Biblia inasema ombeni mtapewa, tafuteni mtapata, bisheni mtafunguliwa, maana yake mambo haya yote unapaswa kuyafanya kwa wakati mmoja! kuna watu wanashindwa kuelewa maandiko, wanasoma palipoandikwa msisumbuke na mambo ya kesho mle nini mvae nini, wangalieni ndege wa angani hawavuni na hawakusanyi ghalani lakini Baba wa Mbinguni huwalisha.
Lakini ukilitafakari vyema hilo andiko haliko kama watu wanavyofikiri kwamba hawapaswi kufanya kazi, maana hata hao ndege wa angani ni kweli kwamba Mungu huwalisha lakini wanapaswa kutoka kwenye viota vyao kwenda kutafuta chakula! Mungu anachokifanya hapa ni kuwaonyesha na kuwaongoza wapi kipo chakula!
Vivyo hivyo na wanadamu, Mungu yuko tayari kukupatia kila kitu, lakini hakupi mkononi ila atakuonyesha wapi vinapatikana, ni wajibu wako sasa kuvifuata ama kuacha!
ndio maana akasema ombeni,tafuteni na bisheni! sasa hapa maana yake ni kwamba mwombe Mungu akuonyeshe vitu unavyohitaji mahara vilipo, kisha toka nenda huko alikokuonyesha ukavitafute! ukizingatia hili Mungu atakufanikisha! barikiwa kwa jina lipitalo majina yote!