kwa watu wa Ninawi tu, nabii Musa quran inatwambia alikuwa nabii mwislam aliyetumwa kwa ajili ya kuwakomboa wana wa israeli kutoka utumwani na baada ya kuwakomboa Allah anatwambia ndani ya Quran kuwa alimpa torati kwa ajili ya kutawala taifa teule la Israeli, Nabii Lut alikuwa nabii muislamu alitumwa kwa ajili ya watu wa sodoma kabla hata israeli yenyewe haijawepo n.k, Ndugu Rich, quran inatwambia walikuwa manabii waislam wote hao.Soma hata biblia yako utakuta hata bwana yesu anasema hakutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya israeli.Sasa ndgu yangu jibu ni rahisi tu wewe siyo muisraeli lakini ukisoma quran hakuna sehemu utakuta inasema au katka hadith mtume aseme nimetumwa kwa mataifa ya kiarabu, hapana, hata siku moja hutakuta, kwa maana hata hao warabu wenyewe hawajatajwa kabisa ndani ya quran tofauti na yesu katika biblia ni israeli mwanzo mwisho, hata miji yenyewe aliyozaliwa na kufia mtume wetu haijatajwa ndani ya quran tukuf lengo likiwa ni kukuonesha ni jinsi gani hakuwa mtume wa sehemu au kikundi flani bali kwa ajili ya dunia nzima.tofauti na biblia utasikia mara bethlehemu, mara golgotha n.k hiyo kwenye quran hamna kwa sababu quran siyo ya bethlehem, saudi arabia wala india bali ni kwa ajili ya ulimwengu mzimam.Biblia inaonesha wasio waisraeli wamefananishwa na mbwa na nguruwe na wana wa israeli wameitwa wana, kuonesha kwamba lengo la Yesu siyo wewe mbwa bali wana, kuonesha kwamba hakutumwa ila kwa ajili ya Israeli, lakini Mtume sisi anatwambia hakuna ubora juu ya rangi au kabila la mtu bali mbora mbele ya Mwenyezimungu ni mchamungu.

    Ndugu Rich, kwa kumalizia jibu la swali lako, ni kwamba sheria hizi tulizonazo ndani ya quran ni sheria hizohizo walipewa manabii waislam kwa ajili ya Taifa la Israeli waliomtangulia mtume, naamini kabisa hilo ndo jibu sahihi la swali lako sasa hapo sitaki kusikia unasema mara oooh, tunasikiaga, mara tunaonaga, sitaki kusikia tena lawama hizo majibu sahihi hayo hapo.

    Ndgu Rich, Mtume aliyetumwa kwa ajili ya ulimwengu wote ni kipenzi cha Allah mbora na mwisho wa Mitume woote, yaani Mtume Muhammad ibn Abdillah(S.A.W), ndiyo maana tunaposoma katika hadith inaonesha alishatuma wanafunzi/maswahaba zake Afrika nchi iliyokuwa ikijulikana kama Uhabeshi sasa hivi Ethiopia. Kuonesha kuwa Yeye hakuwa mtu me wa warabu kama alivyokuwa yesu mtume wa waisraeli tu na kama yesu mwenyewe anavyojitambulisha ndani ya Biblia. Pia katika wanafunzi wa mtume kulikuwa na mwanafunzi mweusi tii kutoka Afrika aliyekuwa akijulikana kama Bilal ibn Rabaa na mtume alimpenda pendo la kupindukia hadi akamteua kuwa mtoa adhana katika msikiti wake, tofauti na yesu anayeonekana kuitwa watu kwa lugha za matusi wasiokuwa waisraeli.

    Ndgu Rich, tofauti na nyie mnaodai kuwa hao walikuwa wakiristo, ni tofauti kabisa kwani biblia hakuna mahala inaposema kuwa hao walikuwa wakiristo bali tunaona ukiristo ni dini iliyaoanza baada ya kuondoka bwana Yesu duniani yaani ni dini mpya na dini ya uongo iliyoanzishwa na mtu ambaye anaonesha alikuwa muuwaji na mtesi wa wanafunzi wa Yesu, ilianzishwa na mtu mmoja aliyeitwa Paulo. Kwa hivyo basi ni ushaidi tosha kuwa bwana yesu dini yake ilikuwa ni uislam kama waislam wengine waliomtangulia na wakiristo na ukiristo ni neno ambalo kwanza hakuwahi kulitamka wala hata kulisikia lakini tumeona bwana Yesu alishawahi kuwaambia wanafunzi wake wawe waislam kama alivyo yeye soma ndani ya biblia mwenyewe utaona.Kwa hiyo ndugu yangu usisumbuke Bwana Yesu alikuwa muislam mwenzetu aliyetumwa kwa ajili ya taifa la Israeli.Ndugu Rich hizi hoja nimeshazijibu saana sana hata ndugu yako Mhina Nilimjibu mpaka akanielewa.

    Ndugu Rich, jambo kintaotushangaza na kututia kichefuchefu sisi waislam, ni pale tunapoona nyie wakiristo mnadai kuwa manabii wa zamani walikuwa wakiristo wenzenu ilihali sheria zao mnazipinga kwa 100% na mnadai zimepitwa na wakati , tena wakati mwingine mnadai amri walizopewa manabii hao zimebatilika, Sasa kama amri hizo walipewe wakiristo wenzenu halafu zikabatiklika basi bila shaka na nyie imani yenu ni batili, au mnataka kumaanisha Mungu alileta ukiristo wa kwanza halafu akaubatilisha halafu tena akaleta ukiristo mwengine mpya, sisi waislamu tunasema huo ni msiba, kama mungu wenu anaibatilisha dini yenu halafu anaunda dini hiyohiyo basi inaonesha kabisa yehova alikuwa hana uhakika na anchokifanya. Naomba nirudie kumnakiri tena mchungaji mosespk kwa faida yako ndugu yangu Rich, alipokuwa akichangia mojawapo ya mada kwenye blog hii amesema hivi:

    By Mosespk “AMRI KUMI, TORATI NA AGANO LA KALE YOTE YAMESHAONDELEWA!
    Mungu alitabiri kwamba ataondoa agano la kale na kufanya agano jipya lililotofauti……….”

    Ndugu Rich, huyo bwana ni mchungaji mkubwa na mwenye elimu yake ya kichungaji kabisa, kuliko hata wewe Ndugu Rich, yeye anadai hata zile amri kumi alizopewa musa zishaondolewa yaani kwa mfano ile amri inayosema usizini au usiibe au usisime uongo sasa zishaondolewa hivyo kusema uongo ruksa, kuiba ruksa, kuzini ruksa n.k lakini jambo la kushangaza utakuja kuta hata yeye biblia yake bado inalo agano la kale ndani yake, sasa je ni ya nini basi kama sheria zake zimepitwa na wakati ?

    Tena mchungaji huyu anaendelea kwa kusema ;
    By Mosespk “Misitari hii yaonya kwamba agano jipya linadumu bali agano la kale limebatilika”

    Sasa kama agano la kale limebatilika, ni kwa nini basi mnapohubiri mara nyingi mnatumia agano la kale ?Hebu ndugu Rich, tuambie agano la kale limebatilika hivi ni mara ngapi wewe mwenyewe umeshuhudia kanisani kwenu mchungaji wenu anawambia mara soma kitabu cha mwanzo, mara kitabu cha hesabu mara kutoka n.k, sasa vipi tena mnatumia maandiko batili ndugu zangu wakiristo?

    SWALI LAKO: Pia wewe ulituambia huko juu kuwa bwana yesu sie nabii wa waislamu bali ni nabii wa wana wa israel pekee.

    JIBU:Nabii Yesu alikuwa nabii muislam aliyetumwa kwa ajili ya taifa la israeli, hivyo Yesu ni nabii wa kiislam na ni muislam mwenzetu aliyetumwa kwa ajili ya taifa la israeli.

    Naamini nimekujibu maswali yako yote mawili kwa ufasaha ingawa yamekuwa ni marudio ya maswali waliyokuwa wakiuliza ndug zako akina mhina n.k lakini usihofu sisi tutaendelea kuwapa majibu mpaka mridhike na naamini hapo ulipo umeridhika na kuelewa ndugu yangu.

    Ahsante ndugu yangu.
    Wabillah tawfiq.

    Like

  203. Rich says:

    Kaka mhamad, umesema kuwa manabii wote walitumwa kwa ajili ya israel pekee, tena unasema kuwa manabii wote hao walikuwa ni waislamu kama nyinyi, ndugu yangu, hivi unataka kuniambia kuwa dini ya wana wa israel ilikuwa ni uislamu kama hao manabii wao waliowaletea hizo sheria kutoka kwa Mungu?, mbona katika vitabu vya torati, zaburi na injili sheria zake ni tofauti kabisa na sheria za kitabu chenu mnachokitumia wakati wewe unasema kuwa sheria za manabii wa nyuma ni hizo hizo zilizokuwemo kwenye quran? tena hapo hupaswi kusema kuwa neno la Mungu la sasa limeharibiwa na kuchafuliwa kwa sababu, kwa mujibu wa Allah, alisema kuwa kamwe neno lake, yaani hizo sheria alizo wapa manabii wa zamani, haziwezi kuchafuliwa wala kubadilishwa na mwanadamu yeyote. Lakini pia nikuulize kuwa, hivi kigezo cha kuwa muislamu ni nini haswa ili tuone kama manabii wa zamani kama ni kweli walikuwa ni waislamu kwa kufuata vigezo hivyo. Au tuseme mtu yeyote anaweza kuwa muislamu bila ya utaratibu na nguzo zilizo onyeshwa kwenye quran? Pia kama sheria za muongozo na utaratibu wote wa uislamu ulikwisha kamilishwa na manabii wa kale, kilichompa unabii mtume wenu mhamad mpaka akawa ni mtume aliye bora kuliko mitume wote wa Mungu walioukamilisha uislamu ni nini na wakati yeye hajawaletea waislamu sheria yoyote mpya kutoka kwa Mungu?,mwisho nikuulize kuwa, kama unasema kuwa manabii hawa wa nyuma walitumwa kuleta sheria na muongozo wa Mungu kwa ajili ya israel pekee, iweje tena hizo sheria walizozileta pamoja na muongozo wake ziwahusu ninyi ambao sio waisrael?….ndugu yangu mhamad, pia usinihukumu kwa ajili ya mawazo ya mtu mwingine. Swala la huyo bwana sijui mosespk na mitazamo yake yote ulionielezea kamwe hainihusu mimi tena wala simjui kabisa. Hebu jaribu kumtafuta ili kumhoji mambo yote usiyo yaelewa kwake. Mimi naamini kua hakuna mwalimu wa kweli wa moja kwa moja aliye sahihi kwa kila jambo zaidi ya bwana yesu. Kuwa mwalimu sio kigezo kabisa cha kuwa sahihi kwa kila jambo, ndio maana maandiko yanatuambia kuwa sisi wote ni viungo kila mmoja ni kiungo kwa mwenzie. Inawezekana hata yeye akipitia blog yake hii, anaweza kujifunza mambo mengi asiyoyajua mpaka yeye mwenyewe akashangaa. Sasa, wewe unaniambia kuwa yeye ana elimu kubwa kuliko mimi, umetumia kigezo gani kama sio uzushi huo!!. Basi mimi naomba niishie papa, kama utapenda kuyatolea ufafanuzi hayo maswali yangu kama nilivyo hoji tena hapo juu, basi itakuwa ni vyema. Kwaheri ndugu yangu.

    Like

  204. Rich says:

    ndugu mhamad, mimi kwa upande wangu ninaiona dini ya kiislamu ni nini yenye uongo wa ki- wanazuoni wa hali ya juu kwelikweli mtu kuweza kuutambua huo uwongo wake. Hebu hata ukipitia hoja zako huko juu, wewe ulitoa mpaka aya inayoelezea kuwa, Allah aliteremsha sheria za kale kupitia manabii ili kusadikisha waliokuwa mwanzo kabla ya Muhamad halafu akateremsha quran iwe muongozo kwa watu wote, lakini chakusikitisha ni kwamba hapo juu umepingana tena na kitabu chako cha muongozo kwa kusema kuwa sheria na muongozo uleule wa nyuma wa manabii ndio huo huo mnao utumia hivi sasa pasipo kubadilisha sheria yoyote, tena ukaongezea kwa kusema kuwa mpaka jinsi walivyokuwa wanaswali na nyinyi waislamu wa leo mnaswali hivyohivyo !!!. Sasa kwa hali hiyo ndugu yangu isiyoeleweka, itabidi mimi unisamehe sana kwa kuwa huwa ninatabia mbaya sana inayoitwa udadisi wa uhakika wa ukweli wa mambo. Ndiyo maana ninapokuambia kuwa yesu ndiye njia pekee basi hakika haitabadilika bali itakuwa hivyo hivyo milele na milee hata kama wanaadamu watajaribu kupinga na kukataa.

    Like

  205. Rich says:

    nyinyi waislamu wa leo mnasheria mpya za mhamad za kwenda kwenye kaburi lake la huko makka na kumpiga mawe shetani asie onekana huku mkiwa mmevaa shuka nyeusi kama freemason, mambo ambayo kamwe kamwe hayajawahi kuwepo wala kutekelezwa katika sheria za manabii wote wa nyuma!!!!!. Sasa, mimi nabaki kujiuliza kuwa, kama ni kweli kuwa sheria walizozitumia manabii wa nyuma, ndizohizohizo wanazozitumia waislamu wa leo hii, wakijaribu kujitetea hivyo ili wasigundulike kuwa wamepotezwa….mbona sasa wanafanya mambo ya ajabu na tofauti kabisa na ukweli wenyewe?!!, kazi kwako ndugu yangu ili na wewe ujiweke kwenye tafakari kuu na udadisi wake kama mimi .

    Like

  206. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Rich,
    Kwanza nimshukuru Allah sub-hana wata’ala, aliyenijalia neema ya afya lakini zaidi nimshukuru kwa kuniingiza katika nuru ya uislam, kwa uchache wa shukrani niseme Alhamdulillah.

    Pili nikushukuru wewe ndugu Rich kwa jinsi ulivyouliza maswali yako, kwani ki-ukweli nisifiche umeuliza maswali ya msingi mno tofauti na ulivyokuwa ukiuliza mwanzo, kwa jinsi ulivyouliza unaonesha unayo nia ya kutaka kufahamu na siyo kubishana.na mimi kwa uwezo wa Allah nitajitahidi kuyajibu kama inavyostahili na naamini kwa uwezo wa Allah utaridhika na majibu yangu inshaalllah.

    Ndugu Rich, Tukianza na swali la kwanza ambalo umeuliza je kama manabii wa Israeli walikuwa waislam, ina maana hata dini ya wana wa Israeli ilikuwa ni uislam?
    Ndugu Rich, siwezi sema kwa ujumla kuwa dini ya wana wa Israeli ilikuwa ni uislam, ila ninachoweza sema ni kuwa quran inaonesha kuwa walikuwa waislam wale tu waliofanikiwa kuwakubali, kuwapokea na kuwatii manabii wa Allah, hao tu ndio waliobahatika kuwa waislam ila waliobaki waliendelea kuwa makafiri, tena wengine waliwaua manabii bila haki yoyote ya kuwauwa, ila wachache walikuwa waislam.
    Ndugu Rich, ukisoma quran inaonesha kuwa hata wanafunzi wa Yesu walikuwa waislamu, lakini tofauti na tukisoma biblia kwani ndani ya biblia tunaona dini ya ukiristo haikuwepo mpaka Yesu katoka dunianina kibaya zaidi mwanzilishi wa dini ya kikiristo ni mtu aliyekuwa akiwatesa na kuwauwa wanafunzi wa Yesu;

    Ndugu Rich, ukisoma quran tukuf Allah anatwambia kama ifuatavyo.

    SURA 5. SURAT AL MAIDA
    110. Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo SURA ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!
    111. Na nilipo wafunulia Wanafunzi kwamba waniamini Mimi na Mtume wangu, wakasema: Tumeamini na shuhudia kuwa sisi ni Waislamu.

    Ewe ndugu Rich, ukisoma iyo aya ya 111, inaonesha kabisa kuwa wanafunzi wa Yesu walikuwa waislam, ila ukisoma mistari ya mwisho aya ya 110 inaonesha kuwa kuna baadhi ya wana wa Israeli walikufuru wakamwita Isa mchawi kwa vile alivyoonesha miujiza kwa idhini ya Allah, hivyo hao hawakuwa waislam.

    Ndugu Rich, pia umeuliza kuwa sheria za quran mbona ziko tofauti na sheria za Quran na pia ukasisitiza kuwa Allah anasema neno lake hakuna wa kuliharibu sasa vipi mbona kuna utofati ?
    Ndugu Rich, kwanza kabisa naomba nikukosoe kidogo kuwa hakuna sehemu ambayo Allah anasema neno lake haliwezi kubadilishwa, bali Allah anasema maneno yake ndani ya quran tu ndiyo hayawezi kubadilishwa na mtu yoyote, lakini Allah anatuambia kwa uwazi kabisa jinsi watu waisraeli walivyoweza kuwauwa baadhi ya manabii na kubadilisha neno lake.

    SURA 2. SURA AL- BAQARA
    59.Lakini walio dhulumu waliibadili kauli isiyo kuwa waliyo ambiwa. Kwa hivyo
    tukaiteremsha juu ya wale walio dhulumu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya
    walivyo kuwa wamepotoka. »

    Ndgu Rich, watu walibadili maneno ya kweli ya Allah ndani ya torati na kuweza kuingiza matashi yao, hivyo hivyo neno la kweli la Allah neno la Injili watu waliweza kubadili na kupotosha kwa jinsi walivyojua wao.
    Ndugu Rich,kwa hakika haya si maneno ya quran tu, bali hata biblia yako inatwambia ni jinsi gani wana wa israeli walivyoweza kubadilisha maneno ya torati na kuweka maneno yao wakidai yametoka kwa Mungu. Kwa mfano soma aya ifuatayo ndani ya biblia.

    YEREMIA .8:8 « Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo. »

    Ndugu Rich, andiko hilo ndani ya biblia linathibitisha kabisa kuwa kuna waandishi waliotumia kalamu zao kuweza kulibadili neno la Mungu wa kweli ndani ya torati na kuabadilisha yale maneno waliyokuwa wakihisi hawayapendi na kuyaacha yale waliyokuwa wakiyapenda.Sasa hayo siyo maneno ya waisla ni biblia yako ndiyo inayosema.

    Ndugu Rich,ukisoma (Matayao 23:1-30)utaona ni jinsi gani Bwana yesu aliwataadharisha sana na wanafunzi wake dhidi ya waandishi na farisayo, ambao kazi yao ilikuwa ni kulibadili neno la Mungu kwa kujifanya wao wachamungu kumbe ni waongo.
    Sasa ndugu yangu Rich, kama kweli wewe ni msomi wa Biblia utawezaje sema neno la mungu la torat halikubadilishwa ?

    Ndugu Rich, waandishi wenyewe waliotafsiri biblia wamekiri kabisa kuwa kuna mambo walilazimika kuyabadilisha kwa mfano soma walivyoandika kwenye dibaji ya biblia zile ndogo zenye kava gumu na jeusi.

    «…. maendelezo ya majina yote ya watu na ya mahali ilikuwa lazima yafikiriwe tena na mengine kutengenezwa jambo hili ilikuwa kazi kubwa sana kwa sababu yapo majina zaidi ya 3,500 tuliyotengeneza »

    Hapo tu kwa biblia uliyoshikilia mkononi soma kwenye dibaji ukakutana na maneno hayo ni kweli utaendelea kuwa na imani na neno la biblia na ili hali waandishi wenyewe wanakiri kabisa kuwa mikono yao imeshiriki kuweka majina ambayo hata yehova mwenyewe aliyasahau hivyo wenyewe ikabidi wamkumbushe yehova baadhi ya majina ya watu na maeneo aliyoyasahau, sasa je si watu hao wanakosoa kile ambacho wanaamini mungu wao alikisahau ? ndugu Rich utasemaje neno la mungu halikubadilishwa ?

    Ndugu Rich, kubadilishwa kwa maneno ya Mungu hakuishii hapo bali tunaona pia biblia mlizo nazo hazifanani kabisa, kwani ile ya waroma ina vitabu vingi zaidi vya agano la kale hivyo kufanya idadi kuwa 73, lakini biblia ya makanisa ya born again ina vitabu 67,ambayo ni deficient ya vitabu 6, ukiwauliza wakiristo wa makanisa ya borna gain ni kwa nini hamuamini vitabu 6 vilivyopo kwenye biblia ya roman catholic utaambiwa ni kwa sababu maneno yake yalifanana sana na yale yaliyomo ndani ya quran hivyo kanisa likaamua vitabu hivyo vitolewe ili kulinda heshima ya kanisa. Ndugu Rich, utasema kweli neno la mungu halibadilishwi ?

    Ndugu Rich, kutokana na ushahidi niliokupa hapo juu naamini kabisa utakuwa umekubaliana na mimi kuwa maneno mengi yamebadilishwa, na si kwamba nasema hivyo kwa sabbu mimi ni muislam, la bali ni maneno ya biblia yenyewe yanathibitisha hivyo.
    Ndug Rich, kutokana na kuwa neno la biblia limebadilishwa saana sana hivyo sisi waislam, huwa hatuamini ukweli wa jambo lolote ndani ya biblia mpaka liwe linaendana na lile neno la kweli ambalo halijabadilishwa na kiumbe yeyote asiyekuwa Allah, hivyo basi sheria yoyote ile kutoka ndani ya biblia inayopingana na quran, hiyo lazima ndugu Rich utambue kuwa ni sheria ya uongo na si sheria ya torati ya kweli ya Mungu wa kweli ambaye ndiye Allah.

    Ndugu Rich, pia umeuliza kigezo cha kuwa muislam ni nini hasa ili tupate kujua kuwa kweli manabii wa zamani walikuwa waislam. ?
    Ndgu Rich, ili uwe muislam ni lazima uamini katika mambo yafuatayo:1.Kuamini kuwa mwenyezimungu Ni Mmoja 2. Kuamini malaika wake 3.kuamini vitabu vyake 4.kuamini mitume wake 5. Kuamini kuwa kuna siku ya kiyama 6.kuamini kheri zake na shari zake pia 7. Kusali 8.kutoa zaka 9.kufunga saum

    Ndugu Rich, ukiangalia manabii wote vigezo hvyo walikuwa navyo hivyo basi walikuwa waislamu wenzetu, tofauti na nyie kigezo kikubwa cham tu kuwa mkiristo ni kubatizwa ingawa katika historia tunaona manabii wa mwanzo walikuwa hawabatizwi, sasa sijui walikuwa ni wakiristo wa namna gani.

    Ndugu Rich, swali lako lingine unauliza ni kwa nini mtume alipewa utume na pia akawa mtume bora kuliko wengine ili hali wao washapewa shera ambazo ni sawa na za kwake ?

    Ndugu Rich, kilichompa ubora juu ya mitume wote mtume Wetu Muhammad ni kwa sababu tu yeye ametumwa kwa ajili ya watu wote Duniani na siyo kwa ajili ya taifa moja tu, kama ilivyokuwa kwa watangulizi wake.Ndugu Rich,mtume alipewa jukumu kubwa kuliko manabii wote waliokuwa watangulizi wake, pia yeye amekuwa mtume na nabii wa mwisho wa Allah.
    Pia mtume alikuja kuondoa mafundisho yote ya uongo yaliyowekwa na waandishi wa uongo kuwa Yesu ni mungu aliyeuvaa mwili na wengine wakidai Yesu ni mwana wa mungu na ili hali mungu hana mtoto bali yeye ni muumbaji tu.maneno hayo tunasema ya uongo kwa sabbu bwana Yesu mwenyewe hakuwai kudai kuwa ni Mungu bali yeye mwenyewe alikuwa akimuomba Allah, na alifanya miujiza mingi kwa idhini ya Allah, ikiwemo kufufua wafu kwa idhini ya Allah, kupofua vipofu n.k lakini yote hayo kwa idhini ya Allah, lakini yeye hakuwa Mungu bali alikuwa mtume na nabii wa Mungu aliyepewa uwezo wa kufanya miujiza na Mungu mwenyewe.

    Ndugu Rich, uliuliza pia kama manabii wa mwanzo walitumwa kwa ajili ya Israeli iweje tena sisi waislam wengine tuseme sheria hizo hizo zinatuhusu ?

    Ndugu Rich, kutokana na kwamba wana wa israeli walipotosha maneno ya mungu kwa kutumia waandishi wao na kwa kuwatumia watu waliokuwa na elimu miongoni mwao hivyo sheria za mungu zikapotea,watu wakaiamini torati isiyo ya kweli na ile torati ya kweli ikatupwa pembeni kama tulivyoona kwenye YEREMIA 8 :8 hapo juu, Hivyo Allah aliamua amtume Mtume ili aje kuzifufua na kuzipa uhai sheria zake kwa mara nyingine tena katika kitabu cha quran, huku Allah akiapa kuwa atazilinda sheria alizoziteremsha ndani ya Quran na hakuna kiumbe chochote kitaweza kuzibadilisha kama walivyofanya huko mwanzo.Ndugu Rich, na ndiyo maana mtume alifundisha waislam kuhifadhi quran kwenye vifua vyao na ndio maana mpaka sasa hivi waislam tunahifadhi quran kichwani, na kwenye vifua vyetu hivyo mimi sehemu yoyote ninapokuwa naweza kuisoma quran kwa sura nilizohifadhi hata kama sina kitabu. Ingawa wapo wengine wamehifadhi quran yote kichwani, hivyo hakuna upotoshwaji tena wa neno la Allah kama ilivyokuwa mwanzo.

    Mwisho umezungumzia msimamo wa mchungaji Mosespk kuwa huo ni msimamo wake yeye binafsi na wala sio mtizamo wa kanisa au siyo mtizamo wa wakiristo wote pamoja na wewe ukiwemo, sasa ndugu Rich naomba unipe wewe msimamo wako, je sheria za agano la kale ambalo kwa mujibu wenu ndimo ilimo torati na zaburi, je zimebatilika baada ya Yesu kufa msalabani hivyo akaondoka na laana zake, au bado sheria hizo ziko hai na wakiristu wanazitii na kuzitumia kwa moyo wote.

    Ndugu Rich, kwa leo naomba niishie hapa ila kama hujaelewa unaweza kuendelea kuuliza tu, wala usijali kuona mimi pekee nimejitolea kuweza kuwasaidia wakiristo mliofanikiwa kutembelea blog hii, mimi naamini hata waislamu wengine wanasoma maneno haya na wengine wanaopata muda kadri Allah anavyowajalia wanatoa michango yao pia.

    Lakini pia Allah anatuambia ndani ya quran kuwa popote anapokuwa muislam mmoja mwenye imani kama anapambana na makafiri basi uwezo wake ni sawa na uwezo wa makafiri 100, sasa nyie wakiristo ninaojadiliana na nyie mpo watatu tu, kwa hiyo ile idadi aliyoisema Allah haijafika hata robo.

    Ndugu yangu nakushukuru, ila naomba wakati unajibu maswali haya pia ujibu na hoja zangu zinazothibitisha biblia inavyomdhalilisha Yesu, pengine hata mimi nitaweza kuelimika zaidi.

    Nakushukuru sana ndugu yangu.
    Wabillah tawfiq.

    Like

  207. Rich says:

    Kaka Mhamad, ni aibu kubwa sana kwako, pamoja na waislamu wenzio kuona kuwa, unajisifu kwamba, umeshindana na wakristo watatu ukiwa peke yako. Kwanza. Kwanza, sisi wakristo hatutakiwi kushindana na waislamu maana nyie na dini nyingine zote tulikwisha washinda miaka zaidi ya 2000 iliyopita kwa kifo cha bwana wetu yesu kristo pale msalabani. Lililobaki kwetu ni sisi kuwahubiria injili ya bwana yesu ili muungane na sisi tuje kuurithi uzima wa milele kwa pamoja tukiwa wote ni mmoja katika kristo yesu. Allah ndiye bado hajashinda wala hana uhakika wa mambo yake ndio maana anawafundisha nyie kushindana. Unasema kuwa Allah kakwambia kwamba hata waje wakristo 100 kwa wewe mmoja hawatakuweza. Sasa mimi naona ungemuuliza Allah kwamba, mbona mpaka sasa katika mijadala yako yote huko juu umepata sifuri !!. Pia ninakuona kuwa unafanya mchezo wa kujibu maswali yangu na kuchanganya hoja ambazo ulikwisha jibiwa huko juu. Mambo yote ya usahihi wa biblia na majibu ya maandiko yake kama ile (yeremia 8:8) tulikwisha kujibu vyema kabisa pamoja na kuyatolea ufafanuzi maandiko hayo jinsi yalivyo maanisha kwa ujumla wake. Sasa, kwanini unalazimisha ushindi wa majibu yako kwa kurudia mambo ya uongo ndugu yangu!!. Hilo ndilo tatizo lako kubwa ndugu yangu, yaani unajikaza kutetea dini yako mpaka unasahau huko nyuma ulikotoka.Hebu jaribu ku ‘come down’ ili twende vizuri na kuwafaidisha na wengine. Tazama mimi nilikuuliza kuwa, wewe ulituonyesha aya ya quran inayofundisha kuwa, sheria za nyuma za manabii waliopita, kazi yake ilikuwa ni kusadikisha wale wote waliokuwepo kabla ya mtume wenu mhamad, halafu quran ndiyo inasheria za muongozo kwa ajili ya watu wote hapa duniani kwa sasa. Ona (quran 3:al-imran). Sasa, mbona hapo juu umebadilika ndugu yangu, kwa kusema kuwa, sheria zilezile za manabii wa nyuma, ndizo hizo hizo tena mnazozitumia mpaka hivi sasa pasipo kubadilishwa kitu?,usichoke nijibu. pili nikuulize kuwa kama ni kweli ninyi waislamu mnafuata utaratibu wa sheria za manabii wa nyuma pasipo kubadilisha wala kuongeza jambo, hivi huo utaratibu wenu wa ibada ya kwenda kwenye kaburi la mtume wenu kule makkah na kuvaa shuka kama waganga wa kienyeji huku mkimpiga shetani asiyeonekana mawe, utaratibu huo mlipewa na nani katika ibada zenu maana wote sisi tunajua kuwa mambo hayo hayakufanywa na manabii wa nyuma kwenye ibada zao kwa kuwa nyakati zao hakukuwa na kaburi la mhamad. Usichoke nijibu. Mwisho ili nisikuchoshe ndugu yangu naomba tukubaliane kuwa, manabí wa zamani hawakuwa waislamu kama unavyo lazimisha wewe, kwa kuwa, ukitizama vile vigezo vinne vya kuwa muislamu kamili, basi utagundua kuwa, wao hawakuwa na kigezo kile cha kuiamini, kuifuata na kuitumia quran katika maisha yao. Pia hawamjui hata huyo mletaji wake (mhamad) kwa kuwa alikua hata kuzaliwa kwake bado!!!. Usichoke nijibu. Kuhusu mtazamo wangu katika sheria za Mungu katika torati na manabii ni kwamba, Bwana yesu hakuja kufuta na kuondoa sheria takatifu za Mungu, bali kutimiza kama Mungu mwenyewe alivyo mtabilia aje kufanya.KIVIPI ?!!….Mungu aliahidi zamani sana, kupitia nabii yeremia, hivi: ” NITATIA SHERIA YANGU NDANI YAO NA KATIKA MIOYO YAO NITAIANDIKA, NAMI NITAKUWA MUNGU WAO, NAO WATAKUMA WATU WANGU. Soma(Yeremia 31:31-34). Wakati wa Yehova umetufikia sasa, badala ya kushika sheria zake kwa mambo ya mwili na adhabu zake, kwa mf: kuwakata mikono waizi wanapo iba au kuwapiga mawe mpaka kufa wazinifu, Mungu mwenyewe ametimiza ahadi yake ya kutia sheria yake ndani ya mioyo yetu, na kuondoa utaratibu wa adhabu za mwili kama sheria zake takatifu zilivyokuwa zinadai matekelezo hayo yanayotakiwa kutekelezwa na viongozi waaminifu wa kidini . Mungu amefanya hivyo baada ya kuona kuwa ” hakuna muaminifu mwenye haki ya kumhukumu mwenzake hata mmoja!!…wote sisi tumeoza, tena tunadhabi, soma(zaburi 14:2,3). Kwa hiyo, sheria zote za Mungu, kama usiibe, usizini, usiue nk, zinafuatwa kwa njia ya rohoni….soma(rumi 8:4). Hali hiyo kamwe haiondoi wala kufuta sheria za Mungu bali inawezesha sheria hizo za Mungu kuitwa kutoka ndani ya nia ya mtu ikimuongoza kutenda mapenzi ya Mungu kwa asili yake ya rohoni, soma(rumi 7:14). Watu wakitii sheria kupitia roho zao, inakuwa inafanya kazi kama alama ya watu waliochaguliwa na Mungu. Hivyo basi, kwa kuwa sheria ya Mungu imo moyoni mwetu, tunajikuta tunajihukumu kwa kujikubali au kujikataa sisi wenyewe. Ndiyo maana biblia inatuambia ” ile imani uliyonayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu, heri mtu yule asiye jihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali, Soma(rumi 14:22). Kwa hali hiyo ya siri za zambi zetu rohoni mwetu, inakuwa wa kutuhukumu wa mwisho wa haki aliye muaminifu anakuwa ni Mungu pekee ambaye ni wa haki na mkamilifu. Soma(mathayo 12:36-37) Pia (Mhubiri 12:13-14)….Hapo ndiyo maana biblia inatuambia kuwa “KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE YEYE MWENYEWE MBELE ZA MUNGU. Soma(rumi 14:10-13). Ndugu mhamad, nimefafanua zaidi jibu langu ili watu wote wafaidike vizuri ili waachwe kuulizwa tena swali hilo na waislamu. Hebu sasa nakuomba umalizie kunijibu maswali yangu na hayo, ili nikitosheka, na mimi nikujibu ile hoja yako huko juu. Usiwe na wasiwasi ndugu kwa kuwa hiyo hoja yako kamwe sitaiacha na wala haitapotea. Mtu ambae anachelewesha mambo ni wewe mwenyewe kwa kuwa huwa unajibu maswali kwa kushindana mno…badala ya kujibu kitu ulichoulizwa moja kwa moja kwa ufasaha, wewe unaanza kuchanganya humo humo na mahoja yasiyo husika na ambayo tayari yaliyokwisha jibiwa huko juu!!. Haya kaka uwanja ni wako sasa, karibu tuendelee…..

    Like

  208. Rich says:

    ndugu mhamad, siku zote unaposikia au kuona maandiko ya mitume katika biblia yanasema ‘yesu ni mwisho wa sheria au wakristo atufuati sheria au wakristo hatupo chini ya sheria au wakristo atuishi kwa sheria…basi ujue maana yake ni kwa jinsi kama nilivyoelezea hapo juu, kuwa sheria za Mungu zinafuatwa kwa njia ya rohoni na kamwe sio katika matendo ya mwili tena eti ili tuifanye na kuipata haki ya Mungu kwa njia hiyo ya mwili, hakika haitawezekana kufikia viwango vya haki vya Mungu kwa kuwa sisi sio wakamilifu kama nilivyo onyesha kwenye ile (zaburi 14:2-3). Ijapokuwa uwelewa wa watu na mawazo yake yanaweza tofautiana lakini mimi ninaamini hivi kwa 100%.

    Like

  209. Rich says:

    Kaka Mhamad, pole sana, kwa kuwa nilichogundua hapo ni ugumu wa hayo maswali niliouliza ndiyo yanayo kufanya ushindwe kujitokeza!!. Nimeyatazama na mimi, nikayaona, kwakweli hakuna Muislamu yeyote atakae jaribu kuyajibu!!. Sasa, mimi nakupa onyo kuwa, usije tena kwenye blog yetu hii, mpaka umehakikisha umekuja na majibu yetu sisi wakristo!!. Na kwa kuwa nilikuahidi kukujibu ile hoja yako uliyo itoa huko juu, basi naomba nitimize ahadi yangu sasa hivi. Ndugu mhamad, katika ile ( luka 4:1) ulishutumu kuwa, bwana yesu alionekana kuwa na urafiki wa kuongea na ibilisi baada ya ibilisi huyo, kumnyakua na kwenda nae jangwani!!. SIOKWELI. Ndugu mhamad, shetani kwa asili yake, hana rafiki, kwa kuwa, yeye ni mpingaji na muuaji. Pia, shetani sio jijitu linalotisha na lenye mapembe, linaloweza kukaa na mtu au kumnyakua mtu, HAPANA!!, Ila shetani ni kiumbe wa roho (roho ovu) isiyo onekana inayotushawishi tufanye mambo ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu wetu, halafu tukishamsikiliza yeye madanganyo yake, anakwenda mbele za Mungu kutushtaki kuwa tumetenda kinyume na mapenzi ya Mungu, ndio maana biblia inatuambia “mshtaki wenu ibilisi kama simba angurumae, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze” ,soma(1petro 5:8). Sasa, kwa kuwa Mungu ni mwenye haki, hawezi kumnyima shetani haki yake ya kutushtaki sisi, kwa kuwa, ni kweli sisi tumetenda kinyume na mapenzi ya Mungu, ndiyo maana biblia inasema “MSIMPE IBILISI NAFASI”, Soma(waefeso 4:27). Shetani ni Baba wa uongo, Yeye alifanikiwa hata kumwambia Hawa, uongo, ndio maana, jina lake jingine anaitwa “LILE JOKA LA ZAMANI !!. Soma(ufunuo 20:2-3). Mungu kupitia simulizi za biblia, alikuwa akiwatumia manabii wake katika majaribu yao, yaliyo wapata katika maisha yao, ili kutufundisha sisi, tujue jinsi ya kuishi kwa kumtegemea yeye peke yake, bila ya kusikiliza sauti ya mshauri mmbaya ibilisi. Soma(Ayubu 1:9-11). Hii ndiyo maana hata hivi leo, Mungu anaruhusu majaribu na matatizo yatupate sisi ili tuwe na nguvu ya kumtegemea yeye pekee. Sasa, bwana Yesu akiwa ndiye kuhani wetu mkuu mbele za Mungu, alikuwa anatufundisha jinsi ya kuyashinda majaribu ya ibilisi, kupitia maisha yake aliyoishi hapa duniani, ndiyo maana, baada ya kumshinda ibilisi yule, alimwambia “NENDA ZAKO SHETANI, KWA MAANA IMEANDIKWA, MSUJUDIE BWANA MUNGU WAKO, UMWABUDU YEYE PEKE YAKE”, Soma(Mathayo 4:10). Baada ya hapo, Biblia inadhihirisha ushindi wa bwana yesu kwa kusema “KISHA SHETANI AKAMUACHA !!!,Soma(Mathayo 4:11). Mungu alimtumia bwana yesu kwa njia za rohoni ili aje kuzivunja nguvu za shetani kwa ajili yetu, ili sisi wote tupate kukombolewa kupitia kristo yesu. Biblia inasema hivi: “ATENDAYE DHAMBI NI WA IBILISI, KWA KUWA, IBILISI HUTENDA DHAMBI TANGU MWANZO, KWA KUSUDI HILI MWANA WA MUNGU ALIDHIHILISHWA ILI AZIVUNJE KAZI ZA IBILISI”, Soma(1Yohana 3:8)……..Sasa, ndugu mhamad yohn, hebu tuje kwenye ile (Yohana 10:8) Uliyodai kuwa, bwana yesu alisema “wote walionitangulia ni wevi na wanyan’ganyi !!. Je, hebu tujiulize kuwa, hao ni manabii wetu wa nyuma, yaani wakina Musa,isaya, Daudi nk?!!!. Jibu ni HAPANA. Kwanza hapo inatupasa kujiuliza kuwa, iweje tena, eti manabii ambao ndio walio mtabiri na kumuandika bwana yesu katika vitabu vyao, eti halafu bwana yesu aje kuwaita wevi na wanyan’ganyi?!!, inawezekana kweli jambo hilo?, kwa mfano: Bwana yesu aliwaambia wayahudi hivi: “KWA MAANA KAMA MNGALIMWAMINI MUSA, MNGENIAMINI MIMI PIA, KWA SABABU YEYE ALIANDIKA HABARI ZANGU, LAKINI MSIPO YAAMINI MAANDIKO YAKE, MTAAMINI VIPI MANENO YANGU?, Soma(Yohana 5:46-47). Istoshe, Bwana yesu, pia, alisisitiza kuwa, yale yote anayo yatimiza aliandikiwa kutoka katika vitabu vya torati ya Musa+Zaburi na manabii, Soma(Luka 24:44), Sasa tujiulize kuwa, iweje tena, eti bwana yesu aanze tena kuwaita, manabii wake hao, waizi na wanyan’ganyi?!!, jibu ni “HAPANA HAIWEZEKANI. Kivipi haiwezekani?,……..jibu lake sahihi ni kuwa, Bwana yesu, alitufundisha, kigezo cha kuwajua, hao wachungaji wevi na wanyanganyi. Ukirudi nyuma ya hilo andiko, katika ile (Yohana 10:1), Bwana yesu anasema “Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo “HUYO NI MWIVI, NAYE NI MNYANG,ANYI,!!. Sasa, kwa kigezo hicho cha bwana yesu, utatambua kuwa, manabii wote waaminifu, hawahusiki kwa kuwa, wao, walitembea katika njia ya Mungu, huku wakichunga vyema kondoo wa zizi, mfano: Musa na israel, kuwatoa misri mpaka jangwani israel. Hekima na tabiri za wakina isaya, Daudi,yeremia nk. katika kuongoza kwao vyema na kumtabiri kristo. Pale, Bwana yesu, alikuwa akimaanisha wale wachungaji wote walio mtangulia, na ambao walikwenda kinyume cha ile kweli yake, na kushindwa kuwachunga kondoo, kwa kuwa hata kondoo wenyewe walikataa kusikiliza na hatimaye, kutawanyika, Soma(Yohana 10:5). Lakini, kamwe haitoshi, ni lazima tuwajue, hao, wachungaji waliokuwa wanapinga neno la kweli na kuchunga vibaya kondoo wa bwana.Wachungaji hao wabaya katika injili ni hawa hapa: Waeseni, Wazerati, Wafesayo, Pamoja na Masadukayo wasioamini hata habari za ufufuo. Ukiisoma injili vizuri, utaona kuwa, makundi hayo pamoja na baadhi ya mafarisayo, kazi yao kubwa ilikuwa ni kumpinga bwana yesu kila alichokuwa anasema, wakati wote. Mafarisayo wakati fulani, walimuuliza bwana yesu hivi:”mbona wanafunzi wako wanakula mikate siku ya sabato bwana?, bwana yesu akawajibu “MIMI NDIMI BWANA WA SABATO. Katika vitabu vya agano la kale, unaweza kuwaona wachungaji wevi na wanyan’ganyi kwa kusoma( ezekie 34:1-20)….. Ndugu mhamad, Pia nijibu hoja zako nyingine kwa pamoja kutokana na kufanana kwake. Nijibu kwa kusema kuwa, Bwana yesu alikuwa akiwaita wayahudi: KIZAZI CHA ZINAA, KIZAZI CHA NYOKA, KIZAZI KISICHOAMINI NK, Kwa kuwa wayahudi walikuwa, wakimpinga na kumkataa bwana yesu, wakati wote, hata kufikia hatua ya mwisho ya kumuua kwa kumsulubisha pale msalabani, pasipo sababu yoyote ya msingi, zaidi ya masingizio matupu!!!. Wayahudi walikuwa hawamuheshimu, hawampendi wala kumkubali kuwa ndiye mesiya aliye ahidiwa na Mungu kwao. Wao, walifikia hata hatua ya kumwambia “UNAPEPO WEWE!!, Lakini tunamuona bwana yesu kwa upole kabisa akiwajibu hivi: “MIMI SINA PEPO, LAKINI MIMI NAMHESHIMU BABA YANGU, NINYI MWANIVUNJIA HESHIMA YANGU!!!. Soma(Yohana 8:49). Lakini pia, ni kweli kabisa, na wala sio matusi kuwa, Yeyote anaempinga na kumkataa bwana yesu, basi anakuwa ni mtoto wa shetani, yaani anakuwa “kizazi cha nyoka, na hivyo, kustahili zile sifa mbaya zote alizozitoa bwana yesu, kwa kuwa, tukisoma vitabu vya mwanzo, tunaona jisi shetni alivyo mdanganya ” Hawa” Yule Mama yetu wa mwanzo, Soma(Mwanzo 3:13-15). Katika maongezi hayo na mafundisho yake hayo bwana yesu, sio kweli kuwa sisi wakristo tunahusika kwa kuwa, wakati ule, hakukuwa bado na wakristo wa mataifa ila bwana yesu alikuwa akiongea na wayahudi pekee. Na kuhusu wale baadhi ya wanafunzi wake bwana yesu aliokuwa akiwakemea, hayo ni mambo ya kawaida kabisa, kwa wanafunzi wale kukosea na kukemewa, hakuna mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke alafu eti awe mkamilifu pasipo kukosea wakati fulani, Soma(zaburi 51:4-5). Ndugu mhamad, nimalizie na ile (mathayo 7:6), Wakristo kuitwa ngurue na bwana yesu. SIO KWELI.,…..Alipokuwa akiwatuma wanafunzi wake kuihubiri injili, bwana yesu aliwaagiza hivi: “NA MTU ASIPOWAKARIBISHA WALA KUYASIKILIZA MANENO YENU, MTOKAPO KATIKA NYUMBA ILE AU MJI ULE, KUNG’UTENI MAVUMBI YA MIGUU YENU. Soma(Mathayo 10:14). Bwana yesu hakupenda kabisa injili yake kupokewa na watu wasio na imani thabiti na mioyo isiyo ya unyenyekevu. Bwana yesu alitumia maneno, mbwa, ngurue nk, katika injili yake, ili kuonyesha jinsi asivyopend mtu kuhubiriwa injili yake halafu mtu huyo badala ya kuiamini na kuipokea kwa moyo mnyenyekevu, Yeye anaanza kuikashifu na kuidharau kama mnavyofanya ninyi waislamu. yeye alikuwa analielezea jambo hilo kupitia mifano na mafumbo mbalimbali. Kwa mfano, Pale aliposema” msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya ngurue wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao wakageuka na kuwararua. Soma(mathayo 7:6). Hapo bwana yesu, mfano wake huo ulikuwa unamaanisha kuwa kwa sababu wakati wa kuwahubiria injili watu wa mataifa ulikuwa bado, basi ni lazima wahubiriwe injili wayahudi kwanza kabla ya kuwahubiria watu wa mataifa kwa kuwa, kwasababu kwa kutokuelewa kwao watu wa mataifa, basi wanaweza pia kuidharau injili yake. soma(mathayo 10:5-7). Lakini unaweza pia kuona mfano wa yule mama asiye myahudi ambaye binti yake alikuwa na mapepo. Bwana yesu alimwambia”siwezi kukitoa chakula cha watoto na kuwapa mbwa. Lakini yule mama akamjibu kwa unyenyekevu bwana yesu “naam bwana lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto. Bwana yesu baada ya kusikia imani kubwa ya yule mama akamponya binti wa yule mama kwa kumwambia “kwa sababu ya neno hilo, nenda zako binti yako amepöna!!.unyenyekevu na imani ya kweli ndio kitu muhimu kilichokua muhimu mno mbele za bwana yesu. (marko 7:26-29). Mwisho.

    Like

  210. Rich says:

    Ndugu waislamu, ndugu yenu ameingia mitini baada ya kuona mambo ni magumu!!!. Naomba ajitokeze mwalimu mwengine wa kiislamu ili asaidie kutoa msaada, lakini itampasa ajibu kwanza hayo maswali yangu matatu kwanza. Nilazima mjadala wetu uanzie katika hayo maswali. Karibuni isipokuwa viwango vya ufahamu vya kitoto pamoja na kurudia mambo yaliyokwisha tolewa majibu sihitaji.

    Like

  211. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Rich,
    Nakupongeza sana kwa tabia yako ya kupenda kuwa mdadisi wa mambo kama ulivojiita mwenyewe ingawa mimi naona kuwa hiyo ni tabia nzuri kabisa inayostahili kuigwa na siyo tabia mbaya kama ulivyoainisha wewe.

    Ndugu Rich,naomba nikunukuu halafu nikupe majibu ya msingi;
    “ Hebu hata ukipitia hoja zako huko juu, wewe ulitoa mpaka aya inayoelezea kuwa, Allah aliteremsha sheria za kale kupitia manabii ili kusadikisha waliokuwa mwanzo kabla ya Muhamad halafu akateremsha quran iwe muongozo kwa watu wote, lakini chakusikitisha ni kwamba hapo juu umepingana tena na kitabu chako cha muongozo kwa kusema kuwa sheria na muongozo uleule wa nyuma wa manabii ndio huo huo mnao utumia hivi sasa pasipo kubadilisha sheria yoyote”
    Ndugu Rich, pamoja na udadisi na uchunguzi wako mzuri lakini nafikiri hujaelewa nini maana ya neno kusadikisha , hebu ndugu yangu kama unajua maana ya neno kusadikisha naomba uniambie.nina imani 100% kwa jinsi ulivyouliza swali hili hujui nini maana ya neno kusadikisha.

    Ndugu Rich, kusadikisha ni neno la kiarabu ambalo mzizi wake ni sadqi yaaani ukweli, ndugu Rich, hata tunaposoma katika vitabu vinavyozungumzia maisha ya Mtume kabla hajawa Mtume wa Allah tunaona kuwa watu walimuita jina la utani yaani nick name ya “assadiq al-amin” yaani mkweli mwaminifu,hivyo pia kuna neno as-siddiq pia ambalo maana yake ni mkweli na katika quran katika aya niliyoiweka aya ya 3 katika surat imran imeandikwa hivi kwa kiarabu “mussaddiqa llimaa baina yadaih” yaani “kusadikisha yaliyokuwa kabla yake” ndugu Rich,hapo limetumika neno ” mussaddiqa”yaani kusadikisha ambayo maana yake ni “kuthibitisha ukweli” au kuyakinisha ukweli, yaani kwa maana nyingine kama jambo lilikuwa kweli halafu kweli yake ikapotea sasa linathibitishwa kuwa lilikuwa kweli , hivyo ndiyo maana ya kusadikisha na neno hilo “mussaddiqa” limetumika mara nyingi ndani ya quran likionesha kuwa quran inasadikisha yaliyopita kabla yake ndani ya torati, na injili, na pia kuna sehemu ndani ya quran neno kusadikisha limetumika kuonesha injili inasadikisha yaliyokuwa kabla yake katika torati.

    Ndugu Rich, kwa kuwa maana ya kweli ya neno kusadikisha kama ilivyotumika katika iyo aya ya quran, ikionesha kuwa quran inasadikisha yaliyopita kabla yake katika torati na injili, maana yake ni kwamba quran inathibitisha ukweli, au maana yake inayakinisha ukweli wa vitabu vilivyotangulia vya taurati na injili kwa mayahudi ambao walikuwa hawamuamini Mtume kwa sababu walidhani alikuwa na dini ya uongo yenye sheria mpya tofauti na zile walizonazo za manabii waliotangulia, vivyo hivyo injili inathibitisha ukweli wa taurat kama quran inavyotwambia pia.
    Ndugu Rich, ni lazima basi tuangalie ni nini maana ya kuthibitisha ukweli wa torat, na injili je maana yake ni kwamba hiyo ni sheria mpya na sheria iliyotofauti? Ndugu Rich hata kwa akili yako naamini utakubaliana na mimi kuwa sheria ambayo ni tofauti na sheria ya mwanzo haiwezi na kamwe haiwezi kuthibitisha kweli ya sheria iliyoitangulia, hivyo basi kama quran inathibitisha ukweli wa sheria zilizotnagulia ni lazima sheria hizo zote zifanane.chukulia hata katika mazingira ya kesi mathalan, ushahidi wa kwanza ukiendana sawa na ushahidi wa mtu mwingine ambaye hakuwepo wakati shahidi wa kwanza akitoa ushahidi wake, basi maana yake huwa tunasema huyu shahidi wa pili amethibitisha ukweli wa shahidi aliyetangulia, kwa kuwa wote kauli zao hazikupishana lakini wakitofautiana kauli kama biblia agano la kale linatofautiana na agano jipya hivyo kuna mkanganyiko, huwezi sema huyu amemsadikisha shahidi aliyetangulia, kwani wanakuwa wametofautiana.Hivyo basi kufanya shaidi mmoja kuwa muongo au wote wawili, vivo hivyo na kwa biblia agano la kale tofauti na agano jipya hivyo lazima agano moja la uongo au yote mawili ya uongo.

    Ndugu Rich, lakini pia utauliza swali ni kwa nini basi quran ithibitishe ukweli wa vitabu vya mwanzo? Ndugu Rich quran imepewa jukumu la kuthibitisha ukweli wa vitabu vya mwanzo mara baada ya ukweli huo kupotoshwa na manabii wa uongo waliotangulia kama akina Paulo n.k, hivyo watu wakawa wanaukimbia ukweli wa torati na injili ya kweli ya Bwana Yesu, watu wakawa hawazitaki tena sheria za Allah na wanakumbatia maneno ya manabii wa uongo wanaodai eti sheria hizo zimefutika, kwa hiyo Allah akatuletea quran ili kuthibitisha kuwa kweli bado sheria hizo zipo na hazijafutwa kama baadhi ya watu wanavyodanganywa na manabii wa uongo, na wavivu kufuata sheria za Allah kwa kisingizio eti zimefutwa na ilihali kwenye vitabu vyao bado zimo.

    Ndugu Rich, tofauti na upande wa biblia kwa maana tumeona agano jipya haisadikishi agano la kale, badala yake agano jipya inabatilisha agano la kale na kufanya neno la mungu wa agano la kale kubatilika na kuwa halina maana tena kwa ulimwengu wa sasa.sheria na amri za agano jipya zinapingana kabisa na sheria za agano la kale hivyo kukosa sifa ya kusadikisha.Ndugu Rich, kutofautiana kwa yehova katika maagano hayo mawili inatutia mashaka sana kwani inaonesha kabisa huyu yehova mungu wa Israel, mungu wa yakobo alikuwa kabisa hana uhakika na anachokifanya, hii inaonesha kabisa mungu wenu yahwe alikuwa anababaika sana,mara leo kasema sheria flani inafaa lakini leo anabadilika anasema haifai, yaani alikuwa anababaika babaika tu, huku hayuko wala kule hayuko kitu ambacho kinatuthibitishia kabisa kuwa huyo yehova hakuwa na wala hatakuwa Mungu wa kweli.

    Ndugu Rich, nikikunukuu hoja yako nyingine umesema :
    “Mungu mwenyewe ametimiza ahadi yake ya kutia sheria yake ndani ya mioyo yetu, na kuondoa utaratibu wa adhabu za mwili kama sheria zake takatifu zilivyokuwa zinadai matekelezo hayo yanayotakiwa kutekelezwa na viongozi waaminifu wa kidini”

    Ndugu Rich, hapo ndipo nilipopataka ndug yangu, ina maana Mungu wenu yahwe alipoona sheria zake hazifai kutekelezwa kama ilivyokuwa mwanzo akaamua kuondoka nazo kwa kufa kifo cha laana pale msalabani, kwa hiyo unachokimaanisha ni kwamba katka biblia ambayo unaenda nayo kila siku kanisani ndani yake kuna sheria ambazo hazitakiwa kabisa kufuatwa, na zilishapitwa na wakati na zimekwisha batilika.

    Lakini pia ndugu Rich, umesema sheria hizo zilitakiwa kutekelezwa na viongozi wa dini wenye uaminifu, kwa hiyo ndugu Rich unamaanisha zamani za agano la kale walikuwepo viongozi waaminifu ila sasa hivi zama za agano jipya viongozi waaminifu hakuna.Duh huu ni msiba na ni aibu kubwa kwa wakiristo.

    Lakini pia umesema mungu wenu mwenyewe ameitimiza sheria yake ndani ya mioyo yenu kwa hivyo hakuna tena sheria kama kuiba ukakatwa mkono, je mungu huyo yehova alishindwa nini kuitimiza sheria hiyo mioyoni mwa watu toka mwanzo ili sheria kama hizo zisiwepo za watu kukatwa mikono? Kwa nini sasa yehova anakosa msimamo leo anasema hivi na kesho anabadili kauli?sasa hiyo si dalili ya uongo wa yehova?

    Ndugu Rich, pia umetoa hoja ya kwenda makka kuhiji lakini ukaipresent kwa uongo eti sisi huwa tunavaa nguo nyeusi, ndugu yangu huo ni uongo uliopitiliza,unahubiri injili ya uongo kwa kutumia uongo, Ndugu Rich, kule makka waislam huwa tunavaa nguo nyeupe, na Mtume Muhammad alisema vaeni nguo nyeupe kwa maana hilo ndilo vazi la peponi sasa vp ndugu yangu useme sisi tunavaa nguo nyeusi, kwanza naomba utuombe radhi kwa hilo.

    Lakini pia kuna swala la kupiga shetani mawe, kweli hilo lipo na hicho ni kiashirio kuonesha ni jinsi gani waumini wa kiislam wanatakiwa kumchukia shetani popote alipo, na wala haimanishi kwamba ndo shetani anaonekana pale ingawa wewe umepingana na biblia yako kwa sababu wewe unaamini shetani haonekani, lakini yesu mbona anaamini shetani anaonekana, tena mmojawapo wa mashetani ni Petro? Sasa vip ndug yangu hata biblia yako unashindwa kuisoma ukaelewa?

    Lakini pia umesema manabii wa zamani walikuwa hawaendi kufanya hija kwa hiyo sisi waislam tumeleta sheria mpya ya kwenda kuhiji, sasa kama hivyo ndivyo ilivyo ni kwa nini nyie wakiristo tunaona siku hizi na nyie mnaenda kuhiji katika ardhi ya kiislam kule yerusalem nchi ya palestina alikozaliwa nabii Yesu?

    Lakini pia kwa kuthibitisha kuwa unahubiri injili ya uongo kwa kusema uongo, umesema uongo eti tunaenda kwenye kaburi la Mtume kule makka, Ndugu Rich, hiyo siyo kweli ndug yangu, hatuendi kuzulu kaburi la mtume na hayo ni makosa makubwa mno kwenye uislam kwenda kwenye kaburi la mtume kuomba, hiyo ni shiriki kubwa mno na wala hakuna muislam anayefanya hivyo na Mtume mwenyewe alishakataza hata kabla hajafa swala la watu kwenda kuomba kwenye kaburi lake, ashakataza kabisa na ni dhambi kubwa kufanya hivyo.

    Ndugu Rich, katika quran kuna aya nyingi mno ambazo Allah ametumia neno kusadikisha na hizi ni baadhi tu ya aya lakini sehemu nyingi mno limetumika neno hili.Hizi hapa chini ni baadhi tu

    SURA 5. SURAT AL MAIDA
    46. Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake
    katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo
    sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa
    wachamungu.

    Kwa hiyo ndugu yangu Rich, maana ya neno kusadikisha ni kuthibitisha ukweli wa sheria za Mungu kwa watu wajue kuwa sheria walizonazo ni kweli ni sawa na zile alizokuja nazo Mtume Muhammad, na siyo maana yake eti ni kuleta sheria mpya, Tena Allah, anasema katika sura Yunus,

    SURA 10. SURAT YUNUS
    37. Na haiwezekani Qur’ani hii kuwa imetungwa na haitoki kwa Mwenyezi Mungu.
    Lakini hii inasadikisha yaliyo tangulia, na ni mfafanuo wa Kitabu kisicho na
    shaka ndani yake, kutokana na Mola Mlezi wa viumbe vyote.

    Ndugu Rich, Allah mwenyewe amekupa jibu hapo juu kwenye surat Yunus, kuwa haiwezekani quran iseme uwongo na ili hali inasadikisha yaliyokuwa kabla yake, yaani inawathibitishia kabisa wana wa israeli kuwa hayo waliyokuwa nayo katika t0rat na injili ni sawa kabisa na yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad.

    Mwisho kabisa ndugu Rich, sioni kama ulitakiwa kumpinga Mch. Mosespk kwa sababu hata wewe bado unaendelea kubeba biblia ambayo ndani yake kuna sheria ambazo unaamini zilibatilishwa na yahwe, hivyo kufanya na imani yako iwe batili, pili hiyo inathibitisha kabisa kwamba manabii wa zamani walikuwa siyo wakiristo bali walikuwa waislam kwa sababu sheria walizopewa na Mungu nyie kwenu wakiristo ni batili na wakati sheria hizo ni sawa na sheria walizopewa waislam katika quran, hivyo ndiyo maana mnatuonea wivu sisi ambao sheria zetu zinafanana na sheria za manabii waliopita, hivyo ni wazi kabisa ukiristo ni dini mpya,na dini iliyojengwa kwenye misingi ya shetani Petro na dini ya uongo, na uislam ni Dini kongwe na dini ya manabii wote wa zamani wa Mungu akiwemo Nabii Yesu mwenyewe.

    Allah akupe mwanga uingie katika nuru ya Uislamu ndugu Rich.

    Wabillah tawfiq
    Wahaadha ssalaam.

    Like

  212. Muhammad Yohana says:

    Ndugu Rich,
    Siyo kwamba nilikukimbia ndugu yangu ila nilisubiri kwanza ujibu hoja za biblia kumdhalilisha yesu halafu ndo niendelee na mjadala.

    Like

  213. Rich says:

    Ndugu mhamad, kwanza nikushukuru kwa kupata ujasiri wa kurudi uwanjani. kwakweli ninamuomba Mungu akupe nguvu zaidi ili tuendelee kuwafaidisha na wengine wasije wakakalia njia za mauti pasipo kujijua kwa sababu ya watu wachache wanaokazana kupindisha ile kweli ya Mungu. Kwanza mimi hebu nianze na lile swali langu ulilolikwepa bila ya kulijibu kabisa!!. Wewe ulituambia kuwa Manabii wote wa nyuma walikuwa ni waislamu. Halafu ukanipa vigezo vya mtu kuwa muislamu kuwa ni pamoja na kuviamini vile vitabu vya torati, zaburi, injili pamoja na quran. Kwanza kabisa unaweza kugundua kuwa, nyinyi waislamu wote, sio wanyenyekevu wa kweli mbele za Mungu kwa kuwa ninyi siku zote mnakikataa hicho kigezo cha kuiamini injili ya bwana yesu kwa kisingizio kuwa bwana yesu alitumwa kwa ajili ya taifa la israel pekee, hivyo mnadai kuwa, injili haiwahusu ninyi. Pia mimi niliuliza kuwa, kama ni kweli kuwa, manabii wa zamani walikuwa waislamu wenzenu, mbona tena, hawana hicho kigezo cha kuiamini, kuifuata na kuitumia quran?, kwa kuwa, nyakati zile za nyuma hakukua na kitabu hicho, wala nguzo zake hizo za kumfanya mtu awe muislamu wa kweli… Muhamad mtume wenu, bado alikuwa hajazaliwa ili kuwaletea nguzo hiyo wanadamu, ndio maana hata quran inawaita manabii wa nyuma “watu wa kitabu” .Iweje sasa, ninyi waislamu wa leo, mseme kuwa, manabii wale wa nyuma walikuwa ni waislamu kama ninyi, na wakati wao hawakuwa na kigezo hicho muhimu cha kuwa muislamu?, inamaana hata wanadamu wa leo, wanaweza kuwa ni waislamu bila ya kuifuata na kuiamini quran kama walivyokuwa wale manabii wa nyuma?!!. pia, ndugu mhamad, kusadikisha ni kuthibitisha ukweli kwa kuwaaminisha hao wanaotakiwa waamini. Mimi sitaki tubishane kwa jambo la kitoto hapa, lakini ninataka niende kama wewe unavyotaka ili ukweli ubaki kuwa wazi vilevile. Ndugu mhamad, nyie waislamu siku zote, ndio mnaosema kuwa, torati, zaburi na injili, ni vitabu vilivyo chafuliwa na wayahudi, tena havifai kwa imani!!. Sasa, mbona tena, unaanza kubadilika kuwasingizia manabii wasiojulikana kuwa ndio waliosema kuwa vitabu hivyo vimechafuliwa!!. Kwa hiyo, unataka kuanza kukubali tena, kuwa torati, zaburi na injili ni vitabu sahii visivyo badilishwa wala kuchafuliwa kutokana na hiyo kazi ya Allah aliyoifanya ya kuwasadikisha na kuwahakikishia wayahudi kuwa vitabu vyao ni sahihi kabisa??. Pia, kama ni kweli Allah aliwasadikisha wayahudi kuwa vitabu vyao ni sahihi, huoni kuwa, huyo mtume wenu mhamad atakuwa ni baadhi ya hao manabii wa uongo waliokuja kusema kuwa, vitabu vya manabii wa kale havifai tena kwa imani, kwa kuwa vimeharibiwa!!. Nyie waislamu mnasema kuwa, vitabu vyote vya injili, torati na zaburi, vimeharibiwa na wayahudi wenyewe na sio sahihi tena kwa imani. lakini kumbe AIIah alikwisha vithibitisha mbele ya wayahudi kuwa vitabu hivyo bado ni sahihi kabisa. Lakini kwa kuwa ninyi waislamu hammwamini Mungu wenu Allah, Mkaamua kuwasikiliza wale manabii wa uongo wanaopotosha kuwa vitabu hivyo havifai kwa muongozo!!. Kwanza ninyi, adui wenu mkubwa mnaesema kua ndie aliyebadilisha vitabu vya kale ni Paulo, lakini jambo la ajabu ni kwamba, kipindi kile ambacho, Allah anathibitisha kwa wayahudi usahihi wa vitabu vya torati, zaburi pamoja na injili, Yule mtume Paulo mnae msingizia kua amechafua na kubadilisha vitabu hivyo, alikuwa amekwisha kufa zaidi ya miaka 400 iliyopita!!!!. Na hapo ndipo mtu anapoweza kugundua uongo wa waislamu kuwa, kumbe hata historia ya hizi dini na watu wake, wao hawajui….ndio maana huwa wanatuletea hoja za kitoto sisi wakristo na kuwapotosha wale wajinga wote wanaofuata dini kwa mapokeo na mazoea kutoka kwa wazazi wao!!!. Jamani ndugu zangu waislamu wote, tusipende kutetea dini, bali tupende kutetea neno la Mungu kwa kuwa manabii waongo wa zamani, walikuwa wanapenda kutetea dini zao sana, lakini sisi warithi wa maandiko ni lazima tukae pamoja ili kutafuta neno la kweli la Mungu wetu, pamoja na njia zake. Acheni kurithi ujinga wa dini bali tafuteni kurithi neno la Mungu la kweli. Hebu jitazame ndugu mhamad unavyosema, ngoja na mimi nikunukuu, eti “HIVYO NI LAZIMA AGANO MOJA LA UONGO AU YOTE MAWILI YA UONGO”. Kauli hiyo ni kauli ya mtu asie na uhakika na kile anachosema, kuwa ni agano lipi la wakristo ni sahihi?, lile jipya au lile la kale? Au yote hayafai?…..lakini jambo la ajabu hapo ni kuwa, nyie waislamu kupitia wayahudi walewale mnaowaambia kuwa walibadilisha maagano hayo, ndiyo haohao Mungu wenu Allah alikuja kuwathibitishia kuwa maagano yao ni sahihi, wasipotoshwe tena na manabii wa ungo ila waendelee kuviamini vitabu vyote vile vya Mungu!!!. Hivyo, hapo unaweza kupata jibu kuwa kwa mujibu wa maneno ya Allah, Muhamad mtume wenu ndiye nabii wa uongo na mpotoshaji. Hoja nyingine uliyojitetea kuhusu waislamu kuvaa shuka nyeupe na sio shuka nyeusi kama nilivyosema, oky…mimi nawaomba mnisamehe kwa mimi kubadilisha hiyo rangi pekee. Lakini ukweli utasimama pale pale kizazi mpaka kizazi kuwa, kwenda makkah kuhiji ni moja ya nguzo muhimu mno kwa waislamu, tena ni lazima kabisa kwa waislamu wote, kwa kuwa ni nguzo ya kidini au tuseme kuwa ni moja ya sheria kuu ya Allah aliyoiagiza na kuipasisha kabisa kabisa kwenye kitabu chake cha muongozo cha quran, huku mkijitamba kuwa mnafuata sheria na nguzo zilezile za manabii wa nyuma bila ya kuongeza kitu au utaratibu wowote!!!. Hebu ndugu yangu, hapa jaribu kujitetea kama mtu uliyekwenda shule, kama umeshindwa basi liache hili swali. Wewe badala ya kujibu swali kulingana na dini yako, unaanza tena kujibu kwa kujilinganisha na wakristo, kwa nini dini yenu haiwezi kujitetea yenyewe eti mpaka ilalie na kujilinganisha na ukristo!!!. Kwanza hizo hija za wakristo ni hija za ki hiari pekee, sio hija za lazima ndio maana hata mimi mwenyewe sijawahi kwenda na wala sina mipango ya kwenda kwa kuwa, hayo ni mambo ya hiari tu, hakuna ulazima wowote wa Mungu wetu Yehova, eti atulazimishe kwenye biblia kuwa ni moja ya sheria yake, umeona wapi sheria hiyo kwenye biblia kama mlivyo amrishwa nyie na Mungu wenu Allah!!!!. Sisi wakristo hata ukitushtaki, haileti maana kwa kuwa neno la Mungu halija lazimisha hivyo, tena wala halina mambo hayo katika sheria na muongozo wake, lakini wewe muislamu utawezaje kujitetea kuwa, hamjabadilisha sheria za manabii waliopita na miongozo yake na wakati ushahidi mnao katika hizo sheria zenu mpya za hija ya mtume wenu mhamad katika quran!!!!. Amkeni ndugu, acheni mambo ya zamani. Hii leo, waarabu wenyewe wanakuwa wakristo kila wakati huko kwao, sembuse ninyi mlioletewa tu, dini hiyo!!. Sio kwamba nawalazimisha ila nawaeleza ukweli ulio hata mioyoni mwenu ninyi wenyewe. Nimalizie na lawama zako katika ule mtazamo wangu niliotoa. Umejaribu kupinga na kutafsiri vitu ambavyo hata mimi sivijui wala sijavielezea!!. Nianze kukujibu kuwa, Zamani za kale kulikuwepo na viongozi walio waaminifu kabisa, lakini ukamilifu wao na uaminifu wao, haukuweza kufikia vile viwango vya mwisho vya haki mbele za Mungu, na Mungu yeye ni Mungu mwenye haki kamilifu. Unapo kosea kidogo, ukaamuru mtu akatwe mkono, kumbe mashahidi walitoa ushahidi usiosahihi kwa 100%, huoni kuwa jambo hilo litamuuzi sana Mumgu wetu aliye mtakatifu mno na anaependa mambo ya haki? Na pia, hebu fikiria wewe mwenyewe kuwa, ingekuwaje kama Mungu angeendelea kuacha utaratibu ule uendelee mpaka leo katika dunia yetu hii ya leo iliyojaa rushwa na uonevu mpaka kwa viongozi wetu wakubwa? Si, tungekua tunasingiziana adhabu na malipizi yasio sahihi ovyo ovyo katika sheria zile za Mungu?!!. wanyonge wangeumizwa na kuuliwa kila siku kama wanyama lakini matajiri na watoto wa wakubwa, wangeachwa na kuonekana kua ndio wanadamu wenye haki ya kutopewa adhabu. Sasa mambo hayo ndiyo yaliyokuwa yanawapata watu wa zamani wakatifulani kutokana na baadhi ya viongozi kuonekana kua hawakua waaminifu kutenda haki. Sasa hivi, kuhani wetu bora aliyemuaminifu kwa 100% ni bwana yesu pekee, ambae anatuombea na kutupatanisha na Mungu pale tunapokosea akiwa yeye ni mpatanishi wetu mbele za Mungu. Musa alitakasa dhambi kwa damu za wanyama, lakini bwana yesu yeye anatakasa dhambi kwa damu yake yeye mwenyewe, soma(lawi 17:11) linganisha (waebrania 9:12-15). Na kuhusu swali lako kua, kwanini Mungu, asingetimiza sheria zake hizo tangu zamani? Biblia inajibu kuwa kama Mungu angefanya hivyo, basi sisi wanadamu wote tusingejua maana ya dhambi na maana ya ubaya wa kutenda dhambi dhidi ya sheria zake, soma(warumi 7:7:12). Biblia inasema kuwa ugumu uliwapata watu wa zamani, ili sisi tujifunze na kukamilishwa kwa neema na huruma wa Mungu mwenyeme. (ebrania 11:40).Hii ndio neema ya Mungu kwa kuwa, Mungu wetu hatuchukulii sisi kwa hasira yake tena, ila anatuchukua na kutufundisha kwa upole na upendo tukiwa ni watoto wake. Torati ilikaa kama kiongozi au mwalimu kwa wakati ule ili kutuleta kwa bwana yesu wote sisi, ambae ndie mwalimu na kuhani bora kuliko wote. Tetea majibu yako hayo vizuri ili tuelewe sio unajin’gata ng’ata hapa!!!!!!!.

    Like

  214. Rich says:

    ndugu mhamad. Hakuna hata nabii mmoja wa zamani alietekeleza nguzo za kisheria za Mungu, huku eti amevaa shuka nyeupe akimrushia shetani mawe huku anazunguka zunguka kaburi la marehemu fulani!!!, hizo zilikuwa ni sheria mpya na nguzo za kichawi za mtume wenu mhamad.

    Like

  215. Rich says:

    ndugu mhamad, kutokana na maelezo unayoendelea kuyatoa wewe mwenyewe, mimi binafsi nimepata jibu la uhakika kutoka kwenye dini yenu ya uislamu kuwa, kumbe dini au njia ya kweli ya Mungu ni mmoja tu, kwa mujibu wa dini zote mbili kwa kua dini zote zinakubaliana kwa 100%, jambo hilo kwamba, dini ya kweli ni ile inayoamini vitabu vya torati, zaburi na injili. Sasa, hapo utagundua kua, wakristo tunaamini hivyo kwa 100%. Na pia waislamu wanaamini hivyo kwa 100%, ila wao wana kitabu cha ziada cha 4, ambacho kwa mujibu wa maelezo ya ndug yohana ni kwamba, kitambu hicho cha 4 hakikuja kupinga au kubadilisha chochote ila kilikuja kwa ajili ya kuthibitisha kua, hivyo vitabu vya torati, zaburi na injili, havijachafuliwa, na tena bado vinafaa kwa muongozo. Lakini ili sasa tujue kuwa ni upande upi utakuwa ni sahihi na ni upande wa Mungu wa kweli kwa 100% , inatupasa kutazama kwa makini mno ule upande wenye kile kitabu cha ziada kisicho husika wala kisichotakiwa kupadilisha au kufundisha elimu yeyote ya ziada kumhusu Mungu kwa kuwa hiyo sio kazi ya kitabu hicho. Sasa hapa ndipo tunaweza kumuona vizuri yule nabii wa uongo jinsi anavyojaribu kupotosha waislamu kutoka kwenye hicho kitabu chao cha ziada, yaani quran. Utaona kuwa, nabii huyu muongo amejaribu kupingana na kila kitu kutoka kwenye vile vitabu vitatu vya asili kwa muongozo!!. Biblia imezitaja sifa zake zote na jinsi atakavyo jiinua yeye mwenyewe na kujifanya ni mbora kuliko manabii wote waliopita, yeye anaitwa ni mpinga kristo, yaani analipinga lile neno la mwisho la ukombozi wa watu wote ambalo ni injili ya bwana yesu. mtume wa waislamu, mhamad ndiye yule nabii muongo anaeonekana kuwa na sifa Zote mbaya za mpinga kristo kutoka kwenye kile kitabu chake cha ziada cha 4 alichokipata kule mapangoni, akikitumia kitabu hicho kwa ajili ya kuwaimanisha na kuwapotosha waislamu kutoka katika yale maneno ya Allah kuwa vile vitabu vitatu vya wayahudi ndivyo sahihi pekee kwa ajili ya muongozo!!. Ndugu waislamu, hebu jitafakarini upya kwa kua, neno la Mungu linasema “MTAKAPO NITAFUTA KAMA PESA NDIPO MTAKAPO NIONA!!!.

    Like

  216. Ndugu Rich,

    Kwanza kabisa nimshukuru Allah aliyenijalia kunipa uhai na afya lakini zaidi akanijalia neema kubwa kushinda zote yaani neema ya uislam.

    Ndugu Rich, kwanza niseme nafurahi zaidi kuona najadiliana na wewe, nakufundisha mambo mbalimbali ambayo ulikuwa huyajui, nazidi kumuomba Allah kwa neema hii aliyokupa ya kujadiliana na mimi ikusaidie kuingia katika nuru ya uislam inshaallah.

    Ndugu Rich, tunapoendelea kujadiliana huwa najisikia faraja sana kuona unanielewa halafu unajitoa akili kujifanya hujanielewa hii yote ikiwa ni katika kutetea dini yako ambayo siku hizi inapoteza muelekeo siku hadi siku,Ndugu Rich nikianza na hoja ya vitabu vya zamani yaani torati zaburi na injili, hakuna sehemu nimesema kuwa quran imekuja kuthibitisha kuwa vitabu hivyo havijachafuliwa kama ulivyojidai kujidanganya mwenyewe na kunisingizia mimi, kwa kauli yangu na nimetoa nukuu kutoka ndani ya quran na biblia pia zinazoonesha kuwa vitabu vya torati, injili na zaburi vimechafuliwa sanasana na manabii wa uongo katika biblia nimekupa ushahidi kuwa ukasome (MATAYO 23:1-30) utaona ni jinsi gani Bwana Yesu aliwatahadhalisha watu na manabii wa uongo wanaobadilisha neno la kweli la Mungu na pia Ndugu Rich nikakwambia ukasome (YEREMIA 8:8) utaona ni jinsi gani biblia inavyoeleza kuwa kuna watu waliobadilisha neno la kweli la torati, lakini kwenye quran nikakupa

    “SURA 5:13. Basi kwa sababu ya kuvunja agano lao tuliwalaani, na tukazifanya nyoyo zao
    kuwa ngumu. Wanayabadilisha maneno kutoka pahala pake, na wamesahau sehemu ya
    yale waliyo kumbushwa. “

    “SURA 4:46 AN-NISAI. Miongoni mwa Mayahudi wamo ambao hubadilisha maneno kuyatoa mahala pake, na husema: Tumesikia na tumeasi,..”

    Ndugu Rich, hizo zote ni aya kutoka ndani ya quran zinazothibitisha ni jinsi gani mayahudi walivyozibadili aya za Allah, katika vitabu vya torati, zaburi na injili hivyo kwa sababu ya uchafu huo na watu kuondoa baadhi ya amri na sheria za Allah na badala yake kuweka amri zao hivyo Allah akamtuma Mtume wake, ili kuzipa uhai sheria zake zilizokuwa zimeachwa na hivyo kuwathibitishia watu ambao walidhani sheria hizo zimeisha kuwa bado zipo na na ni za kweli kabisa na Mungu alifanya hivyo Kupitia kwa mbora wa viumbe vyote na mbora wa daraja , kipenzi cha Allah Mtume Muhammad(S.A.W)
    Sasa ndugu yangu Rich, ni ya nini kunisingizia eti nimesema kuwa quran inathibitisha kuwa vitabu hivyo yaani injili,zaburi na torati havijachafuliwa kwa 100%? Ndugu Rich, ina maana kwa aya hizo zote kutoka ndani ya biblia na quran bado hukunielewa au basi tu unataka ubishi wa kitoto.

    Ndugu Rich, tena kwa kuendelea zaidi nikasema Allah baada ya Allah kumtuma Mtumee wake na kumpa quran hakuna yeyote awezaye kubadilisha sasa kwa vile kila nukta ya quran watu wemehifadhi kwenye mioyo yao, kupitia vichwa vyao, hivyo ni vigumu kwa mtu yeyote kulibadili neno la Allah na sheria zake kama walivyofanya manabii wa uongo katika vitabu vilivyotangulia. Na pia utagundua ndio maana hata biblia zinatofautiana kwa kiasi kikubwa na kila toleo (version) inatofautiana na version nyingine kutegemea na waandishi, hivyo ni rahisi kubadili kila mtu kuweka lake, na pia nikakupa mfano wa hilo nikakwambia soma dibaji ya biblia waandishi wenyewe wanakiri kabisa kuwa kuna baadhi ya majina ya sehemu na majina ya watu zaidi ya 25000 yameongezwa na mengine kupunguzwa, sasa ndugu yangu sijui mpaka hapo unataka ushahidi gani, pia nikakwambia ukiangalia idadi ya vitabu ndani ya biblia za kiroman ni kubwa kuliko biblia za makanisa ya prtoestants hii yote ni kuonesha ni jinsi gani watu wanavyoweza kuichezea biblia kwa sana kadiri kila mtu awezavyo kitu ambacho kwenye quran haiwezekani kabisa.sasa ndugu Rich unataka kuniambia maelezo yangu yote hayo hukuyaelewa au unataka ubishi tu usio na tija, tena ndugu yangu Rich kwa kauli tu ya waandishi wa biblia kwenye dibaji ingekutosha kabisa kuona kuwa neno la biblia halifai kuwa mwongozo kwa sababu wanadamu pia wanaonekana kufukia mashimo ambayo wanahisi yehova aliyasahau.

    Ndugu Rich, katika kujitahidi kwako kujitetea ukasema kuwa nyie wakiristo mnaamini torati kwa 100% kitu ambacho sio kweli kabisa kwani kama mngekuwa mnaamini torati kwa asilimia hizo basi isingewezekana nyie mpinge sheria za torat na mseme hazitakiwi kufuatwa kwa ulimwengu wa sasa kwa sabbu zenu tu za kibinadamu mnazoweka eti kwa mfano unasema watu wangepata sababu za kuwasingizia wenzao, na wakati sote tunajua masingizio hayajaanza leo wala jana bali hata enzi za manabii wa zamani watu walikuwa wakisingiziwa lakini hilo halikuweza kufanya sheria za Mungu zisitumike.sasa iweje leo hiyo ndo iwe sababu? Hivyo unaona jinsi mnavyojaribu kutafuta vijisababu visivyo na msingi ili mradi tu mzikatae sheria za Mungu.

    Ndugu Rich, ukatoa pia hoja ya kwenda kuhiji ukailezea vibaya kwa kusema eti katika uislam ni lazima kuhiji,Ndugu Rich, suala la kuhiji katika uislam lipo lakini pia sio lazima, hivyo basi kama kuna baadhi ya manabii wa zamani walihiji au baadhi hawakuhiji suala hilo sio lazima kabisa katika nguzo za imani ya uislam na hiyo ndiyo nguzo pekee ambayo Allah amesema anaweza fanya mtu yeyote Yule atakayeona anaweza, hivyo sio lazima na kwa mtu yeyote asiyefanya hija bado anaendelea kuwa muislam.Ndugu Rich, hata mimi sijaenda kuhiji, lakini pia nisipoenda mpaka nikafa haitaniondoa mimi katika uislam, tofauti na nguzo nyingine katika uislam. Lakini pia ajabu sana siku hizi tunaona hata nyie mnajaribu kutuiga kwenda kuhiji kule Palestine kwenye nchi ya kiislam, mkitembelea makaburi ya mnaowaita watakatifu na sehemu mbali mbali, lakini nashangaa sana sijui mnatumia ushahidi wa andiko gani kutoka ndani ya biblia yenu, labda kwa sababu wewe ni mjuzi wa biblia unaweza nisaidia.

    Ndugu Rich,pia ukahoji kuwa kwa kuwa manabii wa zamani hawakutumia quran hivyo basi hawastahili kuwa manabii waislam, Ndugu Rich, Allah ameshasema manabii hao aliwatuma na akawapa torati, zaburi na injili zenye sheria sawa na zile za quran, na akaleta quran kusadikisha kweli ya sheria hizo, hvyo sheria zote ni sawa kwani kinachoangaliwa hapo sio majina ya vitabu bali tunaangalia sheria za Mungu ndani ya vitabu hivyo na wala siyo majina ya vitabu kwani majina hata manabii wenyewe walikuwa na majina tofauti lakini wote walileta neno lile lile la Mungu mmoja, huwezi ukauliza eti kama walileta neno lile lile mbona majina yao yanatofautiana, kwa hakika utaonekana bwege mkubwa.

    Ndugu Rich, lakini pia ukasema pia ukasema kuwa quran ndicho kitabu kimeongezeka tofauti na nyie wakiristo ambao mna vitabu vyote yaani injili torati na zaburi, kwanza kabisa ni uongo mtupu ukisema nyie mna injili na ili hali ile mnayoita injili ni maneno ya waandishi ambayo watu waliandika tu kwa kusimuliwa kwa mfano nikakwambia soma (LUKA 1:1-4) Luka mwenyewe anasema ametafuta tafuta tena kutoka kwa wasimuliaji waliomsimulia mambo yalivyokuwa kipindi cha Yesu, sasa hiyo ndugu yangu utaiita injili ya Yesu, yaani mtu tena mtu mwenyewe Luka aliyekuwa mganga wa kienyeji ”witch doctor” anasema alikuwa anaenda kwa watu anauliza wanamwambia then anaandika halafu nyie wakiristo mnasema hiyo mliyo nayo ni injili! Tena bora bwana huyu angesema malaika ndio waliokuwa wakimpa funuo, lakini hapana! Sasa je ndug yangu Rich hujui nini madhara ya fasihi simulizi?

    Ndugu Rich, katika dini zote waislam pekee ndio wanaoamini injili ya kweli ya Yesu, kwani Allah alimfunulia Mtume wake kupitia kwa malaika sheria zote za injili, lakini nyie wakiristo mnaamini injili za uongo na nyingine zimeandikwa na waganga wa kienyeji na bado mnaziita injili,

    Ndugu Rich, injili maana yake ni funuo alizokuwa akipewa Bwana Yesu, hivyo ni maneno yote aliyoyasema Bwana Yesu, lakini ukitaka kujua kuwa hiyo mliyo nayo siyo injili ya Yesu, soma biblia za kiingereza zinazoitwa Red lettered Bible, ambazo kila neno alilotamka bwana Yesu limewekwa katika Red, biblia hizo zinapatikana hata kwenye mtandao ambazo kila neno alilolisema Bwana Yesu waandishi wa bblia hizo wamewekea Red maandishi hayo, ukiicopy biblia hiyo kwenye Microsoft excel then ukacalculate asilimia ya maneno ambayo yamewekwa katika Red katika biblia ya agano jipya ambayo mnaita injili, utaona maandishi mekundu kwa maana maneno aliyoyatamka Bwana Yesu ni 1.01% tu ya maneno yote ndani ya biblia ya agano jipya ambayo mnajidanganya kuwa ni maneno ya Injili ya Yesu na maneno ya Yesu yapo katika vitabu vine tu yaani luka, matayo, marko na yohana vitabu vingine 23 vilivyobaki hakuna hata doti ya neno alilotamka bwana Yesu, je wewe utajidanganya kuwa unayo injili ya kweli ya Bwana Yesu?Hapo usijidanganye ndugu yangu umeingizwa chaka, uongo mkubwa mno na utagundua kuwa mliyo nayo haifai hata kwa chembe kuitwa Injili ya Yesu kwani haimuwakilishi Yesu, bali waandishi tu wameweka maneno yanayowafurahisha wao, wakajidai eti ni injili ya Yesu.Ndugu Rich, Ukisoma vitabu vyote vya Paulo huwezi ukajua Yesu alisema nini, na kuonesha ni jinsi gani Paulo hakuwa mtume wa kweli, anasema kabisa wazi kuwa baadhi ya amri Mungu hakumpa, hivi ndugu Yangu Rich, kweli jiulize ni nabii gani ambaye Mungu hakumpa baadhi ya amri kwa ajii ya binadamu? Tena amri ya muhimu kuhusu masuala ya Mahusiano? Sasa ni Mungu gani msahaulifu kiasi hicho ndugu yangu, sisi tunaamini kabisa huyo yehova anayesahau sahau kabisa kabisa hawezi na wala hakuwa mungu wa Kweli bali ni shetani.

    Ndugu Rich, Tukirudi huko juu kwenye mada inayohusu ni jinsi gani Biblia inavyomkashifu bwana Yesu, huko ndiko umeonesha ni jinsi gani ulivyo na ubishi wa msuli ndugu yangu wala hutafuti kufahamu kwani umeonesha kuutetea ujinga wazi wazi.

    Kwa mfano umesema Yehova hakuwa rafiki wa Ibilisi, lakini ndugu Rich unawezaje kukataa swala kama hilo na ili hali biblia yako inaonesha wazi kabisa kuwa mahusiano yaliyokuwepo kati ya yehova na ibilisi ni mahusiano ya urafiki tena siyo urafiki tu bali urafiki wa kushirikiana katika suala nyeti kabisa la kumteka bwana Yesu kwa masiku 40, kwa upande wetu sisi waislam hatuamini kama Mungu wa Kweli Allah sub-hana wataala anaweza kushiriakiana na Ibilisi kiasi hiki, sisi katika uislam tunaamini Allah huwa anawatuma malaika wake watiifu peke yao na wala hashirikiani kabisa na Ibilisi hata siku moja kama alivyo mungu yehova wa biblia.katika uislam tunaamini Allah anao malaika maelfu na maelfu hivyo haiwi kwa Allah hata siku moja akamtuma Ibilisi, Ndugu Rich, sisi waislamu tunaamini Ibilisi anatumwa na ibilisi mwenzie na wala sio mungu kumtuma Iblisi, hivyo basi hata yehova mwenyewe ni ibilisi tena mkubwa wa maibilisi kwani ameonekana akimtuma shetani kwenda kumjaribu Bwana Yesu.

    Ndugu Rich, ushirikiano huo wa Yehova na Ibilisi biblia inaonesha kuwa ulianza zamani za enzi za Ayubu Kwani ukisoma kitabu cha AYUBU 4:1 -7 utaona wazi ushirikiano wa maibilisi wawili mmoja akiwa yehova wanaenda kumtesa Ayubu, hakika huu ni ushirikiano wa karibu mno, sasa ndugu Rich kama yehova anashirikiana kiasi hiki na Ibilisi hiyo siku ya kiyama Yehova atawezaje kumuhukumu shetani na ili hali yeye ndiye aliyekuwa bosi wake akimtuma huku na huko? Hebu naomba unijibu swali hili ndugu yangu, yehova anamtuma ibilisi, halafu siku ya mwisho amuhukumu ibilisi hii inawezekana kweli ndugu yangu? Huoni kwamba yehova atakuwa ameshapoteza nguvu na uwezo wa kumuhukumu yehova kwani kama maasi yeye yehova ndiye aliyekuwa akimtuma kuyafanya.

    Tena ndugu Rich ukatetea ujinga mwingine eti bwana Yesu aliwaita watu nguruwe ili azijaribu imani zao,kama ziko madhubuti au la, ndugu Rich, mimi naamini kabisa ulipokuwa ukijibu hoja hizi hata nafsi yako ilikuwa ikikusuta kwa kutetea upuuzi, hivi kujaribu imani za watu ndio kuwaita nguruwe, tena hapo bwana Yesu alionesha kabisa ubaguzi wa rangi, na ukabila wazi wazi pale aliposema huwezi chukua chakula cha watoto na kuwatupia nguruwe, yaani huo ni ukabila wa waziwazi eti waisreali watoto halafu sisi wengine ni mbwa na nguruwe, Ndugu Rich sikutegemea kabisa kama ungekubaliana na matusi haya ya Yesu ndani ya biblia kwa watu wasiokuwa wa kabila lake, hii imenithibitishia ni jinsi gani unavobishania msuli na wala sio kwa kutaka kuelewa, pia ndugu Rich kama ni suala la kujaribu imani za watu zipo kauli nyingi tu nzuri za kutumia na wala sio kuwaita watu nguruwe na mbwa viumbe ambao hata biblia yenyewe inatambua kuwa ni najisi.Sisi waislam hatuamini kabisa kama nabii wa kweli wa Mungu anaweza akasema maneno haya yenye kufedhehesha mno, bali tuanaamini ni maneno tu ya manabii wa uongo walioyaingiza ili kumchafua Bwana Yesu na wala sio maneno ya Yesu, kwani sisi quran inatwambia bwana Yesu alikuwa na kauli njema kwa watu na alikuwa mpole na mwema soma SURAT MARIAM ni sura ya 19 ndani ya quran utaona sifa hizi za Bwana Yesu.

    Ndugu Rich, pia ukaendelea kutetea upuuzi katika ile aya ambayo bwana Yesu aliwaita wanafunzi wake vizazi vya nyoka na majoka kwa kutetea eti aliwaita vile kwa sbabu walimtaabisha sana. Ndugu Rich, manabii wote Mungu alipowatuma duniani walijua kabisa kuwa watataabishwa na wengine watauwawa, na kwa kifupi kila nabii alitaabishwa mno, tena nabii Muhammad ndiye aliyepata taabu zaidi, kwani tunasoma katika sira alipigwa hadi akatolewa meno ya mbele yote, tena kuna sehemu nyingine alipigwa mawe mpaka kanzu yake yote ikalowa damu, lakini hakuna siku hata moja alitumia kauli zisizo na nidhamu hata kidogo.

    Ndugu Rich, pamoja na hayo tukisoma ndani ya biblia wale watu ambao Yesu aliwaita mashetani na vizazi vya nyoka sio wale waliomtaabisha kama ulivyodanganya wewe, bali ni wale waliokuwa wanafunzi wake vipenzi, tena ambao wengine biblia inasema aliwafanya mitume, hawa ni wale waliokuwa wakimtambua kama mwalimu na wala sio wale waliokuwa wakimtaabisha. Kwani hata tukisoma katika biblia katika Matayo 17:17, Matayo 12:34, na kuendelea tunaona walikuwa wanafunzi, lakini pia hata kama kigizo ni kutaabishwa mbona hata Petro aliyempenda sana Bwana Yesu naye alitukanwa? Sisi waislam hatuamini kama nabii wa kweli anaweza akawa na majivuno na matusi kiasi hiki, hatuamini kabisa katika hilo bali tunaona ni mojawapo ya uongo ndani ya biblia.

    Ndugu Rich, katika juhudi zako za kuendeleza ubishi ukaitetea ile kauli ya Yesu aliposema wote walionitangulia ni wezi na wanyang’anyi kwa kuunganisha unganisha vimistari ambavyo hata haviusiani ili kuonesha kuwa wote maana yake siyo wote, Ndugu Rich hapa unajaribu kujitoa akili na kujifanya huelewi maana ya neno “ wote”, kwa lugha ya Kiswahili wote maana yake ni wote wala hakuna maana nyingine ambayo mtu anaweza akajifanya anapachika pachika, hivyo basi Bwana Yesu wa biblia aishasema wote waliomtangulia ni wezi na wanyang’anyi, hayo ni matusi ya wazi kabisa ambayo hata mtu ajitahidi kusafisha kwa namna gani haiwezekani, kwa maana yesu wa biblia anaonekana kabisa kutowatambua watukufu wote waliomtangulia bali yeye anawatambua kuwa walikuwa wanyang’anyi, kitu ambacho kinatufanya sisi waislamu tuamini kabisa kuwa hii biblia kuna maneno mengi mno ya manabii wa uongo wanaomsingizia yesu mambo ambayo hata hakusema.

    Ndugu Rich, hoja zipo nyingi mno ila kwa uchache niishie hapa ili nikupe muda wa kujifunza na kuelewa badala ya kuendekeza ubishi usio na msingi wala mwelekeo katika maisha ya akhera.

    Allah akupe wepesi, uingie katika nuru ya uislam sote tulikuwa wabishi kama wewe tena zaidi hata ya wewe lakini mwisho wa siku kwa fadhila za Allah na wala si kwa ujanja wetu tuliuona mwanga na nuru ya uislam na sasa tunajivunia kuwa waislam.Wallah Allah ni mkubwa mno.

    Wabillah tawfiq,
    Alhamdulillah.

    Like

  217. Rich says:

    Kaka mhamad, hebu punguza pupa na kuacha jazba kiasi hicho ndugu yangu!!!!!, Mijihasira na mijiubishe kibao mpaka unaanza tena kuhoji hoja za siku tatu zilizopita na wakati maswali yangu huja yakamilisha ipasavyo. Yaani umehoji na kuandika kwa hasira na jazba mpaka unatoa vijimate vya mdomo vilivyo nifikia huku niliko!!.Hilo ndilo tatizo la kufundishwa jinsi ya kuitetea dini mpaka kufa. Ndugu yangu mhamad hebu nijibu maswali yangu kwa haki alafu ndio na wewe utaanza kuhoji upya majibu ya maswali niliyo yatoa. Wewe unafanya vurugu kujibu haya maswali yangu ili na mimi nisahau kutazama majibu yako kama ni sahihi. Ndugu mhamad inakupasa kua na akili ya ziada wakati unapoyajibu haya maswali, usijaribu kuniletea majibu ya kitoto mtu kama mimi. Hebu sasa tazama ujinga wako katika hayo majibu uliyo nipa mimi. Nianze na lile swali la mimi kukataa kua manabii wa zamani kamwe hawakua waislamu kama ninyi. Nianze kwa kusema kuwa, nguzo ya quran inasema kuviamini vitabu vyote vinne, ili uwe muislamu kamili, na kamwe sio eti kuviamini vitabu vitatu kama walivyoamini manabii wa nyuma!!!. Kama ni kweli quran ingekua ni sawa na vile vitabu vitatu vya mwanzo kwa 100%, kama unavyo dai wewe na pia kama walivyo amini manabii wote wa nyuma, basi hicho kitabu cha nne cha quran, kingepaswa kisiwepo. Sio kweli kabisa eti wale manabii wa zamani walioamini vitabu vitatu vya torati, zaburi na injili eti pasipo kuamini na nguzo ya kile kitabu cha nne, ambacho ni quran, eti nao wawe na haki ya kuwa waislamu kama ninyi na wakati wao walipungukiwa na kitabu cha mwisho cha nne. Nguzo inasema ni kuviamini vitabu vyote vinne, kama mnavyoamini ninyi waislamu kwa sasa, na kamwe sio kuviamini vitabu vitatu pekee kama walivyoamini wale manabii wa nyuma.Hivyo, kwa sababu hiyo pekee inatosha kabisa kutuonyesha kuwa wale manabii wa nyuma, kamwe hawakuwa waislamu kama ninyi kwa kuwa wao wakati ule kitabu cha quran chenye hiyo nguzo ya nne hakikuwepo, tena hata huyo mletaji wake mtume wenu mhamad bado alikuwa hajazaliwa. Pia ndio maana nilikuuliza kuwa, inamaana hata hii leo, mtu akiviamini vitabu vitatu pekee vya torati, zaburi na injili bila ya kile kitabu cha nne cha quran kitacho kamilisha idadi ya vitabu vinne vya nguzo ya Alla je, nae anayo haki ya kuwa muislamu??!!, wewe badala ya kujibu swali hili, ukaanza kukwepa kwa kutoa mambo ya majina ya watu na vitabu, kitu ambacho kamwe mimi sikuuliza!!. Ukome kabisa kujaribu kutudanganya sisi wakristo kwa kutupa majibu ya uongo kama mnavyo danganyana huko misikitini kwenu.JIBU VIZURI SASA. Swali la pili pia umelikwepa na kuanza kumdharau Mungu wako wewe mwenyewe!!!. wewe unatuambia kuwa kule hija hakuna maana yeyote ya lazima kwa muislamu hata akifa bila ya kwenda, lakini jambo la ajabu Mungu wako Allah alikusisitiza kuwa, katika maisha yako yote walau usikose hata mara moja!!!. Wewe unaniiga mimi mkristo nilivyo sema na wakati wewe hiyo kwako ni sheria ya Allah aliyokuandikia katika quran ili uitekeleze, hivi ni muislamu wa aina gani wewe?, mbona kama sikuelewi!!, unabadilisha na kuzikataa kwa kuzidharau mpaka sheria za Mungu wako, ilimradi tu, utetee dini yako, Mwandawazimu mkubwa wewe!!!. Lakini ili tusipigiane kelele na kupoteza muda katika swali hili, mimi nakuomba uyaache yote haya, hahafu moja kwa moja unijibu swali husika nililo uliza kuwa, “HUO UTARATIBU WA KISHERIA ULIOANDIKWA KWENYE SHERIA ZENU ZA IBADA KATIKA QURAN, KUWA NINYI MUENDE HIJA KUVAA SHUKA NYEUPE NA KUMPIGA SHETANI KWA MAWE….MLIPEWA NA NANI KATIKA SHERIA ZENU NA WAKATI MANABII WA ZAMANI MNAO SEMA MNAWAFUATA KATIKA SHERIA ZAO BILA YA KUONGEZA WALA KUBADILISHA KITU, WAO HAWAKUWA NA UTARATIBU HUO WA AJABU?? Fulstop, jibu point bila ya maelezo ya uongo. Halafu sasa, Mimi ninawaomba wafuatiliaji wote wa mjadala huu, wathibitishe jinsi ndugu yetu mhamad pamoja na Mungu wake Allah na waislamu wote jinsi wanavyo viamini na kuvifuatilia vitabu vya wakristo vya injili, torati na zaburi ijapokuwa kwa mtazamo wao wa nje, wanajifanya kuwa hawavifuatilii wala kuviamini kwa lengo la kutuvunja imani yetu sisi wakristo mbele ya Yehova Mungu wetu, jambo ambalo kamwe halitawezekana hata mpaka mwisho wa dunia hii. Ushahidi ni mwingi mno, lakini mimi nitamnukuu huyu ndugu yetu mhamad yohana katika hoja yake ya hapo juu kidogo ya “JANUARY 15,2014 AT 11:36 AM, ili mumuone nyie wenyewe jinsi anavyo vikubali na kuvifananisha vitabu vya wakristo vya injili, torati na zaburi kuwa ni sawa na vile vyakwao vya Allah walivyo vipata kule mapangoni kupitia mashetani, jambo ambalo mimi simuungi mkono kua eti vinafanana wakati vyao walipewa na mashetani wakati sisi tulipewa kwa kurithishwa kutoka kwa manabii wa Mungu wa kweli. Nitaanza kwa kumnukuu alivyosema yeye mwenyewe, halafu kwenye ile point muhimu nitaandika kwa herufi kubwa. Naanza kumnukuu alivyosema ndugu mhamad yohana ” ndugu Rich, Allah mwenyewe amekupa jibu hapo juu kwenye surat Yunus, kuwa haiwezekani quran iseme uongo na ili hali inasadikisha yaliyokuwa kabla yake, yaani “INAWATHIBITISHIA KABISA WANA WA ISRAEL KUWA “HAYO WALIYOKUWA NAYO KATIKA TORATI NA INJILI NI SAWA KABISA NA YALE ALIYOKUJANAYO MTUME MUHAMAD”, Kama haitoshi ndugu zangu, huyu kinyago wa kiislamu akaendelea kwa kusema, namnukuu tena ila kama kawaida yangu kuwa, kwenye maandishi ya herufi kubwa ndio pointi yangu. Tazama namnukuu jinsi alivyo malizia mwisho wa hiyo hoja yake “Mwisho kabisa ndugu Rich, Sioni kama ulitakiwa kumpinga mch Mosespk kwa sababu hata wewe bado unaendelea kubeba biblia ambayo ndani yake kuna sheria ambazo unaamini zilibatilishwa na Yahwe, hivyo, kufanya na imani yako iwe batili, pili, hiyo inathibitisha kabisa kwamba, manabii wa zamani walikuwa siyo wakristo bali walikuwa waislamu, kwa sababu sheria walizopewa na Mungu, nyie wakristo ni batili na wakati “SHERIA HIZO NI SAWA NA SHERIA WALIZOPEWA WAISLAMU KATIKA QURAN”. Mwisho wa kumnukuu. Ndugu zangu wote mnaofuatilia mjadala huu, nafikiri ninyi wenyewe mmejionea uwandawazimu mkubwa wa huyu muislamu anaejiita “MHAMED YOHANA”. Hoja zake zote huko juu, kazi yake ni hiyo hiyo ya kutetea dini yake kwa nguvu zote hata kufikia hatua ya kumtukana Mungu wake Allah kuwa, sheria zake sio za lazima sana kutekelezwa kwa kuwa haziwezi kupunguza ile heshima ya wao waislamu!!!. kila hija inapokuja waislamu wengi hujitahidi kutimiza nguzo yao hiyo, lakini ndugu Mhamad yeye, anatufundisha kuwa sio lazima kufuatwa. Swali la msingi hapa ni kuwa, je, ni kweli sio lazima kufuata baadhi sheria za Mungu, na wakati Mungu aliekuagiza ni Mtakatifu katika mambo yake!!, na mwisho hapo kama mlivyoona huyu bwana jinsi anavyo viheshimu na kuvikubali vitabu vyetu vya ibada mpaka hata kuvifananisha ng vile vya kwao walivyopewa na mashetani, jambo ambalo sisi wakristo kamwe hatukubaliani nae kua eti vitabu vyetu na vyao ni sawa!!!!!. Ndugu mhamad, baada ya mimi kuongea kwa siri na watu wote kwenye blog hii, wanaotufuatilia, nakugeukia wewe kwa kukuambia kuwa, bado mlango uko wazi, bwana yesu bado anakuhitaji, usichelewe kabisa, maana yeye anakuona jinsi unavyo tapa tapa na kuangaika. Mwisho ni kwamba, hebu rudia kutoa majibu ya kweli ya hayo maswali yangu…halafu nikiridhika ndipo unaweza uliza mambo mengine. Ni lazima twende kwa utaratibu unaofaa na kamwe sio vurugu kama unavyotaka wewe tufanye. Bwana yesu anakupenda sana ndugu yangu ili uwe kondoo wake wa kweli kama alivyokata shauri mtume paulo. Wewe wangoja nini ndugu?!!!.

    Like

  218. Ndugu Rich,

    Naomba nikujibu kwa ufupi halafu niendelee, najua umenielewa saaana ila una aibu jinsi utakavyoacha kuuliza, unaogopa kuwaangusha wakiristo wenzako.

    Kuhusu utaratibu wa kwenda hija waislam tumeambiwa kwenda hija na Allah ndani ya quran, lakini wewe unasema manabii wa zamani hawakuenda hija naomba unipe ushahidi kuwa manabii wa zamani hawakufanya hija.lakini pia nikakwambia wawe walifanya au hawakufanya, hiyo siyo lazima na haimuondoi mtu katika uislam, Ndugu Rich na hayo si maneno yangu bali nguzo yenyewe ya uislam inasema hivi kwa kiarabu “hijju lbait manistatwa’aa ilayhi sabila” maana yake kwa kiswahili “kwenda kuhiji makka kwenye nyumba ya Mwenyezimungu kwa mwenye uwezo” mwishoni imemalizia kwa mwenye uwezo, hivyo anayeweza anahiji asiyeweza haendi kuhiji, hivyo hakuna ulazima katika hilo, na hili muulize muislam yoyote Yule aliye karibu yako kama hija ni lazima au hiyari nafikiri jibu utalipata.

    Lakini pia ukiniuliza ushahidi wa hija, quran inaonesha kuwa swala la hija halijaanza kipindi cha Mtume Muhammad bali kuanzia kipindi cha nabii Ibrahim, kwani kwenda kuhiji maana yake ni kwenda kuizulu nyumba ya ibada iliyojengwa na Nabii Ibrahim katika jangwa alipomuacha mwanae Ismael.na hapa naomba nikupe ushahidi wa quran tukuf

    SURA 22. SURATUL HAJJ
    26. Na pale tulipomweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia: Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut’ufu, na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao sujudu.
    27. Na watangazie watu Hija; watakujia kwa miguu na juu ya kila ngamia aliye konda, wakija kutoka katika kila njia ya mbali.

    Kwa hiyo ndugu yangu swala la hija halijaanza leo bali quran inatwambia lilianza hata kipindi cha nabii Ibrahim, ambaye ndiye baba wa imani yetu. Kwa aya hiyo naamini kabisa nimejibu swali lako nimekuonesha aya kutoka ndani ya quran.

    Lakini pia kwa upande wenu wakirsto tunaona siku hizi mnaiga utaratibu wa kwenda hija kama sisi naomba sana sana sana hii ni mara ya nne sasa nauliza swali hili sijaona ukifurukuta walau hata kujibu, naomba uniambie mnatumia andiko gani? Sawa siyo lazima lakini kwa andiko gani? Kwa kweli nyie mnachekesha sana kwa sababu mnaamini swala la kufanya hija ni swala la uzushi na swala ambalo halikuwepo na wala manabii hawakulifanya, lakini nashangaa nyie mnafanya!!! Sasa je nyie ni wafuasi wa waislamu ambao tunafanya hija au ni wafuasi wa manabii ambao hawakufanya hija?ndugu Rich, ama kwa hakika kwa kitendo hiki kinadhihirisha ni jinsi gani mnavyoikubali dini yetu lakini hadi mnaacha kuwaiga manabii wenu ambao mnaamini hawakufanya hija, badala yake mnatuiga sisi.

    Ndugu Rich, lakini pia uligusia swala la kuvaa mashuka ukasema eti tunavaa mashuka kama wachawi na ma free mason, mimi kwa ujumla sijaelewa imani hii umeipata wapi kwamba wanaovaa mashuka wanakuwa wachawi au ma free masorn, kwa sababu hata Yesu mwenyewe alikuwa akivaa mashuka meupe, je na yeye alikuwa free mason, au alikuwa mchawi? Lakini pia umeambiwa na nani kuvaa shuka ni alama ya uchawi? Kwa sababu hata wamasai mavazi yao ni mashuka je na wao ni wachawi? Ndugu yangu tatizo lako zinakupotosha movie za kinigeria matokeo yake unakuta unachanganya mambo.

    Ndugu Rich, ukaeleza pia kuwa mojawapo ya sababu za uislam ni kuviamini vitabu vinne zaburi, injili taurati na quran, kwa ujumla sijui neno hili umelitoa wapi kwa sababu Allah ndani ya quran hajaweka limit ya idadi ya vitabu, kama ulivyosema wewe, Allah ndani ya quran amesema “antu-uminu billah, wa-malaikatihi, wa-kutubihi, wa-rusulihi” yaani maana yake kwa Kiswahili “kumuamini, Mwenyezimungu, na malaika wake, na vitabu vyake, na mitume wake” hakuna sehemu ambayo Allah amesema kuviamini vitabu vinne. Kwa hiyo kinachotakiwa ni kuamini vitabu vya Allah, na kuamini vitabu vya Allah maana yake ni kuamini maamrisho na sheria za Allah zilizo ndani ya vitabu hivyo.kwa hiyo mtu yeyote hawezi kuwa muislam kama haamini vitabu vya Allah, kwa hiyo sawa na nguzo hiyo manabii wote wa zamani walikuwa waislam kwa sabbu waliamini katika vitabu vya Allah.

    Ndugu Rich, unachotakiwa kujua ni kuwa hiyo nguzo ya uislam haisemi kigezo cha kuwa muislam ni kuamini quran, hapana nguzo hiyo inasema kuwa muislam ni kuamini vitabu vya Allah, hivyo ukihisi quran, zaburi na injili ni vitabu vya Allah basi wewe ni muislam.

    Ndugu Rich, tofauti na nyie ndugu zetu kigezo cha kuwa mkiristo ni kubatizwa tena kwa kuzamishwa ndani ya maji! Lakini sasa je mbona hatuoni sehemu yoyte manabii wa zamani walikobatizwa? Je nyie kweli kama mnaamini manabii hao walikuwa wakiristo wenzenu ilikuwaje wakawa wakiristo bila kubatizwa? Maswali haya ni miongoni mwa maswali yaliyoshindikana kabisa kujibika kwa maana nimeyarudia hii ni mara ya kumi na zaidi, hakuna jibu, wala hata kujaribu kujibu.

    Ndugu Rich, pia umesema sisi tunajitahidi kuvifuata vitabu vyenu wakiristo yaani zaburi, injili na torati, nashukuru kuwa umetambua sasa kuwa sisi tunaviamini vitabu hivi, lakini cha ajabu unasema ni vya wakiristo, ok tuassume ni kweli ni vitabu vyenu vipi sasa sheria zake mnasema zimebatilika kama ni vitabu vyenu kweli? Sheria za torati mnazikataa na mnasema zimebatilika halafu bado mnasema ni vitabu vyenu, si unafiki huo ndugu yangu?au ndio nyie mnaosema lakini hamtendi sawa na mnavyosema, mnasema vitabu hivyo ni vyenu lakini sheria zake si zenu, je nyie tutawatofautishaje na masadukayo na farisayo ambao yesu aliwakemea vibaya mno kwa tabia yao ya kusema wasioyatenda? Nyie si ndio wale wale kweli ndugu yangu Rich, hebu nipe tofauti kati ya wewe na farisayo.

    Lakini mnageuza sisi waislamu tunaosema sheria hizo ziko hai, na hazijafa ndio mnasema eti sheria hizo si zetu,yaani kwa mfano Allah anasema mwizi akatwe mkono, na torati nayo inasema hivyo hivyo, lakini wewe mkiristo unapinga eti kwa sababu watu watasingiziana, hivi unataka kuniambia kusingiziana kumeanza leo!!! Hii ni hoja ya kipuuzi kabisa inayotumiwa na wakiristo kupinga sheria za Allah, lakini kama kweli kama sheria hiyo ilishabatilika, ni kwa nini basi mdai mnaifuata torati kwa 100% kama ulivyosema huko juu na ili hali baadhi yenu sheria zake mnazipinga ? Hebu nijibu ndugu yangu! Swala hili nimelihoji hii ni mara zaidi ya kumi lakini sijaona mkiristo yoyote aliyejaribu kujibu.

    Ndugu Rich, niseme nakushukuru jinsi ulivyonitukana na kuniita mwendawazimu n.k, lakini mimi sishangai kwa sababu si kosa lako bali hata biblia yako yenyewe inasema mti hutambulika kwa matunda yake, hivyo “like father like son”, hayo ni matunda ya mafundisho ya yesu ndani ya biblia ambaye kazi yake ilikuwa ni kutukana tu, pale alipokuwa akishindwa kujibu hoja za ndugu zake, hivyo hata wewe sikushangai kabisa kwa maana wewe ni tunda huna hatia wenye hatia ni mti uliokubeba, mimi sikurudishii matusi, kwa sababu kutukana si hulka ya mwislamu, bali kutukanwa, na kufedheheshwa ni sunna ya manabii wote wa Allah, tena unaponitukana mimi nasema Alhamdulillah kwa sababu najua ujumbe umekufikia na umekuingia.

    Wabillah tawfiq.
    Wwahaadha ssalaam.

    Like

  219. Rich says:

    ndugu mhamad, mwendawazimu ni neno la kawaida sana katika mijadala kama hii, tofauti kabisa na wewe ulivyo tuita huko juu makafiri. Zaidi ya yote ukamuita Mugu “Malaya”, jitazame wewe mwenyewe huko juu ya hoja zako!!!. Sasa, sijui ulikuwa unafikiria nini wakati ulipokua unatoa hayo matusi.Lakini mimi kwa upande wangu naomba unisamehe km neno hilo la mwandawazimu limekuuz. Nikija kwenye majibu yako, swala la hija ,kwanza nimefurahi sana sana kwa wewe kuvikubali hivi vitabu vyetu vya injili, torati na zaburi kuwa vyote ni sahihi kwa muongozo. Kwa hiyo, kupitia vitabu hivyo vya Mungu katika biblia, ndipo nilipogundua kuwa ninyi waislamu, huwa hamfuati sheria na miongozo ya Mungu kama biblia inavyofundisha. Istoshe, kama ulivyoonyesha jinsi kuran ilivyo wapotosha kwa kuingiza miongozo ya ziada ya kwenda hija, jambo ambalo kamwe halipo katika biblia na vitabu vyake vyote. Swali la idadi ya vitabu vyenu vya ibada, hapo ndugu yangu naona umechemka kabisa kwa kuwa waislamu wote pamoja hata na mimi mkristo tunatabua kuwa idadi ya vitabu vya ibada ya waislamu ni vinne tu, kwa mujibu wa Allah mwenyewe. Tena ndugu mhamad, hata wewe mwenyewe mara nyingi sana ulikua unavitaja kuwa ni vinne pekee. Hata ulipoandika zile nguzo za dini yako, ukavitaja mwenyewe kua nguzo moja wapo ni kuviamini vitabu vinne vya Allah. Sasa, mimi ninakushangaa ndugu yangu wewe, kwa kuwa wewe unataka kulikwepa swali langu, ukaamua ujifanye kuwa ni muislamu asiejua hata idadi ya vitabu vyake vya imani!!!. Maajabu makubwa sana hayo. Hebu jitetee kwa haki ya kuheshimu misingi ya dini yako ndugu, kwanini eti unajifanya kuwa hata idadi ya vitabu vyako vya ibada huvijui? Maona huko juu ulitutajia kuwa ni vinne? Halafu, hata kama unadai kuwa hujui idadi yake, utagundua kuwa, kitabu cha quran ni kimoja wapo, kwa hiyo, swali litabaki pale pale kwamba, je, hao manabii wa nyuma, walikiamini kitabu hicho ili nao tujue kuwa walikuwa ni waislamu wenzenu??…kwa kuwa hata kama nguzo inasema ni kuviamini vitabu vyote, bado utagundua kuwa, kitabu cha quran, hakijaaminiwa na manabii wa zamani ili nao watimize nguzo ya Allah ya kuviamini vitabu vyote na kuwa waislamu. Hebu usikimbilie hoja za kitoto ambazo mimi nitazijibu zote hizo, tumalize kwanza mjadala huu kuujibu kwa 100%. Haya hebu jitetee tena, lakini swala la ukamilifu wa biblia yetu, tumesha limaliza kwa wewe mwenyewe kukubali usahihi wa biblia yetu…ndio maana ulishindwa kutetea vile nilivyo kunukuu maneno yako huko juu. Usije ukaanza tena kuikataa biblia kwa kuwa ukianza kubadilika na kuikataa, basi haitakua na maana yoyote kwa mimi kukujibu maswali yako yote kwa kutumia kitabu ambacho kumbe wewe hukiamini. Jibu tena sasa tuendelee ndugu yangu…..

    Like

  220. Rich says:

    ndugu mhamad, mimi sifahamu mambo ya hija za wakristo kwa kuwa, kama biblia ndio ingeandika hivyo, basi ingenifaa mimi mkristo niitetee biblia yangu. Lakini kwa kuwa swala hilo mimi silitekelezi wala silielewi, basi pia siwezi kujifanya eti nawatetea wakristo, mimi siko hapa ili nitetee wakristo au udini ila niko hapa ili nitetee njia yangu ya biblia pekee aliyonipa Mungu ili nimuamini kupitia njia hiyo. kwa hiyo, ndugu Mhamad, swala la hija za wakristo hupaswi kuniuliza kabisa ila wewe inakupasa uwatafute hao wanaokwenda ili wakupe majibu. Maswali ninayojibu ni ya biblia neno la kweli la Mungu pekee na kamwe sijibu tabia fulani fulani za watu fulani…ndio maana hata swala la huyu mwenye hii blog nilikuambia pia umtafute na kumuuliza yeye mwenyewe, sio eti mimi nimjibie hapana. Mimi sitetei mtu wala dhebebu la mtu, ila ninatetea neno la Mungu pekee.

    Like

  221. Joseph says:

    FRANCIS
    Pole sana ndugu yangu. Nakushauri uache kupotoa maandiko, yale usiyoyajua uyaache, zungumza ukijuacho.
    *Petro alijulikana kama Kefa yaani – Mwamba/Jiwe. Yesu Kristo alimwambia Wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu. Alimaanisha kanisa litajengwa kupitia mafundisho ya kweli.
    *Pia Yesu Kristo alipomwambia Petro Toka nyuma yangu shetani maana huyawazi yaliyo ya Mungu ….. Alimaanisha kuwa kuna hila za shetani zimeingia kwa Petro, Kwa hiyo alimuona shetani akinena sio Petro.
    Kumbuka shetani yupo akiwajaribu watu, na mtu yeyote anaweza kujaribiwa wakati wowote hasa amchaye Mungu wa kweli. Mfano, umewahi kuona wakristo wakikemea pepo au jini limtoke mtu? Je, ukiona utasema yule mtu ni pepo au jini? Kwa hiyo, unaposoma kifungu cha biblia, lazima uzingatie vitu vifuatavyo:
    1.Mazingira
    2.soma kifungu kwa ukamilifu
    3. Historia
    Hapo ndo unaweza kupata maana halisi. Vinginevyo utachanganyikiwa.
    Yohana 14:6 Yesu anasema “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya mimi”. Hakuna mtume wala nabii aliyetamka tumfuate yeye, tutapata uzima, ISIPOKUWA Yesu tu.

    Unaweza kutunga mistari yako na kupotoa maandiko ujuavyo, lakini ukweli bila kupindisha maneno, kama unataka kwenda Mbinguni, changamka, “Njoo kwa Yesu haraka”.

    Soma maneno haya ya Yesu: Yohana 11:25 “yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi ajapokufa, atakuwa anaishi;
    Lakini Pia Soma Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”.
    Kwa hiyo, nakushauri wewe na wenzako wote, kimbilieni kwa Yesu, mpate amani moyoni. Yesu ni njia ya Uzima.

    Like

  222. Ndugu Rich,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah, na niwatakie rehma na amani mitume wake wote.

    Ama baada ya kumshukuru Allah, naomba niendelee kukuelimisha kwa kifupi kabisa kuhusu mambo yanayokutatiza kwenye uislam ili inshaallah kwa uwezo wa Allah, akupe mwanga kiumbe wake uingie katika dini yake, dini ya uislam, dini ya mitume wote wa Allah waliotangulia.

    Ndugu Rich, nikianza na hoja ya idadi ya vitabu, ni kweli kabisa kama ulivyosema kuwa katika maelezo yangu nilikuwa nikivitaja vitabu vinne yaani zaburi torati injili na quran, lakini sikusema hivyo ndivyo vitabu pekee vya Allah, bali nilitaja hivyo kwa sababu hivyo ndivyo vitabu ambavyo Allah alivitaja kwa majina lakini sio kwamba hivyo ndivyo vitabu pekee vya Allah, kwa sababu katika quran ametaja kuwa hata nabii Ibrahim alimpa kitabu ingawa Allah hakutaja jina la kitabu, lakini aliimpa kitabu, tena maelfu ya miaka kabla nabii Musa hajapewa torat, ndugu Rich, na hayo siyo maneno yangu bali Allah mwenyewe ndivyo anavyotwambia ndani ya quran soma Aya ya quran ifuatayo.

    SURA 87. SURAT AL- AA’LAA
    “16. Lakini nyinyi mnapenda maisha ya dunia!
    17. Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
    18. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
    19. Vitabu vya Ibrahimu na Musa. »

    Ndugu Rich, Allah hakuweka limit ya idadi ya vitabu vyake kwamba ni vinne tu kama unavyosema wewe, la hasha, bali vitabu alivovitaja kwa majina ni vitabu vinne, na hii ni sawa na Allah alivyofanya kwa manabii kwa sababu manabii aliowataja ndani ya quran idadi yao ni 26 tu, lakini Allah mwenyewe anasema kuna manabii zaidi ya laki moja hakuwataja majina lakini siyo kwamba hawapo lah, wapo ila kaamaua kuwataja wachache kwa majina, Ndugu Rich, kama nilivyokwisha kujibu kwamba Allah anaposema amempa nabii kitabu siyo kwamba maana yake amempa nabii huyo kitabu chenye karatasi kama vitabu hivi tulivyonavyo leo “physical paper” yaani vitabu vya karatasi, hapana, hapana ndugu yangu Rich, kitabu maana yake ni zile funuo anazokuwa anawapa manabii wake, hizo ndizo vitabu, kwa mfano tunaposema kitabu cha injili alipewa Bwana Yesu, haimaanishi bwana Yesu amezaliwa akiwa ameshikilia kitabu chenye kurasa mikononi, hapana ndugu yangu Rich, hatuwazi hivyo ! hatuwazi hivyo kabisa, ndugu Rich Mungu anaposema vitabu maana yake ni zile funuo ambazo nabii anakuwa akipewa na Mungu, na pia tunaposema nabii Musa alipewa torati maana yake ni zile funuo alizokuwa akipewa nabii Musa, kwani hata ukisoma katika biblia yako inasema kuwa nabii Musa alipokuwa akipokea funuo alikuwa akiandika katika Mbao kwa ajili ya kumbukumbu na sio kitabu cha karatasi kama tulivyo navyo leo, Ndugu Rich vivyo hivyo hata nabii wetu, Nabii Muhammad(S.A.W) alivyopewa kitabu cha Quran maana yake ni zile funuo alizokuwa akipewa na Allah kupitia kwa malaika, na kwa ajili ya kumbukumbu funuo hizo zilikuwa zikihifadhiwa vifuani mwa watu, kupitia vichwa vyao, na wengine walikuwa wakiandika katika mawe, magome ya miti na mbao. Kwa hiyo ndugu Rich tunaposema kuhusu idadi ya vitabu, kwa hakika tunaweza kuzungumzia kuhusu torati, injili , quran, zaburi lakini hatuwezi tukasema vitabu ni hivyo tu pekee na hakuna vitabu vingine.Ndugu Rich, vitabu hivi tunavyoviona leo vya karatasi ni matokeo ya mapinduzi ya technologia tu lakini siyo kwamba manabii hao walizaliwa wamevishikilia vitabu hivyo.kwa hiyo ndugu yangu swala la idadi ya vitabu nafkir tumemalizana kabisa, na tumeona ni jinsi gani Allah hakuweka limit ya idadi ya vitabu, bali amevitaja vitabu vichache tu kwa majina kwani tumeona hata nabii Ibrahim alipewa kitabu.

    Ndugu Rich, katika swali lako ulilouliza kwamba je kama kigezo cha kuwa muislam ni kuiamini quran tukuf mbona manabii wa zamani hawakuisoma quran tukuf ?Ndugu Rich swali hili nimeshalijibu mara kumi zaidi na nilishakwambia kuwa hakuna sehemu yoyote ambayo Allah alisema kigezo cha kuwa muislam ni kuiamini quran, la hasha bali Allah anasema kigezo cha kuwa muislam ni kuviamini vitabu vyake « wa kutubihi » na nikakwambia tunaposema vitabu maana yake ni zile funuo zenye sheria za Allah, na nikakwambia sheria za Allah katika vitabu vyote vya Allah zipo sawa kabisa kwani dini ya Allah ni moja na wala haibadiliki, hivyo manabii wote waliziamini na kuzitenda sheria na amri zote zilizo ndani ya quran kwani tunaposema quran hasa maana yake ni zile funuo zenye sheria na wala sio makaratasi, kwa sababu zamani hizo karatasi hizi hazikuwepo bali funuo zilikuwepo.Hivyo manabii hao walikuwa waislam kabisa kabisa. Ndugu Rich, na hayo si maneno yangu bali Allah mwenyewe anasema ndani ya quran tukuf akimwambia kipenzi chake mtukufu wa daraja Mtume Muhammad (S.A.W) katika sura ya 42.

    SURA 42. SURAT ASH-SHUURA
    13. Amekuamrisheni Dini ile ile aliyo muusia Nuhu na tuliyo kufunulia wewe, na tuliyo wausia Ibrahim na Musa na Isa, kwamba shikeni Dini wala msifarikiane kwayo. Ni magumu kwa washirikina hayo unayo waitia. Mwenyezi Mungu humteua kwake amtakaye, na humwongoa kwake aelekeaye.

    Kwa hiyo ndugu Rich, Allah anamwambia Mtume, kuwa amemuamrisha dini ile ile aliyomuusia Musa,Nuhu Yesu na Ibrahim, dini ni ile ile amri na sheria za Allah ni zile zile kwa mitume wote.

    Ndugu Rich,naomba usikihukumu kitabu kwa jina lake, bali kihukumu kitabu kwa sheria zake, tofauti kabisa na kwa upande wa wakiristo kwani tunaona amri zilizo ndani ya biblia iliyoandikwa na Paulo ni tofauti kabisa na amri za Mungu wa biblia ya kale, tofauti kabisaaaaaaaaaaaaa!Ndugu Rich, yaani mungu wa agano la kale aliweka amri na sheria ambazo yeye mwenyewe anapingana nazo katika agano jipya.Ndugu Rich, kwa hakika mungu anayejipinga yeye mwenyewe hastahili kabisa kuwa Mungu wa kweli, kwa sababu Mungu wa kweli ni lazima awe na msimamo na kauli, kwa kuwa kwa kawaida ukitaka kumjua muongo angalia kauli zake, mara nyingi kauli zake lazima zipishane, yaani leo aseme hivi na kesho aseme vile, hiyo ndiyo dalili kuu ya mtu muongo, hivyo hivyo hata yahwe sisi waislam tunamkuta na sifa hizi hizi za wanadamu, sifa za kubadili kauli hivyo kuumuingiza yahwe katika kundi la waongo. Ndugu Rich, usipotee wala kujisumbua yahwe hatakufikisha popote, kwa sababu ameshaonekana kuwa kigeugeu, atakugeuka siku ya mwisho, na atakukana hivyo utajikuta ukihitaji sana msaada Allah ambaye huku duniani unamkataa.Lakini kama kawaida Allah atakwambia kwani hakukujia mwonyaji, bila shaka utasema alinijia ndugu Yohana, mimi nikamtukana nikamwita mwendawazimu, basi Allah atakwambia ingia katika moto wa jehannam kwa vile alikujia mwonyaji na ukamtukana, Ndugu yangu Rich, mimi sitaki wewe ufike huko kote na wakati muda unao, na uwezo unao unakosa nia tu, basi jitahidi Kutafakari na Allah atakuonesha njia ya iliyonyooka, njia ya uislam.

    Ndugu Rich, naomba pia nikuulize kijiswali kimoja kidogo mno, ndugu Rich, kwa kuwa mojawapo ya kigezo cha kuwa mkiristo ni kuiamini biblia ya agano jipya, yenye vitabu vya marko, mathew,yohana, matendo mpaka ufunuo, swali langu ni je? Hata hao manabii wa zamani ambao mnadai kuwa walikuwa wakiristo wenzenu akina Ibrahim,Isaka, Yakobo, Musa, Nuhu, Luti, n.k walitumia vitabu hivyo ili tujue kweli walikuwa wakiristo wenzenu?Hebu naomba unijibu kijiswali hiki ndugu yangu kwa kuwa mimi maswali yako yote yanayohusu vitabu na manabii wa zamani nimeyajibu kwa ufasaha kabisa na wala sikuacha hata nukta.

    Ndugu Rich, pia naomba nikuulize kijiswali kingine, ndugu Rich kwa kuwa tunajua katika ukiristo kulipa kisasi ni dhambi, hutakiwi kulipa kisasi bali kusamehe, na si kusamehe tu bali ukiiibiwa chupi uvue na nepi, na si hilo tu bali kulipa kisasi ni dhambi katika ukiristo, ndugu Rich mungu wenu yahwe huyuhuyu tunaona akiwaagiza wana wa Israeli kulipiza kisasi katika (Hesabu 31:1), je hamuoni kuwa yahwe alikuwa akiwaagiza watu kutenda dhambi ya kulipa kisasi kinyume na maamrisho ya dini yake ya kikiristo?

    Ndugu Rich, pia katika suala la kwenda hija huwa kuna upotoshwaji mkubwa sana unaofanywa na mababa paroko,wachungaji na mapadre wa kikiristo wakiwadanganya wakiristo eti tunaenda kuzulu kaburi la mtume, ndugu yangu huo ni upuuzi usiotakiwa kusikilizwa hata kidogo, kwa sababu kama ni hivyo mbona hata Mtume mwenyewe alifanya hija? Je alienda kutembelea kaburi lake mwenyewe na ili hali yuko hai, je hii inaingia akilini ndugu yangu hii, kwa hiyo ndugu Rich, mimi sikulaumu ndugu yangu ila nombao uwe unatuuliza sisi waislam kupitia mitandao kama hivi na Inshallah kwa uwezo wa Allah tutakuwa tanawapa majibu sahihi kabisa, kuliko kusikiliza kauli za maadui wa uislam.

    ndugu Rich, kwa kuwa bado nina mambo mengi ya kujadiliana na wewe, naona bora niishie hapa kwa leo, ila kabla sijamaliza nikuulize vijiswali vidogo tu kuhusu hija.ndugu Rich, kwa kuwa wakiristo wote ni ndugu, na kwa kuwa si vyema kumwacha mkiristo mwenzako apotee bali unatakiwa kumkosoa ili wote mje kupata ufalme wa mbinguni, hivyo basi kwa kuwa siku hizi wakiristo wenzako wanaenda hija, naomba kusikia kutoka kwako wewe kama mkiristo mwenzao, je wewe ungependa kuwashauri nini kupitia blog hii? Je waendelee kwenda hija au waache mara moja kwa kuwa biblia haijaagiza wakiristo kwenda hija?pili kwa kuwa hija ni ibada ya waislam je huoni hao wakiristo wanaoenda hija wakiwemo wachungaji wakubwa na wengine wanajiita mitume na manabii, je huoni kuwa wanakuwa wafuasi wa waislam katika ibada hii, kwa sababu hija ni ibada ya waislam?je hao wakirsto wanaoenda hija wako sawa au wanafanya makosa?Ndugu Rich, wewe kama mkiristo naamini hautakosa la kuwashauri wakiristo wenzio katika hili suala la kwenda hija kama tunavyofanya waislam.

    Nakushukuru sana ndugu yangu Rich, naomba kwa leo niishie hapa , na karibuni nitawaletea mwendelezo wa mada jinsi biblia inavyomdhalilisha Yesu.

    Wabillah tawfiq.
    Wwahaadha ssalaam.

    Like

  223. Ndugu Joseph,

    Kwanza kabisa nimshukuru Allah, kwa vile alivyokuleta mja wake katika blog, hii ili uweze kujifunza mambo mbalimbali kupitia hoja za waislam.

    Ndugu Joseph, kwa kuwa umeguswa na moja wapo ya hoja yangu, niliyoitoa huko juu nikionesha ni jinsi gani biblia inavyoonesha Bwana Petro alivyokuwa shetani,Ndugu Joseph kwa kuwa jina hilo la shetani alilopewa bwana Petro hakupewa na mtu baki la, jina hilo alipewa na nabii wa Mungu kabisa ambaye ni Yesu ambaye mimi na wewe tunaamini kabisa kuwa alikuwa hasemi uongo bali maneno ya kweli kabisa sioni kama kuna haja mimi na wewe kuanza kujiuliza tena eti petro alikuwa shetani au la? Au sioni haja ya mtu kuanza kujenga vioja mbuzi eti kuonesha kuwa Petro hakuwa shetani na ili hali Bwana Yesu mwenyewe ashatwambia Petro alikuwa shetani, Ndugu Joseph kwa kufanya hivyo tutakuwa tunampinga Yesu waziwazi kabisa, kitu ambacho hasa wewe mkiristo kitakufanya uwe anti-christ yaani mpinga kristo kwa kupinga kauli zake waziwazi.Ndugu Joseph, mimi naamini kabisa kama kweli unampenda Yesu, huna haja ya kutilia shaka kauli zake, bali kila jambo alilosema Yesu wewe unatakiwa kulikubali wala siyo kuanza kutafuta vijisababu vya kukataa maneno yake.Ndugu Joseph mbona Yesu aliposema waongo na wezi hawatauona ufalme wa mbinguni ulikubali moja kwa moja wala hukuanza kutafuta visabababu sababu!??mbona hapo ulielewa moja kwa moja wala hukutaka kuhuoji? sasa vipi leo hii yesu anasema Petro shetani unaanza kutia doubt tena ndugu yangu?

    Ndugu Joseph, ama kwa hakika siyo kwamba Yesu alimwita Petro shetan kwa bahati mbaya, hapana bali kwa mujibu wa biblia ushetani wa Petro umejidhirisha katika maeneo mengi mno, Ndugu Joseph ukisoma katika kitabu Cha Matayo tuangalie pale Yesu na wanafunzi wake walikuwa katika chombo akiwemo na Petro bwana Yesu aliwaambiaje.

    MATAYO 8:26 Naye Yesu akawaambia, ‘Kwa nini mnaogopa, enyi wa imani haba?’ Kisha akaondoka na kukemea dhoroba na mawimbi, nako kukawa shwari kuu.

    Kwa hiyo kutokana na aya hiyo, na kutokana na ukweli kuwa kwenye chombo kile naye Petro alikuwemo, basi bwana Yesu anatwambia ni jinsi gani wanafunzi wake walivyo na imani haba yaani maanake wanaamini nusu na nusu iliyo baki hawamuamini, yaani kwa maana nyingine ni wanafiki nusu ya upendo wao ni kwa shetani na nusu wanamwamini hivyo wana imani haba sana.

    Ndugu Joseph, tukiendlea kusoma biblia hiyo hiyo ili tuone pamoja na kuwa bwana Yesu alisema kwa ujumla kuonesha kuwa wanafunzi wake wana imani haba, lakini tukiendelea mbele katika kitabu cha matayo hiyo hiyo na katika tukio lilelile tutaona kuwa Bwana Yesu aliposema hivyo alikuwa akimlenga nani hasa mwenye imani haba, hebu soma

    MATAYO 14:31Mara Yesu akanyosha mkono Wake na kumshika(Petro), akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?’

    Ndugu Joseph pamoja na ndugu Wakiristo kwa ujumla, hapo tumeona vizuri kabisa kumbe hata kule kwenye chombo bwana Yesu alikuwa aishamuona Petro kuwa yeye ana imani haba sana, yani nusu anamwamini shetani na nusu anamwamini Yesu.

    Ndugu Wakiristo, ushetani wa Petro haukuishia hapo bali tukisoma biblia katika kitabu cha (MATAYO 26:37-45) Tunaona kuwa Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa siku hiyo wanatakiwa wakeshe na yeye wakiomba , hebu ndugu mkiristo twende wote hapa tuone ni nini kilitokea, na baada yapo tutaona je bwana Yesu aliposema Petro ni shetani alisema kwa bahati mbaya au alisema kwa kumaanisha.

    (MATAYO 26:37)Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, naye akaanza kuhuzunika na kufadhaika. 38Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja name tukiomba.”

    Kwa kuwa Yesu aliamini pengine Petro angeshajirekebisha na kuwa mtu badala ya Shetani, alimchagua miongoni mwa wanafunzi wachache alioamini wataweza kufanya ibada nay eye usiku huo sasa hebu angalia katika msitari ufuatao ni nini kilitokea?

    (MATAYO 26:40) Kisha (Bwana Yesu) akarudi kwa wanafunzi wake na kuwakuta wamelala. Akamwuliza Petro, “Je, ninyi wanaume, hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?”

    Ndugu Joseph, pamoja na kuwa Bwana Yesu, alishagundua toka zamani dalili ya ushetani, lakini hapa alikuwa akizidi kupata uhakika zaidi ya ushetani wa Petro kwani inaonesha kabisa kabisa jinsi gani bwana Yesu alivyosikitika sana kuona Petro ndiye kiongozi wa mgomo! Yaani Petro alishindwa hata kutumia saa moja kutii amri ya Yesu, sisi waislam tunaamini kabisa kuwa mtu yeyote anaweza kuwa shetani endapo mtume wa Mungu anamuamrisha jambo halafu yeye halitekelezi, kabisa kabisa huo ni ushetani uliopitiliza, kwa sababu amri ya mtume siku zote inakuwa imetoka kwa Mungu hivyo mtume wa Mungu anavyokuamrisha kutenda jambo halafu ukakataa, basi hakuna jina linguine unalostahili kuitwa zaidi ya shetani, kwa sababu kazi ya shetani ni kupinga amri ya Mungu, Ndugu Joseph hivyo basi bwana Yesu alivyomwita Petro shetani alikuwa hajakosea hata kidogo.Hivi ndugu Joseph, fikiria hata wewe kwa hako kaimani walau uliko nako, assume Bwana Yesu akwambie walau tumia saa moja tu ukiomba pamoja nay eye , kweli usingizi ungekusogelea ndugu yangu? Mimi naamini hata angekwambia masaa kumi ungejipigapiga walau kwa uchache hata vijisaa viwili, je vipi kwa Petro ambaye anaheshimika mpaka leo katika ukiristo anamfanyia Bwana Yesu kitendo kibaya hivi?yaani wallah nisidanganye nilipokuwa nikisoma sehemu hiyo nikaona jinsi bwana Yesu anavyomlaumu Petro kwa kushindwa kutii amri yake, wallah nililengwa na machozi hasa inavyoonesha ni jinsi gani bwana Yesu alivyosikitka mno kwa tukio hilo la usaliti waliomfanyia wanafunzi wake nyakati hizo za Mwisho.

    Ndugu Joseph, kwa ujumla ushetani wa Petro haukuishia hapo bali tunaposoma,kitabu cha (MATAYO 26:50) pale maadui wa Bwana Yesu walipokuja kumkamata ili wamtese biblia Inatwambia hivi “ Ndipo wanafunzi wote wakamwacha wakakimbia.”hapo tunaona kabisa akina Petro walitimua mbio, tena inasemekana kwa mbio alizotokanazo Petro kama yangelikuwa mashindano ya marathon hata Yule bingwa wa dunia Usain Bolt asingefua dafu , basi hakuna aliyekuwa tiyari kuonekana yuko pamoja na Yesu. Sasa ndugu Yangu huo si usaliti wa wazi kwa Bwana Yesu aliyetumia mda mwingi kuwafundisha Imani wanafunzi wake?sasa hiyo si kazi ya shetani? Je utasema Petro hakuwa shetani?

    Ndugu Joseph, ushetani wa Petro ulizidi kukomaa siku hadi siku lakini sasa hapa ndiyo ilikuwa funga kazi, hebu soma kitabu cha (MATAYO 26:69-75), Ndugu Joseph ukisoma hapo unaona jinsi Petro alivyomkana Bwana Yesu mara tatu mfululizo, lakini ili tujue kuwa kweli bwana Yesu alimaanisha kuwa Petro alikuwa shetani wala hakusema hivyo kwa bahati mbaya kama ulivyojaribu kudanganya ndugu Yangu Joseph, Bwana Yesu alishasema “atakayenikana mimi mbele za watu na mimi nitamkana mbele za Baba”
    Kwa hiyo moja kwa moja tunajua kuwa Hivi sasa huko aliko Petro bila shaka yuko jikoni anakaangwa, wala hakuenda peponi kwa sababu bwana Yesu ashasema ukimkana hata mara moja yeye anakukana mbele za Baba yake, sasa ndugu Joseph, kwa sababu zote hizi nilizokuwekea utaanzaje kutafuta vijisababu mbuzi ambavyo havina kichwa wala mguu ili upinge kauli za Bwana Yesu,wewe huoni matukio ya Petro kumsaliti Yesu yamekuwa Mengi mno! Tena hilo la kumkana mbele za watu ndio funga kazi?

    Ndugu Joseph, kwa hiyo ni kweli kabisa mimi nakubaliana na wewe kuwa Petro ni mwamba lakini lazima tujue kuwa ni mwamba wa shetani, tena mwamba wa shetani aliyeshindikana, mpaka Bwana Yesu anaamua kuliweka kanisa juu ya mwamba huu wa shetani mpka leo kweli kabisa hii inadhihirisha ushetani wa Petro ulivyokomaa.

    Ndugu Joseph, mimi nakukaribisha katika blog hii kama una vioja oja vyako usisite kutuuliza sisi waislam tupo kwa ajili yenu, ama kwa hakika nakuahidi utaelimika mno, kama wakiristo wenzako ambao umekuta tunawaelimisha, na wanatuelewa, na wengine wanasilimu, na wengine wanakaribia kusilimu huko waliko.

    Allah akuoneshe mwanga na nuru ya uislam inshaallah.

    Wabillah tawfiq!
    Wwahaadha ssalaam.

    Like

  224. Rich says:

    Ndugu Mhamad, mimi nafikiri kuwa unataka ujibiwe hayo maswali uliyouliza. Maana ulidai kuwa uliyauliza mara kumi na hakuna mkristo hata mmoja aliye kujibu. Nianze kwa kusema kuwa, Hakuna hata mkristo mmoja, aliyesema kua, Manabii wa zamani, walikua ni Wakristo !!. Hilo ni dai lenu ninyi waislamu, kuwasingizi manabii wa zamani kua, walikua waislamu wenzenu, ili eti dini yenu, ionekane ni kongwe na ya zamani!!. Sisi wakristo, biblia haitufundishi kuwa, manabii wa zamani eti walikuwa ni wakristo wenzetu, ila, biblia inatuonyesha kua, ukristo ulianza kipindi ambacho, kilikua ni cha baadae kabisa, pale injili ya bwana yesu ilipohubiriwa kwa watu wa Mataifa. Manabii wa zamani, kamwe hawakua wakristo kama sisi, ila, wao walikaa kwenye mahekalu na masinagogi yao ya asili, wakitumia vitabu vya torati, zaburi na manabii katika ibada zao. Kwa hiyo, Sisi wakristo, agano lile la kale, hatulikatai wala kulipinga, kwa sababu, vitabu vyake vyote vya nyuma, ndivyo vimekua msingi wa imani yetu sisi wakristo. Istoshe, vitabu vile pia, ni muongozo unaotusaidia kujua, tabiri mbalimbali alizoahidi Yehoha mbele ya manabii wake, lakini pia, vinakamilisha maana ya neno, “BIBLIA”, Yaani, Mkusanyiko wa vitabu vyote vya Mungu. Pia, uliuliza kuwa, “NI VIPI SISI WAKRISTO, VITABU VYA SHERIA, TUNASEMA SHERIA ZAKE ZIMEBATILIKA KAMA NI VITABU VYETU KWELI ?, HALAFU UKATAKA NIKUPE TOFAUTI KATI YA MIMI NA FARISAYO. Ndugu Mhamad, Sheria za torati,sisi wakristo hatuziping wala kuzikataa, kwa kua, hizi ni sheria takatifu za Mungu. Labda mimi naona, tungeongelea kua, ni jinsi gani tunavyozikubali, kulingana na mpango aliotuwekea Mungu mwenyewe. Bwana yesu alisema “sikuja kuitangua torati na manabii bali kutimiza”,Soma(Mathayo 5:17). Bwana yesu, ndiye aliekuja, kutimiza sheria kwa ajili yetu. Ametimiza vipi kwa ajili yetu?, Yeye, alitekeleza mahitaji yote ya torati kwa 100%, Pasipo kufanya dhambi, na kwa njia hiyo, akatuleta watu wote katika muafaka kamili na Mungu, Soma(wagalatia 4:4-6). Kwa hiyo, Wakristo tumepokea, asili ya Mungu ambaye ni roho mtakatifu, anae tuambia kuwa, Mungu ni Baba yetu. Kwa hiyo, tunapo mpokea bwana yesu na kuokoka kupitia imani yetu kwake, hali hiyo, inamfanya Mungu kua ni Baba yetu, tunae muita “ABBA”, Yaani “BABA”, Soma(galatia 4:6)(1Yohana 3:1-3). Asili ya Mungu pamoja na sheria zake zote ni ya rohoni.Soma(warumi 7:14). Mungu ni upendo, Yeye anawapenda watu wote. Kumpenda Mungu na kuwapenda watu wote, ndiyo asili ya torati yote na manabii, Soma(Mathayo 22:35-40). Kwa hiyo,tunafuata sheria za Mungu rohoni mwetu, Lakini sio kwa sababu ya kutafuta haki, bali ni kwa sababu ya utiifu wetu mbele za Mungu, kupitia Yesu kristo ambaye, Yeye ndiye, haki yetu na amani yetu. Hebu ndugu Mhamad, Soma ile (Yohana 8:3-11). Utaona kuwa, Wale Waandishi na Mafarisayo, walipokuwa wanataka kumhukumu yule mwanamke kwa kumpiga mawe kwa kosa la uzinifu, kama torati ya Musa ilivyo amuru, Bwana yesu aliwauliza hivi “YEYE ASIYE NA DHAMBI MIONGONI MWENU, NA AWE WA KWANZA WA KUMTUPIA JIWE”. Lakini baada ya wale waandishi wa sheria na Mafarisayo kuulizwa hivyo na bwana yesu, biblia inasema “NAO WALIPOSIKIA, WAKASHITAKIWA NA DHAMIRA ZAO, WAKATOKA MMOJA MMOJA, WAKIANZIA TANGU WAZEE HATA WA MWISHO WAO, AKABAKI YESU PEKE YAKE, NA YULE MWANAMKE AMESIMAMA KATIKATI !!!. Kwa hiyo ndugu yangu Mhamad, Kumbe Yesu kristo ndiye jibu letu na thawabu yetu mbele za Mungu, Ndiyo maana Mungu alisema “SIKUWAAMBIA WAZAO WA YAKOBO NITAFUTENI BURE, Kwa kua Yeye ni Bwana, asema haki, anena mambo ya adili !!!!!, Soma(Isaya 45:19-20). Kwa hiyo ndugu yangu Mhamad, thawabu, tunaipata kwa kujua njia ya Mungu, iliyo ndani ya Yesu kristo. Hapo ndipo unaweza kuona tofauti ya Mimi mkristo nisiyekimbilia, kuwahukumu wengine, kwa sababu ya kuijua njia ya kweli ya sasa aliotukusudia Mungu ndani ya Yesu kristo, na Wale Mafarisayo ambao, walikuwa wakitaka kukimbilia kuua, na wakati kumbe wao wenyewe, walikua hawajakamilika kufanya hukumu hiyo. Lakini pia, ndugu Mhamad, uliniuliza kuwa, hivi kusingiziana katika sheria za Mungu, kumeanza leo?, hapana ndugu Mhamad, kusindiziana katika sheria za Mungu kulikuwepo tangu zamani, hiyo ni hulka au, tabia ya asili ya dhambi,….ni hali ya kutokukamilika kwa mwanadamu katika mambo yake, kwa sababu ya dhambi. Lakini sasa, baada ya huyo mwanadamu, kutengwa na Mungu kitambo, ili ajionee madhara ya dhambi na maana haswa ya dhambi na hasara zake, Mungu kwa kumtuma bwana yesu, alidhamiria kutukomboa yeye mwenyewe. Huu ulikua ni mpango wa Mungu mwenyewe, kuamua kutuokoa sisi wanadamu baada ya kuona kua, tunaendelea kufanya dhambi na kupotea, kutokana na matumizi mabaya ya wanadamu, dhidi ya sheria zake katika miili yetu. Biblia inasema kua, agano la kale ni kile ambacho, mwanadamu alijitahidi kumtimizia Mungu, Mahitaji yote ya sheria zake, kwa kutumia, nguvu na akili zake mwenyewe, ili aweze kuishi kwa hizo sheria, Soma( walawi 18:5) (kutoka 19:8)….Wakati, agano jipya ni kile ambacho, Mungu mwenyewe ndiye aliyeahidi kuwakomboa watu wake wote, baada ya kuwaona watu hao, wanaendelea kushindwa kudumu vema, kwenye lile agano lake la awali,Soma (Yeremia 31:31-34). Hitimisho: Ndugu mhamad, ninyi waislamu, hebu jiulizeni kuwa, kama Allah, aliagiza watu wakiiba, basi wakatwe mikono, mbona hatuja wahi kuwasikia hata siku moja, mkitekeleza sheria hiyo na nyingine zote kwa vitendo?!!, je, mnafuata sheria za Mungu kwa midomo tu, au pamoja na vitendo vyake, kama sheria takatifu zinavyo agiza?, na kwa hali hiyo, sisi tuliookolewa kwa neema ya Mungu mwenyewe na ninyi mnaoshikilia sheria za Mungu kwa midomo pekee, ni kundi lipi, lililokaa katika njia ya hatari au njia kama ya wale mafarisayo ambao walikua wanashikilia kutekeleza sheria za torati pasipo kujua haswa maana ya sheria na Makusudi haswa ya Mungu katika sheria zake??, mimi sijui jibu lake, ila, kwa elimu niliyokupa kidogo, inaweza kukupa tafakari nzuri ya kupata jibu ambalo, litakufumbua macho na akili yako. Mimi kazi yangu ni kujitahidi kadili niwezavyo, kwa kutumia, nguvu zangu, biidii yangu na hekima yangu, kadili Mungu, anavyonijakia na kunitumia, ili niiweke kweli yake, machoni mwa watu wote. Agizo lake alilonipa ni moja tu, nalo ni hili, “MWANANGU,UWE NA HEKIMA NA KUNIFURAHISHA MOYO WANGU ILI NIPATE KUMJIBU ANILAUMUYE, (Mithali 27:11). Nami nimemjibu “Kwa udhaifu wangu wa kibinadamu, siwezi BWANA, lakini kwa kuwa wakaa rohoni mwangu kuniongoza, nitayaweza yote kwa utukufu wa jina lako.

    Like

  225. Rich says:

    Ndugu mhamad, mimi naomba niishie hapa, kwa kua kubishana katika mambo ya imani sio hulka yetu sisi wakristo, ila lengo letu ni kuwafumbua wale ambao wako tayari kumtumikia Mungu katika njia ya kweli.Hata mtu yeyote mwenye akili, akitazama jinsi unavyojitahidi kujitetea kwa maelezo yasiyo husika, anangundua kua, swali hilo limekushinda kabisa kabisa….kilichobaki hapa ni maelezo ya kupinga na kubishana pekee!!. Usinilaumu mimi kwa kua, sie nilieandika nguzo za kiislamu, nikaviita ni vitabu na kuvitaja kua ni vinne pekee. Hata kama vingekua mia, kama mtu akikosa kimoja kukiamini, huyo hawezi kua muislamu kwa mujibu wa Allah, maana, Allah amekwisha sema kua, ili uwe muislamu ni kuviamini vitabu vyote kwa mf: 100 na kamwe sio 99, !!!. Manabii wa zamani hawakua ni waislamu wenzenu kwa kua, wao hawakuviamini vitabu vyote, vilivyo tajwa na Allah katika nguzo zake za mtu kua muislamu!!!. Lakini, pia hata kama sehemu nyingine alisema, kuviamini vitabu vyote, malaika wote….bado itakua ni malaika wote na vitabu vyote vilivyomo ndani ya nguzo zake za muongozo, na kamwe si vinginevyo. Vile vitabu vyote vidogo dogo na manabii wengine vinakua au wanakua ndani ya hivyo vitabu vikubwa vinne vilivyotajwa, na Mungu wenu Allah, na kamwe si vinginevyo!!.Sasa, kwa mfano, mimi mkristo, eti nikimbilie kuviamini vitabu vyote vya manabii wa nyuma, halafu eti niache kumuamini mtume wenu Mhamad pamoja na mafunuo yake aliyopewa kule mapangoni na mashetani, hivi ni kweli, kwa mujibu wa Allah nitakuwa na haki ya kuwa muislamu??!!, basi ndugu mhamad, huu mfano niliokupa, ndio mambo unayotaka kutumaanisha hivyo, na wakati kamwe Mungu wako hakumaanisha kama hivyo. Kuhusu hii hoja mpya ya maswali ulionipa, ukisoma hoja yangu hapo juu, basi utakua umeelewa kilakitu. Kwa ufupi ni kwamba, agano la sheria za malipizi na mambo yake yote, bwana yesu alifanya kwa ajili yetu. Sisi wakristo, hatupo tena chini ya agano la sheria za malipizi, ila bwana yesu alitukomboa na kutuleta katika agano la amani. “TUMESULUBIWA PAMOJA NA KRISTO, LAKINI TU HAI WALA SI SISI TENA BALI NI KRISTO YU HAI NDANI YETU NA UHAI TULIONAO SASA KATIKA MWILI, TUNAO KATIKA IMANI YA MWANA WA MUNGU AMBAYE ALITUPENDA AKAJITOA NAFSI YAKE KWA AJILI YETU. Soma(galatia 2:20). Kwa hiyo ndugu mhamad, sisi, katika agano lile la malipizi, ni wenye haki wa Mungu, ndani ya Yesu kristo.

    Like

  226. Rich says:

    ndugu yangu mhamad, mimi ninatamani niishie hapa, ninaweza nikakupasua kichwa bure, kwa kua, Mimi ninaamini kabisa kua, majibu mengine ninayokupa, sio saizi yako kabisa kabisa!!, labda unaweza kuchukua miaka kama 8 hivi, ili uweze kunielewa. Endelea kutafakari kidogokidogo kwanza mambo niliyo andika tangu huko juu, kabla ya kutamani mambo mapya.

    Like

  227. Ndugu Rich,
    Kwanza kabisa nimshukuru Allah, Allah ambaye alimtuma Mtume wake kwa haki, na dini ya kweli ili iwe ushindi juu ya dini zote.

    Ama baada ya kumshukuru Allah subuhana wata’aala, sina budi kukushukuru pia ndugu yangu Rich kwa jinsi unavyonipa ushirikiano katika mijadala hii, ama kwa hakika unanifanya niweze kutoa elimu ya dini ya kiislam kwa mamia ya wakiristo wanaofatilia na kusoma blog hii kupitia maswali unayouliza, lakini pia maswali yako yanasaidia kuongeza idadi ya waumini wa kiislam kutoka katika ukiristo kutokana na majibu ya ukweli na uhakika tunayowapa.

    Ndugu Rich, ama kwa hakika nimefurahi sana sana kuona unakiri na kukubali kuwa manabii wa zamani kamwe hawakuwa wakiristo wenzenu, tofauti na wakiristo wenzako waliokuwa na mtazamo tofauti kabisa na wewe ambao wao waliamini kuwa kwa kuwa majina ya manabii hao yamo ndani ya Biblia basi hao ni wakiristo wenzao, ama kwa hakika ungejitokeza mapema kwenye blog hii basi bila shaka mijadala kama hii ingeshaisha zamani, Ndugu Rich, naomba usiseme kuwa hakuna wakiristo waliosema kuwa manabii wa zamani walikuwa wakiristo wenzao kwenye blog hii, naamini kabisa kwa kauli hiyo ndugu Mhina huko aliko utakuwa umemwangusha sana kwa vile yeye ndiye aliyekuwa ameshikilia kauli kwamba manabii hao walikuwa wakiristo wenzenu, na pia itakuwa kama ulivyomwangusha ndugu Mosespk kwa kukana kauli zake waziwazi kwa kuwa yeye aliamini torati imebatilika,kumbe wewe ukasema hapana torati haijabatilika bali baadhi ya sheria ndio zilizobatilika na pia kama ulivyowaangusha na kuwalet down wakiristo wenzako wakiwemo wachungaji wakubwa wanaokwenda hija, kwa kuwakemea na kuwaonya kuwa siyo katika maandiko ya kikiristo, Ndugu Rich nina uhakika kwa kauli zako za kuwakana wakiristo wenzako wazi wazi tena kwenye blog itafikia kipindi wataacha kukuamini hivyo hawatakutuma tena uwawakilishe.tena mimi naamini ni vema haukuwa na haja ya kufanya mjadala na mimi bali mgefanya mijadala nyinyi wenyewe kwa wenyewe badala ya kutusumbua sisi waislam kutumia muda wetu mwingi kuwaelewesha.ni imani yangu mtaendelea kukataana tena kukimbiana kabisa kadri sisi waislam tunavyoendelea kuwapa hoja za ukweli.

    Ndugu Rich, kwa kuwa umekiri kwa kinywa chako kuwa yahwe hasemi lolote kuhusu dini za manabii za manabii wa zamani, bali yahwe amekaa kimya kabisa akiwaacha mtumie akili zenu kama watoto yatima, mfukie mashimo aliyo yaacha, na mjaze nafasi zilizo achwa wazi na yahwe, akiwaacha mkibishana mara wengine wanasema walikuwa wakiristo mara wengine wanakataa,wengine sheria zimebatilika wengine hazijabatilika, wengine hija ruksa wengine si ruksa, yani ili muradi tu, basi huna budi kukubali ukweli wa Allah ndani ya quran, kwa sababu Allah ashasema manabii wa zamani walikuwa waislam, na pia Allah ashasema dini yao ndiyo dini yetu na dini yenyewe ni Islam. Basi kumbe sababu ya kumpinga Allah hamna, kwa sababu ukisema manabii hawakuwa waislam nitakuuliza dini yao ilikuwa ni ipi kwa mujibu wa yahwe ndani ya biblia? Bila shaka utabaki kung’aa sharubu kwa sabbu yahwe hajakwambia.

    Ndugu Rich, pia nimefurahishwa sana kuona unakiri kabisa kuwa ukiristo umeanza juzi juzi tu hapa, tena umekiri mwenyewe kuwa ukiristo umeanza wakati Bwana Yesu aishaondoka duniani wakati wa injili kuubiriwa mataifa, basi naona ni bora umuelimishe ndugu Mhina na wakiristo wengine waliokuwa wanadai ukiristo ulianza zamani, kwa maana umetambua kuwa hata Yesu akirudi leo duniani ukiristo hautambui kwa sababu hakuacha kitu kama hicho duniani, bali ukiristo ni mambo tu ya kuzua, yaliyoletwa na mtu aliyekuwa adui mkubwa wa wanafunzi wa Yesu, aliyewataabisha na kuwauwa wanafunzi wa Yesu mtu huyo si mwingine bali Paulo na yeye ndiye aliyeanzisha ukiristo pale antiokia miaka kibao baada ya Yesu na hayo siyo maneno yangu bali biblia yenyewe ndivyo inavyosema(Matendo 11:25)

    Ndugu Rich, nikirudi kwenye majibu ya maswali yako, swali la kwanza uliuliza vipi mbona hatuoni waislam mkitekeleza sheria zilizo ndani ya quran kama kwa mfano wezi kukatwa mikono n.k, ndugu Rich, sheria za quran wapo waislam wanaozitekeleza wengi tu, sema labda wewe hujapata bahati ya kusikia au kuona au labda umesikia lakini unajitoa akili, ndugu Rich unataka kuniambia toka unazaliwa hadi unafika umri huo ulionao hujawahi kusikia mwizi amekatwa mkono kwa sheria za kiislam, au hujawahi kusikia watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja wakiuliwa kama inavyoagiza quran?Kama ni kweli hujawahi sikia mimi sikulaumu kwa sababu pengine hapo unapokaa huna hata redio, wala tv, sasa hilo sio jukumu langu mimi. Ndugu Rich, sheria za Allah zinatekelezwa mno na waislam katika maeneo mengi duniani.

    Ndugu Rich, lakini pia nakubali wapo waislam ambao hawazitekelezi sheria za Allah, kwa udhaifu wao wa imani, kwa mfano mtu anapoiba hawamkati mkono, sisi hatuwezi tukaihukumu dini ya uislam kwa kuangalia udhaifu wa watu wachache, hapana ndugu Rich dini inabaki ile ile na sheria za Allah zinabaki vilevile, uwe unazitaka uwe huzitaki , uwe unazitenda uwe hauzitendi sheria za Allah zinabaki kama zilivyo na mwisho wa siku wanaozifuata na kuzitenda hao ndio wanaofaulu. Kwa hiyo ndugu Rich wewe usikatae kuingia kwenye uislam kwa kuangalia eti mbona quran imekataza pombe mbona kuna waislam wanalewa, au uislam umekataza kuzini mbona wapo waislam wanazini, ndugu Rich hapo utakuwa unakosea kabisa ndugu yangu kwa maana hao waislam ni binadamu wa kawaida tu na siyo mitume wala manabii, wanafanya makosa kama binadamu wengine wowote wale.Wewe unachotakiwa ni kuangalia uislamu unasemaje na kutekeleza, au quran inasemaje na kufuata siyo kumuangalia Fulani na Fulani, kwa sababu siku ya kiyama Allah anatwambia kila mtu ataulizwa alichokitenda, kila mtu atahukumiwa kwa mujibu wa matendo yake.

    Ndgu Rich, baada ya kujibu swali lako vizuri mimi pia nina kijiswali kidogo. Ndugu Rich, kwa kuwa Bwana Yesu alifundisha kwamba mtu akikupiga kofi la kushoto wewe umgeuzie la kulia, mtu akikuibia pensi umpe na singlend, je ndugu Rich nyie wakiristo amri hii mnaitekeleza? Na pia je unaona hiyo amri ni sawa au inatia watu ujinga?mimi binafsi siamini kama haya maneno ni ya Yesu bali ni maneno ya wakoloni ndio walioyaingiza ndani ya biblia ili watutawale, ndugu Rich utakubaliana na mimi kuwa hakuna wema wa namna hiyo kabisaa, wala hautakuwepo bali ni ujinga na upumbaf, yaani mtu akupige kofi la kulia umgeuzie la kushoto ! kwa ujumla kauli hii inachochea machafuko na uvunjifu wa amani kwa sababu kama kweli tungeishi kwa kuitumia kauli hii bila shaka duniani kungekuwa kuna maovu yasiyo na mipaka, yaani mtu badala anapofanya kosa aadhibiwe au apewe onyo ili asirudie, wewe unamfanya tena aendelee kutenda maovu, kwa mfano ndugu Rich na wewe fikiria kama kweli umeoa, halafu ugundue mtu anatembea na mke wako, wewe badala ya kumpa adhabu inayostahili kwa kosa alilofanya wewe unamletea na binti yako, sasa hapo utakuwa umemsaidiaje mtu huyo? Au mtu anaingia dukani kwako, anakwambia leta hela zote za mauzo ya leo, wewe unampa halafu unamwambia twende wote nyumbani nikakupe hata hela ya mauzo ya jana! Kweli ndugu yangu Rich amri hii unaona inafundisha upendo au inatia ujinga na inafanya watu waone kuwa kufanya makosa ni jambo la kawaida tena jambo lenye manufaa makubwa.

    Ndugu Rich, kwa kuwa wakiristo wengi au tunaweza sema wote wameelimika sasa wamegundua kuwa amri hii ni ya kipuuzi ajabu na ndiyo maana hakuna mkiristo hata mmoja duniani ambaye alishawahi kupigwa kofi mkono wa kushoto akageuza kulia, hakuna kabisa kwani tunaona hata Bwana Yesu mwenyewe hakuweza kuitekeleza amri hii pale alipopigwa kofi, kama kweli Bwana Yesu ndiye aliyetamka kauli hii basi tungeona wakati alipopigwa kibao anageuza upande mwingine apigwe tena lakini wapi hakuweza kufanya hivyo, sasa ndugu Rich unaweza kuniambia ni kwa nini Bwana yesu alipopigwa kofi hakugeuza upande mwingine kama amri yake inavyosema? Lakini pia ndugu Rich ni kwa nini amri hii wakiristo tunaona hamuitekelezi kama kweli mnampenda Yesu?mbona tunaona mnapopigwa mnakimbilia mahakamani?

    Ndugu Rich, pia umesema kuwa bwana Yesu aliitimiza torati kwa 100% katika maisha yake hapa duniani, ndugu Rich, naamini kabisa hapa unataka kunidanganya kama kipofu au kama mtu asiyejua kusoma na kuandika kwa sababu tunavyosoma katika biblia tunaona Bwana Yesu akiipinga torati kwa 90%, mifano ni mingi lakini mfano kidogo tu angalia swala la kupiga wazinifu mawe, masuala ya kulipa kisasi, masuala ya kutoa talaka n.k, ambayo yapo kwenye torati Bwana Yesu ameyapinga waziwazi sasa utasemaje aliitimiza kwa 100% ndugu yangu na ili hali maisha yake kwa asilimia kubwa anaonekana kabisa alikuwa mpinga torati? Mimi siamini kabisa kama Yesu wa kweli anaweza kuwa mpinga torati kwa kiasi kikubwa hivi halafu litokee jitu limtetee eti ametimiza kwa 100%, hivi ndugu yangu unajua nini maana ya asilimia au unasema tu kwa sababu una uhuru wa kusema. Ndugu Rich Mtume Muhammad ndiye aliyetimiza torati kwa 100% kwani sheria zote za torati mtume kazitekeleza na siyo yesu ndani ya biblia anayeonekana kupinga torati waziwazi ili kuwafurahisha maadui wa sheria za Allah wasiotaka kutii sheria za Allah.halafu unatetea eti katimiza sheria zote za torati, hebu ndugu Yangu Rich unaweza ukanipa mfano wa sheria hata moja ya torati aliyoitimiza bwana Yesu, hebu ongea kwa mifano bwana siyo unaongea maneno ya dhahania tu na wakati biblia yenye ushahidi unayo mikononi mwako.

    Ndugu Rich, Bwana Yesu katika kuipinga torati hakuishia hapo, bali tunaona anasema hivi : 21“Mmesikia walivyoambiwa watu wa amani kwamba, ‘Usiue, ye yote atakayeua atapasiwa hukumu.’ 22Lakini mimi nawaambia kwamba, ye yote atakayemkasirikia ndugu yake wa kiume au wa kike, atapasiwa hukumu.

    Hapo tunaona bwana Yesu anasogeza karibu zaidi adhabu ya kifo kuliko ilivyokuwa kwenye sheria za torati kwa maana sheria za torati zinasema yeyote atakayeua na yeye atauwawa lakini hapo tunaona bwana Yesu hasemi kuua tu bali hata mtu akikukasirikia tu, kama ni ndugu yako anatakiwa auwawe, sasa amri hii mbona hatuoni wakiristo mkiitekeleza? Mbona hatuoni mnawauwa wanaowakasirikia?

    Ndugu Rich, tena kwa mujibu wa biblia tunaona wanawake hawaruhusiwi kunena wawapo kanisani bali kukaa kimya na kusubiri kurudi nyumbani kuwauliza waume zao kitu ambacho ni ukandamizaji wa wanawake, lakini je mbona nyie wakiristo tunaona siku hizi wanawake wananena makanisani na si Kunene tu bali kwa wachungaji kitu ambacho biblia inakikemea kwa nguvu zote.

    Ndugu Rich, pia tunaona biblia inakataza kuomba kwa kupayuka payuka kama watu wa mataifa, bali kuomba kwa utulivu kama waislamu tunavyoomba kwa utulivu, vipi nyie siku hizi tunaona ndio mahodari wa kupayuka makanisani?

    Ndugu Rich, pia kwa kuwa nyie ni wafuasi wa Yesu, nilitegemea hata utaratibu wenu wa Ibada uwe kama alivyofundisha Bwana Yesu katika biblia, je unaweza ukanionesha ni wapi Bwana Yesu alienda kusali kwa kuimba na kupiga miziki katika nyumba ya ibada kama mnavyofanya nyie?

    Nitakushukuru sana ndugu yangu endapo utajibu vijiswali hivi, ili unitoe dukuduku.

    Wabillah tawfiq.
    Wwahaadha ssalaam.

    Like

  228. Rich says:

    Narudia kwa mara ya mwisho, hakuna mkristo katika blog hii, aliefundisha kua, manabii wa zamani, walikua ni wakristo wenzetu!!!. Kama ipo kichwani mwako, basi ifute elimu hiyo. Mimi nimepitia huko juu kwa umakini sana, lakini sijaona mkristo aliefundisha hivyo, labda kama wewe mwenyewe hukuelewa kilichotaka kumaanishwa, “TUMEJENGWA KATIKA MISINGI YA MITUME NA MANABII”. Tumekua jengo mmoja au kitu kimoja au njia mmoja na Manabii wa nyuma. Soma(efeso 2:20-22). Mwisho, bwana yesu ni kweli alitimiza torati na manabii kwa ajili yetu, pasipo kufanya zambi, kama alivyoahidi kwenye ile (mathayo 5:17). Soma maandiko yafuatayo kwa ushahidi zaidi. (Yohana 7:19)(Yohana 8:46) (ebrania 4:14-15). Yeye bwana yesu, yale mambo aliyokua anayafundisha, yalikua ni mambo yanayohusu injili, na kamwe hayakua mambo ya torati. Sasa ndugu mhamad, ukisema kua, alitengua torati ambayo alikwisha itimiza, hivi unataka tukueleweje!!. Yaani yeye ni mkombozi halafu wewe unataka atufundishe mambo ya torati ya agano la kale tena!!!!. Agano la kale lilikuwa na mwalimu wa agano hilo ambaye alikua ni Nabii Musa, lakini agano jipya mjumbe wake au mwalimu ni kristo yesu. Biblia inasema “Torati ilitolewa kwa mkono wa Musa bali neema na kweli zimekuja kwa mkono wa yesu kristo”, Soma(Yohana 1:17). Ndiyo maana biblia inasema “KWA MAANA DHAMBI HAITAWATAWALA NINYI, KWA SABABU HAMUI CHINI YA SHERIA, BALI CHINI YA NEEMA”, Soma(Warumi 6:14). Bwana yesu alikuja kufundisha mambo ya adili, haki na upendo kutoka kwa Mungu, na kamwe hakuja kufundisha mambo ya torati na malipizi yake kama Musa. Ndio maana agano jipya, linaitwa agano la amani kwa watu wote, kwa kua ni Mungu mwenyewe ndiye aliyefanya kwa ajili ya watu wake wote. Bwana yesu alitufundisha kua, tusiwe watu wa kulipiza visasi bali tuwe ni watu wanaopenda kusamehe, kwa kua, hata Baba yetu wa mbinguni, hutusamehe sisi mara nyingi mno pale tunapo mkosea. Huo sio ujinga na upumbavu kama unavyofikiri ndugu yangu mhamad, bali, tabia hiyo, humfanya adui akuheshimu zaidi na kukuogopa kama ni kweli utasimama si kwa sababu ya ujinga bali kwa sababu ya haki.Na hiyo ndiyo haswa tabia ya Mungu mwenyewe…..”BWANA, KAMA WEWE UNGEHESABU MAOVU, EE BWANA, NANI ANGESIMAMA? LAKINI KWAKO KUNAMSAMAHA, ILI WEWE UOGOPWE. Soma( Zaburi 130:3-4). Kwa mfano ndugu mhamad, hebu chukulia ninyi waislamu mlivyokua mkichoma makanisa na kunywa divai zetu na mikate ya bwana kwenye madhabau!!, Sisi, tulisisitizwa na viongozi wa dini kua, tusimame katika neno la kristo, kutolipiza visasi, matokeo yake hata wewe unayaona, ni viongozi wa dini zote, kupendana, hata kufikia wakati kukaa pamoja ili kujadili mambo mbalimbali ya maisha. Je, huoni kua, kusamehe kwa wakristo na kutolipiza kumeleta upendo na amani zaidi? Au ndugu mhamad, wewe ulitaka wakristo tuwalipizie ninyi waislamu ili tuvuruge amani ya nchi??. Basi, hizo ndizo faida za kutopenda kulipiza kisasi, kwa kua, tukifanya hivyo, tutamfurahisha Mungu wetu pamoja na wanadamu tunaoishi nao. Ndugu mhamad, mimi naomba niishie hapa. Sina cha ziada. Nakushukuru sana kwa kua, kupitia wewe, naamini nimeihubiri vya kutosha injili ya Bwana. Usikubali kufa na dini yako ya uislamu, kwa kua, hakuna uzima wa milele huko, bali ni msiba mkubwa mno unawangojea. Bwana yesu ndiye kila kitu ndugu yangu, mtu wala kiongozi yeyote yule asije akakudanganya. Lakini pia unisamehe kama nilikukwaza katika mijadala yangu yote niliokuandikia kwa kua ni udhaifu wa kibinadamu tu. Asante.

    Like

  229. Rich says:

    MAMBO MUHIMU MNO YA WAISLAMU KUTAKIWA KUJUA: Torati sasa imekua ya rohoni kwa ajili ya kudumisha upendo na kuithibitisha haki ya Mungu na kamwe sio kwa ajili ya mwiii ili kuitekeleza haki ya Mungu. Bwana yesu alitimiza torati yote katika mwili kwa ajili yetu, yaani ali iishi katika maisha yake hapa duniani bila ya kutenda dhambi.Soma(warumi 8:1-8). Baada ya hapo, inakua, kwenye vitabu vya injili, hatufundishwi tena mambo ya torati ile, bali tunafundishwa mambo ya injili ya agano jipya la amani la Mungu. Narudia tena, tusimlaumu bwana yesu kua, alitengua torati ya Musa, kwa kua, yeye hakuja kufundisha torati, bali alikuja kufundisha injili pekee. Tazama alivyokua anawaambia wayahudi kuhusu mambo ya torati “MSIDHANI KWAMBA MIMI NITAWASHITAKI KWA BABA, YUKO ANAYEWASHITAKI, NDIYE MUSA, MNAYEMTUMAINI NINYI. Soma(Yohana 5:45). Pia soma(Yohana 7:19). Pia yule mtume wetu Paul,waislamu wanae muandama na kumsingizia kua, amebadili sheria za Mungu, Yeye kama bwana yesu pamoja na mitume wengine wote kwenye agano jipya, hawakufundisha mambo ya torati ya Musa tena bali wao, kama bwana yesu mwenyewe, walifundisha injili neno la Mwisho la Mungu la uzima kwa watu wote hapa duniani. Ndio maana Paul, katika ile (galatia3:3), aliwakemea wagalatia kwa kuwaambia”JE” MMEKUWA WAJINGA NAMNA HII? BAADA YA KUANZA KATIKA ROHO, MNATAKA KUKAMILISHWA SASA KATIKA MWILI ?. Swali hili pia, linawafaa sana ndugu zetu waislamu wanaotaka kukamilishwa katika taratibu za kisheria za mambo ya mwili. Yehova katika neno lake, anataka tuwe ni watu wa kuzitafakari nyakati zake.Bwana mhamad aliniuliza kua, je, kwa hali hiyo, wakristo mwa batilisha sheria?, hapana ndugu yangu, kwa halh hiyo, sisi wakristo, “TWAITHIBITISHA SHERIA KUPITIA MWANA WA MUNGU ALIYEKUJA KWA AJILI YETU ILI KUTUKOMBOA. Soma(warumi 3:31) linganisha na (isaya 42:21). Maswali ya kitoto kama ulivyo kiri wewe mwenyewe, sikuyajibu ila niliwaachia na watoto nao wakujibu, pale watakapopitia blog hii. Au kama utaona kua nimekwisha yajibu basi itakua ni vizuri.

    Like

  230. Ndugu Rich,

    Namshukuru Allah aliyemteremshia mja wake Nabii Muhammad(S.A.W) kitabu cha quran, kinachowabashiria waumini makazi mema ya peponi, na kinachotoa onyo kwa wale wote wanaosema Mwenyezimungu ana mtoto yaani wakristo.

    Ndugu Rich, ama kwa hakika nimefurahishwa sana na ushiriki wako kwenye mjadala huu kwa muda wote uliojitolea muda wako kujaribu kulisaidia jahazi la dini ya kikiristo lililokwisha zama, mimi nakupongeza kwa vile msimamo wako umekuwa upande wa waislam tunaosema manabii wa zamani hawakuwa wakiristo wenzenu, bali walikuwa waislam wenzetu, na nimependa zaidi ulipokiri kuwa ukiristo ni dini iliyoanza juzi juzi tu hapa, na ili hali uislam ni dini waliyokuwa nayo mitume Wote wa Allah sub-hana wata’ala, ndugu Rich kwa kweli umetanzua mtanziko mkubwa baina yangu na Ndugu Mhina ambaye ukisoma maelezo yake alikuwa anadai hao manabii ni wakiristo wenzenu mimi sina haja ya kunukuu ila naomba usome mijadala niliyofanya na ndugu Mhina mwezi December,

    Ndugu Rich, umenifurahisha sana pia ulivyowakemea wakristo wenzako kwa nguvu zote, wakiwemo wachungaji wako, mababa paroko, mitume na manabii wa uongo wote wa kikiristo wanaoiga ibada yetu ya kwenda hija kwa bahati nzuri bila kujua wakapata bahati ya kutimiza moja wapo ya nguzo ya uislam,wewe ukawakemea kwa nguvu zote ukasema no, hapo wanakuwa wafuasi wa kiislam.

    Ndugu Rich, kwa kuhitilafiana huko kwa wakirsto baada ya waislam kuwapa hoja za nguvu hakujaanza leo bali hata enzi za Mtume Muhammad kulikuwepo pale mtume alipokuwa akiwapa hoja wakirsto mpaka wanaanza kutofautiana wenyewe na mwisho wa siku wengine wakawa wanaona ni bora wawe waislam kwa sababu yahwe alikuwa hawapi majibu ya kutosha kuwaridhisha

    Ndugu Rich, pamoja na hayo ningependa nimalizie kwa hoja yako ya mwisho uliyojitahidi kutoa ukitetea kauli ya yesu ndani ya biblia aliyosema “ukipigwa kofi mkono wa kushoto geuza kulia ukipigwa kulia geuza kushoto” ndugu Rich, ukubali ukatae kauli hii hakuna mkiristo anayeweza kuitekeleza duniani , bali hata Yesu mwenyewe alishindwa kabisa kuitekeleza amri hii aliyoitoa mwenyewe.

    Ndugu Rich, kwa kujitahidi kutetea amri hii , ukatolea mfano wa makanisa yaliyochomwa ukasema eti mngeamua kulipa kisasi ingekuwaje? Hivyo mliamua kusamehe. Ndugu Rich ukisoma vizuri na kuilewa kauli hii ya Bwana Yesu haizungumzii kabisa suala la kusamehe hata kidogo, kauli hii inachokimanisha sio kusamehe bali ni kupigwa upande mmoja na kugeuza upande wa pili ili upigwe tena, kwa hiyo hata nyie wakiristo kama kweli mnaamini katika amri hii bila shaka yalipochomwa makanisa yenu, mngetafuta hata makanisa mengine mkawaita wale waliochoma makanisa ya kwanza ili wachome tena makanisa mengine, hiyo ndiyo maana ya kauli ya kipumbaf hii iliyo ndani ya Biblia ambayo iliwekwa na wakoloni ndani ya biblia ili watutawale na wachukue resources zetu kwa kisingizio eti Yesu ndiye aliyesema vile, na hiyo kauli iliwasaidia sana wakoloni kuitawala afrika na kuiba maliasili na rasilimali zetu, kwa kigezo cha kuanzisha mission na kujenga makanisa kwa wingi huku wakfundisha watu ujinga.

    Ndugu Rich mimi ningewaona wa maana sana kama mngechomewa kanisa moja mkawapa na mengine ili wayachome, tena hapo tungewaona amri hii mnaitii kumbe nyie wenyewe mshaiona ilivyo ya kipumbaf tena haitekelezeki ndio maana hakuna mkiristo hata mmoja anayeweza kuitimiza.

    Ndugu Rich, lakini pia umegusia suala la kuchoma makanisa, mbona wakirsto walivyochoma msikiti huko Mbeya, wakitaka kuchinja mbona hiyo hujaisema ndugu yangu? Mbona sisi waislam tulikaa kimya? Au kwa sababu nyie vyombo vya habari huwa vinawabeba kiasi kwamba hata mapadre waliopigwa risasi kwa kudhulumu hela ya wauza madawa ya kulevya na wao eti mnasingizia kuwa waislam ndio waliowauwa, kwa nini msizuie viongozi wenu waachane na biashara ya madawa ya kulevya?

    Ndugu Rich, lakini pia imenishangaza sana nchi uonevu wenu kwa waislam, pale mnapofanya matukio nyie wenyewe halafu mnasingizia waislam kwa mfano kule Arusha kuna bomu lilipuka kanisani na kuuwa watu watatu, vyombo vyote vya habari viliandika eti waliofanya vile na waislam waarabu waliokuwa wamevaa kanzu, masikini wakakamatwa waarabu wote waliokuwa wapo Arusha kwa kipindi hicho, lakini mwisho wa siku anakuja kukutwa na hatia alikuwa ni kijana Mkiristo aliyeitwa Victor Ambrose. Sasa Ndugu Rich utasemaje wanaochoma makanisa yenu ni waislamu? Mbona huyo victor Ambrose alikuwa mkiristo mwenzenu?

    Ndugu Rich, lakini pia tumeona mwaka 2011 wakiristo wamempiga na kumuua kijana Jumanne Idd kule Shinyanga, pale alipokwenda kuripoti polisi kuhusu kanda ya kwaya ambayo serikali ya mkoa wa Shinyanga iliipiga marufuku kwa sababu ilikuwa inaukashifu uislamu.wasabato walimpiga na kumuua mbona sisi waislam, tulikaa kimya au kwa sababu vyombo vya habari %90 vinaegemea upande wa ukiristo? Hivyo matukio yanayohusu waislam na uislam hayawashughulishi?

    Ndugu Rich, tukizungumzia masuala ya kukojolea na kuchoma quran hayo ndiyo usiseme kwani kwa hapa nchini limeshakuwa jambo la kawaida, mwaka 1992 mwanamke mmoja wa kikiristo aliwaita waandishi wa habari na akaichoma quran, mwaka juzi tumeona kijana wa kikirsto akikojolea quran na matukio mengi tu hapa nchini ya namna hiyo yamekuwa yakishamiri, mbona hayo hujayaongelea ndugu yangu? Hivi ndugu Rich nikuulize ushawahi sikia muislam yeyote Yule kakojolea au kachoma biblia? Ushawahi sikia wapi hebu ndugu yangu? Je huoni kuwa uislam umejengwa juu ya misingi ya heshima tunaheshimu vitabu vyenu vya ibada lakini nyie heshima hiyo hamna kabisa, nah ii mimi siamini kuwa inatokea kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya mafundisho ya chuki dhidi ya uislam mnayofundishwa makanisani, nakumbuka hata mimi nilivyokuwa mdogo, kwenye parokia moja tulikuwa tukifundishwa chuki chuki tupu dhidi ya uislam, tena nilikuwa mtoto mdogo lakini bado nakumbuka sana.

    Mwisho ndugu yangu Rich, mimi nakushukuru kama umeamua kuishia hapa ni sawa kabisa mimi sina kipingamizi, lakini naomba pia usisite kujitokeza tena endapo ukiguswa na mada mbalimbali tutakazokuwa tukiendelea kuzijadili humu ndani, Kitu cha muhimu ndugu yangu Rich, ni kuzingatia yale niliyokufundisha nina uhakika utafaidika sana na huwezi jua pengine Allah anaweza akaleta nusra yake na wewe siku moja ukawa muislam,yote tumwachie Allah yeye ndiye mjuzi wa siri na dhahiri.

    Ndugu Rich, namalizia kwa kusema nashuhudia ya kwamba hakuna Mola Apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah na Mtume Muhammad ni Mtume wake, na yeye ni mwisho wa mitume wote wa Allah.

    Wabillah tawfiq.
    Wwahaadha ssalaam.

    Like

    • Paul Michael says:

      kwa waislam wote

      Sisi wakristo tunaamini Mtume wenu muhamad alikua nabii wa uongo sababu tunazo nyingi. Katika quran 53:19:20,,,,,muhammad aliisifu na aliisujudia miungu mitatu ya kipagani LATI,,UZZA,,,na MANNAT,,,,watu wapagani wa kabila lake muhammad maquresh wakasema hatujawahi kumuona muhammad akiisujudia miungu yetu kama alivyo fanya leo. Kwa kuanzia na point hii mtume muhammad nabii wa waislamu alikua na bii wa uongo ambaye shetani aliweka maneno yake katika kinywa chake,,,,,Muislam yoyote hawezi kupinga ukweli huu,,,

      Like

      • shaaban says:

        HYO AYA NI HIYO HAPO SJIUI NDUGU YANGU HUAJAIELEWA WAPI KWA SABABU IPO WAZI KABISA…………
        19. Je! Mmemuona Lata na Uzza? 19

        20. Na Manaat, mwingine wa tatu? 20

        21. Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake? 21

        22. Huo ni mgawanyo wa dhulma! 22

        23. Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.23

        24. Ati mtu anakipata kila anacho kitamani? 24

        25. Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.25

        Like

      • mpalestina says:

        ndugu yangu hizo haya umepewa hapo chini na ndugu shabani haya tuoneshe huyo muhammad(s.a.w) alipo hisujidia hiyo miungu! kiko wapi aibu imekukumba ndugu yangu hata la kujibu huna ,hivi ninyi ndugu zangu mmepotea wapi? mpaka mkauchukia uislamu kiasi hiki wakati uislamu unakuelezeni ukweli! hivi wewena akili yako unaweza kuamini fundi seremala ndio mungu wako? MARKO 6-3

        Like

  231. Rich says:

    Oky, ijapokua, umeninukuu kwa kunisingizia mambo ambayo, siku yasema. Naomba Mwenyezi Mungu, akusaidie Sana sana ndugu yangu!!.

    Like

  232. we muslims r ready to share

    Like

  233. Omari says:

    Njia bora ni uIslamu kwa sababu ni dini yenye mtiririko mzuri wa mahadili na ni dini ya kw
    eli.

    Like

    • Steven k says:

      Maadili gani hayo unayoyazungumzia wewe?!!, Mimi jambo linalonisikitisha sana kuhusu maadili ya dini ya kiislamu ni ile hali ya kuona kua, heshima ya ndoa inalindwa kupitia upande mmoja wa wanawake. Unakuta, Mwanamke anatakiwa alinde heshima ya ndoa kwa kutakiwa kua muaminifu wa Mume mmoja, lakini kwa upande wa Mume Yeye si lazima kulinda heshima ya ndoa yake, ndio maana anaruhusiwa kuongeza wake wengine watatu zaidi ndani ya nyumba yake, ambapo Pia, akikasirika hata kwa jambo lake binafsi la kipuuzi, Allah amempa mamlaka ya kumuacha mke wake yeyote katika wale alio waoa, huku Allah akilichukulia jambo hilo kua ni la haki, ilimradi huyo anaejiita Mume bora ameamua hata kama maamuzi yake hayo, si ya haki !!!. Jambo langu jingine lisiloniingia akili kuhusu maadili ya dini ya kiislamu, ni… eti, kile kitabu cha Mungu ambacho ndicho kingetumika kuwaongoza watu kwa hekima, busara na huruma katika kuamua magomvi yao, unakuta kinafundisha kuhukumu na kuumiza watu wake kwa kumpa mamlaka shekhe ya kusoma kisomo ambacho kinauwezo wa kumtia mtu kichaa na uwendawazimu kwa sababu kisa chake labda eti mtu fulani kaibiwa mali yake au labda kaonewa!!!. Hili nalo ni shida kwangu kuniingia akilini, maana mimi ninavyojua na kuamini ni kwamba, kazi ya Mungu wa kweli ni kujenga na kamwe sio kubomoa. Sasa basi, kama watu wanapewa mamlaka ya kubomoa na kuharibu wengine kwa kutumia vigezo vya neno la Mungu badala ya kujenga hao watu wake, hili jamani haliingii akilini na pia, huyo Mungu kamwe hawezi kua Mungu wa kweli, wa haki na maadili.

      Like

    • AH WAPI BROO ? UISLAMU NI WA KWELI KVP NIPE UKWELI UNAOUAMIN NIPE AMRI KUMI ZA MUNGU ZISEMAVYO ALAFU NIELEZE MTUME MOHAMMAD NDO NANI ? NA KWA SASA YUPO WAPI ?

      Like

  234. RUNGU LA YESU KRISTO says:

    waislam katika bible wanaamin zabur, torati na injili wanasema ndo vitabu vya kweli na kuruani yao….swali langu ni je, kama mnaamni torati sasa ni kwa nini amtoi sadaka ya kuteketezwa ya kondoo na mbuzi kama torati ilivyoelezea?na kama mnaamin zaburi vip kuhusu zaburi 82:6?

    Like

  235. RUNGU LA YESU KRISTO says:

    mungu wa waislam ukimuomba lazima ugeukie kibla la sivyo umefanya sifuri….sasa huyu ni mungu gan ambaye yupo kibla?kama cku ukipigwa kabali upande mwingine ambao co kibla utamuombaje?

    Like

  236. Isaac says:

    SIJUI ni Mpe nini Huyu Ndugu Mhina Ubarikiwe sana sana tu JEHOVAH akuongoze kwenye Uzima wa milele”””””” unaijua Biblia hadi unanikosha ndugu Mhina, sidhani kama kuna mtu wakushindana na wewe kwenye blog hii wala hatatokea kwenye Sayari hii Be Blessed!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    Like

  237. Isaac says:

    Barikiwa Mhina

    Like

  238. Eliya Herbert says:

    Nimeipenda hii shule

    Like

  239. Dismas Aretas says:

    HAPA MUISLAM HAKANYAGI’ MOTO WA YESU UKO JUU.

    Like

  240. shaaban says:

    poleni sana msipomuelewa ndugu yangu mohammed yohana…hamuelewi tena nyie,,,subirini moto tu.

    Like

  241. haji abdalah says:

    Yote maisha ndugu 2situkanane

    Like

  242. Isaac says:

    Nilikua kipofu wa Moyo ila nashukuru sana Mungu alinipitisha kwenye Blog hii namshukuru sana Ndugu M.Mhina kwa kunijenga kiimani upya Ubarikiwe sana sana tu sina cha kukupa. Ila JEHOVAH akulinde milele Haleluya!!!!!!!!

    Like

  243. johnson kashushura says:

    naomba ndg wakristo muwe mawakili wa kuwaelimisha ndg zetu wa mama mdogo hawakujaliwa roho mtakatifu mioyoni mwao yesu hakumkemea petro alimkemea yule roho mchafu aliyemuingia ambaye kwao waislam ni mlinzi wao ndio maana quran imeelekeza namna namna ya kusoma aya ya kuyaita maruhani na majini huyo ndiye aliyemuingia petro yesu akagundua akaikemea ile naomba ndg wakristo muwe mawakili wa kuwaelimisha ndg zetu wa mama mdogo hawakujaliwa roho mtakatifu mioyoni mwao yesu hakumkemea petro alimkemea yule roho mchafu aliyemuingia ambaye kwao waislam ni mlinzi wao ndio maana quran imeelekeza namna namna ya kusoma aya ya kuyaita maruhani na majini huyo ndiye aliyemuingia petro yesu akagundua akaikemea ile naomba ndg wakristo muwe mawakili wa kuwaelimisha ndg zetu wa mama mdogo hawakujaliwa roho mtakatifu mioyoni mwao yesu hakumkemea petro alimkemea yule roho mchafu aliyemuingia ambaye kwao waislam ni mlinzi wao ndio maana quran imeelekeza namna namna ya kusoma aya ya kuyaita maruhani na majini huyo ndiye aliyemuingia petro yesu akagundua akaikemea ile naomba ndg wakristo muwe mawakili wa kuwaelimisha ndg zetu wa mama mdogo hawakujaliwa roho mtakatifu mioyoni mwao yesu hakumkemea petro alimkemea yule roho mchafu aliyemuingia ambaye kwao waislam ni mlinzi wao ndio maana quran imeelekeza namna namna ya kusoma aya ya kuyaita maruhani na majini huyo ndiye aliyemuingia petro yesu akagundua akaikemea ile roho

    Like

  244. Shadrack batoromeo binno

    Like

  245. kasoga says:

    Ni mafundisho mazuri hususani kwangu ambaye ninatafuta ukweli kuhusu dini kiislam

    Like

  246. Mhina says:

    UFAHAMU MWEMA: YESU KRISTO “MWANA WA MUNGU NA NENO LA MUNGU”. Waislamu wengi wamekua wakiniuliza kua, Yesu kristo ni nani haswa?…nami nimeona nirudi kwenye blog hii, kwa kazi moja tu, ya kutoa jibu langu kulingana na Biblia takatifu. Yesu kristo ni “MWANA WA MUNGU” ambaye, Mungu mwenyewe amesema na sisi kupitia njia ya mwanae, “MIMI NITAKUA KWAKE BABA, NA YEYE ATAKUA KWANGU MWANA, Soma(Waebrania 1:1-2 , 5).(Zaburi 2:7). Biblia kumhusu Yesu kristo inasema hivi: ” Amedhihirishwa kwa uweza kua mwana wa Mungu kwa jinsi ya roho ya utakatifu, Soma(Warumi 1:4). Mungu alidhihirishwa katika Mwili “AKAJULIKANA KUA NA HAKI KATIKA ROHO” Soma(1timotheo3:16) (Yohana 1:18), ndiyo maana Bwana yesu pia anaitwa “NENO LA MUNGU” Kwa kua katika yeye au “KWANJIA YAKE” akiwa ndiye neno la Mungu, ndipo Mungu nae aliuumba ulimwengu na vitu vyote, vinavyoonekana na visivyoonekana, Soma(wakolosai 1:16) linganisha na (Ufunuo19:13). Je, ni kweli?, ndiyo ni kweli kwa kua tunafahamu ya kwamba “KWA IMANI ULIMWENGU ULIUMBWA KWA NENO LA MUNGU, HATA VITU VINAVYOONEKANA HAVIKUFANYWA KWA VITU VILIVYODHAHIRI ” Soma(Waebrania 11:3). Biblia inasema kua, Mungu kwa “neno lake” akasema: “IWE NURU” ikawa nuru, Soma(Mwanzo1:3-5). Neno la Mungu ni Mwanga na taa ya njia zetu na “NURU YA UZIMA” Soma(Zaburi 119:105). Yesu kristo ndiye neno la Mungu na nuru ya uzima “NAYE NENO AKAFANYIKA MWILI ” Soma(Yohana 1:14) Linganisha na (Yohana 8:12) (Yohana 12:46-50). Hapo Mwanzo, neno alikua Mungu kwa kua ni Mungu Mwenyewe ndiye aliyeumba ulimwengu wote huu kwa “Neno lake hilo” Soma(Zaburi 33:6), ndiyo maana neno nae, bado alikua kwa Mungu, Soma(Yohana 1:1-5). Lengo kubwa kabisa la Mungu kwa Mwanae Yesu kristo, lilikua ni “KUTAKA YEYE ATUKUZWE NDANI YA MWANA WAKE” Soma(Yohana 14:13)(Yohana 5:43) Linganisha na (Isaya 9:6). Kwa hiyo, Sisi wote tukiwa ni watoto wa Mugu, Kwakweli hatupaswi kabisa kukiri kwa kuwaambia watu wa Mataifa kua, eti Yesu kristo ndiye Mungu muumba mbingu na vyote, HAPANA, isipokua inatupasa tukiri na kuwaambia watu wa mataifa kua, Yesu kristo ni “MWANA WA MUNGU” ili na sisi tuwe “WANA WA MUNGU” ndiyo maana Biblia inasema hivi: “KILA AKIRIYE YA KUWA YESU NI MWANA WA MUNGU, MUNGU HUKAA NDANI YAKE, NAYE NDANI YA MUNGU” Soma(1Yohana 4:15) Linganisha na(1Yohana 3:1-2).Hata Yesu kristo mwenyewe, alikuwa akijiita mwana wa Mungu mara zote, lakini wayahudi ndiyo waliokua wanamsingizi kuwa anajiita yeye ni Mungu ili wamsingizie kua “AMEKUFURU” kwa hiyo, hatupaswi kabisa kunaswa na ule mtego wa wayahudi kama wahubiri wengi leo wanavyofundisha!!. Soma kwa makini (Yohana 10:33) Linganisha na (Yohana 10:36). Ukweli ni kwamba, tangu zamani, majina Mungu\ Miungu, Mwana wa Mungu Yalitumika kibiblia tangu zamani kwa wale waliojiliwa na Mungu mwenyewe,(YEHOVA) kwa njia ya uwezo wa roho mtakatifu wa Mungu, lakini haikua na maana kua wao ni Miungu au Mungu kama Yehova hapana, ila walipewa uwezo wa uungu ili Baba mwenyewe atukuzwe ndani yao. Soma(Zaburi 82:6-7) (Yohana 10:34-35). Nitatoa mfano wa kweli ulio wazi kwa nabii Musa, Mungu alivyomjilia kwa uwezo nabii Musa awe kama Mungu, kamwe haikumaanisha kua, Musa ndiye Mungu muumba mbingu na vyote, ila Mungu alitaka “ATUKUZWE NDANI YA NABII MUSA” hiyo ndiyo tabia ya Mungu isiyojulikana na watu wengi sana ya kua, Mungu ni “ROHO” aabudiwaye na kutukuzwa rohoni. Soma kwa makini, (Kutoka 4:16-17) (Kutoka 7:1) (Kutoka 9:16)…..Vivyohivyo, Mungu alitaka atukuzwe ndani Ya Mwana wake wa Pekee kabisa Yesu kristo, Soma(Yohana 14:13) (Yohana 5:43) (Isaya 9:6). SWALI MUHIMU LA KUJIULIZA: je, Bwana yesu anayo ya ziada na ya kipekee, aliyotufanyia na kutuletea kuliko manabii na mitume wote?…Jibu ni rahisi tu, NDIYO, Tena bila Yeye, haiwezekani kabisa sisi wanadamu, kupatanishwa na Mungu. Bwana Yesu ndiye “CHEPEO YA WOKOVU NA UPANGA WA ROHO AMBAO NI “NENO LA MUNGU, Soma(Waefeso 6:17) Linganisha na masomo yafuatayo: (Isaya 59:17) (Isaya 11:4) (Isaya 49:2) na (Isaya 51:16). Ndiyo maana, Biblia kumhusu Bwana yesu kwenye (Ufunuo 19:15), Inasema: “NA UPANGA MKALI HUTOKA KINYWANI MWAKE ILI AWAPIGE MATAIFA KWA HUO!!!, Na jina lake anaitwa “Neno la Mungu” Soma(ufunuo 19:13). Kwanini?, ni kwa sababu, neno la Mungu ndilo roho na kweli itakasayo, mwili haufai kitu, Soma(Yohana 6:63), ndiyo maana Yesu kristo kwa kua ndiye neno la Mungu, alijitoa wakfu yeye mwenyewe ili na sisi wanadamu, tutakaswe na ile kweli iliyomo ndani yake. Soma(Yohana 17:17-19). Kwa kujitoa kwake huko kwa ajili Yetu “anakua amefanya tendo la utakaso na upatanisho kati ya Mungu na wanadamu wake katika maagano” ndiyo maana biblia inatuambia hivi: KATIKA MAPENZI HAYO, MMEPATA UTAKASO KWA KUTOLEWA MWILI WA KRISTO MARA MOJA TU, Soma(Waebrania 10:10), kwa nini?, Kwa sababu, Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi, ili manabii wote wa nyuma wasikamilishwe pasipo sisi, Soma(Waebrania 11:40). BASI VITU VYOTE VIKIISHA KUTIISHWA CHINI YAKE (Mwana), NDIPO MWANA MWENYEWE NAYE ATAJITIISHA CHINI YAKE YEYE ALIYEMTIISHA VITU VYOTE (Mungu), ILI KWAMBA MUNGU AWE YOTE KATIKA WOTE, Soma(1Wakorintho 15:28). HITIMISHO: Kwa hiyo, ndugu waislamu, Yesu kristo haswa kwa sisi wakristo ni “MWANA WA MUNGU” aliyekuja duniani katika mwili ili kuukomboa ulimwengu na kufanya mapenzi ya Mungu Baba aliyemtuma. FULLSTOP!!!. Waislamu Njooni kwa Yesu. Mbarikiwe wote mliyesoma jibu hili.

    Like

  247. shewa says:

    Tumeisha watambuwa vizuri sana waislam! Muko wapinga Kristu munataka Wakristo wawafuate kuzimuni?

    Like

  248. Sheikh Mstaafu says:

    Mungu Awabariki Kwa Huduma Yenu Nzuri.

    Like

  249. alfa says:

    waislam kama kawaida yao kupindua maandiko ili kutetea dini chafu,wameanza kudai kabur la musa liko palestina na eliya hakupalizwa mbinguni,ni kwamb wayahoud na wakrist waliokuwa tangu zama za zama hawakuyagundua bal wao wameibukia cjui wapi,juz tu hapo ndo wameyagundua,hawa wa2 wa allah wanatia huruma,kwa faida someni mwanzo na agano la kale mpate faida,mwili wa musa umechukuliwa mbnguni na elia alichukuliwa na upepo wa kisulisuli mbele ya elisha,shaabani acha pumba,tatizo lenu mmezoea kuabudu miungu xo mnazuxha ni makabur ya manabi wa israel kumb majini yenu,tumieni uongo wenye akili,MUHAMAD NDIYE KAOZA KA BIBI ZANG NA BABU ZANG,halaf hakuna ardh ya wapalestina,kuna wapelistina wanaokalia ardh ya israel,huo ndio mgogoro uliopo mpaka xaxa!,kwa hyo danganya hvi(makabur yao yapo israel).ulitaka uthbitisho,kasome agano la kale lote ili upate na vya ziada.

    Like

  250. Samuel James says:

    Ndugu yangu sijalifahamu jina lako walakini nimeona kuna upotoshaji mkubwa katika hoja yako ya kusema makanisa ni ya shetani,kiukweli uenda ni kukosa kwako kuelewa ndiko labda kumekupelekea kufanya upotoshaji huu mkubwa,andiko ulilotoa kuthibitisha maelezo yako kutoka katika Math 13:38 siyo kweli aizungumzii kwa habari hiyo, wacha nikufundishe walau uone udanganyifu uliokuwa unajalibu kuufanya Math 16:18 aielezi kama wewe unavyosema kwamba kanisa lilijengwa juu ya Petro hoja hiyo sio kweli, jina la Petro limetokana na jina Kefa ambapo majina yote hayo mawili yana maana moja ila lugha mbali mbali jina Kefa ni kiebrania na tafsiri yake ni jiwe soma Yohana 1:42″ Akampeleka kwa Yesu,naye Yesu akamtazama,akasema, Wewe u Simoni mwana wa Yohana,nawe utaitwa Kefa(tafsiri yake Petro,au Jiwe).ukija katika kitabu cha Mathayo 16:13-18 Yesu aliuwauliza wanafunzi wake kuwa watu wanammnena yeye ni nani? katika wanafunzi wake kila mmoja aliweza kumjibu Yesu vile alivyosikia,walakini Petro akamjibu akisema kwa matazamo wa imani yake sawa sawa na Mungu alivyomfunulia akajibu akamwambia , Wewe ndiwe Kristo,Mwana wa Mungu aliye hai,hapo ndipo Yesu akamjibu na kumwambia Heli wewe Simoni Bar-yona kwa kuwa mwili na damu havikufunuliwa hili,bali baba yangu aliye mbinguni,ndipo hapo Yesu akamwambia wewe ndiwe Petro (yaani Kefa na tafsiri yake ni jiwe Yhn 1:42) na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu,mwamba katika lugha ya Kiyunani sio Petro, Petro kwa Kiyunani ni jiwe ila mwamba petras kwa kiyunani,na maneno yote haya mawili yanapatikana katika kitabu hicho cha Math 16:18,biblia aijawai kumwita kuwa Petro ni mwamba ila Mwamba ni Yesu mwenyewe, katika ukweli aliousema Petro ndio ambao Yesu aliaidi kujenga kanisa lake katika huo ukweli ambao unamuhusu Yesu mwenyewe na wala sio Petro, Hoja ya pili ya kusema Petro amelaaniwa au ameitwa shetani ni hoja nyepesi na ya kimafikiriko zaidi, hata kama Petro alikosea ina maana Mungu asamei watu makosa yao?

    Like

  251. risasi says:

    ukafiri unamambo kweli, mambo mengi ukweli kidogo

    Like

    • Mhina says:

      Hapana, Siokweli ndugu yangu Risasi na waislamu wote wenye mtazamo kama huo wakwako. Mafundisho yote kwenye blog hii, Yamesimama katika kweli ya Mungu kwa asilimia zote. Tatizo ni kwamba, ninyi wenyewe waislamu mnaifanya mioyo yenu kua ni migumu kuamini ukweli na kuufuata!!. Kwa mfano mdogo, hebu tazama ukweli wa sheria za Mungu kwetu, kama nilivyofafanua huko juu…kamwe sisi wanadamu hatuwezi kuishi kwa kushika sheria za Mungu kwa miili yetu na malipizi yake kama waisrael wakati ule, kwa sababu kutokana na uovu ulioendelea duniani kote, sheria hiyo nayo “IMELEGEA” Wala hukumu ya haki haipatikani, kwa maana watu wabaya huwazunguka wenye haki, na kwa sababu hiyo, hukumu ikipatikana inakua nayo “IMEPOTOKA !! ” , ndiyo maana Mungu nae kupitia nabii Habakuki na wengineo wengi katika biblia, alitangaza injili ya wokovu wa haki kwa ajili ya watu wake: “ANGALIENI, ENYI MLIO KATI YA MATAIFA, KATAZAMENI, KASTAAJABUNI SANA, KWA MAANA MIMI NATENDA TENDO SIKU ZENU, AMBALO HAMTALIAMINI HATA MKIAMBIWA (waislamu) !!!, Soma(Habakuki 1:4-5). Basi na ijulikane kwenu, ndugu zangu waislamu, ya kua, kwa huyo, yaani yesu kristo, Mnahubiriwa msamaha wa dhambi, na kwa yeye, kilaamuaminiye, huhesabiwa “HAKI” katika mambo yale yote asiyeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ambayo ni torati ya Musa ninyi mnayodai kua mnaifuata yote kwa ukamilifu wake !!!!….kwa kua kama mkiendelea kujifariji wenyewe kwa uongo huo, basi, litawajilia hilo hapo juu lililosemwa na Mungu kupitia nabii habakuki. Soma( Matendo 13:38 – 41). Kwa hiyo, wewe ndugu yangu Risasi na waislamu wenzio, mnapoidharau injili ya wokovu wa Bwana, kwetu sisi injili yetu ya wokovu wa Mungu ndipo inapoendelea kutimiza unabii wake uliobaki kwetu, na siku ya mwisho ikija, basi hutakua na nafasi tena ya kujifunza kwa moyo wa haki na kutii ili uokolewe…Lakini utakapobadilika na kumtii Mwenyezi Mungu kupitia njia ya Mwana wake Yesu kristo, basi na wewe utakua umejinusuru kutoka kwenye adhabu ya Mungu itakayowashukia wale wasiotii na kuamini. Ndugu zangu waislamu, Mimi bado nawapenda sana, njooni kwa Yesu, asanteni na Mungu awasaidie, kwaherini.

      Like

      • kwelikweli kaka yangu mimi ni kiziwi ambaye dini yangu ni ukristo japo sisikii vizuri ila vishawishi ni vingi ninavyovipata kutoka kwa waislamu il nang’ang’ania lile neno katika matendo ya mitume lisemalo ,FILIPO akasema ukiamini kwa moyo wako wote yanawezekana Akajibu,Akanena Naamini ya kwamba yesu kristo ndiye mwana wa mungu>……

        Like

    • maneno mengi ukweli kidogo ?ila kwa muumba ukweli mwingi kupitiliza hakuna siri yoyote ktk mahubiri ht iwe vp tutahubiri mpk mtachoka na baraka zinazid kutufuata ninyi mmewahi kuubiri nn ? kumbuka tangu nizaliwe waislamu mmekuwa vigugumiz sana kuhubiri kwa nini ?

      Like

  252. shaaban says:

    salaam..eti hakuna ardhi ya wapalestina!!! haa hvi ww ndugu yangu una matatizo gani?? unaona raha damu za watu kumwagika pale??….hivi ww asili yko wapi?? unawajua waenye asili ya tanzania?? leo hii wakikusanyika waluguru wote duniani wakisema sisi tuondoke hapa wewe utakubali???? acha mawazo finyu na kusuport umwagikaji damu amabao hauna msingi….ile ardhi waesrael pale hawana tena hati miliki kwa sababu walishatoka pale zaidi ya karne 2 bila kugusa…na hata historia inawaumbua kwa sababu wenye asili ya pale ni wakanaani na wao asili yao nabii ibrahim wakurdi kwao iraq, sasa wao wanabaki kutumia mabavu tu…..hata hivyo vitabu vya dini wanavyotumia pia vinawakataa hawana hati miliki pale deadline yao ishaosha baada ya kuwaua manabii na kufanya uchafuzi wa maandiko…..badilika kaka usipende umwagikaji damu ambao hauna msingi waisrael waachie ardhi ya watu wenyewe wakae.

    Like

    • shaaban says:

      halafu kingine ndugu zangu mi siiamini biblia kwa sababu kuna matusi mengi sana ambayo sipaswi kuiamini hata kidogo******mungu kupigwa kabali na yakobo******mungu kuitwa malaya*****pia na haina tafsida ya maneno, mi siamini kitabu cha mungu kina maneno machafu amabayo ukikaa na mtoto wako huwezi kuyasema…………mi hata uniambie kasome mathayo 1:1 ntaangalia kama yana mantiki na yana wiana na kitabu kitukufu cha qur an ndo ntasema haya ya mungu lakini venginevyo ni maneno ya waandishi wahuni waliochafua maneno ya mungu laana ya mungu iwe juu yao….ni hayo tu assalaam alaykum.

      Like

      • nanoi kakwambia biblia ina matusi ? je wewe unaielewa biblia vizuri ? hadi sasa umesoma kurasa ngapi za biblia mi najua ninyi waislamu ni watu waovu msiosema ukweli niambie hizo sura zenye matusi huo ni unafiki mtupu mbele ya muumba na ushindwe ktk jina la yesu. najua na naona tabia za uislamu sio nzuri kuna msichana aliniambia yesu amefeli je ninyi si ndo chanzo cha matusi usitupe mtego hapa sema lililo la kweli biblia ukisoma unaweza kunifafanulia kwa urahisi wewe ? na ushindwe kabisa

        Like

  253. Mohamed says:

    Uislam na ukristo ipidini ya kweli?

    Like

  254. sande says:

    amen

    Like

  255. ninyi msioamin neno la bwana na kuongelea maneno yasiyompendeza mungu jueni kuwa co vizur ht kidogo mimi iman yangu ni ukristo mpaka kufa nanyi endeleeni na dini amuitakayo maana sisi hatuwalazimishi ila ni nyinyi na nafsi na mioyo yenu tu maana mimi nashangaa waislamu kusema wakristo tunaenda moton mara yesu alivaa kanzu mara watu wa kale walivaa mabaibui je mliwaona au mlimwona mungu anasema kuwa wakristo wote waende motoni ninyi kama nani ? dini ya kweli ni ile inayofundisha maneno yanayompendeza mungu na si vinginevyo .nashangaa ninyi mnaanza kumshawishi mtoto mdogo km miaka mitano maneno yasiyo ya kweli kwa nini dini yenu ni ya kushawishi na si kuongea maneo ya kweli nipeni jibu nyinyi waislam

    Like

  256. bahati jacob says:

    biblia imeweka wazi mitume na manabii je muhamad katabiliwa wapi? na Allah ni nani?

    Like

  257. Aloyce Andrew says:

    Habar zenu wa2 wa Mwenyezi Mungu Mmoja.Kwa kwel nmefurahshwa sna na hoja za ndug mhina,mohamed yohana na ibra kwa kwel nmejfunza meng sna ingawa nlchokiona ni kwamb kuna baadh ya maandko ukyatzama yako waz kabsa na yanamuonyesha Yesu kuw ni nabii mtakatfu wa Mungu,sas cjui tatzo ni jinc iman ilivyopandkizw na paulo!jambo lingne nnaloshangaa m2 anasem eti Muhamad S.A.W co nabii wa Mungu eti kwa sabab alipgana vta je hawajasoma habar za nabii Daud alipgan na kuwauw makafr wa kifilist?hata nabii Musa aliwa2ma wapelelez ktk nch ya ahad na aliiwaamur kuuwa kla watakae muon lkn wote hao wanakubalka kuw n manabii wa kwel.Mim nnadhan upotoshwaj wa maandko ndo unaowagharmu wakristo kwan viongoz wao wamekuw waktafsir maandk uongo kwa mfano kutoka 3:4-6 Mungu anamwambia Musa avue via2 mahal patkatfu mckie mchungaj atakavyokufundsh atakuambia via2 hvyo co vya miguun n dhamb ya kuua,lakn andko la kut.4;1-4 atakuambia ukwel kuw fmbo iliyogeuk nyok n fmb ya kwel.sas unategemea andko linalohus uislam ltakubalka ktk bible?!!

    Like

    • Mhina says:

      Ndugu Aloyce: Biblia haifundishi kwamba, manabii wa zamani, walikuwa wakamilifu kama malaika, hapana, isipokua, Mungu aliwachagua, akawasamehe na kuwaimarisha, ili wawe vipaza sauti wake wa haki, duniani kote. Jambo la Muhimu sana hapo ni “ile hali ya kuchaguliwa na kuimarishwa na Mungu mwenyewe, ili uwe ni nabii wa kweli wa Mungu. Sasa tatizo ni kwamba, Mhamad hakuchaguliwa na Mungu awe nabii wa watu, ndiyo maana pia, hakunena kwa roho mtakatifu. Pia ni muhimu kufahamu kua, israel ni watoto wa Mwili, na Mataifa ni watoto wa ahadi, ndiyo maana biblia inasema hivi” BASI MAMBO HAYO YALIWAPATA WAO KWA JINSI YA MIFANO (Mwili), YAKAANDALIWA ILI KUTUONYA SISI, TULIOFIKILIWA NA MIISHO YA ZAMANI !!, Soma(1Wakorintho 10:11). Bwana yesu ndie nabii wa Mwisho wa Mungu aliyekuja kukamilisha makosa yote ya wakina Musa na wengineo, kwa kua yeye ndie hekalu takatifu la Bwana, ndiyo maana biblia inasema” KWA MAANA HUYO, AMEHESABIWA KUWA, AMESTAHILI UTUKUFU ZAIDI KULIKO MUSA, KAMA VILE YEYE AITENGENEZAYE NYUMBA, ALIVYO NA HESHIMA ZAIDI KULIKO HIYO NYUMBA, Soma(waebrania 3:3). Kwa hiyo ndugu aloyce, mhamad mtume wa waislamu, ukiisoma quran vizuri, utagundua kua, vita vyake vingi na mauaji yake, yalihusu kugombania madaraka na mali, na kamwe si kwa ajili ya haki ya Mungu. Hata yeye mwenyewe, kuhusu vitabu vya Mungu vya torati, zaburi na injili, amewahubiria wafuasi wake kua, hawawezi kwenda mbinguni, bila ya kuua na kuuliwa kwa ajili ya kugombania madaraka ya kusimamia dini yake ya uislamu. Tazama(quran 9:111) , anawaambia wafuasi wake hivi” HAKIKA MWENYEZI MUNGU, AMENUNUA KWA WAUMINI WAKE, NAFSI ZAO NA MALI ZAO, KWA KUA, WAO WATAPATA PEPO, WANAPIGANA KATIKA NJIA YA MWENYEZI MUNGU, WAKIUA NA KUULIWA, NA HII NI AHADI ALIYOJILAZIMISHA KWA HAKI KATIKA VITABU VYA TORATI, ZABURI, INJILI NA QURAN !!!. Kwakweli, mafundisho hayo ya Mhamad, yanathibitisha wazi wazi kua, yeye sie nabii wa kweli wa Mungu, aliyekuja kutimiza vile vitabu vya Mungu vya torati, zaburi na injili kwa kua, hilo lengo lake alilolifundisha katika quran, halikua ni lengo la kweli la mwisho la Mungu kwetu. Kwanza Mungu hakuwahi kuchagua na kutumia nabii yeyote nje ya taifa la israel, ndiyo maana Mungu mwenyewe akamwambia israel ” KWA MAANA WEWE U TAIFA TAKATIFU KWA BWANA MUNGU WAKO. BWANA MUNGU WAKO, AMEKUCHAGUA KUWA WATU WAKE HASA , ZAIDI YA MATAIFA YOTE WALIOKO JUU YA USO WA NCHI. Soma(kumbuk 7:6).

      Like

  258. Mhina says:

    WANA WA MUNGU WA PEKEE MPAKA MWANA WA MUNGU WA PEKEE…..Mungu alisema kwa Israel kupitia kinywa cha Mfalme Daudi hivi” NDIWE MWANANGU MIMI LEO, NIMEKUZAA, UNIOMBE, NAMI NITAKUPA MATAIFA KUA, URITHI WAKO, NA MIISHO YA DUNIA KUA MILKI YAKO, Soma(Zaburi 2:7-8). Mungu alilichagua, Taifa la Israel, ili kupitiaTaifa hilo, “apate kutukuzwa Duniani kote”, ndiyo maana anamuita israel “MWANANGU”. Soma(kutoka 4:22-23). Mahala pengine, Mungu anamwambia israel hivi” NAMI NITAKUPOSA UWE WANGU KWA MILELE, NAAM NITAKUPOSA KWA “HAKI” NA KWA “HUKUMU” NA KWA “UFADHILI” NA KWA “REHEMA” !!!.Soma(Hosea 2:19-20) (Isaya 44:21). Kwa hiyo, Bwana yesu, tunamuita ni mwana wa Mungu wa pekee, kwa sababu, Mungu yuleyule aliesema na Manabii, mwisho wa siku hizi, anasema na sisi, kupitia Mwana “ALIYEMUWEKA KUWA MRITHI WA WOTE NA WA VYOTE” Soma(ebrania 1:1-2). Kwa hiyo, Kristo Yesu, amekua ni Mwana mpendwa wa pekee kwa kua, Yeye ni “MRITHI”, ndiyo maana yeye mwenyewe akasema hivi” NIMEKABIDHIWA VYOTE NA BABA YANGU, WALA HAKUNA AMJUAYE MWANA ILA BABA, WALA HAKUNA AMJUAYE BABA, ILA MWANA NA YEYOTE AMBAYE MWANA APENDA KUMFUNULIA .Soma( Mathayo 11:27). Pia, kama nilivyosema huko juu ya kwamba, Mungu alikuwa, ndani ya Kristo, kwa kua, Yeye aliyesema kule Mwanzo kwamba “IWE NURU”, Soma(Mwanzo 1:3), ndiye aliye angaza Mioyoni mwetu, ili atupe nuru ya elimu ya utukufu wake(neno lake) katika uso wa “YESU KRISTO” !!!. Soma( 2Wakorintho 4:6). Kwa hiyo, sisi wakristo, tunaweza kushiriki uungu wa Baba yetu, kwa njia ya Yesu kristo, bwana na mwokozi wetu, na kufanywa na sisi”WARITHI”, ndiyo maana biblia yatuambia hivi” NA KWA KUA, NINYI MMEKUA WANA, MUNGU ALIMTUMA ROHO WA MWANAYE MIOYONI MWETU, ALIYE “ABA” (BABA) , KAMA NI HIVYO, WEWE SI MTUMWA TENA BALI U MWANA, NA KAMA U MWANA, BASI U MRITHI KWA MUNGU. Soma(galatia 4:6-7). Kwa hiyo ndugu zanguni wote, kwa kuwa Mwana wa Mungu amekwisha kuja kukamilisha kazi za wana wote wa Mungu waliopita, ndiyo basi tena, hakuna Yeyote tena, anayeweza kuja kwa jina la Mwenyezi Mungu, ndiyo maana, Biblia nayo, yatuthibitishia hilo kwa kusema “WALA HAKUNA WOKOVU KATIKA MWINGINE AWAYE YOTE, KWA MAANA, HAPANA JINA JINGINE CHINI YA MBINGU, WALILOPEWA WANADAMU, LITUPASALO SISI KUOKOLEWA KWALO”!!!!!. Soma(Matendo 4:12). Biblia ninaipenda sana, kwa sababu, imeweka ukweli waziwaz kabisa ndugu zanguni, bila ya ubabaishaji wowote. Hebu tazameni ninyi wenyewe: TAZAMA > Zile ahadi za Agano la kale, za nabii Musa katika torati na manabii, kumhusu Bwana yesu “ZIMETIMIA !!!!!. Soma(Luka 24:44-49). TAZAMA > Yule nabii, mfano wa Musa, aliyetabiriwa, kuja na kuweza kuonekana waziwazi mbele ya mashahidi wengi “AMEONEKANA WAZI WAZI !!!!!. Soma(Yohana1:45). TAZAMA > Zile sheria za agano la kale, zilizohitaji malipizi ya mwili kwa ajili ya haki ya Mungu “ZIMETIMIZWA NA BWANA YESU, KWA ASILI YAKE YA ROHONI, ILI TUWEZE KUKAA NA WATU WOTE KWA UPENDO NA AMANI !!!!!. Soma(Warumi 7:14) (Warumi 7:4-6). Pia soma katika torati ya Musa, (kumbukumbu 6:4-9) na katika injili, (mathayo 22:35-40). Mwisho kabisa, lenye umuhimu sana, ni kwamba, Agano jipya tulilonalo, limefungwa katika damu ya Yesu kristo, nalo ni la mwisho, mpaka hapo arudipo tena yeye mwenyewe, ndiyo maana pia biblia inasema hivi” YESU KRISTO NI YEYE YULE, JANA NA LEO NA HATA MILELE, MSICHUKULIWE NA MAFUNDISHO YA NAMNA NYINGINE NYINGINE, !!!!!!!! X 100. Kwa hali hiyo, Muislamu akiniambia kua, mhamad ndiye aliyetabiriwa kwenye biblia, akiitwa sijui “AHMED” Ila jina lake lilifutwa, kwakweli ninamuonea huruma sana, kwa kua, nafahamu kua, amedanganywa kitoto, nae akadanganyika. Asanteni wote na kwaherini.

    Like

  259. Aloyce Andrew says:

    Nmefurahishw sna na maon ya ndug mhina,mudy yohana na ibra.Kwa kwel jamaa wameonyesh ukomav wa hali ya juu kimaandko ingawa n kwel wap wanaoshabkia na kushndw kuukubal ukwel mm nadhan sual la Mtume kupgana vta halna tofaut na nabii Daud alipgan vta na akauw ma10 elfu pamoja na goliat so ni hak kupgana na yeyot anayel2kana jna la Mungu hat nabii Musa aliuw adui wa Mungu na tena ali2ma wa2 wapelelez wak wakawauw wenyej wa nch ya kaanan.Sual la Yesu kuw mungu huo ni uzush mungu hawez kukubal apit ktk tupu ya kiumb wake then anyony tit z kiumb wake,ajinyee, aogeshwe,atahriwe na viumb wake.Mm nadhan kla m2 anatambua maish ya mwanadam tok akiw mtot jnc anavyokuw so 2mien akl yy hakuwah kusem kuw yey n mungu dat why mashahd wa Yehova wamejiondoa kwny hyo iman Mola Awajalie wazd kuuona ukwel mwisho waje kuclimu wauondoe na uwana wa mungu kabsa wao wanakr kabsa kuw utat wa mungu uli2ngw ktk mkutano wa nicea jaman somen vtabu vyao vya amken mtagundua meng wao pia n wakristo wenzenu.

    Like

  260. je yesu na ala ni mungu kweli na ni nani mungu wa kwelli.

    Like

  261. je yesu ni mungu na kama mungu alla atakuwa nani mungu wa waisilamu

    Like

  262. namushukuru bwana Yesu.kwa kuwa nimungu wangu.na atabaki kuwa mungu

    Like

  263. Eradius kalomba says:

    umeongea sana,ila ni mawazo yako sibshi,lakn kama m2me kafuata jn na mi2me walo tanglia walimfuata nan?na una uhakka kuwa bible ya mkristo isa anaijua?kabla ya kwenda mbal chunguza maana ya neno kristo na chanzo chake ndo ucmame kiiman kupotosha/kukomboa umma acha chuki binafsi mwsho wake mbaya.nachkr m/mungu akuongoze ahsanten.

    Like

  264. SEM DEDE says:

    Mungu awape mafunuo zaidi muifunue kweli yake

    Like

  265. Yohana J. Mzuri says:

    Hivi tunajua kuwa quran imempa kipaumbele zaidi Isa bin Mariam (Yesu) kuliko mtume muhamad? quran yenye sura 114 na maneno 6666, imemtaja muhamad mara nne (4) tu, lakini Isa bin Mariam (Yesu) ametajwa mara ishirini na tano (25).
    Hivi tunajua kuwa katika quran hakuna jina la mwanamke lililotajwa, si la mama yake mtume muhamad, si la wake zake au dada zake, ila jina moja tu la Mariam mama wa Isa (Yesu). Na ya kuwa sura ya kumi na tisa (19) ya quran imepewa jina la Mariam mama wa Isa (Yesu)?
    TAFAKARI- Ikiwa quran yenyewe imeona umuhimu mkubwa Isa bin Mariam (Yesu Kristo) na mama yake Mariam, wewe muislam unasubiri nini?

    Like

    • Basi leo yohana umesababisha nikumbuke kitu cha muhimu sana. Biblia inasema hesabu ya mnyama itakuwa mia sita sitini na sita. Tunaona qruan inamaneno elfu sita mia sita sitini na sita. Hii undo hesabu ya mpinga kristo. Ndugu tusihangaike kusubiri mpinga kristo wakati tayari alishakuja, yeye atendaye kazi ya kuliudhi kanisa la Bwana akichoma moto mahekalu na kuwaua wakristo.

      Like

    • shaaban says:

      sorry qur an ina maneno 6,236..aman kwenu

      Like

    • shaaban says:

      salaam…maelezo yako yanatosha zaidi kueleza kiasi gani qur an inampenda sana Issa(yesu)(rehma na amani ziwe juu yake) na waislam tunampenda sana ndio maana tunasimama kumtetea na fikra za wanadamu kumlinganisha na mungu…..fikiri then chukua hatua uislam hauna chuki na Issa(yesu)(rehma na amni ziwe juu yake) bali wanaomchafua na kumuita mungu ndio tunawapinga kwa nguvu zote.salaam.

      Like

    • shaaban says:

      salaam…maelezo yako yanatosha zaidi kueleza kiasi gani qur an inampenda sana Issa(yesu)(rehma na amani ziwe juu yake) na waislam tunampenda sana ndio maana tunasimama kumtetea na fikra za wanadamu kumlinganisha na mungu…..fikiri then chukua hatua uislam hauna chuki na Issa(yesu)(rehma na amni ziwe juu yake) bali wanaomchafua na kumuita mungu ndio tunawapinga kwa nguvu zote.salaam.

      Like

  266. mm kimanga says:

    ni vema wakristo wajuwe kwamba ukristo ndio njia pekee ya kufika kwa MUNGU na ndio njia pekee ambayo shetani anaijitaidi kuzuwiya watu wasifike kwa MUNGU kwa kuwape pesa ili wamuasi MUNGU kwa hawa waislam shetani ni kicheko tu kwani ni watu wake kabisa nashukuru MUNGU sana kwani nimezaliwa muislam nimelelewa na wazazi wangu waislam lakini nilipata njia ya wokovu wa yesu toka mwaka 1997 hadi sasa kwakweli kwa wale wasiojua ndio wata endelea kuwa waislam kwa au wale wanao amua kujidanganya ukweli ni kwamba wapo watu wanao jua kabisa ukweli kuhusu uislam na wengine hawajuwi ukweli ni kama bahadhi ya wakristo wengine hawajuwi ukweli kabisa na ndio wengi wao wana pelekwa katika makanisa ya misingi ya kishetani sio siri kuwa shetani anajaribu kuuteka ukristo kwa kubadili taratibu za kuabudu na sheria za MUNGU kwani vita vipo vya kiroho kwa sisi wakristo na roho wa giza na sio wengine wanao tafutwa na shetani bali ni wakristo tu.

    Like

  267. Pastor Joseph Kazungu Chivatsi. says:

    Ndugu zangu waislam hebu natuwe wa kweli.Soma nami yafuatayo:SURA 29:46>”WALA MSIBISHANE NA WATU WALIOPEWA KITABU (KABLA YENU) ILA KWA YALE(MAJADILIANO) YALIYO MAZURI,ISIPOKUWA WALE WALIODHULUMU MIONGONI MWAO.NA SEMENI:TUNAAMINI YALIYOTEREMSHWA KWETU NA YALIYOTEREMSHWA KWENU,NA MUNGU WETU NA MUNGU WENU NI MMOJA;NASI NI WENYE KUNYENYEKEA JWAKE.”Amri hii imeelezwa zaidi katika Sura 2:136>”SEMENI NYINYI(WAISLAMU WAAMBIENI MAYAHUDI NA MANASARA;WAAMBIENI):TUMEMWAMINI MWENYEZI MUNGU NA YALE YALIYOTEREMSHWA KWA IBRAHIMU NA ISMAILI NA ISA-HAQA NA YAAQUBU NA KIZAZI(CHAKE YAAQUBU);NA WALIYOPEWA MUSA NA ISA NA PIA YALE WALIYOPEWA MANABII(WENGINE) KUTOKA KWA MOLA WAO;HATUTOFAUTISHI BAINA YA YO YOTE KATIKA HAO.(WOTE TUNAWAAMINI);NA SISI TUMENYENYEKEA KWAKE.”(Sura 42:14;29:46;10:94).Qurani inashuhudia UKWELI WA BIBLIA.Sura 6:115>”NA YAMETIMIA MANENO YA MOLA WAKO KWA KWELI NA UADILIFU.HAKUNA AWEZAYE KUYABADILISHA MANENO YAKE.NA YEYE NDIYE ASIKIAYE(NA) AJUAYE.”NAWAMBA NGUGU ZA MUISOME QURANI NA MUILEWE,MUIZINGATIE NA MUIISHI SAWA SAWA NA INAVYOWAELEKEZA! Wasalam alae-kum!

    Like

    • shaaban says:

      Salaam…kama unaamini hayo maneno tafakari vizuri kati yetu na nyie nani anabagua manabii na kusema huyu hatumtaki na huyu tunamtaka?????jibu unalo tafakari vizuri…….salaam.

      Like

  268. BWANA YESU
    APEWE SIFA
    NAWATHALIMU KWA NDUGU WAKRISTO KWA JINA TEULE LA YESU KRISTO ALIYE HAI
    Napenda kuwapongeza watumishi wamungu ambao mmeonyesha nijinsi gani mlivyosimama katika neno Kwa Sababu Hawa Waislamu Wanaisoma Biblia Kama Vile Wanasoma Gazeti Na Wanaisoma Bila Uongozi Wowote Ila Kwa Ufinyu Wao Wa Kufikiri Wanaielezea Kipumbavu. Biblia Inatakiwa Kusomwa Kwa Uongozi Wa Roho Mtakatifu Maana Huyu Roho Ndie Mwalimu Wetu Na Mtu Usipokuwa Na Karama Ya Roho Kamwe Hutaweza Kujua Siri Ya Mungu Kwa Sababu Roho Mtakatifu Hujua Hata Mafumbo Ya Mungu Lakini Jambo Hili Lisiwashangaze Ndugu Wakristo Kwa Hawa Waislamu Kumpinga Bwana Yesu Na Kufanya Matukano Na Makufuru Juu Ya Patakatifu Pake Yehova Mungu Wa Kweli Ndugu Wakristo Mtambue Kuwa Shetani Alimuasi Mungu Na Alijinua Ili Alingane Na Mungu Na Akawadanganya Na Baadhi Ya Malaika Ili Wamuasi Mungu Ndipo Walipo Fukuzwa Huko Mbinguni Lakini Hata Sasa Shetani Amejiinua Huku Duniani Ilikufanya Matukano Na Makufuru Mbele Za Mungu Yehova Alie Hai Kwa Kuwapiga Upofu

    Like

  269. michael says:

    Ndugu zangu wa upande wa islamic religion mnapotea kwa kukosa knowlage,haven”t not read that jesus our saviour shares nothing with demons?John;8;49-51

    Like

  270. Azidah maalim says:

    as/aleykum

    Like

  271. REDEMPTA SALVATORY says:

    KWELI MIMI NILIKUA NIMEPOTOSWA NA WAISLAM SASA NAMUSHKRU MUNGU MMENIFUNGUA YESU NDIE MUKOMBOZI WETU AMINA

    Like

  272. Yohana Mzuri says:

    Karibu tena kwa YESU wetu, maana kwa YESU ni amani na upendo, hakuna atakaye kupotosha.
    Mungu wa Bwana wetu YESU KRISTO akuimarishe na kukutia nguvu, AMINA.

    Like

  273. r.m... says:

    jamani waislam, mhamd alijuaje kua yesu hakusulubiwa msalabani ila aliesulubiwa ni mtu mwingine, wakati nyakati zile alikua bado hajazaliwa? Hivi wewe unaweza kupinga kua nyerere hajatawala nhi ya Tanzania, wakati alipokua anatawala ulikua hujazaliwa? si utaonekana ni mwana historia wa uongo usiejua chochote!!!!

    Like

  274. jawad amri says:

    Uislam. Ndo dini haki.natena hakuna hapaswae kuambudiwa kwa. haki isipokuwa allah. Nashangaa kuwa wenzetu wanasema kuwa yesu ni mungu.mungu gani anapigwa. Na wanadam.

    Like

  275. simbongano Mtendjwa says:

    Bwana Yesu asifiwe sana!ninawaombea sana wanao pambana nao mashetani wanao utesa ulimwengu huu. Hata mimi ninaitaji kupambana nao lakini ukosefu wa biblia una ni sumbua.

    Like

  276. Shayo Conscious says:

    ipi njia ya kweli

    Like

  277. simbongano Mtendjwa says:

    Bwana Yesu asifiwe.kufuatana na mada hii ya uislam na ukristo,maono haya ni mazuri ambayo kwa uweza wake Mungu tunaweza kuzivuja ngome kwa maombi ambayo ndiyo silaha kubwa kwetu sisi wakristo. ombi ; nawaombi biblia ili tusaidiane kazi ya Mungu kwa kuwavuta waislam wengi katika ukristo.Mimi ni mkimbizi katika kambi ya nyarugusu tanzdnia

    Like

  278. magomgo pesa says:

    dini ya kweli ni ile iliotangulia AMBAYO NI UKRISTO hio ndio dini ya ukweli
    ukiangalia mwili wa wakristo ni hekalu la mungu ambapo roho mtakatifu hukaa ndani yetu na kuwa na uwezo wa kumfukuza shetani

    ila HAO WENJETU WA ISLAM HUAMINI KUA WAKATI WAMELALA USIKU PUA NDILO HEKALU LA WAISLAM WOTE HUWA SHETANI NDIKO
    ANAKO LALA NDO MAANA LAZMA UKIAMKA UPGE CHAFYA ILI KUMTOA SHETANI AU KUIOSHA VIZURI PUA

    WAKRISTO WOTE SHETANI HARUHUSIWI KABISA KUFANYA Mkazi ndani ya pua
    MALAIKA WA MUNGU PEKEE NDIE MWENYE MAMLAKA YA KUKAA NDANI YA MWILI WA MKRISTO

    Like

  279. THOBIAS FRANK says:

    Nampongeza Dr.paul hussein kwa kuwapa waislamu mwanga wa kuitambua giza ndani ya imani yao na hatima ya maisha yao baada ya kifo.

    Like

  280. Abdul yasiin says:

    Its nice and smart kujadiliana ili kumjua mwenyezi mungu WA kweli.

    Like

  281. Isaack says:

    Jamani naomba nifahamu, je Yesu ndiye huyu Mungu yule mmoja aliye umba ulimwengu na vyote?

    Like

  282. Isaack says:

    Jamani naomba nifahamu, je Yesu ndiye huyu Mungu yule mmoja aliye umba ulimwengu na vyote?
    Naomba tuelimishane na kuelekezana kwenye ule ukweli mmoja

    Like

    • rich says:

      ndiye kwa jinsi ya rohoni, siye kwa jinsi ya mwilini. Maana yake ni kwamba: Mungu ni roho akaaye ndani yake. Kwa ukamilifu na utakatifu wa Yesu kristo, amemfunua Mungu Baba kwa asilimia zote kwa jinsi ya rohoni kwa yale yote aliyotufundisha…yesu kwa jinsi ya mwili, ni Mungu kwa jinsi ya rohoni, ndiyo maana anamuita Mungu Baba yake.

      Like

  283. Ephraime Kaingu Ngari says:

    Hallelujah napenda sana mijadala Hui.

    Like

  284. jamila says:

    Kwa ndungu zangu waislamu Assalamu aleykum kwa kweli wakristo wanashangaza wanataka waone moto wa jahanam ndio wa amin naitakuwa ni let na watatamani wangekuwa mchanga sahi tunawaonya wanaziba masikio kana kwamba awasiki lakin tusubiri na wao wasubir tutajua ninani alie potea

    Like

    • sunday says:

      jamila dada yangu…mhamad ameupotosha ulimwengu kwa madai yake kuwa yeye ndie nabii wa mwisho aliyetumwa na Mungu. Anadai kua amekuja kurekebisha torati, injili na vitabu vyote vya nyuma ambavyo anadai wakristo na mayahudi wamevichakachua!!. Kwanza, hapo anamaanisha kua, wale manabii wa nyuma kama Musa, lsaya, Daud, n.k…walimtabiri yeye kua atakuja nabii Mhamad, kurekebisha vitabu vyao vitakavyokuja chakachuliwa na wayahudi. Swali: wakati ule walijuaje kwamba vitabu vyao vya ibada walivyopewa na Mungu vingekuja chakachuliwa, mpaka eti wamtabiri huyo Mhamad kwamba atakuja kuvirekebisha?!!!.maana hiyo ndio kazi aliyoifanya nabii huyu akidai alitumwa na Mungu kurekebisha maandiko ya manabii wenzake. Pili, mambo ya hadithi na maelezo mbalimbali ya maisha ya nabii huyu katika quran yanahusiana vipi na torati, zaburi na injili neno la Mungu ambalo anadai kua, bila kuongeza chochote, amekuja rekebisha tu??. leo hii ninyi waislamu kila mkiulizwa maswali magumu ya Mungu basi mnachofanya ni kujibu kwa kutumia hadithi za maisha ya mtume wenu Mhamad…je, hizo hadithi za maisha yake ndio neno la Mungu kwenu??….je, hizo hadithi za maisha yake ndizo torati, zaburi na injili alizotoa kwa Mungu ili asawazishe vile vitabu vya nyuma ili awapeleke na nyinyi mbinguni?!!!!!!! au dada jamila wewe hujui historia za dini na ukweli wa mambo?????…Poleni sana ndugu zetu, lakini itafika wakati mtatutafuta kama maandiko yanavyoahidi.

      Like

  285. Benn says:

    MILA NA DESTURI NA MAHUSIANO YA BINADAMU NA YEHOVA

    Viumbe wa kiroho wenye mafungamano na maisha ya binadamu na namna wanavyomwathiri binadamu katika afya ya kisaikolojia na kimwili
    Shetani, \Majini, Mizimu, Mapepo na Mahayawani
    (i) Shetani
    Malaika huyo hakuitwa Shetani alipoumbwa. Jina hilo ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu.
    Kiumbe huyo wa roho akaanza kukuza hisia za kiburi na za kushindana na Mungu. Alitaka wengine wamwabudu yeye. Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu alipokuwa hapa duniani, Shetani alimtaka Yesu ‘amfanyie tendo la ibada.’—Mathayo 4:9.
    Shetani “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alidai kwamba Mungu alikuwa mwongo, ilhali kwa kweli, yeye ndiye alikuwa mwongo. Alimwambia Hawa kwamba angekuwa kama Mungu, lakini ni yeye hasa aliyetaka kuwa kama Mungu. Na kupitia mbinu zake za ujanja, alitosheleza tamaa yake yenye ubinafsi. Alimfanya Hawa amwone kuwa mkuu kuliko Mungu. Kwa kumtii Shetani, Hawa alimkubali kuwa mungu wake.—Mwanzo 3:1-7.
    Kwa kuchochea uasi, malaika huyo ambaye awali alikuwa mwenye kuaminika akawa Shetani, yaani, mpinzani na adui ya Mungu na wanadamu. Neno “Ibilisi,” linalomaanisha “Mchongezi,” likawa pia jina la malaika huyo mwovu. Malaika huyo ambaye aliongoza katika kutenda dhambi mwishowe aliwachochea malaika wengine wakose kumtii Mungu na wamwasi kama yeye. (Mwanzo 6:1, 2; 1 Petro 3:19, 20) Kwa kufanya hivyo malaika hao waliwaongezea wanadamu shida. Kwa sababu ya kuiga njia za Shetani zenye ubinafsi, “dunia ikajaa jeuri.”—Mwanzo 6:11; Mathayo 12:24.
    Namna gani, kwa nini, na ni lini Shetani alianguka kutoka mbinguni?”

    Kuanguka kwa Shetani kutoka mbinguni kimfano niv vile ilivyoelezwa katika Isaya 14:12-14 na Ezekieli 28:12-18. Wakati vifungu hivi viwili vinamaanisha hasa wafalme wa Babeli na Tiro, wao pia hurejelea nguvu za kiroho zinazo wasukuma wafalme hao, yaani, Shetani. Vifungu hivi huelezea kwa nini Shetani alianguka, lakini haisemi hasa wakati kuanguka kulitokea. Tunachojua ni hiki: Malaika waliumbwa kabla ya nchi (Ayubu 38:4-7). Shetani akaanguka kabla ya yeye kuwajaribu Adamu na Hawa katika bustani (Mwanzo 3:1-14). Kuanguka kwa Shetani, kwa hiyo, ni lazima kuwa kulitokea mahali fulani baada ya muda malaika waliumbwa na yeye kabla ya kuwajaribu Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni. Kama kuanguka kwa Shetani kulitokea dakika chache, masaa, au siku chache kabla ya yeye kuajaribu Adamu na Hawa katika bustani, maandiko hayasemi hasa.

    Kitabu cha Ayubu chatuambia kwamba, kwa wakati angalau, Shetani bado alikuwa anaweza kuingia mbinguni, na kwa kiti cha enzi cha Mungu. “ilikuwa siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda katiyao. BWANA akmwuliza Shetani akamhibu BWNA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.” (Ayubu 1:6-7). Inavyoonekana wakati huo, Shetani alikuwa bado akitembea kwa uhuru mbinguni na duniani, akizungumza na Mungu moja kwa moja na kujibu kwa shughuli zake. Wakati ambapo Mungu alimkomesha kupata ruhusa ya kuingia mbinguni haijulikani.

    Kwa nini Shetani alianguka kutoka mbinguni? Shetani alianguka kwa sababu ya kiburi. Alitamani kuwa Mungu, si kuwa mtumishi wa Mungu. Taarifa nyingi “Mimi …” kauli katika Isaya 14:12-15. Ezekieli 28:12-15 inamwelezea Shetani kama malaika mzuri mno. Yawezekana kuwa Shetani alikuwa juu ya malaika, mzuri zaidi ya wote wa viumbe na Mungu, lakini hakuwa ameridhika katika nafasi yake. Badala yake, Shetani akataka kuwa Mungu, kwa kimsingi “kumtoa Mungu katika kiti chake cha enzi ” na kuchukua utawala wa ulimwengu. Shetani alitaka kuwa Mungu, na cha kuvutia, ni kwamba hichi ndicho Shetani aliwajaribu Adamu na Hawa kwalo katika bustani mwa Edeni (Mwanzo 3:1-5). Shetani aliangukaje kutoka mbinguni? Kwa kweli, kuanguka si maelezo sahihi. Itakuwa mbali zaidi sahihi kusema kuwa Mungu alimtupa Shetani kutoka mbinguni (Isaya 14:15; Ezekieli 28:16-17). Shetani hakuanguka kutoka mbinguni, badala yake, Shetani alisukumwa kutoka mbinguni
    (ii) Majini
    Maana na Chimbuko lao
    Majini au mapepo ni viumbe ambavyo havionekani kwa macho, ni viumbe kama malaika isipokuwa majini na mapepo yalifukuzwa mbinguni pamoja na shetani baada ya kuasi, na yalitupwa duniani yakisubiri siku ya mwisho ya hukumu.
    Majini ni viumbe ambao wameumbwa kwa Moto na walikuwa wakiishi duniani kabla ya binadamu miaka Milioni nyingi iliyopita.
    Viumbe hawa wana tabia kubwa mbili;

    Yaani ya kibinadamu kwa maana wanakuwa wanafanya mapenzi, wanazaa na wanakufa.
    Tabia nyingine ni ya Kimalaika ambayo ni kwamba wana uwezo wa kujigeuza katika umbo lolote wanalotaka na vile
    Shetani na majini, wanajua kabisa kuwa jehanum ya moto ipo kwa ajili yao, ndiyo maana wanafanya kila mbinu wasiingie peke yao huko jehanum, shetani ni mwongo, laghai anawatumia sana wachawi, waganga wa kienyeji, wasoma nyota kupandikiza majini, kuiba nyota yako ya mafanikio, kuchukua watu misukule nk.
    Aina za majini na kazi zao:
    Kuna aina nyingi za majini baadhi yake ni kama:-
    1) Murafari – hili ni jini linalozuia mafanikio ya kupata fedha, mafanikio ya elimu nk.
    2) Latifu – hili jini linaloleta ufukara, mateso, hata ukipata pesa matumizi yake yanakuwa ni hovyo
    3) Jahari – Jini anayetumiwa kuiba mali na kuzuia biashara kustawi
    4) Hasinani – jini hili ni la fujo, ulevi wa pombe, bangi na dawa za kulevya
    5) Jube – jini hili linasababisha utasa
    6) Subiani – jini la ajali, linasababisha wanawake kutokupata siku zao, na kunyonya damu za akina mama siku zao za hedhi ambapo wanapata maumivu makali sana.
    7) Sumil – jini hili huangamiza mimba changa
    8) Waidadat – jini hili husababisha wanaume kuvaa hereni kusuka nywele na kutoga masikio.
    9) Alibadiri – jini la kifo, likikupata kifo hutokea wakati wowote.
    10) Anzura – Linawazuia vijana wa kike na kiume kuolewa/kuoa
    11) Maimuna – linawakamata wanaume wenye ndoa zao hadi ndoa inavunjika
    12) Makata – linasababisha vifo vya mfululizo kwenye familia
    13) Faziur – jini la maandishi. Unaletewa barua ukiisoma tayari umelikwaa
    14)Subha – jini hili linasababisha mtu kuwa na kiburi sana na kujiinua.
    15) Maulan – jini linalofanya watu kuwa kichaa, au mtu ananuka wakati wowote
    16) Al-maul – jini hili linamfanya mtu kuwa ombaomba
    17) Zuhura au Zohari – Jini la fujo
    18) Araba – Jini hili linafanya mtu apende sana ubani
    19) Farkh – jini hili linatumwa hasa kwa wakristo kuangalia kama ana kinga (Wokovu)
    20) Baradi – jini hili likikupata basi ndoa yako ni lazima itavunjika.
    21) Shamsu – jini hili huvaa umbile la binadamu kwa sura yoyote.(sasa hivi mitaani majini haya yapo mengi sana)
    22) Abuni – jini wa hasira
    23) Kaimu – jini la kutambua nyota za watu
    24) Tajuruni – jini la utajiri wa kichawi – ni lazima utoe kafara ya mwanao, mkeo au kufanya tendo la ndoa na mama yako mzazi
    25) Al-taliki – jini hili linapoteza watu katika mazingira ya kutatanisha
    26) Naluju – linasimamia lugha
    27) Janatusi – linatumwa alfajiri kabla ya adhana kuleta usingizi kwa Wakristo wasifanye sala
    28) Riyaron – jini hili linamfanya mtu afanye kila kazi peke yake
    29) Zaitun – Jini hili linasababisha wasichana kuwa na maringo
    30) Ruyati – jini linalosim amia ndoto mbaya
    31) Al-rahabu – jini linalosababisha hitilafu ya umeme
    32) Hadharaji – jini hili linafanya kazi ya kukata kichwa cha mtu ili wapate damu
    33) Anazihaji – jini hili ndilo linachukua roho yako ukifa kwenye dhambi
    34) Nghruk – linasababisha maafa
    35)Munkara – jini la makaburini
    36) Takadhuru – jini linaloleta mali za masharti.
    37) Rabindi – jini la Waislamu pekee yao ili wafanye fujo.
    38) Balishebe – jini la magonjwa yasiyopona
    39) Sajiduri – jini linalokusaidia kupata pesa, kisha zinapotea kwa haraka
    40) Rumiran – linasimamia uwongo
    41) Lairlihabi – linasimamia hofu, kutojiamini na kukata tamaa
    42) Rohani – jini la mateso na fujo
    43) Betrah – jini hili linasimamia mapambo, kwa mwanamke huwa anajipamba isivyo kawaida, halikadhalika mwanaume
    44)Hanshari – linatumiwa sana na waarabu kulinda maduka yao
    45) Walihuni – linazunguka nyumba likilinda biashara
    46) Kurasih – jini la kupoteza fahamu
    47) Tarik – huondoa amani nyumbani, kazini. Linafanya watu wasielewane
    48) Atha – mungu wa kiarabu wa kuabudu sanamu
    49) Munakir – linapoteza watu kimiujiza
    50) Malik – jini la kumiliki biashara
    51) Ghatabu – jini la kulainisha macho wa wanawake. Wanakuwa wanarembua
    52) Khatuh – jini la uchawi wa kuchukua kucha, nywele na nguo za ndani
    53) Fanken – jini hili linasimamia mtu kuzunguza kiswahili cha pwani
    54) Zamzam – jini la marashi na kusimamia mikataba ya imani. Mkristo anaposilimishwa basi hutupiwa jini hili kupofushwa akili yake.
    55) Mukitala – linatumwa kuangalia kinga za watu
    56) Laufili – jini la uvivu
    57) Al-khah – linakula damu iliyoganda
    58 Abasaa – jini la hasira wivu na jeuri
    59) Aherumi – jini la homa za mara kwa mara
    60) Muba – jini la maradhi ya kuambikiza
    61) Kamariram – jini hili linatoa kinga kwa majambazi
    62) Zubiran – jini la uongo na uzushi
    63) Abadi – Jini la wizi, umalaya na ujambazi
    64) Muzamili- jini la matambiko ya kiarabu
    65) Ruhadi – jini la wizi, umalaya na umasikini
    66 Usuran – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
    67)Tubuyali – jini hili linamfanya mtu kuiba vitu vya ndani ya nyumba. Haibi nje ya nyumba
    68) Zirach – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
    69) Ashuran – jini la utasa na maradhi ya akina mama

    Dalili za uwepo wa majini katika maisha ya watu:
    Dalili zifuatazo ni za mtu ambaye ama ana majini au anafuatiliwa na majini:-
    • Unakuwa unaota ndoto upo ndani ya maji; ama unatembea ndani ya maji, unaingia majini au unatembea juu ya maji.
    • kila wakati unajikuta umeona au umeokota pete za dhahabu; mara nyingi majini wanaotaka kukutana kimwili na wanadamu hutegesha mikufu au pete ili kuunganishwa naye.
    • Mara nyingi unapotembea unakuwa unasikia harufu ya udi, ubani au marashi. Si lazima majini hayo yawe ndani yako lakini yanaweza kuwa yanakufuatilia ili kukudhuru.
    • Wakati wa usiku unasikia vitu vimepigwa kwenye bati au darini bila kujua chanzo na mwisho wake.
    • Kudondoka chooni ni dalili nyingine ya mtu anayefuatiliwa na majini.
    • Wewe ni mkristo lakini ukisikia adhana unajisikia kuipenda; na ndio maana watu wengi wakija kuombewa wanalipuka mapepo yanayopiga adhana.
    • Kukonda kupita kiasi.
    • Kupenda kuvaa nguo za nusu uchi.
    Jinsi ya kuyashinda majini
    Kinga ya majini haya ni nyepesi ni KUOKOKA na kusimama katika neno la Mungu. Kama unayo dalili yoyote iliyosababishwa na majini hayo hapo juu na umeokoka, taja jina la hilo jini, ni lazima litaitika, kisha liwashie moto.
    Kama hujaokoka usiyarushie mawe au moto yatakuumiza. Mwuone kiongozi yeyote wa kanisa akuongoze sala ya toba, kisha anza kuwasha moto, hakika yatakimbia na kuacha biashara, kazi, ndoa, na watoto wako huru.
    (iii) Mizimu
    Mizimu (Family spirit) ni mapepo yaliyotokana na malaika walioasi pamoja na shetani (Ufunuo 12:7-9) ambayo watu waliyafanya kama ndugu kutoka kizazi hadi kizazi katika ukoo. Mizimu inaweza kujidhirisha na kuonwa na wanadamu ama wanyama katika namna tofauti tofauti kama vile muonekano ( hapa mizimu ,huwatokea ndugu, jamaa na marafiki zao wakiwa katika maumbo ya sura zao wakati wanaishi duniani na mara nyingi huwatokea wakiwa na nguo walizo penda kuzivaa wakati wa uhai wao ), sauti, harufu( hapa kwenye harufu mzimu unapo mtokea muhusika,hujidhihirisha kwa harufu yake ya mwili ( kila mtu ana harufu yake ya mwili, watu huweza kuwatambua watu wao wa karibu kwa harufu zao za mwili ), ama pafyumu ( katika pafyumu, mzimu utamtokea mtu kwa harufu ya marashi ambayo alikuwa anapenda kuyatumia wakati yupo duniani katika ulimwengu wa nyama. Wakati mwingine, mzimu huweza kuwatokea ndugu jamaa na marafiki zake kwa kuwashika.

    Kwa ufupi mzimu huwa ni roho ambayo imewahi kuishi katika ulimwengu wa nyama kama mwanadamu ama mnyama.
    Ukweli kuhusu mizimu

    1; Mizimu ni malaika walioasi mbinguni

    2;Mizimu ni wapelelezi wa shetani

    3;Mizimu inauwezo wa kutoa nyaraka au taarifa ya mtu

    4;Mizimu inafanya kazi kupitia wafu.
    Waebrania 9;27 ”Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”
    5;Mizimu inafanya kazi kupitia waganga wa kienyeji

    Mzimu
    6.Hutumika katika uganga na utabiri
    Roho inayofanya kazi kupitia kwa waganga au watabiri na wanajimu ina chanzo chake kwa
    roho chafu. Watu wenye vipawa hivi wanaweza kuona yajayo au kufunua yaliyopo, kama
    msichana yule mwenye roho ya uaguzi alivyofanya kutabiri (Mdo 16:16). Ingawa mambo hayo
    yanaonekana ni ya maana, ni ya kishetani na hutumika kwa ajili ya faida ya kifedha kwa
    wanaotenda kazi hiyo; kwa kawaida huwa yanasababisha wasiwasi na hofu.

    7;Mizimu inauwezo wa kutunza taarifa za mtu, ukoo au kabila
    *Kuhusu wafu mtu akifa kuna sehemu mbili tu za kwenda.

    (a) Paradiso –ni mahali pa mangojeo kwa uzima wa milele.
    (b) Kuzimu –ni mahali pa mangojeo pa jehanamu

    Mtu akifa anatengana na wewe ukiomba mtakatifu yeyote ni kuomba mizimu, ibada za wafu ni kuabudu mizimu Luka 16:22-26{Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.}
    Ndugu zangu hakuna mawasiliano baina ya mfu na walio hai hivyo mizimu hubeba sura ya mtu aliyekufa na sauti yake na kumtokea mtu kwa ndoto au maono au hata kumtokea moja kwa moja,
    Jambo jingine la kutambua ni kwamba shetani huwafanya watu waamnini kwamba hata wao wakifa watakuja kuwatokea watu na hata wakiendelea na uovu hata wakifa wapo watu watawaombea na MUNGU atawatoa kuzimu na kuwapeleka mbinguni kitu ambacho hakipo na sio kweli. Hebu tafakari viongozi wengi wakuu wa serikali kuna siku maalumu umetengwa kwa mwaka kwamba ni siku yao na kila siku hiyo ikifika tunaenda kwenye makaburi yao na kuwaombea MUNGU awasamehe. Je wale wavuvi wanaokufa baharini na hakuna hata mmoja anayejua makaburi yao yalipo na hakuna hata mmoja anayewaombea je MUNGU siku hizi anaupendeleo? Yaani ukiwa rais wa nchi lazima uingie pema peponi maana utakua na waombeaji wengi tena watakua na juhudi kukuombea kila mwaka siku yako ikifika jambo ambalo sio la kweli, MUNGU atusaidie na tutambue kuwa muda wa kumpa YESU maisha ni sasa wala sio baada ya kufa maana tukifa tu ni kuzimu au mbinguni na sio vinginevyo. Katika Isaya 8:19 Biblia inasema
    ”Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong’ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?”
    Ndugu zangu pazia limekwisha kupasuka hivyo tunanaingia patakatifu moja kwa moja bila kuombewa na mtakatifu wa zamani maana BWANA YESU aliondosha kile kiambaza kilichokuwapo baina ya MUNGU na wanadamu ndiyo maana kupitia yeye(YESU) tunapata uzima bure kwa njia ya imani matendo 4:12 ”Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”.
    ila uzima huo tunaupata tungali hai sio tukifa.Kutumia majina ya watu wanaoitwa “watakatifu” ni kutafuta msaada kutoka kwa mizimu.Utakatifu wa mtu upo katika roho yake na ni Mungu pekee ndiyo anayewajua watakatifu wake,siyo anayetangazwa na mwanadamu.Tumepewa jina moja tu “Yesu” ambalo wanadamu tunapaswa kulitumia kutafuta wokovu.

    Mizimu no roho za shetani ambazo ni chukizo kwa MUNGU Kumbukumbu 18:9-12 ”Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo BWANA, MUNGU wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale. Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA; kisha ni kwa sababu ya hayo BWANA, MUNGU wako, anawafukuza mbele yako.”yanayozungumza hapo tuliposoma ni kuwahusu WAGANGA WA KIENYEJI, WACHAWI, WANAJIMU,WASIHIRI NA WANAOWAOMBA WAFU, mambo ambayo yote ni machukizo kwa MUNGU na wote hawa wanatumia mizimu kufanikisha mambo yao na kwa wale wanaomba maiti(wafu) hawa wanaomba mizimu hivyo wanahusika moja kwa moja na mizimu maana mtu aliyekufa hawezi kamwe kukusikia na hata kama anakutokea usiku tambua tu kwamba ni mizimu ambayo ni majini yanavaa sura ya ndugu yako na kuja kwako na kumbuka kuwa jini anaweza kuiga kila kitu kuanzia sauti hadi sura na kwa
    sababu shetani anataka umkosee MUNGU wakokwa kumtii yeye, atakuambia mambo mengi ya kufanya, Yupo mama mmoja alikua anatokewa na mama yake na kumwambia kwamba ”siku hizi umenisahau kabisa hata kaburi langu hufagii hivyo kesho asubuhi sana kafagie na unyunyizie damu ya kuku juu ya kaburi langu.Jambo hilo lilipelekea yule mama kwenda kwa mganga wa kienyeji na kumbuka kuwa hakuna mganga wa kienyeji asiyetumia mizimu na majini.Akajikuta anahusika na mambo mabaya zaidi hadi kumua mtoto wake maana yule mzimu alianza kwa kutaka damu ya kuku baadaye anataka kafara ya damu ya mtoto wa yule mama maana ilifika kipindi vitisho vikawa vyingi na kwa sababu mama yule alishaingia maagano na mizimu ile kwa kutii maelekezo ya kwanza akaanza kupata shida sana na akaambiwa atapata mikosi maisha yake yote na hali hiyo ikapelekee kuua mtoto wake na cha ajabu shetani alimtumia yule mganga wa kienyeji kuongeza vitisho kwa mama na kutoa ushauri wa kumwua mtoto. Ndugu zangu jina la YESU KRISTO pekee linaloweza kuondoa mizimu maishani mwako hivyo kama unasumbuliwa na mikosi ya ukoo, mizimu ya ukoo, utasa au magonjwa ya ukoo basi kimbilia kwenye maombezi katika kanisa la kiroho karibu na wewe na utafunguliwa na kuwa salama kabisa mbali na laana zote za ukoo na masharti ya kishetani na katika BIBLIA kitabu cha Mambo ya walawi 19:4 inasema ”Msigeuke kuandama sanamu, wala msijifanyizie miungu ya kuhusubu mimi ndimi BWANA, MUNGU wenu.” ndugu moja ya miungu ambayo wanadamu wanaiabudu ni mizimu na kumbuka kwamba waganga wa kienyeji wanatumia mizimu katika kazi zao na ndio maana mama mmoja ambaye sasa ameokoka alikua mganga wa kienyeji zamani aliwahi kuniambia kuwa kama mgojwa mwenye majini akija kwake kutibiwa yeye anachofanya anaongeza majini ndani ya mgojwa na kumpa mashariti ya kufanya ili abaki mzima na moja ya mashariti hayo alikua anawaambia wateja kurudi kwake kila baada ya miezi mitatu maana anajua muda wa majini kutaka damu umefika na kila mteja akija lazima aje na kuku mwenye rangi moja kama ni mweupe awe mweupe pote na kama ni mweusi awe mweusi pote.Katika 1 Samweli 28:7 BIBLAI inasema ”Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori.” Huyu Sauli alikua ni mfalme wa taifa la Israel ambaye aliamua kuwafuata waganga wa kienyeji na kitendo hicho kilikua ni machukizo makuu kwa MUNGU na kupelekea kunyang’anywa ufalme akapewa Daudi na huyo sauli akafa vitani na jambo lile wa kwenda kwa waganga liliongeza balaa kwa taifa badala ya kupunguza . Ndugu please please usikubali kwenda kwa waganga wa kienyeji wala kusoma nyota maana watakupoteza na utakua mbali sana na MUNGU wako aliyekuumba na hakika kwa kitendo hivyo utakua unajichimbia shimo mwenyewe. ni heri kumpelekea BWANA YESU shida zako na yeye ni mwaminifu na wa haki atakuponya na utakua huru daima maana amesema katika Mathayo 11:28 kwamba ”Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”
    MUNGU akubariki sana wewe usiye na mizimu maishani mwako maana ulimpa BWANA YESU maisha yako na ukatengwa mbali na mizimu ya ukoo ambao ipo katika kila mtu ambaye hajasafishwa kwa damu ya YESU maana mizimu hiyo ipo tangu kizazi na kizazi na mambo mengi yanawapata ukoo fulani fulani tu kwa sababu ya mizimu, ukielewa hivyo chukua hatua kwa kumpa YESU maisha yako na utakua huru pia utakua ufunguo katika ukoo wetu kuwafukuza mizimu ya mababu ambayo imeleta balaa kubwa katika maisha. Maana wapo watu wao wanajifahamu ni watu wasio na akili shuleni yaani ukoo mzima hakuna anayeweza kufaulu kwenda sekondari na hawajui tatizo ni nini lakini kumbe tatizo ni mizimu ya ukoo.

    MAGOJWA YANAYOSABABISHWA NA MIZIMU

    Kuna magonjwa ya ukoo ya kuhama kutoka kizazi hadi kizazi na magonjwa haya husababishwa na mizimu.
    Pia kuna baadhi ya magonjwa yanasababishwa na mizimu mfano Pumu, kuumwa miguu, miguu kufa ganzi, vivimbe mbalimbali katika mwili, kutokukua kiroho, matumizi mabaya ya pesa na kutokupona magonjwa. Ndugu kimbilia maombezi na utakuwa huru mbali na uonevu huu wa shetani.

    Mizimu pia hutumia manabii wa uongo kwa udanganyifu au upotoshaji, mizimu pia hutumiwa na wachawi na wapandisha pepo, Mizimu pia hutumiwa na dini za uongo.

    3.MAPEPO
    Mapepo ni malaika walio anguka au walio asi kule mbinguni na yule shetani.Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa nyoka wa zamani aitwaye ibilisi na shetani audanganyaye ulimwengu wote akatupwa hata nchi na malaika zake wakatupwa pamoja naye.”
    Mapepo wana nguvu sana lakini Mungu amewapa kadiri au kipimo. imeandikwa Marko 1:27 “Wakashangaa wote hata wakaulizana wakisema ni nini hii ni elimu mpya! maana kwakuwa waamuru hata pepo wachafu nao wamtii!”.
    Mapepo ni “malaika waliofanya dhambi,” viumbe wa kiroho waliomwasi Mungu. (2 Petro 2:4) Malaika wa kwanza kabisa kuasi na kuwa pepo alikuwa Shetani Ibilisi, ambaye Biblia inamwita “mkuu wa pepo.”—Mathayo 12:24, 26, Biblia Habari Njema.
    Malaika walioasi katika siku za Noa
    Biblia imerekodi simulizi la malaika walioasi kabla ya Gharika ya Siku za Noa: “Ndipo wana wa Mungu wa kweli wakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu, kwamba ni wenye sura ya kupendeza; nao wakajichukulia wake, yaani, wote waliowachagua.” (Mwanzo 6:2) Malaika hao waovu, walishuka duniani na ‘kuyaacha makao yao wenyewe yanayofaa,’ yale ya mbinguni na wakajivika miili ya wanadamu ili wafanye ngono na wanawake.—Yuda 6.
    Mungu alipoleta gharika, malaika hao waasi walijivua miili ya kibinadamu na kurudi mbinguni. Hata hivyo, Mungu aliwafukuza katika familia yake. Mojawapo ya adhabu walizopewa ni kwamba mapepo wamezuiwa kujibadili ili wawe na miili ya kibinadamu na hawawezi tena kufanya hivyo.—Waefeso 6:11, 12.
    Yesu ananguvu kuliko mashetani (Luka 4:35-36) “Yesu akamkemea akisema fumba kinywa mtoke. Ndipo yule pepo akamwangusha katikati, akamtoka asimdhuru neno, Mshangao ukawashika wote wakasemezana wakisema ni neno gani hili maana waamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu nao hutoka.”
    Mashetani wako je leo? adui haonekani lakini vuta viko imeandikwa Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”
    Tukinyenyekea mbele za mungu yule shetani atatoroka ( Yakobo 4:7 ) “Basi mtii mungu, mpingeni shetani naye atawakimbia.”

    MUNGU akubariki sana
    Wako katika kueneza ujumbe na matakwa ya MUNGU kwako.
    Benisius Danda
    Kwa msaada wa mtandao na Testimonies
    ratshega@gmail.com

    ***************************************************************************

    Like

  286. Benn says:

    Skip to News Feed
    Facebook
    Search Facebook
    Benn
    Home4
    Friend Requests
    1
    Messages
    1
    Notifications
    Account Settings
    People You May Know
    See All
    People You May Know
    Zaina Luambano
    2 mutual friends
    Sahuda Asedy
    1 mutual friend
    Aloyce Singano
    Friends with Ney
    Stanford JR Kifaru
    28 mutual friends
    Catherine Mbano
    1 mutual friend
    Rahul Raj
    1 mutual friend
    English (US) · Kiswahili · हिन्दी · ગુજરાતી · Español
    Privacy · Terms · Advertising · Ad Choices
    · Cookies ·
    More
    Facebook © 2016

    News Feed
    Max Shimba Ministries
    February 12, 2014 ·

    JE MUNGU WA WAISLAMU (ALLAH S.W) NA MUNGU WA WAKRISTO (YEHOVA) NI MMOJA?

    UTANGULIZI.
    Imekuwa ni kawaida sasa kwa miaka zaidi ya ishirini hivi, kusikia katika mihadhara inayoendeshwa na wahadhiri wa dini ya Uislamu, ambayo imeenea sehemu mbalimbali Duniani na haswa katika nchi za Africa Mashariki na Kati,(East and Central Africa). Wahadhiri hao hufundisha jamii kupitia Qurani na Biblia kwa kusema kuwa Mungu ni Mmoja tu. Wasema Mungu kwa Kiebrania anaitwa Yehova , kwa Kiarabu Allah, kwa Kiingereza God na kwa Kiswahili ni Mungu. Kwa hivyo wasema Mungu Allah kama Qurani inavyofundisha, ndiye Yehova kama Biblia inavyofundisha. Mihadhara hiyo inayoendeshwa na Waislamu imeenea sana, mfano Nchini Tanzania kuna vikundi vingi na kimoja wapo kinaitwa Al-Marid International Propagation Center. Hawa wameandika katika bango lao kwa kunukuu katika Biblia maneno aliyoandika Mtume Paulo katika Waefeso 4:4-6. Maneno waliyoyanukuu yanasema hivi “Bwana mmoja , Imani moja ….., Mungu mmoja , naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote. Nilipotembelea mkoa wa Morogoro pale mjini, eneo la kiwanja cha ndege nikaona Msikiti mmoja umeandikwa maneno haya ya Waefeso 4:4-6. Na nilipotembelea mji wa Nairobi Nchini Kenya pia nikaona kuna vikundi vingi vinavyoendesha mihadhara na kikundi kimoja wapo kinaitwa Kibera Islamic Propagation Centre. Hawa nao katika bango lao wameandika ujumbe unaosema hivi “Acha Biblia Ijisemee na kunukuu injili aya hii” Yohana 8:32 Tena mtaifahamu kweli nayo hiyo kweli itawaweka huru.

    Kwa hivyo utaona kuwa wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu hufundisha jamii kwa kutumia Qurani na Biblia na kusema Allah Sub-Hana Wataala ndiye YEHOVA. Fundisho hili wanalieneza kwa kupitia Radio, Vijarida, Mihadhara, vitabu na Kanda (cassettes) za Video na Audio. Na hivyo kuwafanya baadhi ya Wakristo kuacha Imani yao na kuingia katika Dini ya Uislamu. Na baadhi ya Wakristo wengine ingawa hawajabadili dini wanaamini hivyo. Swali la muhimu la kujiuliza kwa kila mkristo, je, ni kweli Mungu Allah kama inavyotuhadithia Qurani ndiye Yehova kama Biblia inavyotufundisha? Nakusihi fuatilia somo hili kwa makini ili kujua Ukweli……

    SEHEMU KUU ZA SOMO HILI NI HIZI……

    1. Hoja za waislamu kusema Allah ndiye Yehova.

    2. Je, jina la Mungu kadiri ya Qurani na Biblia ni moja?

    3. Je, Malaika mkuu wa Allah ndiye wa Yehova?

    4. Je, ni nani muumba,Allah au Yehova?

    5. Mji aliochagua Allah je, ni sawa na wa Yehova?

    6. Allah anavyofundisha kuhusu kujitakasa nafsi je, ni sawa na Yehova?

    7. Je, mbingu ya Yehova ni sawa na ya Allah?

    8. Mwisho wa wanaomwabudu Allah ni wapi?

    1. Hoja za waislamu kusema Allah ndiye Yehova

    Wahadhiri wa Dini ya Uislamu wanasema Mungu Allah ndiye Yehova kwa sababu Manabii wa Mungu kadiri ya Biblia na Qurani walifundisha kwa kusema Mungu ni mmoja tu. Na wanasoma aya hizi…

    Nabii Musa alivyosema

    Kumbukumbu la Torati 6:4

    Sikiza ee Israeli; BWANA Mungu wetu BWANA ndiye mmoja.

    Nabii Isaya alisema hivi

    Isaya 45:18,21

    Maana BWANA , aliyeumba mbingu, asema hivi, yeye ni Mungu ,ndiye aliyeumba Dunia na kuifanya ….. si mimi BWANA? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi. Mungu mwenye haki , mwokozi hapana mwingine zaidi ya mimi.

    Nabii Daudi Alisema

    Zaburi 86:10

    Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, wewe ndiwe mfanya miujiza , ndiwe Mungu peke yako.

    Yesu alisema hivi

    Yohana 17:3

    na uzima wa milele ndio huu wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliye mtuma

    Paulo naye Alisema hivi

    1 Wakorintho 8:4

    Basi kwa habari ya kuvila vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu; twajua ya kuwa sanamu si kitu katika ulimwengu, na yakuwa hakuna Mungu ila mmoja tu.

    Hapa wahadhiri wa Dini ya Uislamu wanasema Manabii wote kadiri ya Biblia wanafundisha kuwa Mungu ni mmoja tu. Je, Muhammad (s.a.w.) alifundisha nini kuhusu Mungu? Wanasoma aya hizi za Qurani……..

    Qurani 41:6 Suratul Haa Mym Sajdah (Kusujudu)

    Sema; bila shaka mimi ni mtu kama nyinyi. Nimeletewa Wahyi (inafunuliwa kwangu)ya kwamba Mungu wenu ni Mungu mmoja tu……

    Hapa wahadhiri wanasema kama vile manabii wote walifundisha Mungu mmoja ndivyo ilivyo fundisha Muhammad.

    Qurani 29:46-47 Suratul Al- Ankabuut (Buibui).

    Wala mshibishane na watu waliopewa kitabu (kabla yenu) ila kwa yale (majadiliano) yaliyo mazuri, isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao. Na semeni :tunaamini yaliyoteremshwa kwetu, na yaliyoteremshwa kwenu. Na mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja : nasi ni wenye kunyenyekea kwake. Na namna hivi tumekuteremshia kitabu (hiki cha Qurani) basi wale tuliowapa kitabu (kabla ya hiki kama taurati na injili) wanakiamini (hiki kitabu ulichoteremshiwa kwani hakipingani na hivyo walivyoteremshiwa). Na miongoni mwa hawa (Waarabu wasiokuwa na Kitabu chochote)wako wanaokiamini. Na hawazikatai aya zetu isipokuwa wale wanaotaka kuficha haki.

    Hapa wahadhiri wa kiislamu wakisha soma aya hizi husema vitabu vya Torati na Injili havipingani na Qurani, na vitabu hivyo walipewa Wayahudi na Manasara(yaani Wakristo) na Mungu wa Waislamu na Wakristo ni mmoja tu.

    Je, hoja hii ni kweli? Nitaijibu huko mbele.

    Majibu kuhusu Mungu mmoja

    Ukitazama kwa haraka haraka namna wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu wanavyolinganisha aya za Qurani na Biblia unaweza ukashawishika kuamini hicho wanachokifundisha, lakini ni vyema tukajifundisha kwa undani kadiri ya Qurani na Biblia na kisha tuone kama kuna ukweli juu ya hayo mafundisho yao, ya kusema Allah Sub-hana Wataala ndiye Yehova.tukumbuke kuwa Mungu tunayeabudu alitutahadhalisha sana Wakristo kwa kusema hivi…

    Kutoka 20:1-3

    Mungu akanena maneno haya yote akasema Mimi ni BWANA Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa usiwe na Miungu mingine ila mimi.

    Tahadhari hii Ya Mungu wetu ya kusema usiwe na Miungu inamaanisha kuwa Miungu mingine yenye kuabundiwa na watu ipo. Kwa sababu katika Biblia neno Mungu Kiebrania“Elohim” Kiyunani “Theos” limetanjwa mara 3979 lakini pia miungu ya uongo imetanjwa mara 271. baadhi ya miungu hiyo ya uongo ni hii

    mungu Dargoni Waamuzi16:23

    mungu Baal Wafalme 18:21

    mungu mke wa Waefeso aitwae Artemi Matendo 19:24-28.

    Aidha tusomapo Qurani pia imetaja miungu mbalimbali iliyokuwa inaabundiwa kule Makka nayo ni hii;

    Qurani 53:19-20,23 Suratul An- Najm (Nyota).

    19. Je, mumewaona Lata na Uzza? 20. Na Manata (mungu wenu) mwingine wa tatu (kuwa ndio waungu hao badala ya mwenyenzi mungu)? 23. hayakuwa haya (majina ya Lata mungu mwanamke na Uzza mungu mwanamke mwenye enzi. Na Manata mungu mwanamke anayeneemesha ila ni majina tu mliowapa nyinyi na baba zenu…..

    Hivyo basi tunaona kuwa miungu yenyewe kuabudiwa ni mingi na kila mwenye kuabudu humtegemea huyo mungu wake na kusema ni mmoja. Mfano waliyemuabudu Dagoni walisema ni mungu mmoja, waliyemwabudu Baali walisema ni mungu mmoja , waliyemwabudu Artemi walisema Artemi ndiye mungu mkuu. Kadharika Manabii.

    walimtumikia Mungu mmoja aitwaye Yehova, naye Muhammad alimwabudu mungu mmoja aitwaye Allah. Ninachotaka kukifundisha kwa jamii ijue je, huyo Allah ndiye Yehova?,

    2: Je, jina la Mungu kadiri ya Qurani na Biblia ni moja?

    Jambo moja la msingi linalo tambulisha kitu au mtu, mnyama au chochote kile ni jina , hivyo ili tuweze kujua kama Mungu anayeabudiwa na Waislamu ndiye tunayemuabudu Wakristo, ni lazima tuangalie jina. Je, ni moja?

    Qurani 17: 110 Suratul Bani Israil (Wana wa Israil)

    Sema; muombeni (Mwenyenzi Mungu) kwa (jina la )Allah au muombeni (kwa jina la ) Rahman. Kwa jina lolote mnalomwita (katika haya itafaa). Kwani ana majina mazuri mazuri………

    Hapa tunaona Allah anafundisha kwa Waislamu kuwa wamuombe kwa jina la Allah au Rahman. Ukisoma Qurani utaona jina Allah limetajwa mara 2,866, kumbuka Qurani ina Juzu 30 Sura 114. hivyo Mungu anaye abudiwa na Waislamu kadiri ya Qurani jina lake anaitwa Allah.

    Jina la Mungu anayeabudiwa na Wakristo ni hili;

    Kutoka 6:2-3

    Kisha Mungu akasema na Musa akamwambiaaa “Mimi ni YEHOVA Nami nalimtokea Ibrahimu, na Isaka na Yakobo, kama Mungu mwenyenzi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.

    Hapa tunaona Mungu tunayemuabudu Wakristo analitambulisha jina lake kwamba ni Yehova katika Biblia limetumika neno au jina BWANA, kwa Kiingereza wanasema LORD, likimaanisha jina lililo Takatifu sana la Mungu katika Biblia jina hili limetanjwa mara 6751. kumbuka Biblia ina jumla ya vitabu 66 Sura 1189 Aya 31,102.

    3: Je, Malaika mkuu wa Allah ndiye wa Yehova?

    Ikiwa Allah ndiye Yehova, basi ni wazi kuwa malaika mkuu atakuwa mmoja pia. Ikiwa si mmoja hata malaika mkuu watakuwa tofauti. Tuanze kuangalia Allah anavyosimulia katika Qurani naye anasema hivi

    Qurani 81:19-21 Suratul At-Takwyr( Kukunja/jua litakapokunjwa)

    Kwa hakika hii (Qurani ) ni kauli (aliyokuja nayo) mjumbe mtukufu (Jibrili) Mwenye nguvu,mwenye cheo cha hishima kwa mwenyenzi Mungu. Anayetiiwa huko (mbinguni na malaika wenziwe) kisha muaminifu.

    Ufafanuzi wa aya hizi.

    ulio ndani ya Qurani unaelezea aya hizi 19-21, unafundisha hivi…….

    Mjumbe mtukufu na mwenye kutiiwa huko mbinguni ni Jibrili, ambaye ndiye mkubwa wa malaika wote

    Malaika mkuu wa Mungu Yehova ni huyu;

    Yuda 1:9

    Lakini Mikaeli Malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthumbutu kumshitaki kwa kumlaumu bali alisema Bwana na akukemee

    hapa tunaona aya zinatufundisha waziwazi kuwa malaika mkubwa wa Mungu aitwae Allah anaitwa Jibril na Malaika mkuu wa Mungu wetu Yehova anaitwa Mikaeli. Swali; Kwa kuwaMalaika hao ni tofauti, je, Allah ndiye Yehova? Kwa kujua zaidi tofauti ya malaika, jipatie nakala ya somo la: Malaika Jibrili na Gabrieli, je ni Malaika mmoja. Somo hilo tunalo, jipatie.

    4: Je, ni nani muumbaji, ni Allah au Yehova?

    Kila mtu mwenye kufuata Dini huamini kuwa Mungu ndiye muumbaji ambaye ameumba wanandamu, wanyama na vyote tunavyoviona na vile tusivyoviona. Hivi yafaa tuangalie kile kinachosemwa na Yehova kuhusu uumbaji na vile Allah anavyosema. Je, kauli zao zinapatana au zinatofautiana?

    Je, mtu ameumbwa kwa mfano wa nani?

    Allah anasema hivi;-

    Qurani112:1-4 Suratul Al-Ikhlas (utakaso)

    Sema: Yeye ni Mwenyenzi Mungu mmoja (tu) Mwenyenzi Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyake vyote kwa kumuabudu na kumuomba na kumtegemea) Hakuzaa wala hakuzaliwa Wala hana anayefanana naye hata mmoja.

    Kadiri ya aya hii Allah asema kuwa mungu hakuzaa wala hakuzaliwa wala hana mfano wa mtu au watu Yehova anasema hivi kuhusu mtu au watu……

    Mwanzo1:26-27

    Mungu akasema “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini, ndege wa angani na wanyama , na nchi yote, pia na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

    Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba.

    Hapa tunaona Mungu wetu Yehova ameumba mtu kwa mfano wake, lakini Allah anasema hana anayefanana naye hata mmoja……Swali kwako mfuatiliaji: Je, Allah ndiye Yehova? Tafadhali usome aya hizi ili kujua zaidi (Mwanzo 5:1-2, 9:6, 1Korintho 11:7, Kolosai 1:15, 3:10, Matendo 17:28-29, Yakobo 3:9). Pengine waweza kusema Je, Mungu amefanana na mimi kivipi?Jua kwamba Mungu ni Roho (Yohana 4:24) Naye alitupa pumzi(yaani roho ya uhai (Mwanzo 2:7))isitoshe Mungu ndiye Baba wa roho zetu (Waebrania 12:9) Mungu anasema Roho zetu ni mali yake(Ezekieli 18:4,Hesabu 16:22)

    Kuapa kwa Mungu kuhusu viumbe

    Qurani 91:1-7 Suratul Ash-Shams (Jua)

    Naapa kwa jua na kwa mwangaza wake. Na kwa mwezi unapoliandama. Na kwa mchana unapolidhihirisha. Na kwa usiku unapolifunika.Na kwa mbingu na kwa Aliyezijenga. Na kwa ardhi na Aliyeitandaza. Na kwa nafsi (roho) na Aliyeitengeneza.

    Qurani 92:1-3 Suratul Al-Layl (Usiku)

    Naapa kwa usiku ufunikapo (kila kitu). Na kwa mchana uangazapo. Na kwa aliyeumba kiume na kike.

    Hapa tunaona Allah Mungu anayeabudiwa na Waislamu anaapa kwa mbingu na kwa aliyezinjenga, kwa ardhi na aliyeitandaza. Je, huyo mtandazi wa ardhi na mjengaji wa mbingu ni nani? Qurani inaendelea kuhadithia hivi……..

    Qurani 45:22 Suratur AL- Jathiyah (kiyama/ kupiga magoti)

    Na mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi kwa haki…

    Qurani 44:7-8 Suratul Ad-Dukhan (moshi)

    Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake,ikiwa mnayo yakini (basi yakinisheni haya) Hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye anahuisha na kufisha. Mola wetu na ni mola wa wazee wenu (wote) wa mwanzo (na mola wa kila kitu)

    Hapa tunaona kuwa Allah kupitia Qurani anasema kuwa mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi na tena anasema hakuna aabudiwaye ila yeye. mjengaji wa mbingu na mtandazaji wa ardhi anajieleza hivi ……

    Isaya 44:24

    BWANA,mkombozi wako yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi, “Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote, nizitandaye mbingu peke yangu, niienezaye nchi. Ni nani aliye pamoja nami?”

    Mungu wetu Yehova anasema mimi ninafanya vitu vyote.

    (Soma Isaya 45:6-7, 11-12, Yeremia 27:5) Bila shaka Yehova ndiye muumbaji wa vitu vyote

    JE Mungu Yehova aliapia vitu alivyoviumba kama Allah?

    Isaya 45:22-23

    Niangalieni mimi mkaokolewe, Enyi ncha zote za dunia. Maana mimi ni Mungu hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba, mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.

    Waebrania 6:13-16

    Kwa maana Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake. akisema “Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza, Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo kwa kuyathibitisha.

    Hapa tunaona Mungu wetu Yehova haapi kwa mtu wala vitu alivyoviumba kama Allah anavyoapa, bali Yehova anasema “Naapa kwa nafsi yangu”.Waweza pia kusoma jinsi Yehova alivyoapa kwa nafsi yake katika aya hizi;-(Isaya 14:24 na Mwanzo 22:16)

    5: Je, mji aliouchagua Allah ni sawa na wa Yehova?

    Mji wa Allah:

    Qurani 27:91 An-Naml (sisimizi/mchwa/wadudu chungu)

    Bila shaka nimeamrishwa nimuabudu mola wa mji huu (wa Makka) ambaye ameutukuza na ni vyake tu (Mwenyezi Mungu) vitu vyote…

    Qurani 3:96 Suratul Aal-Imran (watu wa Imram)

    Kwa yakini nyumba ya kwanza iliyowekwa kwa ajili ya watu (kufanya ibada) ni ile iliyo Makka yenye baraka na uwongozi kwa ajili ya walimwengu wote.

    Qurani 106:3-4 Suratul Quraysh (Makureshi-kabila)

    Basi nawamuabudu Bwana wa nyumba hii (Al-ka’ba) Ambaye anawalisha (wakati Waarabu wenzi

    wao wamo) katika njaa na anawapa amani wakati wenzi wao wamo katika khofu.

    Hivyo tunaona kuwa Allah ndiye bwana wa Al-ka’ba kadiri ya aya hii na Al-ka’ba iko katika Makka. Kupitia aya hizi tunaona Allah mungu anayeabudiwa na Waislamu amechagua mji wa Makka kuwa ndio mji wake mtakatifu na tena Muhammad (s.a.w) aliamrishwa amuabudu mola wa mji huo wa Makka ambaye ndiye Allah.

    Je, Mungu wetu aitwae Yehova alichagua mji gani? Endelea ……..

    Mji aliouchagua Mungu wetu Yehova ni huu…

    2 Nyakati 6:4-6

    Akasema, BWANA, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena kwa kinywa chake na baba yangu Daudi, akalitimiza kwa mikono yake, akasema, Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wowote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu yeyote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, lakini nimeuchagua Yerusalemu, jina langu liwe humo, na Daudi nimemchagua awe juu ya watu wangu Israeli.
    Maandiko hayaelezi mji mwingine wowote aliouchagua Mungu wetu hapa duniani bali ni mji wa Yerusalemu tu. (tazama 2 Nyakati 12:13,Ezra 6:12; 7:15,27; Zaburi 26:8; Zakaria 2:12)

    Kupitia aya hizi tunaona Mungu wetu Yehova, mji wake aliouchagua niYerusalemu. Neno Yerusalemu ni la lugha ya Kiebrania na maana yake ni “chimbuko la amani”. Hata Waisraeli walipokuwa mbali na mji wa Yerusalemu bado walipiga magoti na kuelekeza nyuso zao Yerusalemu. (Tazama Danieli 6:10). Mji aliouchagua Yehova ni Yerusalemu, na mji aliouchagua Allah ni Makka. Na hii ndio tofauti ya mji wa Allah na Yehova.

    6: Allah anavyofundisha kujitakasa nafsi, je ni sawa na Yehova?

    Allah anafundisha hivi….
    Qurani 53:32 Suratul Al-Najm (nyota)

    Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipokuwa makosa hafifu (hakuma aliyesalimika nayo) bila shaka, mola wako ndiye mwenye maghufira mengi yeye ndiye anayekujueni sana tangu alipokuumbeni katika ardhi na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. basi msizitakase nafsi zenu….

    Qurani 12:53 Suratul Yusuf

    Nami sijitakasi nafsi yangu, kwa hakika (kila) nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu isipokuwa ile ambayo mola wangu ameirehemu. Hakika mola wangu ni mwingi wa kusamehe (na) mwingi wa kurehemu.

    Kadiri ya Qurani Allah anayo nafsi pia Tazama Qurani 5:116. Kwa hivyo hapa tunaonaAllah ana agiza watu wasizitakase nafsi zao na tena anasema sijitakasi nafsi yangu. Hii ni ajabu sana!

    Mungu wetu Yehova anavyosema kuhusu kujitakasa nafsi, yaani utakatifu:

    Isaya 43:3

    Maana mimi ni BWANA Mungu wako, mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako. Nimekutoa Misri kwa ukombozi wako, nimetoa Kushi na Sheba kwa ajili yako.

    Hapa tunaona Mungu anasema ‘Mimi ni mtakatifu’, hili pia ni jina la sifa la Mungu wetu Yehova kwa lugha ya Kiebrania husema ‘kadosh’. Nabii Isaya ameandika kuwa Mungu ni Mtakatifu mara 32 kwa ufupi tu soma Isaya 40:25, 48:17 na 57:15. Isitoshe kwa kuwa Mungu wetu Yehova ni mtakatifu pia aliagiza kwetu hivi.

    Walawi 11:44

    Kwa kuwa mimi ni BWANA Mungu wenu takaseni nafsi zenu basi; iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu, wala msitie uchafu nafsi zenu…

    Mtume Petro anatuagiza hivi;

    1 Petro 1:15-16

    Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.Kwa maana imeandikwa, mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

    Mtume Paulo pia ameagiza kujitakasa nafsi na kuwa watakatifu(2 Wakorintho 7:1) waweza pia kusoma agizo hilo la kuwa watakatifu katika Walawi 19:2, 20:26.

    Kwa hivyo tunaona Yehova anaagiza tujitakase nafsi zetu ili tuwe watakatifu, lakini Allah anaagiza kwa Waislamu kuwa wasizitakase nafsi zao.

    Swali kwako mfuatiliaji, Je, Allah ndiye Yehova?

    7: Je, mbingu ya Yehova ni sawa na pepo (mbingu) ya Allah?

    Mbingu ya Yehova:

    Luka 20:34-36

    Yesu akawaambia wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa, lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule. Na kule kufufuka katika wafu hawaoi wala hawaolewi. wala hawawezi kufa tena. Kwa sababu huwa sawa sawa na malaika, nao ni wana wa Mungu kwa vile walivyo wana wa ufufuo.

    Maandiko haya yanatuthimbitishia Wakristo kuwa tutakapofufuliwa na kuingia mbinguni, hakuna mambo ya kuolewa wala kuoa, maana tutakuwa na miili ya kiroho (1 Korintho 15:43-54) Aidha maandiko yanatufundisha kuwa ufalme wa Mungu siyo kula wala kunywa bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu. (Tazama Warumi 14:17). Mungu wetu anafundisha wazi wazi kuwa kule mbinguni katika ufalme hakuna njaa, wala kiu wala jua kutupiga (Ufunuo 7:16-17.)

    Pepo au Mbingu ya Allah itakuwa hivi:

    i). Maghorofa

    Qurani 39:20 Suratul Zumar (makundi/vikosi)

    Lakini waliomcha mola wao watapata ghorofa zilizojengwa juu ya ghorofa chini (mbele) yake hupita mito. Ndiyo ahadi ya Mwenyenzi Mungu, Mwenyenzi Mungu havunji ahadi yake.

    ii) mito ya maji, maziwa, ulevi, asali na matunda

    Qurani 47:15 Suratul Muhammad

    Mfano wa pepo waliyoahidiwa watawa (wacha Mungu itakuwa hivi). Imo mito ya maji yasiyovunda, na mito ya ulevi wenye ladha kwa wanywao na mito ya asali iliyosafishwa. Tena humo watapata matunda ya kila namna, na samahani kutoka kwa mola wao. Basi hao watakuwa sawa na wale wataokaa motoni na kunyweshwa maji yachemkayo yatakayokata chango zao?.

    Je Matunda hayo ni sawa na ya wapi?

    Qurani 2:25 Suratul Al- Baqarah (ngombe jike)

    Na wabashirie walioamini na kufanya vitendo vizuri, kwamba watapata mabustani yapitayo mito mbele yake. Kila mara watakapopewa matunda humo kuwa ni chakula watasema “haya ndiyo yale tuliyopewa zamani (ulimwenguni) kwani wataletewa (matunda hayo) hali yatakuwa yamefanana (na yale waliyokuwa wakiyajuwa ulimwenguni wataletewa kwa sura hiyo lakini

    utamu mwingine kabisa) na humo watapata wake waliotakasika (na kila mabaya na machafu) na watakaa milele humo.

    iii). Watapata wanawake aina hizi na nyama za ndege

    Qurani 56:15-23 Suratul Al Waaqiah (Tukio) nanukuu aya ya 21-23 tu

    Na nyama za ndege kama watakavyotamani (wenyewe). Na wanawake wenye macho mazuri na makubwa (ya vikombe). (wanapendeza na safi) kana kwamba ni lulu zilizofichwa (katika machaza yake, ndio kwanza zinapasuliwa)

    Qurani 37:48-49 Suratul As-Saaffat (Wapangao mistari)

    Na pamoja nao watakuwa wanawake wenye macho mazuri makubwa. (Safi) wanawake hao kama mayai (ya mbuni) yaliyohifadhiwa.

    Qurani 37:44-46 Suratul As-Saaffat (Wapangao mistari)

    Wako juu ya vitanda (viti vya enzi vya fahari), wamekabiliana (wanazungumza). Wanazungushiwa gilasi zenye (vinywaji) safi.Vyeupe yenye ladha kwa hao wavinywao.

    Kupitia aya hizi tumeona kuwa Allah Sub-haana Wataala Mungu anayeabudiwa na Waislamu ametoa ahadi ya kuwaingiza Waislamu peponi (mbingu) na kuwa watapata mito ya maji, mito ya maziwa na ulevi na pia mito ya asali vilevile watapata matunda,nyama ya ndege na pia wataozeshwa na Allah mungu wao wanawake wenye macho makubwa kama mayai ya mbuni. na wengine makubwa kama vikombe.

    Jambo la kushangaza zaidi ni pale tunaposoma kitabu cha Hadithi, maana imani ya Dini ya Uislamu imejengwa pia katika vitabu vya hadithi. Soma

    Qurani 42:10 Suratul Ash-Shuura (mashauriano)

    Mkihitalifiana katika jambo lolote (rejeeni kitabu cha Mwenyenzi Mungu na Hadithi za mtume kwani)…

    Tunaposoma kitabu cha Hadithi ya mtume kiitwacho Sunnan Ibn-1- Majah vol 5 ukurasa wa 546 Hadithi No: 4337 kuna maelezo haya

    Imesimuliwa na Abu’ Umama ya kuwa mjumbe wa Allah (baraka na amani ya Allah iwe juu yake) alisema Allah hatamruhusu yeyote kuingia peponi ila kwa idhini ya Allah, Mwenye nguvu na utukufu naye atamwozesha mwanamume wake sabini na mbili. Wawili watakuwa mabikira (mahurul-ain) yaani wanawake wa peponi wenye macho makubwa, na sabini watakao warithi ambao watu (mabwana zao) wametupwa katika moto wa jahanamu kila mmoja wao (hao wanawake) wana uke wa kupendeza. Na mwanamume, Nguvu ya uume wake katika kujamiana hautapinda (kusinyaa) bali utadumu sana

    Kwa kiingereza Hadithi hii inasomeka hivi:-

    Abu-Umama (Allah be pleased with him) reported that Allah’s messenger (peace and blessings of Allah be upon him)said Allah will not admit anyone in the paradise but Allah the mighty and Glorous, will marry him with seventy two wives two will from virgins (haurine) with big eyes and seventy will be his inheritance from the people of the Hell- Fire (1).Everyone of them will have apleasant vagina and he (the man) have sexual organ that does not bend down (during sexual intercouse)

    Hivi ndivyo Allah Mungu wa Waislamu alivyoahidi. Hili ni jambo ambalo kwa Mkristo linamshangaza sana kwani jambo hili linalofundishwa na Allah halipo kabisa kwa Mungu wetu Yehova hapa ulimwenguni ndiko kwenye ulevi,matunda,nyama za ndege, kuoana, maghorofa, magari, mito, bahari na vinginevyo.

    Tafakari, je huyo Allah ni nani?

    8: Mwisho wa wanaomwabudu Allah ni wapi?

    Tunajua kuwa Wakristo tutaishi na Mungu wetu Yehova milele (tazama 1Thesalonike 4:13-17 na Ufunuo 21:3-7) Hivyo Mungu wetu hana mwisho ni wa milele. Lakini tunaposoma Qurani na Hadithi za Muhammad, mtume wa Waislamu tunaona mafundisho haya…

    Qurani 51:56 Suratul-Adh-Dhaariyat (upepo)

    Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu

    Qurani 6:128 Suratul Al An-Am (Wanyama)

    Na (wakumbushe) siku atakapowakusanya wote (awaambie) “Enyi makundi ya majini! Hakika nyinyi mmechukua wafuasi wengi katika wanaadamu” na marafiki wao katika wanadamu (watawagombania) waseme “mola wetu! Tulinufaishana sisi na wao, na tumefikia muda wetu uliotuwekea” Basi (Mungu) atasema:”moto ndio makazi yenu, mtakaa humo milele…..

    Katika aya hizi tunaona kuwa majini pamoja na watu wote watatupwa motoni. Je Allah naye ni vipi? tunaposoma kitabu cha hadith za mtume (s.a.w) cha Sahih al-Bukhari Vol: VI Hadithi No: 371.ukurasa wa 353 Kuna maneno haya:

    Qurani 50:30 Suratul Qaf (kuapa)

    Siku tutakayoiambia Jahanamu, ‘Je! Umejaa?’ Nayo itasema ‘Je kuna ziada (zaidi?Naije tu!

    )

    Imesimuliwa na Anas kuwa: mtume alisema watu watatupwa jahanamu, Naye Allah ataiuliza jahanamu akisema je umejaa nayo jahanamu itasema kwani kuna nyingine zaidi na ije tu? Mpaka Allah atakapo ingiza mguu wake nayo jahanamu itasema inatosha! Inatosha

    Kwa kiingereza Hadithi hii inasomeka hizi:-

    Allah’s statement:It (Hell) will say Are there any more (to come)? (50:30).

    Narrated Anas: The prophet said the people will be thrown into the (Hell) Fire and it will say Are there any more (to come)?’ (50:30) till Allah puts His Foot over it and it will say Qai! Qat!(Enough! Enough!)

    Katika aya hii tunaona Allah mungu wa Waislamu anaiuliza Jehanamu kama imejaa, nayo Jehanamu itamuuliza Allah je, kuna zaidi. Yaani swali hili linaonyesha kuwa Jahanamu ilikuwa bado haijajaa,.

    Maelezo ya Hadithi hii inadhibitisha kuwa Allah ataingiza mguu katika Jahanamu na ndipo Jahanamu itakaposema kuwa inatosha! Inatosha!, yaani imejaa kwa tendo la Allah kuingiza mguu wake humo. Jambo hili ni tofauti kabisa na ilivyo kwa Mungu wetu Yehova., Mungu wetu ameiweka jahanamu maalum kwa ajili ya watu wabaya, na ibilisi, pamoja na malaika zake. Tafadhali soma aya hizi; Mathayo 25:41,46, Ufunuo 20:10, 21:8.

    Aya hizi zote zinaonyesha kuwa mwisho wa wabaya, Ibilisi na malaika zake ni katika ziwa la moto. Swali kwako Ndugu mpendwa, Je, Allah ni nani?

    Ni matumaini yangu kuwa umeweza kujua kwa undani kupitia Qurani na Biblia na vitabu vya Hadith za mtume wa Waislamu aitwae Muhammad kuwa Allah Sub-Haana Wataala Mungu anayeabudiwa na Waislamu. Siyo Yehova Mungu tunaye muabudu Wakristo.

    Like

    • Benn says:

      ni pepo hilo

      Like

      • Chaka says:

        Ctatusi dini yeyote, dini hikupeleki mbinguni!!ww na Maisha yako naucha mungu wako ndo njia, cha muhimu kufahamu unapodhalilisha mwenzako unamdhalilisha mungu mwenyewe! Mola awaongoze mnapo ongea!!kirini kila usiku na mola atawasikia

        Like

  287. Robert says:

    Islamic vs christianity

    Like

  288. Baninge peter says:

    All two faith are true way to go to God..no greater than and no less than all faith are equal..coz all two are the faith of a truly prophent of God.!

    Like

  289. kijukuu says:

    kwa upande wa imani ya kikiristo, je majini au mashetani wameumbwa na nani?

    Like

  290. Joshua says:

    Wa Islamu Hivi Ninyi Mnajua Kwanini Munamfuata Muhamadi Ambaye Hajulikani Hata Katika Mitume Wengine Wa Wakati Wa Yesu, Walio Kuwa Na Ujumbe Wa Mwanzo( Wa Waliotangulia)? Lakini Yesu Ameweza Kufundisha, Lakini Huyo Mwingine Hakuna Habari Hata Moja Tuliyo Wahi Kuisikia Kuhusu Huyo Ki Historiya. Na Vitabu Vyake Hakuna.

    Like

  291. Sabra says:

    Yote mlioongea yanaweza kuwa kweli au si kweli,ila kitu kimoja ninachokiamini dini haikuingizi peponi hata siku moja huwezi niambia wewe ni mzinifu au mshirikina hadi kufa kwako eti kisa umetoka dini fulani basi utaingia peponi…Sidhani kama kipo kitu kama hiko..Kuwa na matendo mema ya kumfurahisha Mungu ndio yatakayokuingiza peponi,pia tuwe watu wa toba sana maana hakuna mkamilifu isipokuwa Mungu…Kujua sana dini kwako iwe christian or muslim sio sababu ya mtu kuingia peponi,ila fanya mema yalioamrishwa na Mungu kupitia imani yako ndo kitu pekee kitakupeleka peponi….Maana wachungaji,mapadri na masheikh wangapi wanajua dini na bado wanamuhasi Mungu?Fanya matendo mema kwa kuilinda kesho yako.Mungu atubariki sote.

    Like

  292. Jia ya kweli ni ya ukiristo kwa sabu .waisilamu usema yakwamba eri kufa kwakutetea mungu lakini wakiristo tunasema yesu alikufu kwa ajili yetu .ukusema katika kitubu SA wamuzi 6:24 kinaelesa vyenye Gidioni alivyo jengea mwenyexi mungu madhabu kisha akayobomoa Yale ya sanamu usiku abayo baba yake na hao watu wa inchi walikua waki uthuria .ukulifo fika usubui wata wakwasa kulisana ninani aliye bomoa madhabu ya baeli wakajua ni Gidioni wakaenda kwa babake Gidioni wakamwambia toa mwanawe tukamue kwasabu amebomoa madhabau ya baeli .naye babayake Gidioni aka wambia hao watu .kama Gidioni amebomoa madhabau ya baeli akiwa mpeke yake .basi baeli na ajitete mpeke yake kwa kua nimungu wenu kwa sababu baeli nimungu wenu mwenye nguvu si apigane na Gidioni peke yake .. Dio hao watu wakasema nikweli baeli akiwesa si ajitete mpeke yaka kwa kua kama .angalikua mungu si angekubali kubomelewa na kubujwa bujwa? Kisha wazee alimwaa Gidioni na akajengea mwenyexi mungu madhabu mungu wangu wa Gidioni akawakoa watu wake kwa watesi wao … Mbali baeli akiwesa kuamka kujitetea .. Sasa ikiwa baeli akiwesa kujitetea anawesa kutetea binandamu ? Kwaivyo nikumanisa uwesi kupigania mwenyenzi mungu yeye ujipakania mwenyewe. Tena yeye dia anafaa kukupigania ! Dugu sangu kama kweli muamend agelikua kama yesu siangejufufua kwa wafu .kwakua yesu alipigania mwenyewe na kotoka kwa kifo na bando Hui kwasabu yeye ni njia ya husima mbali muhamad ni jia ya mauti kwa sabubu ajawai fufuka tena ajawa i jipigania .. Yesu ni jia ya ukweli

    Like

  293. Raphael Kimaro says:

    Nimefuatilia mazungumzo ila kitu alichosahau shekh ni kuwa shetani alisilimishwa na Muhammad na hivyo wanasali nae msikitini. Sasa ukisala na yeyote yule si tu ni rafiki lakini pia mnaenda sehemu moja.

    Like

  294. Ev. Omba says:

    Yesu ndiye njia,kweli na uzima.
    Waislamu acheni kuwadanganya watu nakubalisha maneno ya biblia.Musipo fuata yesu(siyo issa) hakika mutaangamia milele.
    Ukweli unabaki ukweli tu. Mimi kibinasfi sioni shida ya waislamu ni nini?
    1. Wanasema Yesu hakufa msalabani lakini mwenyewe alitabiri atakufa na atafufuka.waliona kifo yake pia walishuhudia.
    2. Wanasema wanaamini injili ya Yesu,wakipewa andiko toka injili hiyo hiyo wanakataa.kuma wana injili yao wanao amini isipokuwa injili inne ndani ya Biblia ebu watuambie.
    3. Wanakataa Yesu siyo Mungu.ndugu waislamu musifananishe Yesu na issa ao na Muhammad hawa ni tofauti kabisa.sitaongea kuhusu issa ao Muhammad. Lakini juwa kuwa Yesu ni Mungu (Jehovah) 100% usimulinganishe na yeyote.kwanza gisi alipo zaliwa,ki science mwislam gani anaweza prove hiyo? Pili maisha yake,mwanadamu gani anaeza ishi duniani miaka 33 bila kufanya zambi.Waislamu kwa nini ujinga mpaka hapo yaani muko hapo kuitetea dini ao je? Sisi wakristo hatutetee dini ila tunasema ukweli ni wajibu wako kukubali ao kukataa.
    Tena Biblia is spiritual usiichukwe kama Quran.Biblia muna mafumbo nakama hauko wa Roho hauzi fafanua hizo fumbo.sasa waislamu hamuna Roho mtakatifu mutafafanua je kitabu cha Roho? Acha walio wa Roho wawafafanulia na mkipinga mtakua mnamupinga Roho.
    Waliyo kuwa na yesu( siyo issa) wali amini na kiri wamemuona Masihi( the Christ) sasa ni sheikh gani upinge? Ndugu zangu Yesu ni yote ndani ya yote. Mubarikiwe na Yesu pia awatembelee nakuwafundisha njia iliyo ya kweli.

    Like

  295. Peter Venance says:

    Mm kama mkristo nimependa huduma ya biblia ni jibu ila ninaomba mfanye training za kutosha kwa walimu inapotokea mihadhara mbalimbali

    Like

    • Justine says:

      Habari.
      Naomba anayejibu au kuchangia mada hii, atueleze mambo yafuatayo hasa kwa ushahidi wa maandiko, itapendeza zaidi.
      1. Misingi ya imani husika.
      2. Kwa nini watu waiguate hiyo imani
      3. Sifa za kiongozi anayeaminiwa katika dini husika
      4. Je, huyo kiongozi aliyaishi aliyofundiaha?
      5. Je, tunaendaje mbinguni kwa dini husika?
      6. Kuna nini huko mbinguni, yaani kwa mafundisho husika nitapata nini? Kuna faida gani mbinguni? (Mungu atanipa nini?)
      Je, kuna nafasi ya kutubu tunapokufa?

      Ni hayo tu kwa sasa. Mada njema.

      Like

  296. Anthony Meji says:

    Naomba nijue “kibra” ni nini? Na

    Like

  297. Saidi says:

    Asalam alaykum
    Naomba kuuliza swali
    Bwana mtume mohammadi, Allah amlehemu
    Aliomba dua na alinyoosha mikono yake je? Alifuta usoni

    Like

  298. Fundi Eddy says:

    Nadhani itapendeza zaidi ikiwa tutakumbushana USAHIHI katika kutekeleza mafundisho ya NJIA (hapa zote ni SAHIHI) zinazompendeza Muumba.

    Like

Leave a reply to chidy rakim Cancel reply