Namna ya kupokea mahitaji yako

Biblia inasema ombeni mtapewa, tafuteni mtapata, bisheni mtafunguliwa, maana yake mambo haya yote unapaswa kuyafanya kwa wakati mmoja! kuna watu wanashindwa kuelewa maandiko, wanasoma palipoandikwa msisumbuke na mambo ya kesho mle nini mvae nini, wangalieni ndege wa angani hawavuni na hawakusanyi ghalani lakini Baba wa Mbinguni huwalisha.

Lakini ukilitafakari vyema hilo andiko haliko kama watu wanavyofikiri kwamba hawapaswi kufanya kazi, maana hata hao ndege wa angani ni kweli kwamba Mungu huwalisha lakini wanapaswa kutoka kwenye viota vyao kwenda kutafuta chakula! Mungu anachokifanya hapa ni kuwaonyesha na kuwaongoza wapi kipo chakula!

Vivyo hivyo na wanadamu, Mungu yuko tayari kukupatia kila kitu, lakini hakupi mkononi ila atakuonyesha wapi vinapatikana, ni wajibu wako sasa kuvifuata ama kuacha!

ndio maana akasema ombeni,tafuteni na bisheni! sasa hapa maana yake ni kwamba mwombe Mungu akuonyeshe vitu unavyohitaji mahara vilipo, kisha toka nenda huko alikokuonyesha ukavitafute! ukizingatia hili Mungu atakufanikisha! barikiwa kwa jina lipitalo majina yote!

Posted in HOME | 3 Comments

Theres a way out from your trouble!

Whatever situation is going wrong, wherever you are in trouble, don’t worry God will make a way out for you! don’t los hope, there is the way out from your trouble

Posted in HOME | 1 Comment

Jiji la Yerusalem mpya laonekana angani nchini Marekani

Jesus city

Watu wakionyeshana mji wa Yerulemu ya mbinguni ukionekana kwa mbalikatika mawingu huko california nchini USA

katika hali isiyokuwa ya kawaida, jiji la Yesu yaani Yerusalem mpya limeonekana angani likiwa limefunikwa na mawingu katika baadhi ya sehemu zake. Hii si mara ya kwanza kwa jiji hili kuonekana angani, mwaka 2011 lilionekana nchini nigeria, mnamo mwaka 2015 lilioneka katika mji mmoja huko china na october 2015 limeonekana katika anga la mji wa California nchini marekani, mashuhuda wanadai kwamba waliona majengo mazuri na sauti za mashine zikisikika kutoka katika mji huo.

Zaidi sana inadaiwa kwamba mji ule ule na majengo yale yale yaliyoonekana china ndiyo yameonekana tena october 2015 California nchini marekani.

Hii ni dalili ya kuwa mwana wa adamu yuko mlangoni, na inawezekana huu ndiwo wakati ambao kanisa linanyakuliwa ili kupisha nafasi ya mpinga kristo. mimi na wewe tupambane twende katika unyakuo wa  kwanza, maana taabu dhiki na mateso vitaikumba dunia.

Bwana atusaidie kwa jina la Yesu…….

Posted in HOME | 1 Comment

Niko kwenye maombi, tafadhali tuma mahitaji yako nikuombee

Shalom, niko kwenye maombi siku ya leo nikiombea mahitaji ya wengine, tafadhali nitumie mahitaji yako ili nikuombee, unaweza ku-coment hapa au whatsapp +255755961270

Ev.moses

Posted in HOME | Leave a comment

NHM: mision to Uganda january 17-21/2016

We are very happy to let you know that we will have a mission trip to Uganda on january 17-21.20116, the event will take place at Namtumba town, two hour driving from the capital city (Kampala city) please keep praying  for us….

Stay in touch

Posted in HOME | Leave a comment

Sitamtolea shetani sadaka

Hivi punde nimemaliza kuongea na mtu mmoja kwa njia ya simu kutoka Ghana, alikuwa anataka kuni-support na dollar $50,000.00 kwajili ya NHM. lakini alitaka kwanza nitoe sadaka kwa miungu yake, kondoo wawili na manukato, na alidai kwamba mimi sitahusika na zoezi la kutoa sada hiyo ila nimpe kibali tu yeye atafanya badala yangu. nimemwambia NAMWAMINI MUNGU WANGU MTAKATIFUSIWEZI KUTOA SADAKA KWA MUNGU MWINGINE.

Shetani anawinda watumishi kwa nguvu sana

 

Posted in HOME | Leave a comment

The Lord God will enable you to close this year

The Lord almighty God bless you and enable you to close the 2015 into 2016. coment AMEN if you want to receive..

Posted in HOME | 2 Comments

Tb Joshua adhulu Tanzania

TB JMhubiri maarufu barani africa, nabii Temitope belgun Joshua wa Kanisa la Sinagosi la mataifa yote lenye makao yake makuu mjini lagos nchini Nigeria.

Ziara ya Joshua imekuja mara baada ya mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi Dr.john magufuli kushinda kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika october 25 20015.

Magufuli ambaye alikwenda kuombewa kwa nabii huyo miaka michache kabla ya uchaguzi, ameonekana mwenye furaha yeye na familia yake wakiwa uwanja wa ndege kumpokea mhubiri huyo.

Inasemekana kuwa ujio wa Joshua nchini tanzania ni kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa rais mteule wa nchi hiyo.

Posted in HOME | 1 Comment

Baada ya uchaguzi Tanzania

Bwana wetu Yesu kristo apewe sifa!

Tunamshukuru Mungu kwa kuimarisha na kuendelea kuimarisha amani na usalama katika taifa la Tanzania ambalo lilikuwa na uchaguzi mgumu na wenye harufu ya damu. lakini kwa maombi ya watakatifu amani imeendelea kuwepo katika nchi.

Asante Yesu kwa kuwa wewe ni amani yetu.

Na sasa ndugu zangu wapenzi mambo ya siasa na chuki na hasira za kisiasa tuziweke pembeni na kuangalia mstakabali wa taifa letu. mambo ya uchaguzi yamepita  na tunamshukuru Mungu Rais amepatikana.

pamoja na hayo lakini tuendelee kuombea amani kule upande wa zanzibar ambako hadi sasa hakuna Rais.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu tutetee watu wako

Posted in HOME | Leave a comment

Bwana Mungu wa majeshi akubariki

image

Nakuombea. Bwana akubariki uumalize mwaka huu salama kwa jina la Yesu

Posted in HOME | 1 Comment